Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

    Report Post
    Page 2 of 10 FirstFirst 1234 ... LastLast
    Results 21 to 40 of 189
    1. #1
      WATANABE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th April 2011
      Posts : 783
      Rep Power : 570
      Likes Received
      272
      Likes Given
      83

      Default Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      katika kuthibitisha ukosefu wa umakini ndani ya serikali, mchana huu mwandishi wa Clouds Redio ameripoti kuwa wagonjwa katika hospitali ya Muhimbili hawakupata huduma yeyote ikiwemo kushuhudia zaidi ya ambulance 7 zikileta wagonjwa toka hospitali mbali mbali na kulazimika kuondoka na wagonjwa wao kutokana na kukosekana kwa huduma katika hospitali hiyo. Hii inashiria kuwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda ameshinde kutekeleza ahadi yake kupelekea madajatari toka JWTZ na JKt akama alivyoahidi jana wakati akitoa kauli za dharau dhidi ya madakatari wanaogoma.

      My take: Tukumbuke kiini cha mgogoro huu ni madakatari walioko mafunzoni yaani interns katika hospitali ya Muhimbili kunyanyaswa na uongozi wa Wizara ya Afya hivyo kutakiwa Waziri Dr Haji Mponda, Katibu Blandina Nyoni na Mganga Mkuu Ngd Deo Mtasiwa kuondolewa mara moja kwa kuishawishi serikalim kuchukua hatua za kionevu dhidi ya madakatari hao waliokuw akatika mafunzo. Ni kwanini Serikali inakubali watanzania wafe katika kuwalinda wazembe watatu?

      Ni imani yangu watatu hao wakiondolea hata leo madakatari walioko katika mgomo watakuwa tayari kuzungumza na serikali kuhusu madaia yao.
      Hofstede, Riwa, kiraia and 23 others like this.

    2. FemaTV & Radio

    3. #21
      mizambwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2008
      Posts : 1,438
      Rep Power : 974
      Likes Received
      367
      Likes Given
      1807

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Quote By davidie
      je huyu pm yupo kundi lipi?
      yupo kundi la viongozi LEGELEGE.

      MIZAMBWA
      INANIUMA SANA!!!
      SASA NIMEAMINI KUWA TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA!!!!, TUANDAE KABURI LA KUIZIKA MWAKA 2015

    4. #22
      Bumpkin Billionare's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th January 2012
      Location : Msangabunyesa
      Posts : 1,280
      Rep Power : 696
      Likes Received
      557
      Likes Given
      198

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za dsm

      Quote By mmbangifingi
      Najiuliza hao madaktari kutoka jeshini huwa wapo tu hawana kazi?what i know wanatumika ktk hospitali za huko/jeshini. Sasa ukiwaondoa what next?na ni wengi kiasi hiko? kauli nadhani ilitoka kwa jazba
      Shida ni hivi kaka, viongozi wetu wanadhania madaktari wanapatikana kwa kura baada ya kampeni ndio maana hakuna anayefikiri umuhimu wao. Wanadhania wapo kama wao ambapo unaweza kumfanya Said Meck Sadiq kuwa mkuu wa mkoa wa Lindi na hapo hapo akakaimu ukuu wa mkoa wa Dar. Kwa hiyo alifikiri madaktari wa lugalo nao watakaimu muhimbili huku wanaendelea kuhudumia lugalo.
      Bigirita, dkims and Kiwewe like this.
      An Idea isn't responsible for the people who believe in it.
      Donald Robert Marquis (1878 - 1937)
      American Writer


    5. #23
      sifugi naloga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th August 2011
      Location : Near To Heaven.
      Posts : 28
      Rep Power : 397
      Likes Received
      2
      Likes Given
      5

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Ilikuwa lazima ifike huko maana nilikuwa nataka kujua battle itaishaje lazima ifike hapo.

    6. #24
      Mtumishi Wetu's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 12th October 2010
      Location : Arusha
      Posts : 2,841
      Rep Power : 3545
      Likes Received
      537
      Likes Given
      5148

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Quote By lukindo
      mkuu bora umeturudisha kwenye hoja ya msingi, maana PM yeye anaongea tu kuwa anaweza kureplace doctors wote wakati serikari hiyo hiyo imeshindwa kupeleka hata madawa kutoka MSD lakini haisiti kuja na ahadi kubwa within 24hrs!!!

      Kama kuna mtu anayeweza kutathmini hasara iliyosababishwa na mgomo mpaka sasa ndio atajua kuwa kuondoka kwa Mh. Mponda, Nyoni, Mtasiwa nk ilikuwa ni nafuu sana kwa taifa.

