Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

    Report Post
    Page 3 of 10 FirstFirst 12345 ... LastLast
    Results 41 to 60 of 183
    1. #1
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,863
      Rep Power : 7377
      Likes Received
      6196
      Likes Given
      22555

      Default Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Wanabodi,
      Baada ya kujadili mazuri na mafanikio ya rais wetu, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, kila kwenye mafanikio hapakosi matatizo, mapungufu au changamoto ambazo zikifanyiwa kazi zinabadilisha hali iliyopo sasa na kutupeleka hali bora zaidi.

      Katika kujadili mapungufu, nawaombeni sana tujadili kwa nidhamu na staha kwa kuzingatia huyu tunayemjadili ni rais wetu, hivyo sitegemei kuona lugha za kebehi, machukizo, matukano, au maudhi, kwa kifupi lugha zozote ambazo hazina staha!.

      Katika kujadili mapungufu, madhaifu, matatizo na changamoto zinazomkabili rais Jakaya Kikwete, nawaombeni tujadili kwa spirit ya constructive criciticism kwa kueleza mapungufu hayo in good faith kwa nia ya kujenga na sio kubomoa.

      Watanzania tumekuwa ni watu wa kilalamika na kunung'unika wakati wote bila kuchukua hatua zozote positive za kurekebisha!. Naomba hii thread sio thread ya malalamiko au manunguniko dhidi ya JK bali thread ya kutoa ushauri nini cha kufanyika!.

      Kwa kuanzia moja ya mapungufu makubwa ya JK ni mtu wa huruma iliyopitiliza mipaka matokeo yake kutafsiriwa kama ni weakness, yaani "JK ni rais dhaifu", weak!, asiyeweza kufanya maamuzi magumu!.

      Mfano wa kwanza wa udhaifu huu wa huruma uliyopitiliza ni pale alipoyasamehe yale majizi ya EPA kwa kuyaruhusu yarudishe fedha yalizo kwiba kwa exchange ya kusemehewa na kutofikishwa mahakamani!. Hata Spika Sitta pia alimlaumu rais JK kwa upole huu!. Lingekuwa ni bunge makini, imperchment process ingeanzia pale pale right away kwa sababu rais hana mamlaka ya kuizuia sheria kuchukua mkondo wake!, huu ni uvunjaji wa katiba ya JMT!.

      Ni upole huo huo ndio unaopelekea hajamwajibisha Waziri wa Afya na naibu wake kwa sababu anawahurumia!.

      Ushauri ni kwa JK kuwa bold na kufanya maamuzi magumu!. Mfano kwenye huu mgomo wa sasa, siungi mkono JK kuitikia shinikizo la madaktari na wanaharakati kumwajibisha Mponda na naibu wake, hiyo nayo ni weakness. Bold decision ni wahusika watakaosabisha kifo chochote, kupandishwa kizimbani kwa murder!.

      JK anatakiwa kupunguza huruma na upendo wa mshumaa kumulikia wenzake huku yeye kwake kunateketea!. Huruma na upendo alioisha uonyesha sasa unatosha!. JK anatakiwa awe mkali kama alivyokuwa Nyerere watu kujua wamefutwa kazi ni kupitia taarifa ya habari ya saa 2:00 usiku ya RTD tena ikisomwa na David Wakati!.(RIP).

      Ni huruma na upendo huu uliopitiliza ndio unapelekea kuwahurumia baadhi ya mawaziri na wasaidizi wake ambao hawamsaidii hivyo kuendelea kuwabeba!.

      Kwa vile JK hawezi kufanya kila kitu, piga chini wale wote ambao hawakusaidii hata ikibidi kumpiga chini Pinda, piga chini ili uliokoe taifa katika kipindi hiki chako cha miaka 3 kilichobakia!.

      Nawatakia majadiliano mema.

      Natanguliza shukrani kwa kuzingatia spirit ya constructive criticisim in good faith kwa nia ya kujenga na sio kubomoa!.

      Wasalaam

      Pasco wa jf.

