Kampeni ya magazeti mapya ya Karamagi & Co. Dhidi ya JK - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 17th November 2008, 12:58 AM   #1
Kampeni ya magazeti mapya ya Karamagi & Co. Dhidi ya JK
LazaroSMtindi LazaroSMtindi is offline 17th November 2008, 12:58 AM


Kampeni ya kummaliza kisiasa JK, Spika na wabunge kadhaa "wakorofi", imeanzishwa rasmi na Karamagi & Co. (Lowassa na Rostam) kupitia magazeti yao maalum ya AHSUBUHI NJEMA, TAZAMA, NYUNDO, TAIFA NA UMMA. Nia ni kuhakikisha JK anakuwa Rais kwa muhula moja tu na Spika Samuel Sitta na wabunge "wakorofi" hawarudi Bungeni mwaka 2010.

Magazeti hayo ambayo huchapishwa kila siku ya kazi kwa mpangilio, toka Jumatatu hadi Ijumaa, yanabeba ujumbe mahsusi wa ushawishi kwa umma kwamba: JK hana shukrani, kawatosa rafiki zake na kuwakumbatia "maadui"; Membe ni msaliti na anampotosha JK; Lowassa ni kiongozi safi na bora ambaye alionewa tu na Kamati ya Dk. Mwakyembe; bila Lowassa, Rostam, Karamagi, Makamba, Kingunge na wanamtandao wengine, JK hashindi uchaguzi wa 2010; Spika Sitta, Naibu Spika Anne Makinda na wabunge "wakorofi" wa CCM akina Anne Kilango, Mwakyembe, Selelii, Manyanya, Ole Sendeka, Kimaro, Zambi, Nkumba, Mpendazoe, Shellukindo (Bw. & Bi.), Mpesya, Ruth Msafiri na Nyalandu, ni wapinzani wa Serikali ya Awamu ya Nne.

Magazeti haya yanahaririwa na waandishi walewale mamluki: Deodatus Balile, Manyerere Jackton, Charles Charles, Muhingo Rweyemamu, Prince Bagenda na Gama wa gazeti la HOJA. Baadhi ya makala huchangiwa na Salva Rweyemamu na Premy Kibanga wa Ikulu na Mbunge wa Kigoma Peter Serukamba ambaye alibubujikwa machozi na kuugua baada ya Lowassa kujiuzulu. Yalianzishwa kwa mtaji wa sh. milioni 300 alizotoa Karamagi kwa niaba ya Lowassa na Rostam, mara baada ya Lowassa kujiuzulu.

Taarifa ndani ya Chama Tawala zinasema magazeti haya yana baraka zote za Makamba. Ndiyo maana baadhi yake yanahaririwa kwenye ofisi za UVCCM na kwa kutumia kompyuta za jumuiya hiyo.

Kwa mujibu wa kikao cha KALOKIRO kilichokaa Morogoro hivi karibuni, magazeti hayo yatasaidiwa baadaye (karibu na uchaguzi mkuu) na magazeti ya RAI, MTANZANIA na THE AFRICAN. Mwakani, mtandao huo wa mafisadi unaanzisha kituo cha redio na televisheni. Lengo kuu ni kuwamaliza wote hao kisiasa na kumwinua Lowassa agombee Urais mwaka 2010.

Matoleo ya wiki mbili zilizopita za magazeti hayo yote yalikuwa na makala za kumsafisha Lowassa na kudai kuwa Sitta anamhujumu JK, Sitta ana lengo la kuhamia CHADEMA, Kimaro kapora shamba la chuo, Mwakyembe ni mkabila, Membe ni mfuasi wa Malecela, JK hana fadhila mfano wa dereva aliyesaidiwa kwa kusukumwa kutoka kwenye matope lakini akakataa kuwabeba waliomsaidia ili wasichafue gari lake n.k. NGOMA IMEANZA, MAKUBWA ZAIDI YAJA!