      Namshauri PM (japo mimi ni mtu mdogo sana na siwezi hata kumkaribia) aache porojo na ku-victimize viongozi wa mgomo badala yake ashughulikie madai kama ni ya kweli na kama sio ya kweli basi atwambie maana yeye ni juzi tu wakati wenzie wanaenda Apollo India yeye alienda London kucheck afya yake!

      Hawa wakubwa wana lugha za kilaghai na maneno ya kijanja tena wanafiki kabisa, mtu anazungumza utafikiri jambo analozungumza ni rahisi tuu!!! Mipango yao mingi ni ndoto za Alinacha, kujenga hekalu mwezini. Sasa nimeamini Tanzania hakuna mzima tuna viongozi wasanii kwelikweli, tunamuomba mheshimiwa PM Pinda akae chini apange mipango mizuri ya kutatua madai ya Madaktari. Yeye ni mtu mkuu tunamuheshimu aache porojo!!!! Kama hajui kuna kipindi nchini USA walitoa tangazo kuwa wanahitaji madaktari 400 toka hasa TANZANIA!!!!!!!!!!

      Mzee wa Rula likes this.

    7. #25
      MachoMakavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Posts : 348
      Rep Power : 645
      Likes Received
      36
      Likes Given
      11

      Default Pinda: Cheo kimempanda kichwani?

      This is getting out of hand! huwa nina heshima za dhati kwa Pinda maana namuona kama mwenzetu,hana makuu, ila kwa jinsi alivyohandle ishu hii ya madaktari..inaonekana kabadilika sana!

      1. Madaktari walianzisha mazungumzo na wizara mapema..ikakataa kuwaskiliza.

      2. Wamefanya vikao mara kadhaa kuomba kuonana na Dr. Haji, ila mara zote anawatreat kwa dharau

      3. Baada ya kuona dharau zake, wakakosa imani nae. Wakaomba kuonana na Pinda, yeye akakataa kuonana nao kidharau kwa hoja kwamba madai yao yako ndani ya wizara!

      4. Wakarudi wizarani na kumwita waziri, yeye akawasakizia Naibu waziri. Wakamwambia wanakutana Don Bosco, yeye akawajibu kwa kejeli hawezi kukutana nao vichochoroni..waje kwenye ukumbi wa serikali..Arnatoglue!

      5. Wakamjibu Anatoglue ukumbi mdogo, aje Don Bosco, yeye anaenda na kuita vyombo vya habari Ilala ili viripoti kwamba madaktari wamekataa kuja kuonana nae.

      6. Baada ya kuona serikali haina nia ya kuwasikiliza, wakatangaza mgomo rasmi. Wizara ikawa inapinga kwamba hakuna mgomo uliotangazwa na yenyewe "haina taarifa"

      7. Siku ya pili mgomo umeshika kasi, wizara bado inacheza na propaganda za magazeni na TV, kuonesha wodi chache na kusema hakuna mgomo!!

      8. Baada ya kuona inakua ishu, ndo Pinda akasema atakutana nao! huyu huyu ambaye walimkimbilia mwanzoni akakataa kuonana nao!

      9. Wao toka ijumaa wamemwambia jumapili ni siku ya kupumzika kama kuonana nao aje jumamosi au jumatatu. Badala yake, yeye jumamosi katuma ujumbe, na jumapili kaenda ukumbini ilhali akijua kwamba hatakuta mtu!

      10. Sasa anasema JKT ihakikishe hakuna sehem yoyote ambayo madaktari wanakutana. Anasahu kwamba revolution za Misri na Tunisia hazikuhitaji mkutane face to face kupanga maandamano au migomo. Age hii Social Networks ni kumbi tosha za watu kukutana! au ndo kupitwa kwa kasi ya maendeleo ya dunia kwa viongozi wetu?

      Nabaki najiuliza cheo kimempanda kichwani!

    8. Miaka 50

    9. #26
      Kabembe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2009
      Location : ITETE-Kandwesi
      Posts : 876
      Rep Power : 702
      Likes Received
      170
      Likes Given
      169

      Default

      Quote By Cynic
      Nani anakubali watanzania wafe? Kama ni hukumu, basi huwa kuna hukumu 1st hand murder & 2nd hand murder. Hapa nadhani 1st-hand murders ni nyinyi madaktari msiowahudumia hao wagonjwa na 2nd-hand murders ni hao wengine. Wekeni ubinadamu mbele ..
      Unaongea kama baba yako na mama yako kijijini wanaishi nyumba ya ghorofa na wakiumwa ambulance inawafata kuwawaisha airport kuelekea Apollo India.
      Unstoppable likes this.

