TiGo Maps
    Show/Hide This

    Topic: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 30 of 52
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 26,634
      Rep Power : 22539
      Likes Received
      8482
      Likes Given
      4308

      Default Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Utangulizi


      Nilipata wazo la kuandika utenzi huu* kuanzia mwaka jana. Nilikuwa nimekusudia kuandika Utenzi wenye beti 1000 kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania. Lakini katika uvivu wangu na mihangaiko ya dunia nimejikuta nimeishia kwenye hizi beti 100 za utenzi huu wa Tanzania. Maadhimisho ya miaka hamsini ya Uhuru ni maadhimisho siyo ya mipaka ya nchi, siyo ya jina na kwa hakika kabisa siyo maadhimisho ya kupita kwa muda. Ni maadhimisho – naamini- ya utu wetu.

      Kwamba, katika miaka hamsini iliyopita tumeweza kufanya kile ambacho hakikuwahi kufanywa kwa miaka 2000 iliyopita katika eneo letu. Yaani, kuwaunganisha watu watu wetu wote, chini ya mipaka ile ile, wakiwa huru na haki sawa. Katika utenzi huu nimeelezea jinsi eneo letu lilivyojulikana kama Azania katika masimulizi ya Wagiriki au kama Zenji kwa Waarabu na wakati mwingine kuhusiana na majina ya maeneo ya Kushi na Nubia katika Biblia. Kama jamii ya watu tumepitia mambo karibu yote ambayo yamepitiwa na jamii nyingine za dunia. Kuanzia maisha ya ujima, utumwa, vita, mapigano, na hatimaye uhuru.

      Kumbe basi historia yetu haina tofauti sana na historia ya jamii nyingine za watu ambazo zimesimama katika pande za dunia. Unaposoma utenzi huu ni matumaini yangu utakufanya ujisikie fahari kuwa wewe kama vile mimi ni zao la historia hii. Tumefungamanishwa na historia kiasi kwamba haiwezi kufunguka. Mbele yetu wametutangulia wengi katika historia ambao nao walisimama kutambua utu wao na kuudai mbele ya watawala wa zama zao. Ni hiki ndicho tunachokifurahia kwamba leo tuko huru kuwa watu sawa na wengine – kwa kila hali.

      Ni utu wetu ndio ulikuwa msingi wa kupigania uhuru wetu na unatakiwa kuwa ndio kiini cha kushangilia uhuru huo. Ni vipi tumetumia uhuru huo kuinua utu wetu hili ni swali jingine ambalo kizazi chetu kama kizazi kinachokuja kitahiji kujibu. Je, mambo tunayoyafanya na kufanyiana yanalingana na utu huo? Je, tunatendeana kama watu wenye utu katika sera, sharia, mipango, na mambo tunayoyafanya? Utenzi huu basi ni kukumbushia utu wetu.

      MMM Disemba 5, 2011


      SIFA KWA MUNGU!
      1. Ee Mola ninakujia
      Kwako ninasujudia
      Sifa nakurudishia
      Utukufu enzi pia



      2. Ewe uliye Jalia
      Mmiliki wa Dunia
      Hukumu ni zako pia
      Na adhabu ya Jehania



      UTANGULIZI



      3. Kalamu naishikia
      Naandika beti mia
      Kwa tungo nazipangia
      Zinasifu Tanzania


      4. Ni tungo za historia
      Ni wapi tulianzia,
      Na wapi tumefikia,
      Lengo ni kukumbushia


      5. Nataka kusimulia
      Kwa hizi tungo mia
      Huku nawahisabia
      Mpaka zitapotimia


      6. Tangu walipoingia
      Wageni toka Asia
      Na wale wa Yuropia
      Makabila yalohamia


      7. Ishirini na mia,
      Makabila ya Tanzania,
      Makubwa madogo pia
      Hapa nawasimulia


      8. Na beti zikitimia
      Zikifika hizo mia
      Kalamu nitaachia
      Lengo nitalifikia.


      9. Ujumbe nauanzia
      Wa hizi beti mia
      Kwa kina nitagusia
      Ni wapi tulianzia

      ...

      Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
      Disemba 5, 2011
      Email: mwanakijiji@jamiiforums.com
      Facebook: "mimi mwanakijiji"

      NB:* - Utenzi huu unaweza kuchapwa popote na mahali popote bila kubadilisha maneno kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru. Haki zote za kuunakili zimeruhusiwa bila kubadilisha jina la mtunzi au utenzi wenyewe; lazima kuweka maelezo ya mawasiliano kama yalivyo.
      Attached Files
      Last edited by Mzee Mwanakijiji; 5th December 2011 at 09:47.
      mwanakijiji@jamiiforums.com
      Binafsi NAKERWA, NAKASIRISHWA, NA KUCHUKIZWA sana na haya mambo kwamba eti "ameshauriwa vibaya na wasaidizi wake!" Huwa mara zote najiuliza ikiwa anashauriwa vibaya ni kwanini basi kila wakati awe anachukua huo ushauri mbaya!! - NasDaz


    2. #2
      RealMan's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 9th November 2010
      Location : Daslam
      Posts : 1,259
      Rep Power : 2829
      Likes Received
      355
      Likes Given
      175

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Sasa ndugu yangu Mwana kijiji mbona Tanzania haijawahi kupata uhuru.

      Wazungumzia Tanzania ipi?

    3. #3
      AirTanzania's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2011
      Location : Uwanja Wa Ndege
      Posts : 726
      Rep Power : 476
      Likes Received
      200
      Likes Given
      801

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      ngoja niendele kuisoma kwa umakini kabla sijaijibu
      Last edited by AirTanzania; 5th December 2011 at 10:30.
      CCM to me is like al Qaeda or al Shabaab, terrorize the nation and his people.CCM is an organization of thug regime lead by criminal and corrupt, put in power by NEC

    4. #4
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 26,634
      Rep Power : 22539
      Likes Received
      8482
      Likes Given
      4308

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By RealMan View Post
      Sasa ndugu yangu Mwana kijiji mbona Tanzania haijawahi kupata uhuru.

      Wazungumzia Tanzania ipi?
      Ukisoma vizuri utaona nazungumzia ipi.
      mwanakijiji@jamiiforums.com
      Binafsi NAKERWA, NAKASIRISHWA, NA KUCHUKIZWA sana na haya mambo kwamba eti "ameshauriwa vibaya na wasaidizi wake!" Huwa mara zote najiuliza ikiwa anashauriwa vibaya ni kwanini basi kila wakati awe anachukua huo ushauri mbaya!! - NasDaz

    5. #5
      Ndahani's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 3rd June 2008
      Location : Somewhere
      Posts : 5,363
      Rep Power : 1579
      Likes Received
      997
      Likes Given
      1667

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By RealMan View Post
      Sasa ndugu yangu Mwana kijiji mbona Tanzania haijawahi kupata uhuru.

      Wazungumzia Tanzania ipi?
      I sense the call for Tanganyika is coming! Where does it come from???
      Patience,practice,and ceaseless importunity can a man enter the door of the temple of knowledge.

    6. #6
      Mkuu wa chuo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2011
      Location : Kibada
      Posts : 1,413
      Rep Power : 718
      Likes Received
      222
      Likes Given
      13

      Default

      nimekubali

    7. #7
      Gaijin's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2007
      Posts : 9,241
      Rep Power : 5160
      Likes Received
      3276
      Likes Given
      1973

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Awali ya yote

      Thalatha inamaanisha tatu na sio thelathini
      Aroba (arba) inaamisha nne na sio arobaini (arbaini)
      kama ambavyo tisa inamaanisha tisa na sio tisiini

      Pili, ningeomba kuelezewa huu 'utenzi', unafuata kanuni gani za uandishi wake?

