MWENYEKITI wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, amemwelezea Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, kuwa ni mtu anayefaa kuwa Rais wa Tanzania kutokana na msimamo na uwezo aliouonesha katika kila wizara aliyoongoza.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika hitimisho la ziara yake Mbeya Vijijini mjini Mbalizi juzi, Profesa Lipumba alisema uwezo aliouonesha Profesa Mwandosya, unatosha kumfanyia tathmini kwamba ni kiongozi anayefaa kuongoza nchi.
"Katika wagombea wa CCM waliojitokeza mwaka 2005, Profesa Mwandosya walau alionesha kuwa na dalili za kuwa kiongozi mzuri ... huyu ndiye angefaa kuwa Rais wa nchi yetu ni mtu makini," alisema Profesa Lipumba.
Profesa Lipumba mwaka 2005 alikuwa mmoja wa wapinzani waliosimama kugombea urais akitumia tikiti ya CUF na kuangushwa na Jakaya Kikwete, ambaye aligombea kwa tikiti ya CCM.
Aidha, Profesa Lipumba alisisitiza kauli yake ya mara kwa mara, kwamba Watanzania hawajalaaniwa na Mwenyezi Mungu, kwani wana ardhi yenye rutuba ambayo inamea kila aina ya mazao na kwamba iwapo nchi ingekuwa na viongozi wanaojali watu wake, hakuna mwananchi ambaye angekufa na njaa.
"Watanzania hatuna laana ya umasikini kutoka kwa Mwenyezi Mungu ... tukiungana na kuimarisha umoja wa kitaifa, tutajikwamua katika lindi la umasikini lililotugubika kwa zaidi ya miaka 40," alisema.
Profesa Lipumba yuko katika ziara ya siku tano mkoani hapa, ambapo amehutubia mikutano ya hadhara katika kata za Mbeya Vijijini, akisisitiza azma yake ya kuwataka wananchi waachane na CCM akidai kuwa kimekuwa kikiwalaghai wananchi kwa ahadi hewa bila utekelezaji yakinifu.
Ujio wa Mwenyekiti huyo wa CUF umetafsiriwa kuwa ni sehemu ya kukipigia debe chama hicho katika ubunge kutokana na kiti hicho kuwa wazi baada ya aliyekuwa Mbunge wa Jimbo hilo, Bw. Richard Nyaulawa, kufariki dunia Novemba 9 mwaka huu.
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
Lipumba ni mtu ambae tunaweza kusema amewosh kutokana na kuwepo ughaibuni kwa muda mwingi na kuona nchi za wengine zinavyopiga hatua ,hivyo matamanio yake ni kuona tunajikwamua katika hali iliyopo bila ya kuzingatia itikadi za kichama,maoni yake kuwa fulani anafaa basi hilo linatosha kuona yeye ni mtu wa jinsi gani katika kuiendeleza Tz.
Naamini kama akiukwaa Uraisi basi hatosita kuwashirikisha viongozi wengine ambao anawaona ni watu wenye kupenda kuona Mtz anajikwamua katika hali duni ya maisha ya kila siku ambayo ni makali bila ya kujali ni wa Chama gani.Naamini kabisa kuwa Chama chake na wananchi wataridhika na ndivyo siku hizi mambo yanavyokwenda ,inafika sehemu inabidi mushirikiane ili kuijenga nchi yenu na sio kusema sisi tumeshinda ndio sisi tu hakuna mwengine. Wandugu kwa siasa za siku hizi hufiki mbali na ndio tunavyoiona CCM kwa kujiona ni wao tu ,wanavuruga kila kitu japo wenyewe wanajiona wanaleta maendeleo.Na hili si jingine ila ni kiburi cha viongozi wao ,Mtazameni Obama anavyochanganya watu kuna wengine ambao wamo kwenye serikali ya Bush inasemekana huenda wakabakia ,na hii yote ni kipimo hata Wananchi wa huko wanakiona kuwa ni sahihi kwa kumpima yule aliechaguliwa kwamba kazi yake haikuwa na dowa na alikuwa mchapa kazi kwa taifa lake.
Light travels faster than sound. This is why some people appear bright until you hear them speak.
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
By Zakumi
Kwani hao wana ubaya gani Mamii? Yaani swali lako ni sawa na kuuliza hivi Tanzania hakuna chama kingine cha kuongoza zaidi ya CCM?
