Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

    Report Post
    Page 5 of 24 FirstFirst ... 3456715 ... LastLast
    Results 81 to 100 of 477
    1. #1
      Regia Mtema's Avatar
      R I P Array
      Join Date : 21st November 2009
      Posts : 2,988
      Rep Power : 1115
      Likes Received
      764
      Likes Given
      397

      Default Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Wakuu habari! Nimatumaini yangu kuwa tunaendelea vizuri na majukumu yetu ya kila Siku.

      Nimeamua kuanzisha Uzi huu kwa lengo la kukuza ya kero,maoni,ushauri na chochote toka kwenu ili tuweze kuyasimamia ndani na nje ya Bunge.Kwa kutambua kuwa wanaJF wamesambaa kila mahali,maofisini,mashuleni,mit aani,majumbani na huko kote kuna kero mbalimbali zinazohitaji attention ya Serikali lakini mambo hayaendi na ungpenda kuona suala hilo linafanyiwa Kazi na hivyo unapendekeza Kambi ya Upinzani izibebe na kuzisimamia. Basi tafadhali toa kero,maoni,ushauri au hata mapendekezo yako hapa.

      Tafadhali kero ziwe za kijamii na sio za mtu binafsi.

      Natanguliza Shukrani zangu za dhati kwa Ushirikiano wenu.

      Wenu katika Ujenzi wa Taifa
      Regia Mtema
      Kilombero For Change(K4C)-Mfuko wa Maendeleo Kilombero


    2. #81
      babap's Avatar
      Member Array
      Join Date : 22nd April 2011
      Posts : 63
      Rep Power : 425
      Likes Received
      11
      Likes Given
      0

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Hakuna swali la msingi kama hili najua na wewe utasita kuwauliza wabunge wenzako. Swali lenyewe utekelezwaji wa matumizi ya mfuko wa jimbo? Na je huu mfuko upo kwa faida ya nani?
      Regia Mtema likes this.

    3. #82
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,979
      Rep Power : 6860
      Likes Received
      2415
      Likes Given
      3177

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Ragia

      Bado naendelea ........

      [20] Shirikisho la EAC likataliwe kwa nguvu zote.Nchi za Uganda,Kenya Rwanda na Burundi zote zimeungana dhidi ya Tanzania.Waziri wa Afrika Mashariki ni vyema akaambiwa wazi masuala yafuatayo kamwe yasikubaliwe.

      [A] Masuala ya Ulinzi na Usalama yabaki jukumu la kila nchi.

      [B]Masuala ya Ardhi yasiingizwe katika EAC.

      [C] Soko moja la Utalii Tanzania ikatae kwa nguvu zote.Sote tunajua jinsi Kenya ilivyodanganya ulimwengu kwamba mlima Kilimanjaro na mbuga ya wanyama ya Serengeti ziko kwao.Tanzania ikikubali upumbavu wa soko moja la utalii.

      [D] Pasport itumike kuingia na kutoka kwa wageni wote wa EAC.


    4. #83
      mzee wa miba's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 20th December 2011
      Posts : 152
      Rep Power : 409
      Likes Received
      25
      Likes Given
      7

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Quote By Regia Mtema View Post
      Wakuu habari! Nimatumaini yangu kuwa tunaendelea vizuri na majukumu yetu ya kila Siku.

      Nimeamua kuanzisha Uzi huu kwa lengo la kukuza ya kero,maoni,ushauri na chochote toka kwenu ili tuweze kuyasimamia ndani na nje ya Bunge.Kwa kutambua kuwa wanaJF wamesambaa kila mahali,maofisini,mashuleni,mit aani,majumbani na huko kote kuna kero mbalimbali zinazohitaji attention ya Serikali lakini mambo hayaendi na ungpenda kuona suala hilo linafanyiwa Kazi na hivyo unapendekeza Kambi ya Upinzani izibebe na kuzisimamia. Basi tafadhali toa kero,maoni,ushauri au hata mapendekezo yako hapa.

      Tafadhali kero ziwe za kijamii na sio za mtu binafsi.

      Natanguliza Shukrani zangu za dhati kwa Ushirikiano wenu.

