Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

    Report Post
    Page 10 of 13 FirstFirst ... 89101112 ... LastLast
    Results 181 to 200 of 243
    1. #1
      EasyFit's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th July 2011
      Posts : 840
      Rep Power : 571
      Likes Received
      575
      Likes Given
      196

      Default Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Zuberi Kabwe, amesema kuwa hana nia ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama chake katika Uchaguzi wa ndani wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu.

      Zitto aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na NIPASHE jijini Mbeya, alikokuwa amekwenda kuongeza nguvu katika kampeni za uchaguzi wa udiwani katika kata ya Kiwira wilayani Rungwe.

      Alisema kuwa hana nia ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama hicho kwa sababu anaona timu ya sasa ya uongozi wa chama hicho inatosha na inafaa kuendelea kukiongoza kwa miaka mingine mitano ijayo.

      “Sina interest (nia) na sifikirii kama nitagombea uongozi ndani ya chama katika uchaguzi wa ndani wa Chadema mwaka huu, naona timu iliyopo inatosha na inafaa kuendelea kukiongoza chama,” alisema Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini.

      Alisema ingawa katika uchaguzi uliopita alijitosa kuwania nafasi ya mwenyekiti wa chama hicho, lakini safari hii nafsi yake haimtumi kufanya hivyo kwa kuwa ana imani kuwa uongozi wa sasa unastahili kuendelea kuwa madarakani kwa manufaa na maslahi ya chama na Watanzania kwa ujumla.


      Chanzo: Gazeti la Nipashe

      UPDATE:
      Kairudia kauli hii Juni 16, 2012 akiwa Iringa (M4C)


    2. #181
      tarizle's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th November 2011
      Posts : 55
      Rep Power : 395
      Likes Received
      5
      Likes Given
      5

      Default

      Quote By Consigliere View Post
      "Nimeamua kugombea Uenyekiti wa Chadema sababu nimeona Chama kimepoteza mwelekeo na kimekuwa cha kikanda zaidi na baadhi wanajinufaishi zaidi na Chama, hivyo lengo langu ni kukifanya Chama kiwe na sura ya kitaifa tofauti na ilivyo hivi sasa ambapo chama ni cha wachache mwenyekiti ni dhaifu na chama kina makundi"

      "Nimeamua kubatilisha uamuzi wangu wa kugombea uenyekiti wa CHADEMA sababu nimeridhika na hali ndani ya CHAMA na nina Imani na Mwenyekiti wetu aendelee kutuongoza"

      Sitagombea ubunge wa Kigoma Kaskazini mwaka 2010. Najiandaa kugombea kati ya Kahama, Kinondoni.....kwani watu wa huko wamenitumia ujumbe kuwa wananiitaji na mimi nimetuma watu wangu wafanye utafiti wa kisayansi ili niamue nikagombee wapi"

      "..................Sitagom bea tena Ubunge mwaka 2010 nataka nijiandae kwenda kufundisha kwani iyo ndiyo ndoto yangu ya muda mrefu"

      "Nitagombea Ubunge wa Kigoma Kaskazini mwaka 2010"

      ".....ndiye alietoa wazo la CHADEMA kwenda kuonana na rais kuhusiana na suala la katiba mpya"......
      (Ufafanuzi ulitolewa kuhusiana na suala hili kuhusu kikao gani kilitoa maamuzi hayo)

      The latest kauli
      ......"Sitagombea Uongozi ndani ya CHADEMA"

      Hizi ni kauli za mtu mmoja, lakini kwasabu ya mapenzi yaliyopita kiasi cha kuwezo kupofua upeo mtu katika kufikiri, mashabiki either hawazikumbuki au wamezisahau haraka sana......hapa ndipo tatizo la msingi lilipo.....
      Hongera kwa kutufumbua macho...

    3. #182
      mwongozo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th October 2011
      Posts : 45
      Rep Power : 396
      Likes Received
      9
      Likes Given
      21

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      naona fitna zimeanza kwa kuwa uchaguzi hauko mbali sn! mbowe na slaa mawesema kauli ngapi zinazogongana! siasa ndivyo ilivyo. zitto alisema maneno yale kwa malengo anayoyajua mwenyewe. usipandikiza chuki dhidi ya zitto. ni mtu muhimu sn ktk chadema

    4. #183
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 16,053
      Rep Power : 14671
      Likes Received
      2955
      Likes Given
      2099

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Zitto maji yamemfika shingoni, hana cha kufanya tu, anajikaza kisabuni. Nna uhakika hata Mwenyekiti kisha ona madudu yaliyopo makao makuu, mchumba kuwa bosi? Dah! hatari kubwa sana.

