Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda jinsi Kagame anavyotawala?

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 59
    1. Iga
      #1
      Iga's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 17th December 2007
      Posts : 113
      Rep Power : 606
      Likes Received
      5
      Likes Given
      0

      Default Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda jinsi Kagame anavyotawala?

      WAKATI Bw. Kagame huko Rwanda kafunga soko la serikali kuhodhi magari yanayokula mabilioni ya fedha za umma bila kuwa na manufaa ya moja kwa moja kwa raia wa kawaida ila tu kwa wale wanaoyatumia na jamaa zao, hapa Tanzania magari ya kifahari zaidi ya 700 ndio kwanza yanapakuliwa bandarini.

      Je, huu si unafiki kulalama mzigo anaobebeshwa mwananchi wa kawaida anayeteseka kwenye usafiri wa umma usio na heshima wala taadhima usiku na mchana, akienda na kutoka kazini au hospitali au shule au kwenye shughuli zake nyingine na kisha kuwa wasanii kwa kuthubutu bila aibu kuwaambia watu kuwa huu ni mzigo wa mwisho wavumilie tu.

      Magari hayo mia saba kwa bei za haraka haraka ni kwambwa yameigharimu serikali shilingi bilioni 70. (Tshs. 70,000.000,000/=). Magari haya yakiuzwa kwa watu na mashirika binafsi kwa hiyo yanaweza kuipatia serikali fedha za kuwalipa wastaafu wa EAC na kuondokana na maapizo na laana zao kwa Watanzania wote na vile kumaliza kabisa matatizo madogo madogo ya walimu.

      Nilulize swali moja, je, serikali ya awamu ya nne inaona ugumu gani kuwauzia au kuwakopesha magari hayo watumishi wa serikali ili angalau tupunguziwe mzigo wa pettroli na spea pati? Au hii ndio tabia na hulka yake halisi ya kusema maneno tofauti na kile inachokiamini kama vile kutudanganya sisi ni wajamaa na kumbe nchi ni ya kibepari?

      Ingawa gharama ya kununua magari hayo ni kama bilioni 70 lakini gharama za kuyajaza mafuta na kuyahudumia kiufundi ni bilioni 200 kwa mwaka. Hivi tunataka kuwakomboa Watanzania au tunawafanyia usanii kwa namna hii?

      Hivi kweli tutashangaa Rwanda inaelekea kwenye GDP per capita ya dola 3,000 sisi tunaogelea ogelea kwenye dola 600 kwa miongo kadhaa sasa?


      Na wakubwa hawajui jinsi tunavyoila Krismasi ya mwaka huu, mwaka mpya wa Kiislamu na mwaka mpya wa Kikirsto kwa taabu na dhiki kubwa ajabu?

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Mfumwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th August 2008
      Posts : 1,470
      Rep Power : 842
      Likes Received
      14
      Likes Given
      1

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Labda Serikali inataka kuiokoa Toyota katika mtikisiko huu wa hali ya kifedha duniani. Manake haiingii akilini ununue mashangingi 700 wakati unafunga shule hakuna chakula, hospitali watu wanalala chini nk.

    4. #3
      Calnde's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th October 2008
      Location : Still looking where to settle
      Posts : 1,367
      Rep Power : 815
      Likes Received
      251
      Likes Given
      148

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Na hapo ndo ujuha unaanzia! Mambo ya msingi yanawekwa pembeni wanarukaruka na maslahi yao binafsi. nadhani hawana team work hata kidogo. Kila mmoja hukurupuka na lake asubuhi. Pinda anasema magari tupunguze bandarini yanaletwa 700. Ni katika ufujaji kama huu wanatuambia tuwe wazalendo na kuipenda nchi yetu!
      In the end will remember,not the words of our enemies but the silence of our friends.

