Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

    Report Post
    Page 2 of 2 FirstFirst 12
    Results 21 to 30 of 30
    1. #1
      Izack Mwanahapa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st April 2011
      Location : Mwanza
      Posts : 314
      Rep Power : 471
      Likes Received
      129
      Likes Given
      94

      Default Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Swala la muungano wa Tanganyika na Zanzibar limekuwa likizua mijadala kila kukicha, hasa inapofikia kwenye mahali ambapo zanzibar na Tanganyika wanatakiwa kushiriki pamoja katika maamuzi makubwa ya nchi kama hili linaloendelea sasa kuhusu Muswada wa katiba. Je kama Mtanzania unayejiamini na kujitegemea kimawazo, nini maoni yako kuhusu muungano huu?
      Daudi Mchambuzi likes this.

    2. FemaTV & Radio

    3. #21
      kitumanga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 16th August 2011
      Posts : 45
      Rep Power : 402
      Likes Received
      4
      Likes Given
      1

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Hakuna sababu ya kuwa na muungano kama hakuna serikali moja. Na hata wale wanaosema kuwa pawe na serikali tatu yaani sesikali ya mapinduzi Zbar, serikali ya jamuuri ya Tanganyika na serikali ya jamuuri ya muuanga ya Tanzania pia naona hawatakua na jipya kwani bado hapatakuwa na faida yoyote zaidi ya kuOngeza matumizi ya pesa za walipa kodi kwa ajili ya kulipa msururu wa viongozi kwenye serikali hizo. Kama ni mahusiano ya kiuchumi tutakutana kwenye East African Community kwisha. Kama Zbar wana katiba yao inayowatambua kama nchi kwa nini watanganyika na sisi tusiwe na yetu? why? TO ma side mi naona hakuna chenye mwanzo kisicho na mwisho, hakuna kinachozali kisichokufa so huu ndio wakati muafaka wa kuiua Tanzania na kubakia na nchi mbili i.e. Tanganyika na Zanzibar kwa kua hata wazbar wanataka hivyo.
      Izack Mwanahapa likes this.

    4. #22
      kalasinga's Avatar
      Member Array
      Join Date : 12th November 2011
      Posts : 25
      Rep Power : 385
      Likes Received
      1
      Likes Given
      0

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Quote By Tigga Mumba
      Wavivu hao waende zao
      tugawe mbao tu tumechoka kuletewa majambazi na wakabaji wachia mbali viongozi mafisadi ..kufa leo kama walivyokufa waasisi

    5. #23
      Nsee's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 25th May 2009
      Posts : 6
      Rep Power : 510
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Thumbs up Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Wao wanauzanzibari (utaifa wao) wakati sisi tumeuua utanganyika wetu halafu wanataka usawa katika masuala ya katiba. this is unfair
      Quote By themankind
      Maoni yangu,
      1.Huu muungano wa nchi Mbili ni lazima uzalishe serikari moja(Serikari ya jamuhuri ya Muungano ya Tanzania)-ni kiini macho cha hali ya juu kuwa nchi mbili zilizoungana zinazalisha serikali mbili eti ya Muungano na ya Zanzibar,hata mtoto mdogo wa darasa la chekechea anaelewa kuwa ilitakiwa serikali moja tu au ilitakiwa serikali tatu.
      2.Haki ya mtanganyika imemezwa na Muungano huu,ni lazima tuutafute utanganyika wetu(asili yetu) kwa namna yoyote ile,kila binadamu ana asili yake nasi kama watanganyika tunataka asili yetu ya kuwa mtanganyika mtanzania.
      3.Mambo ya muungano yaelezwe kinagaubaga pasipo maficho yoyote yale,Tunaficha nini?
      4.Ikishindikana kabisa ningependa Muungano uvunjwe na kila nchi ibaki na haki zake kama nchi.

      nawasilisha

    6. #24
      Topical's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 5,050
      Rep Power : 1231
      Likes Received
      853
      Likes Given
      707

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Quote By matunge
      Mimi naona Wazanzibar waachwe waamue hatma ya nchi yao. Lakini sote tunatokana( kama wanadamu) na BABA wa BWANA yetu YESU CHRISTO. Wale tunaomwamini YESU kuwa alikufa akazikwa na siku ya tatu akafufuka kwa ajili yetu, tutakutana katika UFALME ujao wa MUNGU na wale wasioamini makao yao ni katika ziwa lile liwakalo moto na kiberiti.
      Duh! mapambio utafikiri uko wapo radio..

    7. #25
      Kibanga Ampiga Mkoloni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th August 2007
      Location : Here! here!
      Posts : 4,777
      Rep Power : 1630
      Likes Received
      1186
      Likes Given
      1701

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Hivi ni Mungano wa nani na nani?
      For the Holy Quran says in Sura 42, verse 41: 'All those who fight when oppressed incur no guilt, but Allah shall punish the oppressor, Come the day.

