Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

    Report Post
    Page 1 of 23 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 442
    1. #1
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6153
      Likes Given
      22273

      Default Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Wanabodi,
      Naangalia TBC Live, Rais Jakaya Kikwete yuko hewani!
      Miongoni wa mazuri ya JK, ni having a good sense of humour, akiongea, huchoki kumsikiliza!.
      Alipokuwa akiongelea kilimo cha ndizi kijijini kwao Msoga, Bagamoyo, akasema wakulima wana bananisha migomba mingi kwenye shina moja, matokeo yake kila mgomba unatoa kichane kimoja au viwili ya vindizi vilivyokondeana!.

      Akasema wanakijiji wale wanalima hivyo kwa sababu hawajui kuwa kama wakiacha mgomba mmoja kwenye shina moja, mgomba huo utatoa mkungu mkubwa wa ndizi, na ndizi zenyewe zitakuwa ni ndizi za shibe kama "Mrisho Mpoto"!. Ukumbi mzima ulizizima kwa vicheko, watu hawana mbavu!.

      Kuwa na 'good sense of humour' ni kipaji na ni miongoni mwa mambo mazuri machache ya rais wetu Jakaya Kikwete, besides good looking!.

      Kwa wale wenye kumbukumbu ya hotuba za Mwalimu, ukiondoa ile hotuba yake ya kutangaza vita, hotuba za Mwalimu, watu walikuwa wanacheka na hutamani amalize kuzungumza!.

      Hii ni thread ya miongoni mwa mazuri ya JK, kama na wewe unalo zuri lolote la JK ambalo unalijua, unaweza kuliweka.

      Kwa vile tunazungumzia mazuri, ningeomba wale ambao hawana zuri lolote la kuzungumzia JK, sio lazima mchangie, wala zuri hili la "good sense of humour", haimaanishi JK sasa ndio rais bora kwa Tanzania, wala haina maana ndio hana mabaya yake!, leo tuzungumzie mazuri yake!

      Angalizo:
      Wanabodi wenzangu, tunajukumu la kujimoderate sisi wenyewe kulinda hadhi ya jukwaa letu, haiwezekana kila siku sisi tukawa ni watu wa kulalamika tuu, au kubonda tuu, mara moja moja kwenye mazuri, pia tutoe sifa pale panapo stahili!.

      Natanguliza Shukrani kwa kunielewa!

      Asanteni!

      Pasco (wa jf)

      Note: Pasco wa jf, sio mwanachama wa chama chochote cha siasa, bali ni muumini wa ukweli "seek the truth, and the truth will set you free"!. Kwa wale wanaofikiri Pasco wa jf, ni mshabiki wa CCM, tafuteni thread yangu ya "CCM Imechokwa" !.


      --------------------------------------------
      Hoja Nyingine za Thread ya kibananhukhu iliyounganishwa #148
      Quote By kibananhukhu
      Pamoja na list ya mambo lukuki ambayo wakuu mnamlaumu JK, lakini ni kweli kuwa kuna kitu anafanya siyo kwamba amelele fofofo. Kuna mapungufu pia ni kwa nia njema mnayaainisha kusaidia uboreshaji kazi. Nimefuatilia na kuyaona baadhi ya mazuri ya JK Kama list inavyoainisha, ninaweza kuwa na upungufu kidogo katika takwimu hii itatokana na mimi kutumia kumbukumbu zangu nipo tayari kusahihishwa takwimu. Tupitie mazuri ya JK HAPA CHINI

      1. Mpango wa kuiruhusu bandari (THA) kufanya kazi kwa kuanza na technologia mpya ili dereva tu ndiye awe anakwenda bandarini kupakia mzigo na mengine yote yatamalizwa kwa njia ya mtandao, e-port. Kumbukeni TICTS walikuwa na mkataba mbaya sana kwa miaka 15, na ulirejewa kwa mazingira ya kutatanisha.

      2. Dar tayari nyumba 50 zimeanza kutumia gesi kwa matumizi mbali mbali ya ndani, kama ulaya na kwingineko kwa mara ya kwanza. Mikocheni wameanza jiandaeni kuvuta gesi majumbani kwenu.