    5. #4
      Tikerra's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd September 2008
      Location : Morogoro
      Posts : 1,588
      Rep Power : 864
      Likes Received
      100
      Likes Given
      3

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Hongera sana ndugu yangu kwa taarifa hii,umeiandika kwa hisia, nadhani inatoka rohoni.Tuko pamoja.
      Quote By Iga
      WAKATI Bw. Kagame huko Rwanda kafunga soko la serikali kuhodhi magari yanayokula mabilioni ya fedha za umma bila kuwa na manufaa ya moja kwa moja kwa raia wa kawaida ila tu kwa wale wanaoyatumia na jamaa zao, hapa Tanzania magari ya kifahari zaidi ya 700 ndio kwanza yanapakuliwa bandarini.

      Je, huu si unafiki kulalama mzigo anaobebeshwa mwananchi wa kawaida anayeteseka kwenye usafiri wa umma usio na heshima wala taadhima usiku na mchana, akienda na kutoka kazini au hospitali au shule au kwenye shughuli zake nyingine na kisha kuwa wasanii kwa kuthubutu bila aibu kuwaambia watu kuwa huu ni mzigo wa mwisho wavumilie tu.

      Magari hayo mia saba kwa bei za haraka haraka ni kwambwa yameigharimu serikali shilingi bilioni 70. (Tshs. 70,000.000,000/=). Magari haya yakiuzwa kwa watu na mashirika binafsi kwa hiyo yanaweza kuipatia serikali fedha za kuwalipa wastaafu wa EAC na kuondokana na maapizo na laana zao kwa Watanzania wote na vile kumaliza kabisa matatizo madogo madogo ya walimu.

      Nilulize swali moja, je, serikali ya awamu ya nne inaona ugumu gani kuwauzia au kuwakopesha magari hayo watumishi wa serikali ili angalau tupunguziwe mzigo wa pettroli na spea pati? Au hii ndio tabia na hulka yake halisi ya kusema maneno tofauti na kile inachokiamini kama vile kutudanganya sisi ni wajamaa na kumbe nchi ni ya kibepari?

      Ingawa gharama ya kununua magari hayo ni kama bilioni 70 lakini gharama za kuyajaza mafuta na kuyahudumia kiufundi ni bilioni 200 kwa mwaka. Hivi tunataka kuwakomboa Watanzania au tunawafanyia usanii kwa namna hii?

      Hivi kweli tutashangaa Rwanda inaelekea kwenye GDP per capita ya dola 3,000 sisi tunaogelea ogelea kwenye dola 600 kwa miongo kadhaa sasa?


      Na wakubwa hawajui jinsi tunavyoila Krismasi ya mwaka huu, mwaka mpya wa Kiislamu na mwaka mpya wa Kikirsto kwa taabu na dhiki kubwa ajabu?

    6. #5
      Baba_Enock's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2008
      Location : Bunju "B"
      Posts : 5,818
      Rep Power : 1900
      Likes Received
      1162
      Likes Given
      977

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      VX 700? - Kweli Tz ni TAJIRI bali WaTz ni maskini! Shame on our "Viongozi"!

    7. Miaka 50

    8. #6
      PanguPakavu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th July 2007
      Posts : 224
      Rep Power : 655
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      halafu jitu linasimama kwenye jukwaa na kusema linaipenda tanzania na linampango wa kuiendeleza.jiiiiiiiiiiiiiiz.. .,
      these guys are there for the money...,nothing else..,
      till something changes abruptly we are gon be poor forever...,atleast us "walalahoi"
      2 them big shots in the government...,recession my **s!
      "I may not agree with you. However, I will defend your right to express your opinion"

    9. #7
      SaidSabke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th September 2006
      Posts : 592
      Rep Power : 766
      Likes Received
      27
      Likes Given
      6

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Watanzania tuache kulalama bila sababu za msingi.tunadai kuwa watumishi serikalini hawaendi vijijini kuhimiza maendeleo.tunataka viongozi waende vijijini kusimamia maendeleo sasa unataka waende kwa kutumia punda.haya magari munayoita ya gharama gari gani ambalo sio gharama siku hizi landrover seris three hazipo siku hizi mbona watu wanakuwa hawaelewi chochote na kujifanya kujua hebu nieleze gari lililorahisi ni lipi ukilinganisha na ukubwa wa nchi hii ubovu wa barabara za vujijini nk.

