Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CHADEMA Haitoungana na Chama Chochote

    Report Post
    Page 1 of 9 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 176
    1. #1
      HabariLeo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th January 2007
      Posts : 29
      Rep Power : 640
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default CHADEMA Haitoungana na Chama Chochote

      Chadema imesema kwamba haina mpango wa kuungana na chama chochote cha siasa kwa wakati huu

      Habari zaidi zitawajia baadaye

      Mzee Zitto ulikuwepo katika lile kongamano, tunaomba utufafanulie katibu wenu alisema nini sababu za nyie kutoungana na chama chochote.


    2. #2
      Kadogoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2007
      Location : Moshi
      Posts : 1,957
      Rep Power : 953
      Likes Received
      263
      Likes Given
      567

      Default

      Hawa CHADEMA tunawajuwa kuwa ni CCM ndogo ndio maana hawataki kusikia chochote kuhusu muungano! CHADEMA tunayoijuwa ya wakati ule wa Mzee Edwin Mtei sio sawa na ya sasa kwani ya sasa imesheheni viongozi wengi mamluki au wa kupandikizwa toka CCM ambao lengo lao ni kuwahadaa wananchi na mbwembwe za helkopta ili kuvunja nguvu za upinzani kwa kuinufaisha CCM!

    3. #3
      Kyaruzi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd March 2007
      Posts : 115
      Rep Power : 649
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default They r bigger than that

      Gr8!

      Chadema ni chama Kikubwa kama kuungana vyama vidogo ndio vije kujiunga na Chadema.

      Kwa kasi wanayokwenda nayo hii uwazi, viongozi vijana, Mbowe, Zitto, Mnyika, Akwilombe nk wana very bright future.

      Sijasikia migogoro Chadema, pamoja na kuwa wanapata ruzuku zaidi ya Mil 30. Kama angekuwa mtani wangu Mrema hapo saa hizi wapo mahakamani.

      Wakati suala la kuungana kuwa ni zuri, kwa Chadema wakati muafaka bado kwa maoni yangu.

    4. #4
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,048
      Rep Power : 2571
      Likes Received
      794
      Likes Given
      29

      Default

      Kadogoo
      Umetoa madai mazito sana hebu yafafanue ili tulete hoja hapa .

    5. #5
      Kadogoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2007
      Location : Moshi
      Posts : 1,957
      Rep Power : 953
      Likes Received
      263
      Likes Given
      567

      Default

      Kama CHADEMA sio tawi la CCM kwanini wanapinga ushirikiano wa vyama hasa vikuu vya upinzani au ushirikiano wa kuachiana majimbo pale panapoonekana chama fulani kinanguvu? kwa mfano uchaguzi wa Tunduru CUF mgombea wake alikuwa ana kubalika kwa wananchi wa hapo lakini CHADEMA walikataa katakata kuwaunga mkono wenzao wakati wakijuwa kuwa hawakuwa na matumaini yoyote ya kushinda jimbo hilo!

      Mwaka 2000 CHADEMA walijifanya kushirikiana na CUF lakini ushirikiano huu ulikuwa wa kinafiki kwasababu vyama hivi viliachiana majimbo lakini ktk utafiti wetu wa chini kwa chini tulikuja gunduwa kuwa wenzetu CHADEMA waliwapa kura wagombea wa CCM huku wapiga kura wa CUF kwa moyo mkunjufu waliwapa kura wagombea wa CHADEMA na walijifanya kumuunga mkono Profesa Lipumba ktk kugombea urais lakini utafiti ulionyesha kuwa CHADEMA walimuunga mkono kwa mdomo tu huku kura zao zote walimpa mgombea wa CCM! siri hii ilikuja fichuka baada ya mashushushu wetu ndani ya CHADEMA kugunduwa barua za siri walizokuwa wakitumiana viongozi waandamizi kwenda kwa viongozi wao wa ngazi zote!

      Sasa CHADEMA kama sio CCM ndogo ni nani basi wao? wanachotaka ninini? kwanini hawataki ushirikiano na CUF huku wakijuwa TZ upinzani bila ya ushirikiano basi tusitegemee kuishinda CCM ngumu! chama chenye mizizi mizito!


    6. #6
      omarilyas's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2007
      Location : Morogoro
      Posts : 2,495
      Rep Power : 1138
      Likes Received
      69
      Likes Given
      5

      Default

      Hivi kati ya CUF na CHADEMA ni nani alikuwa akimfanya mwenziwe -----? Na kati ya vyama vya upinzani ni chama gani ambacho daima kimekuwa tayari kuacha maslahi yake kwa ajili ya kujenga upinzani imara hata kuwa tayari kutosimamisha rais wakati wakijua bila ya kufanya hivyo wanajipunguzia wigo wa kujitangaza kwa wananchi?

      CUF inabidi isome nyakati na kugundua ni kwanini CHADEMA wanaamua kuaply LOYAL OPPOSITION politics badala ya siasa za Confrontation ambazo hazilipi kwa wapiga kura wa Tanzania.

      Tanzanianjema
      Last edited by omarilyas; 10th April 2007 at 06:51.

    7. #7
      Mpaka Kieleweke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2007
      Posts : 2,793
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      724
      Likes Given
      11

      Default

      Kwa wale wote mliofanikiwa kuwa salama mara baada ya sherehe za pasaka napenda wote kwa pamoja tuweze kumshukuru mwenyezi Mungu,kwa wale waliopata shuruba za hapa na pale napenda wote kuwapa pole za dhati kabisa,

      Nipende kutoa maoni uyangu kuhusiana na swala la kuunganisha vyama pamoja na ukweli kwamba mimi sio mwanachama wa CHADEMA,kama ifuatavyo,.
      1.Ni kweli kuwa kuna haja ya kuungana ila pia kuungana huku kusukumwe zaidi na lengo. hivi lengo la kuungana ni ili kuiondoa CCM ama lengo ni nini haswa?na kama lenggo ni kuingoa tuu CCM and then waishie hapo sioni haja ya CHADEMA kuingizwa kwenye huo mtego .
      2.Niulize hivi kati ya CHADEMA na CUF ni nani wakala wa CCM? nauliza hivyo kutokana na ukweli kwamba kuna mazungumzo ya muafaka yanaendelea kule ZNZ na kwa kuwa CUF haioni wadeau wengine kwenye siasa zaidi ya huyo CCM ndio maana hawakupenda hata kushinikiza basi walau vyama vyenye wabunge vihusishwe ila wanawaona CCM kama ndio wenzao je?CHADEMA pamoja na kuwa na viongozi makini unafikiri watashindwa kuliona hilo?

