Kampeni ya kummaliza kisiasa JK, Spika na wabunge kadhaa "wakorofi", imeanzishwa rasmi na Karamagi & Co. (Lowassa na Rostam) kupitia magazeti yao maalum ya AHSUBUHI NJEMA, TAZAMA, NYUNDO, TAIFA NA UMMA. Nia ni kuhakikisha JK anakuwa Rais kwa muhula moja tu na Spika Samuel Sitta na wabunge "wakorofi" hawarudi Bungeni mwaka 2010.
Magazeti hayo ambayo huchapishwa kila siku ya kazi kwa mpangilio, toka Jumatatu hadi Ijumaa, yanabeba ujumbe mahsusi wa ushawishi kwa umma kwamba: JK hana shukrani, kawatosa rafiki zake na kuwakumbatia "maadui"; Membe ni msaliti na anampotosha JK; Lowassa ni kiongozi safi na bora ambaye alionewa tu na Kamati ya Dk. Mwakyembe; bila Lowassa, Rostam, Karamagi, Makamba, Kingunge na wanamtandao wengine, JK hashindi uchaguzi wa 2010; Spika Sitta, Naibu Spika Anne Makinda na wabunge "wakorofi" wa CCM akina Anne Kilango, Mwakyembe, Selelii, Manyanya, Ole Sendeka, Kimaro, Zambi, Nkumba, Mpendazoe, Shellukindo (Bw. & Bi.), Mpesya, Ruth Msafiri na Nyalandu, ni wapinzani wa Serikali ya Awamu ya Nne.
Magazeti haya yanahaririwa na waandishi walewale mamluki: Deodatus Balile, Manyerere Jackton, Charles Charles, Muhingo Rweyemamu, Prince Bagenda na Gama wa gazeti la HOJA. Baadhi ya makala huchangiwa na Salva Rweyemamu na Premy Kibanga wa Ikulu na Mbunge wa Kigoma Peter Serukamba ambaye alibubujikwa machozi na kuugua baada ya Lowassa kujiuzulu. Yalianzishwa kwa mtaji wa sh. milioni 300 alizotoa Karamagi kwa niaba ya Lowassa na Rostam, mara baada ya Lowassa kujiuzulu.
Taarifa ndani ya Chama Tawala zinasema magazeti haya yana baraka zote za Makamba. Ndiyo maana baadhi yake yanahaririwa kwenye ofisi za UVCCM na kwa kutumia kompyuta za jumuiya hiyo.
Kwa mujibu wa kikao cha KALOKIRO kilichokaa Morogoro hivi karibuni, magazeti hayo yatasaidiwa baadaye (karibu na uchaguzi mkuu) na magazeti ya RAI, MTANZANIA na THE AFRICAN. Mwakani, mtandao huo wa mafisadi unaanzisha kituo cha redio na televisheni. Lengo kuu ni kuwamaliza wote hao kisiasa na kumwinua Lowassa agombee Urais mwaka 2010.
Matoleo ya wiki mbili zilizopita za magazeti hayo yote yalikuwa na makala za kumsafisha Lowassa na kudai kuwa Sitta anamhujumu JK, Sitta ana lengo la kuhamia CHADEMA, Kimaro kapora shamba la chuo, Mwakyembe ni mkabila, Membe ni mfuasi wa Malecela, JK hana fadhila mfano wa dereva aliyesaidiwa kwa kusukumwa kutoka kwenye matope lakini akakataa kuwabeba waliomsaidia ili wasichafue gari lake n.k. NGOMA IMEANZA, MAKUBWA ZAIDI YAJA!
Hivi wakuu si kuna wakati hapa JF tulisema Pastor Laizer aliyesimamia mapokezi ya Lowassa jimboni kwake baada ya kujiuzulu kwamba ni mwenda wazimu alipomsifia mkuu huyu? Halafu tukasema kwamba wananchi waliompokea huko jimboni kwake ni wenda wazimu! What happened to all that? Ooh my God, only in Tanzania.
Yaani kiongozi aliyetufikisha taifa kulipa dola laki moja na nusu kwa siku kwa ajili ya umeme ambao haukuwepo, na kuwaacha wananchi wakiishi kwenye giza, huku zile hela zikienda mifukoni mwake na washikaji zake, eti ni bora sana na ni mchapa kazi hodari?