    10. #8
      Endaku's's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th May 2007
      Posts : 242
      Rep Power : 661
      Likes Received
      19
      Likes Given
      72

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Quote By Baba_Enock
      VX 700? - Kweli Tz ni TAJIRI bali WaTz ni maskini! Shame on our "Viongozi"!
      These leaders once they got any professional carrier its for marketing themselves for various political posts ,thats why they fully politicians they even forget what is to be done to achieve economic development for TANZANIA they are just talking blabla !!!! Dr ,Prof going to do politics its
      not bad but are they fully utilising themselves for their country benefits or
      just happy to receive handsome payments only and readings nice reports and
      plugging the figure that per capital income is growing what a nonsense go to the real life and see how difficults things are !! Sometimes i just wish to do .............................. . for sure !
      "I am not afraid of storms for I am learning how to sail my ship - Louisa May Alcott"

    11. #9
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,875
      Rep Power : 1978
      Likes Received
      2356
      Likes Given
      3046

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Quote By Iga
      WAKATI Bw. Kagame huko Rwanda kafunga soko la serikali kuhodhi magari yanayokula mabilioni ya fedha za umma bila kuwa na manufaa ya moja kwa moja kwa raia wa kawaida ila tu kwa wale wanaoyatumia na jamaa zao, hapa Tanzania magari ya kifahari zaidi ya 700 ndio kwanza yanapakuliwa bandarini.

      Je, huu si unafiki kulalama mzigo anaobebeshwa mwananchi wa kawaida anayeteseka kwenye usafiri wa umma usio na heshima wala taadhima usiku na mchana, akienda na kutoka kazini au hospitali au shule au kwenye shughuli zake nyingine na kisha kuwa wasanii kwa kuthubutu bila aibu kuwaambia watu kuwa huu ni mzigo wa mwisho wavumilie tu.

      Magari hayo mia saba kwa bei za haraka haraka ni kwambwa yameigharimu serikali shilingi bilioni 70. (Tshs. 70,000.000,000/=). Magari haya yakiuzwa kwa watu na mashirika binafsi kwa hiyo yanaweza kuipatia serikali fedha za kuwalipa wastaafu wa EAC na kuondokana na maapizo na laana zao kwa Watanzania wote na vile kumaliza kabisa matatizo madogo madogo ya walimu.

      Nilulize swali moja, je, serikali ya awamu ya nne inaona ugumu gani kuwauzia au kuwakopesha magari hayo watumishi wa serikali ili angalau tupunguziwe mzigo wa pettroli na spea pati? Au hii ndio tabia na hulka yake halisi ya kusema maneno tofauti na kile inachokiamini kama vile kutudanganya sisi ni wajamaa na kumbe nchi ni ya kibepari?

      Ingawa gharama ya kununua magari hayo ni kama bilioni 70 lakini gharama za kuyajaza mafuta na kuyahudumia kiufundi ni bilioni 200 kwa mwaka. Hivi tunataka kuwakomboa Watanzania au tunawafanyia usanii kwa namna hii?

      Hivi kweli tutashangaa Rwanda inaelekea kwenye GDP per capita ya dola 3,000 sisi tunaogelea ogelea kwenye dola 600 kwa miongo kadhaa sasa?


      Na wakubwa hawajui jinsi tunavyoila Krismasi ya mwaka huu, mwaka mpya wa Kiislamu na mwaka mpya wa Kikirsto kwa taabu na dhiki kubwa ajabu?

      Mkuu Iga asante kwa taarifa muhimu sana.