      3. Ni Lipumba huyu huyu aliyekuwa mshauri mkuu wa Mwinyi na Museveni sio ajabu kuwa hata hili la museveni kutaka ku7wa rais wa EAC alishauriwa na Lipumba naye klwa kuwa ni sehemu ya watawala hajawa tayari kuwaeleza watanzania ukweli wa kile alichokuwa anakishairi wakati ule akiwa mtoto wa ikulu.
      4. Ingekuwa ni kweli kwamba CUF ipo kwa ajili ya maslahi ya watanzania ingefaa basi kutueleza kuwa zile 13bilioni kutoka EU mgawanyo wake umekuwaje na wao wanapanga kuzitumiaje hizo fedha ili watanzania waweze kuuelewa ukweli wa hou muafaka .
      5.Kwangu binafsi sioni haja ya kuuuwa vyama vyote na watanzania wote ama watakiwwe kujiunga na CCM am cuf KWANI HII INAUWA MAANA NZIMA YA DEMOKRASIA YA WATU KUWEZA KUCHAGUA VYAMA WANAVYOVITAKA.

      6.Naamini kuwa kwa chama kama CHADEMA ni lazima kwanza kwa wao wastiki kwenye principals kwa mfano hadi leo hii tunalaumu shirikisho kutokufuata sheria na pia viongozi kujichukulia maamuzi mikononi mwao ile hali wananchi wakiwa wanafanywa rubber stamps ,naamini kuwa kuna haja ya vyama hivi kufuata mchakato wa ndani ya vyama vyao kwanza na wanachama ndio wapewe jukumu la kuamua na sio kuwapa viongozi mamlaka juu ya wanachama na Lipumba ni lazima awe anayasema maamuzi ya wanachama wake na sio kusema ili aonekane kuwa yeye ndio champuioni wa muunganao wa vyama na ikikumbukwa ya kuwa MBOWE ndio aliyekuwa wa kwanza kwenye ule mkutano wa jangwani akiwataka viongozi wenzake waanze kuangalia ni jinsi gani wanaweza kushirikiana.

      7.Ikukmbukwe pia kwamba kuna taarifa ya vyama hivi kuandaa roadmap ya kuungana na ili8elezwa ya kuwa walipenda kuungana kwenye masuala zaidi yaaani issues na pia ilielezwa kuwa wana mpango wa muda mfupi,wa kati na wa muda mrefu ni bora hawa CUF wanaolalamika wakarejea hayo maamuzi ambayo sisis wengine tuliyasiki8a kupitia vyombo vya habari.

      Mwisho nipende kuwaasa hawa wenye vyama haswa cuf wasitake kuwaona CHADEMA wakiwa wanawaunga mkono kama TLP walivyofanya na siku zote chama ni taasisi na sio swala la kiongozi kuamka na kufanya maamuzi bila ya wadau kushirikishwa .CHADEMA kuweni macho ni kwa nini cuf wasiwaunge nyie mkono ila wanataka wao ndio waungwe mkono?ni sera zipi mtafuata baadfa ya hapo ama mtakuwa waliberali kama walivyo wana cuf na kuhalalisha uhuru wa kutumia miili ?

    8. #8
      Mugongo Mugongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2006
      Posts : 469
      Rep Power : 739
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default

      They will never do it. Mbowe anaogopa kufunikwa na Lipumba kama CHADEMA ikiungana na CUF.

    9. #9
      Mpaka Kieleweke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2007
      Posts : 2,793
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      724
      Likes Given
      11

      Default

      Ndugu mugongo wa mugongo nadhani hata wewe unashindwa sasa kuyasoma majira ya nyakati kwani unajua kabisa kuwa mvuto wa Lipumba hapo 2010 ama 2015 atakuwa amezeeka na kuishiwa kabiosa kwa hiyo ni kama mtu aliyekalia kuti kavu na pia waanze kuungana kwenye issues na watengeneze katiba ya hicho chama kipya.
      Cuf wao hawana mbunge hata mmoja huku bara iweje wao ndio waungwe mkono ile hali hawana nguvu hizo kwa huku bara ?
      Pia ijulikane kuwa kwa upande wa madiwani CHADEMA kina madiwani 100 ile hali CUF wao wana madiwani 72 tuu.

      CHADEMA kinaongoza halmashauri mbili za wilaya na wanangoja kuwa na ya tatu ya kule tarime baada ya rais kuamua kuifanya Rorya kuwa wilaya na Tarime kuwa ni wilaya huyo MBOWE anaogopa kufunikwa kwenye lipi?

    10. #10
      Mpaka Kieleweke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2007
      Posts : 2,793
      Rep Power : 1196
      Likes Received
      724
      Likes Given
      11

      Default

      Kwa wale wote mliofanikiwa kuwa salama mara baada ya sherehe za pasaka napenda wote kwa pamoja tuweze kumshukuru mwenyezi Mungu,kwa wale waliopata shuruba za hapa na pale napenda wote kuwapa pole za dhati kabisa,

      Nipende kutoa maoni uyangu kuhusiana na swala la kuunganisha vyama pamoja na ukweli kwamba mimi sio mwanachama wa CHADEMA,kama ifuatavyo,.
      1.Ni kweli kuwa kuna haja ya kuungana ila pia kuungana huku kusukumwe zaidi na lengo. hivi lengo la kuungana ni ili kuiondoa CCM ama lengo ni nini haswa?na kama lenggo ni kuingoa tuu CCM and then waishie hapo sioni haja ya CHADEMA kuingizwa kwenye huo mtego .
      2.Niulize hivi kati ya CHADEMA na CUF ni nani wakala wa CCM? nauliza hivyo kutokana na ukweli kwamba kuna mazungumzo ya muafaka yanaendelea kule ZNZ na kwa kuwa CUF haioni wadeau wengine kwenye siasa zaidi ya huyo CCM ndio maana hawakupenda hata kushinikiza basi walau vyama vyenye wabunge vihusishwe ila wanawaona CCM kama ndio wenzao je?CHADEMA pamoja na kuwa na viongozi makini unafikiri watashindwa kuliona hilo?

      3. Ni Lipumba huyu huyu aliyekuwa mshauri mkuu wa Mwinyi na Museveni sio ajabu kuwa hata hili la museveni kutaka ku7wa rais wa EAC alishauriwa na Lipumba naye klwa kuwa ni sehemu ya watawala hajawa tayari kuwaeleza watanzania ukweli wa kile alichokuwa anakishairi wakati ule akiwa mtoto wa ikulu.
      4. Ingekuwa ni kweli kwamba CUF ipo kwa ajili ya maslahi ya watanzania ingefaa basi kutueleza kuwa zile 13bilioni kutoka EU mgawanyo wake umekuwaje na wao wanapanga kuzitumiaje hizo fedha ili watanzania waweze kuuelewa ukweli wa hou muafaka .
      5.Kwangu binafsi sioni haja ya kuuuwa vyama vyote na watanzania wote ama watakiwwe kujiunga na CCM am cuf KWANI HII INAUWA MAANA NZIMA YA DEMOKRASIA YA WATU KUWEZA KUCHAGUA VYAMA WANAVYOVITAKA.