      Wenu katika Ujenzi wa Taifa
      Regia Mtema
      Hivi jamani kila mtu anaona jinsi maaskari polisi huku wilayani Rombo,walivyoibuka matajairi na kumiliki magari ya kifahari ghafla,kila mtu anaona na aliona jinsi walivyokesha usiku na kushiriki kusindikiza mali za magendo sukari,mchele,magari ya wizi,mambo yanafanyika kila mtu anaona hata mbunge wetu wa CDM anajua yote haya,siyo uongo hata ukiongea na watoto wadogo,Selikali ya tanzania imewatelekeza na inawalipa mshahara kidogo,hata wabunge wetu wanajua kuwa posho ya siku mbili ya mbunge wa nchi maskini ya tanzania ni sawa na mshahara wa copro wa polisi.Maaskari tunakunywa nao bia baa hata wao wanaropoka kuwa serikali haiwezi kuwafanya kitu kwani hata mshahara wanaolipwa hautoshi hata matumizi ya siku 10,

      Pia nazidi kulia na wabunge wetu wa CHADEMA, ukweli mumetutelekeza hata nyie katika kikao kilichopita mlichukua posho ya 200,000/= kimyakimya mkanyamaza hadi gazeti letu la mwanahalisi na mwananchi yaalipotufumbua macho sisi watanzania,hivi manatupeleka wapi? wakati sisi tulidhani mko bungeni kwa maslahi yetu na siyo ubinafsi.
      Hii inaskitisha sana najua mnazifahamu shida zetu kuwa tunaishi katika vichuguu,matembe,mabanda,mahan daki,misonge,hatuna nafuu kabisa,mafuta ya taa mlishiriki kuidhinisha yapandishwa kodi na beii iende juu,simenti na bati ,nondo na mbao bei haikamatiki,hivi vitu vimekuwa ni anasa.Naomba mjitathimini nyinyi wenyewe mmeshiriki vikao vingapi vya kuhamasisha maendeleo katika jamii/kaika majimbo yenu huko vijijini ili kuhamasisha ujenzi wa nyumba bora na namna ya kujiongezea kipato kwa maskini mtanzania?
      Hivi kwanini hiyo posho msikate hata Robo yake ili muajiri wataalamu washauri vijijini watakaowashauri wanakjiji jinsi ya kujiongezea kipato na kujenga nyumba bora,hata hiyo mifuko ya maendeleo ya majimbo mnaitafuna wenyewe hata hatushirikishwi,mapato na matumizi yake hatuioni,Hivi tunauliza mlipoipitisha fasta fasta hatujui kumbe ilikuwa ni lengo la kutafuna kimyakimya pia.
      NAOMBA MTUMIEE ELIMU ZENU NA UTASHI WENU KUWEKA REKODI SAWA KWAMBA PAMOJA NA KUWA HAMJAKAMATA DOLA LAKINI FANYENI KAZI NA WANANCHI VIJIJINI KILIMO,UFUGAJI,NA MUWASAIDIE NA KUWASHAURI KWANI HATA WATAALAMU WA UGANI WA SERIKALI WAMESHINDWA KUTULIZA KIU YA MASKINI WA TANZANIA KUJIKOMBOA NA KUPATA MAENDELEO ENDELEVU,CHONDECHONDE MSIACHE MBACHAO KWA MSALA UPITAO.

    5. #84
      Mr. Zero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th June 2007
      Posts : 4,103
      Rep Power : 1445
      Likes Received
      485
      Likes Given
      72

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Quote By Ngongo View Post
      Heshima kwako Regia,

      Kero yangu kubwa ni kama ifuatavyo.

      [1] Wabunge kujiongezea posho.Huu ni uhuni mkubwa hamkuomba ubunge hili mjiongezee maslahi mliomba hili mtutumikie ajabu mmegeuka kero kila siku kilio cha posho kwa kisingizio maisha magumu tangu lini maisha magumu yamekuwa ni kwa wabunge pekee yao.

      [2] Viti maalumu na viti 10 vya Rais vifutwe mara moja.Utafutwe utaratibu mwingine ambao utahakikisha wabunge wanawake wanachaguliwa na wanawajibika kwa wapiga kura.

