Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Sitta autamani Urais 2015

    Report Post
    Page 1 of 5 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 92
    1. #1
      Superman's Avatar
      JF Tanzanite Member Array
      Join Date : 31st March 2007
      Location : On Move
      Posts : 5,421
      Rep Power : 1823
      Likes Received
      1415
      Likes Given
      1216

      Default Sitta autamani Urais 2015

      Please note: Huu si Mkenge wa April's Fools Day. Akili zako changanya na za Mbayuwayu!

      Source 1:
      Sitta atangaza nia kuwania urais ‘akiombwa’ | FikraPevu.com

      Source 2:
      Sitta kugombea Urais 2015

      Source 3:http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=28475 (Sitta: Ninafaa Urais)

      * ATAKA KUONGOZA MIAKA MITANO AWAACHIE VIJANA


      Na Sheilla Sezzy, Mwanza

      MWANASIASA machachari ambaye pia ni Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu ujao mwaka 2015 na kutamba kuwa ana nafasi nzuri kutokana na sifa alizojijengea ndani ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi(CCM).

      Sitta alitaja sifa hizo kuwa ni pamoja ile ya kuwa mteule wa rais, kwa awamu zote nne za uongozi taifa, tangu Tanzania ilipotaka uhuru wake, Desemba 9 mwaka 1961.

      Spika huyo mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , alisema kwa sasa anawasikiliza wananchi kama wataona anafaa na haoni ubaya wowote wa kushika nafasi hiyo ya juu katika uongozi wa taifa kwa miaka mitano tu na kuwaachia vijana waendelee.

      “Mimi nawasikiliza wananchi kama wataona nafanana na rais wanayemtaka, basi nitachukua maamuzi kwa wakati huo. Sioni ubaya wowote kama wakiniachia kuongoza nchi hii hata kwa miaka mitano halafu niwaachie vijana waendelee,”alisema Sitta.

      Alisema kuwa ifikapo mwanzoni mwa mwaka 2014, kila kitu kitakuwa wazi na haweza kukataa majukumu atayopewa na wananchi wake kwani anatambua wanamuamini kwamba ana uwezo wa kuchapa kazi.

      Sitta ambaye pia ni Mbunge Urambo Mashariki na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa( NEC) ya CCM, aliyasema hayo jana muda mfupi kabla ya kupanda jukwaani kufunga kampeni za udiwani za CCM, Kata ya Kirumba.

      Mwanasiasa huyo ambaye umaarufu wake umepanda kwa kasi katika miaka ya hivi karubuni kutokana na msimamo wake wa kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi ndani ya CCM, alitamba kuwa amefanya mambo mengi ndani ya Serikali ya CCM, ambayo yamesaidia kuleta mageuzi makubwa nchini.

      Alisema kadri siku zinavyokwenda rais wa Tanzania atajulikana kwa matendo yake na kubainisha kuwa mtu mbaya hawezi kubadilika kuwa mzuri kwa kipindi kifupi.

      “Sioni sababu ya mtu kuutafuta urais wakati wananchi wanaona na wanajadili kila siku ni rais wa aina gani wanayemuhitaji kutokana na mahitaji yao,”alisema

      Alisema anachofanya kipindi hiki ni kutimiza wajibu wake na wananchi ni mashahidi kila nafasi anayopewa, anatimiza wajibu wake ipasavyo na kusisitiza kuwa amefanya mengi yanayoonekana machoni pa watu na kudhihirisha kwamba ni kiongozi bora.

      Akizungumzia umri wa urais, alisema mijadala kuwa vijana hawawezi kuongoza haina msingi. Alifafanua kuwa kiongozi mzuri ni yule mwenye uwezo wa kuwaongoza wananchi na kuwaletea maendeleo.

      Alisema rais anachaguliwa na wananchi hivyo maamuzi yote ya nani anafaa kwa nafasi hiyo na umri upi, ipo mikononi mwa wananchi wenyewe.