      NB. Kama hauwezi constructive criticisim unaweza kujisomee tuu na kuishia zako bila kuchangia, kwani sio lazima uchangie kila thread!.
      Last edited by Pasco; 2nd February 2013 at 06:06.


    2. #41
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 12,501
      Rep Power : 24259
      Likes Received
      5136
      Likes Given
      2743

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By crazyworld View Post
      Zumbemkuu nimekubaliana nawe.
      Alisema wakati madakatari walipogoma alikaa kimya akaenda Davos kula kuku. Waliporejea kazini akijitokeza na kusema atahakikisha mgomo hautatokea tena. Leo hii tunashuhudia chini ya wiki mbili baada ya kauli hiyo wamegoma na yuko kimya. Sijui anajiandaa kwenda kula kuku tena wapi!!!
      Vile yuko kaskazini lazima atinge Bilila Kempiski(sijui na yenyewe ishakuwa Hyatt)

      Pasco and zumbemkuu like this.

      Zogolo Dangu Dawika Miye!


    3. #42
      Jembe_Ulaya's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 109
      Rep Power : 458
      Likes Received
      32
      Likes Given
      7

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Sidhani kama ana huruma, mimi naona ni kiburi, huwa hashauriki hasa kwa mambo sensitive yanayohusu nchi. Ni mtu wa kupokea tuu ushauri kutoka kwa wasaidizi wake matokeo yake nchi inaendeshwa kwa majungu na visasi. Kwa maana nyingine hana uwezo wa kutoa maamuzi.

      Mfano mzuri badala ya kutumia bongo kuongoza na kukuza uchumi kwa kutumia rasilimali tulizokuwa nazo yeye anaamini kuwa omba omba kwa mataifa ya nje ndiyo uchumi utakuwa.

      Kwa kweli matarajio yangu kwake yamekwisha kabisa.
      Pasco likes this.

    4. #43
      zimmerman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2011
      Posts : 347
      Rep Power : 567
      Likes Received
      260
      Likes Given
      66

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Mapungufu ya Kikwete unaweza kuyatambua haraka sana hasa ukimlinganisha na urais wa Mkapa. Kwanza, Kikwete ni mtu aliyetamani sana kwenda Ikulu. Na Mwalimu alionya kwamba ukiona mtu ana uchu wa kupitiliza kuwa rais hyo tu inapaswa kuwa signal kwa wapiga kuara kuwa huyo mtu hatufai kama kiongozi na ni wa kuogopa kama ukoma. Sasa sijui sisi wabongo tunamuenzi vipi Nyerere ikiwa hata maonyo yake ya msingi tuliyapuuza 2005 na tukayapuuza tena 2010.

      Pili, kama ambavyo wengine wameshasema, Kikwete ana popstar mentality hivi. Hauchukulii urais kama kazi ya kihistoria ya kubadilisha maisha ya watanzania. Yeye kwake ni bora liende -- "Nyerere alianza hakuyamaliza, Mwinyi akaja hakuayamaliza, Mkapa akapita hakuyamaliza na hata yeye watu wasitegemee kwamba mimi nitayamaliza".

      Tatu, tofauti na Mkapa, Kikwete hana kipaji cha kupanga timu nzuri ya wasaidizi yenye kuleta matokeo bora kiuchumi na kimaendeleo. Namba mbili wake kwa awamu zote ni bogus, Lowassa ni fisadi aliyekubuhu, Pinda amepinda balaa. Kule Ikulu yupo Wassira na Lukuvi, astagafirulahi! Mwenye auheni katika timu yake ni Magufuli tu, na ukijaribu kuchunguza sana, Magufuli alisajiliwa na Mkapa.
      Pasco and Henge like this.

    5. #44
      Safari_ni_Safari's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th October 2007
      Location : Kibaruani
      Posts : 12,501
      Rep Power : 24259
      Likes Received
      5136
      Likes Given
      2743

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Nadhani anawaogopa wasaidizi wake.........au hapendi kuwaudhi kimaamuzi
      Pasco likes this.

