Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: CCM, CUF vyajibu mapigo ya Chadema; Dr. Kafumu Mkichagua Chadema hawawezi kuitoa CCM madarakani

    Report Post
    Results 1 to 5 of 5
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,149
      Rep Power : 3543
      Likes Received
      3036
      Likes Given
      460

      Default CCM, CUF vyajibu mapigo ya Chadema; Dr. Kafumu Mkichagua Chadema hawawezi kuitoa CCM madarakani

      *Vyaanza kutumia helkopta kukamilisha kampeni zao
      *Magufuli aunguruma, aahidi kutoa bajeti maalumu
      *Rage apigwa faini 100,000/- kukampeni na bastola


      Na Benjamin Masese, Igunga

      VYAMA vya CCM na CUF vimefanikiwa kujibu mapigo ya CHADEMA katika kampeni za
      lala salama katika Jimbo la Igunga baada ya kuanza rasmi matumizi ya helkopta ili kufikia maeneo mengi zaidi.

      Helkopta hizo ambazo juzi zilikwama kufika Igunga, jana ziliwasili kwa nyakati tofauti, ambapo ya CCM iliwasilia asubuhi na kuanza kazi huku ya CUF ikiwasili jioni ikitarajiwa kuanza kazi leo.

      Helkopta hiyo ya CCM ilitua katika viwanja vya Sabasaba saa 4:00 asubuhi na kulakiwa na umati wa wapenzi na mashabiki wa CCM na wafuasi wa vyama vingine

      Magufuli na bajeti maalumu

      Katika mkutano wa CCM, Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli jana alitinga Igunga na kueleza kwamba atatoa bajeti maalumu kwa ajili ya barabara na daraja la Mbutu ambalo limekuwa likilalamikiwa sana na wananchi wa Igunga kwa miaka zaidi ya 10.

      Akihutubia mkutano wa hadhara wa kampeni za mgombea ubunge wa CCM jimbo la Igunga, Dkt. Dalaly Kafumu katika viwanja vya Sabasaba, Dkt. Magufuli alisema katika mwaka wa fedha wa 2012/2013 Wizara yake itatoa bajeti maalumu ili kuhakikisha barabara za Igunga zinatengenezwa na kuwa katika hali nzuri tofauti na ilivyo sasa.

      Alisema serikali inayoongozwa na Chama Cha Mapinduzi imejitahidi katika upande wa barabara katika Mkoa wa Tabora, na baadhi yake zipo katika matengenezo kwa kiwango cha lami.

      Alizitaja barabara hizo kuwa ni ile ya kutoka Igunga hadi Shelui yenye urefu wa Kilometa 110, Tabora hadi Nzega (km. 115) na Tabora hadi Urambo Kilometa 90 ambazo kwa pamoja zimeanza kujengwa kwa kiwango cha lami.

      “Hawa wenzetu wanashangaza sana, wakati wanasema CCM haijafanya chochote kwa miaka 50, wanatoka Dar es Salaam kuja na kupita kwenye barabara hii nzuri ya lami hadi Igunga iliyojengwa na CCM, hawa watu kweli wanasema wanachokiamini?”

      “Msiwachague wale ambao katika kupitisha bajeti wanatoka, je, watajengewaje barabara?”

      “Ndugu wana Igunga, achaneni na uongo wa Chadema na CUF, leo hii mkichagua Chadema, hata wakipata wabunge wengine 10 hawawezi kuitoa CCM madarakani, nawaombeni vyama vyote kura zote kwa Dkt. Kafumu ili akafumue maendeleo ya Igunga,” alisema.

      Aidha Dkt. Magufuli alimgeuzia kibao Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) na mgombea ubunge wa chama hicho, Bw. Leopald Mahona kwamba kitendo cha wao kwenda kwenye ufunguzi wa kampeni zao huku wakiwa wamepanda wanyama (Punda) ni kosa kwa mujibu wa sheria za wanyama No. 18 na 19 ya mwaka 2008, sheria hiyo ya ustawi wa wanyama ya mwaka 2008 inazuia kuwatumia wanyama kwa mtindo huo,” alisema.

