Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CUF kwa nini tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa Igunga

    Report Post
    Page 1 of 11 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 212
    1. #1
      Julius Mtatiro's Avatar
      Member Array
      Join Date : 4th September 2011
      Posts : 24
      Rep Power : 393
      Likes Received
      86
      Likes Given
      0

      Default CUF kwa nini tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa Igunga

      Lazima nikiri kuwa washindani wetu wakubwa CCM na CHADEMA wametushinda katika uchaguzi mdogo wa Igunga.

      Kwa matokeo ambayo nimeyashayapokea kutoka kwenye asilimia 88 ya vituo kwa ujumla tumefanya vibaya sana. Japokuwa tumekuwa na mgombea mzuri sana na tumemnadi kwa kutumia uwezo wetu wote ambao kwa hakika kila mtu ameuona, lakini matokeo hatuwezi kuyageuza.

      Ninachojifunza zaidi ni kuwa wapiga kura wengi ndani ya Tanzania bado wanaamini zaidi propaganda kuliko hali halisi ya mazingira yanayowakabili na hii ikizidi kushabikiwa ndivyo ambavyo wananchi watakosa fursa bora siku za mbele.
      Ikiwa hali hii itaendelea hivi ina maana bado nchi ina safari ndefu ya kufikia demokrasia ya kweli na maendeleo yatakayoonekana kwa macho.

      Katika uchaguzi huu wa Igunga CUF tumepambana na changamoto kubwa ya kujibu propaganda zilezile kuwa eti "Sisi ni CCM B", kila tulikoenda tumekutana na kikwazo hiki, tumejaribu kwa dhati kuwaelimisha wananchi bila mafanikio na muda umekuwa ukikimbia kuliko upepo.

      Hata hivyo bado naamini kuwa tutapata fursa kubwa ya kuwaelimisha wananchi siku za usoni. Mimi na wenzangu hatutakata tamaa kwani MAFANIKIO KATIKA NYANJA YA SIASA huhitaji mioyo migumu.

      Natambua kuwa uongozi ni dhamana nzito inayohitaji kujipanga zaidi na zaidi, Na CUF itazidi kujipanga zaidi na zaidi na kila tutakapoanguka tutanyanyuka na kuanza safari, hakika TUTAFIKA.

      Chama changu kinakabiliwa na changamoto kubwa sana mbele ya safari na kwa hakika inahitaji tuzidi kujipanga na kujiimarisha. Kama chama hatutajilaumu kamwe, tumeonesha uwezo mkubwa na kufanya kampeni sahihi tukiwa na mgombea wa kiwango kizuri kwa mpiga kura yeyote anayehitaji kiongozi. Lakini kusimamisha mgombea mzuri na kufanya kampeni nzuri wakati mwingine siyo sababu ya kufanya vizuri. Maamuzi ya nani awe mbunge, ni mzuri au mbaya, anafaa au hafai yako kwa wananchi.

      Wananchi wa Igunga tunawashukuru kwa namna walivyotuunga mkono na tunawaomba wawe kitu kimoja katika kuiendeleza Igunga yao kwani mshindi akishatangazwa yeye ni mbunge wa wananchi wote. Vyama vyetu hivi vipo ili kuisaidia jamii kupata kiongozi mzuri tu, nasi kama chama tumetimiza wajibu wetu.

      Mimi kama kiongozi wa ngazi ya juu wa CUF - Tanzania Bara(Bila kujali nimekuwa kiongozi wa ngazi ya juu miezi minne tu iliyopita tu) nabeba dhamana kwa matokeo yote tuliyopita, najitwika mzigo wa kusimama imara kuiimarisha CUF. Sitatoka CUF na kukimbilia kwenye vyama vyenye nguvu Tanzania bara kama CHADEMA n.k. eti kwa sababu tu CUF imefanya vibaya kwenye uchaguzi. Ninaamini katika CUF na nitaisaidia Tanzania yangu nikiwa CUF, ninaamini siku moja wakati CUF imeimarika nitatajwa kati ya watu ambao hawakukata tamaa na hawakuyumbishwa na magumu yaliyowakabili na walisimama kidete kwenda mbele.

