TiGo Maps
    Show/Hide This

    Topic: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

    Report Post
    Page 3 of 4 FirstFirst 1234 LastLast
    Results 61 to 90 of 111
    1. #1
      mluga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th October 2010
      Posts : 460
      Rep Power : 477
      Likes Received
      124
      Likes Given
      129

      Default Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Kikwete agoma kusaini waraka

      Posho za Wabunge

      Mwandishi Wetu


      Rais Jakaya Kikwete

      Wabunge wageukana, sasa 'kidole na jicho'

      RAIS wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, anatajwa kugoma kutia saini waraka wa mapendekezo ya viwango vipya vya ongezeko la posho za “kukaa kitako” bungeni zinazolipwa kwa wabunge kutoka Sh. 70,000 za sasa hadi Sh. 200,000, Raia Mwema limeelezwa.

      Habari zinasema, wakati Kikwete akigoma kusaini waraka huo wa posho, zipo taarifa kuwa malipo ya posho mpya yamekwishafanyika kinyemela kwa matarajio kuwa angesaini.

      Hata hivyo, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila, amekana kufanya malipo hayo akisema kiasi cha ziada kilicholipwa kwa wabunge ni stahili isiyohusiana na nyongeza ya posho.

      Kwa upande wake, Kikwete amegoma kutia saini waraka husika kwa mujibu wa mamlaka yake. Taratibu zilizopo ni kwamba, Rais hufikishiwa mapendekezo hayo na yeye anaweza kuidhinisha kwa kutia saini ikiwa ni kibali kinachowezesha Bunge kwenda Wizara ya Fedha kuchukua fedha hizo tayari kwa shughuli iliyokusudiwa.

      Mbali na kibali hicho cha Rais kuwezesha Bunge kupewa fungu la fedha husika kutoka Hazina (Wizara ya Fedha) lakini pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) hufanya ukaguzi wa hesabu husika kwa kutumia masharti yaliyopo kwenye waraka unaotiwa saini na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

      Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya uhakika vya habari, Rais Kikwete alipelekewa waraka huo mapema na ilitarajiwa angeweza kutia saini haraka; lakini imekuwa kinyume, kielezwa kuwa ‘kelele’ za makundi mbalimbali ya jamii zimechangia kumfanya asite kutia saini kama ilivyotarajiwa.

      “Huo waraka wa mapendekezo ni kweli umefikishwa kwa Rais kwa muda sasa lakini hajatia saini, ingawa anakubali posho za sasa haziwatoshi wabunge lakini pia anatambua kuwa hali ya uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja si nzuri, na kwa hiyo, ni vema hili suala kulishughulikia kwa umakini mkubwa”, kilieleza chanzo chetu cha habari kutoka Ikulu.

      Wakati hali ikiwa hivyo kwa upande wa Rais, taarifa za Bunge zinaeleza kuwa mchakato wa nyongeza za posho ulipitia hatua karibu zote katika Bunge.

      Hatua hizo ni pamoja na kujadiliwa na kupitishwa na Tume ya Bunge inayoundwa na makamishna ambao ni wabunge pia, Kamati ya Uongozi ya Bunge inayoundwa na wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge na mwisho, wabunge wote kupewa muhtasari husika na kujadili na kisha, kukubali au kutokubali taarifa husika.

      Kwa hiyo, Raia Mwema, kupitia vyanzo vyake vya habari, limejiridhisha kuwa Bunge lilifikia uamuzi wa kuongeza posho hizo na wabunge wa kambi ya upinzani na chama tawala kwa ujumla wao, walikubali uamuzi huo.

      Inaelezwa kuwa mbunge pekee mwenye msimamo mkali dhidi ya kuchukua posho ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, ambaye hata hizi posho za zamani amegoma kuzichukua kwa muda mrefu sasa.

      Hata hivyo, wabunge wenzake katika chama chake wamekuwa wakichukua posho hizo na hata zile za semina mbalimbali kwa wabunge, ikiwamo semina iliyofadhiliwa na fedha kutoka Wizara ya Nishati na Madini, na kugharimu kibarua cha aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, David Jairo.

      Mbali na uamuzi huo wa Rais kutosaini ili kuidhinisha posho mpya, kumekuwa na madai kwamba katika Bunge lililopita wabunge walilipwa posho hizo kwa viwango vipya kabla ya kuidhinishwa na kwamba kwa sasa, wanaweza kutakiwa kuzirejesha kwa njia ya makato yenye utaratibu maalumu.

      Kutokana na madai hayo, Raia Mwema iliwasiliana na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila ambaye alikiri wabunge kulipwa kiwango fulani cha ziada cha fedha lakini akikanusha kuwa si nyongeza ya posho kama ilivyoelezwa.

