Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

    Report Post
    Page 1 of 10 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 183
    1. #1
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7367
      Likes Received
      6150
      Likes Given
      22265

      Default Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Wanabodi,
      Baada ya kujadili mazuri na mafanikio ya rais wetu, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, kila kwenye mafanikio hapakosi matatizo, mapungufu au changamoto ambazo zikifanyiwa kazi zinabadilisha hali iliyopo sasa na kutupeleka hali bora zaidi.

      Katika kujadili mapungufu, nawaombeni sana tujadili kwa nidhamu na staha kwa kuzingatia huyu tunayemjadili ni rais wetu, hivyo sitegemei kuona lugha za kebehi, machukizo, matukano, au maudhi, kwa kifupi lugha zozote ambazo hazina staha!.

      Katika kujadili mapungufu, madhaifu, matatizo na changamoto zinazomkabili rais Jakaya Kikwete, nawaombeni tujadili kwa spirit ya constructive criciticism kwa kueleza mapungufu hayo in good faith kwa nia ya kujenga na sio kubomoa.

      Watanzania tumekuwa ni watu wa kilalamika na kunung'unika wakati wote bila kuchukua hatua zozote positive za kurekebisha!. Naomba hii thread sio thread ya malalamiko au manunguniko dhidi ya JK bali thread ya kutoa ushauri nini cha kufanyika!.

      Kwa kuanzia moja ya mapungufu makubwa ya JK ni mtu wa huruma iliyopitiliza mipaka matokeo yake kutafsiriwa kama ni weakness, yaani "JK ni rais dhaifu", weak!, asiyeweza kufanya maamuzi magumu!.

      Mfano wa kwanza wa udhaifu huu wa huruma uliyopitiliza ni pale alipoyasamehe yale majizi ya EPA kwa kuyaruhusu yarudishe fedha yalizo kwiba kwa exchange ya kusemehewa na kutofikishwa mahakamani!. Hata Spika Sitta pia alimlaumu rais JK kwa upole huu!. Lingekuwa ni bunge makini, imperchment process ingeanzia pale pale right away kwa sababu rais hana mamlaka ya kuizuia sheria kuchukua mkondo wake!, huu ni uvunjaji wa katiba ya JMT!.

      Ni upole huo huo ndio unaopelekea hajamwajibisha Waziri wa Afya na naibu wake kwa sababu anawahurumia!.

      Ushauri ni kwa JK kuwa bold na kufanya maamuzi magumu!. Mfano kwenye huu mgomo wa sasa, siungi mkono JK kuitikia shinikizo la madaktari na wanaharakati kumwajibisha Mponda na naibu wake, hiyo nayo ni weakness. Bold decision ni wahusika watakaosabisha kifo chochote, kupandishwa kizimbani kwa murder!.

      JK anatakiwa kupunguza huruma na upendo wa mshumaa kumulikia wenzake huku yeye kwake kunateketea!. Huruma na upendo alioisha uonyesha sasa unatosha!. JK anatakiwa awe mkali kama alivyokuwa Nyerere watu kujua wamefutwa kazi ni kupitia taarifa ya habari ya saa 2:00 usiku ya RTD tena ikisomwa na David Wakati!.(RIP).

      Ni huruma na upendo huu uliopitiliza ndio unapelekea kuwahurumia baadhi ya mawaziri na wasaidizi wake ambao hawamsaidii hivyo kuendelea kuwabeba!.

      Kwa vile JK hawezi kufanya kila kitu, piga chini wale wote ambao hawakusaidii hata ikibidi kumpiga chini Pinda, piga chini ili uliokoe taifa katika kipindi hiki chako cha miaka 3 kilichobakia!.

      Nawatakia majadiliano mema.

      Natanguliza shukrani kwa kuzingatia spirit ya constructive criticisim in good faith kwa nia ya kujenga na sio kubomoa!.

      Wasalaam

      Pasco wa jf.

      NB. Kama hauwezi constructive criticisim unaweza kujisomee tuu na kuishia zako bila kuchangia, kwani sio lazima uchangie kila thread!.
      Last edited by Pasco; 2nd February 2013 at 06:06.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,089
      Rep Power : 13049
      Likes Received
      14065
      Likes Given
      14838

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!.

      aliingia kwenye urais bila vission wala mission.
      Hili ni pungufu kubwa sana hata katika maisha ya mtu mmoja mmoja.