      Katika hatua nyingine Sitta, aliwashangaa wanasiasa wanaopigana vijembe majukwaani na kueleza kwamba tabia ya kumtukana mtu mmoja mmoja, haina maana yoyote.

      Aliwashauri viongozi wa CCM kutojibu mapigo ya wapinzani na kuwataka kutumia busara kila wanapokutana na kauli chafu kwani nia ya kudumisha amani ya nchi.

      Alionya kuwa amani ya nchi ikitoweka, itakayobebeshwa lawama ni CCM na Serikali yake.

      “Kauli nyingi za majukwaani zinachochea chuki miongoni mwa wananchi, matokeo yake zinaweza kuibua machafuko na waathirika watakuwa wananchi wenyewe, tena wale wasio na uwezo wa kujiokoa,’’ alisema Sitta.

      Alisema kuwa katika miaka 50 ya utawala wa CCM, kuna mambo mengi yamefanyika na kwamba wapinzani hawana haja kubeza kwani yanaonekana kwa macho.

      Alisema kuwa katika mafanikio hayo, kuna mengi yamefanywa na Rais Jakaya Kikwete, mfano mzuri ni kampuni tano za madini kulipa kodi na wananchi kuanza kufaidika na rasilimali za nchi yao.

      Hofu ya mahasimu wake

      Akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali katika Tamasha Vyombo vya Habari lililofanyika wiki iliyopita kwenye Ukumbi Msasanki Beach, Dar es Salaam, Sitta alieleza kuwa anashangazwa na watu wanaoweweseka wakisikia anataka kuwania urais mwaka 2015.

      "Nashangaa watu wanapata kiwewe kusikia nataka kuwania urais, kuwania urais ni haki ya kila Mtanzania na Watanzania ndiyo watakaoamua nani ni mzuri na atawafaa," alisema Sitta na kushangiliwa na waliohudhuria tamasha hilo.

      "2015 tunataka kuwa na mwelekeo mzuri, nikiwa na maana mambo ya hongo, ubadhirifu hatutaki yawe na nafasi, alisema Sitta na kuongeza:

      Alisema watu wanatumia fedha nyingi kusaka urais na hata wengine kutumia ndumba kwa kwenda Mlingotini, Bagamoyo, kwa nia ya kutaka uongozi na matokeo yake wanaposhinda lengo lao la kwanza linakuwa kurudisha fedha walizotumia.

      Source:
      Sitta kugombea Urais 2015

      MY TAKE:
      Kwa Changamoto za leo ambayo Nchi Yetu inazo, bado Mh. Samuel Sitta hana uwezo wa kuleta mageuzi ya Kimaendeleo katika Tanzania. Alipata mafasi kamili kama Kiongozi wa moja Mhimili kamili wa Kikatiba kama Spika wa Bunge kusimamia kuondoa uovu kikamilifu pamoja na Ufisadi Mwingine lakini akaamua kukumbatia uovu kuinusuru serikali yake ya CCM.

      Japo anaweza kuwa anakubalika na baadhi, Mzee Sitta hawezi kuwa udhubutu wa kutupa Tanzania tunayoiota, na hata huko Wizara ya Afrika ya Mashariki bado hatujaziona cheche zozote.
      Pasco, bucho and Pelekaroho like this.
      Kwa kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wanyonge . . . . . . “Ni heri kutoa kuliko kupokea”


    2. #2
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,661
      Rep Power : 1345
      Likes Received
      796
      Likes Given
      663

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Kwa upande wangu nasema hakuna ccm kama sita,afadhari yeye anaweza kuliko hao wengine,labda tumpe magufuri tatizo tu huwa hatupendi kuambiwa ukweli

      Lakini ccm ya leo sitta ama magufuri ndio wanaweza angarau kutusogeza
      rmashauri likes this.

