| Find/Invite Friends | Register | Calendar | Search | Today's Posts | Mark Forums Read |
| FAQ | Members List | Bongo Flava | Zilipendwa | Taarab | Injili |
|
|
#1 | |||||||||||||||||||||||
|
||||||||||||||||||||||||
|
Views: 6606
|
||||||||||||||||||||||||
|
#2
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Sina wasi wasi na JF.Ongera ya maneno haitoshi.Binafsi ndo nimekuja huku kupiga boksi,nikisimama mchango wangu utafika.Hii ni sehemu ambayo unaweza dhani uko pale sinza Corner bar unaongea na washikaji.You really feel to be home though you're away.
Thank you JF. |
|
#3
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Na unaanzia kuanzia dola kumi kwa mwaka, na kuendelea. Ukitoa hata ...... kwa mwaka ni nyongeza kubwa sana katika kuweka Tbites kadhaa ndani ya Hard disc ya JF, maana kila tunavyoandika, viaenda kutunzwa sehemu na hiyo inabidi isiwe moja maaja ikianguka moja basi ipo ya akiba. Hii shule imenifungua mengi na kunikutanisha na wengi. Humu tumeshakuwa jamii moja kubwa sana. Ila wanasema "hakuna mtu atakupa ugali wa bure". Tujipigepige hivyohivyo na tuwasaidie wenzetu. Ikifika sehemu waweze kusimama wenyewe kwa matagazo ya biashara, hapo tunaweza kusema sasa endelea mwenyewe. Penye nia pana njia, zitapatikana tu.
__________________
.... hata kama akitambika uchi huyu mwakyembe, ukweli utabaki pale pale kuwa yeye nimiongoni mwa wale wabunge waliokula milioni 5 za rostam wakati wa kampeni (By: Game Theory) |
|
#4
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Mkuu wangu Sikonge,
Ukweli ni kuwa siku za nyuma tulijaribu sana kuwafahamisha members kuwa JF haiendeshwi kwa fedha za watu flani bali kwa kujitolea. Tukatanabaisha wazi kuwa wanachama na wote wenye mapenzi mema inabidi watambue kuwa tuna mzigo mkubwa wa kubeba kwa niaba yao. Nyakati hizo tulikuwa na wanachama waliojisajili karibia 2,000 hivi na tukasema endapo kila mwanachama (aliyejisajili) angechangia Tshs 10,000/= basi ilimaanisha kuwa tungepata Tshs 20,000,000/= ambayo kwa wakati huo ingetosheleza kuiendesha JF kwa karibia mwaka mzima bila wasiwasi. Maisha yakabadilika, Server tuliyokuwa nayo ilikuwa ndogo sana kumbe kulinganisha na uhitaji wa watanzania, balaa lilionekana wazi Mwezi Februari 2008 pale Mhe. Lowassa alipokuwa akijieleza Bungeni... Server ikachemsha kubeba mzigo mkubwa. Kwa wakati huo tukaona ni vema tukaangalia namna ya kuweza kuwashirikisha wanachama juu ya ugumu tunaokumbana nao... Tukalazimika kununua server kubwa zaidi mbili na zenye back up za kila baada ya masaa 6 kwa nyakati tofauti. Hilo likasaidia japo kwa gharama ambazo zilitoka mfukoni mwa mwanachama mmoja! Ndiyo, kulipia server hizo kila mwezi ni $940 na ameendelea kufanya hivyo kwa imani kuwa kuna siku mambo yataenda sawa. JF inahitaji SANA michango ya watanzania na wote wenye mapenzi mema. Kuna wanachama ambao humu mnawaona wana usernames ambazo ni bolded, hawa ni Premium Members. Hawa walau wamechangia kwa kiwango cha kuanzia $5 na wawili walau $300 tangu JF inaanzishwa mwaka 2006 (ikijulikana kama JamboForums). Tangu JF inaanza (2006) mpaka sasa Januari 9 2009, tumekwishapokea jumla ya US$ 1,450/= toka kwa wanachama waliojisajili na wasiojisajili. Wengi wa waliohitaji kuchangia walikuwa wanatuma barua pepe nasi tunawapa maelekezo juu ya namna ya kutufikishia michango hiyo. Ukweli ni kwamba kwa wasio wanachama wa JF wakiwa wanasoma hapa wanaona matangazo mengi ya Google kuliko wanachama waliojisajili. Dhamira yetu si kuweka matangazo haya ya Google kwani hayaingizi kwa kiwango kikubwa hivyo, watu hawabonyezi matangazo hayo na hivyo income yake inategemea pale mtu atakapokosea akabonyeza tangazo ndipo tupate vijisenti kidogo kwa clicks hizo. Gharama za uendeshaji bado zinatoka mfukoni mwa mtu mmoja mpaka sasa na baadhi ya Premium Members ambao wameendelea kuona umuhimu wa kufanya hivyo. Mpaka sasa JF ina wanachama waliojisajili karibia 8,000. Endapo waliojili hawa wangechangia walau Tshs 10,000/= kwa mwaka basi inamaanisha JF ingetengeneza Tshs 