      6.Naamini kuwa kwa chama kama CHADEMA ni lazima kwanza kwa wao wastiki kwenye principals kwa mfano hadi leo hii tunalaumu shirikisho kutokufuata sheria na pia viongozi kujichukulia maamuzi mikononi mwao ile hali wananchi wakiwa wanafanywa rubber stamps ,naamini kuwa kuna haja ya vyama hivi kufuata mchakato wa ndani ya vyama vyao kwanza na wanachama ndio wapewe jukumu la kuamua na sio kuwapa viongozi mamlaka juu ya wanachama na Lipumba ni lazima awe anayasema maamuzi ya wanachama wake na sio kusema ili aonekane kuwa yeye ndio champuioni wa muunganao wa vyama na ikikumbukwa ya kuwa MBOWE ndio aliyekuwa wa kwanza kwenye ule mkutano wa jangwani akiwataka viongozi wenzake waanze kuangalia ni jinsi gani wanaweza kushirikiana.

      7.Ikukmbukwe pia kwamba kuna taarifa ya vyama hivi kuandaa roadmap ya kuungana na ili8elezwa ya kuwa walipenda kuungana kwenye masuala zaidi yaaani issues na pia ilielezwa kuwa wana mpango wa muda mfupi,wa kati na wa muda mrefu ni bora hawa CUF wanaolalamika wakarejea hayo maamuzi ambayo sisis wengine tuliyasiki8a kupitia vyombo vya habari.

      Mwisho nipende kuwaasa hawa wenye vyama haswa cuf wasitake kuwaona CHADEMA wakiwa wanawaunga mkono kama TLP walivyofanya na siku zote chama ni taasisi na sio swala la kiongozi kuamka na kufanya maamuzi bila ya wadau kushirikishwa .CHADEMA kuweni macho ni kwa nini cuf wasiwaunge nyie mkono ila wanataka wao ndio waungwe mkono?ni sera zipi mtafuata baadfa ya hapo ama mtakuwa waliberali kama walivyo wana cuf na kuhalalisha uhuru wa kutumia miili ?

    11. #11
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,940
      Rep Power : 6971
      Likes Received
      1102
      Likes Given
      36

      Default

      Quote By Kadogoo View Post
      Kama CHADEMA sio tawi la CCM kwanini wanapinga ushirikiano wa vyama hasa vikuu vya upinzani au ushirikiano wa kuachiana majimbo pale panapoonekana chama fulani kinanguvu? kwa mfano uchaguzi wa Tunduru CUF mgombea wake alikuwa ana kubalika kwa wananchi wa hapo lakini CHADEMA walikataa katakata kuwaunga mkono wenzao wakati wakijuwa kuwa hawakuwa na matumaini yoyote ya kushinda jimbo hilo!

      !

      Kadogoo: hii forum sasa hivi imeshavuka level ya cheap politics kama hizi. Yaani kwa sababu CHADEMA hawataki muungano (kama ni kweli) basi ndio wamekuwa tawi la CCM? Acha hizi; siasa nyepesi za namna hii zimepitwa sana na wakati. Naamini unaweza ukajenga hoja nzito zaidi.

      Narudia tena kiwango cha hii forum sasa hivi ni cha juu mno, nawe unaturudisha nyuma mno kwa hoja nyepesi namna hii!
      A Struggle Without Casualties is No Struggle-Steve Biko

    12. #12
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,940
      Rep Power : 6971
      Likes Received
      1102
      Likes Given
      36

      Default

      Quote By Kadogoo View Post
      !

      Mwaka 2000 CHADEMA walijifanya kushirikiana na CUF lakini ushirikiano huu ulikuwa wa kinafiki kwasababu vyama hivi viliachiana majimbo lakini ktk utafiti wetu wa chini kwa chini tulikuja gunduwa kuwa wenzetu CHADEMA waliwapa kura wagombea wa CCM huku wapiga kura wa CUF kwa moyo mkunjufu waliwapa kura wagombea wa CHADEMA na walijifanya kumuunga mkono Profesa Lipumba ktk kugombea urais lakini utafiti ulionyesha kuwa CHADEMA walimuunga mkono kwa mdomo tu huku kura zao zote walimpa mgombea wa CCM! siri hii ilikuja fichuka baada ya mashushushu wetu ndani ya CHADEMA kugunduwa barua za siri walizokuwa wakitumiana viongozi waandamizi kwenda kwa viongozi wao wa ngazi zote!
      Kadogoo: this is also so cheap and low! Kwanza utafiti gani huo wa chinichini hata uitwe utafiti? Pili, yaani hadi leo huwezi kuelewa kuwa kupiga kura ni jambo la mtu binafsi tena la siri? Sasa kama viongozi walikubaliana kuachiana majimbo, haina maana kwamba waliwanyan'ganya wanachama wao (wananchi) uhuru wa kuwachagua watu walio wataka! Ndugu yangu, nenda juu kidogo, hii forum hii ni jukwaa kubwa la hoja nzito na pana!
      Last edited by Kitila Mkumbo; 10th April 2007 at 12:08.
      A Struggle Without Casualties is No Struggle-Steve Biko

    13. #13
      John Mnyika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th June 2006
      Location : Tanzania
      Posts : 926
      Rep Power : 13542
      Likes Received
      1096
      Likes Given
      11

      Default CHADEMA haijasema kwamba haitaungana na vyama vingine vya siasa!

      Dr Slaa hakuwahi kutoa kauli hiyo wala gazeti la habari leo halikuandika habari kama hiyo. Gazeti la habari leo la 9/4/2007 liliandika habari "CHADEMA yaeleza hofu ya kuungana", habari imeeleza ni mchakato gani ni vyema ukapitiwa katika kuunganisha vyama na kwa ujumla hatua gani imefikiwa. Sina soft copy ya hiyo habari( naomba "habari leo" aliyeanzisha hii thread atuwekee habari husika). Ila mimi hapa ninayo soft copy ya Makala ya Mtanzania ya leo ambayo kidogo imejibu baadhi ya maswali kuhusu yaliyojiri kwenye mjadala wa wa elimu ya juu ambapo pamoja na kujadili mambo mbalimbali mwisho wa mjadala tulikuwa na kikao cha wanavyuo vikuu walioko Morogoro(tuliingiza wanachama wapya zaidi ya 400).