      Tunawashukuru wale wote waliotuunga mkono katika uchaguzi huu na wale wanaotuunga mkono siku zote na wale watakaotuunga mkono siku zijazo. Kwa hakika wote tunawashukuru sana na CUF itasimama imara.

      Mungu awabariki sana.

      "HAKI SAWA KWA WOTE"

      Julius Mtatiro,
      Naibu Katibu Mkuu,
      Chama Cha Wananchi - CUF,
      Tanzania Bara,
      02 Oktoba 2011,
      Igunga - Tabora.

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      kiche's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 339
      Rep Power : 545
      Likes Received
      105
      Likes Given
      0

      Default Re: Mtaji wa CUF igunga

      Quote By Jidundufila
      Nakumbuka wakati kampeni zinaaoza CUF walisema wameanza na mtaji wa kura 11 elfu je umeyeyukia wapi?
      Hazijayeyuka mkuu!!!!,bado wanaendelea kuhesabu!,kumbuka wapiga kura wapo 170000!!!!zilizohesabiwa hata hizo 11,000 bado!tuwasubiri

    4. #3
      Wizzo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th November 2010
      Location : Arusha
      Posts : 432
      Rep Power : 515
      Likes Received
      79
      Likes Given
      34

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      poa..umeongea vizuri bigup
      Saint Ivuga likes this.

    5. #4
      Kiranja Mkuu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th February 2010
      Posts : 2,084
      Rep Power : 886
      Likes Received
      284
      Likes Given
      34

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      Vunjeni ndoa yenu na CCM na acheni siasa za udini
      Nyumbu-, wende, Lyceum and 1 others like this.

    6. #5
      sweetlady's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 24th December 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 15,307
      Rep Power : 36527
      Likes Received
      7468
      Likes Given
      4604

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      Poleni sana!

    7. Miaka 50

    8. #6
      Eshacky's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th April 2011
      Posts : 824
      Rep Power : 576
      Likes Received
      155
      Likes Given
      3

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      Poleni sana,ila "kama huwez kupingana nao bas jiunge pamoja nao", huo msemo mwepesi hauitaji Phd kuuelewa na kuutekeleza.

    9. #7
      chomete's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Posts : 1,056
      Rep Power : 637
      Likes Received
      107
      Likes Given
      0

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      huo ni ukomavu wa kisiasa na unatakiwa uwe ngangali

    10. #8
      Nemesis's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th February 2008
      Posts : 2,654
      Rep Power : 1515
      Likes Received
      31
      Likes Given
      91

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      pole mkuu, mnatakiwa kuwa wapinzani wa kweli siyo wavuruga upinzani, mlipoiponda cdm mlitegemea nini?
      Kaa la Moto, Lyceum and Kalila like this.


    11. #9
      samirnasri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 1,210
      Rep Power : 674
      Likes Received
      169
      Likes Given
      50

      Default Re: Mtaji wa CUF igunga

      hawakujua tu hizo zilikuwa za chadema jamaa wakaamua kupigia cuf kwa kuwa cdm hawakuweka mgombea.

    12. #10
      DASA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Location : JF
      Posts : 1,000
      Rep Power : 624
      Likes Received
      260
      Likes Given
      220

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      Quote By chomete
      huo ni ukomavu wa kisiasa na unatakiwa uwe ngangali
      Hamia Chadema.

    13. #11
      jnuswe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 460
      Rep Power : 525
      Likes Received
      96
      Likes Given
      0

      Default Re: Ule mtaji wa kura 11,000 za CUF uko wapi Igunga?