LazaroSMtindi
Senior Member
Points: 5,119,422, Level: 100 Points: 5,119,422, Level: 100 Points: 5,119,422, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Tue May 2008
Posts: 79
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Views: 7189
Reply With Quote
  #2  
Old 17th November 2008, 01:59 AM
Mkandara Mkandara is offline
Mkandara Aviator
JF Premium Member
Points: 580,378, Level: 100 Points: 580,378, Level: 100 Points: 580,378, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Thu Mar 2006
Location: T dot
Posts: 7,288
Thanks: 460
Thanked 741 Times in 324 Posts
Rep Power: 80
Mkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the rough
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

LazaroSMtindi,
Quote:
Magazeti hayo ambayo huchapishwa kila siku ya kazi kwa mpangilio, toka Jumatatu hadi Ijumaa, yanabeba ujumbe mahsusi wa ushawishi kwa umma kwamba: JK hana shukrani, kawatosa rafiki zake na kuwakumbatia "maadui"; Membe ni msaliti na anampotosha JK; Lowassa ni kiongozi safi na bora ambaye alionewa tu na Kamati ya Dk. Mwakyembe; bila Lowassa, Rostam, Karamagi, Makamba, Kingunge na wanamtandao wengine, JK hashindi uchaguzi wa 2010; Spika Sitta, Naibu Spika Anne Makinda na wabunge "wakorofi" wa CCM akina Anne Kilango, Mwakyembe, Selelii, Manyanya, Ole Sendeka, Kimaro, Zambi, Nkumba, Mpendazoe, Shellukindo (Bw. & Bi.), Mpesya, Ruth Msafiri na Nyalandu, ni wapinzani wa Serikali ya Awamu ya Nne.
Hivi kuna ukweli ktk maneno uliyo andika mkuu wangu!.. Na kama kuna ukweli mkuu wangu basi haya ndio magazeti ya kufungiwa.. Kilichoandikwa hapa ni kizito kuliko hata Mwanahalisi na kinapotosha wananchi waliowachagua viongozi hawa...
Kama kweli Chiligati ni mtetezi wa haki basi maelezo hayo hapo juu yanatosha kabisa kufungia magazeti haya ama kuwapeleka mahakamani wahusika wote...Nina hakika ushahidi wa madai yao ni mgumu kupatikana kuliko ule wa gazeti la Mwanahalisi..
__________________
Exploration of reality
Reply With Quote
  #3  
Old 17th November 2008, 02:20 AM
Pasco Pasco is offline
Pasco has no status.
JF Premium Member
Points: 800,358, Level: 100 Points: 800,358, Level: 100 Points: 800,358, Level: 100
Activity: 11% Activity: 11% Activity: 11%
 
Join Date: Mon Sep 2008
Posts: 2,107
Thanks: 1,725
Thanked 1,217 Times in 468 Posts
Rep Power: 66
Pasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the roughPasco is a jewel in the rough
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

Kama ni kweli. Politics is really a dirty game.
Pia nakiri kuelekea uchaguzi ndio kipindi cha kuvuna kwa waandishi wa habari sio siri waandishi wanateseka sana kwa kusota juani kwa malipo duni huku wanataaluma wengine kama wanasheria wanapeta sana kwa malipo manono tena kivulini.
2010 ni mwaka wa neema kwa wana habari.
Reply With Quote
  #4  
Old 17th November 2008, 04:20 AM
Nurujamii Nurujamii is offline
Nurujamii is afirm and impartial
JF Senior Expert Member
Points: 154,491, Level: 100 Points: 154,491, Level: 100 Points: 154,491, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Thu Jun 2007
Posts: 437
Thanks: 105
Thanked 20 Times in 12 Posts
Rep Power: 23
Nurujamii will become famous soon enoughNurujamii will become famous soon enoughNurujamii will become famous soon enoughNurujamii will become famous soon enoughNurujamii will become famous soon enoughNurujamii will become famous soon enoughNurujamii will become famous soon enoughNurujamii will become famous soon enough
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

