Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 7th October 2008, 07:23 PM   #1
Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa
Bubu Ataka Kusema Bubu Ataka Kusema is offline 7th October 2008, 07:23 PM

Date::10/7/2008
Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa
Na Jackson Odoyo
Mwananchi

UMOJA wa Vyuo Vikuu nchini (Tahiliso) umepanga kufanya mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu vyote nchini utakaofanyika Oktoba 27 mwaka huu serikali itakapo kubali kubadili sera ya elimu nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Katibu Mkuu wa umoja huo, Mtatiro Julius alisema katika mgomo wanafunzi hawataingia darasani mpaka hapo serikali itakapo kubali mapendekezo yao.

Alisema lengo la mgomo huo ni kuishinikiza serikali ibadili sera zote zinachangia kudidimiza maendeleo ya elimu nchini ili usawa wa elimu uwepo kati ya mtoto aliyezaliwa katika familia isiyokuwa na kipato kizuri na familia yenye kipato kizuri.

Aliongeza kuwa moja ya mambo watakayo yapinga katika sera hiyo ni kitendo cha wanafunzi kufukuzwa chuoni kufukuzwa wasimafanye mitihani ama kunyimwa matokeo yao baada kufanya mitihani.

''Sera inayosimamia maendelea ya elimu nchini inachangia kudidimiza elimu ya nchi na hasa kwenye suala la ada ya wanafunzi ambalo husababisha wanafunzi kufukuzwa chuo kwa kushindwa kulipa ada,'' alisema Mtatiro.

Alifafanua kuwa kitendo cha serikali kumpunguzia ama kumfutia ada mwanafunzi aliyetoka katika familia isiyokuwa na uwezo wakati akisoma elimu ya chini lakini anapingia elimu ya juu alipie sawa na wale wenye uwezo haileti uwiano wa elimu nchini.

Aliongeza kuwa hali hiyo ndiyo inayosababisha wanafunzi wa vyuo vikuu kufukuzwa chuo kila wakati, kama ilivyotokea katika Chuo Kikuu cha Ardhi mwaka huu.

''Kitendo cha serikali kuwafukuza wanafunzi 227 wa chuo hicho ni kuongeza migogoro vyuoni, makazini na hata kuongeza utitiri wa vyeti bandia maofisini,'' alalamika Mtatiro.

Hata hivyo, alisema serikali inashindwa kuwajali wasomi watakaoisaidia nchi baadaye na badala yake inawakumbatia wawekezaji wasiokuwa na uwezo wa kulipa mishahara ya wafanyakazi wao.

Alifafanua kitendo cha serikali kushindwa kuwatetea wasomi wanaotoka katika familia maskini bila kujali kwamba wao pia ni sehemu ya jamii ya watanzania nikuwanyima haki yao ya msingi.
__________________
~*~Life is Good~*~

 
Bubu Ataka Kusema's Avatar
Bubu Ataka Kusema
JF Premium Member
Points: 12,662,314, Level: 100 Points: 12,662,314, Level: 100 Points: 12,662,314, Level: 100
Activity: 69% Activity: 69% Activity: 69%
Join Date: Sun Feb 2007
Location: Mfaranyaki
Posts: 12,663
Thanks: 1,027
Thanked 1,190 Times in 691 Posts
Views: 247
Reply With Quote
  #2  
Old 7th October 2008, 08:21 PM
Kevo's Avatar
Kevo Kevo is offline
Kevo is stuff is tough
JF Senior Expert Member
Points: 238,924, Level: 100 Points: 238,924, Level: 100 Points: 238,924, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Jun 2008
Location: Around the World
Posts: 1,301
Thanks: 0
Thanked 24 Times in 12 Posts
Rep Power: 24
Kevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enough
Default Re: Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa

Fighting the govt is quite a long process and to get what you want is another stage!Wnafunzi wanakandamizwa kwa kweli na sijui kama watawahi kusikilizwa maana as we all know sheria ipo kwa ajili ya kumlnda yule mwenye nafasi kubwa zaidi ila siyo wa lower class
__________________
'I could have annihilated all the Jews in the World,but I left some of them so you will know why I was killing them'-Adolf Hitler;Mien Kampf
Reply With Quote
  #3  
Old 8th October 2008, 04:37 AM
Mwikimbi Mwikimbi is offline
Mwikimbi hakuna aliye bora kuliko taifa lake
JF Senior Expert Member
Points: 339,417, Level: 100 Points: 339,417, Level: 100 Points: 339,417, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
 
