Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Slaa: Kikwete akipuuza nchi haitatawalika

    Report Post
    Page 1 of 13 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 250
    1. #1
      EasyFit's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th July 2011
      Posts : 830
      Rep Power : 565
      Likes Received
      572
      Likes Given
      196

      Default Slaa: Kikwete akipuuza nchi haitatawalika

      Quote By Mchaga 25
      Amini usiamini wale walioko ndani na system wamelitambua, mkuu wa kaya akiri kabisa mambo hayaendi, kufuatia mfumuko wa bei, kuporomoka shilling kwa mara ya pili, kupanda kwa bei ya mafuta tunapo kutarajia hivi karibuni, migomo inayojiri na ambayo usalama wa taifa wa wamesha tahadharisha kuwa iko likely kutokea mwanzoni mwa mwezi wa pili.

      Busara za wadau wengine zinaanza kutafutwa, hakika tuko pabaya.

      KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willibrod Slaa, amemtaka Rais Jakaya Kikwete kuwa makini na kuchukua hatua za haraka kurejesha amani kabla Watanzania hawajaishiwa uvumilivu na utawala wa serikali yake.

      Dk. Slaa amesema kuongezeka kwa matukio ya matumizi ya nguvu ya dola katika kulinda uhalali wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kiasi cha kufikia hatua ya kuua watu wasiokuwa na hatia, yanadhihirisha kuwa muda si mrefu ujao nchi itakuwa haitawaliki tena ikiwa Kikwete ataendelea kufumbia macho mauaji hayo.

      Akifungua Ofisi ya Baraza la Vijana wa chama hicho (Bavicha) Mtaa wa Togo, Dar es Salaam jana, Dk. Slaa alisema kuwa mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola chini ya serikali ya CCM kupitia kwa viongozi wake hususan Jeshi la Polisi, hayawezi kuvumilika tena na yanawasukuma wananchi kufikia mwisho wa uvumilivu.

      Alisema sasa kuna dalili zote za wazi zinazotishia amani na mustakabali wa nchi na watu wake, zikiifanya nchi isitawalike, na wala serikali haiwezi tena kukwepa lawama za kuhusika na mauaji ya wananchi, na kutolea mfano wa tukio la kutwangwa risasi kwa watu wanne wasiokuwa na hatia waliokuwa wakiandamana kudai haki ya kulindwa na serikali yao mkoani Ruvuma mapema wiki hii.

      Dk. Slaa akizungumza kwa uchungu alisema mauaji ya Songea yalitokana na uzembe wa hali ya juu wa viongozi wa serikali na vyombo vya dola ngazi ya wilaya na Mkoa wa Ruvuma.

      “Napenda kutoa kauli juu ya mauaji dhidi ya raia yaliyofanywa na Jeshi la Polisi huko Songea. Kwa taarifa nilizonazo, mauaji yale yametokea kwa sababu ya uzembe wa hali ya juu na ufinyu tu wa akili ya viongozi, akiwamo mkuu wa Mkoa na polisi wale. Hivi unawaambiaje raia wenye uchungu na vifo vya wananchi wenzao, waliojikusanya na kuamua kuandamana kudai haki, eti wachague kiongozi wa kuonana na mkuu wa mkoa,” alisema.

      Aliitaka serikali kuunda tume huru ya kuchunguza mauaji hayo ya Songea na kudai kuwa hakuna uhalali wowote wa viongozi wa serikali wa mkoa ambao ni watuhumiwa wa mauaji hayo kuunda chombo cha kuchunguza.

      “Tunawapongeza wananchi na hasa vijana wa Songea kwa kuandamana kudai haki. Tunataka ufanyike uchunguzi huru juu ya mauaji hayo, yatakayoihusisha mahakama (Korona) na mkuu wa mkoa na polisi hawana uhalali wa kuunda tume za kuchunguza kwani wao pia ni watuhumiwa katika tukio hilo,” alisema.

      Katibu mkuu huyo wa CHADEMA alilaani tukio la juzi usiku, ambapo polisi katika mji wa Tunduma wanadaiwa kushusha bendera za chama hicho katika maeneo mbalimbali ya mji huo.