    3. #3
      nimie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2011
      Location : Humu humu
      Posts : 516
      Rep Power : 500
      Likes Received
      97
      Likes Given
      96

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Hana akili! angekuwa mjanja angepigania kuwepo kwa mgombea binafsi, sasa anafikiri atapitia wapi? Kwa hicho chama chake hawampitishi. Akisumbua sana ataondolewa kwa zengwe lile lile la zamu ya kina mama na Asha Migiro atasimamishwa. Labda arudi CCJ.
      Chakunyuma likes this.
      Think Big - by Ben Carson

    4. #4
      nyabhingi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th October 2010
      Posts : 3,276
      Rep Power : 1305
      Likes Received
      1387
      Likes Given
      2703

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      na leo ni siku ya wajinga

    5. #5
      nimie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2011
      Location : Humu humu
      Posts : 516
      Rep Power : 500
      Likes Received
      97
      Likes Given
      96

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Quote By engmtolera
      Kwa upande wangu nasema hakuna ccm kama sita,afadhari yeye anaweza kuliko hao wengine,labda tumpe magufuri tatizo tu huwa hatupendi kuambiwa ukweli

      Lakini ccm ya leo sitta ama magufuri ndio wanaweza angarau kutusogeza
      Magufuli naye asingekuwepo hapo alipo kama sio nafasi yake kwa jinsi alivyojijenga kwa wananchi. Na ili agombee lazima apitishwe na chama, tatizo "wenye chama walioshika hatamu" hawamtaki. Na mbaya zaidi amejiingiza mno kutangaza chama badala ya wa utendaji wa serikali, hivyo basi amelipunguza kundi la kati lililokuwa likimuunga mkono.
      Chakunyuma likes this.
      Think Big - by Ben Carson


    6. #6
      Mshuza2's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th December 2010
      Posts : 1,310
      Rep Power : 692
      Likes Received
      201
      Likes Given
      17

      Default

      Sitta yuko sahihi kuweka wazi nia yake hiyo,tatizo ni mfumo uliopo ndani ya CCM,uongozi wa mtandao! angalau kidogo ana uthubutu wa kuzungumzia yale mabovu ya ndugu zake!

    7. #7
      mbwagison's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th February 2012
      Posts : 51
      Rep Power : 382
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By nimie
      Hana akili! angekuwa mjanja angepigania kuwepo kwa mgombea binafsi, sasa anafikiri atapitia wapi? Kwa hicho chama chake hawampitishi. Akisumbua sana ataondolewa kwa zengwe lile lile la zamu ya kina mama na Asha Migiro atasimamishwa. Labda arudi CCJ.
      Hana ubavu! Akiwa Spika wa bunge hakututendea haki hata kidogo! aliuzima mjadala wa Richmond kidikteta, je alihongwa ahadi ya kugombea Urahisi 2015? huyu mtu ni hatari sana!

    8. #8
      Stoudemire's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2012
      Posts : 317
      Rep Power : 428
      Likes Received
      64
      Likes Given
      237

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      April fools

    9. #9
      KIM KARDASH's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2011
      Posts : 4,254
      Rep Power : 0
      Likes Received
      565
      Likes Given
      56

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Watanzania kama tunataka rais mzalendo basi ni huyu!NA KUWEKA WAZI MAPEMA NI KUJIAMINI KWA UADILIFU,WANAOJIFICHA SIO WAADILIFU NDIO MANA WANAOGOPA KUJITOKEZA MAPEMA,HONGERA MZEE SIX,JAPO SAFARI HII NI ZAMU YA ZANZIBAR SIJUI ITAKUWAJE TUTAJUA MBELE!

    10. #10
      ITEGAMATWI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th January 2012
      Posts : 1,814
      Rep Power : 809
      Likes Received
      478
      Likes Given
      914

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Dah!Leo nakuwa mzito sana kukubaliana na habari yeyote ile maana nyingi ni za kusherehekea sikukuu ya wajinga!Kama ni kweli haya basi yetu macho tu!!

    11. #11
      busar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd December 2011
      Posts : 353
      Rep Power : 448
      Likes Received
      40
      Likes Given
      0

      Default

      We unadhan nani anafaa? Lowasa?

