Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 Oct 2011

    Report Post
    Page 1 of 14 12311 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 261
    1. #1
      nice 2's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th August 2011
      Posts : 699
      Rep Power : 939
      Likes Received
      503
      Likes Given
      285

      Default Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 Oct 2011

      Wana JF,
      Hii ni email kutoka kwa Mh. Zitto Kabwe. Nimeona ni vyema niiweke hapa ili tuweze kujua kwapamoja hali yake inavyoendelea.
      Nawasilisha,
      Nice 2


      Ndugu zangu,

      Kwanza kabisa napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kuniwezesha muda huu kuwa na nguvu za kukaa katika kiti na kuweza kuandika haya machache kwenu. Nawashukuru sana Wanamabadiliko kwa salaam zenu nyingi za pole mara mliposikia ninaumwa na kulazwa hospitalini. Najua hamkuwa na taarifa kamili za kuumwa kwangu na kwa kweli suala la kuumwa ni suala la mtu binafsi (hata kwa mtu mwenye dhamana ya kiuongozi wa umma japo umma nao una haki ya kujua kinachomsibu kiongozi husika).

      Mwanzo

      Nilianza kupatwa na maumivu ya kichwa usiku wa siku ya Ijumaa tarehe 20 jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili kutoka Jimboni tayari kwa kazi za Kamati za Bunge ambapo Kamati yangu ilikuwa imekwishaanza kazi wiki hiyo kwa kupitia mahesabu na utendaji wa Mamlaka za Maji nchini.

      Kama kawaida yangu niliona maumivu hayo makali kama ni sehemu tu ya uchovu wa ziara za Jimboni na safari za mara kwa mara nilizofanya kuinigilia ziara za Jimboni ikiwemo kuhudhuria Mdahalo wa Umeme na Mkutano wa Uwekezaji Kanda ya Ziwa Tanganyika.

      Hivyo nililala na nilipoamka kichwa kilikuwa kimepona na hivyo nikahudhuria kikao cha Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma katika Ofisi ya Bunge mpaka saa saba mchana.

      Siku ya Jumapili saa kumi na moja jioni nikiwa katika Hoteli ya Southernsun nilipatwa na homa kali ghafla. Nilikatisha mkutano niliokuwa nao na kuamua kurejea nyumbani, lakini nilishindwa kuendesha gari na hivyo kumwomba Dereva wa Mhe. Mhonga anifuate ili anisadie kunifikisha nyumbani.

      Nilipofika nyumbani kwangu Tabata, homa ilizidi kupanda na hivyo kuamua kwenda Hospitali mara moja. Nikapelekwa Agakhan Hospital na nikapata huduma.

      Nilipochukuliwa vipimo ilionekana sina malaria wala homa ya matumbo na pia hawakuweza kuona sababu ya homa ile namna ile (maana ilifikia degree 40).

      Walituliza homa, nikapewa Panadol na baadaye nikaruhusiwa kurudi nyumbani mnamo saa tano usiku. Nilipoamka siku ya Jumatatu nikaenda kazini kuongoza Kikao cha Kamati ya Bunge ambapo tulikuwa tunashughulikia Hesabu za Bodi ya Utalii na Benki ya Posta Tanzania.

      Nilipita Agakhan kupata majibu ya ziada na kuambiwa nipo sawa ila nipumzike nisifanye kazi kwa siku kadhaa na nitakuwa sawa.

      Hali kubadilika

      Siku ya Jumanne niliamka nikiwa salama, kichwa kikiuma kwa mbali lakini sio vya kutisha. Nikawajulisha wajumbe wenzangu wa kamati kuwa sitakwenda kazini na wao waendelee na kazi.

      Hata hivyo ilipofika saa sita kamili nilianza kutetemeka mwili mzima na homa kuwa kali sana huku kichwa kikiniuma sana sana sana!

      Dada zangu wakamwita Driver na kunikimbiza Hospitali ya Agakhan. Wakarejea vipimo vilevile na matokeo yakawa yaleyale. Joto lilifika degree 39.8 Hivyo wakanipa dawa za kupoza homa na maumivu ya kichwa kwa drips na sindano kadhaa.

