Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party??.

    Report Post
    Results 1 to 15 of 15
    1. #1
      kulwa12's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2009
      Posts : 107
      Rep Power : 529
      Likes Received
      21
      Likes Given
      3

      Default Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party??.

      Ndugu zangu naandika hili kwa uchungu mkubwa kutokana natabia inayokua sasa kwa kasi kati yetu sisi watu tunayoitakia mema chama cha Chadema,tabia ya baadhi yetu kutoa maneno ya kejeli na matusi hasa kwa watuwanaochangia humu katika JF na kwingine mawazo yanayopingana na sera au misimamoya viongozi wa chama.

      Naomba leo nichangie mambo mawili ambayo wengi sana nimeona tuna dhalau umuhimu wake lakini yana hatari kubwa sana kama ya kibaki kama yalivyo.

      Kwanza ni la chama chetu kuwa na ushusiano na chama cha Conservative cha Uingeereza na pili ni chama chetu kuwa na sera (ideology) za Ubebari (Capitalism) na soko huria (Freemarkets).

      Ni ukweli usiopingika kabisa kwamba CDM inauhusiano wa damu na wakaribu sana na Chama cha mabeberu cha Conservative cha uingereza,ambacho kinajulika na sera zake za upebari(Capitalisim) zenye kukumbatia matajili na watu wenye uwezowa kifedha na huu ndio misingi mkuu hasa vyama vya Ki-conservative duniani kote(Kujali tabaka la matajiri).

      Katika vyombo vingi vya kimagharibi hasa UingerezaCDM inajulikana kama Conservative Party of Tanzania na kama chama chenye sera za Ubepari(Capitalisim) na kinachoaminikatika soko huria (Free Markets).

      CDM kwa miaka mingi sana imekua ikipata misaada ya kifedha na kiutaalamu wa kisera kutoka chama cha Conservative cha uingereza.Ushaidi nimetoa wapi kusema haya?? Kuna ushahidi mwingi sana na hililiko wazi kabisa.

      Mwaka 2005 kuelekea uchaguzi mkuu wa Tanzania,chama cha Conservativekilimtuma Tanzania mtaalamu na nguli wachama hicho aitwae Reberat Halfon akiungana pamoja na mtaalamu muelekezi maarufu duniani wa sera za Kibepari na siasa aitwae John Earl ili kuja Tanzania kukisaidia chama cha CDM katika uchaguzi wa 2005 hasa katika mambo yafatayo,kwanzakusaidia CDM kutambua ipeleke katika majimbo gani rasilimali za kusaidiakushinda majimbo hayo wanayoyalenga kushinda (hii ni sawa na kuja kusimamiamatumizi ya fedha ambazo nyingi zilitolewa na chama cha conservative),Pili kusaidiaCDM kuunda kauli mbiu ya uchaguzi na ujumbe au sera za kutumia kwenye kampenina mwisho kusaidia kuratibu mpangilio(Orgainise) na mawasiliano katika makao makuu ya CDM.

      Mtaalamu huyu baada ya kumalizika kwa uchaguzi aliandika makala katika mtanadao maarufu huko wingereza wa the Social Affair Unity, yenye kichwa cha bari "Chadema offersTanzania real change and genuine democracy", katika makala hii inatoa ushaidi zaidi juu ya hoja zangu kwamba CDM inasaidiwa na Conservative party na pili ni chama chenye sera za kibepari(Capitalism).

      Kwa kifupia mtaalamu huyuanasema mambo yafatayo kuhusu chadema katika makala yake,naomba kunukuu hukunikitoa ufafanuzi,"Thus in 1993, Chadema was born. This was a politicalmovement that believed in an open society with open markets, that the best way of ending poverty was through a strong economy based on capitalism",akimanisha (mwaka 1993 Chadema ilizaliwa.Hii ilikua ni harakatiza kisiasa zinazoamini katika jamii iliyo wazi yenye masoko huria,na njia boraya kumaliza umasikini ni kupitia uchumi imara unaoelemea mfumo wakibepari),maelezo hapo juu yanazihirisha wazi kwamba CDM inaamini katika ubepari (Capitalism) na sera za soko huria.