      Wakuu ni dhahiri kabisa serekali yetu imeshindwa kutoa kipaumbele kwa mambo muhimu yanayoweza kulisaidia taifa letu kupiga hatua zaidi,kwakuwa wananchi walio wengi mambo kama haya hawajui kwamba yanauhusiano wa moja kwa moja na umasikini unaowazunguka.
      Tsh 70 bilioni zingetumika kununua matrekta zaidi ya 1800 ambayo kila mkoa ungeweza kupata mgao wa matrekta 82.Hivi tunahitaji wataalamu kutoka nje kutuambia tuache kununua magari ya kifahari !!!!.

      Mwl J Nyerere aliwahi kusema ili nchi iendelee inahitaji watu,viongozi bora,siasa safi na ardhi.
      Tanzania ina watu miloni 40,ina ardhi yenye ukubwa wa 364,900 sq miles.
      Tanzania ina mito mikubwa na maziwa makubwa ambayo kama tungeamua kuwekeza katika kilimo tu leo hii tungekuwa na uwezo kuilisha Afrika.Kenya inategemea kupata chakula kama mahindi,maharage na nk kutoka Tanzania.Pengine Kenya wamegundua watanzania hawaitumii ardhi yao vizuri ndiyo maana wanataka ardhi iwe huru kwa wananchi wa EAC.
      Hakuna ubishi tene kwamba Tanzania imekosa siasa safi na uongozi bora.
      Viongozi tulionao hawana vision na mission ya kuliondoa taifa katika umaskini.
      Viongozi wetu waliofanikiwa kukwea hadi ngazi za juu wana sifa zifuatazo majungu,fitna,ufisadi,uongo na ubinafsi.
      Policies nyingi zimebaki kwenye vitabu bila utekelezaji,MKUKUTA,MKURABITA na nk ni mfano mzuri wa namna wanasiasa walivyo waongo hasa kipindi cha kampeni.

    12. #10
      Sober's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th June 2008
      Posts : 290
      Rep Power : 640
      Likes Received
      38
      Likes Given
      31

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Tatizo ni zile 10% za D.T Dobie na International Motors... wenyewe wanaziita "commision" kwa kuwaletea biashara. The higher the deal, the higher the commision.

    13. #11
      Companero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2008
      Posts : 4,755
      Rep Power : 6504
      Likes Received
      955
      Likes Given
      1107

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Mheshimiwa Waziri Mkubwa ameshatoa msimamo wa Sirikali kuhusu kupunguza matumizi ya mashangingi. Msiwe na haraka kuliko upesi. Vuteni subira. Utekelezaji wa maagizo ya Serikali unakwenda hatua kwa hatua. Mathalani:

      - Kupunguza semina kulianza kwa hatua ya kuwa na semina kuhusu kupunguza semina
      - Kupunguza matumizi ya magari kumeanza na hatua ya kumalizia kwanza manunuzi
      - Kutekeleza maazimio ya Kamati ya Richmond bado kuko kwenye hatua ya hatua
      "Each generation must, out of relative obscurity, discover its mission, fulfil it, or betray it"/Kila kizazi, katika utata wa kipindi chake, lazima kiutambue wajibu wake na kiutekeleze au kiusaliti - Frantz Fanon

    14. #12
      Modereta's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 24th July 2008
      Location : Dar
      Posts : 166
      Rep Power : 586
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Quote By SaidSabke
      Watanzania tuache kulalama bila sababu za msingi.tunadai kuwa watumishi serikalini hawaendi vijijini kuhimiza maendeleo.tunataka viongozi waende vijijini kusimamia maendeleo sasa unataka waende kwa kutumia punda.haya magari munayoita ya gharama gari gani ambalo sio gharama siku hizi landrover seris three hazipo siku hizi mbona watu wanakuwa hawaelewi chochote na kujifanya kujua hebu nieleze gari lililorahisi ni lipi ukilinganisha na ukubwa wa nchi hii ubovu wa barabara za vujijini nk.
      Ndugu yangu wewe WATANZANIA sio Mbumbumbu, hayo magari yanayokwenda vijijini tunayaona na hapa mjini yakipeleka watoto shule na kuchukua majani ya ngombe tunayaona si kwamba watu hawajui. Ukumbuke wngine hao wanayoyatumia ni ndgu zao na wanajua matumizi ya hayo magari. Hebu tuache kutetea vitu ambavyo viko wazi. Nasikia kule kwa Kagame hakuna vijiji!!!!!!!!!!!
      Mwenzetu angalia hata alama za nyakati, kwako wewe ni sawa tu wagonjwa mwananyamala, amana, temeke na hospitali zote za serikali wanakosa dawa ni sawa?????????