      Zitto kajionea aah, bora akae pembeni awaachie wenye uchu wa madaraka watoane roho, hajasahau yaliyomkuta.
      System At Work

      "nimetembea angani na ardhini Tanzania nzima sijaona Rais na serikali iliyotukuka kiutendaji kama hii ya KIKWETE." - Freeman Aikaeli Mbowe

    5. #184
      Kaa la Moto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Location : Bristol
      Posts : 6,987
      Rep Power : 1980
      Likes Received
      466
      Likes Given
      4506

      Default Re: Zitto kabwe:sitagombea cheo chochote ndani ya chama

      Quote By Tume ya katiba View Post
      Na angethubutu kugombea tu angeundiwa TUME. Kasoma alama za nyakati. Bora awe nje ya uongozi wapange wanayoyataka.
      Kwa hizi propaganda unajisumbua bure. Chadema c sisi m, ni wanasayansi katika politiki, tulia kijana subiri kuwa mpinzani tu!
      wakati Cuf wanataka kuchukua nchi mwaka 2000 CCM walikuja na single ya kusema Cuf ni waislamu na kwa sasa wanadai sisi Chadema ni chama cha wakristo sasa CCM nacho ni cha watu gani? Watu wakajibu mashetaaaaaniiiiii.!---Wana Kigoma.

      ....Pamoja na kansa ya uongozi wa CCM watu wataendelea kukichagua,au watu wanaweza wakachoka na kusema potelea mbali wakachagua chama KINGINE....Julius. Kambarage. NYERERE"

    6. #185
      Ben Saanane's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th January 2007
      Posts : 6,948
      Rep Power : 45018
      Likes Received
      5327
      Likes Given
      6535

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Bado mnajadili haya mambo tu? you guys .........!
      Wametuonyesha Jeuri ya ukaburu,tuwaonyeshe jeuri ya Umkhontho we sizwe kupitia Red Brigade.Tukiwaonyesha woga wetu, itakua silaha imara zaidi kwao kutumaliza-Ben Saanane


    7. #186
      manucho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th April 2012
      Posts : 562
      Rep Power : 473
      Likes Received
      79
      Likes Given
      0

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Zomba tufafanulie tujue yapi yalimkuta bwana ZZK, naona kama uko deep sana na masuala ya CDM

    8. #187
      Shardcole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th January 2012
      Posts : 4,834
      Rep Power : 1376
      Likes Received
      1096
      Likes Given
      4

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Proccm mnapenda kumtumia zitto kuipangalanyisha CDM xaxa mnenoa aibu yenu.........

    9. #188
      juu kwa juu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th April 2011
      Posts : 211
      Rep Power : 457
      Likes Received
      23
      Likes Given
      1

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Wewe zitto, acha kujikweza huwezi kupata huo uongozi wa cdm, acha nafasi hizo za wachaga. Uking'ang'ania yatakupata ya mh. Wangwe.

    10. #189
      mzee wa njaa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th June 2011
      Posts : 1,340
      Rep Power : 673
      Likes Received
      194
      Likes Given
      107

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Bora kasema mapema wadau wajitokeze.

    11. #190
      Man KKK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd April 2012
      Location : Ndani ya Laptop
      Posts : 789
      Rep Power : 521
      Likes Received
      94
      Likes Given
      46

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Quote By EMT View Post
      Na wewe kama yamekushinda huko Chadema si uhamie kwenye hiki chama kimya?
      Mipasho star search imeanza naona mnakipaji ndugu zangu mnakaribishwa

    12. #191
      nice 2's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2011
      Posts : 699
      Rep Power : 943
      Likes Received
      503
      Likes Given
      285

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Quote By Ben View Post
      Bado mnajadili haya mambo tu? you guys .........!
      while the dude is very busy working for this Nation ,very interesting!
      Ben Saanane likes this.

    13. #192
      Kachanchabuseta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th March 2010
      Posts : 2,977
      Rep Power : 1058
      Likes Received
      441
      Likes Given
      1133

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Hivi na leo kasemaje?

    14. #193
      Jakubumba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th March 2011
      Location : United states
      Posts : 1,214
      Rep Power : 730
      Likes Received
      312
      Likes Given
      130

      Default

      Quote By Jeykey View Post
      Hivi na leo kasemaje?
      Jk vipi mbona unafunua old threads?