      Zogolo Dangu Dawika Miye!


    6. #45
      Mr Rocky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Hungumalwa
      Posts : 9,728
      Rep Power : 68647
      Likes Received
      7106
      Likes Given
      5619

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By jouneGwalu View Post
      Duh!
      Siamini kama na wewe Pasco unanunua huo utumbo...
      Kwa mara ya kwanza nimeanza kuelewa mjadala wako na MTM..



      Ok, sawa "JK ameangushwa"
      sasa itasaidia nini sisi kuorodhesha mapufu yake hapa??
      Sababu hao "watendaji" aliowategemea ni bado anawategemea....
      Kwa maana yako ni kuwa JK yupo chini kaanguka na hatoamka sababu bado yupo na watendaji walewale...
      Haitafaa kitu kwa miaka hii 3 iliyobaki.
      Mkuu tegemea maafa zaidi ya haya kwa miaka mitatu ijayo
      Maana hakuna litakalofanyika na wala tusitegemee lolote kuwa bora chini ya watu waliopo hapa kwa sasa
      Pasco and jouneGwalu like this.
      When you are in Love you can't fall asleep because reality is better than your dreams


    7. #46
      Lu-ma-ga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2010
      Posts : 1,936
      Rep Power : 835
      Likes Received
      549
      Likes Given
      8

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      JK hakujiandaa yeye binafsi kuwa rais wa Tanzania, bali aliandaliwa na wana-mtandao ambao nao walijiandaa kuja kukwapua mara baada ya kumuweka ikulu.JK alizidiwa kwa mbali sana na wakuu wa mtandao RA na EL, WOTE HAWA LEO HAWANA shida naye tena. RA tayari ameshatoka kwenye chama na hivyo tracing ya his where about is too remote.EL yeye amejikusanyia njugu za kutosha kuhakikisha anatinga magogoni at any cost.

      JK kaachwa hana pa kushika kila kitu anaona mzigo kwani hata washauri wake ni wanamtandao waliowekwa na RA na EL na hivyo hawako kwa maslahi ya JK
      Pasco likes this.

    8. #47
      iduda's Avatar
      Member Array
      Join Date : 5th February 2012
      Posts : 33
      Rep Power : 378
      Likes Received
      5
      Likes Given
      0

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Kaka, I really buy your comments!!!!!!!!!!!!!!! This government headed by this guy is like a bunch of commedians, I can not see anyone and anywhere within this government who can act diligently for the benefits of the nation............. Wote wamepotea na wamepoteza ujasiri hakuna hata mwenye mark ya uzalendo, tunakwenda wapi ndugu zangu. Mbaya zaidi mkulu wao ndo haeleweki haeleweki, kwa mtu mwenye akili timamu huwezi kumteua mtu akusaidie kuongoza then anakudiappoint unalalamika badala ya kuact accordingly..... Haina jipya huyu jamaa na hana la kujitetea............ Kazi tunayo, sioni Tanzania baada ya uongozi wa Kikwete...........
      Pasco likes this.

    9. FJM is offline
      FJM
      #48
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,213
      Rep Power : 2580
      Likes Received
      5344
      Likes Given
      4607

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Rais Kikwete ana tatizo moja tu, anapenda kuwa rais lakini hapendi/anakwepa majukumu yanayoambata na urais. Cheng nyingi!
      Pasco likes this.

    10. #49
      Kongosho's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st March 2011
      Location : Location loading...
      Posts : 26,193
      Rep Power : 25454
      Likes Received
      14890
      Likes Given
      15864

      Default

      JG, kuna msemo
      'everyone has a price, the problem is to know what it is'

      (am just thinking loud)

      Quote By jouneGwalu View Post
      Duh!
      Siamini kama na wewe Pasco unanunua huo utumbo...
      Kwa mara ya kwanza nimeanza kuelewa mjadala wako na MTM..
      Last edited by Kongosho; 8th March 2012 at 14:54.
      Pasco likes this.