    15. #13
      mti_mkavu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd December 2008
      Posts : 23
      Rep Power : 535
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Quote By Iga
      WAKATI Bw. Kagame huko Rwanda kafunga soko la serikali kuhodhi magari yanayokula mabilioni ya fedha za umma bila kuwa na manufaa ya moja kwa moja kwa raia wa kawaida ila tu kwa wale wanaoyatumia na jamaa zao, hapa Tanzania magari ya kifahari zaidi ya 700 ndio kwanza yanapakuliwa bandarini.

      Je, huu si unafiki kulalama mzigo anaobebeshwa mwananchi wa kawaida anayeteseka kwenye usafiri wa umma usio na heshima wala taadhima usiku na mchana, akienda na kutoka kazini au hospitali au shule au kwenye shughuli zake nyingine na kisha kuwa wasanii kwa kuthubutu bila aibu kuwaambia watu kuwa huu ni mzigo wa mwisho wavumilie tu.

      Magari hayo mia saba kwa bei za haraka haraka ni kwambwa yameigharimu serikali shilingi bilioni 70. (Tshs. 70,000.000,000/=). Magari haya yakiuzwa kwa watu na mashirika binafsi kwa hiyo yanaweza kuipatia serikali fedha za kuwalipa wastaafu wa EAC na kuondokana na maapizo na laana zao kwa Watanzania wote na vile kumaliza kabisa matatizo madogo madogo ya walimu.

      Nilulize swali moja, je, serikali ya awamu ya nne inaona ugumu gani kuwauzia au kuwakopesha magari hayo watumishi wa serikali ili angalau tupunguziwe mzigo wa pettroli na spea pati? Au hii ndio tabia na hulka yake halisi ya kusema maneno tofauti na kile inachokiamini kama vile kutudanganya sisi ni wajamaa na kumbe nchi ni ya kibepari?

      Ingawa gharama ya kununua magari hayo ni kama bilioni 70 lakini gharama za kuyajaza mafuta na kuyahudumia kiufundi ni bilioni 200 kwa mwaka. Hivi tunataka kuwakomboa Watanzania au tunawafanyia usanii kwa namna hii?

      Hivi kweli tutashangaa Rwanda inaelekea kwenye GDP per capita ya dola 3,000 sisi tunaogelea ogelea kwenye dola 600 kwa miongo kadhaa sasa?


      Na wakubwa hawajui jinsi tunavyoila Krismasi ya mwaka huu, mwaka mpya wa Kiislamu na mwaka mpya wa Kikirsto kwa taabu na dhiki kubwa ajabu?

      Nimepita Muhimbili Hospitali leo ni balaa tupu! Kuna tatizo la umeme vipimo havifanyiki. Jamani hizi hela mngewanunulia majenereta.

      Ni aibu tupu!!!!

    16. #14
      Companero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2008
      Posts : 4,755
      Rep Power : 6504
      Likes Received
      955
      Likes Given
      1107

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Quote By mti_mkavu
      Nimepita Muhimbili Hospitali leo ni balaa tupu! Kuna tatizo la umeme vipimo havifanyiki. Jamani hizi hela mngewanunulia majenereta.