      Katika ngazi ya uraisi ni balaa zaidi.

      Cha kumsaidia, walio karibu naye wampe vission japo ya muda huu mchache uliobaki.
      Bora achegue hata sekta moja aiendeleze japo akitoka tumkumbuke kwa hilo.

      Sasa hivi tutamkumbuka sikui kwa kitu gani labda safari za nje.

    4. #3
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,089
      Rep Power : 13049
      Likes Received
      14065
      Likes Given
      14838

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!.

      Hivi kushindwa kuwawajibisha wasaidizi wake ni huruma na upendo??

      Huruma na upendo kwa nani?
      Kwa maslah ya nani?

      Mimi naona kama kutojiamini katika maanuzi na kujaribu kuficha uozo wa uteuzi wake wa wasaidizi wake ambao wengi ni washkaji, wengine vilaza ili wasiweze kumchaleni sana.

      Baadhi ya mabosi hasa kama hajiamini hata maofisi anayependa surbodinates waliosmart kuliko yeye.
      Pasco, zumbemkuu, Kaunga and 1 others like this.

    5. #4
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7367
      Likes Received
      6150
      Likes Given
      22265

      Default

      Quote By Kongosho
      aliingia kwenye urais bila vission wala mission.
      Hili ni pungufu kubwa sana hata katika maisha ya mtu mmoja mmoja.

      Katika ngazi ya uraisi ni balaa zaidi.
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.

    6. #5
      lukindo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th March 2010
      Posts : 1,575
      Rep Power : 781
      Likes Received
      415
      Likes Given
      481

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Pasco
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.
      Mkuu Pasco, kubali tu kuwa mkulu hakuwa na hivyo vitu, na kama ni ilani ya uchaguzi alikili mwenyewe kuwa alikabidhiwa pale jangwani!
      Jasusi and Pasco like this.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,089
      Rep Power : 13049
      Likes Received
      14065
      Likes Given
      14838

      Default

      ile ilikuwa ya chama
      yeye kama individual alitaka kuacha mark gani kwa watanzania?

      Hata kama chama kiandae vission nzuri kiasi gani, kama individual unayesimamia utekelezaji wa mission hiyo kama wewe mwenyewe huna motivation hakuna linaloweza fanyika.

      Lazima chama kiwe na vission na mtu anayeenda kukalia kiti hicho awe na vission inayosapoti vission ya chama chake.

      Inaweza kuwa vission ya chama chake ni nzuri, lakini interest zake as an individual zinzkwamisha zoezi zima.
      Kwa hiyo vission ya chama inakuwa haina mantiki kwa wananchi.

      'conflict of interest'

      halafu hii ya kusema watendaji wamemwangusha, msiwe mnasema kabisa kumtetea. Sababu mnazidi kum-expose zaidi weakness zake.

      Kama hawezi kujua na kuchagua watu wa kumsaidia kazi basi hafai hata kidogo.

      Hivi ukishindwa kujenga kwako na kusomesha watoto wako utamlaumu nani? Mkeo? Hausi gelo? Watoto?
      What an excuse!
      Quote By Pasco
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.
      Last edited by Kongosho; 7th March 2012 at 11:44.
      senator, Mindi, Mr Rocky and 6 others like this.

    9. #7
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,089
      Rep Power : 13049
      Likes Received
      14065
      Likes Given
      14838

      Default

      kama wanataka tumsaidie
      wavumilie tumpasue jipu tu bila ganzi

      kuanzia mwanzo
      hakuwa na inner motivation kama raisi
      hata hiyo ilani ya chama sijui hata kama aliielewa
      na kujaribu kuifanya ioane na ilani yake binafsi ya kugombea.

      Quote By lukindo
      Mkuu Pasco, kubali tu kuwa mkulu hakuwa na hivyo vitu, na kama ni ilani ya uchaguzi alikili mwenyewe kuwa alikabidhiwa pale jangwani!
      Pasco and zumbemkuu like this.