    12. #12
      Ilongailunga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th January 2012
      Posts : 60
      Rep Power : 386
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Samuel Sitta ni mtu ambaye ameitumikia serikali ya CCM zaidi ya nusu ya Umri wake wote, na yeye alikuwa mwanamtandao.Inasikitisha sana watu kuhadaiwa eti Sitta anapinga ufisadi, Sitta anatumia neno ufisadi kwa maslahi ya kisisiasa na pia kuwachafua wapinzani wake kisiasa. Si ndo huyu Sitta alipopata nafasi ya kuwa kiongozi wa serikali bungeni povu lilimtoka kuwashambulia na kuwadharilisha wapinzani,na kuitetea serikali na chama kwa kuviita "waadilifu" na wasikivu? mnaomshabia huyu gamba opportunist ni vema muangalie na mtathmini misimamo yenu ya kisisiasa.
      LIAMA likes this.

    13. #13
      Ilongailunga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th January 2012
      Posts : 60
      Rep Power : 386
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Samuel Sitta ni mtu ambaye ameitumikia serikali ya CCM zaidi ya nusu ya Umri wake wote, na yeye alikuwa mwanamtandao.Inasikitisha sana watu kuhadaiwa eti Sitta anapinga ufisadi, Sitta anatumia neno ufisadi kwa maslahi ya kisiasa na pia kuwachafua wapinzani wake kisiasa. Si ndo huyu Sitta alipopata nafasi ya kuwa kiongozi wa serikali bungeni povu lilimtoka kuwashambulia na kuwadharilisha wapinzani,na kuitetea serikali na chama kwa kuviita "waadilifu" na wasikivu? mnaomshabia huyu gamba opportunist ni vema muangalie na mtathmini misimamo yenu ya kisiasa.
      LIAMA likes this.

    14. #14
      Ilongailunga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th January 2012
      Posts : 60
      Rep Power : 386
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Samuel Sitta ni mtu ambaye ameitumikia serikali ya CCM zaidi ya nusu ya Umri wake wote, na yeye alikuwa mwanamtandao.Inasikitisha sana watu kuhadaiwa eti Sitta anapinga ufisadi, Sitta anatumia neno ufisadi kwa maslahi ya kisiasa na pia kuwachafua wapinzani wake kisiasa. Si ndo huyu Sitta alipopata nafasi ya kuwa kiongozi wa serikali bungeni povu lilimtoka kuwashambulia na kuwadharilisha wapinzani,na kuitetea serikali na chama kwa kuviita "waadilifu" na wasikivu? mnaomshabia huyu gamba opportunist ni vema muangalie na mtathmini misimamo yenu ya kisiasa. Even if it is a fools day We cannot be fooled by cheap politics of Sitta and co.

    15. #15
      Precise pangolin's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 4th January 2012
      Posts : 5,756
      Rep Power : 1930
      Likes Received
      1609
      Likes Given
      684

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Hizi thread za tarehe 1/4/2012 bora nichangie za jana

    16. #16
      Superman's Avatar
      JF Tanzanite Member Array
      Join Date : 31st March 2007
      Location : On Move
      Posts : 5,421
      Rep Power : 1823
      Likes Received
      1415
      Likes Given
      1216

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Source: http://www.habarileo.co.tz/kitaifa/?n=28475

      Sitta: Ninafaa urais

      Imeandikwa na Grace Chilongola, Mwanza; Tarehe: 31st March 2012

      WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, amesema ana vigezo vya kuwa Rais wa Tanzania kutokana na kutimiza wajibu wake vizuri kwa miongo minne iliyopita, kwa kuteuliwa kushika nyadhifa mbalimbali.

      Alisema hayo jana kwenye mkutano na waandishi wa habari mjini hapa, muda mfupi kabla ya kwenda kufunga kampeni za udiwani katika kata ya Kirumba ambapo alisema amefanya mambo mengi katika Serikali ya CCM yaliyoleta mageuzi makubwa.