      Alisema kitendo hicho ni uchokozi tosha kwa CHADEMA na kimelenga kuleta fujo nyingine zinazoweza kuleta uvunjifu wa amani.

      “Niliwasiliana na Mkuu wa Wilaya ya Mbozi, pia mkuu wa mkoa, niliwaambia mimi sipendi kugombana nao kwa masuala ya hovyo kama hayo, tupo kwa mujibu wa sheria, bendera zetu zinatokana na kodi za Watanzania, wakasema eti zingine ziko sokoni, nikawauliza za CCM huwa zinawekwa wapi?

      “Watu hawana maji, hawana zahanati, elimu inashuka, mkuu wa wilaya hajawahi kuamuka usiku, lakini kwenye kushusha bendera za CHADEMA wanaamka usiku wa manane,” alisema.

      Alitumia wasaa huo kuwataka vijana wa CHADEMA wasimamie haki na kupinga dhuluma na uonevu popote pale wanapofanyiwa Watanzania na wahakikishe wanajua kinachoendelea katika maeneo ya Songea na Tunduma ili chama hicho kijue hatua za kuchukua.

      Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bavicha, John Heche, mbali ya kumshukuru Dk. Slaa na makao makuu ya chama hicho kwa kuwawezesha kuwa na ofisi yao, alisema kuwa watakuwa mstari wa mbele kusimamia malengo ya chama hicho hasa katika kutetea haki za Watanzania, kudai uwajibikaji wa viongozi na serikali kwa wananchi, pia kulinda rasilimali za taifa.

      Alisema kuwa vijana watakuwa mstari wa mbele katika vuguvugu la mageuzi yanayoendelea nchini, akisema kuwa ofisi hiyo itakuwa sehemu sahihi ya kuendeshea mipango ya ukombozi wa taifa ambalo pamoja na utajiri wa rasilimali za kila aina, bado wananchi wake wanaishi katika umaskini wa kupindukia.
      DEUS NSHANGE and kygrykos like this.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Taja's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th December 2011
      Location : Zanzui - Maswa
      Posts : 95
      Rep Power : 396
      Likes Received
      33
      Likes Given
      46

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      hivi ni kiongozi gani aliitoa kauli hii.
      tedo likes this.

    4. #3
      Papa D's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 615
      Rep Power : 557
      Likes Received
      88
      Likes Given
      75

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      hivi hii nchi ina usalama wa taifa kweli?!!!
      wizi mkubwa na wa kimafia umekithri wala hatuwaoni?
      Nafikiri ungesema usalama wa ccm ndo wametoa hiyo tahadhari!!!
      Majimoto, fredmlay and IWILL like this.

    5. #4
      Power G's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 20th April 2011
      Location : Msoga Kijijini
      Posts : 2,407
      Rep Power : 991
      Likes Received
      773
      Likes Given
      259

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Inapofikia hata watu kama mchaga25 wanaanza kuuona ukweli, ni dalili nzuri. Naona baada ya muda watabaki wachache sana wale wanaoona ukweli lakini wanajifanya hawaoni kama FF, Rejao na Ritz.
      Mafie PM likes this.

    6. #5
      Saint Ivuga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Posts : 20,664
      Rep Power : 10164
      Likes Received
      5650
      Likes Given
      12666

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      benki ya dunia nayo si wameshazipa developing countries alert kuwa lazima wapigike sasa hivvi.
      JF the best place to be. and the POWER of God be with us all the time.

    7. Miaka 50

    8. #6
      nitonye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th December 2011
      Posts : 4,261
      Rep Power : 1289
      Likes Received
      1472
      Likes Given
      27

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      dalili za kushindwa kutawalika maana yake nguvu ya umma itabide ishike madaraka
      Mungi and ELIAHKAMWELA like this.

    9. #7
      Mnyamahodzo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd May 2008
      Posts : 1,417
      Rep Power : 966
      Likes Received
      314
      Likes Given
      217

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Hadi Jumatano ya wiki iliyopita, mfumuko wa bei ulikuwa 19.9%.
      Nawezaje kuipenda Tanzania?