80,000,000/= kwa mwaka na hivyo tusingeweka matangazo KABISA na tungejitahidi kupata moderators ambao watakuwa wanalipwa kwa kazi yao na wangeifanya kwa umakini mkubwa zaidi. Ukiangalia katika historia ya Forums nyingi, huwa zinashindwa kuhimili traffic inapokuwa kubwa kutokana na servers kuhitaji umakini zaidi na Forum owners hujikuta wanaona ni mzigo usio na faida hivyo forums hizo kufa. Tumshukuru Maxence kwa kuendelea kulipia gharama hizi kila mwezi kwa kujitolea mpaka sasa huku akilipia na Chat Server (IRC Server). Wapo wanachama kama Ogah, Nyambala, SteveD, FairPlayer, Mchukia Fisadi na Phillemon Mikael ambao huchangia walau kila wanapopata wasaa... Hawa nao wamesaidia kwa kiwango kikubwa katika jitihada za kuhakikisha JF inakuwa hewani. Bila kuwasahau wadau waliochangia walau $200 hivi initially kama Mtanzania, Field Marshal ES na Halisi. Ninachoamini binafsi ni kitu kimoja, Tshs 5,000/= kwa mwaka inawezekana kabisa kwa watanzania tulio na uwezo wa kuingia mtandaoni. Na uzuri, benki zetu Tanzania zinaruhusu mtu ku-deposit Tshs 5,000/= kama kiwango cha chini. Endapo kuna mwanachama anaguswa (kutoka moyoni) na angependa kuiwezesha JF kuendelea kusimama imara na kufanya vema zaidi bila mizengwe ya kifedha, basi anaweza kukubali kuchangia Tshs 5,000/= walau kwa mwaka. Benki zetu (hapa naongelea NBC na CRDB kwa haraka) hazikulazimishi unayetuma hela kuandika jina lako la kweli bali lile ambalo ungependa mpokeaji alitambue. Kwa walio Tanzania wanaweza kuichangia JF kwa kutuma katika akaunti za NBC au CRDB. Akaunti ambazo tangu awali tulipendekeza zitumiwe ni za Maxence Melo (as the JF Founder) na tukawaomba wanaotuma waandike Nicks za kuweza kutanabaisha kuwa wao ndio walotuma. ================================= Michango inaweza kutumwa kwa njia kuu nne: 1. Kwa walio nje wanaweza kutumia PayPal au Credit Cards au Debit Cards kwa kufuata link hii ( http://www.jamiiforums.com/payments.php) iliyo kwenye sahihi yangu (linapoonyesha dole gumba) na pindi mchangiaji anapoweka chochote tunakuwa notified nasi tunafanya kuwasiliana na mhusika ili aweze kupandishwa kwenda katika group la Premium Members. Paypal users: Send via email - macdemelo@gmail.com moja kwa moja itafika na utaarifiwa ndani ya dakika 60 kuwa mchango wako umepokelewa. 2. Njia ya pili ni kutumia Western Union au Money Gram na kutuma kwenda kwa Maxence Melo Mubyazi wa Dar es Salaam. 3. Njia ya tatu ni kutumia Bank accounts za Maxence kama ifuatavyo: NBC: Acc #: 033201064359 Jina: Maxence Melo Mubyazi CRDB: Account Name: Maxence Melo Mubyazi Bank: CRDB Pugu Road Branch Swift Code: CORUTZTZ Acc No: 01J2092391800 4. Njia ya nne: Unaweza kutuma recharge vouchers za tiGO, Zain, VodaCom au Zantel kwenda kwa Maxence - 0713444649 naye atakufahamisha kuwa kazipokea. ================================= Ikumbukwe, SI LAZIMA kuandika jina lako la kweli na SI LAZIMA kwenda mwenyewe bank kutuma pesa hizo (kwani unaweza kumpa unayemwamini na kumpa account details na jina lako ambalo ungependa aandike). Tunaweza kuandika mengi lakini ukweli unabakia pale kuwa JF inahitaji michango yenu kwa sana tu. Kwa wenye maswali zaidi wanaweza kuwasiliana na Maxence kupitia namba yake ya simu +255713444649. Nasikitika kuwa yawezekana hata hivi natembeza bakuli ![]()
__________________
Ficha Upumbavu wako; Usiifiche Hekima yako! ![]() Thank you for supporting JF! <---(click to support us) Waliochangia 2010: <--- (click to read) JINSI YA KUCHANGIA JF<---(click to read) ![]() 24/7 Email SUPPORT: support@jamiiforums.com ![]() |
| The Following 9 Users Say Thank You to Invisible For This Useful Post: | ||
Ab-Titchaz (17th January 2010), Baba_Enock (15th January 2010), ejogo (19th December 2009), Lekanjobe Kubinika (4th March 2010), madule (4th February 2010), Mchukia Fisadi (17th January 2010), mkurugenzi1 (16th February 2010), Mnyonywaji (16th February 2010), ThinkPad (11th February 2010) | ||
|
#5
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Wadau na wapenzi wote wa JF.....! Heshima mbele!