    8. #8
      Megawatt B's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 23rd August 2011
      Posts : 114
      Rep Power : 361
      Likes Received
      19
      Likes Given
      1

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Ukisoma vizuri utaona nazungumzia ipi.
      Wewe Mwanakijiji nilikua nakuamini sana, lakini hili...... HAPANA. Hapa unazungumzia Tanzania bwana, Tanzania haijapata uhuru na wala haijafikisha miaka hamsini(50) usituzuge acha kufuata mkumbo
      williamu lee likes this.

    9. #9
      UMMATI's Avatar
      Member Array
      Join Date : 18th May 2011
      Posts : 59
      Rep Power : 364
      Likes Received
      10
      Likes Given
      0

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Uhuru wa Tanganyika sio TANZANIA!

    10. #10
      MAMENGAZI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 598
      Rep Power : 492
      Likes Received
      65
      Likes Given
      67

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Hongera kwa beti mia
      sote tumejionea
      kusoma nimepania
      punde nitachangia

    11. #11
      Matola's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 5,872
      Rep Power : 10399
      Likes Received
      2479
      Likes Given
      1794

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Tanzania haijawahi kutawaliwa na haina siku ya uhuru bali ni siku ya Muungano tu, atakaepotosha ukweli huu amelaaniwa duniani mpaka mbinguni.
      Nawapenda sana Tanganyika Law Society walijiondoa kwenye unafki huu tangu awali.
      williamu lee likes this.


    12. #12
      Crucifix's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 850
      Rep Power : 536
      Likes Received
      171
      Likes Given
      217

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Utangulizi


      Nilipata wazo la kuandika utenzi huu* kuanzia mwaka jana. Nilikuwa nimekusudia kuandika Utenzi wenye beti 1000 kwa ajili ya maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania.................
      Nimeishia hapa. Siwezi kuendelea kusoma beti 100 za uhuru wa tanzania. Nitaweza kusoma au hata kuimba beti 10,000 za Tanganyika baada ya uhuru wa kweli tutakapoachana na Zanzibar. Anza kutunga.......
      Ninakuombea ubarikiwe hadi ushangae!

    13. #13
      semako's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th November 2011
      Posts : 102
      Rep Power : 348
      Likes Received
      6
      Likes Given
      4

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Tanzania haijapata uhuru wewe

    14. #14
      MAMENGAZI's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 598
      Rep Power : 492
      Likes Received
      65
      Likes Given
      67

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Beti nimemalizia
      yote nimejionea
      asante kwa historia
      na mengi kujifunzia

      hongera kwa kuyaona
      makosa yalotendeka
      nchi mbili kuungana
      na mbili kupatikana

      Tanganyika kupotea
      ndilo linatusumbua
      muungano twakosoa
      kwani unatuumbua

      Kutenda kosa si kosa
      kosa kurudia kosa
      tuyakosoe makosa
      haki tusije ikosa

    15. #15
      Borakufa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th May 2011
      Location : Tohell
      Posts : 819
      Rep Power : 520
      Likes Received
      174
      Likes Given
      135

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Aaah! amechanganya historia ya tanganyika na zanzibar huyu mie nimemwelewa hivyo! lakini ameskip! 9.december ni uhuru wa nchi ipi! mwanakijiji umenunuliwa? maana katika utenzi huu unaonyesha kuwa kwa jinsi mwingiliano wa maisha wakati wa ukoloni tulitakiwa kuwa tanzania since before sivyo? Huoni hii ni history ya kufikirika hii! ebu tengeneza utenzi kama huu specific kwa Tanganyika sawa mkuu usibadilike kaka!

    16. #16
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 26,634
      Rep Power : 22539
      Likes Received
      8482
      Likes Given
      4308

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Hivi Tanganyika ni nchi ya nani? Kwanini watu wanalilia nchi ya mkoloni?
      The Boss, Akili Kichwani and Mkono like this.
      mwanakijiji@jamiiforums.com
      Binafsi NAKERWA, NAKASIRISHWA, NA KUCHUKIZWA sana na haya mambo kwamba eti "ameshauriwa vibaya na wasaidizi wake!" Huwa mara zote najiuliza ikiwa anashauriwa vibaya ni kwanini basi kila wakati awe anachukua huo ushauri mbaya!! - NasDaz

    17. #17
      Matola's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 5,872
      Rep Power : 10399
      Likes Received
      2479
      Likes Given
      1794

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Hivi Tanganyika ni nchi ya nani? Kwanini watu wanalilia nchi ya mkoloni?
      Labda ungetusaidia kutuonesha Tanzania bara iko wapi nadhani huu utata wote utaisha. United Kingdom inaonesha kila kitu na kila kisiwa status yake,kwa nini sisi tunakuwa matapeli?