      “Si kweli wabunge wamelipwa hizo posho mpya. Hakuna aliyelipwa. Mimi nitapata wapi fedha za kuwalipa....kutoka kwenye fungu gani? Kwa sababu hadi sasa hakuna kibali chochote kilichotolewa kutoka mamlaka husika kwamba posho zimeongezwa, haya mambo yanazo taratibu zake za kisheria....si utashi wangu kusema posho imepanda na kwa hiyo niwalipe wabunge.”

      “Kwa hiyo, uongozi wa Bunge hauwezi kufanya uamuzi wowote nje ya taratibu za kisheria zilizopo. Hata kama hiyo posho ingekuwa imepanda, kuna maswali mengi ya kujiuliza na kupata majibu. Je, viwango vipya vinapaswa kuanza kulipwa wakati gani, je, ni kuanzia mikutano iliyopita ya Bunge? Je, ni kuanzia mwanzo wa Bunge hili au kuanzia mikutano ijayo ya Bunge?” alisema Kashilila.

      Katika hatua nyingine, Raia Mwema imebaini kuwapo kwa mawasiliano yasiyo rasmi kati ya Rais na baadhi ya wabunge, wakimshauri kutoongeza posho hizo kwa sababu kufanya hivyo ni kuzidisha pengo kati ya wenye nacho na wasio nacho katika jamii ya Watanzania, wengi wao wakiwa masikini.

      “Wapo ambao wameamua kumpa ushauri Rais kwamba si wakati muafaka kutia saini waraka wa nyongeza ya posho mpya. Wanadhani kwamba kuna sababu nyingi za msingi ambazo zinahusisha hali za Watanzania wa kawaida, wakiwamo watumishi wa Serikali na kubwa zaidi, hali ya uchumi haijatulia kiasi hicho,” alieleza mmoja wa wasaidizi wa Rais Kikwete.

      Kutokana na ushauri huo kwake, Rais Kikwete ananukuliwa akiwajibu kwa kusema; “Mimi ndiyo mwamuzi wa mwisho.”

      Lakini wakati hali ikiwa hivyo, yapo mapendekezo mengine mbadala miongoni mwa wabunge na baadhi ya viongozi waandamizi serikalini ambao hata hivyo, wamekataa majina yao yasiandikwe gazetini kwa sasa.

      Wabunge na maofisa hao wanapendekeza kuwa posho ya ‘kukaa kitako’ bungeni si lazima kuongezwa, lakini malipo kwa wabunge yanayostahili nyongeza ni malipo ya posho ya kujikimu wakiwa nje ya kituo cha kazi (per diem).

      Kwa sasa wabunge hulipwa posho ya kujikimu Sh. 80,000 kwa siku. Posho nyingine ni mafuta Sh. 50,000 kila mwezi na posho ya ‘kukaa kitako’ (sitting allowance) bungeni Sh.70,000.

      Wabunge na maofisa hao wanashauri nyongeza ya per diem kwa kuzingatia kuwa gharama za maisha zimepanda, ikiwamo hoteli ambazo wengi huishi wakiwa katika shughuli za Bunge Dodoma, ingawa wengine wanazo nyumba zao binafsi.

      “Nadhani kama ni ongezeko la per diem sawa kwa sababu gharama za hoteli na masuala mengine zimepanda mno. Hata kama wakilipa Sh.300,000 si tatizo kwa hadhi ya mbunge ambaye huwa na nyaraka mbalimbali na kwa hiyo, ni lazima aishi sehemu ya uhakika.

      “Lakini kulipana posho ya kukaa kitako tu kufikia 200,000 ni ngumu sana kueleweka kwa wananchi wetu. Ni kuzidi kujichonganisha na wananchi,” alisema mbunge mmoja katika mazunguzo yake na gazeti hili.

      Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwa Rais Jakaya Kikwete kwa mara ya mwisho aliwahi kusaini waraka wa nyongeza ya posho kwa wabunge Oktoba, mwaka jana, kupitia waraka namba CAB111/338/01/83.

      Waraka huo unatambulika kama waraka wa Rais kuhusu masharti ya mbunge. Hata wakati mjadala wa kususia au kutosusia posho za wabunge ulipoibuka bungeni, hususan Bunge la bajeti mwaka huu, utetezi ambao hata hivyo ni dhaifu, ulieleza kwamba, kuchukua posho ni sehemu ya masharti ya mbunge.


    2. #61
      Njowepo's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 26th February 2008
      Location : Santiago
      Posts : 5,693
      Rep Power : 21659
      Likes Received
      490
      Likes Given
      193

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Hajasign kwa sababu ifuatayo
      1.Bse bunge limekomaa na watu wake wa karibu akina Jairo na Luhanjo so anataka kuwakomoa kuwa nae anaweza
      or
      2.Yuko bize na maandalizi ya sherehe za uhuru
      or
      3.Anatafuta umaarufu hasa baada ya ngumi za usoni za Lowasa kule NEC
      WB Tanzania lead economist Jacques Morisset said the GDP doubled in 10 years, but it has failed to produce any significant decline in poverty levels.