    11. #50
      Bulesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2008
      Posts : 3,384
      Rep Power : 1252
      Likes Received
      350
      Likes Given
      74

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Pasco View Post
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.
      Kufuatana na maelezo yako inaelekea hujui tofauti kati ya VISION na MISSION!! Vision ni maono yako unavyotaka vitu viwe na Mission ni jinsi utakavyofanikisha kufikia hayo malengo ya maono yako!! Tukirudi kwenye mada, Jakaya ana mapungufu ya kuamini sana ushirikina katika utendaji wake!![ usiniambie nikupe ushahidi kwani Sheikh Yahya kafa!!] Maisha bora kwa kila mtanzania haiwezi kuwa mission!!

    12. #51
      Sumba-Wanga's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd February 2011
      Location : Gambushi
      Posts : 4,326
      Rep Power : 1290
      Likes Received
      873
      Likes Given
      938

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Zion Daughter View Post
      Safari za nje ya nji zipungue.Sometimes anaambata na umati wa watu na wote wanagharamiwa na kodi ya wananchi.Sometimes kuna safari amabazo waziri wa mambo ya nje au mawaziri husika wanaweza kuwakilisha na wapunguze idadi ya wasindikizaji.
      JK anasafiri na umati wa watu, wenhi wao hawana lolote, wanakwenda SHOPPING!
      Ni mzigo kwa wananchi.
      No wonder teachers and doctors are striking!
      "A man's or woman's best or worst choice in life is his or her spouse"

    13. Awo is offline
      Awo
      #52
      Awo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 12th April 2010
      Posts : 440
      Rep Power : 0
      Likes Received
      159
      Likes Given
      36

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Tatizo la Kikwete ni moja tu - uvivu! Si mchapakazi. Hasomi wala hafikiri wala haandiki. Rais gani huyo?

    14. #53
      Keil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2007
      Posts : 2,381
      Rep Power : 1094
      Likes Received
      756
      Likes Given
      292

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Pasco View Post
      Mfano wa kwanza wa udhaifu huu wa huruma uliyopitiliza ni pale alipowasamehe majizi ya EPA na kutaruhusu yarudishe fedha yalizo kwiba na kusemehewa kutofikishwa mahakamani!. Spika Sitta pia alimlaumu rais JK kwa upole huu! Lingekuwa ni bunge makini, imperchment process ingeanza right away!
      Mkuu Pasco,

      Si kweli kwamba ni huruma ndio ilimfanya awaache waachiwe. Ni kwamba the whole saga ya EPA ilikuwa inagusa fedha za kampeni yake na pia ilikuwa inagusa watu wake wa karibu na hakuwa tayari kuwashughulikia. Ndio maana mpaka leo hii akina Maranda wanatumikia kifungo na wengine kesi zao hazisongi mbele na wengine hawajafikishwa mahakamani, lakini ki-misingi wote walifanya makosa yanayofanana. Lugha nzuri hapa ni kwamba JK ni mnafiki, huwa haamanishi kile anachosema.

    15. #54
      Gwalihenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2011
      Posts : 2,494
      Rep Power : 909
      Likes Received
      650
      Likes Given
      414

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Waberoya View Post
      hizi sentensi huwa zinasemwa sana na majuha wa CCM

      Juzi mnyika kasema hivi hivi
      leo ww unasema hivi hivi

      kesho sijui nani atasema

      You are dead wrong my dear pasco........all i can say no is think again and you have a room to correct that view!
      Kwani Mnyika naye ni juha wa CCM?, au ni Mnyika gani unaye mzungumzia hapa?

    16. #55
      Keil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd July 2007
      Posts : 2,381
      Rep Power : 1094
      Likes Received
      756
      Likes Given
      292

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Sasa nitoe constructive criticisms.