      Ni aibu tupu!!!!
      Kuna kitu kinaitwa mistari ya bajeti, hii huwa haivukwi hivi hivi tu.
      "Each generation must, out of relative obscurity, discover its mission, fulfil it, or betray it"/Kila kizazi, katika utata wa kipindi chake, lazima kiutambue wajibu wake na kiutekeleze au kiusaliti - Frantz Fanon

    17. #15
      mti_mkavu's Avatar
      Member Array
      Join Date : 23rd December 2008
      Posts : 23
      Rep Power : 535
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Kweli halipitwi lakini ni wangapi wanaletewa bajeti kama walivyoomba. Angalia tangazo la haki elimu.

      hela hazifiki kaka
      sijui lakini!!!

    18. #16
      Companero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2008
      Posts : 4,755
      Rep Power : 6504
      Likes Received
      955
      Likes Given
      1107

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Quote By mti_mkavu
      Kweli halipitwi lakini ni wangapi wanaletewa bajeti kama walivyoomba. Angalia tangazo la haki elimu.

      hela hazifiki kaka
      sijui lakini!!!
      Hela hazifiki zikifika zinaliwa zisipoliwa hazitoshi zikitosha hazitumiwi zikitumiwa hazibaki zikibaki zinarudishwa zikirudishwa hazisaidii zikisaidia...
      "Each generation must, out of relative obscurity, discover its mission, fulfil it, or betray it"/Kila kizazi, katika utata wa kipindi chake, lazima kiutambue wajibu wake na kiutekeleze au kiusaliti - Frantz Fanon

    19. BAK
      #17
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,619
      Rep Power : 44968
      Likes Received
      8371
      Likes Given
      8347

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Serikali yetu haina vipaumbele kabisa. Wakati mahospitali yetu hayana vitanda, madawa na vifaa muhimu, wakati mashule yetu hayana vyumba vya madarasa vyenye hadhi ya kuitwa madarasa, vyoo, walimu, na vifaa muhimu vya mashuleni, wakati wasomi wanaomaliza katika vyuo vikuu mbali mbali hawana ajira, wakati umeme wetu bado ni wa kubahatisha, wakati maji safi bado ni adimu mno cha muhimu walichokiona wao ni kwenda kununua magari ya kifahari ambayo hayaongezi tija yoyote na kuleta maendeleo kwa Watanzania. Halafu bila haya hata aibu 2010 watarudi kwa wananchi kuomba tena kupewa awamu nyingi ya kuebdelea kuiangamiza Tanzania. Shame on you JK na serikali yako!!!
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    20. #18
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,020
      Rep Power : 2562
      Likes Received
      788
      Likes Given
      28

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Najua Zitto anaujua undani wake na Malecela ndiye kapelekwa Mbeya kuchukua jimbo .Wacha tusikie wananchi wa Mbeya ni waelewa wa namna gani na Jimbo watampa kuna issues nzito na hizi Mbeya ni sehemu yake .Mchungaji kumbe ana lake jambo .Mie nilitaka kushangaa aina ya Lwakatare kuingia CCM na huku hawaachi Makanisa maana yake nini .Wacha tusikilizie wakati Brussels hawana heating system magari yanamwagwa ? Jamani duh!!

    21. #19
      Bongolander's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th July 2007
      Location : Tandale
      Posts : 4,035
      Rep Power : 1418
      Likes Received
      610
      Likes Given
      44

      Default Re: Serikali yamwaga mashangingi: Hatujifunzi tu kutoka Rwanda na Kagame anavyotawal

      Watu wanagombea nafasi mbalimbali, na kutaka vyeo mbalimbali serikalini na kwenye idara nyingine kutokana na kutaka kuyatumia magari hayo. Ndio maana itakuwa vigumu sana kwa serikali(yaani wanaoataka madaraka ili watumie magari hayo) kupiga marufuku kabisa matumizi ya magari hayo. Naona badoi ni politics tu. Hatuwezi kujilingansha sisi na Rwanda, Rwanda tayari wako steps ahead of Tanzania. Wana uwezo mkubwa wa ku-manage nchi yao na ku-manage raslimali zao, sisi ni kinyume kabisa na Rwanda, labda tulinganishwe kidogo na Somalia, ingawa sisi hatuna vita na hatuuani kama wenzetu Somalia.