    10. #8
      Fidel80's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2008
      Location : UVUNGUNI
      Posts : 18,931
      Rep Power : 9474
      Likes Received
      3052
      Likes Given
      1192

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Pasco
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.
      Mbona hiyo Ilani aliyo inadi ameshindwa kuisimamia na kutekeleza yote aliyo ahidi?
      Pasco likes this.
      **^^+..Ukiuza Utumbo usiogope nzi..+^^**
      Chuda Raha
      Email: [email protected]

    11. #9
      capito's Avatar
      Member Array
      Join Date : 16th November 2011
      Posts : 21
      Rep Power : 383
      Likes Received
      7
      Likes Given
      15

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Serikali imeshindwa kuwabana wawekezaji na kuhakikisha kuwa wananchi wanafaidika na rasilimali zilizopo hapa nchini, migodi inachimbwa dhahabu statistics kwenye soko la dunia zinaonesha dhahabu toka tanzania imeuzwa kiasi kadhaa lakini sisi tumeambulia karibia na sifuri.
      Pia serikali haijaonesha nia ya dhati ya kupunguza matumizi makubwa yasiyo ya lazima mfano, magari ya kifahari, misafara mikubwa wanapokwenda nje ya nchi na kufikia hotel za bei kubwa, kusafiri kwenye business class au first class kwa vigogo wa serikali. Mtoto wa mkulima alikataa gari lakini bado linatumika kwa hiyo hamna tofauti yoyote iliyoonekana katika kupunguza matumizi.
      Serikali pia iwe na scale of preference, siyo tunatumia billioni kadhaa kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya uhuru au kukimbiza mwenge wakati watoto wetu wanakaa chini kwa kukosa madawati na shule kibao za kata hazina vifaa.

    12. #10
      Kingo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2009
      Posts : 368
      Rep Power : 583
      Likes Received
      50
      Likes Given
      106

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!.

      Quote By Kongosho
      Hivi kushindwa kuwawajibisha wasaidizi wake ni huruma na upendo??

      Huruma na upendo kwa nani?
      Kwa maslah ya nani?

      Mimi naona kama kutojiamini katika maanuzi na kujaribu kuficha uozo wa uteuzi wake wa wasaidizi wake ambao wengi ni washkaji, wengine vilaza ili wasiweze kumchaleni sana.

      Baadhi ya mabosi hasa kama hajiamini hata maofisi anayependa surbodinates waliosmart kuliko yeye.
      Anatumia "leiza fea" leadership style and democracy hata kwa mambo ya msingi ambyo kiongozi imara na shupavu, anayejua wajibu wake hawezi kushindwa kufanya. Na pia kiongozi bora lazima ajue wajibu wake (both accountability and resposibility) kwa anaowaongoza na kutenda kwa ujasiri na uimara na pia usahihi na kusimamia maamuzi yake kwa weledi.
      Sasa kwa JK hata umpigie ngoma hawezi cheza, filimbi hasikii, hata sijui yupo kwa maslahi ya nani!
      Pasco and Philipo Kidwanga like this.
      GOOD TIMBER DOES NOT GROW WITH EASE. THE STRONGER THE WIND THE STRONGER THE TREES.

    13. #11
      Maundumula's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 4,896
      Rep Power : 3090
      Likes Received
      1324
      Likes Given
      5608

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Mr Prezida anatakiwa kuwa mkali na watendaji wazembe serikali, especially wale ambao anaweza kuwawajibisha moja kwa moja. Kama maswala ya Miundo mbinu; Reli, Bandari, , ATC haya anatakiwa ayabebee bango jino kwa jino maana naona kuna uzembe mkubwa sana ulifanyika na unaendelea kufanyika katika miundombinu.

      Kwenye kilimo sasa tutoke kwenye makarabrasha na tukaendeleze kilimo kwanza kwa vitendo, aibane wizara husika isaidie kuboresha mazingira kwa wakulima , wajuu, wa kati na wachini ili wote wanufaike.

      Ajira, ajitahidi kubana ajira za wageni maana wageni wanaongezeka kila leo wengine wanafanya kazi ambazo kwa kweli wenyewe tunaziweza.

      Kodi, Awabane wahusika wahakikishe kila anayestahili kulipa kodi analipa. Kwa sasa ni makampuni makubwa tu ndio yanalipa lakini nayo bado yanaleta janja. Tuwabane hawa wafanya biashara wa kada zote, Ifike wakati mama ntilie, fundi cherehani, Fundi viatu, muuza chips, Fundi baskeli, nk wote wachangie pato.