    3. #62
      shizukan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th January 2011
      Posts : 779
      Rep Power : 592
      Likes Received
      370
      Likes Given
      156

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Kiukweli alishasaini (kwa mujibu wa Mh. Mama). Sasa baada ya kuona migomo ya waalimu na hekaheka za madiwani ndio wameamua kwa pamoja kuchana pepa ya kwanza na kuweka nyingine ambayo hijasainiwa ili kutuzuga. Nilimsikia Mh. Mama akisema kwa mdomo wake ndani ya runinga yangu ya HITACHI (made in Japan sio China, kwa hiyo iko gado) kuwa mchakato ulishamalizika na Rais amesaini baada ya kuona inafaa. Sasa hizi ni juhudi za kukinusuru chama na wala msidhani ni kwa kutujali wananchi.

      Kwa upande mwingine hao maafisa waliotoa maoni ni majambazi wakubwa. Kusema sitingi alawansi kupandishwa hadi 200,000 ni mbaya hapo hapo kusema per diem ifike 300,000 maana yake ni nini? Ni sawa na kusema HATUTAWABAKA bali TUTAWAINGILIA KWA NGUVU. Nawashangaa ndugu zangu mliokuwa wepesi wa kumpongeza Mh. Dokta as if mna hakika kutosaini ni kwa manufaa yetu.

      Sasa hawa waandishi wetu feki sijui wanafanya kazi gani! Kafulila anasema hazijasainiwa na hazijalipwa, Mh. Mama anasema zimesainiwa na zilishaanza kulipwa, mbona hakuna mwandishi aliyemhoji Kafulila kuhusu kauli ya mama?
      'the World is a COMEDY to those who think. A TRAGEDY for those who feel'

    4. #63
      MpigaKelele's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 6th November 2010
      Posts : 1,039
      Rep Power : 674
      Likes Received
      204
      Likes Given
      408

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By jmushi1 View Post
      Anataka kuchukua credit kutoka kwa wananchi kuwa anajali matumizi.
      Anafikiria namna ya kuwa 'Neutral' katika hili lakini haiwezekani maana ama asaini au asisaini, vinginevyo waraka ufutwe.
      Curiosity.........
      A well tight cornered rat can bite a Cat...

    5. #64
      chitambikwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Location : KAISHO
      Posts : 1,600
      Rep Power : 701
      Likes Received
      190
      Likes Given
      92

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By mluga View Post
      Kikwete agoma kusaini waraka

      Posho za Wabunge

      Mwandishi Wetu


      Rais Jakaya Kikwete

      Wabunge wageukana, sasa 'kidole na jicho'

      RAIS wa Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, anatajwa kugoma kutia saini waraka wa mapendekezo ya viwango vipya vya ongezeko la posho za “kukaa kitako” bungeni zinazolipwa kwa wabunge kutoka Sh. 70,000 za sasa hadi Sh. 200,000, Raia Mwema limeelezwa.

      Habari zinasema, wakati Kikwete akigoma kusaini waraka huo wa posho, zipo taarifa kuwa malipo ya posho mpya yamekwishafanyika kinyemela kwa matarajio kuwa angesaini.

      Hata hivyo, Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila, amekana kufanya malipo hayo akisema kiasi cha ziada kilicholipwa kwa wabunge ni stahili isiyohusiana na nyongeza ya posho.

      Kwa upande wake, Kikwete amegoma kutia saini waraka husika kwa mujibu wa mamlaka yake. Taratibu zilizopo ni kwamba, Rais hufikishiwa mapendekezo hayo na yeye anaweza kuidhinisha kwa kutia saini ikiwa ni kibali kinachowezesha Bunge kwenda Wizara ya Fedha kuchukua fedha hizo tayari kwa shughuli iliyokusudiwa.

      Mbali na kibali hicho cha Rais kuwezesha Bunge kupewa fungu la fedha husika kutoka Hazina (Wizara ya Fedha) lakini pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) hufanya ukaguzi wa hesabu husika kwa kutumia masharti yaliyopo kwenye waraka unaotiwa saini na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

      Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya uhakika vya habari, Rais Kikwete alipelekewa waraka huo mapema na ilitarajiwa angeweza kutia saini haraka; lakini imekuwa kinyume, kielezwa kuwa ‘kelele’ za makundi mbalimbali ya jamii zimechangia kumfanya asite kutia saini kama ilivyotarajiwa.