      Wanafunzi walijadili Taifa

      APRILI 7, mwaka huu, baadhi ya wanafunzi kutoka Vyuo Vikuu vya Mzumbe, Sokoine, Tumaini, Dar es Salaam (UDSM) na St. Joseph walishiriki kongamano kuhusu hali ya elimu ya juu nchini, nafasi ya wanataaluma kutetea haki zao na za wanyonge, pamoja na hali ya kisiasa nchini. Kongamano hilo lilifanyika katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Forest Hill, Morogoro. Mwandishi Wetu GODFREY DILUNGA aliyehudhuria kongamano hilo anaeleza zaidi.

      ILIKUWA saa nane mchana, katika Ukumbi wa Shule ya Forest Hill, baadhi ya wanafunzi wakiwa na vijitabu vidogo vya kuandikia (note book) kwa ajili ya kuweka katika maandishi kitakachozungumzwa, walionekana kugubikwa na shauki ya kusikia na kujadili kuhusu masuala muhimu yanayohusu taifa lao.

      Wanafunzi hao walionekana kuwa na uvumilivu mkubwa, hasa baada ya kubainika kuwa taarifa waliyokuwa nayo awali kuhusu kuanza kwa kongamano hilo haikuwa hivyo. Awali, walielezwa kwamba kongamano litaanza saa tatu asubuhi, lakini kutokana na sababu mbalimbali lilianza saa nane, hata hivyo hawakukata tamaa.

      Naam! Muda uliwadia, Dk. Wilbroad Slaa, Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ndiye aliyefungua kongamano hilo. Huku hotuba yake ikikatishwa kwa makofi na vifojo kutoka kwa wanafunzi waliokuwa wakimsikiliza.

      “Wanafunzi wa vyuo vikuu na wengine siku hizi mnashindwa kufuatilia, kuhoji a kushauri kuhusu mambo ya msingi kwa Taifa lenu. Umakini miongoni mwenu umeteketea. Haupo, mnashindwa kuhoji hata kuhusu MKUKUTA (Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kuondoa Umasikini Tanzania).

      “Mnataka nani afanye kazi hiyo? Mnatakiwa kuibana Serikali kuhusu ngonjera hii ya MKUKUTA. Maana ya MKUKUTA haionekani, ninyi wasomi mmebaki kimya. Hamfahamu unapAswa kuwasaidia vipi kuhusu elimu. Hamhoji ni kwa nini pamoja na kuwa na semina nyingi za MKUKUTA, idadi kubwa ya Watanzania hawafahamu chochote.

      “Nchi hii inaporomoka, ninyi mmebaki kimya. Baadhi ya wasomi kwa idadi kubwa wanakimbilia CCM kugombea nafasi mbalimbali za uongozi, mjiulize ni kwa nini na nini kinawasukuma kufanya hivyo?

      “Hata hivyo, wakishagombea ndani ya CCM na kupata uongozi wanabaki kimya, hawana msaada kwa Taifa. Nitoe mfano? Kuna Mbunge mmoja wa CCM aliwahi kupewa adhabu ya kutochangia hoja bungeni kwa miezi 18, baada ya kuonekana ni tatizo,” alidai Dk. Slaa bila kutaja jina la Mbunge huyo.

      “Wapo wabunge ni Maprofesa, lakini hawawezi kutumia akili zao kwa kulinda na kutetea maslahi ya Taifa. Wameligeuza Bunge kuwa kama ‘rubber stamp’. Wanatuliza profession (taaluma) zao kwa sababu ya itikadi, msomi gani anakubali kuuza nchi yake kwa sababu ya itikadi tu. Msomi gani ‘una-compromise principles’ za taaluma yako.

      “Hatuna wasomi bungeni bali tuna kundi la watu wenye vyeti tu. Ninavyofahamu msomi wa kweli ni yule anayesimamia misingi ya taaluma yake. Halafu kuna jambo jingine kwa mfano, mishahara ya wabunge na rais ni kwa nini iendelee kuwa siri wakati inatokana na kodi ya wananchi. Mishahara ni lazima iwe wazi ili kuimarisha, kwa nini iwe siri? Nchi kama Mauritius jambo hili linafanyia. Tunaogopa nini?

      “Ndani ya Bunge kuna kitu kinaitwa ‘Malt-party Dictatorship’. Bunge linaburuzwa na kufikia uamuzi wa jumla kama Bunge, lakini katika uamuzi huo hakuna ridhaa ya wabunge wa upinzani. Hii yote inatokana na kuwepo kwa idadi ndogo ya wabunge wa upinzani. Ndiyo maana Bunge wakati mwingine linaafiki uamuzi usio na maslahi kwa wengi.

      “Nizungumzie suala la vyama vya upinzani kuungana ili kuing’oa madarakani CCM. Kimsingi wingi wa vyama maana yake ni kwamba kunakuwa na utajiri wa mawazo tofauti. Suala la vyama kuungana ili kuing’oa CCM hatuwezi kulikubali moja kwa moja. Mnatakiwa mjiulize baada ya kuing’oa mtafanya nini.

      “Tunachokikubali kwa sasa ni kwamba kama tunakubaliana kuungana kwa ajili ya kuondoa sera mbovu zisizo na maslahi kwa Taifa, hatuna tatizo. Ni lazima suala la kuungana lihusishe mtakachofanya baada ya kufanikiwa lengo hilo. Halafu ninyi wenyewe muwe mfano bora wa demokrasia ndani ya vyama vyenu.

      “Kwa sasa CHADEMA tuko tayari kuungana katika mambo ya msingi kama vita dhidi ya rushwa. Si suala la kukimbilia Ikulu pekee. Tusiwaze kukimbilia Ikulu kwanza na baadaye mambo mengine yafuate. Tuungane kwanza kudai kuondolewa kwa sheria kandamizi.

      “Suala jingine, nizungumzie Shirikisho la Afrika Mashariki. Niwaulize ninyi wasomi, tunalitaka Shirikisho kwa Katiba ipi, kwa mfumo gani wa uongozi, je, ni ‘presidential leadership’ au ‘parliamentary leadership’? Hii Tume ya Kukusanya Maoni imetengewa Sh bilioni 2.3 eti kwa ajili ya kuuliza swali Watanzania kuhusu ‘fast tracking ya federation’, kwa hiyo uamuzi tayari umefikiwa na viongozi.”

      Akizungumzia mikopo ya Sh bilioni moja kwa kila mkoa nchini inayotolewa na Serikali, Dk. Slaa alisema, “Serikali makini haikimbilii kutoa fedha bila kuandaa mikakati endelevu. Nadhani na kuna uwezekano mpango huu kutokana na kutokuwa na mikakati endelevu ukafifia na kufa kabisa. Na fedha iliyokwishatolewa ikawa sadaka.”