    10. #27
      Izack Mwanahapa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st April 2011
      Location : Mwanza
      Posts : 314
      Rep Power : 471
      Likes Received
      129
      Likes Given
      94

      Default Athari za Tamko la Pinda dhidi ya mgomo wa Madaktari

      Nianze kwa kusema: Ninaogopa sana kama kweli madactari watarudi kazini kwa vitisho kwa necha ya taaluma yao na kazi wanayoifanya kwa sababu moja tu ya “hofu ya kupoteza kazi” Hili likitokea Madactari hawa watakuwepo kazini lakini morali yao ya kufanya kazi itakuwa imepotea kabisa na hili linaweza kupelekea “Mgomo baridi” ambao kwangu nauona ni hatari zaidi kuliko mgomo unaoendelea sasa.
      Athali za matumizi ya ubabe katika mambo ya msingi

      Tumeona mfano mara baada ya kuzuwia kwa vitisho kwa mgomo wa waalimu hapa nchini, matokeo yake ni kwamba walimu wanakwenda shuleni kama wajibu lakini hawatekelezi kazi ipasavyo na kimsingi huu ni mgomo baridi ambao bado unaendelea matokeo yake wanafunzi wanamaliza elimu ya msingi lakini hawajui kusoma, kuandika wala kuhesabu. Wapo wanafunzi wa darasa la tano lakini hawawezi kujibu mtihani wa darasa la pili. View Uwezo Study Report at Uwezo.net

      Serikali imechukua hatua gani juu ya tatizo la kufeli kwa wanafunzi?

      Naamini wote hapa ni wafuatiliaji wazuri wa habari, zifuatazo ni baadhi ya hatua ambazo serikali imezichukua ambazo si kati ya kelo zinazolalamikiwa na walimu: 1. 1.Matumizi ya simu za mkononi yamepigwa marufuku
      2. 2. Waziri wa elimu anasema wanafunzi waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza watapimwa tena kabla hawajaanza sekondari na atakayefeli mkuu wake wa shule atawajibishwa ilhali anafahamu wasahishaji ni baraza na si mwalimu mkuu
      3. 3. Mtihani wa kidato cha pili umerejeshwa
      4. 4. Michango ya masomo ya ziada imepigwa marufuku

      NOTE:

      Matokeo ya kidato cha nne mwaka 2010 kati ya wanafunzi 353840 waliofanya mtihani huo ni wanafunzi 40,388 tu ndio waliofaulu kwa daraja la kwanza hadi la tatu.
      Kwa upande wa Madactari

      Sasa tujiulize, kama madactari nao watarudi kazini na kuendesha mgomo baridi watanzania tutakuwa kwenye wakati gani? Ni bora ya sasa kila mtu anajua wamegoma hivyo anakwenda kwenye hospitali binafsi lakini katika mgomo baridi hatutajua madactari wanaweza wakawepo na wakatupa matibabu tofauti yatakayopelekea athari mbaya kwa wananchi. Lakini pia Tanzania haina madactari mbadala wa kujaza nafasi za madactari hawa ikiwa wataondolewa kazini kama inavyosemwa. Siamini kama matumizi ya mabavu yatalete suluhu katika jambo hili na mwisho wa siku wanaokuja kuumia ni masikini waliopewa jina “WATANZANIA WA KAWAIDA”

      Nini maoni yako?
      Askofu and Kiwewe like this.

    11. #28
      Edson's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2009
      Posts : 7,308
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      433

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      pinda ni mpuuzi
      I'm Naturaly Evasive..

    12. #29
      Msarendo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2011
      Location : Rich Forever.
      Posts : 2,526
      Rep Power : 926
      Likes Received
      322
      Likes Given
      7

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Hivi kweli mtu mwenye akili yako timamu unaweza ukamchulia Pinda serious.
      Bigirita likes this.

    13. #30
      Mlosi K. Mtulutumbi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th October 2010
      Posts : 604
      Rep Power : 611
      Likes Received
      187
      Likes Given
      195

      Default Re: Athari za Tamko la Pinda dhidi ya mgomo wa Madactari

      Hili mtoto wa mkulima halijui kuwa waweza kumpleka mbuzi mtoni ila huwezi kumlazimisha kunywa maji
      Kufanya Jambo Baya ni Dhambi, twafahamu hilo, Ukiwa na nia ya Kutenda au kuamua jema badala yake ukatenda jambo baya kwa Kuogopa kukaripiwa na wafanya Mabaya ni Unafiki na Ufukara wa Fikra!