    18. #18
      Lenana's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2010
      Posts : 352
      Rep Power : 455
      Likes Received
      40
      Likes Given
      24

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      aliyekuambia Tanganyika nchi ya mkoloni nani!?

    19. #19
      Crucifix's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 850
      Rep Power : 536
      Likes Received
      171
      Likes Given
      217

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Hivi Tanganyika ni nchi ya nani? Kwanini watu wanalilia nchi ya mkoloni?
      Kwa mara ya kwanza unisamehe ndugu......napata taabu kutamka hili.......lakini nahisi swali hili.....lakini nisamehe kwa sababu nakuheshimu....ila hata kama mkubwa hajambi......akikosea lazima tumseme.......katika hili.....UMETUMIA MASABURI KUPOST.

      Tanganyika ni nchi yangu na si nchi ya mkoloni. Kama ingekuwa nchi ya mkoloni isingesubiri hadi 1964 kusilimu au kubatizwa na kuitwa Tanzania
      Ninakuombea ubarikiwe hadi ushangae!

    20. #20
      Crucifix's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 850
      Rep Power : 536
      Likes Received
      171
      Likes Given
      217

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By MAMENGAZI View Post

      hongera kwa kuyaona
      makosa yalotendeka
      nchi mbili kuungana
      na mbili kupatikana
      Na mimi naongezea
      Beti moja kujazia
      Tanganyika kurejea
      Dua ninaiombea
      MAMENGAZI and Sangarara like this.
      Ninakuombea ubarikiwe hadi ushangae!

    21. #21
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 26,634
      Rep Power : 22539
      Likes Received
      8482
      Likes Given
      4308

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Tanganyika haikuwahi kuwa zao la watu wa Tanganyika; vinginevyo wazee wasingetaka uhuru kutoka kwa Mwingereza. Tanganyika ni zaidi ya nchi au mipaka au jina. Labda watu warudi nyuma na kujifunza historia yetu kidogo. Tanganyika ilizaliwa katika misingi yake ambayo mtu aliposema "Mtanganyika" ilijulikana anamaanisha nini. Labda watu mrudi na kusoma hotuba za kuelekea Uhuru, ya siku ya Jamhuri na Hotuba ya Nyerere Umoja wa Mataifa baada ya maadhimisho ya Uhuru. Misingi ambayo ilikamilika katika Tanzania. Tanzania ni zao la njozi ya Tanganyika.

      Inanishangaza watu wanatukuza "Tanganyika" lakini hawataki kuangalia misingi ya Tanganyika ilikuwa nini na wengine hata hawajui ilikuwa ni nini. Huwezi kuwa na Tanganyika bila kurudia misingi yake! Ni sawa na mtu ambaye anataka kurudia nyumba aliyokuwa nayo lakini bila kurudia alipoijengea. Aidha utakachopata sicho - japo inaweza kufanana na ukaita ni chako. Tanganyika na Tanzania haviwezi kutenganishwa. Hata bila Zanzibar - Tanzania inaweza kuwepo kwa sababu Tanzania ni zao la Tanganyika.