      Kwa upande wake, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zito Kabwe akizungumzia nafasi ya wasomi nchini katika kutetea maslahi yao na ya Taifa, alisema wanafunzi wa vyuo vikuu na wengine wa vyuo vya elimu ya juu wanapaswa kuwa watetezi wa haki zao na za wanyonge, hususan waliopo vijijini.

      “Serikali inawajibika kusomesha wanafunzi wake bila masharti. Serikali inayoshindwa kusomesha raia wake haipaswi kukusanya kodi, hivyo haifai kuwepo madarakani. Lakini pia ari ya wasomi kutetea makabwela nchini imeshuka sana.

      “Kwa sasa Rais Jakaya Kikwete amepata sifa ya pekee ya kumudu kutuliza mgomo wa wanafunzi bila kutumia virungu vya FFU. Wanafunzi walikuwa na madai yao. Akawaita pale Diamond Jubilee akawaeleza kuwa atashughulikia madai yenu, hadi leo hakuna kitu.

      “Ni lazima wanafunzi wawe ‘organized’ kutetea haki zao pamoja na za wadogo zao watakaokuja kusoma katika vyuo vikuu baadaye. Mapinduzi yote huanzia kwa wanafunzi wa vyuo vikuu. Mapinduzi kama yale ya dhidi ya sheria mbovu, na mengineyo.

      “Mfano sasa hivi Wizara ya Mipango, Uchumi na Uwezeshaji inaonekana kushindwa kuwa na mipango madhubuti ya kuhakikisha nchi inazalisha. Wanafunzi wa vyuo vikuu mmebaki kimya, hamchambui masuala muhimu ya nchi. Mnashindwa kuhoji. Mnataka nani ahoji, mkulima wa kijijini? Nini faida ya kuwa msomi ndani ya nchi yako.”

      Naye Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA), Suzan Lyimo akiwasilisha mada yake kuhusu elimu ya juu nchini, alisema Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limekuwa likitengewa bajeti nono zaidi kuliko sekta nyingine muhimu kama ya elimu na hata kilimo.

      Kwa upande wake, mwanaharakati Ndimara Tegambwage akiwasilisha mada kuhusu hali ya siasa nchini, alisema tatizo la msingi nchini ni wanasiasa. Alisema Serikali inaongozwa na idadi kubwa ya wanasiasa wachafu, wasiokuwa na aibu wakishiriki kuliangamiza Taifa kutokana na ubinafsi walionao.

      Baada ya hapo, wanafunzi waliokuwa wakiwasikiliza watoa mada hao walipata nafasi ya kueleza wanachofikiri kwa maslahi ya Taifa lao.

      Mwanafunzi aliyeanza kuchangia ni kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA), aliyeonyesha kukerwa kwake suala la uchangiaji wa asilimia 40 ya gharama za masomo. Kilichomkera zaidi mwanafunzi huyo ni hatua ya baadhi ya wanafunzi wanaoshindwa kulipa asilimia hiyo 40 kunyimwa matokeo yao.

      “Baadhi ya wenzetu wananyanayaswa ndani ya Taifa lao. Wananyimwa matokeo yao kwa sababu ya kushindwa kulipa kwa wakati asilimia 40 ya uchangiaji gharama za masomo. Kwa nini umasikini wetu unatumika kutunyanyasa kiasi hiki?”

      Naye, mwanafunzi mwingine kutoka Chuo cha Falsafa cha Salvatorian kilichopo mkoani Morogoro alisema tatizo la msingi nchini si wanafunzi kushindwa kufuatilia au kuhoji masuala ya msingi kuhusu maendeleo ya Taifa lao. Bali tatizo kubwa ni mfumo mzima wa elimu nchini.

      Kwa mujibu wa mwanafunzi huyo, mfumo wa elimu nchini unawashurutisha wanafunzi kusoma kwa ajili ya kujibu mitihani yao na kisha kuhitimu masomo yao. Akisisitiza kuwa mfumo huo hautoi fursa kwa wanafunzi kujadili masuala ya msingi ya Taifa lao na ulimwengu kwa ujumla.

      Mwanafunzi mwingine, kutoka Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine, alizungumzia ukusanyaji wa maoni kuhusu Shirikisho la Afrika Mashariki, akisema tume inayohusika na ukusanyaji wa maoni hayo isiwakimbie wasomi na badala yake ijadiliane nao kwa maslahi ya Taifa.

      Katika hatua nyingine, mwanafunzi huyo alimtaka Waziri wa Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Peter Msolla kuchukuliwa hatua kwa kuchunguzwa na tume inayohusika na usimamizi wa maadili ya viongozi, kutokana na waziri huyo kuonekana kuyumba kuhusu suala zima la usimamizi wa mikopo kwa wanafunzi.

      Naye mwanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe alisema “Umasikini wetu usitumike kutudharau, hasa katika suala hili la kuchangia asilimia 40 ya mikopo.” Alidai kuwa vyuo takriban vyote vya elimu ya juu nchini vimegeuzwa kuwa taasisi za Chama cha Mapinduzi (CCM).

      Alisema kwa kuwa siasa ndiyo sehemu muafaka ya kutafakari na kuamua mustakabali wa Taifa, ni vema wasomi wakaingia katika vyama vingine vya siasa mbali na CCM ili kupata mbadala wa uongozi nchini.

      Mwanafunzi mwingine wa Chuo Kikuu Mzumbe, alihoji ni maana ya mtu kuitwa msomi. Akisema hivi msomi maana yake nini, “Je, usomi ni kuwa na ‘degree’ moja? Kama hivyo sivyo ni kwa nini wanafunzi wa ‘masters’ wasipewe mikopo na Serikali?”

      Mwanafunzi mwingine wa kutoka SUA alihoji kuhusu mrabaha unaopata Serikali kutoka kwa makampuni makubwa ya madini nchini. Alihoji akisema, “Hivi huu mrabaha wa asilimia tatu umebadilishwa na kuwa asilimia ngapi kwa sasa. Nakumbuka Rais Kikwete aliahidi kurejea mikataba ya madini. Sasa nini kimebadilika?”

      Akijaribu kujibu baadhi ya hoja, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zito Kabwe alisema suala la wanafunzi kuchangia asilimia 40 ya mkopo wa elimu ya juu linaweza kufikishwa mahakamani kutokana na suala hilo kuwa na mahusiano na haki zinazobainishwa katika Katiba ya nchi.