Mwandishi wa JK (Premy) naye yuko? Mbona naona kama ni contradiction?
Reply With Quote
  #5  
Old 17th November 2008, 05:30 AM
Rev. Kishoka's Avatar
Rev. Kishoka Rev. Kishoka is offline
Rev. Kishoka has no status.
JF Premium Member
Points: 1,758,658, Level: 100 Points: 1,758,658, Level: 100 Points: 1,758,658, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
 
Join Date: Mon Mar 2006
Location: USA
Posts: 3,472
Thanks: 965
Thanked 700 Times in 258 Posts
Rep Power: 132
Rev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to all
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

Quote:
View Post
LazaroSMtindi,

Hivi kuna ukweli ktk maneno uliyo andika mkuu wangu!.. Na kama kuna ukweli mkuu wangu basi haya ndio magazeti ya kufungiwa.. Kilichoandikwa hapa ni kizito kuliko hata Mwanahalisi na kinapotosha wananchi waliowachagua viongozi hawa...
Kama kweli Chiligati ni mtetezi wa haki basi maelezo hayo hapo juu yanatosha kabisa kufungia magazeti haya ama kuwapeleka mahakamani wahusika wote...Nina hakika ushahidi wa madai yao ni mgumu kupatikana kuliko ule wa gazeti la Mwanahalisi..
Mkandara,

Penye moshi kuna moto unafukuta. Sasa ukisoma vizuri hiyo listi ya wanaotaka angamizwa, ndio hao ninaowaita CCM Mageuzi ambao wanang'angania kubakia CCM huku wajanja wachache hawawataki.

Hii habari pamoja na kuwa imeletwa kama maoni, ni kitu ambacho nimekiona na kukizungumza upenuni tangu mwezi wa pili kuwa kutakuwa na kampeni kubwa sana ya kuwan'goa wale wote ambao si CCM Mafisadi ndani ya CCM.

Je sasa waelewa kwa nini Mchungaji anakuwa mkali?
__________________
Amani Iwe Nanyi,

Camerlengo

Plu Camerlenghi- Revolutionary Right Reverend Kishoka

"Any existence deprived of freedom is a kind of death." Gen. Michel Aoun

'Who comes to give greeting to the Inkosi-kaas? Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas!"
Reply With Quote
  #6  
Old 17th November 2008, 06:45 AM
WildCard WildCard is offline
WildCard has no status.
JF Premium Member
Points: 118,432, Level: 100 Points: 118,432, Level: 100 Points: 118,432, Level: 100
Activity: 11% Activity: 11% Activity: 11%
 
Join Date: Tue Apr 2008
Posts: 1,482
Thanks: 39
Thanked 323 Times in 191 Posts
Rep Power: 24
WildCard will become famous soon enoughWildCard will become famous soon enoughWildCard will become famous soon enoughWildCard will become famous soon enoughWildCard will become famous soon enoughWildCard will become famous soon enoughWildCard will become famous soon enoughWildCard will become famous soon enough
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

Magazeti yenyewe hayana soko. Hayauziki. Wanajihangaisha kama ni kweli.
Reply With Quote
  #7  
Old 17th November 2008, 07:01 AM
Phillemon Mikael Phillemon Mikael is online now
Phillemon Mikael has no status.
JF Premium Member
Points: 645,130, Level: 100 Points: 645,130, Level: 100 Points: 645,130, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Sun Nov 2006
Location: mwanza,/uk/santa clara
Posts: 3,017
Thanks: 23
Thanked 332 Times in 153 Posts
Rep Power: 30
Phillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enoughPhillemon Mikael will become famous soon enough
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

Quote:
View Post
Magazeti yenyewe hayana soko. Hayauziki. Wanajihangaisha kama ni kweli.