      Anaendelea kusema kuhusu ushirikiano kati ya Chadema na Conservative Party na jinsi ambavyo alitumwa Tanzania na Conservative Party na akikili wazi kwamba wataalamu wengi sana kutoka conservative party wamekua wakija Tanzania kutoa mafunzo kwa viongozi wa chadema,naombakunukuu,"In the UK, the Conservative Party International Office has been instrumental in giving Chadema advice and training support. I was sent to Chadema along side John Earl, a highly respected political consultant (once running field operations at CentralOffice), our job was to help Chadema target resources at target seats, position the movement in terms of their values and help define a political message as well as organise their Party HQ. All these activities were given strong support by Chadema staffers and the Party Central Committee. Many other Conservative Party trainers have gone to Tanzania to support Chadema in every way possible.).

      Ndugu zangu naomba sana sana tuungane kuwahoji viongozi wetu juu ya mambo haya makubwa mawili kwani nawambia wazi kwa jinsi Watanzania walivyo ichoka CCMhakika tutashinda uchaguzi ujao,ila hatutadumu madarakani kama Chadema kinaingiamadarakani na sera hizi za ubepari na kwa msaada wa chama cha kibepari chaconservative,sera hizi zitawafanya wananchi wazidi takua na hali mbaya zaidizadi kuliko nyuma na hawataona tofauti yoyote kati ya CDM na CCM.

      Tukumbuke sasa duniani mapambano yaliopo ni kati ya wananch na mfumo wa ubepari(Capitalism),angalia marekani nzima sasa wananchi wanaandamana na wameanzisha vuguvugu wanaloliita occupy wall street Movement,kupinga mfumo wa huu wakibepari na sera za soko huria zilizosababisha wananchi 99% wawe masiki wakutupa marekani na 1% ya idadi ya wananchi matajiri wa kutupa.Sasa tujiulize kama hizindio sera za Chadema je tutafikia lengo la kukomboa masikini wa nchi hii??.

      Naomba nitoe mfano wa mwisho halisi kabisa amabao utatuonesha nini kinatokea chama kinachoingia madarakani kwa nguvu ya umma na huku kwa ndani kimekumbatia seraza ubepari na pia kimeingia madarakani kwa msaada wa chama cha Conservative,

      Miaka mitano tu iliopita nchini Liberia, Chama cha UNITY PARTY (UP) kikiongozwa namgomea wake mama Sirlef-Johnson kilipataushindi wa kishindo nchini Liberia nakupewa idhini ya kuchukua dola,tukumbuke uchaguzi huu ulisimamiwa na nchi zamagharibi (UN) na mgombea wa UP aliungwa mkono na na chama cha Conservative nanchi zingine za magharibi ili kushinda uchaguzi huu na tukumbuke huyu mamaaliishi muda mrefu nje ya nchi na akifanya kazi UN.

      Kwa manufaa ya wote chamahiki UP ni chama rafiki sana cha chadema na kinamisingi,imani na mtazamo sawakabisa na Chadema,Chama hiki cha UP pia kinakumbatia sera za Ubepari (Capitalism) na soko huru kama sera zakerasimi na msingi wa chama kama ilivo Chadema.Pia tukumbuke Chama cha UP ni mwanachama pamoja na chama cha chademakwenye ummoja wa vyama vikuu vinne vya Africa unaoitwa Democratic Union of Africa (DUO),ni muungano wa vyama vinavyoamini katika sera za Ubepari(Capitalism) na Soko huria (Free markets),ummoja huu unapata masada mkubwa wakifedha,kisera na kitaalamu kutoka chama cha Conservative cha uingereza,ikiwemo kufadhilia miradi mbalimbali ya vyama hivi.

      Tarehe 18,march,2011,kulikua namkutano wa ummoja huu uliofanyika nchini Liberia na uliandaliwa na chama cha Conservativena cha cha UP cha Liberia,katika mkutano huu Chadema kiliwakilisha na mheshimiwaMbowe .Mkutano huu ulihutubiwa na Hon. Andrew Rosindell,ambaye alikiwakilishachama cha Conservative party,bwanaRosindell ni mbunge wa bunge la uingereza kupitia chama cha Conservative na piani mjumbe wa kamati y amambo ya nje ya bunge la Uingereza.Katika hotuba yakealisema nanukuu “ expressed the commitment of the Conservative Party to support member parties and further continue the sponsorship of DUA programmes”.

      Chama cha UP kutawala Liberia kwa muda wa miaka mitano tu,na sasa kimechokwa na wananchi,Makao makuuy achama hiki yamechomwa moto na wananchi miezi michache iliopiata na katikauchaguzi mkuu wa mwaka huu mgombea wake wa urais Sirleff-Johnson(ambaye ndieRaisi alieko madarakani)amepata asilimia 43 tu ya kura zidi ya asilimia 32 zaWinston Tubman ,ambaye alikua mgombea wachama cha upinzani cha Congress forDemocratic Change(CDC),Kutokana na chama tawala (UP) kushindwa kupata ushindiwa moja kwamoja na imebidi uchaguzi uludiwe mara ya pili leo tarehe 9 mwezi huu.