      “Huo waraka wa mapendekezo ni kweli umefikishwa kwa Rais kwa muda sasa lakini hajatia saini, ingawa anakubali posho za sasa haziwatoshi wabunge lakini pia anatambua kuwa hali ya uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja si nzuri, na kwa hiyo, ni vema hili suala kulishughulikia kwa umakini mkubwa”, kilieleza chanzo chetu cha habari kutoka Ikulu.

      Wakati hali ikiwa hivyo kwa upande wa Rais, taarifa za Bunge zinaeleza kuwa mchakato wa nyongeza za posho ulipitia hatua karibu zote katika Bunge.

      Hatua hizo ni pamoja na kujadiliwa na kupitishwa na Tume ya Bunge inayoundwa na makamishna ambao ni wabunge pia, Kamati ya Uongozi ya Bunge inayoundwa na wenyeviti wa kamati za kudumu za Bunge na mwisho, wabunge wote kupewa muhtasari husika na kujadili na kisha, kukubali au kutokubali taarifa husika.

      Kwa hiyo, Raia Mwema, kupitia vyanzo vyake vya habari, limejiridhisha kuwa Bunge lilifikia uamuzi wa kuongeza posho hizo na wabunge wa kambi ya upinzani na chama tawala kwa ujumla wao, walikubali uamuzi huo.

      Inaelezwa kuwa mbunge pekee mwenye msimamo mkali dhidi ya kuchukua posho ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, ambaye hata hizi posho za zamani amegoma kuzichukua kwa muda mrefu sasa.

      Hata hivyo, wabunge wenzake katika chama chake wamekuwa wakichukua posho hizo na hata zile za semina mbalimbali kwa wabunge, ikiwamo semina iliyofadhiliwa na fedha kutoka Wizara ya Nishati na Madini, na kugharimu kibarua cha aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, David Jairo.

      Mbali na uamuzi huo wa Rais kutosaini ili kuidhinisha posho mpya, kumekuwa na madai kwamba katika Bunge lililopita wabunge walilipwa posho hizo kwa viwango vipya kabla ya kuidhinishwa na kwamba kwa sasa, wanaweza kutakiwa kuzirejesha kwa njia ya makato yenye utaratibu maalumu.

      Kutokana na madai hayo, Raia Mwema iliwasiliana na Katibu wa Bunge, Dk. Thomas Kashilila ambaye alikiri wabunge kulipwa kiwango fulani cha ziada cha fedha lakini akikanusha kuwa si nyongeza ya posho kama ilivyoelezwa.

      “Si kweli wabunge wamelipwa hizo posho mpya. Hakuna aliyelipwa. Mimi nitapata wapi fedha za kuwalipa....kutoka kwenye fungu gani? Kwa sababu hadi sasa hakuna kibali chochote kilichotolewa kutoka mamlaka husika kwamba posho zimeongezwa, haya mambo yanazo taratibu zake za kisheria....si utashi wangu kusema posho imepanda na kwa hiyo niwalipe wabunge.”

      “Kwa hiyo, uongozi wa Bunge hauwezi kufanya uamuzi wowote nje ya taratibu za kisheria zilizopo. Hata kama hiyo posho ingekuwa imepanda, kuna maswali mengi ya kujiuliza na kupata majibu. Je, viwango vipya vinapaswa kuanza kulipwa wakati gani, je, ni kuanzia mikutano iliyopita ya Bunge? Je, ni kuanzia mwanzo wa Bunge hili au kuanzia mikutano ijayo ya Bunge?” alisema Kashilila.

      Katika hatua nyingine, Raia Mwema imebaini kuwapo kwa mawasiliano yasiyo rasmi kati ya Rais na baadhi ya wabunge, wakimshauri kutoongeza posho hizo kwa sababu kufanya hivyo ni kuzidisha pengo kati ya wenye nacho na wasio nacho katika jamii ya Watanzania, wengi wao wakiwa masikini.

      “Wapo ambao wameamua kumpa ushauri Rais kwamba si wakati muafaka kutia saini waraka wa nyongeza ya posho mpya. Wanadhani kwamba kuna sababu nyingi za msingi ambazo zinahusisha hali za Watanzania wa kawaida, wakiwamo watumishi wa Serikali na kubwa zaidi, hali ya uchumi haijatulia kiasi hicho,” alieleza mmoja wa wasaidizi wa Rais Kikwete.

      Kutokana na ushauri huo kwake, Rais Kikwete ananukuliwa akiwajibu kwa kusema; “Mimi ndiyo mwamuzi wa mwisho.”

      Lakini wakati hali ikiwa hivyo, yapo mapendekezo mengine mbadala miongoni mwa wabunge na baadhi ya viongozi waandamizi serikalini ambao hata hivyo, wamekataa majina yao yasiandikwe gazetini kwa sasa.