      Kinyume na watu wengi wanavyosema wakati wa Muungano Tanganyika haikupoteza utambulisho wake, iliukamilisha na inapaswa kuendelea kuukamilisha kwa kuelekea Shirikisho la Afrika ya Mashariki. Kuirudia Tanganyika ni kurudia kitu ambacho tulikiacha na kutaka kurudia nyuma ya historia. Ndio maana huwezi kuwakuta wazee waliofahamu uhuru na harakati za uhuru wanalilia Tanganyika - kama wapo wachache tu.
      The Boss and Akili Kichwani like this.
      mwanakijiji@jamiiforums.com
      Binafsi NAKERWA, NAKASIRISHWA, NA KUCHUKIZWA sana na haya mambo kwamba eti "ameshauriwa vibaya na wasaidizi wake!" Huwa mara zote najiuliza ikiwa anashauriwa vibaya ni kwanini basi kila wakati awe anachukua huo ushauri mbaya!! - NasDaz

    22. #22
      Gaijin's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2007
      Posts : 9,241
      Rep Power : 5160
      Likes Received
      3276
      Likes Given
      1973

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Tanganyika haikuwahi kuwa zao la watu wa Tanganyika; vinginevyo wazee wasingetaka uhuru kutoka kwa Mwingereza. Tanganyika ni zaidi ya nchi au mipaka au jina. Labda watu warudi nyuma na kujifunza historia yetu kidogo. Tanganyika ilizaliwa katika misingi yake ambayo mtu aliposema "Mtanganyika" ilijulikana anamaanisha nini. Labda watu mrudi na kusoma hotuba za kuelekea Uhuru, ya siku ya Jamhuri na Hotuba ya Nyerere Umoja wa Mataifa baada ya maadhimisho ya Uhuru. Misingi ambayo ilikamilika katika Tanzania. Tanzania ni zao la njozi ya Tanganyika.

      Inanishangaza watu wanatukuza "Tanganyika" lakini hawataki kuangalia misingi ya Tanganyika ilikuwa nini na wengine hata hawajui ilikuwa ni nini. Huwezi kuwa na Tanganyika bila kurudia misingi yake! Ni sawa na mtu ambaye anataka kurudia nyumba aliyokuwa nayo lakini bila kurudia alipoijengea. Aidha utakachopata sicho - japo inaweza kufanana na ukaita ni chako. Tanganyika na Tanzania haviwezi kutenganishwa. Hata bila Zanzibar - Tanzania inaweza kuwepo kwa sababu Tanzania ni zao la Tanganyika.

      Kinyume na watu wengi wanavyosema wakati wa Muungano Tanganyika haikupoteza utambulisho wake, iliukamilisha na inapaswa kuendelea kuukamilisha kwa kuelekea Shirikisho la Afrika ya Mashariki. Kuirudia Tanganyika ni kurudia kitu ambacho tulikiacha na kutaka kurudia nyuma ya historia. Ndio maana huwezi kuwakuta wazee waliofahamu uhuru na harakati za uhuru wanalilia Tanganyika - kama wapo wachache tu.
      Tueleweshe hiyo historia ili tupate kusherehekea uhuru wa miaka 50 ya Tanzania ambayo haikuwepo miaka 50 iliyopita.

      Btw, tungeomba ufanyie marekebisho tungo yako ili kuondoa makosa ya maneno uliyoyatumia kinyume na maana yake sahihi
      Mzee Mwanakijiji and Taso like this.

    23. #23
      divalicious's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st March 2011
      Posts : 93
      Rep Power : 382
      Likes Received
      15
      Likes Given
      75

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Heh hili la Azania nalo jipya,

    24. #24
      Taso's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th June 2010
      Posts : 956
      Rep Power : 597
      Likes Received
      141
      Likes Given
      43

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Hivi Tanganyika ni nchi ya nani? Kwanini watu wanalilia nchi ya mkoloni?
      Sawa, na iwe ya mkoloni, lakini tunatetea ukweli, tunakataa kupotoshwa. Unachokosea, unataka kulazimisha kwamba Tanzania ina miaka 50, ambao ni uongo wa chiriku, alisema Nyerere, ambae wewe ni zealot wake, kwamba "Ukweli haupendi kudharauliwa" ndio maana unaona kila ukijaribu usanii wa miaka 50 ya Tanzania, kunakuwa na mapingamizi mengi. Hata ingerembwa kwa beti za ngonjera.
      Mzee Mwanakijiji and Gaijin like this.