      3. Magari yameaanza kutumia gesi japokuwa bado kuna baadhi ya vikwazo kwa wasaidizi wa raisi. Mpango wa JK ilikuwa matuzi ya petroli katika gari yapungue kwa 80%, lkn ukiritimba wetu umesababisha yapungue kwa 55%

      4. Kivuko na daraja kigamboni.

      5. Mradi wa daraja Maragalasi na lami Tabora – Itigi – Kigoma

      6. Ujenzi wa barabara lami kutoka Mombo, Mtibwa turiani, Kilosa, Mikumi na baadaye ifakara, mahenge, Malinyi, Songea. Pia Ifakara, Mlimba hadi Njombe. Usafiri wa songea kupunguza safari kwa masaa 5.

      7. Barabara ya Mafinga, Iringa, Kitonga, Ruaha Mbuyuni, Madaraja mawili mpakani na morogoro imekwishapanuliwa kwa uboro wa hali ya juu. Kipande cha Ipogolo kupandisha kwenda iringa mjini kimepanuliwa sana.

      8. Bara bara ya Iringa Kwenda Dodoma Imekwishaanza

      9. Bara bara ya Tunduma hadi Sumbawanga kuna makandarasi watatu wanashindana kwa ubora wa lami.

      10. Viwanja vya ndege mikoani kuboreshwa.

      11. Karekebisha mkataba wa Songas, ulikuwa hauruhusu mtu meingine yetote awaye kujenga tena bomba la gesi. Sasahivi wakuu mnaruhusiwa kujenga mabomba ya gesi kutoka Kusini.

      12. Mkataba wa wachina na serikali kujenga bomba la gesi kutoka Mtwara hadi dar ili kuzalisha MG 2900 za umeme dar.

      13. Barabara Dodoma, Manyara lami.

      14. Ujenzi reli kutoka Tanga, Musoma, Uganda.

      15. Ujenzi bandari, Tanga, Mtwara na Babamoyo

      16. Uwanja wa Ndege Terminal two wajengwa.

      17. Maeneo ya Umwagiliaji maji, hekari 20,000 zimejengwa na lengo ni ekari 1milioni.

      18. Kilimo kwanza mashamba darasa na ongezeko la mavuno kwa ekari.

      19. Tanzania ni ya kwanza kwa export afrika masharik na kati

      20. Mradi wa makaa ya Mawe Mchuchuma na katewaka liganga kuzalisha MGW za kutosha nchi nzima

      21. Mradi wa machimbo mgodi wa chuma Liganga, uzalishaji wa Titanium, Vanadium, Fe kwa ajili ya utengenezaji nondo, malighafi ya mabati, vyuma vya kujengea madaraja na maghorofa, kuweka pembezoni mwa mabarabara kuzalishwa nchini. Viwanda vya kutengeneza vifaa vya ujenzi wa meli, ndege, na magari kujengwa nchini.

      22. Machimbo ya makaa yam awe Ngaka Mbinga Ruvuma, uwezo Kuzalisha pia umeme MG 400.

      23. Hospitali upasuaji moyo kwa mara ya kwanza Tanzania.

      24. Hospitali kubwa mingoni mwa zitakazoheshimika kujengwa Tanzania na Appollo ya India. Maradhi yote kutibiwa Tanzania.

      25. Uboreshaji shirika la nyumba NHC, Baadhi ya watanzania kunufaika na mikopo ya nyumba na nyumba kuanza kujengwa kwa spidi kali.

      26. Ujenzi wa barabara nane Dar hadi chalinze.

      27. Ufumuaji na ujenzi wa reli ya kati dar, hadi kigoma, mwanza, mpanda, Rwanda na Burundi.

      28. Ubareshaji maabara shule za kata ($ 90Milioni)

      29. Idadi ya walimu kwaajili ya shule za kata na nyinginezo kuanzia muda mfupi ujao, walimu elfu 40 kuhitimu kila mwaka.

      30. Baadhi ya shule nyingi binafsi zimeanza kudorola au kufungwa kabisha, wengi wamejiunga na shule za kata na ubora unapanda japo kwa spidi ndogo.

      31. Idadi kubwa ya wanafunzi vyuo vikuu, Udom uwezo elfu 40, SAUT elfu 15, UDSM Elfu 15, Ruco elf 2.5, Mkwawa elfu 2.5 Tumaini elfu 2, Open University elfu 20 nk.

      32. Wafanya biashara wamepewa kipau mbele term ya JK, Wengi husafiri na Mheshimiwa Raisi kutafuta na kupata fursa za biashara nje.

      33. Uhuru wa Vyombo vya habari, waandishi wanafanya mambo kwa uhuru ambao wasingelithubutu enzi ya Mwalimu, Mwinyi wala Mkapa. Hata baadhi ya ninyi wakuu, mnaruhusuwa kutoa mawazo yenu japo wengine wanatukana matusi ya nguoni lakini JK anavumilia sana.