      Quote By chiborie
      Kwamujibu wa matoeo ya awali jimboni Igunga, inaonekana dhahiri shahiri kua CUF sio washindani. Sasa najiuliza ule mtaji waliokua wanajivunia hadi kufikia hatua ya kuwaomba CDM wajitoe umekwenda wapi?
      CUF bara haina nguvu na haitatokea kuja kupata kuwa na nguvu, na ile ndoa ndo kabisaa imewamaliza labda waachike ndo watapanda chart

    14. #12
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,002
      Rep Power : 2557
      Likes Received
      781
      Likes Given
      28

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      Ule mtaji wao umeishia wapi ? Yeye si alidhani kwamba KAFU ni chama huku bara ? Yule naye ni chaka mwache ale posho maana akienda kokote hawezi kupokelewa mwache atumike tu .
      Nasema : CCM tunadhani adui yetu ni Chadema hapana ni Watendaji wetu katika Serikali ya CCM tukawabane hao - Livingstone Kibajaji Lusinde 2013 25 April at 11:54am.

    15. #13
      Bei Mbaya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th November 2010
      Posts : 1,169
      Rep Power : 663
      Likes Received
      299
      Likes Given
      167

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      yoyote awaye vuguvugu amelaaniwa
      Kama si ombwe la Uongozi, kama si udhaifu wa serikali; wallahi kusingekuwepo hiki kinachoitwa 'udini' na ugaidi.

    16. #14
      jambo1's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th July 2009
      Posts : 243
      Rep Power : 626
      Likes Received
      28
      Likes Given
      40

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      Quote By Julius Mtatiro
      Katika uchaguzi huu wa Igunga CUF tumepambana na changamoto kubwa ya kujibu propaganda zilezile kuwa eti "Sisi ni CCM B", kila tulikoenda tumekutana na kikwazo hiki, tumejaribu kwa dhati kuwaelimisha wananchi bila mafanikio na muda umekuwa ukikimbia kuliko upepo.

      Hata hivyo bado naamini kuwa tutapata fursa kubwa ya kuwaelimisha wananchi siku za usoni. Mimi na wenzangu hatutakata tamaa kwani MAFANIKIO KATIKA NYANJA YA SIASA huhitaji mioyo migumu.

      Natambua kuwa uongozi ni dhamana nzito inayohitaji kujipanga zaidi na zaidi, Na CUF itazidi kujipanga zaidi na zaidi na kila tutakapoanguka tutanyanyuka na kuanza safari, hakika TUTAFIKA.

      Chama changu kinakabiliwa na changamoto kubwa sana mbele ya safari na kwa hakika inahitaji tuzidi kujipanga na kujiimarisha. Kama chama hatutajilaumu kamwe, tumeonesha uwezo mkubwa na kufanya kampeni sahihi tukiwa na mgombea wa kiwango kizuri kwa mpiga kura yeyote anayehitaji kiongozi. Lakini kusimamisha mgombea mzuri na kufanya kampeni nzuri wakati mwingine siyo sababu ya kufanya vizuri. Maamuzi ya nani awe mbunge, ni mzuri au mbaya, anafaa au hafai yako kwa wananchi.

      Wananchi wa Igunga tunawashukuru kwa namna walivyotuunga mkono na tunawaomba wawe kitu kimoja katika kuiendeleza Igunga yao kwani mshindi akishatangazwa yeye ni mbunge wa wananchi wote. Vyama vyetu hivi vipo ili kuisaidia jamii kupata kiongozi mzuri tu, nasi kama chama tumetimiza wajibu wetu.

      Mimi kama kiongozi wa ngazi ya juu wa CUF - Tanzania Bara(Bila kujali nimekuwa kiongozi wa ngazi ya juu miezi minne tu iliyopita tu) nabeba dhamana kwa matokeo yote tuliyopita, najitwika mzigo wa kusimama imara kuiimarisha CUF.
      Sitatoka CUF na kukimbilia kwenye vyama vyenye nguvu Tanzania bara kama CHADEMA n.k.
      eti kwa sababu tu CUF imefanya vibaya kwenye uchaguzi. Ninaamini katika CUF na nitaisaidia Tanzania yangu nikiwa CUF, ninaamini siku moja wakati CUF imeimarika nitatajwa kati ya watu ambao hawakukata tamaa na hawakuyumbishwa na magumu yaliyowakabili na walisimama kidete kwenda mbele.
      Hapo kwenye rangi ya Magamba..,mi nadhani Chadema hikina nafasi yako kwa sasa..,lakini kama utakuwa mwanachama mwaminifu kama mimi karibu sana vinginevyo..rudi wa "CCM A" kabisa..!
      Lyceum and Mwanyasi like this.