Pleeeeeease somebody take me to another planet! Maana hapa on earth labda I am lost! Damn it!
Mkuu FMES inasikitisha. Ila wanasema penye udhia penyeza rupia. Niliambiwa kuwa wana-Apolo walisaidia sana katika mapokezi yale. Michangi mikubwa ya fedha hubadilisha akili za watu.
Hayo yaliyotajwa ndiyo yaliyomharibia Lowasa nadhani kuna mtu ana hamu tufyatue dark side of Lowasa humu ndani.
1.Mashangingi ya wabunge yaliyonunuliwa kuna tuhuma za kifisadi za hali ya juu ambazo pengine yeye mwenyewe ndiye aweza eleza alivyopata lile benzi la kutembelea baada ya manunuzi yale ya magari ya wabunge.
2.Fedha za maafa na mafuriko wakati ule zilifisadiwa.Labda atueleze aliwezaje kujenga jumba lile alilopangisha ubalozi wa Afrika ya kusini kwa hela ipi ambayo aliipata wapi kipindi kile?
3.Kufutwa kwa kibali cha ujenzi wa mnazi mmoja kulitokana na ugomvi wake na Kitwana Kondo aliyekuwa meya wa Jiji wakati huo wakati Lowasa akiwa waziri alihisi mwenzie kapata pengine bila kumshirikisha?!!! Kitwana au kumgawia?!!! Akaamua kufuta vile vya mwenzie Kitwana Kondo akabakiza vya kwake ambavyo navyo vilijaa harufu za kifisadi tu ambavyo viliuzwa kwa bei ya chini cha juu kikaenda kwa ....Utajaza.Vingine wakagawiana kiswahiba kifisadi.
Mabati yalibomolewa na wananchi si kwa amri ya Lowasa bali Christopher
Mtikila ndiye alihamasisha machinga kuvamia eneo hilo ambalo lina mnara wa uhuru na kubeba mabati na kutimuka.
Kusema nyota yake iling`ara kwa ajili ya hayo nina wasiwasi.
Kuhusu Richmond alihusika kabisa.Kwa nini kama suala lile aliliona linamzidi uwezo na lina utata kwa nini hakumpelekea faili makamu wa Raisi au Raisi mwenyewe alifanyie uamuzi.Kwa nini yeye alitoa "go ahead" Mradi fisadi wa Richmond uendelee wakati akijua kabisa ulikuwa una utata kama alivyojieleza bungeni? Kwani wakubwa zake Makamu wa Raisi na Raisi walikuwa wamekufa si walikuwepo kwa nini hakuwapelekea wao walifanyie maamuzi kama si ulaji rushwa?
Richmond siyo porojo wala kampeni za kumchafua.Tunasubiri tu. ngoja suala la EPA lishughulikiwe.Tutamshukia kama mwewe asidhani tumelisahau kawekwa kiporo.Tutamshukia tu labda akimbie nchi au akajifiche porini kwenye mashimo lakini hata akijificha kwenye mashimo tutamfuata huko huko kumfukua kama Saddam Hussein alivyofukuliwa.
Kikwete ana udhaifu wake mkubwa tu lakini kwa ufisadi kumlinganisha na Lowasa kwaweza kuwa ni kumwonea.Hajafikia kiwango hicho.Nyerere alimkataa Lowasa sababu ya ufisadi na Kilichomponza hata Kikwete akataliwe na Nyerere ilikuwa ni urafiki wake na Lowasa.Lowasa ndiye alimponza kipindi kile Kikwete.Nyerere alijua kuwa ukiwa rafiki na fisadi lazima na wewe una matatizo au utapata matatizo.
Kipindi cha utawala wa Kikwete Lowasa katoa mchango mkubwa wa kuharibu crediblity ya Raisi Kikwete kuliko waziri mwingine yeyote.Na ametoa mchango mkubwa sana kumfanya Kikwete anuke kifisadi mbele ya umma.
.
Nakubaliana sana na wewe Mkuu. Kwa kuongezea tu, UVCCM ndio waliopendekeza JMK na EL wachukue form za kugombea URais 1995. Na wao (UVCCM) ndio waliahidi kusaidia ushindi wao. Ikumbukwe pia kwamba, mwaka ule walijitokeza wagombea wengi kuliko wakati wowote wa chaguzi za ndani (CCM) siku za nyuma.