      JK ni Rais anayependa sifa, hilo ni tatizo ambalo litagharimu sana legacy yake. Hotuba yake ya kwanza kwa Bunge lake akiwa kama Rais, aliahidi mambo mengi sana ambayo kama angeyatekeleza yangeweza kumpa umaarufu mkubwa sana, lakini ilipokuja kwenye utekelezaji ilikuwa ni zero. Mfano, aliahidi kurudisha nyumba zilizouzwa na serikali ya Mkapa, hakutimiza. Aliahidi kupitia upya mikataba mipya, hakuna kilichofanyika. Aliahidi kupambana na ufisadi, lakini akawa wa kwanza kuficha uvundo wa ufisadi wa Mkapa, Chenge na wengineo wengi ambao walikuwa wamegubikwa na tuhuma za ufisadi ambazo ushahidi wake ulikuwa wazi kabisa.

      Mwaka 2005 hakuuzwa na Ilani ya Chama chake, bali aliuzwa na mtandao, vyombo vya habari na ule unafiki wake kwamba yeye ni mtu wa watu. Ndio maana kila kukicha utamuona yuko kwenye misiba. A day baada ya kuchaguliwa kuwa Rais alidamkia Muhimbili, watu wakasema sasa tumepata Rais atakayejali afya za walalahoi. Sasa kama Rais anajali afya za walalahoi na watendaji wakuu wa Wizara ya Afya wana tuhuma kibao, kwanini hizo tuhuma zisifuatiliwe? Halafu leo anasema hawezi kufanya mabadiliko kwa shinikizo la madaktari, sasa kama wameona kwamba viongozi wa wizara hawafai, wao wafanye nini?

      Nani anafanya assessment ya utendaji kazi wa kiongozi? Ni Appointing Authority au yule anayeongozwa? Mjomba alishasema tutapima size ya kiatu after 5 yrs, so the Drs have all the rights za ku-judge utendaji kazi wa mawaziri wa wizara yao.

      Nije swala la Katiba, pia JK kwa kupenda sifa na alipoona kwamba upinzani unapata umaarufu, alikurupuka na kuahidi katiba mpya. Bahati mbaya hakujua kwamba Katiba mpya inamuweka mahali pagumu zaidi maana wana CCM walikuwa hawataki mabadiliko. Matokeo yake mwanzo kwenye hotuba akawasema wapinzani na kudai kwamba atajaribu u-dictator na baadaye akaja kulamba matapishi yake kwa kuwaruhusu wapinzani wapeleke mapendekezo yao na alikubaliana nao. JK alifanya hivyo baada ya kuona wananchi wako against msimamo wa chama chake. Ndio maana nasema kwamba JK anapenda sana sifa na hiyo ni weakness mbaya sana.

      Kitendo cha kupata 61% kwenye uchaguzi uliopita, lilikuwa ni pigo kubwa sana kwa JK, hakutegemea ashuke kutoka 80% mpaka hapo, na hapo NEC (Tume ya Uchaguzi) ilikuwa imemsaidia sana kuchakachua na yeye anajua hilo. Kama wasingemsaidia, hata hizo 61 zisingefika. Ndipo akaunda Kamati ya Mukama kuchunguza kiini cha CCM kufanya vibaya kwenye huo uchaguzi. Ndipo ikaja Falsafa ya Vua Gamba, ambayo nayo imezidi kumuweka pabaya maana ameshindwa kuitekeleza kama wananchi walivyokuwa wakitegemea.

      To conclude, ni kwamba kwa kuwa Rais wetu anapenda masifa, mara nyingi huwa ni mkurupukaji wa kuweka ahadi tamu na nzuri kusikika masikioni mwa wananchi bila kuzifanyia tathimini ya kina ili kuona kama ni ahadi ambazo zinatekelezeka au la. Matokeo yake sasa, Pinda ndo amekuwa mbebeshwa lawama halafu JK yuko kimya hasemi kitu kabisa na hasa akishapima upepo kwamba wananchi wako against. Ninamuonea huruma Pinda kwa kuwa wakati mwingine ni ngumu sana kufanya kazi na mtu ambaye anapenda credit iende kwake all the time na mabaya yote wabebeshwe wengine.