      Kwa upande wake, Mkurugenzi wa vijana wa Chadema, John Mnyika alisema kwa sasa CHADEMA inaandaa katiba mbadala ya nchi na kwamba rasimu hiyo itakapokamilika itawasilishwa serikalini kabla ya mwaka 2009. Kabla ya kuanza kwa uchaguzi mkuu wa Serikali za mitaa.
      Ni wakati wa Mabadiliko ya Kweli; tuwajibike!
      Napatikana pia kupitia Facebook, Twitter na mnyika.blogspot.com

    14. #14
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,940
      Rep Power : 6971
      Likes Received
      1102
      Likes Given
      36

      Default

      Mnyika: ushukuriwe kwa habari hizi motomoto. Furaha yangu ni jinsi chadema ilivyoitikia wito wa wanaforum hii hasa mzee mwanakijiji; kwamba badala ya kulalamika CCM kuwatumia wanachuo, nasi twende hukohuko, tuingiza wanachama kutoka vyuo. Naamini huu moto uliowashwa hauzimiki. Hakuna kulala.

      You have really made my day!
      A Struggle Without Casualties is No Struggle-Steve Biko

    15. #15
      Ben Saanane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th January 2007
      Posts : 6,946
      Rep Power : 45017
      Likes Received
      5319
      Likes Given
      6535

      Default

      Safi sana,wasomi ni kuwafuata huko huko.Sisi huku kazi tunaimaliza sasa ingawa tuna tatizo kidogo la communication na huko nyumbani.
      Tutarajie Mabadiliko makubwa 2010.

    16. #16
      John Mnyika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th June 2006
      Location : Tanzania
      Posts : 926
      Rep Power : 13542
      Likes Received
      1096
      Likes Given
      11

      Default CHADEMA: Tusichanganye elimu na Siasa

      JUMAMOSI, wiki iliyopita, Kurugenzi ya Vijana ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), iliandaa kongamano la siku moja la wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Morogoro, kujadili hali ya elimu ya juu na siasa hapa nchini, lililofanyika katika Shule ya Sekondari Forest Hill. Katika kongamano hilo, baadhi ya viongozi wa chama hicho walitoa mada mbalimbali zilizokuwa zikikosoa utendaji wa serikali.

      Wa kwanza kuzungumza alikuwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbrod Slaa, ambaye pia ni Mbunge wa Karatu mkoani Manyara.

      Dk. Slaa anasema hali ya mambo ndani ya serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) si nzuri, watu hawana uhuru ndani ya chama hicho, na baadhi ya watendaji serikalini wanashindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo kwa kuhofia kushughulikiwa na chama.

      Anasema hali hiyo imewakuta hata wabunge wa chama hicho - wasomi na wasio wasomi - walioshindwa kufanya kile walichotumwa na wananchi wao, na badala yake wanafanya kile wanachotumwa na chama chao, hata kama kinaliumiza taifa pamoja na wananchi.

      Dk. Slaa anasema utendaji kazi wa wabunge wasomi wa CCM ndani ya Bunge unawafanya waonekane tofauti kabisa na kiwango cha elimu walichonacho - wengi wanaonekana kama watu walionunua vyeti tu.

      “Maana ya msomi ni kutumia elimu yako kulisaidia taifa lako…cha ajabu ni kwamba tunao wasomi wengi tu ndani ya Bunge. Tuna maprofesa wengi, lakini hawaitumii elimu yao katika kutimiza kazi zao za ubunge na badala yake wanashiriki kuligeuza Bunge kuwa muhuri wa kupitisha mambo ya ajabu kabisa.

      “Kuna wanasheria wenye vyeti vizuri tu ambao ni wabunge wa CCM ndani ya Bunge, lakini ni hawa ndiyo waliodiriki hata kusaliti taaluma zao kwa sababu ya itikadi. Wanauza nchi yao kwa sababu ya itikadi za kichama, wanaaibisha misingi ya taaluma zao kwa ajili ya kufurahisha chama chao.

      “Huo si usomi, hatuna wasomi bungeni bali kundi la watu wenye vyeti. Sifa ya msomi ni kusimamia matakwa ya taaluma yake, kushauri kwa manufaa ya taifa. Mimi nawashauri ninyi wasomi, mkihitimu shahada zenu, msikimbilie CCM, huko mtakwenda kushiriki kuua nchi, hakuna uhuru wa kujieleza huko, njooni CHADEMA tujenge taifa kwa kutumia usomi wetu,” anasema Dk. Slaa.

      Anatoa mfano wa Thomas Nyimbo (CCM) kuwa aliwahi kupigwa marufuku kuzungumza bungeni kwa muda wa miezi 18 na uchaguzi uliofuata hakurudishwa tena bungeni kwa sababu wakubwa ndani ya CCM walimchukia.

      Dk Slaa anatahadharisha kuwa wengi wa watu wanaojiita wasomi walio CCM wanapigana vikumbo kuwania ubunge kwa ajili ya kutafuta maslahi.

      “Ninawaambieni ukweli kuwa wanaojiita wasomi ndani ya CCM wanakimbilia huko kwa ajili ya kutafuta maslahi, si kuitumikia na kuijenga nchi yao, ndiyo maana kila siku utasikia wanalilia kuongezwa mishahara na marupurupu, na ukweli mishahara ya wabunge ni mikubwa mno si siri.” Anasema.

      Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, aliyetoa mada kuhusu nafasi ya wasomi katika kutetea haki za wanyonge na wajibu wa serikali kwa wanafunzi wa elimu ya juu, anasema serikali inatekeleza kinyume na sheria ilizozitunga.

      Anasema sheria inaitaka serikali kuwasomesha wanafunzi wote waliochaguliwa na kukubaliwa kujiunga na mosomo ya elimu ya juu, lakini kinyume chake imeweka utaratibu unaopingana na sheria hiyo wa kuwasomesha wanafunzi wanaopata daraja la kwanza la na pili tu.

      “Serikali yoyote inayoshindwa kuwasomesha wananchi wake haina haki ya kukusanya kodi. Na kama haina haki ya kukusanya kodi, basi serikali hiyo haifai kuwapo madarakani kabisa, kwa sababu hakuna serikali iliyoko madarakani isiyokusanya kodi.

      “Rais Jakaya Kikwete alipokutana na wanafunzi wa elimu ya juu Diomond Jubilee, aliwaahidi kuwa suala la mikopo litaangaliwa na hakuna mwanafunzi atakayerudishwa nyumbani kwa kukosa ada ya shule. Lakini sasa serikali yake inawafanyia kinyume kabisa wanafunzi hao hao ambao kwa mdomo wake, aliwaahidi kuwa atahakikisha wanasoma.

      “Ni Kikwete huyu huyu anayesifiwa kwa kumaliza migogoro ya wasomi bila kutumia FFU tofauti na Mkapa ambaye hakuwa na simile, kama ni hivyo basi Rais Kikwete ni hatari zaidi kuliko Mkapa kwa sababu huyu anaua taratibu, anakuua huku anacheka,” anasema Kabwe.