    14. #31
      MachoMakavu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th February 2008
      Posts : 348
      Rep Power : 645
      Likes Received
      36
      Likes Given
      11

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Quote By bona
      pinda ana weakness ya kutumia feelings zaidi ktk maamuzi kuliko hali halisi!
      umemchambua vyema mkuu! Na kiongozi makin i hutakiwi kutumia feelings katika kufanya maamuzi

    15. #32
      Chakaza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2007
      Location : everywhere
      Posts : 3,536
      Rep Power : 1473
      Likes Received
      879
      Likes Given
      521

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Kwani serikali ingeamua kuwasimamisha kazi hao wakina Blandina pending uchunguzi kuwa wao ni chanzo cha Tatizo lililo sababisha huo mgomo na vifo vya wagonjwa na madaktari hao wakarudi kazini nchi ingeathirika wapi kwa wao kusimamishwa? Tatizo pekee ni kulindana tuu na kushindwa kutoa maamuzi magumu.
      Hatutajua chochote iwapo hatutahoji na kudadisi

    16. FJM
      #33
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,170
      Rep Power : 2568
      Likes Received
      5318
      Likes Given
      4585

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Ingekuwa sekta nyingine serikali ingeweza kukaa kimya hoping kwamba wagomaji wakiwa nje ya ajira kwa muda mrefu na wakishaanza kukosa mshahara basi pengine watarudi kazini. Lakini kwenye afya madaktari wakiendelea na mgomo maana yake idadi ya vifo nayo inaongezeka. Serikali, next time pick your battle more wisely!

    17. #34
      sblandes's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th April 2010
      Location : SINGAPORE
      Posts : 521
      Rep Power : 620
      Likes Received
      31
      Likes Given
      63

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Mambo magumu kote kote Serikali haitaki kugeuka jiwe na madaktari wakitunisha misuri ,wakupoteza zaidi ni serikali wananchi watakosa imani na serikali.Yaonekana madaktari wamejipanga vizuri kuliko serikali.Serikali kuwa makini kwa hilo.
      Kiwewe likes this.

    18. #35
      nitonye's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th December 2011
      Posts : 4,262
      Rep Power : 1289
      Likes Received
      1472
      Likes Given
      27

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Pinda vitisho anavyompaga mkewe wake anadhani na madaktari wako hivyo? Mimi naona hali ikiendelea kuwa mbaya raia na sisi tukusanyike tuishinikize serikali yote kujiuzuru
      Kiwewe likes this.

    19. #36
      tembeleh2's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th July 2010
      Posts : 634
      Rep Power : 574
      Likes Received
      120
      Likes Given
      11

      Default Re: Athari za Tamko la Pinda dhidi ya mgomo wa Madactari

      Unajua mgomo huu umekuja kwa sababu madaktari (hata na wananchi wa kawaida) wanaona pesa zote za nchi hii zinakwenda wapi!!! ingekuwa tofauti, yaani maisha yetusisi watumishi wote hayatofautiani sana nina uhakika mgomo huu usingekuwepo. Sasa basi kwa serikali kutumia ubabe, serikali yenyewe inajua matokeo ya ubabe huo, lakini kwa sababu wao wakuu wenyewe na familia zao hawatibiwi kwenye hospitali zetu hawawezi kujali, lolote litakalotokea halitawaathiri. Ila ipo siku mungu atasikia kilio chetu.
      only83 likes this.

    20. #37
      BINARY NO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2011
      Posts : 550
      Rep Power : 483
      Likes Received
      137
      Likes Given
      63

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Rais akitoka ADIS ABABA nadhani kesho kwani hali ilivyo Hawezi kwenda nchi nyingine ATAANZA NA PINDA WAKE KWANI HANA USHAWISHI MKULIMA HUYU then atamalizia na wakina BLANDINA.....TATIZO LA PINDA ANATUMIA HISIA KWENYE MAAMUZI BAADA YA KUTUMIA AKILI NEXT TIME ATATUMIA SABULI LAKE LA UKULIMA

    21. #38
      MPadmire's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2006
      Location : Dar es salaam
      Posts : 859
      Rep Power : 848
      Likes Received
      158
      Likes Given
      76

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Canada na Australia wanahitaji madokta kutoka Tanzania.

      Wakiwafukiza tu basi - wananchi tunaingia barabarani
      When your life becomes a battleground, your mind is the best weapon

    22. #39
      ngamiamzee's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th June 2011
      Posts : 238
      Rep Power : 450
      Likes Received
      16
      Likes Given
      1

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      hivi tuna waziri mkuu nilimshangaa alivyosema ataki uraisi hivi anaona watanzania
      hawana akili mpaka wakampe uraisi uwaziri mkuu awezi au wenzake awamwambii
      ukweli

    23. #40
      Ismaily's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th June 2011
      Posts : 357
      Rep Power : 472
      Likes Received
      49
      Likes Given
      0

      Default Re: Pinda ashindwa kupelekea madaktari wanajeshi ktk hospitali za DSM

      Serikali ya kijambazi ya CCM ni dhaifu na legelege na ndiyo mana huwa wanamawazo legelege na dhaifu!

    Page 2 of 10 FirstFirst 1234 ... LastLast

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...