      34. Amegundua fitna nyingi sana serikalini, majungu, uongo na sasa hivi anakua mwangalifu sana katika maamuzi na inalazimika kuonekana kana kwamba hana maamuzi ili awe na subira. (Ukiwa na hasiri usifanye maamuzi, ahirisha upate busara)

      35. Makampuni ya madini, yamekupali kuanza kulapa 30% kutoka faida zitakazo patikana kuanzia 2012.

      36. Wapinzani wameanza kumwelewa na kumsifia kwa yale anayoyafanya vizuri.

      37. Mnaweza ongeza list nyingine ili nije baadaye na listi ya faida za kiuchumi kwa taarifa tu, inflation inachangiwa na gharama za chakula kwa 16%.

      Kuna mambo madogo ya kiufundi yakirekebishwa inflation inapashwa iwe 8% single digit. Mfano mahindi yanaoza Ruvuma, Iringa, na Sumbawanga yangeweza kutoa mchango katika kupunguza gharama za chakula na mfumuko wa bei ukashuka.Mengine mengi nitaongeza baadaye. Nadhani kwa faida ya wakuu wangu, nitajitahidi kufuatilia pia ilani yake ili nilinganishe na hayo hapo juu. Hata hivyo, ni ukweli kwamba kwa upanda wa barabara tu, miaka 50 tangu uhuru lami ilifikia km 6000, JK Pekee ameweka mikataba ya lami km 11,000.

      Kuna vitu anafanya JK.
      Last edited by Viwango; 6th March 2012 at 11:52. Reason: Adding points of merged thread

    2. Miaka 50

    3. #2
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,646
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      we have a very outgoing president, no doubt about it...but what about other leadership issues?
      Jasusi, Pasco, The Boss and 3 others like this.
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    4. #3
      Songoro's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2009
      Posts : 2,222
      Rep Power : 0
      Likes Received
      487
      Likes Given
      21

      Default Re: BEI MPYA YA UMEME: CHADEMA, wasomi, wanaharakati wapinga bei mpya

      Jk ana moyo wa subira sana hata kwa yale anayozushiwa ana uvumilivu wa kukaa kimya bila kuwatisha wazushi,uhuru wa kujieleza sasa upo juu kuliko kipindi chochote tangu mungu kaumba dunia hii!!,mgogoro wa Znz kaumaliza bila ya watu kutegemea,wanafunzi hata wa div 3 sasa wana uhakika wa kupata shahada, kaikumbuka sana mikoa ya magharibi kuliko Rais yoyote wa Tz kabla yake.

    5. #4
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6153
      Likes Given
      22273

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Quote By Ndahani
      we have a very outgoing president, no doubt about it...but what about other leadership issues?
      Mkuu Ndahani, hiyo "outgoing", nayo ni sifa, huko ndiko kuwa "mtu wa watu"!. mimi nimeziweka mbili, hiyo ya good sense of humour na good looking!, hizo nyingine, naomba uzireserve kwa thread yake, kwa sababu hizi nilizoziweka mimi ndio inawezekana zilizotufanya tumchague in the first place!, kwani imefanywa research yoyote kuangalia Watanzania wanachagua nini, au wanaangalia nini ndipo wachague?!. Njua research iliyofanywa Marekani, wakagundua wanawake wengi wanapenda kumchagua mtu kutokana na "good looking"! na "the way he speaks"!, kwa vile huku hatujafanya utafiti rasmi, miongoni mwa sifa za kuteuliwa CCM, ni jee mgombea, unauzika?, anakubalika?, anatazamika?, anachagulika?, unapitishwa!, sinauhakika kama wanaangalia, jee ana uwezo?!.
      Ndahani likes this.

    6. #5
      Maundumula's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 4,921
      Rep Power : 3095
      Likes Received
      1341
      Likes Given
      5656

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Can mods make this thread sticky even for one day? Obviously no!!
      Pasco, theROOM and lady roranky like this.