      Siku ya pili hospitalini nikafanya vipimo zaidi ikiwemo ultra sound na vyote kuonekana sina tatizo lolote. Niliendelea kuwepo Hospitali na kwa kweli hali ilikuwa inatia moyo sana kwani nilipata nguvu na hata kuweza kuzungumza, homa ilikuwa imepungua sana.

      Pamoja na kwamba Mganga Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Waziri wa Masuala ya Bunge na Daktari wangu binafsi kuwataka waangalie upya vipimo vya malaria, madaktari wa Agakhan waliwahakikishia viongozi hawa na Daktari wangu kwamba hawajaona Malaria na hivyo wanaendelea na uchunguzi wa 'a trigger' ya homa kali niliyokuwa napata.

      Hali kuwa Mbaya

      Usiku wa siku ya Jumatano Hali ilikuwa mbaya sana. Joto lilipanda tena kufikia 40 na kichwa kuuma zaidi. Nilikuwa kama ninatwangwa kwenye kinu kwa kweli. Nilikuwa natetemeka sana. Ilikuwa taharuki kubwa sana katika chumba nilicholazwa.

      Wageni waliokuwa wamekuja kunijulia hali wakati hali inabadilika ilikuwa ni pamoja na Ndugu Murtaza Mangungu na Mohamad Chombo ambao ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya POAC, walishauri mara moja nihamishwe Hospitali kupelekwa Muhimbili.

      Muda si mrefu kupita Waziri Lukuvi na Katibu wa Bunge walifika, wakaafiki na nikahamishiwa Hospitali ya Taifa Muhimbili na kwa hali niliyokuwa nayo nikalazwa katika Chumba wanachokiita Mini-ICU. Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Mama Blandina Nyoni alikuwepo Hospitalini tayari.

      Usiku huo huo nilifanyiwa vipimo upya. Full Blood picture pamoja na BS. Vile vile kufuatia malalamiko kuhusu maumivu ya kichwa ikaamuliwa kuwa nifanyiwe CT Scan usiku ule.

      Ikaonekana nina wadudu wa Malaria 150 na mara moja nikaanza matibabu. Namshukuru sana Daktari kijana Dkt. Juma Mfinanga kwa umahiri mkubwa aliouonyesha tangu nilipofika pale Mini ICU.

      Asubuhi ya siku ya pili nikapata majibu ya tatizo la maumivu ya kichwa. Nimekuwa nasumbuliwa na kichwa kwa miaka zaidi ya Kumi sasa na katika kipindi hicho mara nne nilipoteza fahamu na kuanguka (Mara ya kwanza mwaka 2000 nikiwa Jijini Mwanza nikielekea kwenye Mkutano wa Vijana wa National Youth Forum, Mara Pili Mjini Dodoma katika mkutano kama huo mwaka 2001 lakini ilikuwa usiku, Mara ya tatu Nikiwa chumbani, Hall II mara baada ya kutoka *Prep, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 2002 na mara ya Nne Bungeni siku ya kupitisha Muswada wa Madini 2010 kufuatia wiki nzima ya Kamati na Mjadala wa Bunge (Ndugu Katulanda anakumbuka siku hii kwani yeye ndiye niliyemkamata njiani kunikimbiza Zahanati ya Bunge).

      Tatizo lililogundulika ni SINUSITIS, ambayo tayari imekuwa sugu. Daktari Bingwa wa magonjwa haya Dkt. Kimaryo akanieleza kwa kirefu juu ya tatizo hili na kuniambia suluhisho ni 'surgery' na pale Hospitali ya Taifa hawafanyi hiyo operesheni. Akashauri niletwe India ambapo kuna Daktari mpasuaji wa ugonjwa huu. Nikakubali.

      Baada ya kuwa Malaria imedhibitiwa kwa kufikia nusu ya 'dozi' nilopewa na wadudu kuonekana kutokomea, Ofisi ya Bunge ikaandaa safari. Nimefika India. Nimebakiza sindano mbili ili kumaliza 'dozi' hiyo na tayari nimefanyiwa taratibu zote kwa ajili ya 'surgery' hiyo.

      Sijafa

      Uvumi ulienezwa nimekufa. Kwa kupitia kwenu ndugu zangu Wanamabadiliko, napenda Watanzania wenzangu wajue mimi ni mzima wa Afya. Nimepata maradhi kama Binadamu mwingine yeyote anavyoweza kupata na namshukuru Mungu kwamba ninapata matibabu mazuri kabisa.