      Wabunge na maofisa hao wanapendekeza kuwa posho ya ‘kukaa kitako’ bungeni si lazima kuongezwa, lakini malipo kwa wabunge yanayostahili nyongeza ni malipo ya posho ya kujikimu wakiwa nje ya kituo cha kazi (per diem).

      Kwa sasa wabunge hulipwa posho ya kujikimu Sh. 80,000 kwa siku. Posho nyingine ni mafuta Sh. 50,000 kila mwezi na posho ya ‘kukaa kitako’ (sitting allowance) bungeni Sh.70,000.

      Wabunge na maofisa hao wanashauri nyongeza ya per diem kwa kuzingatia kuwa gharama za maisha zimepanda, ikiwamo hoteli ambazo wengi huishi wakiwa katika shughuli za Bunge Dodoma, ingawa wengine wanazo nyumba zao binafsi.

      “Nadhani kama ni ongezeko la per diem sawa kwa sababu gharama za hoteli na masuala mengine zimepanda mno. Hata kama wakilipa Sh.300,000 si tatizo kwa hadhi ya mbunge ambaye huwa na nyaraka mbalimbali na kwa hiyo, ni lazima aishi sehemu ya uhakika.

      “Lakini kulipana posho ya kukaa kitako tu kufikia 200,000 ni ngumu sana kueleweka kwa wananchi wetu. Ni kuzidi kujichonganisha na wananchi,” alisema mbunge mmoja katika mazunguzo yake na gazeti hili.

      Uchunguzi wa Raia Mwema umebaini kuwa Rais Jakaya Kikwete kwa mara ya mwisho aliwahi kusaini waraka wa nyongeza ya posho kwa wabunge Oktoba, mwaka jana, kupitia waraka namba CAB111/338/01/83.

      Waraka huo unatambulika kama waraka wa Rais kuhusu masharti ya mbunge. Hata wakati mjadala wa kususia au kutosusia posho za wabunge ulipoibuka bungeni, hususan Bunge la bajeti mwaka huu, utetezi ambao hata hivyo ni dhaifu, ulieleza kwamba, kuchukua posho ni sehemu ya masharti ya mbunge.
      Yalikuwa makubaliano ya kuleta muswada upitishwe haraka bila hata kujua kilichomo alfu waongezewe posho. Sasa mwenzao anawageuka maana kuna vitu amehisi wanaccm watamuelewaje
      IT IS TO THOSE WITHOUT TEETH GOD GIVES MEAT

    6. #65
      shizukan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th January 2011
      Posts : 779
      Rep Power : 592
      Likes Received
      370
      Likes Given
      156

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By PIPIJOJO View Post
      Wabunge wa chadema akiwemo Zitto hawakukataa posho bali walitaka ziende majimboni kwao suala ambalo ni sawa na kutoa posho mfuko wa kulia kwenda mfuko wa kushoto. Hoja ya zitto haikuzingatia kwamba huko majimboni kuna mfuko wa fedha wa maendeleo wa jimbo ambao pia unamilikiwa na mbunge. kama fedha za posho zitapelekwa majimboni ni nani mwenye uhakika kwamba zitatumika kwa maendeleo.
      Kuna ukibaraka mwingine ili uufanye inalazimu uwe hayawani. Hivi unataka kuniambia kuwa CHADEMA wanasikilizwa saaana na serikali kiasi wakisema kitu kinafanyika? Huu unaoonesha hapa ni upungufu wa ubongo kwenye kichwa chako, pumba zisizo na mfano. Don't be pathetic, CCM wamekosea ktk hili na wala usitafute namna ya kuwasingizia wengine. Shame on you Kibaraka. (una mawazo ya Faiza Foxxy)
      'the World is a COMEDY to those who think. A TRAGEDY for those who feel'

    7. #66
      sulphadoxine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Location : Iraq
      Posts : 1,588
      Rep Power : 699
      Likes Received
      309
      Likes Given
      819

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By Puppy View Post
      >> Katibu Wa Bunge (Hakuna Ongezeko La Posho)

      >> Spika Wa Bunge (ongezeko La Posho Liko Tokea 8/11)

      >> Rais (Agoma Kusaini Waraka.)

      Nimuamini nani kati ya hawa? Nitegemee nini kutoka kwa hawa? Na Je ni kipi kinafuat?
      wote sio wakuwaamini.
      CHUKI NA UADUI NI MATOKEO YA UPUMBAVU:

    8. #67
      Paul J's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th October 2010
      Posts : 133
      Rep Power : 409
      Likes Received
      26
      Likes Given
      0

      Default

      Na hiki ni kipimo cha uongozi-Government is a well organised system, na katika hilo tulitegemea information follow ziwe well organised vilevile. Lakini kwa kuwa hali halisi inatuonyesha kinyume na hivyo ni dhahiri kabisa kuwa Tanzania inaongozwa na wasanii watupu na si viongozi! Katibu wa Bunge-Hamna nyongeza, Spika Nyongeza imeanza kulipwa tangia 8/11, Rais kakataa kusaini waraka wa Nyongeza! Is that the way the government operates?
      Nina mashaka na miaka minne ijayo, kila mtu serikali atakuwa na lake la kusema!