      [3] Teuzi za Rais [Mabalozi,Mawaziri,Wakuu wa vyombo vya ulinzi na Usalama,Wakuu wa mashirika ya Umma] wathibitishwe na bunge

      [4] Ukubwa wa Serekali upunguzwe.Bajeti inaonyesha 3/4 inatumika kwaajili ya uendeshaji wa serekali 1/4 kwaajili ya shughuli za maendeleo.Hali ibadilike 3/4 maendeleo na 1/4 shughuli za uendeshaji.

      [5] Serekali kwa maana ya viongozi waache kutumia magari ya gharama kubwa eg Land Cruiser VDJ 200 na Nissan Y 61.Haya magari ni kwaajili ya wasanii matajiri wa ulaya na Marekani.Viongozi watumie Suzuki,Corolla,RAV4 au Land Cruiser HZJ 76.

      [6] Serekali ipunguze utegemezi wa Budget toka nchi wahisani.

      [7] Mikataba ya madini itazamwe upya.Kodi na tozo mbali mbali ziongozwe.Serekali imiliki hisa za migodi yote ya dhahabu.

      [8] Wakuu wa Mikoa,Wilaya na manaibu waziri waondolewe mara moja.Zoezi hili litasaidia kupunguza matumizi ya serekali.

      [9] Viongozi wa kuchaguliwa na wananchi wawajibike kwa wananchi waliowachagua na si chama.Kiongozi wa kuchaguliwa avuliwe uongozi na wananchi waliomchagua na si vyama hata kidogo.Ni vyema sheria ikapitishwa haraka hili kumlinda mwananchi.

      [10] Muda wa kupisha budget upunguzwe.Utafutwe utaratibu wa kuwapatia mapema waheshimiwa wabunge mswaada.

      [11] Kiwepo kipengele kinachomtaka mbunge walau awe na shahada ya kwanza.Wabunge ni watunga sheria na wasimamizi wa serekali kumpa mtu ubunge asiyekuwa na elimu ya kutosha ni hatari kubwa.Fikiria ukiomba kazi ya Pump attendant unaulizwa cheti iweje mbunge kigezo kiwe kusoma na kuandika tu !.

      Quote By Barubaru View Post
      Kuna mambo manne tu ambayo watanzania ni lazima yafanyike ili kuikomboa nchi yenu katika kuondoa kero na kuleta hali nzuri kiuchumi kwa wananchi wenu.
      1. Kupata Katiba iliyo bora.
      a. Katiba yenye kulinda maslahi ya taifa lenu na kujali maslahi ya wananchi kwanza.
      b. Katiba yenye kulinda rasilimali za Taifa lenu na kuzimilikisha kwa wananchi
      c. Katiba itakayowafanya viongozi wote waliochaguliwa na wananchi waweze kuwajibika kwa wananchi na sio vyama vya siasa.
      d. Katiba itakayoangalia uwezekano mkubwa wa kuinua hali ya uchumi wa mtu mmoja mmoja mpaka kwa taifa zima kwa kifupi katiba yenye utashi wa kujenga uchumi wenu na kuondoa utegemezi.

      2. Wananchi kupenda kuwajibika katika kulijenga taifa lenu. Hapa panahitajika zaidi kujenga msukumo na tarbia yya wananchi kulipenda kwa dhati taifa lenu na kuwa na kiu ya maendeleo . Kuchukia rushwa na ubinafsi na kupenda kulipa kodi kwa maendeleo ya nchi yenu

      3. Viongozi kuacha kutumia afisi za umma na madaraka katika kujilimbikizia mali binafsi. Hapa panatakiwa kuweka sheria kali kulidhibiti hili


      4. Taifa kuwa na mtazamo wa kiuchumi zaidi na sio siasa. Kila kitu kinachohusi maslahi ya taifa ni lazima kitazamwe kimapana zaidi katika angle ya kiuchumi na si kisiasa

      Mkifanikiwa kurejesha hayo juu basi pasi na shaka mtaanza kusonga mbele.