...hizi taarifa hapa tunazo kitambo.....na ukweli ni kuwa haya magazeti ,tv,na redio vyote vilikuwa tayari kwenda hewani miezi sita iliyopita...lakini vilikatishwa na moto wa ajabu uliounguza WASHIRIKA BUILDING.....mkurugenzi walikuwa wamempachika PRINCE BAGENDA...tunahisi kuwa moto uliounguza washirika building ulichomwa na personal intelligence wa kikwete ili kupunguza speed ya haya magazeti...........nadhani wamejipanga upya..

kaka wild hawa watu wana pesa hawategemei mauzo ya issues ili waendelee .....siunaona RAI haliuzi lakini hawatetereki......
__________________
Reply With Quote
  #8  
Old 17th November 2008, 07:08 AM
LazaroSMtindi LazaroSMtindi is offline
LazaroSMtindi has no status.
Senior Member
Points: 5,119,422, Level: 100 Points: 5,119,422, Level: 100 Points: 5,119,422, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue May 2008
Posts: 79
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 2022
LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

WanaJF Mkandara, Pasco,Nurujamii, Rev. Kishoka na WildCat nimewasoma, nimewaelewa. Naomba mniamini, nilichoandika ni kweli kweli tupu. Kama mnakumbuka, nilishawadokeza kuwa nafanya kazi mojawapo ya kampuni kubwa ya RA. Nikigundulika ni mimi nachangia hapa JF, nitakuwa marehemu kesho ahsubuhi. Hawa watu wana mtandao wa nguvu sana, wana pesa na wana sauti kubwa kwenye vyombo vya usalama. Ni mtandao uleule uliompa ushindi JK. Wachache ni waadilifu, wamebaki na JK. Wengi wamefuata fedha za EPA, Richmond, Import Support - kikao kimoja tu cha KALOKIRO unalipwa 1m/= au 2m/=, utaacha kuunga mkono? Mwenyekiti wa operesheni nzima, kama nilivyosema awali, ni mzee wa Sumbawanga. Salva Rweyemamu hana record ya uzalendo, ni mamluki tu aliyeajiliwa na Richmond kwa msaada wa RA. Leo yuko Ikulu, atabadilika? Premy haelewi kuwa marafiki wa jana wa JK, ndo maadui wake leo. She is naive, anafuata mkumbo tu bila kuwa na bigger picture, bila kujua kuwa anamwumiza bwana mkubwa! Wahariri wa RAI wanajua hilo maana ndo wanaopokea "vigongo" kutoka kwa akina Salva. Niishie hapo maana naandika huku naangaza macho nisijeonekana Internet Cafe ahsubuhi nikichonga taarifa za JF.

Last edited by Invisible; 17th November 2008 at 10:21 AM.. Reason: Rechecking Personal details
Reply With Quote
  #9  
Old 17th November 2008, 07:14 AM
Dark City's Avatar
Dark City Dark City is offline
Dark City The last of the Thomaso's
JF Premium Member
Points: 188,394, Level: 100 Points: 188,394, Level: 100 Points: 188,394, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Sat Oct 2008
Location: Roaming
Posts: 1,441
Thanks: 1,168
Thanked 438 Times in 246 Posts
Rep Power: 24
Dark City will become famous soon enoughDark City will become famous soon enoughDark City will become famous soon enoughDark City will become famous soon enoughDark City will become famous soon enoughDark City will become famous soon enoughDark City will become famous soon enoughDark City will become famous soon enough
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

Quote:
View Post

...hizi taarifa hapa tunazo kitambo.....na ukweli ni kuwa haya magazeti ,tv,na redio vyote vilikuwa tayari kwenda hewani miezi sita iliyopita...lakini vilikatishwa na moto wa ajabu uliounguza WASHIRIKA BUILDING.....mkurugenzi walikuwa wamempachika PRINCE BAGENDA...tunahisi kuwa moto uliounguza washirika building ulichomwa na personal intelligence wa kikwete ili kupunguza speed ya haya magazeti...........nadhani wamejipanga upya..