Wakuu mbona haka kathread tunakasahau sana? Tunalipenda jamvi sana kwa sababu mbalimbali (sitaki kuzieleza, hope kila mmoja anazifahamu), lakini founders wa hii kitu wanaumia sana kuhakikisha jamvi linakuwa hai katika hali tunayoifurahia. Wanaumia,techinically and financially wakuu! Sisi wadau wengine tunaweza tukashindwa kusaidia technically directly but we can do that financially...na kwa maoni yangu silazima uchangie mamilioni wakati huna uwezo wakufanya hivyo, kila mmoja wetu (members) ambao ni registered akitoa Tshs 1,000..kwa mwaka, tunaweza kufanya makubwa kwa kuwasaidia kina Robot na founders wengine kutuboreshea zaidi jukwaa hili kwa manufaa yetu sote! I hope hakuna mtu angependa kusikia ati anaamka asubuhi kujaribu kupata breaking news hapa JF au kasikia tetesi sehemu fulani anataka kuja apate uthibitisho hapa ....unaambiwa the web you are browsing is not found....yaani JF haiko hewani.....! No one will like this to happen! But nina uhakika kama hatuisupport JF one day hii kitu itafungwa kabisa! Kwa hiyo wandugu kwa wote wenye mapenzi mema na JF pamoja na nchi hii, let us join our hands...tuchangie JF kwa moyo wote! Admin please wakumbusheni members hali halisi ya gharama za kuiendesha JF na umuhimu wa michango yao! Ningeshauri pia, mngewajulisha members direct costs za kuimanage JF kwa mwaka...then labda tufungue thread special kwaajili ya members kuweka Pledges zao za hali na mali zitakazowezesha atleast kucover direct running costs za JF kwa mwaka! Kwa kuanzia kule VIP mimi nimeahidi kuirusha kwa Max Tshs 30,000 wiki ijayo.....so wadau mnaweza endeleza hapo! Cheers!
__________________
“Without leaps of imagination, or dreaming, we lose the excitement of possibilities. Dreaming, after all, is a form of planning - GLORIA STEINEM. |
|
#6
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Nashangaa sasa limekuwa jukwa la kutukana matusi na kuwakashifu waislamu mtindo mmoja na hatuwa hazichukuliwi kwa wahusika au ndo wenye jukwaa hao?
|
|
#7
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
Usiharibu thread tfadhali.....hapa sisi tunataka michango kunusuru JF...malalamiko yako si hapa...andikia mods! Hapa tupishe...
__________________
To be able to do everything by knowing nothing is dangerous
E-mail: masanilo@jamiiforums.com |
|
#8
|
|||||||||||||||
|
|||||||||||||||
Pili, ungeweza kutoa dukuduku zako kule kwenye compaints na ungesaidiwa vizuri sana mkuu! Hii thread ni kwa ajili ya fund raising na kutoa maoni ya jinsi ya kuiwezesha JF ijiendeshe mkuu!
__________________
“Without leaps of imagination, or dreaming, we lose the excitement of possibilities. Dreaming, after all, is a form of planning - GLORIA STEINEM. |
|||||||||||||||
|
#9
|
|||||||||||
|
|||||||||||
|
Kuna wakati kama vile speed ya wanajamii kuchangia ilikuwa inaridhisha. Lakini ghafla kumekuwa na kuzorota tena kwa muda mrefu sasa.
Ninafahamu kwamba mchangiaji/mwendashaji mkuu (90%) wa JF ni mmoja tu. Sisi wanachama zaidi ya 5000, mpaka leo waliochangia hawazidi hata 50! Chini ya asilimia moja! Inasikitisha. Kama sisi ndio wasomi, tena wenye uelewa wa hali ya juu, na kipato fulani, tunashindwa kusaidiana mzigo huu wa kifedha, mmmmhhhh!
__________________
Watanzania vilaza watamchagua Kikwete aendeleze ubabaishaji ikulu kwa awamu nyingine - Tafakari |
|
#10
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Wana JF salaam wote,
Yaani hii forum mimi inanikuna sana. Naomba nishauriwe kwa kuchangia kwa njia ya euro moja kwa moja, nifanyeje bila ya peleka kwa a/c za CRDB au NBC ambazo zitahitajika gharama zingine za kutuma michango Tanzania. Kama kuna namna ya kuwakilisha mchango kama euro hapa Netherlands moja kwa moja kwa a/c ya JF nifahamishwe. Asanteni Amandla!
«
Previous Thread
|
Next Thread
»
Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako! All times are GMT +3. The time now is 09:45 PM.
Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com | |||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||