      Shukran
      Nawashukuru sana Madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili chini ya Prof, Mwafongo kwa juhudi kubwa walioonyesha katika kunihudumia. Naishukuru Ofisi ya Bunge kwa Kutimiza wajibu wao kwangu kama Mbunge, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya kwa kuonyesha upendo wa hali ya juu na watumishi wote wa Wizara ya Afya, Katibu Mkuu wa CHADEMA Dkt. Slaa kwa ufuatiliaji wa karibu wa Afya ya Naibu wake, Wabunge wajumbe wa Kamati ya POAC, Dkt. Alex Kitumo, ndugu, jamaa na marafiki zangu wote.

      Nawapa pole wananchi wa Jimbo la Kigoma Kaskazini kwa uvumilivu mkubwa hasa kufuatia uvumi mbalimbali ulioenezwa, pia Watanzania wengine kwa uzito huo huo.

      Nitawajulisha kwa lolote Mungu akipenda. Ninaendelea na matibabu na hali yangu ni nzuri

      Ndugu yenu

      Zitto
      Last edited by nice 2; 30th October 2011 at 09:46.

    2. Miaka 50

    3. #2
      Msharika's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th May 2009
      Posts : 867
      Rep Power : 683
      Likes Received
      44
      Likes Given
      4

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Mwenyenzi mungu akujaalie heri urudi kabla ya Bunge. Tunakuitaji

    4. #3
      Cedar's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th October 2011
      Posts : 12
      Rep Power : 387
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Nakuombea kwa Mungu kaka, Inshaalah upasuaji huo utakuwa salama na wenye matokeo mazuri.
      serio and chaki like this.

    5. #4
      boybsema's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 104
      Rep Power : 455
      Likes Received
      2
      Likes Given
      1

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      pole sana kamanda!Mungu yu pamoja nawe,tunakuombea upone mapema urudi kuchangamsha mjengoni.Get well soon kamanda!

    6. #5
      Kibanikolo's Avatar
      Member Array
      Join Date : 12th August 2011
      Posts : 28
      Rep Power : 398
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Pole sanaa shujaa na mtetea wanyonge,mimi ni padri nilifanya ibaada upone mapema,na Mungu akuepushe na hatari zote .Mungu atakujaria wewe na wenzako wote walioenda kutibiwa huko india amini.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Shiefl's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 31st October 2010
      Posts : 131
      Rep Power : 460
      Likes Received
      30
      Likes Given
      0

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Aksante Mh Zitto kwa taarifa hii. Ni matumaini na maombi yetu kuwa Mwenyezi Mungu atakupa nguvu za kutosha kuhimili hiyo sehemu ya mwisho ya matibabu yako yaani surgery.

      Siisi marafiki zako wapenda mabadiliko tuko nyuma yako tunakuombea kwa dhati kabisa.

      Mungu akutie nguvu upone haraka na kurudi nyumbani mapema kabisa ukatuwakilishe katika Bunge linalofuata.
      serio and KAMALELA like this.

    9. #7
      Panga la Yesu's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 27th April 2009
      Posts : 220
      Rep Power : 557
      Likes Received
      12
      Likes Given
      146

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Mungu Akupe Maisha Marefu, Umjue, Umpende, umtukikie vema na siku moja tufike sote JUU kwake mbunguni
      Pokea Uponyaji kwa jina la Yesu Kristo!

    10. #8
      Kiresua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th May 2009
      Location : DAR/MOROGORO
      Posts : 899
      Rep Power : 690
      Likes Received
      175
      Likes Given
      620

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Ashukuriwe Mungu wa neema nyingi, pole kwa tatizo hil Mh Zitto. Wanamageuzi na wapambanaji na wasio wapambanaji tunakutakia heri katika huduma ya afya utakayopewa huko India. Mungu aliyewajalia uwezo wa kitabibu mabingwa wa tiba duniani atakupitisha hapa salama. Pole sana Kombredi

    11. #9
      TzPride's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2006
      Location : Downhole
      Posts : 1,650
      Rep Power : 973
      Likes Received
      174
      Likes Given
      70

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      tunakutakia afya njema Zitto. Binafsi nakuchuukulia kama kijana wa kwanza Tz kuonyesha vijana ni chachu ya mabadilko. Tunakuombea bwana mdogo.