      Kila la kheir

      Kumbe hata Barubaru na Ngongo wana kerwa na serikali hii
      "The Only Necessary for the Triumph of Evil is for Good Men to do Nothing" Edmund Burke (1729 - 97)

    6. #85
      nashy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Location : MANG'ORA
      Posts : 665
      Rep Power : 560
      Likes Received
      134
      Likes Given
      124

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      thanks Regia,
      kero yangu kubwa bado iko katika sekta ya madini, nashukuru Mungu kwamba nimefanya kazi nyingi za consultation katika migodi na pia nimefanya tafiti mbali mbali katika maeneo hayo. nimegundua kuna tatizo moja kubwa linalowacost watanzania na hasa ni umiliki wa rasilimali. mathalani sheria ya ardhi inamtambua mmiliki na ardhi ila kilicho chini ya ardhi ni mali ya serikali, hivyo wanapoenda kuanzisha mgodi huangalia ukubwa wa ardhi tu na siyo thamani ya dhahabu, tanzanite au madini mengine yaliyopo. hiki ni chanzo kikubwa cha migogoro. wanalipwa kidogo ukilinganisha na mali iliyopo. nadhani ni vema sheria hii ikiangaliwa upya.
      mwisho naomba kama mnaweza mkaraise issue ambayo itawafanya wanakijiji kwenye mgodi kwa ujumla wao wawe share holders nadhani ni njia pekee na ya haraka kwa wao kunufaika kuliko ilivyo hivi sasa.
      for more plz contact me [email protected], we can share many concerning mining sector in Tz


    7. #86
      Topical's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 5,050
      Rep Power : 1235
      Likes Received
      853
      Likes Given
      707

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Maswali ya msingi

      a. Lini serikali ya JMT itahamia Dodoma; na kama mpango huo wa kuhamia dodoma haupo lini serikali itakuwa wazi kuwaeleza wananchi wake; maana kuna faida nyingi kwa serikali kuhamia ikiwemo uchumi wa mikoa ya pembezoni kukua kutokana kuhama kwa fedha nying na watu wa serikalini;

      b. Lini serikali itafuta na kuondoa misamaha ya kodi kwa mashirika ya dini , NGO etc..kwani kwasasa misamaha imekuwa njia kuu ya mafisadi kupitisha pesa chafu na kuiacha serikali ikiwa ombamba

      c. Lini serikali ikaacha kupeleka pesa zake kanisani (kwenye mashirika ya kikristo) ikapeleka pesa hizo kwenye shule zake za kata na dipensari zake ili kuziboresha taasisi zake na si taasisi za kanisa?? kwani serikali haina dini??
      "Mbowe for Presidency 2015""

    8. #87
      Luiz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd May 2011
      Posts : 342
      Rep Power : 477
      Likes Received
      35
      Likes Given
      0

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Watueleze pesa za sherehe ya miaka 50 ya uhuru zemetoka wap? Wkt kwenye bajet hazpo?

    9. #88
      Buchanan's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 19th May 2009
      Location : Somewhere!
      Posts : 9,398
      Rep Power : 9005
      Likes Received
      853
      Likes Given
      340

      Default

      Quote By kkitabu View Post
      Watumishi wa umma kupandishiwa mishahara lakini bado wanalipwa kwa rates za zamani (hawajarekebishiwa mishahara yao)
      Maoni yako pia ni "kero" maana yako too general! Hao wa "wafanyakazi" ni wa Idara au Taasisi gani? Maslahi yao ni ya lini hadi lini? Be specific plse!

    10. #89
      Buchanan's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 19th May 2009
      Location : Somewhere!
      Posts : 9,398
      Rep Power : 9005
      Likes Received
      853
      Likes Given
      340

      Default

      Quote By Luiz View Post
      Watueleze pesa za sherehe ya miaka 50 ya uhuru zemetoka wap? Wkt kwenye bajet hazpo?
      Swali zuri sana, ubarikiwe!

    11. #90
      Buchanan's Avatar
      Super Moderator Array
      Join Date : 19th May 2009
      Location : Somewhere!
      Posts : 9,398
      Rep Power : 9005
      Likes Received
      853
      Likes Given
      340

      Default

      Quote By Regia Mtema View Post
      Wakuu habari! Nimatumaini yangu kuwa tunaendelea vizuri na majukumu yetu ya kila Siku.