      Uchaguzi huu wa marudio umegubikwa na mashakamengi ikiwemo mwenyeketi wa tume ya uchaguzi kujiuzuru na lawama nyingi zauonevu kutoka na chama tawala kutumia nguvu ikiwewo police kuua waandamanji wanejuzi katika maandamano ya amanai yalioitishwa na vyama vya upinzania.Kutokanana uonevu huu vyama vyote saba vya upinzani vimejitoa katika uchaguzi nakumwacha mgombea wa chama cha UP kama mgombea pekee.

      Ikubukwe Kwa hofu yakushindwa chama hiki cha UP kilifanya juhudi nyingi kubadili sheria yauchaguzi na hasa sheria inayotaka mgombea wa uraisi ashinde kwa absolute majority,ikiwana maana lazima ashinde kwa kura zaidi ya nusu ya kura zote zilizopigwa,chamahiki kilitaka sheria ibadiliswe ili mgombea ashinde kwa simple majority,ikiwa na maana mgombea hata akishinda kwa kura moja kama ilivyo hapa Tanzania natangazwa mshindi.

      Chama cha UP killiitisha kura maoni nchi nzima ili wananchi wapige kurakubadili sheria hii ya uchaguzi,wananchi wakapiga kura ya hapana zidi yao,nawakashindwa!!hawakuishia hapo mwenyekiti wa chama hiki cha UP ndugu Varney Sherman alikakata rufaa ili mahakama kuuingilie kuibadili sheria hii japo wananchi walitaka sheria hii ibaki ilivyo,napowakashindwa tena.

      Sasa wana Chadema tunajifunza nini?? chama hiki rafiki cha UP cha Liberia kimechukiwa na wananch ndani ya miaka mitano tu,kutokana na serahizizi ,Je Chadema ikiingia madarakani na sera na msingi hii ya ubepari ninikitatokea??
      watanzania watakaa kimya tu??

      Jamani amukeni,jifunzeni,fatilieni tusichukulia haya mambo ni rahisi sana kama tunakitakia mema cha chetu chaChadema,kama hakitabadili misingi na sera za ubepari na uhusiano wake na chama cha kibepari cha Conservative,nasema wazi Chadema haitadumu madarakanikamwe hata ikishinda 2015! MUNGU IBARIKI TANZANIA.
      Last edited by kulwa12; 9th November 2011 at 21:36.

    2. RukaaJuu Final

    3. #2
      Noti mpya tz's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd March 2011
      Posts : 633
      Rep Power : 603
      Likes Received
      106
      Likes Given
      260

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      So what?
      Tanganyika ya are my mamaland no matter where ya are I believe ya'll comeback home very soon.

    4. Nzi
      #3
      Nzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Location : 740 Park Avenue
      Posts : 3,322
      Rep Power : 21625
      Likes Received
      946
      Likes Given
      828

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Duh!! Jamaa weka basi hata paragraphs katika andiko lako; pangalia kazi yako ivutie na iwe rahisi kusomeka na kuifuatilia.
      "You can't make a scene if you don't have little green"-------Jim Carrey

    5. #4
      kulwa12's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2009
      Posts : 107
      Rep Power : 529
      Likes Received
      21
      Likes Given
      3

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Quote By Noti mpya tz
      So what?
      Usilahisishe mambo magumu,tabia hiyo ndio imetufikisha hapa tulipo.

    6. #5
      LINCOLINMTZA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th March 2011
      Location : Opposite The JF Web Page
      Posts : 1,362
      Rep Power : 696
      Likes Received
      352
      Likes Given
      216

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Huo uchungu ndo umepelekea kuflow maneno tuuuuuuu bila hata mpangilio. Hebu pangailia maneno yako ili usomeke, kumbuka mpangilio mzuri wa maneno huvutia msomaji. Hukusoma uandishi wa insha darasa la tano kabla ya Mungai?
      Love everybody, trust no body. If you can not convince them, confuse them. If you can not teach them, cheat them.

    7. Miaka 50

    8. LAT
      #6
      LAT's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th November 2010
      Posts : 4,526
      Rep Power : 1498
      Likes Received
      1156
      Likes Given
      1659

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      quantitative than qualitative

      i declare tis post as a mere ----

    9. #7
      kulwa12's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2009
      Posts : 107
      Rep Power : 529
      Likes Received
      21
      Likes Given
      3

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Quote By nyandaigobeko
      duh!! Jamaa weka basi hata paragraphs katika andiko lako; pangalia kazi yako ivutie na iwe rahisi kusomeka na kuifuatilia.
      ahsante mdau nimefanya hilo.