    7. FemaTV & Radio

    8. #6
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6153
      Likes Given
      22273

      Default Re: BEI MPYA YA UMEME: CHADEMA, wasomi, wanaharakati wapinga bei mpya

      Quote By Songoro
      Jk ana moyo wa subira sana hata kwa yale anayozushiwa ana uvumilivu wa kukaa kimya bila kuwatisha wazushi,uhuru wa kujieleza sasa upo juu kuliko kipindi chochote tangu mungu kaumba dunia hii!!,mgogoro wa Znz kaumaliza bila ya watu kutegemea,wanafunzi hata wa div 3 sasa wana uhakika wa kupata shahada, kaikumbuka sana mikoa ya magharibi kuliko Rais yoyote wa Tz kabla yake.
      Mkuu Songoro, hiki ndicho ninachokisema kulinda hadhi ya jukwaa letu, pamoja na mabaya yake, pamoja na ubovu wa time yake, pamoja na madhaifu yake kama binadamu yoyote, pia anayo mazuri, anayo mema, etc, mara moja moja kwenye mazuri tukubali kuyakubali na tusifie, na kwenye uborongaji tuendelee kuwabalasa ili wafanye kila walivhopaswa kufanya!. Humu jf, tuna wenzetu wengi wana ugonjwa unaitwa "hate" bila wao kujijua, hivyo kujikuta wanaishia kuwa "hate preachers", kwao hakuna jema, ni chuki tuu kwa kwenda mbele!.

    9. #7
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,623
      Rep Power : 2892
      Likes Received
      3839
      Likes Given
      12234

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Quote By Ndahani
      we have a very outgoing president, no doubt about it...but what about other leadership issues?
      Yeah, sense of humour na kujionyesha kuwa karibu na watu lakini sera zake zinawakumbatia zaidi wanyonyaji na mafisadi.
      Afadhali hata angekuwa comedian badala ya kuwa kiongozi wa nchi.

    10. #8
      Raia Mwema's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th June 2008
      Posts : 536
      Rep Power : 663
      Likes Received
      77
      Likes Given
      27

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Pasco

      leo umeleta thread ya maana hebu tujaribu kuzungumzia japo mazuri machache ya Jk. Hakuna binadamu asiye na zuri hata moja

      Mimi nitamkumbuka kwa kutununulia Panton la magogoni - Kigamboni. kabla ya hapo ilikuwa ni mateso.

      Panton kubwa Afrika Mashariki na kati hadi Mwai kibaki alikuwa kuliona alipotembelea Tanzania na akaahidi kuwanunulia wakenya

      Linabeba magari 60 na abiria 2000

      Na sasa ujenzi wa daraja la Kigamboni umeanza
      Pasco, Ferds, Lokissa and 4 others like this.

    11. #9
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,646
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Quote By Pasco
      Mkuu Ndahani, hiyo "outgoing", nayo ni sifa, huko ndiko kuwa "mtu wa watu"!. mimi nimeziweka mbili, hiyo ya good sense of humour na good looking!, hizo nyingine, naomba uzireserve kwa thread yake, kwa sababu hizi nilizoziweka mimi ndio inawezekana zilizotufanya tumchague in the first place!, kwani imefanywa research yoyote kuangalia Watanzania wanachagua nini, au wanaangalia nini ndipo wachague?!. Njua research iliyofanywa Marekani, wakagundua wanawake wengi wanapenda kumchagua mtu kutokana na "good looking"! na "the way he speaks"!, kwa vile huku hatujafanya utafiti rasmi, miongoni mwa sifa za kuteuliwa CCM, ni jee mgombea, unauzika?, anakubalika?, anatazamika?, anachagulika?, unapitishwa!, sinauhakika kama wanaangalia, jee ana uwezo?!.
      nakubaliana na wewe Pasco...tuliocheza chipukizi tunaelewa unamaanisha nini. Ndo maana enzi nilikuwa naamini kwenye ukubwa na uzuri wa iliyokuwa USSR. Kwa hili la kilichotufanya tumchague ni kipi, kimenifanya nifikiri tofauti na kwa kuanzia nimeamua kukumbuka ule wimbo wetu maarufu ulioonyesha ukuu wa USSR, National Anthem of USSR - YouTube.
      President wetu angelikuwa ni mmoja ya watu vipenzi wa watanzania maana alituvutia kwa mengi, lol!
      Pasco, dewj and statila like this.
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    12. #10
      Ndahani's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 9,646
      Rep Power : 4016
      Likes Received
      2940
      Likes Given
      5063

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Quote By Jasusi
      Yeah, sense of humour na kujionyesha kuwa karibu na watu lakini sera zake zinawakumbatia zaidi wanyonyaji na mafisadi.
      Afadhali hata angekuwa comedian badala ya kuwa kiongozi wa nchi.