Unaona sasa, hakuna swali lisilo na jibu. So swali langu halikutaka mfano wa swali linalorandana bali linataka jibu.
Labda nikuonyeshe mfano wa jinsi ya kujibu swali. Kutokana na swali lako hapo ningekujibu kuwa Tanzania kuna vyama vingine zaidi ya CCM ambavyo vinaweza kuongoza. Baadhi vyama hivyo ni NCCR-Mageuzi, CHAUSTA, Demokrasia Makini, DP, UDP, CUF, CHADEMA.
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
By Mama
Hivi CUF hakuna mtu mwingine anaweza kugombea urais zaidi ya Lipumba na Seif?
Inaonyesha kwa sasa hakuna ,kwani kama angekuwepo angeweza kuchukua fomu na kujitokeza pamoja na kufuata taratibu ambazo chama kimejipangia.Siku ukiwacha kuipigia kura CCM basi na wao ndio wataondoka maana wataona jinamizi la nchi hii limeshatokomezwa.
Light travels faster than sound. This is why some people appear bright until you hear them speak.
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
By Mama
Unaona sasa, hakuna swali lisilo na jibu. So swali langu halikutaka mfano wa swali linalorandana bali linataka jibu.
Labda nikuonyeshe mfano wa jinsi ya kujibu swali. Kutokana na swali lako hapo ningekujibu kuwa Tanzania kuna vyama vingine zaidi ya CCM ambavyo vinaweza kuongoza. Baadhi vyama hivyo ni NCCR-Mageuzi, CHAUSTA, Demokrasia Makini, DP, UDP, CUF, CHADEMA.
Jibu ni D. Hayo yote juu ni sahihi.
If we permit feathers to be freely borrowed, who is to tell the peacock from the crow?
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
By Mwiba
Inaonyesha kwa sasa hakuna ,kwani kama angekuwepo angeweza kuchukua fomu na kujitokeza pamoja na kufuata taratibu ambazo chama kimejipangia.Siku ukiwacha kuipigia kura CCM basi na wao ndio wataondoka maana wataona jinamizi la nchi hii limeshatokomezwa.
Hahahahahahah, mbona unaspeculate ndugu, maana wa CCM wananiambia mie CHADEMA, wa CHADEMA wananiambia mie CUF na waCUF wananiambia mimi CCM kwa maana ya kupiga kura. Okay okay, sasa mimi kura yangu iko free na elimu niliyoipata hapa JF kwa muda mchache nilojiunga humu inaniambia nijiunge na chama. Hapa nipo katika kujua mbichi na mbivu.
Kama nimekuelewa vizuri, nikiamua kujiunga na CUF basi si Lipumba wala Seif watakaokuwa wagombea wa kiti cha urais 2010 kwa Tanzania bara na visiwani respectively. Kwa maana hiyo basi, mmejiandaaje na uchaguzi 2010 ? kuna siku chache tu kuingia 2009.
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
By Mama
Hahahahahahah, mbona unaspeculate ndugu, maana wa CCM wananiambia mie CHADEMA, wa CHADEMA wananiambia mie CUF na waCUF wananiambia mimi CCM kwa maana ya kupiga kura. Okay okay, sasa mimi kura yangu iko free na elimu niliyoipata hapa JF kwa muda mchache nilijiunga humu inaniambia nijiunge na chama. Hapa nipo katika kujua mbichi na mbivu.
Kama nimekuelewa vizuri, nikiamua kujiunga na CUF basi si Lipumba wala Seif watakaokuwa wagombea wa kiti cha urais 2010 kwa Tanzania bara na visiwani respectively. Kwa maana hiyo basi, mmejiandaaje na uchaguzi 2010 ? kuna siku chache tu kuingia 2009.
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
By Mama
Hahahahahahah, mbona unaspeculate ndugu, maana wa CCM wananiambia mie CHADEMA, wa CHADEMA wananiambia mie CUF na waCUF wananiambia mimi CCM kwa maana ya kupiga kura. Okay okay, sasa mimi kura yangu iko free na elimu niliyoipata hapa JF kwa muda mchache nilijiunga humu inaniambia nijiunge na chama. Hapa nipo katika kujua mbichi na mbivu.