      Nimeamua kuanzisha Uzi huu kwa lengo la kukuza ya kero,maoni,ushauri na chochote toka kwenu ili tuweze kuyasimamia ndani na nje ya Bunge.Kwa kutambua kuwa wanaJF wamesambaa kila mahali,maofisini,mashuleni,mit aani,majumbani na huko kote kuna kero mbalimbali zinazohitaji attention ya Serikali lakini mambo hayaendi na ungpenda kuona suala hilo linafanyiwa Kazi na hivyo unapendekeza Kambi ya Upinzani izibebe na kuzisimamia. Basi tafadhali toa kero,maoni,ushauri au hata mapendekezo yako hapa.

      Tafadhali kero ziwe za kijamii na sio za mtu binafsi.

      Natanguliza Shukrani zangu za dhati kwa Ushirikiano wenu.

      Wenu katika Ujenzi wa Taifa
      Regia Mtema
      Regia Mtema, hili swali ninalokupatia ni muhimu sana, usiache kuliuliza: Kwa nini Vocha za Pembejeo za Ruzuku hazijafika Vijijini mpaka sasa? Vocha hizo zitafika lini? Au fedha za kutengeneza Vocha zimeelekezwa kwenye kugharamia sherehe za uhuru?
      Regia Mtema likes this.

    12. #91
      Tumbili's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th October 2011
      Posts : 12
      Rep Power : 392
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Hi Sister,
      Kwanza nakupa hongera sana kwa wazo zuri ilo, unajua kusema kweli sisi watu wengi wa mjini hususan tunaojiona wasomi huwa hatupeleki kero zetu kwa hao wanaojiita wabunge wanaotuwakirisha, unajua kwanini kwakuwa huwa tunapatwa na hasira sana wakati serikali inavyotoa maamuzi ya kipuuzi wakati hata mtoto wa darasa la tatu asingeamua hivyo, hivyo huwa tunaona kama ni kupoteza tu muda kumtafuta mbunge eti umpe kero yako, so bora kwa njia hii uwenda hata sisi wavivu wa kuwatafuta wabunge njaa wetu nasi tukapata fursa ya kutoa maoni.

      1. Hivi serikali inampango gani na kutekereza ule ushauri wote unaotolewaga na tume zinazoundwa na Bunge?, kuanzia tume ile ya Richmond ya kutaka Hosea wa PCCB afukuzwe kazi mpaka hii tume ya mwisho ya Jairo?, jamani mbona hii serikali inatuchosha kweli ktk kuchangia maendeleo ya nchi hii.

      2. Juzi Muswada wa kuunda sheria ya ukusanyaji wa maoni juu ya katiba mpya, kila ,tu aliupinga kuanzia wanaharakati, maprofesa wasomi kama kina Issa Shivji na wengineo na hata mkuu wa nchi alikiri kuwa unamapungufu lkn aliusaini eti akiogopa kuwa asipousaini wenzake wa chama chake hawatamuelewa, sasa jamani kwani hii nchi ni ya chama furani au ni ya wananchi furani?, mbona hii nchi nyie tuliowapa mtuongoze mnatuchezea ati?.