    15. #194
      Zawadi Ngoda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th August 2009
      Posts : 1,797
      Rep Power : 860
      Likes Received
      101
      Likes Given
      99

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Quote By EasyFit View Post
      Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Zuberi Kabwe, amesema kuwa hana nia ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama chake katika Uchaguzi wa ndani wa chama hicho unaotarajiwa kufanyika baadaye mwaka huu.

      Zitto aliyasema hayo juzi wakati akizungumza na NIPASHE jijini Mbeya, alikokuwa amekwenda kuongeza nguvu katika kampeni za uchaguzi wa udiwani katika kata ya Kiwira wilayani Rungwe.

      Alisema kuwa hana nia ya kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya chama hicho kwa sababu anaona timu ya sasa ya uongozi wa chama hicho inatosha na inafaa kuendelea kukiongoza kwa miaka mingine mitano ijayo.

      “Sina interest (nia) na sifikirii kama nitagombea uongozi ndani ya chama katika uchaguzi wa ndani wa Chadema mwaka huu, naona timu iliyopo inatosha na inafaa kuendelea kukiongoza chama,” alisema Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini.

      Alisema ingawa katika uchaguzi uliopita alijitosa kuwania nafasi ya mwenyekiti wa chama hicho, lakini safari hii nafsi yake haimtumi kufanya hivyo kwa kuwa ana imani kuwa uongozi wa sasa unastahili kuendelea kuwa madarakani kwa manufaa na maslahi ya chama na Watanzania kwa ujumla.


      Chanzo: Gazeti la Nipashe

      UPDATE:
      Kairudia kauli hii Juni 16, 2012 akiwa Iringa (M4C)
      Kibano alichokipata wakati alipotaka kugombea uwenyekiti wa CHADEMA, ndio sababu kubwa ya kukaa pembeni safari hii.

      Vile vikao vya wazee havikuwa bure, bali viliambatana na vitisho vya kuhatarisha maisha yake. Hali hii iomemfanya Zitto kukiogopa sana chama chake kuliko hata watanzania au hata CCM kAMA WENGI WANAVYOFIKIRI.

      Huo ni uamuzi wa Busara, kwani hawa watu wa CHADEMA hawajali maendeleo, hata hivyo usingepata hata kama ungegombea mkwani dDHAMBI YAKO NI KUWA HUKUZALIWA KILIMANJARO/ARUSHA.

    16. #195
      Stabilaiza's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th July 2012
      Posts : 145
      Rep Power : 460
      Likes Received
      68
      Likes Given
      5

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Bora aache kugombea maana uhusiano wa Zitto na Jack Zoka ni habari mbaya kwa wapambanaji. Uhusiano kati ya Zitto na Jack Zoka ambao uliwekwa wazi na vyombo mbalimbali ni taarifa mbaya kwa wanasiasa na wananchi wanaoipenda taifa lao la Tanzania. Uhusiano huu wa Zitto na Jack Zoka ambaye ni mkurugenzi msaidizi wa TISS (usalama wa taifa) umeripitiwa kuwa na historia ndefu tangu wakati wa uchaguzi mkuu. Wakati Zitto anajitapa kuwa anatetea maslahi ya wananchi, mshirika wake wa chanda na pete Jack Zoka anatuhumiwa na wanasiasa na wanachi kufanya kazi ya kuwadhuru badala ya kulilinda taifa. Kama mshirika wa Zitto anadhuru wananchi ni wazi kuwa naye Zitto ana masalahi binafsi na mabaya kwa wananchi. Maana ukitaka kujua tabia ya mtu, uliza tabia ya rafiki yake. Ni jambo la kusikitisha Zitto kuwa na uhusiano na huyu mfanyakazi wa usalama wa taifa anayedhuru watu na wakati huohuo anajidai kuwa ni mpambanaji. Uhusiano wa Zitto na Jack Zoka ulishawekwa wazi kuwa walikuwa wanawasiliana kwa simu mara kwa mara wakati wa kipindi cha uchaguzi. Tuwe macho na urafiki wao na ambao si mwema hata kidogo kwa wanasiana na wananchi wenye uchungu na taifa letu.