      Anasema wanafunzi wanapaswa kubadilika na kuwa na moyo wa kijasiri wa kuikosoa serikali, vinginevyo haki zote za wanafunzi hao zitazuiwa na serikali iliyokwishaonyesha kutokujali umuhimu wa taifa kuwa na wasomi wake kwa kukataa hata kuwalipia ada.

      Anaeleza kuwa wasomi wa Tanzania pamoja na kuwa katika wakati mgumu kwa kubanwa na serikali inayotaka kuvifanya vyuo vikuu nchini kuwa kama taasisi zake, ni lazima watambue kuwa wao ndiyo chachu ya kufanyika kwa mapinduzi ya kuelekea katika maendeleo ya kweli ya taifa linalozidi kumonyonyoka.

      “Mapinduzi yote duniani yanafanywa na wasomi wa vyuo vikuu, lakini hapa kwetu hali ni tofauti. Wasomi wengi wanakimbilia kuchukua kadi za CCM…jipangeni kwa ajili ya kupigania haki zenu, hata kama hamuwezi kuingia barabarani kuandamana kwa ajili ya kudai hiyo haki yenu na ya wananchi wengine, jitihadini sauti zenu kama wasomi zisikike kwa ajili ya ustawi wa taifa letu,” anasema Kabwe.

      Mbunge wa Viti Maalumu, Suzane Lyimo, aliyetoa mada kuhusu hali ya elimu ya juu nchini, anasema hali ni mbaya na taifa linaelekea katika shimo la umaskini wa elimu.

      Anawataka wanafunzi wapaze sauti zao kueleza matatizo yao na wasisite kuungana na wanaharakati wengine vikiwamo vyama vya upinzani kuikosoa serikali hasa kwa kufanya maandamano ya amani.

      Anasema wasomi wanapaswa kuanza sasa kupaza sauti zao baada ya serikali kuonyesha nia ya kutotaka kufuata sheria za nchi kwa kuwasomesha wanafunzi wote waliochaguliwa na kuthibitika kuwa wanazo sifa za kujiunga na chuo kikuu.

      “Mazingira ya elimu ya juu yanasikitisha, hakuna semina zinazosaidia kuwajengea wanafunzi ujasiri wa kusimama mbele ya hadhara na kujieleza au kuzungumzia jambo lolote kama wasomi wanaopaswa kuwa viongozi wa wengine.

      “Idaini serikali haki zenu, andamaneni kwa ajili ya kutetea haki zenu pamoja na haki nyingine za kijamii serikali inazowakatili wananchi, kuna ‘usanii’ mwingi sana katika sekta ya elimu unaofanywa na serikali, lakini wasomi mko kimya mnaangalia tu, mnashiriki kuliangamiza taifa.

      “Angalieni mpango wa MMEM na MMES, kweli ni mzuri lakini bila kupanua vyuo vikuu hauna maana, shule za sekondari ndizo zinazobadilishwa kuwa vyuo vikuu, sasa hao wanafunzi wa sekondari watasomea wapi?

      “Walimu wanaofundisha wadogo zenu ni wale waliofeli sekondari, wamepigwa msasa wa miezi kadhaa, wanakabidhiwa jukumu kubwa la kuwa walimu, hiyo ndiyo mipango wa serikali, wanafanya hivyo kwa sababu wanajua hao waliofeli watakubali kwenda kufundisha mahali popote. Ni upuuzi, hakuna elimu hapo, shule zinajengwa kwa malengo ya kisiasa, si kwa nia ya dhati ya kupambana na adui ujinga,” anasema Lyimo.

      Lyimo, Waziri Kivuli katika Bunge la Jamhuri ya Muungano, anasema serikali kwa kutambua unyonge wa wanafunzi, imeamua kuwabana ili wachangie asilimia 40 ya gharama za masomo, jambo lililo kinyume cha sheria.

      Anasema serikali inaidharau sekta ya elimu na afya na kuithamini sekta ya ulinzi. Jeshi la ulinzi limekuwa likitengewa fedha nyingi kila mwaka na hakuna Mtanzania anayejua fedha hizo zinatumika kwa kazi ipi, wakati taifa haliko katika vita.

      “Mnachangia asilimia 40, lakini bado kuna wanafunzi wanawasikiliza wahadhiri wakiwa nje ya madarasa,” alisema Lyimo huku akishangiliwa na umati mkubwa wa wanafunzi hao na kuendelea kuwa.

      “Serikali inawadanganya, eti mnachangia, huo ni uongo kwa sababu baadaye huo mnaoambiwa kuwa ni mchango mnalazimika kuulipa…tunajua mnaonewa na mnasoma katika mazingira magumu na wenzenu wengi serikali imekataa kuwasomesha wakati wana sifa za kusoma vyuo vikuu.

      “CHADEMA tumeliona hilo, tunathamini elimu, wale wote waliokataliwa ufadhili na serikali tuleteeni majina yenu, hata kama kuna ndugu yako ana tatizo hilo, mwambie alete jina lake, tutaona jinsi ya kumsaidia ili asome,” anasema Lyimo, huku akishangiliwa kwa nguvu zaidi na wanafunzi hao.

      Akielezea jitihada zake za kupigania maslahi ya wanafunzi wa elimu ya juu, Lyimo anasema aliiomba serikali iongeze fedha za posho wanazopewa wanafunzi hao kutoka sh 2,500 hadi sh 5,000, kwa siku na serikali iliongeza hadi sh 3,500, kiasi alichosema kuwa bado hakitoshi na ataendelea kuipigania sh 5,000 ya posho ya kila siku hadi hapo serikali itakaposalimu amri.

      Pia anataja jambo jingine analoendelea kulipigania kuwa ni nyongeza ya posho ya siku kwa wanafunzi walio katika mazoezi kwa vitendo, kwamba sh 6,000 wanazopewa sasa hazitoshi na ameiomba serikali iongeze walau iwe sh 10,000, jambo alilodai kuamini kuwa serikali italiafiki hivi karubini.


      Source: Tanzania Daima Makala -CHADEMA: Tusichanganye elimu na siasa
      Ni wakati wa Mabadiliko ya Kweli; tuwajibike!
      Napatikana pia kupitia Facebook, Twitter na mnyika.blogspot.com

    17. #17
      Kazi Ndiyo Kipimo Cha Utu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th March 2006
      Posts : 1,726
      Rep Power : 1026
      Likes Received
      55
      Likes Given
      6

      Default

      Wanaotaka msaada wa kusomeshwa na Chadema kama ilivyoelezwa na Mh.Bi Suzanne Lyimo majina yapelekwe wapi?Mtu yeyote mwenye email yake ambayo anafungua kila siku na kuangalia barua ,Tafadhali naomba aiweka hapa.