    12. #10
      dubu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2011
      Posts : 2,396
      Rep Power : 960
      Likes Received
      583
      Likes Given
      143

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      pole sana mkuu.nakutakia upone haraka.samahani mkuu hii ndo id yako mpya?vipi umeonana na mwakyembe?anaendeleaje?msalimi e mwandosya.tunashukuru kwa taarifa.

    13. #11
      Bujibuji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th February 2009
      Location : NYUMBANI PANONO
      Posts : 13,858
      Rep Power : 11197
      Likes Received
      7046
      Likes Given
      5235

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      shetani ameshindwa tunakuombea upone mapema ili urudi na uendeleze uzalendo wako wa kupambana kwa ajiri ya nchi hii ubarikiwe
      mimi05 likes this.

    14. #12
      Mbavu mbili's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 25th April 2011
      Posts : 101
      Rep Power : 429
      Likes Received
      15
      Likes Given
      7

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      pole kwa yote na tunashukuru kwa kuutoa hofu umma wa Tz...koz umesema ukweli kuwa nu ugonjwa sugu ulokusumbua hata kabla ya kuwa MP....thanks ...get recored soon

    15. #13
      JF-BAN1's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 13th April 2011
      Posts : 10,447
      Rep Power : 0
      Likes Received
      3753
      Likes Given
      2889

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Tunakuombea urudi salama, bado Watanzania tunakuhitaji, mchango wako ni mkubwa kwa Taifa hili.

    16. #14
      Mwita25's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 3,852
      Rep Power : 1317
      Likes Received
      1119
      Likes Given
      43

      Default Re: Mh.zitto kabwe apata nafuu, na atoa shukrani kwa wadau wote waliomjulia hali na kumpa pole

      Ngoja tuone

    17. #15
      Hassan J. Mosoka's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 26th October 2010
      Posts : 538
      Rep Power : 0
      Likes Received
      160
      Likes Given
      183

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Mungu akupe neema ya Afya na awasaidie madaktari wanaoelendelea kukuhumia brother

    18. #16
      serio's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Location : dar es salaam
      Posts : 838
      Rep Power : 577
      Likes Received
      78
      Likes Given
      520

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      wish you a quick recovery..
      you lose some, you win some

    19. #17
      gimmy's's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd September 2011
      Posts : 311
      Rep Power : 514
      Likes Received
      39
      Likes Given
      2

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Pole mh zitto pia asante kwa taarifa ilio nyoofu na kuondoa sintofahamu iliojaa juu ya kuugua kwako,amin amin amin nakuambia mungu u pamoja nawe!

    20. #18
      Alexism's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th August 2011
      Location : Iringa Municipal TZ
      Posts : 843
      Rep Power : 565
      Likes Received
      119
      Likes Given
      18

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Get well soon our beloved one.Inshallah

    21. #19
      Mwita25's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2011
      Posts : 3,852
      Rep Power : 1317
      Likes Received
      1119
      Likes Given
      43

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Mungu akusaidie upone haraka mkuu.

    22. #20
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,919
      Rep Power : 6962
      Likes Received
      1066
      Likes Given
      35

      Default Re: Ukweli kuhusu hali ya mh. Zitto Kabwe - 29 oct 2011

      Ahsante sana kaka Kwa taarifa hii ya kina. Tunaendelea kumuomba Mungu aendelee kukusimamia ili upone mapema.

    Page 1 of 14 12311 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011 - Bajeti Mbadala
      By Maxence Melo in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 103
      Last Post: 16th June 2011, 15:32
    2. Mchango wa mheshimiwa Zitto Kabwe Bajeti 2010/2011
      By Ntemi Kazwile in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 10
      Last Post: 14th June 2010, 17:55
    3. Hotuba Ya Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe Kuhusu Miundombinu Bungeni
      By Mpaka Kieleweke in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 39
      Last Post: 18th December 2008, 00:15
    4. Bunge laonya wanaharakati kuhusu Zitto Kabwe
      By BAK in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 28
      Last Post: 19th August 2007, 14:11

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...