Wasiwasi wangu mkubwa kuhusiana na EL ni ubinafsi wake. Kuna issue moja ambayo hadi leo siielewi, inashangaza na inauma sana. Nayo ni ubomoaji wa jengo kubwa (apartments) karibu na nyumba yake aliyopangisha kwa ubalozi wa SA. Jengo lile lilibomolewa kwa kisingizio kuwa lilikosa hati zilizohitajika kulijenga (building permits). Na hata hati hizo zilipotolewa na wahusika, zilikataliwa na baadhi wa watendaji wa Municipal ya Kinondoni walichukuliwa hatua kutokana na kutoa hati hizo. Inasemekana Jengo lilibomolewa kwasababu kuwepo kwake kulizuia hewa nzuri kufikia nyumba yake (Ubalozi wa SA). Naamini kuwa kama jengo lile lingekuwa la mtu mwingine, lisingebomolewa. Na hata kama halikuwa na uhalali wa kuwepo, ingekuwa busara zaidi kutoza "fine" kubwa kwa wamiliki ili iwe fundisho, kuliko kuacha masalia yake yasiyopendeza kabisa.
Re: Kampeni ya magazeti mapya ya Karamagi & Co. Dhidi ya JK
Phillemon Mikael mkuu, kuna kitu kimoja umekisema katika mchango wako ambacho nadhani wanajanvi hawakichukulii seriously ingawa ni muhimu sana kwa utawala wa Jakaya; nacho ni role ya SANGOMA katika maamuzi. Ni kweli usiopingika kuwa waganga wa kienyeji wanainfluence sana na maamuzi ya muungwana kwahiyo kama alivyosema Mikael siyo ripoti ya Mwakyembe peke yake iliyomfanya Jakaya amtose Lowassa bali ni ushauri wa waganga wake wa kienyeji kuwa huyu bwana alikuwa anampiku mwaka 2010. Hata wakati wa mchakato pale DODOMA mwaka 2005 Jakaya alikuwaanatembea na SANGOMA wake kwenye Cruiser lake.; wengine anaimport toka West Africa!! sasa kwa imani potofu namna hiyo uongozi utaleta maendeleo au maaalbino wataachwa kuchinjwa kweli??
Phillemon Mikael mkuu, kuna kitu kimoja umekisema katika mchango wako ambacho nadhani wanajanvi hawakichukulii seriously ingawa ni muhimu sana kwa utawala wa Jakaya; nacho ni role ya SANGOMA katika maamuzi. Ni kweli usiopingika kuwa waganga wa kienyeji wanainfluence sana na maamuzi ya muungwana kwahiyo kama alivyosema Mikael siyo ripoti ya Mwakyembe peke yake iliyomfanya Jakaya amtose Lowassa bali ni ushauri wa waganga wake wa kienyeji kuwa huyu bwana alikuwa anampiku mwaka 2010. Hata wakati wa mchakato pale DODOMA mwaka 2005 Jakaya alikuwaanatembea na SANGOMA wake kwenye Cruiser lake.; wengine anaimport toka West Africa!! sasa kwa imani potofu namna hiyo uongozi utaleta maendeleo au maaalbino wataachwa kuchinjwa kweli??
...............duh!!!!!!!!!!!!.................... JUJUMAN ndani ya IKULU?????
__________________ Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo
Phillemon Mikael mkuu, kuna kitu kimoja umekisema katika mchango wako ambacho nadhani wanajanvi hawakichukulii seriously ingawa ni muhimu sana kwa utawala wa Jakaya; nacho ni role ya SANGOMA katika maamuzi. Ni kweli usiopingika kuwa waganga wa kienyeji wanainfluence sana na maamuzi ya muungwana kwahiyo kama alivyosema Mikael siyo ripoti ya Mwakyembe peke yake iliyomfanya Jakaya amtose Lowassa bali ni ushauri wa waganga wake wa kienyeji kuwa huyu bwana alikuwa anampiku mwaka 2010. Hata wakati wa mchakato pale DODOMA mwaka 2005 Jakaya alikuwaanatembea na SANGOMA wake kwenye Cruiser lake.; wengine anaimport toka West Africa!! sasa kwa imani potofu namna hiyo uongozi utaleta maendeleo au maaalbino wataachwa kuchinjwa kweli??