    9. #68
      Nyati's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th March 2009
      Posts : 376
      Rep Power : 543
      Likes Received
      42
      Likes Given
      12

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By YEYE View Post
      Af hawa watu mbona wanataka kutufanya Watanganyika hatuna akili?! Mbona Spika amesema zimeshaanza kulipwa toka tar 8/11?!
      Hivi kwa Avatar hii unafikiri watu watafikiri akili inatumika kweli....... TAFAKARI
      I am not the same person today as I was 10, 20, or 30 years ago, for I have welcomed life's changes on my heart, face, and mind.

    10. #69
      Mtumishi Wetu's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 12th October 2010
      Location : Arusha
      Posts : 1,744
      Rep Power : 732
      Likes Received
      289
      Likes Given
      2501

      Default Re: SERIKALI INA DALILI ZA KUFILISIKA?

      Quote By MAFILILI View Post
      Asante sana kwa kumkubali JK ni Rais halali wa TZ. Mwambie Dr. Slaa akubali matokeo
      Mkuu MAFILILI bado tuu umelala usingizi hata mchana kweupe, kwani nani kamesema huyo mheshimiwa Kikwete sio Rais wa nchi hii?????????? Usilale amka kumekucha sisi tunamgoja huyo atakayewekwa na maghamba,s kugombea urais tumkikimishe!!!!!!!!


    11. #70
      King Kong III's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Posts : 5,500
      Rep Power : 1484
      Likes Received
      1136
      Likes Given
      82

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Mmmh hapa kuna dalili ya kumsafisha mzee wa kaya kwa tunavyomjua huyu alivyo kigeugeu kashasign mda mrefu tu

    12. #71
      KIBONGOMKUTI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Posts : 450
      Rep Power : 470
      Likes Received
      92
      Likes Given
      216

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Kama ni kweli wabunge wa upinzani nao hususani CDM wamechukua hizo posho, napata hisia za siasa za ubabaishaji uliotukuka. Nimefuraishwa na TAMKO/Waraka/Msimamo wa CDM kuhusu upingaji wa hizo posho.Nimesoma kwenye sread ya mleta mada inaelekea hata watetezi wetu wetu nao wamevuta posho isipokuwa Mzito Kabwela. Imefikia wakati tuache siasa za kinafiki, kama ni kweli CDM hawajachukua hizo posho wakanushe hadharani ili wajitofautishe na wana Magamba. Vinginevyo wakisubiri mpaka taarifa za JK kugoma kusaini waraka wa kuongeza posho CDM itapigwa bao. Magamba ni wepesi kwenda vijijini na kuanza kuwapumbuza Watanganyika kwa kuwalaghai kuwa Sirikali yao inawajali na watadandia hoja kuwa Magamba wamegomea posho.


    13. #72
      tindo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th September 2011
      Posts : 98
      Rep Power : 353
      Likes Received
      26
      Likes Given
      1

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      wabunge lazima waanze kujilipa maana makubaliano yalikuwa wapitishe mswaada wa katiba nao watapandishiwa posho. Sasa cdm & nccr hawakushiriki hvyo deal imeharibika. Rais anasikia aibu kusaini, wakati wabunge wanataka chao, ndio hapo sasa lugha gongana zinatokea, katibu wa bunge lake, spika lake nk.
      Ame likes this.

    14. #73
      mtoto mpole's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd March 2010
      Posts : 162
      Rep Power : 446
      Likes Received
      35
      Likes Given
      44

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      yaan namuombea Mungu akatae maana akikubali hili Laana iliyopo mbele yake ni kubwa mno.

    15. #74
      Mtumishi Wetu's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 12th October 2010
      Location : Arusha
      Posts : 1,744
      Rep Power : 732
      Likes Received
      289
      Likes Given
      2501

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By tindo View Post
      wabunge lazima waanze kujilipa maana makubaliano yalikuwa wapitishe mswaada wa katiba nao watapandishiwa posho. Sasa cdm & nccr hawakushiriki hvyo deal imeharibika. Rais anasikia aibu kusaini, wakati wabunge wanataka chao, ndio hapo sasa lugha gongana zinatokea, katibu wa bunge lake, spika lake nk.
      Eheee kumbe ni kunawishana mikono, hapo sasa ngoja tuone kama atachomoa dili lishaiva????????