    17. #56
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,353
      Rep Power : 3065
      Likes Received
      3110
      Likes Given
      4232

      Default

      Quote By Pasco View Post
      Quote By Kongosho View Post
      aliingia kwenye urais bila vission wala mission.
      Hili ni pungufu kubwa sana hata katika maisha ya mtu mmoja mmoja.

      Katika ngazi ya uraisi ni balaa zaidi.
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.
      Pasco, kama wasaidizi ndo wanamuangusha, sasa mbona yeye ndo bingwa wa kuwalinda? Mifano ya Jairo, ngeleja, wahusika wa EPA ambao wapo kwenye serikali na chama chake?

      Au tufanye hivi, ni watumishi na wasaidizi wake wepi hao wanaomuangusha? Yeye anajua hilo? Kama anajua anafanya nini? Kama hajui ni kwanini hajui wakati mtu kama wewe pasco wa jf unajua kwamba wasaidizi ndo wanamuangusha?

      This is a lame excuse...!
      * LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF

    18. #57
      Bigirita's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th February 2007
      Location : Under a mango tree
      Posts : 11,353
      Rep Power : 3065
      Likes Received
      3110
      Likes Given
      4232

      Default

      Kail. Salute for the piece well presented!
      Keil likes this.
      * LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF

    19. #58
      nderingosha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th March 2011
      Posts : 871
      Rep Power : 1463
      Likes Received
      457
      Likes Given
      130

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      TZ haijawahi kuwa na haitakuja kuwa na rais dhaifu kama JK....i can swear on this....hata Mzee Mwinyi alikuwa bora mara dufu kumzidi JK......Mwinyi yeye uzuri wake alikuwa anatambua udhaifu wake na hivyo alijitahidi kuweka washauri makini kwenye mambo ya msingi kama uchumi at least akamaliza urais wake bila mabalaa na vilio kama anayoleta JK TZ ya sasa....

      Nasema hatujawa na hatutakuja daima kuwa na rais hovyo kama tulie nae sasa.......mtu anayejifanya mjuaji kumbe hamnazo....mtu aliyepewa madaraka makubwa na katiba kuisimamia nchi lakini anachofanya ni mzaha......mtu mwenye majibu mepesi siku zote kwa mambo makubwa ya nchi.....kwa kifupi hatuna rais serious TZ kuelekea karibu miaka 10 sasa...kosa walilolifanya watanzania kumpa huyu bwana urais watalijutia kwa miaka mingi saaana.......ifike mahali sasa watanzania wajifunze....

    20. #59
      RedDevil's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th April 2009
      Location : Hapa Hapa
      Posts : 1,457
      Rep Power : 807
      Likes Received
      271
      Likes Given
      516

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Mtandao ndiyo sumu ya serikali ya JK!!
      "Never argue with stupid people, they will drag you down to their level and then beat you with experience" Mark Twain

    21. #60
      Kwame Nkrumah's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2008
      Posts : 858
      Rep Power : 709
      Likes Received
      291
      Likes Given
      295

      Default Re: Mapungufu ya JK: Constructive Criticisim!

      Quote By Pasco View Post
      Mkuu Kongosho, mission na vission ni ile ilani ya uchaguzi aliyoinadi na kuchaguliwa. He had a mission ya maisha bora kwa kila Mtanzania na vision Tanzania yenye neema inawezekana kupitia ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya!. Watendaji aliowategemea ndio wamemwangusha!.
      Hamna kitu kinachotukwamisha kimaendeleo kama hii kauli.
      Haina tofauti na mchakato unaendelea, upembuzi yakinifu unafanyika na juhudi za kutafuta wahisani zinafanyika.
      Yeye ni mtendaji mkuu, [ unlike, say Rais wa Israel, au German, au Malkia wa UK], ni mkuu wa majeshi, ana power of the purse, anachagua hao watendaji without approval from anybody/anything.
      Come on Pasco, spare us this nonsense.
      I take it personal with Mafisadi.

    Page 3 of 10 FirstFirst 12345 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...