Ndio maana muungwana huwa anapagawa wakati mwingine ggggrrrrrrrrrrrrrrrrrrhhhh! Kweli Nyerere aliona mengi, aliweza kutueleza machache tu. Mengine tutasoma wenyewe kwa nyakati. Nilifikiri Muungwana kaacha masangomaism!
Mkuu Bulesi,
Hivi hayo Masangoma hayapokei 'rushwa' tuyape hoja zetu za mafisadi na mustakabali wa taifa?
Kampeni ya kummaliza kisiasa JK, Spika na wabunge kadhaa "wakorofi", imeanzishwa rasmi na Karamagi & Co. (Lowassa na Rostam) kupitia magazeti yao maalum ya AHSUBUHI NJEMA, TAZAMA, NYUNDO, TAIFA NA UMMA. Nia ni kuhakikisha JK anakuwa Rais kwa muhula moja tu na Spika Samuel Sitta na wabunge "wakorofi" hawarudi Bungeni mwaka 2010.
Magazeti hayo ambayo huchapishwa kila siku ya kazi kwa mpangilio, toka Jumatatu hadi Ijumaa, yanabeba ujumbe mahsusi wa ushawishi kwa umma kwamba: JK hana shukrani, kawatosa rafiki zake na kuwakumbatia "maadui"; Membe ni msaliti na anampotosha JK; Lowassa ni kiongozi safi na bora ambaye alionewa tu na Kamati ya Dk. Mwakyembe; bila Lowassa, Rostam, Karamagi, Makamba, Kingunge na wanamtandao wengine, JK hashindi uchaguzi wa 2010; Spika Sitta, Naibu Spika Anne Makinda na wabunge "wakorofi" wa CCM akina Anne Kilango, Mwakyembe, Selelii, Manyanya, Ole Sendeka, Kimaro, Zambi, Nkumba, Mpendazoe, Shellukindo (Bw. & Bi.), Mpesya, Ruth Msafiri na Nyalandu, ni wapinzani wa Serikali ya Awamu ya Nne.
Magazeti haya yanahaririwa na waandishi walewale mamluki: Deodatus Balile, Manyerere Jackton, Charles Charles, Muhingo Rweyemamu, Prince Bagenda na Gama wa gazeti la HOJA. Baadhi ya makala huchangiwa na Salva Rweyemamu na Premy Kibanga wa Ikulu na Mbunge wa Kigoma Peter Serukamba ambaye alibubujikwa machozi na kuugua baada ya Lowassa kujiuzulu. Yalianzishwa kwa mtaji wa sh. milioni 300 alizotoa Karamagi kwa niaba ya Lowassa na Rostam, mara baada ya Lowassa kujiuzulu.
Taarifa ndani ya Chama Tawala zinasema magazeti haya yana baraka zote za Makamba. Ndiyo maana baadhi yake yanahaririwa kwenye ofisi za UVCCM na kwa kutumia kompyuta za jumuiya hiyo.
Kwa mujibu wa kikao cha KALOKIRO kilichokaa Morogoro hivi karibuni, magazeti hayo yatasaidiwa baadaye (karibu na uchaguzi mkuu) na magazeti ya RAI, MTANZANIA na THE AFRICAN. Mwakani, mtandao huo wa mafisadi unaanzisha kituo cha redio na televisheni. Lengo kuu ni kuwamaliza wote hao kisiasa na kumwinua Lowassa agombee Urais mwaka 2010.
Matoleo ya wiki mbili zilizopita za magazeti hayo yote yalikuwa na makala za kumsafisha Lowassa na kudai kuwa Sitta anamhujumu JK, Sitta ana lengo la kuhamia CHADEMA, Kimaro kapora shamba la chuo, Mwakyembe ni mkabila, Membe ni mfuasi wa Malecela, JK hana fadhila mfano wa dereva aliyesaidiwa kwa kusukumwa kutoka kwenye matope lakini akakataa kuwabeba waliomsaidia ili wasichafue gari lake n.k. NGOMA IMEANZA, MAKUBWA ZAIDI YAJA!
Nimesoma, hakuna hoja hapa!