      Jasusi, mtoa mada anashauri tujadili kwanini alichaguliwa kwa "kishindo". Ingawa inawezekana kukawa na kufeli kwa "kishindo vile vile"
      Jasusi, Pasco and Ronal Reagan like this.
      We are all inventors, each sailing out on a voyage of discovery, guided each by a private chart, of which there is no duplicate. The world is all gates, all opportunities.
      Ralph Waldo Emerson

    13. #11
      Raia Mwema's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th June 2008
      Posts : 536
      Rep Power : 663
      Likes Received
      77
      Likes Given
      27

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      nitamkumbuka Jk kwa


      katiba mpya.
      kwa chuo cha Dodoma
      Ndahani, Ferds, mkomatembo and 1 others like this.

    14. #12
      tedo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th August 2011
      Location : uchochoroni
      Posts : 5,479
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1259
      Likes Given
      880

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      nitamkumbuka jk kwa kucheka cheka kwake kwani ni rais pekee anayeongoza duniani kwa kukenua hata kama niwakati ambapo hatakiwi kukenua. Pia hilo ni jambo zuri jk alilo jitahidi kulifanya nitamkumbuka sana.
      Njowepo, dfreym and Betranda like this.

    15. #13
      Pasco's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 22nd September 2008
      Posts : 9,839
      Rep Power : 7368
      Likes Received
      6153
      Likes Given
      22273

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Quote By Jasusi
      Yeah, sense of humour na kujionyesha kuwa karibu na watu lakini sera zake zinawakumbatia zaidi wanyonyaji na mafisadi.
      Afadhali hata angekuwa comedian badala ya kuwa kiongozi wa nchi.
      Mkuu Jasusi, kwani Watanzania huwa wanaandaliwa kuchagua nini?. Kama kuwa karibu na watu, ku smile nao,kufurahi nao kwa kuwachekesha (sense of humour) kunakufanya upendeke na kuchagulika, then why not?. Hii inamaana hiki ndicho Watanzania tulichotaka!.

      Mimi nilitanguliza fani ya habari ndipo baadae nikaenda UDSM, nikiwa mtaani niliona jinsi magazeti ya udaku, yanavyonunuliwa kwa wingi!. Nilijiaminisha kuwa magazeti hayo ya udaku yana nafasi kubwa mitaani nikijifariji kuwa washabiki wakubwa wa magazeti ya udaku ni hawa wenzetu walioishia darasa la saba!. Nilipofika UDSM, sikuamini nilipokuta ni magazeti hayo hayo ya udaku ndio yanayoongoza kwa mauzo pale UDSM!. Nimeishi Mabibo hostel miaka 4, ikifika saa mbili usiku TV zinahamishiwa Channel Ten kuangalia "muziki"!.

      Ninahudhuria sana mikutano mingi ya kampeni, burudani na Ze Comedy ndio wanaochukua muda mrefu zaidi na burudani zikiisha, ukifika muda wa kumwaga sera, makundi makubwa ya watu, hujiondokea!. Hii inamaanisha hicho ndicho Watanzania wanachotaka!.

      Kwa mfano msomi mzuri mwenye Ph.D ya kuondoa umasikini akigombea ubunge wa Temeke na Juma Nature, unadhani nani atachaguliwa?!. Lets appreciate baadhi ya mazuri ya rais wetu na tuache kubeza kila kitu!.
      Last edited by Pasco; 29th June 2012 at 08:03.

    16. #14
      ngwini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th April 2011
      Posts : 443
      Rep Power : 500
      Likes Received
      67
      Likes Given
      0

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Nitamkumbuka kwa kupata CPA na faida za kuwa m2mishi wa Umma nikiwa kijana na kupewa u-chief accountant..maana bila CPA hauwez kuwa chief
      Pasco and Ferds like this.

    17. #15
      Bulesi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th May 2008
      Posts : 3,344
      Rep Power : 1240
      Likes Received
      344
      Likes Given
      73

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Quote By Ndahani
      Jasusi, mtoa mada anashauri tujadili kwanini alichaguliwa kwa "kishindo". Ingawa inawezekana kukawa na kufeli kwa "kishindo vile vile"
      Fundi sana wa kuwahadaa wananchi; he never takes things seriously!!
      Ndahani, Pasco, eddo and 1 others like this.

    18. #16
      Jasusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th May 2006
      Posts : 10,623
      Rep Power : 2892
      Likes Received
      3839
      Likes Given
      12234

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      Quote By Ndahani
      Jasusi, mtoa mada anashauri tujadili kwanini alichaguliwa kwa "kishindo". Ingawa inawezekana kukawa na kufeli kwa "kishindo vile vile"
      Sawasawa. Ngoja na mimi nichangie ninayoyajua kwa nini Kikwete alipata 80% supposedly katika uchaguzi wa 2005.