      Kuboresha mazingira ya uwekezaji kwa kuiwezesha TIC iwe ni "one stop shop" ili mambo ya kodi, uhamiaji, ardhi , manispaa yafanyike hapo.

      Kwenye Chama ningependa rais kama mwenyekiti awe mkali, akemee chama ndani ya chama kwakuwa sasa ndani ya CCM kuna vi chama vidogo vidogo vya kina Sitta. Kama vipi awaoneshe mlango wa kutokea waende wakaendeshe CCJ yao nje ya CCM.
      Pasco likes this.

    14. #12
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,645
      Rep Power : 4015
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Pasco
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.
      Is it implemented 100% without choosing what to implement and what not? Kwa mfano unapokataa hukusema una vision ya kuona maisha bora kwa kila mtanzania ina maana hukujua unalosema?
      Pasco likes this.
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    15. #13
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,645
      Rep Power : 4015
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Amechagua wasaidizi ambao wamekuwa mzigo mkubwa kwake kwa kufikiri kidogo, kufanya kazi chini ya kiwango na kupenda kuheshimiwa kuliko hata wao kutoa heshima.
      Pasco likes this.
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    16. #14
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,089
      Rep Power : 13049
      Likes Received
      14065
      Likes Given
      14838

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      @capito

      kwenye madini ndo balaa kabisa.
      Jaribu kufuatilia kisa cha kubadili 1998 ming act to 2010 mining act, utashangaa.

      Hao wasimamizi wenyewe wa hiyo Sheria ya madini hawaijui/hawaielewi kivile.
      Wawekezaji wako ahead of the game, wanaijua kama sala ya asubuhi.

      Wanajua mianya yote ya kufanikisha biashara zao iwe kwa uhalali au haramu.

      Na sehemu inayoshangaza kabisa ni mamlaka ya waziri kusaini mkataba wa uchimbaji ambao una power ya ku-overrule mining code. It's absurd!

      Hili sijui kama nimtupie lawama moja kwa moja mkuu, sababu ni suala la kitaalamu zaidi.
      Pasco, John Kangethe and Kaunga like this.

    17. #15
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,144
      Rep Power : 46179
      Likes Received
      6453
      Likes Given
      5321

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Pasco
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.
      Mkuu Pasco hii ni ile ya Nyani kushindwa kujenga nyumba anasema kwa sababu ya uvivu na kusingizia kesho.

      Umeona kabisa viongozi ulio nao hawaendi na mipango yako unayotaka ni wabovu hawaendi na kaksi unayoitaka au vission na mission yako then bado unao tuu.

      Ya nini kupanda kwenye meli na mzigo ambao unajua kabisa kuwa utawafanya mzame . Kwanini asiwaondoe hao vionzozi wabovu akatengeneza hata team mpya ya watendaji hata kwa kipindi kilichobaki wa kufanya kazi na kuendana na kasi yake.

      Anawalea watu kama hao wa nini iwapo wameshindwa kufanya kazi na kuenda na kile anachotaka yeye
      Suala hapa wala sio viongozi wabovu ila vission na mission yake haieleweki lich aya kusaidiwa na ilani ya chama chake ambayo nayo ni mzigo mwingine.

      Ahadi mia na kitu wakati uwezo wa kuzitekeleza hata moja haupo.

      Mikataba ya ajabu ajabu inasainiwa ya kutorosha rasilimali zetu na usimamizi wa kila kitu uko ovyo, hakuna nidhamu ya matumizi kwemnye serikali yake na kila kiongozi anasema na kufanya kile anachoona kinamtoka au kufaa kwa wakati huo hata kama atakuwa anapingana na wenzake.

      Serikali imebaki jina tuu kila mtu na lwake
      Pasco, bilabaye, zumbemkuu and 2 others like this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    18. #16
      zumbemkuu's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 11th September 2010
      Location : street dweller
      Posts : 5,317
      Rep Power : 1998
      Likes Received
      2114
      Likes Given
      7786

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      1, hasimamii kile anachokisema (kwa ufupi ni muongo)
      2, ni mtu kigeugeu
      3, anajifanya msikivu sana kumbe mnafiki.
      4, ni mdini mkubwa.
      5. hajui ni kwanini yupo ikulu na wala hajui majukumu ya mtu anayefika ikulu ni yapi. (anafikiri ikulu ni dangulo au soko la maharamia)
      "watakaotubeza na kututukana wasameheni wanahitaji ukombozi wa fikra" Mh.G.Lema

    19. #17
      timbilimu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Location : DSM
      Posts : 2,662
      Rep Power : 974
      Likes Received
      576
      Likes Given
      10

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Pasco,

      Kama kuna kosa Kikwete alifanya na sasa serikali yake imekua kama nyumba ya Kambale ni kukubari kuchonganishwa na rafiki yake Lowassa! Matokeo toka amejiuzulu hakuna cha maana kinachoendelea, hakuna nidhamu serikalini, kumebakia fitina, majungu na kulalamika!