    16. #75
      OLESAIDIMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2011
      Posts : 624
      Rep Power : 449
      Likes Received
      183
      Likes Given
      311

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Every nail on a coffin has its meaning
      Hegemony is unlikely ever to be complete (A. Gramsci)

    17. Ame is offline
      Ame
      #76
      Ame's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2011
      Location : Global Citizen
      Posts : 918
      Rep Power : 546
      Likes Received
      337
      Likes Given
      1336

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By tindo View Post
      wabunge lazima waanze kujilipa maana makubaliano yalikuwa wapitishe mswaada wa katiba nao watapandishiwa posho. Sasa cdm & nccr hawakushiriki hvyo deal imeharibika. Rais anasikia aibu kusaini, wakati wabunge wanataka chao, ndio hapo sasa lugha gongana zinatokea, katibu wa bunge lake, spika lake nk.
      Mambo ya Tanzania ukiyafuatilia unaweza kuwa mwendawazimu kwani nadhani viongozi wa Tanzania wanaongozwa na nguvu za giza ndiyo maana mambo ya aibu wao wanayafanya hadharani bila aibu!

    18. #77
      OLESAIDIMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2011
      Posts : 624
      Rep Power : 449
      Likes Received
      183
      Likes Given
      311

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Kugoma = Kukataa ......???
      Hegemony is unlikely ever to be complete (A. Gramsci)

    19. #78
      ndyoko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 4,079
      Rep Power : 1567
      Likes Received
      977
      Likes Given
      1549

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      hongera yenu mnaoona mna rais nchi hii.
      "Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania si mahali pa kutangazia neno la Mungu kinafiki ili kuhalalisha wizi dhidi ya Watanzania"

    20. #79
      OLESAIDIMU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2011
      Posts : 624
      Rep Power : 449
      Likes Received
      183
      Likes Given
      311

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Kugoma kusaini = kukataa........????
      Hegemony is unlikely ever to be complete (A. Gramsci)

    21. #80
      Fasta fasta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th February 2011
      Posts : 410
      Rep Power : 448
      Likes Received
      73
      Likes Given
      151

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By MpigaKelele View Post
      Anafikiria namna ya kuwa 'Neutral' katika hili lakini haiwezekani maana ama asaini au asisaini, vinginevyo waraka ufutwe.
      Ukiona hivyo ujue anapima upepo unakoelekea, kama wamesha anza kulipwa inamaana wameshahalalisha. Angekuwa makini wasingelipwa bila kupewa habari. Kikwete anajua kinachoendelea na anajua kelele hazimtishi. Kumbukeni aliekuwa mstari wa mbele kutea huu upuuzi ni tysoni na Lukuvu na ndio washauri wake wakuu. Mimi ninasema Tanzania inahitaji Politic Technic sio hizi bla bla za ccm.
      MpigaKelele likes this.

    22. #81
      MpigaKura's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 25th January 2007
      Posts : 524
      Rep Power : 682
      Likes Received
      89
      Likes Given
      82

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      NGOMA INOGILE...

      Kwahiyo kikinuka kabisa itabidi wabunge wakwatwe mishahara kulipia posho walizochukua kutoka wizara ya fedha bila idhini ya JK?

      Wanasema life is expensive in dodoma, vp kuhusu mlalahoi/mpiga kura anayeshindia chini ya dola moja kwa siku?

      Hivi tunajifunza nini hapo?
      3:186: NA BILA SHAKA YOYOTE MTASIKIA UDHIA MWINGIKUTOKANA NA WALIOPEWA KITABU KABLA YENU

    23. #82
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 2,603
      Rep Power : 1077
      Likes Received
      483
      Likes Given
      363

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      yaani walikuwa wanaelewa kabisa kuwa ni lazima Raisi ataisaini,kwani wameshazoea kuwa Raisi husaini kila kitu wanacho mpatia bila kuhoji,hii ni hatari sana kwa mstakari wa nchi yetu,kudhani kuwa kila Raisi husaini bila shaka lolote ndio maana wakalipana kabla ya mkuu kusaini
      haya yetu macho
      together we stand

    24. #83
      Matola's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 5,872
      Rep Power : 10399
      Likes Received
      2479
      Likes Given
      1794

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Ukitaka kuamini kwamba misomi ya Tanzania ni hasara tupu, nilitegemea wangefanya maandamano makubwa hasa hawa wa UDOM kuomba nyongeza ya pesa za kujikimu maana maisha ya Dodoma ni ghali mno, na reference ni bunge.
      Ame likes this.

    25. #84
      Huburya Charles's Avatar
      Member Array
      Join Date : 7th December 2011
      Posts : 33
      Rep Power : 330
      Likes Received
      2
      Likes Given
      13

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Tunamuomba saana Mh.saana Kikwete aione hali ya wananchi wake asikubali kusaini huo waraka kwani kama ni kupanda kwa maisha yamepanda kwa watu wote sio kwa wabunge tuu.