    25. #25
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 4,428
      Rep Power : 1349
      Likes Received
      688
      Likes Given
      231

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Mkataa asili yake au kwake ni Mtumwa.
      Mzee Mwanakijiji likes this.
      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho

    26. #26
      kilolambwani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 361
      Rep Power : 516
      Likes Received
      58
      Likes Given
      56

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Nchi yetu Tanganyika,
      Sisi tunahuzunika,
      Jinsi walivyo kuzika,
      Bila sisi kuridhia.

      Hakika umetutoka,
      Moyo umehuzunika,
      Daima twakukumbuka,
      Ni lini utarejea?

      Mwenzio wa ushirika,
      Ambaye uliridhika,
      Mzazi wa uhakika,
      Bado anaendelea.

      Mkazaa Tanzania,
      Wewe ukatokomea,
      Ulezi ukakimbia,
      Kumwacha Zanzibaria.

    27. #27
      Companero's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th July 2008
      Posts : 3,698
      Rep Power : 1266
      Likes Received
      449
      Likes Given
      501

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By Gaijin View Post
      Tueleweshe hiyo historia ili tupate kusherehekea uhuru wa miaka 50 ya Tanzania ambayo haikuwepo miaka 50 iliyopita.

      Btw, tungeomba ufanyie marekebisho tungo yako ili kuondoa makosa ya maneno uliyoyatumia kinyume na maana yake sahihi
      LOL, vina na mizani vitapwaya - labda aandike errata mwisho wa tenzi na kukushukuru mhariri mahiri !
      Gaijin likes this.
      "Each generation must, out of relative obscurity, discover its mission, fulfil it, or betray it"/Kila kizazi, katika utata wa kipindi chake, lazima kiutambue wajibu wake na kiutekeleze au kiusaliti - Frantz Fanon

    28. #28
      Sangarara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2011
      Posts : 906
      Rep Power : 594
      Likes Received
      368
      Likes Given
      323

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Hizi sherehe hizi ni bora serikali izitishe au la kama wanategemea watu wataachana na
      haya mambo sherehe zikimalizika lakini naona kama wanafungua pandorabox.

    29. #29
      Gaijin's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st August 2007
      Posts : 9,241
      Rep Power : 5160
      Likes Received
      3276
      Likes Given
      1973

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By Companero View Post
      LOL, vina na mizani vitapwaya - labda aandike errata mwisho wa tenzi na kukushukuru mhariri mahiri !
      Nilijua imeandikwa kwa kutumia mfumo wa Magharibi flani hivi manake kwa mfumo wa mizani ya kwetu Waswahili, kama ishapwaya tayari. Na ndo maana nikauliza :D
      Mzee Mwanakijiji likes this.

    30. #30
      Kindimbajuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th July 2009
      Posts : 362
      Rep Power : 927
      Likes Received
      90
      Likes Given
      85

      Default Re: Utenzi wa Tanzania - Miaka Hamsini ya Uhuru (Beti 100)

      Quote By RealMan View Post
      Sasa ndugu yangu Mwana kijiji mbona Tanzania haijawahi kupata uhuru.

      Wazungumzia Tanzania ipi?
      bora hata ingepata uhuru, ni kuwa haijatimiza miaka 50 badooooooooooooooooooooo!!!!!! !!!!!!!!!!!

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Eti miaka hamsini ya uhuru au ya umasikini?
      By selengia in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 64
      Last Post: 7th December 2011, 08:51
    2. Replies: 9
      Last Post: 1st December 2011, 16:45
    3. Barabara ya Uhuru na miaka hamsini ya uhuru
      By kyoga in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 4
      Last Post: 28th November 2011, 09:12
    4. Miaka hamsini ya uhuru na ufagio wa chelewa!
      By SIR_KIMANYO in forum Jamii Photos
      Replies: 5
      Last Post: 25th November 2011, 16:40
    5. CountDown kwa miaka Hamsini ya Uhuru
      By Chifunanga in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 3rd January 2011, 13:27

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...