    8. Miaka 50

    9. #26
      BongoLogik's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2009
      Posts : 254
      Rep Power : 548
      Likes Received
      40
      Likes Given
      40

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Kila upande(Tanganyika na Zanzibar) upige kura ya maoni kuamua kama tuwe na muungano au hapana, na kwa kuwa ili muungano uwe imara bila mushkeli inabidi ipatikane ridhaa ya pande zote mbili,na kama kura ya maoni ya upande wowote itasema hapana itamaanisha hakuna haja ya muungano hata kama kura ya maoni ya upande mwingine itasema ndiyo, na kama kura za maoni za pande zote mbili zitasema hapana ndio itathibitisha zaidi haja ya kutokuwa na muungano.Sasa kama kura za maoni za pande zote mbili zitakuwa NDIYO kwa muungano,itabidi tuingie katika hatua ya pili ya kukubaliana ni aina gani ya muungano tuwe nao,hii aina ya muungano tulio nao sasa wa 'Nyerere na Karume' itabidi usiingie kwenye mchakato kwa kuwa umeleta manung'uniko na malalamiko mengi na zaidi ya yote unachanganya vichwa vya watu!tubaki na aina mbili tu za muungano kupigia kura ya maoni yaani muungano wa serikali moja na ule wa serikali tatu, na kwa suala hili pia itabidi kila upande upige kura kuchagua aina gani ya muungano kati miundo hiyo miwili, iwapo matokeo ya kura za maoni ya pande zote mbili yatasema NDIYO kwa muundo unaofanana, huo ndio utakuwa muungano wetu, na hatua itakayofuata ni kuandika katiba itakayoendana na muundo huo (hapa namaanisha kuwa hata mchakato wa katiba wa sasa hauna maana mpaka tupate kwanza suluhisho la muungano) na iwapo matokeo ya kura za maoni ya pande zote yatatofautiana kuhusu muundo wa muungano yaani upande mmoja ukubali serikali tatu na upande mwingine ukubali serikali moja hapo itabidi kila upande uchukue ustaarabu wake yaani hakuna haja ya kuwa na muungano,Tanganyika kwao na Zanzibar kwao kila taifa lijiongoze lenyewe kwa mujibu wa katiba watazotengeneza wenyewe! hayo ndio maoni yangu.
      Izack Mwanahapa likes this.

    10. #27
      DOUGLAS SALLU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th November 2009
      Posts : 3,598
      Rep Power : 1285
      Likes Received
      315
      Likes Given
      905

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Muungano ulikidhi malengo ya wakati ulipo asisiwa,kwa sasa hauna faida yoyote zaidi ya kuwa mzigo kwa walipa kodi wa Tanganyika.MUUNGANO UFE NA WAZENJI WAONDOKE BARA.

    11. RMA
      #28
      RMA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2010
      Posts : 410
      Rep Power : 519
      Likes Received
      87
      Likes Given
      0

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Quote By CULCULUS
      Kama hakuna uwezekano wa kuwa na serikali moja basi Muungano ni bora ufe tu. Maana hata USA wameungana zaidi ya mataifa 40 lakini wameweza kuwa na serikali moja. Kwa nini kwa TANZANIA iwe nongwa?? No Single Government, No Muungano
      Ni vema Wazanzibari wakiamua hatima ya nchi yao. Lakini ni bahati mbaya kwamba jambo hilo halitakuwa zuri kwao kwa kuwa baada ya hapo hoja za uunguja na upemba zitaibuka! Wataingia katika machafuko. Wapemba nao watataka kujitawala kwa kuwa na serikali yao lakini wasiweze. Zanzibar itapitia kipindi kigumu kisiasa na kiuchumi. Baadhi yao watatamani muungano lakini wakati huo watanganyika watakuwa na serikali ya chama kingine ambayo haitakubali kuwepo muungano na Zanzibar.

      Kwa sababu ya hali ngumu ya kisiasa na kiuchumi, vijana wengi wa Zanzibar watarubuniwa na kujiunga katika makundi ya magaidi (sio Al shabab). Wakati huo Al shabab itakuwa imekwishatokomezwa lakini yatakuwa yameibuka makundi mengine yenye msimamo mkali wa kidini na Zanzibar itachukiwa na nchi nyingi duniani kwa sababu ya kuwahifadhi magaidi. Ni bahati mbaya vilevile kwamba kukosekana kwa amani Zanzibar kutaiathiri sana Tanganyika. Kutakuwa na uhasama wa kisiasa baina ya Tanganyika na Zanzibar.

    12. #29
      Shark's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 25th January 2010
      Posts : 4,573
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1305
      Likes Given
      245

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      Wazanzibar Vigeugeu sana,
      Unataka kuolewa halafu bado unataka uendelee kuishi kwenu, ushaona wapi hiyo?
      Ukishachanganya Sukari, Maji na Majani unachopata ni Chai sasa, sio kimojawapo kiendelee ku-exist tena!!
      Bora uvunjike tu tujue moja!!!

    13. #30
      Fatal5's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 1st July 2011
      Posts : 166
      Rep Power : 432
      Likes Received
      28
      Likes Given
      134

      Default Re: Nini maoni yako Kuhusu Muungano?

      kwa vile muungano huu hauna faida na upande wowote ule tokea ulipoanzishwa 1964 basi bora uvunjwe kila nchi iwe kivyake.
      Watanganyika na Wazanzibar watakutana katika mambo ya uchumi na mengineyo katika East Afrika Community.
      Ni bora Zanzibar wakae na nchi yao na Tanganyika kivyao kama hapo zamani kabla ya kuungana. ni nchi nyingi tu duniani ziliungana walipochoka walivunja Muungano na kukaa kila nchi kivyake na wamezidi kufanya maendeleo mazuri tu bila ya kuleteana matatizo.

    Page 2 of 2 FirstFirst 12

    Similar Topics

    1. Replies: 0
      Last Post: 29th April 2011, 16:37
    2. Replies: 23
      Last Post: 6th April 2011, 17:26
    3. Maoni yako Kuhusu Picha Hii
      By ELNIN0 in forum Jamii Photos
      Replies: 8
      Last Post: 5th October 2010, 16:09
    4. RT inahitaji maoni yako kuhusu riadha
      By Kibunango in forum Sports
      Replies: 12
      Last Post: 17th September 2008, 22:55
    5. Nini maoni yako kuhusu mkao wa balozi huyu
      By mstahiki in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 17
      Last Post: 7th January 2008, 10:37

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...