    17. #196
      Bob G's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 5th October 2011
      Location : UK Manyasi
      Posts : 1,733
      Rep Power : 736
      Likes Received
      301
      Likes Given
      36

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Huyu Zitto ni KIGEUGEU, na hisi anatumiwa na ccm si bure

    18. #197
      Zipuwawa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Posts : 2,206
      Rep Power : 875
      Likes Received
      310
      Likes Given
      123

      Default Re: Zitto: Sitagombea uongozi CHADEMA

      Zitto kwanini analazimisha umaarufu huu wa kisiasa kila tukiamka zitto zitto..............
      Maisha yetu ni mafupi lazima tuyatete kwa namna yeyote ile!

    19. #198
      ibange's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 1,372
      Rep Power : 1114
      Likes Received
      407
      Likes Given
      23

      Default Dr Slaa M/kiti, Zitto M/M'kiti

      Wana JF wenye mapenzi mema kwa CHADEMA, nadhani ni muda muafaka sasa kuanza kutoa maoni kuhusu chama chetu hasa uongozi wake maana uongozi ujao ndio utatupa serikali 2015. kwanza nimpongeze sana Mbowe kwa kweli ameonyesha ujasiri mkubwa na ameongoza chama kwa ujasiri na ukakamavu mkubwa.

      Huwezi kuitaja chadema ya leo bila kumtaja Mbowe. Baada ya kazi kubwa na ili kuonyesha chadema kina watu wazuri wengi wanaoweza kuongoza, ningeshauri tu asigombee tena akae pembeni ila abaki kwenye vikao muhimu vya chama.

      Nashauri Dr Slaa sasa angeandaliwa kuwa Chairman, Zitto Kabwe awe makamu Bara, atafutwe katibu mkuu msomi mzuri ambaye anaweza kuratibu shughuli za chama kisomi, Naibu katibu pia awe msomi mzuri, tuwe na graduates makatibu wa kila jimbo la uchaguzi ambapo kazi zao itakuwa kufanya uratibu wa chama, hope chadema tutakuwa tumepiga hatua zaidi towards state house. Ni maoni tu. Peoplessssssssssssss Powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
      ntagunga likes this.

    20. #199
      masopakyindi's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th July 2011
      Posts : 3,886
      Rep Power : 4229
      Likes Received
      1053
      Likes Given
      430

      Default Re: Dr Slaa M/kiti, Zitto M/M'kiti

      Quote By ibange View Post
      Wana JF wenye mapenzi mema kwa chadema, nadhani ni muda muafaka sasa kuanza kutoa maoni kuhusu chama chetu hasa uongozi wake maana uongozi ujao ndio utatupa serikali 2015. kwanza nimpongeze sana Mbowe kwa kweli ameonyesha ujasiri mkubwa na ameongoza chama kwa ujasiri na ukakamavu mkubwa. Huwezi kuitaja chadema ya leo bila kumtaja Mbowe. Baada ya kazi kubwa na ili kuonyesha chadema kina watu wazuri wengi wanaoweza kuongoza, ningeshauri tu asigombee tena akae pembeni ila abaki kwenye vikao muhimu vya chama.

      Nashauri Dr Slaa sasa angeandaliwa kuwa Chairman, Zitto Kabwe awe makamu Bara, atafutwe katibu mkuu msomi mzuri ambaye anaweza kuratibu shughuli za chama kisomi, Naibu katibu pia awe msomi mzuri, tuwe na graduates makatibu wa kila jimbo la uchaguzi ambapo kazi zao itakuwa kufanya uratibu wa chama, hope chadema tutakuwa tumepiga hatua zaidi towards state house. Ni maoni tu. Peoplessssssssssssss Powerrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr
      Una matatizo mkubwa weye!
      Mbowe aondoke?
      Halafu chama amwachie nani?
      "If you don't know where you are going, any road will get you there-nowhere”

    21. #200
      ibange's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 1,372
      Rep Power : 1114
      Likes Received
      407
      Likes Given
      23

      Default Re: Dr Slaa M/kiti, Zitto M/M'kiti

      Quote By masopakyindi View Post
      Una matatizo mkubwa weye!
      Mbowe aondoke?
      Halafu chama amwachie nani?
      Unataka kutuambia kuwa Mbowe pekee ndie anaweza ndani ya Chadema? Chadema ni chama kikubwa kwa sasa nadhani tutakuwa tunaonyesha njia kama tukiendelea na utaratibu wetu wa kubadilishana kijiti hata kama tuna kiongozi imara kama Mbowe. Nyerere alikuwa kiongozo shupavu ila alifika mahali akaonyesha ukomavu wa kisiasa akang'atuka

    Page 10 of 13 FirstFirst ... 89101112 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...