Kama nimekuelewa vizuri, nikiamua kujiunga na CUF basi si Lipumba wala Seif watakaokuwa wagombea wa kiti cha urais 2010 kwa Tanzania bara na visiwani respectively. Kwa maana hiyo basi, mmejiandaaje na uchaguzi 2010 ? kuna siku chache tu kuingia 2009.
Na mimi nilitaka kusema kama alivyosema Mwiba lakini mdomo ulijaa mchele.
If we permit feathers to be freely borrowed, who is to tell the peacock from the crow?
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
MWENYEKITI wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, amemwelezea Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mark Mwandosya, kuwa ni mtu anayefaa kuwa Rais wa Tanzania kutokana na msimamo na uwezo aliouonesha katika kila wizara aliyoongoza.
Hana lolote huyu anacheza politiki tu.Anamtia kiherehere Mwandosya ili achukue fomu 2010 kisha CCM igawanyike,halafu wao upinzani wapete kiulaini.Wanasiasa bwana!!
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
By Zakumi
Mbona una maswali kama tupo polisi?
Kama hayo ndiyo maswali ya polisi,, basi ningependa kuwa polisi.
Inaelekea CUF mmeshagive-up kwenye masuala ya uongozi wa nchi. Ingekuwa vizuri mkaipa nguvu CHADEMA frontline kwenye mapambano as nyinyi hamna uwezo wa kuhimili.
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
Lipumba ni profesa wa uchumi anayeheshimika na mwenye uwezo wa uongozi na pia urais. Kwa urais wa muungano sio siri Lipumba hapiti kwa sababu CUF bado inahusishwa na udini hivyo itakuwa ngumu kuuzika kwa Kanda ya Kaskazini, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini na Kanda ya Ziwa. Watampigia kura kiongozi muislamu toka chama kingine chochote lakini sio CUF.
Lipumba amemsifu Mwandosya ili kumtukana JK kwa kinyume nyume. Infact its very true Prof. Mwandosya is briliant with brain power. JK japo ni graduate haonyeshi briliance as far as brain power is concerned. Alichosema Lipumba ni kuwa CCM imeacha kuchagua viongozi wenye akili kama Prof. Mwandosya kimoyomoyo 'ona sasa nchi inaendeshwa na wajinga wajinga kama waliopo'
Chedema imeonyesha njia Tarime tayari sasa inaaminiwa lakina haina mtu upande wa presidential. Zitto bado ni mchanga, Dr. Slaa hauziki. Mbowe anakabiliwa na laana ya Wachaga na Wahaya kamwe kutogusa uraisi wa nchi hii. Mtu wa Chadema angekuwa Victor Kimesera lakini hakuwahi kuingia bungeni hivyo hajaweza kuonyesha uwezo wake. The time now is too short kufanya hivyo huku akiwa by passed na age.
Kama wapinzani wako serious wakaungana wakampitisha Cheyo mgombea bara makamu akawa yoyote toka Zanzibar. Cheyo atakomba kura zote Kanda ya Ziwa kura zote Kaskazini na Nyanda za Juu Kusini. Mdengereko ataambulia kura za wajinga wajinga wa Kanda ya Mashariki na Kanda ya Kati Dodoma na Singida ambako ni mabendera fata upepo. Lipumba waziri wa Fedha, Mrema mambo ya Ndani, Zito mambo ya Nje. Lissu Mwanasheria Mkuu kuwachukua baadhi ya wasomi kama Prof. Shiviji waziri wa Sheriia na engine wengi. Amini usiamini 2010 CCM Chali!.
Re: Je lipumba anafikiria Nchi kwanza na Si Chama?
By Mama
Kama hayo ndiyo maswali ya polisi,, basi ningependa kuwa polisi.
Inaelekea CUF mmeshagive-up kwenye masuala ya uongozi wa nchi. Ingekuwa vizuri mkaipa nguvu CHADEMA frontline kwenye mapambano as nyinyi hamna uwezo wa kuhimili.
Mama:
Kwanza elewa ni kuwa nchi ni lazima iwe mbele kuliko vyama. Sifa za mtanzania ni lazima ziwe sifa za mtanzania.
Mwanasiasa anapofanya kazi nzuri itikadi iachwe na apewe sifa zake. Hivyo Limumba alichofanya ni sawa kumsifia Mwandosya na sio big dili.
Mimi si CUF au CHADEMA. Kwangu mimi Siasa is the opium of the masses.
If we permit feathers to be freely borrowed, who is to tell the peacock from the crow?
Follow Us Here