      3.Ili la tatu naliwekea bold kidogo kwakuwa linataka kichwa kidogo ndio kilisemee kwani linataka uchunguzi wa kina na ikiwezekana mje na hesabu kidogo ndio muweze kuwaonyesha hawa wenzetu kuwa wana uvuvi wa kufikiri ktk kuleta maendeleo ya kweli ktk nchi hii. Reli ya kati ambayo kwa nchi zilizoendelea Reli ndio uti wa mgongo wa usafirishaji imekufa kabisa yaani ni ovyo kabisa, lkn ktk utafiti uliofanywa hivyo karibuni umeonyesha hiyo sekta inahitaji shilingi bilioni 200 tu tena kwa miaka mitatu ili irudi kuwa bora tena kushinda hata zamani na kuweza kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa na kuwasaidia wakulima wote na usafirishaji ya mizigo toka kigoma mpaka Dar na hata kuzifikia nchi jirani, lkn chakushangaza hizo pesa hazipo bali nimeshangaa jana kujenga daraja la kigamboni tena daraja lenyewe litakalokuwa linapita kule mbali Kurasini ambalo kwa wananchi watembea kwamiguu kuja posta hata halitakuwa suruhisho limepewa shilingi bilioni 264 !!!!!, kwa miaka hiyo hiyo mitatu wakati hata ilo daraja likijengwa pantoni lazima zifanye kazi kwakuwa linajengwa mbali na mjini. Sasa hapa zinatakiwa hesabu ili ionekane nini ni bora kati ya Reli ambayo ingesafirisha abiria na mizigo zaidi au ili daraja la kigamboni tena la kisiasa ambalo sidhani kama litakuwa na tija kiivyo kwa Tanzania. Hapa ndugu yangu akili inatakiwa itulie na hesabu zifanyike ndio uweze kueleweka, hapa mtu kama Mnyika au Zitto Kabwe akipewa swali ili alifanyie kazi najua siku akiwa analiuliza patachimbika.

      4.
      Kisha hv haswa NSSF hivi hizi pesa si za kwetu sisi wanachama, hivi wanapata wapi idhini ya kuzitumia vyovyote watakavyo bila ridhaa yetu sisi wenye pesa jamani?.

      Nihayo tu dada
      Regia Mtema likes this.

    13. #92
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 8,352
      Rep Power : 12087
      Likes Received
      5568
      Likes Given
      5435

      Default Jimbo la Ukonga

      Mh.Regia,
      Hoja nyengine ya muhimu ambayo inahitaji kufanyiwa maamuzi haraka ni kuhusu maslahi ya madiwani.
      Madiwani ni watumishi wa umma ambao wako karibu sana na wananchi na ndio msaada mkubwa sana kwenu wabunge.

      Tunataka muishinikize serikali ianze kuwalipa madiwani mishahara kama inavyowalipa watumishi wengine wa umma.

      Kumlipa diwani posho kiasi cha sh.120,000 kwa mwezi ni kumdhalilisha na hii huchangia sana kushindwa kuwatumikia kikamilifu wananchi. Malipo duni kwa madiwani kunafanya nafasi hizo kutowavutia wasomi na hivyo kujikuta madiwani wengi ni wazee, wastafu ama watu wenye elimu za chini katika halmashauri nyingi na hasa za pembezoni hivyo kutoa mwanya kwa wakurugenzi kuwaburuza na wao kutokuwa na uwezo mkubwa wa kufuatilia bajeti na matumizi ya fedha katika miradi inayopangwa na kutekelezwa katika halmashauri zao.

    14. #93
      SOBY's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th September 2011
      Posts : 1,263
      Rep Power : 3237
      Likes Received
      446
      Likes Given
      125

      Default Re: Jimbo la Ukonga

      Quote By Mwita Maranya View Post
      Mh.Regia,
      Hoja nyengine ya muhimu ambayo inahitaji kufanyiwa maamuzi haraka ni kuhusu maslahi ya madiwani.

      Madiwani ni watumishi wa umma ambao wako karibu sana na wananchi na ndio msaada mkubwa sana kwenu wabunge.

      Tunataka muishinikize serikali ianze kuwalipa madiwani mishahara kama inavyowalipa watumishi wa umma wengine mkiwemo nanyi wabunge.

      Kumlipa diwani kiasi cha sh.120,000 kwa mwezi ni kumdhalilisha na hii huchangia sana kushindwa kuwatumikia kikamilifu wananchi.
      Vilevile malipo duni kwa madiwani kunafanya nafasi hizo kutowavutia wasomi na hivyo kujikuta madiwani wengi ni wazee ama watu wenye elimu za chini, kitu kinachotoa mwanya kwa wakurugenzi wengi kuwaburuza na wao kutokuwa na uwezo mkubwa wa kufuatilia bajeti na matumizi ya fedha katika miradi inayopangwa katika halmashauri zao.
      Madiwani wasilipwe!....
      Wabunge walipwe mil. 3 kwa mwezi... bila posho yoyote, posho zote zifutwe. Kuna mambo mengi ya kushughulikiwa na wanasisa wanalipwa fedha nyingi wasizostahili.