      Sitta, ambaye kati ya mwaka 1967 na 1969 alikuwa Meneja wa Caltex Oil, na baadaye kushika nyadhifa mbalimbali zikiwamo Katibu wa CCM mikoa ya Iringa na Kilimanjaro, Mbunge, Mkuu wa Mkoa na Waziri, alisema Rais ajaye wa Tanzania atajulikana kwa matendo yake na kusema mtu mbaya hawezi kubadilika kuwa mzuri kwa muda mfupi.

      “Sioni sababu ya mtu kuutafuta urais wakati wananchi wanaona na wanajadili kila siku ni Rais wa aina gani ambaye wanamhitaji kutokana na mahitaji yao,” alisema Waziri Sitta ambaye pia alipata kuwa Mkurugenzi wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).

      Alisema yuko tayari kwa majukumu ambayo atapewa na wananchi kwa kuwa wanamwamini kuwa na uwezo wa kufanya kazi na kwamba yeye atawasikiliza kama wataona anafaa na kuchukua uamuzi.

      Alisema katika kipindi hiki anachokifanya ni kutekeleza wajibu wake na wananchi wenyewe wanaona kuwa kila nafasi anayopewa anafanya kazi ipasavyo na kudai kuwa vipo vitu vingi ambavyo amefanya na vinaonekana machoni mwa watu ambavyo vinamfanya kuwa kiongozi bora.

      Akizungumzia umri wa urais, alisema mijadala kuwa vijana au wazee hawawezi kuongoza haina msingi wowote na kusema kiongozi mzuri ni mwenye uwezo wa kuongoza wananchi na kuwaletea maendeleo.

      Aliendelea kusema kuwa, Rais anachaguliwa na wananchi kwa hiyo uamuzi wote wa nani awe rais na kwa umri gani yako mikononi mwa wananchi wenyewe. Desemba atafikisha umri wa miaka 70.

      Katika hatua nyingine, Sitta alishangaa viongozi wa siasa ambao wanapigana vijembe katika majukwaa ya mikutano ya hadhara na kusema tabia hiyo si nzuri.

      Alisema kauli za majukwaani zinawatia wananchi hasira.
      Kwa kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wanyonge . . . . . . “Ni heri kutoa kuliko kupokea”

    17. bht
      #17
      bht's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2009
      Posts : 9,968
      Rep Power : 2507
      Likes Received
      1439
      Likes Given
      916

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      superman mambo? (i come in peace today...lol?)

      Leo mi nimegundua habari nyingi kwenye magazi ni urongo mtupu
      Superman likes this.

    18. #18
      Young Master's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 22nd December 2008
      Location : Arusha, Tanzania.
      Posts : 6,167
      Rep Power : 7434
      Likes Received
      2133
      Likes Given
      1513

      Exclamation Sitta kugombea Urais 2015

      MWANASIASA machachari ambaye pia ni Waziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Samuel Sitta ametangaza nia ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu ujao mwaka 2015 na kutamba kuwa ana nafasi nzuri kutokana na sifa alizojijengea ndani ya Serikali ya Chama Cha Mapinduzi(CCM).

      Sitta alitaja sifa hizo kuwa ni pamoja ile ya kuwa mteule wa rais, kwa awamu zote nne za uongozi taifa, tangu Tanzania ilipotaka uhuru wake, Desemba 9 mwaka 1961.

      Spika huyo mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , alisema kwa sasa anawasikiliza wananchi kama wataona anafaa na haoni ubaya wowote wa kushika nafasi hiyo ya juu katika uongozi wa taifa kwa miaka mitano tu na kuwaachia vijana waendelee.

      “Mimi nawasikiliza wananchi kama wataona nafanana na rais wanayemtaka, basi nitachukua maamuzi kwa wakati huo. Sioni ubaya wowote kama wakiniachia kuongoza nchi hii hata kwa miaka mitano halafu niwaachie vijana waendelee,”alisema Sitta.