      Kama miaka mitatu iliyobakia anataka kubaki ktk kumbukumbu hana budi kumpa Uwaziri Mkuu mtu aina ya Magufuri na kuwatema mawaziri wake wengi wa sasa! Kufanya mabadiliko chanya kwa watendaji serikalini. Huko kuna baadhi Makatibu wakuu, Makamishina na Wakurugenzi waliovimbiwa, sasa wanacheua kwa dharau!
      Pasco and Profesa like this.

    20. #18
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,144
      Rep Power : 46179
      Likes Received
      6453
      Likes Given
      5321

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Kongosho
      @capito

      kwenye madini ndo balaa kabisa.
      Jaribu kufuatilia kisa cha kubadili 1998 ming act to 2010 mining act, utashangaa.

      Hao wasimamizi wenyewe wa hiyo Sheria ya madini hawaijui/hawaielewi kivile.
      Wawekezaji wako ahead of the game, wanaijua kama sala ya asubuhi.

      Wanajua mianya yote ya kufanikisha biashara zao iwe kwa uhalali au haramu.

      Na sehemu inayoshangaza kabisa ni mamlaka ya waziri kusaini mkataba wa uchimbaji ambao una power ya ku-overrule mining code. It's absurd!

      Hili sijui kama nimtupie lawama moja kwa moja mkuu, sababu ni suala la kitaalamu zaidi.
      Unarudi pale pale hakuna wa kulaumu maana yeye ndiye aliyewachagua na kuwateuwa kusimamia rasilimali za taifa. Unapokuwa na team ambayo inawez akukaa hotelini na wawekezaji kwa baraka zako na wakasaini mkataba na ukafanya kazi ukiw ana mapungufu na wewe ukakaa kimya bila kuchukua hatua zozote ni balaa sana.

      Kwenye madini ni uozo mtupu na wala hakuna hata wasi wasi wa kuongea hilo. Wawekezaji wanafanya kile wanachoamua maana unapompa mtu kipisi cha ardhi labda hekta 100 za kuchimba madini hapa juu wakati huko chini ya ardhi hujui anaweza kwenda umbali gani ni balaa.

      Ndo hapo unapokuta mwekezaji aliye maybe Kahama ameshaenda umbali unaozidi ule aliopewa juu ya ardhi chini kwa chini wakati juu yeye juu ya ardhi hana ukubwa huo ni balaa
      Pasco and jouneGwalu like this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams

    21. #19
      mbongopopo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2008
      Posts : 969
      Rep Power : 846
      Likes Received
      123
      Likes Given
      119

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      hivi kwa nini nyie mnaojulikana nani humu huwa mnaanzisha threads na kujiwahi humu kujijitetea, mnata vyeo kiaina fulani au?
      Pasco likes this.
      ^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^ ^^^
      SIPENDI MATAPELI WASIOJUA KUTAPELI YAANI WANAOTAKA KUNIFANYA MIMI MJINGA LIVE KAMA WAANDIKA UONGO MITANDAONI NA UKIWA KATIKA MAONGEZI NAO
      ^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^^ ^^^

    22. #20
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 25,089
      Rep Power : 13049
      Likes Received
      14065
      Likes Given
      14838

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      @brialex

      ni kweli kabisa
      sidhani kama sheria ya madini inaongelea uchimbaji at ana angle. At the same time sidhani kama ni kitu rahisi kihivyo.

      Sababu leseni ya madini haiwi in isolation, kila mwenye leseni yake anachunga leseni yake.
      Am sure huu utakuwa wizi

      Anyway, umenipa homework hapa!
      Pasco and Philipo Kidwanga like this.

    23. Study Abroad
    Page 1 of 10 123 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...