    15. #94
      Topical's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 5,050
      Rep Power : 1235
      Likes Received
      853
      Likes Given
      707

      Default Re: Jimbo la Ukonga

      Quote By Mwita Maranya View Post
      Mh.Regia,
      Hoja nyengine ya muhimu ambayo inahitaji kufanyiwa maamuzi haraka ni kuhusu maslahi ya madiwani.

      Madiwani ni watumishi wa umma ambao wako karibu sana na wananchi na ndio msaada mkubwa sana kwenu wabunge.

      Tunataka muishinikize serikali ianze kuwalipa madiwani mishahara kama inavyowalipa watumishi wa umma wengine mkiwemo nanyi wabunge.

      Kumlipa diwani kiasi cha sh.120,000 kwa mwezi ni kumdhalilisha na hii huchangia sana kushindwa kuwatumikia kikamilifu wananchi.
      Vilevile malipo duni kwa madiwani kunafanya nafasi hizo kutowavutia wasomi na hivyo kujikuta madiwani wengi ni wazee ama watu wenye elimu za chini, kitu kinachotoa mwanya kwa wakurugenzi wengi kuwaburuza na wao kutokuwa na uwezo mkubwa wa kufuatilia bajeti na matumizi ya fedha katika miradi inayopangwa katika halmashauri zao.
      source of money??

      Naona maswali mengi ni ya kuongeza matumizi; semeni na namna ya kupata fedha msiwe kama "wafanyakazi wao ni kudai mishahara tu bila kusema pesa itoke wapi??"
      "Mbowe for Presidency 2015""

    16. #95
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 8,352
      Rep Power : 12087
      Likes Received
      5568
      Likes Given
      5435

      Default

      Quote By SOBY View Post
      Madiwani wasilipwe!....
      Wabunge walipwe mil. 3 kwa mwezi... bila posho yoyote, posho zote zifutwe. Kuna mambo mengi ya kushughulikiwa na wanasisa wanalipwa fedha nyingi wasizostahili.
      Kwanza, tunapinga posho kwa watumishi wote wa umma. Walipwe mishahara ambayo itakatwa kodi na kuchangia pato la taifa. As long as wanasiasa nao ni watumishi wa umma suala la kuwalipa halikwepeki. Labda kama unataka nafasi za kisiasa zifutwe, kitu ambacho hakiwezekani.
      Regia Mtema likes this.

    17. #96
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 8,352
      Rep Power : 12087
      Likes Received
      5568
      Likes Given
      5435

      Default

      Quote By Topical View Post
      source of money??

      Naona maswali mengi ni ya kuongeza matumizi; semeni na namna ya kupata fedha msiwe kama "wafanyakazi wao ni kudai mishahara tu bila kusema pesa itoke wapi??"

      Hujui source of money? Nchi hii kwani ina upungufu wa vyanzo vya mapato? Tatizo letu ni collection and allocation tu, pesa ziko nyingi sana.

      Je ushajiuliza hiyo nyongeza ya posho za wabunge imetoka wapi? Nadhani hauko nchini, kwani kama ungekuwepo ungekuwa unafahamu mapendekezo ya tucta ni yepi katika kutaka nyongeza ya mishahara na vyanzo vya kuongeza mapato.


      Hatahivyo najua ulishachagua upande, na hakuna mshangao kusikia kauli kama hii toka kwako.
      Regia Mtema likes this.