    17. #15
      Jackbauer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th October 2010
      Location : CTU
      Posts : 4,873
      Rep Power : 1690
      Likes Received
      1348
      Likes Given
      277

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      najua umeshapata matokeo ya awali,tueleze mwenenendo wa matokeo unadhani nani ni mshindi?be honest!
      You may succeed in silencing me but that silence comes at a price-Alex litvinenko

    18. #16
      Hossam's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 2nd September 2011
      Posts : 192
      Rep Power : 428
      Likes Received
      73
      Likes Given
      0

      Default

      Pole kamanda, hilo ndo tatizo la uke wenza, mke mkubwa akikasirika basi bi mdogo huambulia sms fupifupi tu, hiyo ndo faida ya kujidai mnakiherehere kuingia muafaka wa kijinga zenji sasa inawakosti, ni afadhali watu wafe ila haki itendeke, sasa maalim seif anachonga tu sharafu zake huko ikulu zenji wewe unaambulia vumbi, jaribu kukua kaka...

    19. #17
      Katavi's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 31st August 2009
      Location : Lyamba Lya Mfipa
      Posts : 19,551
      Rep Power : 16758
      Likes Received
      2474
      Likes Given
      1841

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      Poleni sana, ni muda muafaka wa kujichunguza mlipojikwaa na kujipanga upya.

    20. #18
      politiki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Posts : 1,362
      Rep Power : 1338
      Likes Received
      714
      Likes Given
      128

      Cool Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      Pole sana kwa pilikapilika za uchaguzi,

      Mmejitahidi ingawa kura hazikutosha lakini nina ushauri kwa CUF ingawa leo siyo siku yake lakini ninachoweza kukisema ni kwamba CUF needs seriuos reform kama kweli chama hiki kinataka kuwa na future hasa kwa Tanzania-bara nitakushauri nini cha kufanya wakati mzuri ukiwadia kwa hivi sasa nawatakia mapumziko mema na hongereni sana kwa kupigana mpaka dakika za mwisho ingawaje press iliwaangusha sana kwa kutowapa coverage ya kutosha jihandae kwa kupata ushaurri wangu na wengineo.

    21. #19
      tortoise's Avatar
      Member Array
      Join Date : 6th October 2010
      Posts : 37
      Rep Power : 444
      Likes Received
      5
      Likes Given
      5

      Default

      Mkuu naona unawajengea Ccm mazingira ya uchakachuaji ili wakitangazwa washindi kwa Wizi wa kura chadema nao waige uungwana wenu bandia wa kukubali matokeo !

    22. #20
      palalisote's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th August 2010
      Location : WA HAPAHAPA
      Posts : 2,052
      Rep Power : 2036
      Likes Received
      925
      Likes Given
      3819

      Default Re: Cuf tumefanya vibaya sana katika uchaguzi mdogo wa igunga - mtatiro

      " The history we read is not based on facts at all but rather the series of accepted judgments"

    23. Study Abroad
    Page 1 of 11 123 ... LastLast

    LinkBacks (?)


    Similar Topics

    1. Replies: 1
      Last Post: 7th October 2011, 15:49
    2. Replies: 2787
      Last Post: 1st October 2011, 20:35
    3. Chadema na CCM wanawakati mgumu sana uchaguzi mdogo Igunga.
      By Apta Kayla in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 7
      Last Post: 14th July 2011, 20:07

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...