    10. #8
      Entrepreneur's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2011
      Posts : 911
      Rep Power : 586
      Likes Received
      478
      Likes Given
      153

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Wakati kama huu huwa napenda kupitia ile hotuba ya mwalimu ya September mosi. 1979 inayoitwa "mapambano yanaendelea". Kwa kweli hali ni ngumu kuliko inavyoelezeka na sidhani kama ni busara kuwasubiri hawa wanasiasa waje watutoe hapa walipotufikisha.

      Awali dalili zote za kufika hapa zilikuwa ni dhahiri na wadau wengi walito tahadhari lakini hawakusikilizwa, na sasa ni dhahiri tena tunaelekea kubaya zaidi kwani bado sijaamini kama kweli SERIKALI imeshatoa pamba masikioni mwake. Hivi kama hii issue ya umeme, ni kweli hawajui madhara ya kuongeza Bei? Na bado

      Wananchi tuchukue hatua sasa
      Ame likes this.
      “The first method for estimating the intelligence of a ruler is to look at the men he has around him.” ― Niccolò Machiavelli, The Prince

    11. #9
      Kubingwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd April 2010
      Location : Hapahapa
      Posts : 501
      Rep Power : 561
      Likes Received
      61
      Likes Given
      202

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Ikulu ni mahali patakatifu! Sijui sasa papoje,yangu macho na uzima.
      Mambo yanapoenda mrama kila ufanyalo haliendi.Maofisi hata hao wataalam hawafanyi tena kazi,kazi kutegea ama kufanya kazi zao na wengine hata kama hawana nia ya kwenda shule ndo muda wao wa kwenda kuchukua masomo yao zaidi.

      Mungu tunusuru na haya mambo kama andiko linavyosema Kumb.28:33

    12. #10
      Entrepreneur's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th June 2011
      Posts : 911
      Rep Power : 586
      Likes Received
      478
      Likes Given
      153

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Quote By Mchaga 25
      Amini usiamini wale walioko ndani na system wamelitambua, mkuu wa kaya akiri kabisa mambo hayaendi, kufuatia mfumuko wa bei, kuporomoka shilling kwa mara ya pili, kupanda kwa bei ya mafuta tunapo kutarajia hivi karibuni, migomo inayojiri na ambayo usalama wa taifa wa wamesha tahadharisha kuwa iko likely kutokea mwanzoni mwa mwezi wa pili.

      Busara za wadau wengine zinaanza kutafutwa, hakika tuko pabaya.
      Swali la kizushi tu Mchaga!
      Hivi tunastahili kutawaliwa au kuongozwa? Haa haa haa
      Maundumula and Sometimes like this.
      “The first method for estimating the intelligence of a ruler is to look at the men he has around him.” ― Niccolò Machiavelli, The Prince

    13. #11
      1800's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th December 2010
      Posts : 1,656
      Rep Power : 891
      Likes Received
      414
      Likes Given
      21

      Default

      Quote By Jsaudi
      Inapofikia hata watu kama mchaga25 wanaanza kuuona ukweli, ni dalili nzuri. Naona baada ya muda watabaki wachache sana wale wanaoona ukweli lakini wanajifanya hawaoni kama FF, Rejao na Ritz.
      Mkuu umemsahau na ndugu yetu hojatete

    14. #12
      jmushi1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2007
      Posts : 14,376
      Rep Power : 16492
      Likes Received
      4299
      Likes Given
      5491

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Unajuwa walioko responsible kwa ujumla na hali ya uchumi ya dunia ni mabepari, lakini mabepari wa kwetu, wengi wao ndo hao mafisadi, kwasababu wengi wao chanzo cha utajiri ni pesa za umma na rasilimali za Taifa.

      Ndo maana unaona Obama anataka kuwapandishia kodi mabepari wa marekani ili kusaidia kuinua uchumi, kwasababu they were responsible since wakakati uchumi ukididimia na hali ya wananchi walio wengi kutokuwa njema, wao bado walikuwa ndo wanadouble mishahara, mabonus na maprofit kwa ujumla.