    18. #97
      Patriote's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th July 2011
      Posts : 1,439
      Rep Power : 1113
      Likes Received
      767
      Likes Given
      170

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Quote By King Kong III View Post
      Anza na hili la Nyumba za Umma waliojiuzia bei rahisi Vigogo wa serikali na wafanyabiashara wakubwa tena kwa bei rahisi,chonde chonde anza na hilo kwani lina-effect uchumi wa nchi na tumeona viongozi wa serikali wanakaa hotelin na kua na ofisi hoteli coz nyumba za kukaa hawana kwa sababu mafisadi wamejiuzia,hili mliwekee priority ya kwanza tunahitaji nyumba zote zirudishwe serikalini na sio kua za watu binasfi
      Kweli kabisa na inaonekana hakuna ugumu maana tuna mifano ya matukio kadhaa ambayo tumeona serikali baada ya kuingia mikataba na wawekezaji inatamka na kuzirejesha mali hizo kutoka wawekezaji. Mfano mzuri wa hili ni Serikali kupitia Waziri Mkuu Pinda kumnyang'anya mwekezaji ANBEN aka Mkapa, Mkewe pamoja na Yona Mgodi wa Kiwira. Mfano mwingine ni kunyang'anywa kwa UDA kutoka kampuni ya SGL na mifano mingi mingine, Hii inaonyesha hakuna ugumu wowote kwa Serikali kunyang'anya watu waliouziwa nyumba za serikali katika mazingira tatanishi ni suala la dhamira tu.
      Regia Mtema likes this.

    19. #98
      Mwita Maranya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2008
      Location : Ikorongo Game Reserve
      Posts : 8,352
      Rep Power : 12087
      Likes Received
      5568
      Likes Given
      5435

      Default

      Quote By Ngongo View Post
      Ragia

      Bado naendelea ........

      [20] Shirikisho la EAC likataliwe kwa nguvu zote.Nchi za Uganda,Kenya Rwanda na Burundi zote zimeungana dhidi ya Tanzania.Waziri wa Afrika Mashariki ni vyema akaambiwa wazi masuala yafuatayo kamwe yasikubaliwe.

      [A] Masuala ya Ulinzi na Usalama yabaki jukumu la kila nchi.

      [B]Masuala ya Ardhi yasiingizwe katika EAC.

      [C] Soko moja la Utalii Tanzania ikatae kwa nguvu zote.Sote tunajua jinsi Kenya ilivyodanganya ulimwengu kwamba mlima Kilimanjaro na mbuga ya wanyama ya Serengeti ziko kwao.Tanzania ikikubali upumbavu wa soko moja la utalii.

      [D] Pasport itumike kuingia na kutoka kwa wageni wote wa EAC.

      Ngongo,
      Sasahivi bila kuwa na hii mikataba ya soko la pamoja hawa majirani zetu wamedominate soko la ajira ktk utalii na mabenki. Lazima serikali iwe makini sana vinginevyo watanzania wengi wataumia.
      Ngongo and Regia Mtema like this.

    20. #99
      CHEMPO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2011
      Location : A TOWN
      Posts : 369
      Rep Power : 1936
      Likes Received
      58
      Likes Given
      19

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Naomba alhamisi ya kwanza mheshimiwa pinda aeleze juu ya zile 280000/ alizopokea toka kwa jairo..analizungumziaje swala hilo,
      Regia Mtema likes this.

    21. #100
      Babu Ubwete's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 26th January 2008
      Location : Nangulukuru,Newala
      Posts : 148
      Rep Power : 611
      Likes Received
      18
      Likes Given
      18

      Default Re: Tunakusanya Kero ambazo ungependa zisemewe Bungeni na Nje ya Bunge na Viongozi wa CHADEMA

      Jeshi la police lina kero nyingi.
      Ni kwanini mtu anatuhumiwa ushahidi hakuna anawekwa mahabusu na hatoki mpaka atoe hongo.
      Mbona UK au Rwanda askari wanakupeleleza bila ya mtuhumiwa kujua na wakikusanya ushahidi wote ndio wanakukamata.
      Napendekeza Katiba mpya itamke wazi kama askari hana ushahidi basi asimkamate mtuhumiwa kwani ni uonevu na kupoteza muda na mali pia.
      Magerezania na mahabusu watu wengi wamejaa kwa kesi za chuki na kubambikiwa hili naona ni kero kubwa sana. kwani wafungwa wanamaliza pesa ya Jamhuri wakila,wakiugua, wakifa.
      Regia Mtema and jigoku like this.
      If you can imagine it, you can achieve it; if you can dream it, you can become it.

    Page 5 of 24 FirstFirst ... 3456715 ... LastLast

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...