kaka wild hawa watu wana pesa hawategemei mauzo ya issues ili waendelee .....siunaona RAI haliuzi lakini hawatetereki......
Nakushukuru sana kwa hii taarifa muhimu (it's an eye opener). Sikuwa na taarifa kabisa kuhusu hili (nadhani tuko wengi tu)! Pamoja na kwamba haoy magazeti hayauziki, ila ni muhimu sana kwa majukwaa ya ukombozi kama JF na magazeti yenye uzalendo kuweka hili suala wazi ili Watz wajue hili jambo. Hilo ndilo litakuwa hitimisho la njama zao! Kwani wataandika tu, hata TV itarusha matangazo hewani lakini mwisho wa siku wataambulia hukumu ya umma. Tuwasaidie Watanzania wenzetu wajue hii njama ya hatari sana. Sioni kitu gani EL anaweza kutufanyia akiwa raisi. Itakuwa ni sherehe (party) ya mbwa mwitu wenye njaa kuwararua mbuzi (WaTz) wasio na hatia (poor naive Tzn)! We should not (by hooks and crooks) let this happen.
Reply With Quote
  #10  
Old 17th November 2008, 07:24 AM
LazaroSMtindi LazaroSMtindi is offline
LazaroSMtindi has no status.
Senior Member
Points: 5,119,422, Level: 100 Points: 5,119,422, Level: 100 Points: 5,119,422, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue May 2008
Posts: 79
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 2022
LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!LazaroSMtindi is one of most respected JF members!
Default Re: Kampeni ya magazeti mapya ya karamagi & co. Dhidi ya jk

Mkuu umepiga ndipo! Umelonga kiuelewa. Umenikuna. Hawa watu hawahitaji fedha za mauzo za magazeti yao hayo ya udaku ambayo story zake nyingi ni za ubabaishaji tu. Wao wanauza message na soko lao kubwa ni Dar es Salaam. Fedha ya mauzo ni kwa ajili ya mamluki wao akina Prince Bagenda, Manyerere, Balile, na Muhingo. Magazeti haya yana kazi maalumu. Kwa mfano, gazeti la Nyundo lilipewa kazi moja tu kufanya: kumbomoa huyu kijana Nape kwa kumzulia kila jambo: si mtoto wa Nnauye, mpenda madaraka, mpuuzi, umri mkubwa utadhani Nchimbi ni teenager n.k. Kazi imefanyika, sasa gazeti hilo limesimama kidogo kusubiri assignment nyingine. TAIFA kazi kubwa ni kuwabamiza mastaa wa Mbeya na Kilimanjaro: Kimaro, Mwandosya, Kilango, Mwakyembe n.k. ndiyo maana magazeti mengi ya TAIFA yanauzwa Dar es Salaam, Mbeya na Kilimanjaro. Mkuchika aliingizwa mkenge na Salva na RA kuifungia MwanaHalisi. Walimpa shinikizo kubwa na kumpelekea ujumbe wa siri kuwa kabla ya kuwa Waziri alikuwa mfadhili wa MwanaHalisi. Of course huo ni uongo mkubwa, blackmail tupu. Lakini imefanyakazi.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
dhidi, jk, kampeni, karamagi, magazeti, mapya


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Lazima tuwekane sawa kuhusu UKIMWI Shy JF Doctor 139 18th June 2009 02:00 PM
Karamagi na wanasheria wake watupiana mpira kuhusu tuhuma za ufisadi. Lawson Jukwaa la Siasa 4 12th November 2007 10:12 AM
Kampeni dhidi ya Mkapa asishinde Tuzo ya uongozi bora Mwafrika wa Kike Celebrities Forum 127 23rd October 2007 12:54 PM
Karamagi anasafiri na mihuri yetu? Bubu Ataka Kusema Jukwaa la Siasa 13 20th August 2007 09:19 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 12:00 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com