      Alisema kuwa ifikapo mwanzoni mwa mwaka 2014, kila kitu kitakuwa wazi na haweza kukataa majukumu atayopewa na wananchi wake kwani anatambua wanamuamini kwamba ana uwezo wa kuchapa kazi.

      Sitta ambaye pia ni Mbunge Urambo Mashariki na Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa( NEC) ya CCM, aliyasema hayo jana muda mfupi kabla ya kupanda jukwaani kufunga kampeni za udiwani za CCM, Kata ya Kirumba.

      Mwanasiasa huyo ambaye umaarufu wake umepanda kwa kasi katika miaka ya hivi karubuni kutokana na msimamo wake wa kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi ndani ya CCM, alitamba kuwa amefanya mambo mengi ndani ya Serikali ya CCM, ambayo yamesaidia kuleta mageuzi makubwa nchini.

      Alisema kadri siku zinavyokwenda rais wa Tanzania atajulikana kwa matendo yake na kubainisha kuwa mtu mbaya hawezi kubadilika kuwa mzuri kwa kipindi kifupi.

      “Sioni sababu ya mtu kuutafuta urais wakati wananchi wanaona na wanajadili kila siku ni rais wa aina gani wanayemuhitaji kutokana na mahitaji yao,”alisema

      Alisema anachofanya kipindi hiki ni kutimiza wajibu wake na wananchi ni mashahidi kila nafasi anayopewa, anatimiza wajibu wake ipasavyo na kusisitiza kuwa amefanya mengi yanayoonekana machoni pa watu na kudhihirisha kwamba ni kiongozi bora.

      Akizungumzia umri wa urais, alisema mijadala kuwa vijana hawawezi kuongoza haina msingi. Alifafanua kuwa kiongozi mzuri ni yule mwenye uwezo wa kuwaongoza wananchi na kuwaletea maendeleo.

      Alisema rais anachaguliwa na wananchi hivyo maamuzi yote ya nani anafaa kwa nafasi hiyo na umri upi, ipo mikononi mwa wananchi wenyewe.

      Katika hatua nyingine Sitta, aliwashangaa wanasiasa wanaopigana vijembe majukwaani na kueleza kwamba tabia ya kumtukana mtu mmoja mmoja, haina maana yoyote.

      Aliwashauri viongozi wa CCM kutojibu mapigo ya wapinzani na kuwataka kutumia busara kila wanapokutana na kauli chafu kwani nia ya kudumisha amani ya nchi.

      Alionya kuwa amani ya nchi ikitoweka, itakayobebeshwa lawama ni CCM na Serikali yake.

      “Kauli nyingi za majukwaani zinachochea chuki miongoni mwa wananchi, matokeo yake zinaweza kuibua machafuko na waathirika watakuwa wananchi wenyewe, tena wale wasio na uwezo wa kujiokoa,’’ alisema Sitta.

      Alisema kuwa katika miaka 50 ya utawala wa CCM, kuna mambo mengi yamefanyika na kwamba wapinzani hawana haja kubeza kwani yanaonekana kwa macho.

      Alisema kuwa katika mafanikio hayo, kuna mengi yamefanywa na Rais Jakaya Kikwete, mfano mzuri ni kampuni tano za madini kulipa kodi na wananchi kuanza kufaidika na rasilimali za nchi yao.

      Hofu ya mahasimu wake

      Sitta alieleza kuwa anashangazwa na watu wanaoweweseka wakisikia anataka kuwania urais mwaka 2015.