    26. #85
      Marytina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th January 2011
      Posts : 4,671
      Rep Power : 1337
      Likes Received
      818
      Likes Given
      248

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By KIBONGOMKUTI View Post
      Kama ni kweli wabunge wa upinzani nao hususani CDM wamechukua hizo posho, napata hisia za siasa za ubabaishaji uliotukuka. Nimefuraishwa na TAMKO/Waraka/Msimamo wa CDM kuhusu upingaji wa hizo posho.Nimesoma kwenye sread ya mleta mada inaelekea hata watetezi wetu wetu nao wamevuta posho isipokuwa Mzito Kabwela. Imefikia wakati tuache siasa za kinafiki, kama ni kweli CDM hawajachukua hizo posho wakanushe hadharani ili wajitofautishe na wana Magamba. Vinginevyo wakisubiri mpaka taarifa za JK kugoma kusaini waraka wa kuongeza posho CDM itapigwa bao. Magamba ni wepesi kwenda vijijini na kuanza kuwapumbuza Watanganyika kwa kuwalaghai kuwa Sirikali yao inawajali na watadandia hoja kuwa Magamba wamegomea posho.
      utakuwa outdated!!!!
      posho hapewi mkononi bali huingizwa kwenye akaunti ya mbunge husika together with hela zingine kama mshahara nk.
      hapo kila akaunti ya mmbunge imeorodheshwa na taka ustake hela huingizwa

    27. #86
      njiwa's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 16th April 2009
      Location : ax^2+bx+c=0
      Posts : 2,922
      Rep Power : 1638
      Likes Received
      446
      Likes Given
      407

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By Feedback View Post
      I do not trust my president any more.
      i know the only man you trust ni Lowassa! sometimes Just give a guy a credit akifanya a right thing
      Ame likes this.
      (Kama vipi .... nipotezee )
      Njiwa"ᵀᴴᴱ'ᴼᴿᴵᴳᴵᴻᴬᴸ✯

    28. #87
      mjombo's's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 21st October 2011
      Location : D'SALAAM
      Posts : 205
      Rep Power : 372
      Likes Received
      24
      Likes Given
      17

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      trust no one in this government, bcoz no lie wl live 4eva, hilo ni chenga la macho tu ili kuavoid mass upraisal
      Ame likes this.

    29. #88
      Matola's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 5,872
      Rep Power : 10399
      Likes Received
      2479
      Likes Given
      1794

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By njiwa View Post


      i know the only man you trust ni Lowassa! sometimes Just give a guy a credit akifanya a right thing
      Apewe credit kwa lipi? kwani kugoma maana yake ni kukataa? akieleweshwa si ataweka saini? atoe tamko hadharani kwamba amekataa hapo mimi bila hiyana nitampongeza.

    30. #89
      Bruker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th November 2010
      Location : Morogoro - Tanzania
      Posts : 808
      Rep Power : 519
      Likes Received
      103
      Likes Given
      16

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      sasa akigoma kusaini wenzake kule katika chama watamuelewa?maana muswada wa katiba alikubali CDM wanahoja na anasaini kwa sababu tu wenzake katika chama wasimuelewe vibaya
      "Be the Window through which many young will see their future"

    31. #90
      harakat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th July 2011
      Posts : 587
      Rep Power : 464
      Likes Received
      92
      Likes Given
      1

      Default Re: Kikwete agoma kusaini waraka kuhusu wabunge kujipandishia posho

      Quote By BAK View Post
      Rais kasusa Mkuu!!!! Hatukuwahi kumsikia Mwalimu hata siku moja anafanya usanii kama huu eti wa kususa!!!! Sasa Rais unasusa unamsusia nani!!!? Nchi yetu kweli imepata kiongozi!!!!

      Kama watafanya hivyo itabidi waongeze mishahara ya wafanyakazi Nchi nzima kwani
      mishahara ni midogo mno kama kwenye TGTS MWENYE DEGREE ANAanza na 330,000
      ambayo ndio mbunge atachukua kwa siku

    Page 3 of 4 FirstFirst 1234 LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 62
      Last Post: 7th December 2011, 21:53
    2. JK agoma kusaini sheria mpya
      By Ng'wanza Madaso in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 5
      Last Post: 16th April 2010, 11:08
    3. News Alert: JK Agoma Kusaini Sheria Mpya!
      By Buchanan in forum Jukwaa la Sheria (The Law Forum)
      Replies: 3
      Last Post: 15th April 2010, 10:32
    4. JK agoma kusaini sheria mpya
      By MziziMkavu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 2
      Last Post: 15th April 2010, 08:12

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...