    18. #18
      Kadogoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2007
      Location : Moshi
      Posts : 1,957
      Rep Power : 953
      Likes Received
      263
      Likes Given
      567

      Default

      Quote By mwanasiasa View Post
      Kadogoo: this is also so cheap and low! Kwanza utafiti gani huo wa chinichini hata uitwe utafiti? Pili, yaani hadi leo huwezi kuelewa kuwa kupiga kura ni jambo la mtu binafsi tena la siri? Sasa kama viongozi walikubaliana kuachiana majimbo, haina maana kwamba waliwanyan'ganya wanachama wao (wananchi) uhuru wa kuwachagua watu walio wataka! Ndugu yangu, nenda juu kidogo, hii forum hii ni jukwaa kubwa la hoja nzito na pana!
      MWANASIASA,
      Baada ya uchaguzi wa 2000 CUF tuligunduwa kuwa CHADEMA walitudanganya kuwa tushirikiane na kuachiana majimbo lakini cha kushangaza ni kuwa ktk vituo vya kupigia kura kwa mfano kama waliojiandikisha kupiga kura ktk kituo A ni watu 110 halafu wakati wa kupiga kura wakaja watu 100 tu kati ya 110, kura zilipohesabiwa matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:hapa CHADEMA hawakuweka mgombea kwa sababu makubaliano yalikuwa kura zao wampe mgombea urais toka CUF na matokeo yalikuwa kama ifuatavyo: CCM(80), CUF(15), TLP(5), UDP(1) halafu matokeo ya kura za wabunge (hapa CUF hawakuweka mgombea kwani aliyekuwa na ushawishi kwa wananchi wengi alikuwa mgombea wa CHADEMA!)na makubaliano ya CUF na CHADEMA yalikuwa kuachiana majimbo pale patapoonekana mgombea wao anakubalika na matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:CHADEMA(75), CCM(20), TLP(4), UDP(1)!!!

      Sasa huu ni upuuzi mtupu na utapeli tuliofanyiwa na wenzetu CHADEMA sasa kama tulikubaliana kura za urais apewe mgombea wa CUF na za ubunge apewe CHADEMA mbona ktk matokeo yameonyesha kuwa CHADEMA walimpa kula mgombea wa CCM ktk urais badala ya CUF na ktk kura za ubunge CHADEMA pamoja na CUF wote walimpa kula mgombea wa CHADEMA? huu ni ulagai kabambe uliofanywa na CHADEMA dhidi ya CUF kwani walitutumia kwa maslahi ya CCM! kwani kama kweli CHADEMA walikuwa na dhamira ya upinzani basi kura zao wasingewapa CCM! na hapa nawafahamisha nyie munaohoji utafiti huu tumeupata wapi! kwa mujibu wa sheria ya uchaguzi kura zinatakiwa kuhesabiwa ktk vituo vya kupigia kura na matokeo yasainiwe na wawakilishi wa vyama vyote husika, hivyo sio kazi ngumu kugunduwa utapeli kama huu hata kama upigaji kura hupigwa kwa siri! wewe binafsi huwezi kujulikana umempigia nani lakini matokeo ndiyo yanayoonyesha ni chama gani kimempigia nani!

      Sasa kwa mujibu wa wasimamizi wetu ktk vituo vya kupigia kura na CHADEMA kukataa kushirikiana na wapinzani ktk uchaguzi wa 2005 tunadiriki kusema kuwa CHADEMA ni CCM ndogo!

    19. #19
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,048
      Rep Power : 2571
      Likes Received
      794
      Likes Given
      29

      Default

      Unajua wewe kadogoo unachekesha sana .Kuacha kujipanga kwenu ndiyo kunapelekea mahita na CCM kuwapiga bao kali sana na leo mnalia na Chadema . CUF ni cha ambacho kina nguvu Zanzibar na huongelea mambo ya Wazanzibari muda wote . Ni Chadema kule Visiwani kina watu na uongozi kuonyesha kwamba kipo lakini ukweli ni kwamba hakipo sana kule .CUF ni chama cha wenye vikofia na Hijab ni kosa kubwa sana kwa Chama kama Chadema wataamua kuuza utu wao na kujitumbukiza kwenye matatizo. Sasa you are being set up by CCM na muafaka ngoja mpigwe bao huko baadaye mkiamka basi mtakuwa mmechelewa .Poleni sana .

    20. #20
      Kubwajinga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd January 2008
      Location : Ilala, Tanzania 10001
      Posts : 1,647
      Rep Power : 713
      Likes Received
      72
      Likes Given
      135

      Default Mseto hapana - CHADEMA

      Hivi vyama vinatakiwa viungane, bila ya hivyo sauti zao zitakuwa sawa tu na kelele za mlango zisizozuia mtu kulala.





      Mseto hapana - CHADEMA

      2008-05-07 09:03:59
      Na Richard Makore



      Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema hakiungi mkono hatua ya chama cha CUF kutaka iundwe serikali ya mseto visiwani Zanzibar.

      Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho, Bw. Chacha Wangwe.

      Bw. Wangwe alisema, anashangaa kuona CUF wakikazania kuundwa kwa serikali ya mseto badala ya kuking`oa CCM madarakani kabisa.

      CHADEMA ni miongoni mwa vyama vinne vyenye ushirikiano wa kisiasa ambapo vingine ni NCCR- Mageuzi, CUF na TLP.

      Alisema CHADEMA na vyama vingine vya upinzani lengo lao ni kuweka mikakati ya kuing`oa CCM na sio kutaka iundwe serikali ya mseto itakavyovishirikisha.

      Aliwaambia waandishi wa habari kuwa, licha ya vyama hivyo kuwekeana makubaliano ya ushirikiano wa kisisa lakini kila chama kina sera zake.

      Alisema msimamo wa CHADEMA ni kuhakikisha wanakiondoa madarakani CCM au kuongeza idadi ya wabunge.

      Bw. Wangwe alilazimika kutoa ufafanuzi huo baada ya kuulizwa swali kama vyama vyenye ushirikiano wa kisiasa vinaunga mkono CHADEMA katika maandamano ya kuishikiza serikali kumilikisha wananchi ardhi.

      Alisema CHADEMA kitazunguka nchi nzima peke yake na kuwashirikisha wadau mbalimbali wa ardhi.
      • SOURCE: Nipashe

    Page 1 of 9 123 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 1
      Last Post: 19th September 2011, 11:33
    2. Je ni sahihi Spika wa Bunge na Wasaidizi wake wasiwe wanatoka Chama chochote?
      By Laurence in forum Jukwaa la Sheria (The Law Forum)
      Replies: 1
      Last Post: 29th July 2011, 11:32
    3. Replies: 1
      Last Post: 29th July 2011, 11:32
    4. Replies: 1
      Last Post: 10th December 2010, 12:14
    5. Replies: 15
      Last Post: 7th March 2009, 21:06

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...