Bye bye thread
__________________
'Tough times never last but tough people do' Dr. Robert Schuller
Mod na hii ya Sauti Huru ingewekwa humu kwani ina uhusiano mkubwa kwa kuwa nalo ni miongoni mwa magazeti yaliyoanzishwa mahsusi kuwatetea watu ambao jamii imeamini na serikali imeamini na kuwachukulia hatua. Hii ni hatari, lazima tukatae kulishwa sumu hii mbaya na tena bila hoja. Kuna gazeti moja limethubutu hata kusema kwamba VITA YA UFISADI NI VITA KATI YA WACHAGA NA WAHAYA na bado Mkuchika na jamaa zake wa Maelezo hawajachukua hatua kwa habari/makala inayolenga kuchochea mgawanyiko wa kikabila. HII NI HATARI KUBWA NA SIJUI hao UWT wanafanya kazi gani.
Lakini habari ya Sauti Huru sijui kama ni habari ama makala
Re: Kampeni ya magazeti mapya ya Karamagi & Co. Dhidi ya JK
Nimesoma kwa mshangao sifa anazotupiwa Lowasa,kabla ya kumpamba mtu kwa sifa ni bora uangalie uadilifu wake kwanza Mh: huyu hana tofauti na Mkapa kwa waliyowatendea wananchi wa Tanzania si watu wa kusifiwa hawa. Mkapa ni mung'unye ameharibikia ukubwani ameanza wizi ktk hatua za mwisho za kipindi cha pili cha uraisi wake. Lowasa nimebahatika kumjua kidogo ktk miaka ya mwanzoni mwa 80 nilipokuwa Arusha wakati huo nchi inanuka hamna bidhaa,chakula ,nguo nk naye alikuwa katibu wa CCM mkoa by then alishaharibika kwa ulafi. alipopewa uwaziri ndipo alipofungulia mbwa akasema mtanikoma, kiasi hayati mwl Nyerere akamwambia hafai kuwa raisi mtoto mdogo mwenye tamaa ya mali, bahati mbaya na huyo mtoto mkubwa alietupa ndio akawa MZINGA MBOVU unalipuka ovyo kwa tamaa na ufisadi. kwakifupi hawa jamaa ni ma********* tu hawastahili sifayeyote. wamejivua heshima ya kusifiwa kitambo.
Re: Kampeni ya magazeti mapya ya Karamagi & Co. Dhidi ya JK
Quote:
Nimesoma kwa mshangao sifa anazotupiwa Lowasa,kabla ya kumpamba mtu kwa sifa ni bora uangalie uadilifu wake kwanza Mh: huyu hana tofauti na Mkapa kwa waliyowatendea wananchi wa Tanzania si watu wa kusifiwa hawa. Mkapa ni mung'unye ameharibikia ukubwani ameanza wizi ktk hatua za mwisho za kipindi cha pili cha uraisi wake. Lowasa nimebahatika kumjua kidogo ktk miaka ya mwanzoni mwa 80 nilipokuwa Arusha wakati huo nchi inanuka hamna bidhaa,chakula ,nguo nk naye alikuwa katibu wa CCM mkoa by then alishaharibika kwa ulafi. alipopewa uwaziri ndipo alipofungulia mbwa akasema mtanikoma, kiasi hayati mwl Nyerere akamwambia hafai kuwa raisi mtoto mdogo mwenye tamaa ya mali, bahati mbaya na huyo mtoto mkubwa alietupa ndio akawa MZINGA MBOVU unalipuka ovyo kwa tamaa na ufisadi. kwakifupi hawa jamaa ni ma********* tu hawastahili sifayeyote. wamejivua heshima ya kusifiwa kitambo.
- Mkuu Jujuman, saafi sana maneno mazito sana haya.
Ndio maana muungwana huwa anapagawa wakati mwingine ggggrrrrrrrrrrrrrrrrrrhhhh! Kweli Nyerere aliona mengi, aliweza kutueleza machache tu. Mengine tutasoma wenyewe kwa nyakati. Nilifikiri Muungwana kaacha masangomaism!
Mkuu Bulesi,
Hivi hayo Masangoma hayapokei 'rushwa' tuyape hoja zetu za mafisadi na mustakabali wa taifa?
Hakuna JARS zozote hizo ni imani potofu na zimepitwa na wakati harafu ni stori za vijiweni,kwanza humu duniani hakuna sangoma lolote sangoma ni wewe mwenyewe ama rafiki yako.