      Ukiangalia tulikotokea tangu mfumo wa vyama vingi vya siasa (1992) ni CCM peke yake ndiyo iliyokuwa na ujuzi na uwezo wa kucheza mchezo wa uchaguzi wa kura. Mwaka 1995 Mrema alikuwa maarufu sana lakini alichezewa rafu na CCM kwa sababu upinzani haukujua mchezo wa kushinda kura.

      Come 2005 Kikwete aliahidi maisha bora kwa kila Mtanzania lakini nina hakika Watanzania hawakujua Kikwete ni mtu wa aina gani, personality wise and leadershipwise. Kwa sababu kama Kikwete angekuwa mtu anayejiamini hakuwa na sababu ya kununua waandishi wa habari kumpamba kwamba ni mwanasiasa mkomavu wakati ukomavu wake hata haujathibitika. Kikwete hakudebate na mgombea yeyote kwa hiyo uwezo wake wa kujenga hoja na kujieleza haukuwa challenged. Ni kama vile alipata free pass.

      By 2005 Watanzania wengi waliamini kuwa CCM peke yake ndiyo inayoweza kutoa kiongozi makini kwa sababu baada ya kufifia kwa Mrema upinzani haukuwa na mtu yeyote ambaye angeweza ku challenge CCM. Hiyo ndiyo sababu Kikwete alishinda kwa kishindo.

      Sasa miaka mitano baadaye Watanzania walishagundua ubabaishaji wa Kikwete, kwamba si mtu mwenye uwezo wa kushughulikia matatizo ya nchi, ni mbabaishaji, na anapenda kuzungumza tu bila kuchukua hatua. Na kadri ninavyoona, ni huo huo ubabaishaji wa Kikwete ambao umesababisha/utasababisha kupungua kwa umaarufu wa CCM come next election.
      Sikonge, Ndahani, Pasco and 1 others like this.

    19. #17
      MtamaMchungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th April 2011
      Posts : 1,539
      Rep Power : 806
      Likes Received
      710
      Likes Given
      64

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      That's very true, everytime he speaks, he always find ways to make people laugh.
      Pasco likes this.

    20. #18
      The Boss's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th August 2009
      Location : DARESALAAM
      Posts : 18,164
      Rep Power : 21615
      Likes Received
      13492
      Likes Given
      17791

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      JK angekuwa the best ever president kama tu
      'angebahatika' kuwa na the best and the brightest around him
      na angekubali kuwa 'hajui'
      na anahitaji kusaidiwa......kwa sababu ana sifa nyiingi mno za kiongozi wa kuwa kiongozi bora...

      1.kwanza anapenda sifa ya kuonekana anaweza
      2.pili ni msikivu na mvumilivu na hana papara
      3.ana personality ya a 'movie star'
      watu wanampenda tu hata kama wanajua hawezi
      4.anapenda watu.....haoni tabu kuchanganyika na watu
      5.anapenda anasa,hii angeweza kuitumia kwa faida.mfano anapenda kuvaa suti za gharama
      basi angehakikisha tuna viwanda vya nguo za quality anayotaka

      but too bad mshauri wake mkuu ni Yussuph Makamba
      Watch your thoughts,They become words, Watch your words, They become deeds, Watch your deeds, They become habits, Watch your habits, They become character, Watch your character, It becomes your destiny!

    21. #19
      TOWNSEND's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th May 2011
      Location : kwa ngulelo
      Posts : 1,113
      Rep Power : 629
      Likes Received
      196
      Likes Given
      31

      Default re: Miongoni Mwa Mazuri ya Kikwete: "Has Good Sense of Humour"

      mie tabasamu lake kila na popote pale akikunja uso kuonesha hasira n secunde tu utaona tabasamu... sijawahi ona akitoa hutuba ikanifurahisha kwani zote sio za kweli
      Pasco, eddo, theROOM and 1 others like this.

    22. #20
      Kimbunga's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 4th October 2007
      Location : Kisiwani Juma
      Posts : 7,484
      Rep Power : 6169
      Likes Received
      3058
      Likes Given
      1019

      Default

      Quote By Maundumula
      Can mods make this thread sticky even for one day? Obviously no!!
      Mkuu wamekusikiliza!
      Pasco likes this.

    Page 1 of 23 12311 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...