Habari zenu wakuu.
Leo nina dukuduku ambalo nataka kulitoa. Sijui kama wenzangu linawatatiza pia. Hivi jamani makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ana kazi gani haswa?
Nauliza hivi kutokana na ninayoyaona kwahiyo kama sipo sahihi nitarekebishwa. Kila nikiona kwenye vyombo vya habari namuona makamu wa rais aidha anazindua kitu au ni mgeni rasmi sehemu au anafanya ziara sehemu. Yani amekuwa "mzee wa kukata utepe". Ninachosema ni hivi huyu mtu tunaemuita makamu wa rais tunamlipa na kumhudumia kwa ajili ya kuhudhuria sherehe tu? Kwa nchi masikini kama yetu why do we need a ceremonial leader?
Najua watu wataanza kusema oh ni kwa ajili ya ku-accomodate muungano. Siamini hiyo ni sababu. Kwa maana tunaweza kabisa kufuta nafasi ya makamo wa rais na tukasema rais akitoka upande mmoja wa muungano basi waziri mkuu atoke upande mwingine. Kwanini tupoteze rasilimali za nchi kwa ajili ya kuwa na mtu asiye na shughuli za maana ambazo hata rais na waziri mkuu wanaweza waka gawana na kufanya?
Sina nia ya kumshushia heshima makamu wa raisi wala nafasi ya umakamu wa rais ila ninachosema sasa ifike wakati aidha tumpe makamu wa rais kazi za maana za kufanya au tukifute hiki cheo. Kwa ufahamu wangu, Makamu wa Rais ni msaidizi wa rais kwa maana rais ndiyo anaamua ampe kazi zipi makamu wake. Sasa ni kwamba rais hamuamini makamu wake kumpa kazi zozote za maana?
Jamani hili ndilo dukuduku langu.

Reply With Quote


Follow Us Here