      "Nashangaa watu wanapata kiwewe kusikia nataka kuwania urais, kuwania urais ni haki ya kila Mtanzania na Watanzania ndiyo watakaoamua nani ni mzuri na atawafaa," alisema Sitta

      "2015 tunataka kuwa na mwelekeo mzuri, nikiwa na maana mambo ya hongo, ubadhirifu hatutaki yawe na nafasi, alisema Sitta na kuongeza:

      Alisema watu wanatumia fedha nyingi kusaka urais na hata wengine kutumia ndumba kwa kwenda Mlingotini, Bagamoyo, kwa nia ya kutaka uongozi na matokeo yake wanaposhinda lengo lao la kwanza linakuwa kurudisha fedha walizotumia

      E-mail: [email protected]
      Advertise your products, business & services with us 100% free |www.globaladverts.biz

    19. #19
      Superman's Avatar
      JF Tanzanite Member Array
      Join Date : 31st March 2007
      Location : On Move
      Posts : 5,421
      Rep Power : 1823
      Likes Received
      1415
      Likes Given
      1216

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Quote By bht
      superman mambo? (i come in peace today...lol?)

      Leo mi nimegundua habari nyingi kwenye magazi ni urongo mtupu
      Haaaa haaa Mkuu wangu mimi niko poa kabisa ndo kwanza nimetia timu DSM.

      Mkuu mbona mimi nakufahamu miaka sana na wala sina issue na wewe kabisa. Napenda tu unavyosimamia hoja unazoziamini.

      Kama uko Bongo, let us meet in one of the days. Naona AshaDii kule kishawafunga kamba wengi.

      Niaje habari ya Sitta kuweka hadharani nia yake ya kuwa kuishi makazi ya sasa ya Baba Mwana-Asha?
      Kwa kufanya kazi kwa bidii imetupasa kuwasaidia wanyonge . . . . . . “Ni heri kutoa kuliko kupokea”

    20. #20
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,862
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6195
      Likes Given
      22546

      Default re: Sitta autamani Urais 2015

      Quote By Superman

      MY TAKE:

      Kwa Changamoto za leo ambayo Nchi Yetu inazo, bado Mh. Samuel Sitta hana uwezo wa kuleta mageuzi ya Kimaendeleo katika Tanzania. Alipata mafasi kamili kama Kiongozi wa moja Mhimili kamili wa Kikatiba kama Spika wa Bunge kusimamia kuondoa uovu kikamilifu pamoja na Ufisadi Mwingine lakini akaamua kukumbatia uovu kuinusuru serikali yake ya CCM.

      Japo anaweza kuwa anakubalika na baadhi, Mzee Sitta hawezi kuwa udhubutu wa kutupa Tanzania tunayoiota, na hata huko Wizara ya Afrika ya Mashariki bado hatujaziona cheche zozote.
      Mkuu Superman, tafuta thread ya Mzee Mwanakijiji aliyouliza, "Wapiganaji Walioko CCM, Wanapigania Nini?". 'Wapiganaji' walioko CCM wanapigania nini hasa?

      Nilisema hivi kuhusu hawa wanaojiita wapiganaji.

      Quote By Pasco
      Mzee Mwanakijiji, hao makamanda dhidi ya ufisadi wamegawanyika makundi mawili, miongoni mwao wamo wanapinga ufisadi kwa sababu wanauchungu wa dhati na umasikini wa Watanzania ambao ufisadi umechangia kuongezeka kwa umasikini na unaendelea kuitafuna nchi na utaendelea kwa miaka kadhaa ijayo.

      Kundi la pili ni la wapinga ufisadi wanaopigania nafsi zao, wanahasira kwa sababu nao wanataka share yao kwenye huo mkate na nafasi zikiwakalia vazuri, nao watafisidi vile vile hivyo nawaweka kundi moja na mafisadi tuu.Kwa mtazamo huo kuna makamanda wenye uchungu na makamanda mafisadi.

      Swali ni jee ndani ya CCM, wanapigania nini?. Jibu langu la jumla ni kuwa wanapigania nafsi zao just for survival na wakishapata uhakika wa survival baada ya 2010, mtawashuhudia nao wakifisidi ushahidi ni 'time will tell'.