Join Date: Sat Mar 2008
Posts: 823
Thanks: 0
Thanked 33 Times in 8 Posts
Rep Power: 24
Mwikimbi will become famous soon enoughMwikimbi will become famous soon enoughMwikimbi will become famous soon enoughMwikimbi will become famous soon enoughMwikimbi will become famous soon enoughMwikimbi will become famous soon enoughMwikimbi will become famous soon enoughMwikimbi will become famous soon enough
Default Re: Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa

Tusipoangalia nchi hii watu hawatasoma, nilikuwa iringa wiki hii pale ruaha uniiversity college, ili mwanafunzi asajiliwe ni lazima awe na na tshs 725,000, aidha umepata mkopo au hapana hizi lazima uzitoe ndo uingie chuoni.watoto wameaga kwao kuja shule wanazurura mjini wakisubiri hiyo bodi ya mikopo ambayo haija-process mikopo na haijulikani ni lini itakamalisha kazi hiyo, watoto wa kike ukikutana nao wanakusaklimia bila sababu, muda si mrefu au tayari washajitumbukiza kwenye umalaya.nawaunga mkono hawa kwenye mgomo wao, hawana njia nyingine dhidi ya serikali bubu, isiyowasikiliza waliyoichagua
Reply With Quote
  #4  
Old 8th October 2008, 03:21 PM
PatPending PatPending is offline
PatPending a miserable old sod
Senior Member
Points: 85,065, Level: 100 Points: 85,065, Level: 100 Points: 85,065, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Aug 2007
Posts: 152
Thanks: 41
Thanked 21 Times in 15 Posts
Rep Power: 23
PatPending will become famous soon enoughPatPending will become famous soon enoughPatPending will become famous soon enoughPatPending will become famous soon enoughPatPending will become famous soon enoughPatPending will become famous soon enoughPatPending will become famous soon enoughPatPending will become famous soon enough
Default Re: Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa

Migomo mingine ni ya kujiumiza wenyewe. Vyuo havitobadilisha ratiba zao ipasavyo kuweza kurusu huu "mgomo", na wanafunzi wao wenyewe ndio wataopata shida ya kujaribu kujifunza vile ambavyo walitakiwa wafundishwe awali kufuatana na ratiba ya awali. Matokeo yake? Wanafunzi kushindwa kumaliza kusoma modules vizuri na labda kushindwa kufanya mitihani inavyotakikana.


Hivi wanafunzi wanataka serikali ifanyeje hasa ili iweze kupata ada zao kama sio kuzuia majibu yao ya mtihani?
Reply With Quote
  #5  
Old 8th October 2008, 03:30 PM
Mushobozi's Avatar
Mushobozi Mushobozi is offline
Mushobozi has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 166,787, Level: 100 Points: 166,787, Level: 100 Points: 166,787, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon Aug 2007
Location: Buzwagi
Posts: 405
Thanks: 3
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 23
Mushobozi will become famous soon enoughMushobozi will become famous soon enoughMushobozi will become famous soon enoughMushobozi will become famous soon enoughMushobozi will become famous soon enoughMushobozi will become famous soon enoughMushobozi will become famous soon enoughMushobozi will become famous soon enough
Default Re: Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa

lakini si mtatiro kamaliza chuo? au katiba ya Tahiriso inaruhusu hata watu ambao tayari ni graduates, na hawako chuoni?
__________________
NI HERI NIISHI KAMA BINADAMU ASIYERIDHIKA
KULIKO KUISHI KAMA NGURUWE ALIYERIDHIKA



Though pressed and crooked against walls
I will die fighting back
Reply With Quote
  #6  
Old 8th October 2008, 03:37 PM
Mwana wa Mungu Mwana wa Mungu is offline
Mwana wa Mungu has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 146,436, Level: 100 Points: 146,436, Level: 100 Points: 146,436, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
 
Join Date: Thu Aug 2008
Posts: 483
Thanks: 0
Thanked 41 Times in 26 Posts
Rep Power: 22
Mwana wa Mungu will become famous soon enoughMwana wa Mungu will become famous soon enoughMwana wa Mungu will become famous soon enoughMwana wa Mungu will become famous soon enoughMwana wa Mungu will become famous soon enoughMwana wa Mungu will become famous soon enoughMwana wa Mungu will become famous soon enoughMwana wa Mungu will become famous soon enough
Default Re: Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa

jasho lao ndilo litakalowakomboa, wapiganie chao, kila kitu kinakuwaga hivyohivyo alafu mafanikio yanakuja.selikali inasema imeshindwa kuwalipia watu hadi inawafukuza, wakati mabilioni kibao yanaliwa kama karanga, hii ni nini? si ndo zingesomeshea watoto wetuhizo, afu, kikwete kila siku misafari ya vekesheni marekani kwenye mihoteli ya kufa mtu, watu wanabwia hela mtindo mmoja huko selikalini, matunda yake nini kikwete hadi aanze hizo safari zake? si kutuletea Leon sullivan waliokuwa kuchangia milioni sitini?, ambazo hata mimi ningeweza kuchangia atu ile nauli yake ibakie hapa ipeleke watoto shule? hivi viongozi wetu wana uchungu na nchi yetu kweli? kwanini tusijibane na kupenga mikakati inayotekelezeka ili baadae ulie kivulini?viongozi wanapenda anasa tu. watoto wetu tena toka vijijini hawana hata hela ya kusomea au kunywa maji pala chuo, wakienda mjini hawana nauli wanapishana tu ni migari ya viongozi,migari ya garama. huu si uungwana.
Reply With Quote
  #7  
Old 8th October 2008, 03:57 PM
Domisianus Domisianus is offline
Domisianus has no status.
Senior Member
Points: 73,360, Level: 100 Points: 73,360, Level: 100 Points: 73,360, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Fri Aug 2008
Posts: 117
Thanks: 0
Thanked 13 Times in 9 Posts
Rep Power: 22
Domisianus will become famous soon enoughDomisianus will become famous soon enoughDomisianus will become famous soon enoughDomisianus will become famous soon enoughDomisianus will become famous soon enoughDomisianus will become famous soon enoughDomisianus will become famous soon enoughDomisianus will become famous soon enough
Default Re: Mgomo wa wanafunzi wa vyuo vikuu nchini waandaliwa

Migomo kwa vyuo si jambo la kawaida kama ambavyo watu wanasema.tuangalie huu mgomo hawa wasomi wanataka nini na wamekiomba kwa muda gani mpaka sasa na bado selikeli imekaa kimya.It is just a very simple logic kwa nini serikali inakaa kimya kwa mambo ambayo ni ya msingi wakati upuzi inalipuka kama kifuu cha nazi.Hivi kuna haja gani ya kuwepo kwa bodi ya mikopo hapa Tanzania kwa sasa? iondoke haina maana yoyote zaidi ya kuendeleza ubaguzi.Tunaweza kulalamika kwamba kuna kuvuja kwa mitihani lakini tuangalie source ni nini?
Zamani ulikuwa ukipata division III na ukipata udahili ulikuwa unashangilia na unaaga nyumbani kuwa unaenda kusoma na hata kisaikolojia unajiandaa kwenda kusoma. je hiyo hali kwa sas ikoje wana ndugu? Hiyo mishahara wanayolipa wanafanyakazi wa bodi ni shilingi ngapi na matumizi ya kawaida ya kiofisi ni shilingi ngapi kwa mwaka achilia mbali vikao vya kila siku na night?
Inatakiwa ifike wakati tujikomboe kifkira, hizo bilions za walipa kodi zinazokwapulia na manyan'ganyi zingetumika vizuri, tusingeweza kuwalipia ada hao wanafunzi kweli jamani?
Tanzania tuna migodi mingapi na pesa inayopatikana huko inatumikaje kama siyo kuishia kwenye semina elekezi.Mimi naona wafanye mgomo mpaka kieleweke na hiyo bodi ifutiliwe mbali kabisa ili mtu akifaulu asiwekewe mizengwe tena na kuwa na mawazo jinsi ya kupata mikopo.Ni bora hata waongeze pay as you earn ili watu wasome bure na kupata taifa liloelemika lenye mapenzi na nchi yao.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
mgomo, nchini, vikuu, vyuo, waandaliwa, wanafunzi


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Attention Bodi Ya Mikopo Ya Elimu Ya Juu Kwa Wanafuzi(heslb) HKiboka Jukwaa la Elimu (Education Forum) 236 15th October 2009 04:17 PM
Huyu ndiye the real Kikwete! tibwilitibwili Jamii Intelligence 666 3rd May 2009 03:07 AM
Dira ya Elimu Tanzania Rev. Kishoka Jukwaa la Elimu (Education Forum) 38 24th September 2008 05:16 AM
Wanafunzi wa Zaidi 1000 Vyuo Vikuu Wajiunga Na CCM MegaPyne Jukwaa la Siasa 66 8th November 2007 04:01 PM
Prof Msola Kawasilisha Bajeti Halisi Jukwaa la Siasa 5 22nd July 2007 02:09 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 06:23 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com