Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Serikali corrupt, hali yetu na upofu wa viongozi wetu

    Report Post
    Results 1 to 2 of 2
    1. #1
      Profesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : Anywhere in Africa
      Posts : 510
      Rep Power : 750
      Likes Received
      219
      Likes Given
      322

      Default Serikali corrupt, hali yetu na upofu wa viongozi wetu

      Serikali hii sio kiongozi wake la hasha ila watendaji wake ndio watekelezaji wakuu wa uovu huo, na mbaya zaidi ni pale ambapo hawajali hata kama Raisi au kiongozi anadhalilika... ila hawajui kitu kimoja ... yeye hataaathirika... ni kuwa serikali hiyo itaangamia na watu wake maana walio wengi ndio masikini na wenye kipato cha chini na ndio wapiga kura na sio wachache hivyo nguvu ya pesa haiwezi kamwe kushinda nguvu ya ...

      Ninamaanisha watu walioko serikalini hawaoni mbali na hawahangaiki ipasavyo kuweka mfumo wa kweli unaodumu ambapo hata akija raisi wa upinzani bado sera na mipango inabaki palepale kwa sasa wanajisaliti wenyewe bila kujijua...wanagawa viwanja na ardhi tofauti na sheria na taratibu rushwa yako tu...wanatunga na kuweka sera wakiwa mijini ndani ya kiyoyozi huku akili zao zikiwa na sumu za runinga bila kujali maslahi ya mila, desturi, jamii na hali halisi ya mtu wa kijijini mkulima wa chini na mfugaji wa asili.

      Mfano, wanapowalazimisha wafugaji kuacha uchungaji wa kuhamahama wanaangamiza mila na desturi zetu wanaua indiginous technologies (ufundi wa asili wa kisayansi wa mf matibabu, utabiri wa hali ya hewa, ubashiri wa majanga n.k), wanatoa nafasi serikalini hata idara nyeti kitaifa na za kisiasa kwa ndugu jamaa na ... bila kujali uwezo, wao watoto wao wanakwenda shule za st... academia... ambazo ada zake na mishahara yao halali havina uwiano, wanahudumiwa India na... na wanapopanga sera za Elimu na Afya wanaamini kila mtanzania ana uwezo kama wao, wana uhakika wa mlo wa siku kwa hiyo mifumuko ya bei na hali ngumu ya watu kwao inachukua muda kuwagusa maana wasipokula nyumbani watakula kwenye wekishopu ambapo mlo wa mtu mmoja unawea kuwa mlo wa familia nzima pale Tandale kwa Mfuga Mbwa, wana amini uwezo wa kulindana kwa hiyo hawana hofu na wewe. THIS IS CORRUPTION!

      Hizi ndio serikali nyingi Africa ambazo hazioni kizazi cha sasa kinachokuja ambacho hakijaathirika na sumu za Nyerere wala za Kwame wao wanaamini wanachoamini na wana nafasi ya kuuona ulimwengu kuliko mimi na wewe ambao technohama ilikuja kama mazingaombwe na ikatuchukua muda kuamini kuwa ni kitu real. Wao wamezaliwa nacho na wana spidi yakukijua na kukitumia kuliko mimi nawewe. Je Wazee wa serikali hizi wanalijua hili. HAWA NDIYO WAPIGA KURA WA 2015 kwa Tanzania na kwa nchi nyingine kutegemeana na tarehe zao za uchaguzi.

      Kama ataibuka kiongozi na si mtawala anaejua tofauti zetu wote kisiasa, kiutamaduni, ki-kizazi na hata kijamii basi akanena yale yanayoweza kutufanya tuamke natuhamasike kufanya mambo yetu yenye kuteletea maendeleo yetu, hapo ndipo tutakapokuwa na matumaini. Asieamini uwekezaji bali uwezeshaji ili watu waweze kutumia na kuvuna rasili mali zao wenyewe kwa manufaa yao wenyewe, ambaye anasimamia majadilianho sawa na mataifa ya nje katika maslahi, mwenye kijali kizazi kijacho na si cha sasa tu. Sio aliyekuwa brainwashed na mataifa malafi kwa consept ya 'uwekezaji' yenye baraka za 'taxi holiday' na milungula inayolingana na mishahara yooote na viinua mgongo vyoote kwa viongozi wahusika.

      Kwa sasa nchi nyingi za Africa hazina viongozi zina watawala, NA HILO NDILO LINALOPELEKEA MAPINDUZI KWA STAILI ZAKE MBALIMBALI.
      Last edited by Profesa; 2nd April 2012 at 19:22.
      Sungurampole likes this.

    2. Study Abroad

    3. #2
      Sungurampole's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 17th November 2007
      Posts : 704
      Rep Power : 728
      Likes Received
      121
      Likes Given
      555

      Default re: Serikali corrupt, hali yetu na upofu wa viongozi wetu

      Profesa umunena asante kwa uwasilishaji wa mada mzuri - simple and straight forward. Shida iko kwa viongozi wetu uliowalenga sijui kama wanasoma, na hata wakiisoma zaidi sana watakuwa busy kuona kama waweza kukusakizia vyombo nyeti vya umma vikunyamazisha.

      Wao wako zaidi kwenye message za umbea na ndiyo maana hii thread haina michango, ingekua ya umbea au any business as usual issue reply zingekuwa zinazidi 1000 hadi leo. Cha kusikitisha zaidi hii thread iko jukwa mahsusi la great thinkers.

      Umesema vema kuhusu kutojali kwa viongozi wetu na uvivu wakufikiri walionao japo hawapendi kuitwa dhaifu, nimeyanena pia katika thread zangu za karibuni - Mnyika umesema wao wamethibitisha na udhaifu na ushupavu wa voingozi wetu na ile ya mgomo wa MAs

      ukweli ni kuwa siku za viongozi wa sampuli hii zinaheasabika
      Profesa likes this.
      There is a higher court than courts of justice and that is court of conscience.

      It supersedes all other courts.
      Mohandas Gandhi

    4. Miaka 50

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...