    22. BAK
      #20
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,619
      Rep Power : 44968
      Likes Received
      8371
      Likes Given
      8347

      Default Wakati wanafunzi wakosa madarasa, Serikali yanunua mashangingi 800

      Madarasa yakosesha maelfu sekondari
      Merali Chawe, Mbeya
      Daily News; Tuesday,December 23, 2008 @21:15

      Zaidi ya wanafunzi 20,000 kati ya 41,017 waliofaulu mtihani wa darasa la saba mkoani Mbeya, wamekosa nafasi ya kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza kutokana na upungufu wa vyumba vya madarasa na mabweni.

      Ofisa Elimu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Kaponda aliwaambia waandishi wa habari kuwa wanafunzi 77,072 waliandikishwa na kati ya hao waliofanya ni 74,518 wakiwamo wasichana 37,926 na wavulana 36,592 sawa na asilimia 97.

      Hata hivyo, kiwango cha ufaulu kimeshuka kutoka asilimia 63 mwaka jana hadi asilimia 55 mwaka huu huku kukiwa na mahitaji ya vyumba 620 vya madarasa ili waliobaki waingie katika awamu ya pili.

      Alisema kati ya wanafunzi 41,017 waliofaulu wakiwamo wasichana 18,206 na wavulana 22,811, waliochaguliwa katika awamu ya kwanza kuendelea na masomo ya kidato cha kwanza ni 16,236 na wametengewa nafasi 234 za bweni huku wanafunzi 16,002 wakisoma shule za kutwa.

      Naye John Mhala anaripoti kutoka Arusha kuwa wanafunzi 4,525 waliofaulu mtihani mwaka huu, watakosa nafasi ya kujiunga kidato cha kwanza kutokana na uhaba wa shule za sekondari.

      Ofisa Elimu wa Mkoa wa Arusha, Raymond Mapunda alisema hilo linatokana na pamoja na sababu nyingine, ongezeko la ufaulu mwaka huu ambako watahiniwa 22,738 walifaulu kuingia kidato cha kwanza kati ya 40,884 waliofanya mtihani. Kiwango hicho ni sawa na asilimia 66.5 ya ufaulu na kwamba wastani wa kufaulu umeongezeka kutoka asilimia 85.15 mwaka jana hadi asilimia 115.3 mwaka huu.

      Huko Songea, Juma Nyumayo, anaripoti kuwa wanafunzi 19,085 wamefaulu mtihani wa kumaliza elimu ya msingi mwaka huu mkoani Ruvuma wakiwamo wasichana 8,688 na wavulana 10,397 sawa na asilimia 50.2 ya wanafunzi 38,013 waliofanya mtihani mkoani hapa. Mwenyekiti wa Kamati ya Uteuzi Mkoa wa Ruvuma, Saleh Pamba alitangaza matokeo hayo jana na kusema kuwa matokeo hayo hayaridhishi ingawa kuna ongezeko la asilimia 6.7 ikilinganishwa na asilimia 43.5 ya mwaka jana.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    Page 1 of 3 123 LastLast

    Similar Topics

    1. Rwanda Kumekucha, Maandamano Dhidi Ya Kagame Paris
      By Muke Ya Muzungu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 18th August 2011, 22:52
    2. Rwanda-Siasa-Kagame ni msomi anayeelewa anachokifanya
      By pascaldaudi in forum International Forum
      Replies: 0
      Last Post: 24th June 2011, 15:50
    3. Rwanda opposition challenges Kagame in Chicago
      By engmtolera in forum International Forum
      Replies: 6
      Last Post: 17th June 2011, 21:01
    4. Profile: Rwanda's President Paul Kagame
      By Wacha1 in forum International Forum
      Replies: 2
      Last Post: 16th January 2011, 12:18
    5. Profile: Rwanda's President Paul Kagame
      By BAK in forum International Forum
      Replies: 18
      Last Post: 4th July 2010, 23:51

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...