    10. #8
      Somji Juma's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 2nd July 2011
      Location : mkulanga
      Posts : 485
      Rep Power : 0
      Likes Received
      35
      Likes Given
      21

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Hongera mkuu,umeongea mambo ya msing,acha wakutukane lakini sisi tulio na akili tunajifkiria zaid..BIG UP,YOUR A GREAT THINKER..

    11. #9
      Topical's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd December 2010
      Posts : 5,050
      Rep Power : 1232
      Likes Received
      853
      Likes Given
      707

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Mtu ambaye hajui kwamba chadema ni "Hoax" si mzalendo..tafuteni chama kingine kile ni kwa ajili wazungu na mabepari ..

    12. #10
      kulwa12's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2009
      Posts : 107
      Rep Power : 529
      Likes Received
      21
      Likes Given
      3

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Quote By somji juma
      Hongera mkuu,umeongea mambo ya msing,acha wakutukane lakini sisi tulio na akili tunajifkiria zaid..BIG UP,YOUR A GREAT THINKER..
      .Mkuu nashukuru sana kwa mawazo yako,inasikitisha sana vijana wanaojiita wanaharakati na wenye uchungu wa nchii hii,inapokuakja wakati mjadili mambo ya ukweli wanatyoa matusi na kejeli badala ya kujibu hoja.Mi nilitegemea wajibu hoja sio kutoa majibu lahisi ya kejeli,ipo siku watu watakumbuka haya nilioandika.
      Somji Juma likes this.

    13. #11
      kulwa12's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2009
      Posts : 107
      Rep Power : 529
      Likes Received
      21
      Likes Given
      3

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Quote By somji juma
      hongera mkuu,umeongea mambo ya msing,acha wakutukane lakini sisi tulio na akili tunajifkiria zaid..big up,your a great thinker..
      nashukuru sana mdau nakuambia siku itafika watu wataona maana ya maneno nilioandika leo,inasikitisha sana tunaojiita wasomi na wanaharakati wa kuwakomboa wanachi masiki,tunajenga utamaduni wa kujibu hoja kwa matusi na maneno ya kejeli badala ya kujibu hoja kwa hoja,hivi kweli watu wenye akili zao watatupa kura?? Wengi ni thinkers sio washabiki tu bila kujau wanashabikia nini..
      Somji Juma likes this.

    14. #12
      kulwa12's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 30th June 2009
      Posts : 107
      Rep Power : 529
      Likes Received
      21
      Likes Given
      3

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Quote By lat
      quantitative than qualitative

      i declare tis post as a mere ----
      i highly appreciate,for proving my words,insult and intimidation is best weapon for weak minds,don't insult respond to facts..

    15. #13
      JF-BAN1's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 13th April 2011
      Posts : 10,447
      Rep Power : 0
      Likes Received
      3753
      Likes Given
      2889

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Mtoro wa shule ajifunze? magwanda wanamjuwa nani aliyetoroka shule.

    16. #14
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,091
      Rep Power : 12253
      Likes Received
      6015
      Likes Given
      6854

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      story ndefu kumbe ungewezakufikisha kwa para mbili tu

    17. #15
      SOBY's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th September 2011
      Posts : 1,263
      Rep Power : 3233
      Likes Received
      446
      Likes Given
      125

      Default Re: Chadema tunajifunza nini kutokana na uchaguzi wa liberia na uhusinao wetu na conservative party?

      Hilo mbona linajulikana?..... Tatizo ni kuwa hata CCM kipo kwenye free trade. Ila angalau baadhi ya wana CCM wanaweza kuwaondoa kwenye uongozi wale wote wanaodai kutuletea azimio la Zanzibar, ambalo mpaka leo nimeshindwa kupata nyaraka zake (fake declaration).
      Just pick the less of two evils and move on!!

    Similar Topics

    1. Replies: 1
      Last Post: 20th October 2011, 19:34
    2. Replies: 5
      Last Post: 24th September 2011, 08:00
    3. Watanzania tunajifunza nini kutokana na cable za usa
      By Mtazamaji in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 0
      Last Post: 10th December 2010, 05:03
    4. Replies: 0
      Last Post: 10th November 2010, 21:52
    5. Replies: 0
      Last Post: 5th May 2010, 05:05

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...