      Kitu kibaya zaidi kuhusu baadhi ya hawa makanda ambacho mtakishuhudia ni kwa baadhi yao kuwapigia magoti mafisadi ili kuwanusuru na panga la CCM kupitishwa kugombea 2010 na wakishapitishwa, wataungana na kuwa kitu kimoja kwa ajili ya kuweka mikakati ya 2015.

      Baadhi watakao piga magoti ni wale ambao nguvu ya mafisadi kuhakikisha hawateuliwi na CCM kugombea itatumika, na wakisha toswa na CCM, watatamani kukimbilia upinzani sio ili kuendeleza mapambano, bali kujaribu kuokoa mkate wao wa kila siku na nawahakikishieni, kama mafisadi watamwaga fedha kuhakikisha makamanda hawapiti, na wakihamia upinzani, ndio kwanza sasa chama kitamwaga mapesa zaidi kuhakikisha hakishindwi.

      Baadhi ya makamanda watapigwa chini na hapo ndipo itakuwa mwisho wa habari yao, kitakachofuatia ni kwenda kuwalamba miguu mafisadi kwa kurejea CCM wakiwa wametahayari kama alivyofanya yule kinara wa kundi la G-55.

      Hizi harakati za kujipambanua kwa pamoja na kuzungukiana majimbo ya wapiganaji zamu kwa zamu huku wakitoa michango ya shilingi 500,000 walizopewa na mshitiri, wakisindikizwa na ka 'kipindi maalum' ndani ya taarifa za habari (no 10min news clip) ya kwenye TV ya mshitiri, hizi ni nyimbo tuu za shangwe na mapambio ya kujinusuru na panga la uteuzi wa CCM mwaka 2010, baada ya hapo kutakuwa hawana hili wala lile.

      Sibezi juhudi za makamanda, bali mbinu zilizotumika kuwapambanua bungeni tukianzia kwenye ripoti ya Richmond iliyotumika kumchapa bakora EL kwa kumuhukuma bila kupewa fursa ya kusikilizwa, hivyo ukamanda wao unapimwa ni kwa kiasi gani wanaweza kuzungumza kwa jazba na mapokezi makubwa makubwa kuashiria wananchi wanawakubali.

      Wapiganaji wa kweli ni wale ambao wako tayari to take risk kwa kusimama mbali na uvundo kuwathibitishia watanzania kuwa huku tuliko chama kimetekwa na mafisadi, hivyo baada tuu ya kuvunjwa Bunge mwakani, wataonyesha waliposimama na wananchi watawachagua kwenye chama chochote watakacho simama nacho na hawa ndio watakuwa wapiganaji wa kweli kweli.

      Wale makamanda wanaopigania nafsi zao, mtawatambua kwa kutokubali kurski nafasi zao ndani ya CCM ambako mafisadi wana upper hand. Hawa watasubiri mpaka watakapo temwa na CCM ndipo waje upande wa pili kujaribu kamari ya upinzani, hawa ndio watakao kwenda na maji kwa sababu upinzani Tanzania ni kwenye baadhi tuu ya maeneo, kuna maeneo mengi CCM inachaguliwa sio kwa sababu imekubalika sana, bali kwa sababu ya mazoea tuu na kukosekana kwa elimu ya uraia.

      Kuna sehemu hata akisimamishwa mgombea kiazi vipi, atapita tuu.Kwa vile CCM ina wenyewe, na baadhi ya wenyewe hao ndio hao hao mafisadi na wengine wao ndio hao makamanda, hapa ni mwendo wa mwenye kisu kikali ndie anayekula nyama, na ili ukubaliwe kula nyama ni lazima uchague upande, either with us, or against us, maadamu wenye guvu ni mafisadi, mwenye nguvu mpishe, hao makamanda watajikuta kuliko kuriski loosing, wakijua hawawezi kuwashinda, watatumia formular ya 'if you can't beat them, join them' watajiunga nao na wote wakuwa kwenye tenga moja la samaki, na wote watakuwa ndio hao hao.

    Page 1 of 5 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...