      Since mabepari wetu sisi ndo hao mafisadi, basi mali zao halali ya wananchi, na kama ni kweli hawataki kurudisha pesa na mali walizokwapua, basi hali kwa Tanzania itakuwa mbaya zaidi kwasababu hakuna wa kuwahold responsible.

      Kwenye mjadala wa kuhusu mustakabali wa Taifa, hili la mafisadi kurejesha walivyokwapua haliwezi kuwa out of the question, pia katiba tutakayoipata ni lazima i reflect azma yetu ya kuufutilia ufisadi na mafisadi mbali.
      Wambandwa, fredmlay, Ame and 1 others like this.
      "One of the penalties for refusing to participate in politics is that you end up being governed by your inferiors"-Plato

    15. #13
      Mgaya D.W's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2012
      Posts : 690
      Rep Power : 508
      Likes Received
      235
      Likes Given
      574

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Tunapokosa uzalendo mara nyng viongoz hufikiria mambo yote mabaya huanzishwa na upinzani,napata taabu kuona maisha yasivyotuhurumia.nchi yangu naipenda lakin viongoz hawana huruma,hawana uzalendo hata kidogo ni kama kikundi cha wagen wamekuja kukwiba na kuondoka.mfumuko wa bei unapofika asilimia 19.9 tunaenda wap?kwanin viongoz hawatak kuchukua hatua?dah,lakini tutawapa zawad mwaka 2015 ili wajue upole wetu ktk sanduku la kura.
      Sometimes, tedo and Mchomamoto like this.

    16. #14
      Bangoo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2011
      Posts : 2,269
      Rep Power : 834
      Likes Received
      370
      Likes Given
      0

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Natamani mfumuko uendelee nione serikali ikianguka pwaaaa. Ee Mungu saidia wanao.
      tedo and Bob Lee Swagger like this.

    17. #15
      tedo's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 17th August 2011
      Location : uchochoroni
      Posts : 5,479
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1259
      Likes Given
      880

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Quote By Taja
      hivi ni kiongozi gani aliitoa kauli hii.
      Slaa ofcourse kwani hujui yule ni nanbii.

    18. #16
      kichomiz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2011
      Posts : 4,053
      Rep Power : 1232
      Likes Received
      652
      Likes Given
      80

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      Ndio maana mkulu ameanza kujipendekeza CDM,hana ujanja kwa sasa.
      Bob Lee Swagger and Taja like this.

    19. #17
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,858
      Rep Power : 1843
      Likes Received
      590
      Likes Given
      413

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      akili ni mali endapo wewe ungekabidhiwa nchi na chadema yako mambo yangekwenda vibaya zaidi
      Maundumula likes this.

    20. #18
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,858
      Rep Power : 1843
      Likes Received
      590
      Likes Given
      413

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      njozi kwamba chadema ikishika dola nchi hii itakuwa peponi ni fikra mgando. maendeleo ni zaidi ya chama cha siasa na itikadi zake

    21. #19
      Duble Chris's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th May 2011
      Posts : 2,339
      Rep Power : 871
      Likes Received
      382
      Likes Given
      304

      Default re: Nchi haitawaliki, Chadema was right

      "haya matatizo yanayotokea hapa petu yanatokea pia nchi za ullaya kama Italy" .....anasahau kuwa wenzake wanajiuzuru wanapo ona nchi haiendi ina kuwa na madeni makubwa , mfumuko wa bei juu
      frustration is given by expectationdivide by
      outcome
      ie
      frustration = expectation/outcome


    22. #20
      Gwallo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Posts : 664
      Rep Power : 568
      Likes Received
      80
      Likes Given
      86

      Default

      Quote By Hojatete
      wajinga wengine bana.huyu alieiba mke wa mtu akatelekeza watoto ndo unamuona mungu wako.shule kitu cha mhm sana
      Shule gani unayo wewe, unamsaidiaje aliyeibiwa wife wake na Dr Slaa?

    Page 1 of 13 12311 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...