      Awali Dkt. Magufuli aliwaeleza wananchi hao kuwa amekwenda Igunga kama Waziri wa CCM, ambaye ametumwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa wamchague Dkt. Kafumu kwa sababu ana sifa zote za uongozi.

      “Nilisikia kuna mmoja wa wagombea anasema mkimchagua atajenga daraja la Mbutu kwa siku 60, wakati daraka hilo lina kilometa tatu, linatakiwa kujengwa tuta kwanza na madaraja mengine matatu, lakini cha kushangaza wakati tunapitisha bajeti hawa wenzetu wa CUF na Chadema huwa wanaondoka nje ya Bunge, sasa nawaambia nikitoka hapa nakwenda kukagua daraja la Mbutu,” alisema.

      Naye Mbunge wa Bumbuli Bw. Januari Makamba aliwaeleza wananchi waliofurika katika mkutano huo kuwa dunia nzima imeelekeza macho Igunga, kwamba CCM itaibuka mshindi na kumpeleka Dkt. Kafumu bungeni.

      “Dunia nzima inawaangalieni wana Igunga, msituletee mtu anayekwenda kuomba mwongozo bungeni, mgombea wa CCM, Dkt. Kafumu ni mzito kuliko wengine, kuanzia uwezo, uzoefu, usomi na maarifa,” alisema Bw. Makamba.

      Vijana Chadema wakamatwa

      Katika hatua nyingine vijana watatu wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa Chadema walikamatwa na walinzi wa CCM maarufu kwa jina la Green Guard katika mkutano uliofanyika katika uwanja wa mpira Igunga muda mfupi baada ya helkopita ya chama hicho kuwasili.

      Tukio hilo lilitokea jana saa sita mchana baada ya Waziri
      wa Nchi Ofisi ya Rais, Mahusiano ya Umma, Bw. Stephen Wassira
      kuwauliza wananchi waliokuwa katika mkutano huo kama watakipigia kura Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo baadhi ya vijana walionesha alama ya 'V' inayotumiwa na Chadema.

      Bw. Wassira alilazimika kuuliza kama kuna vijana wa Chadema
      na hakuna aliyenyosha mkono, ndipo alishukuru kwa kutokuwepo kwa vijana hao, lakini ghafla walianza kupiga kelele na miruzi na vigelegele kutoka kila kona ya viwanja huku wakitamka 'Peoples Power' kaulimbiu inayotumiwa na Chadema ikimaanisha nguvu ya umma.

      Baada ya kelele hizo, walikuwepo walinzi wa CCM ambao hawakufurahishwa na hali hiyo waliwakamata vijana watatu na kuwaingiza kwenye gari lao la ulinzi lenye Namba za Usajili T 479 ABT Toyota Land Cruser Hard Top na kuondoka
      uwanjani hapo kwa mwendo wa kasi na kuelekea kusikojulikana.

      Baada ya gari hilo kuondoka, vijana wengine waliondoka mkutanoni hapo na kwenda kufunga barabara iendayo Kituo cha Mabasi Igunga ili kulizuia gari hilo lililoteka wenzao.

      Kutokana na tafrani hiyo waandishi wa habari walilazimika
      kufika Kituo cha Polisi Igunga ili kujua kama vijana waliochukuliwa na Green Guard wamefikishwa hapo lakini Mkuu wa Kitengo cha Tathmini, Ufuatialiaji na Upelelezi wa Makosa ya jinai kutoka Makao Makuu, Bw. Isaya Mngulu hakuwepo
      kituoni.

      Alipotafutwa kwa njia ya simu alisema kuwa yupo nje ya
      kituo na kuomba muda ili kuliwasiliana na kikosi chake.

      Ilipotafutwa baadaye alisema kuwa kwa mujibu wa taarifa
      alizopata vijana waliokamatwa na CCM wamefikishwa kituoni hapo saa nane mchana.

      “Taarifa nilizo nazo vijana hao wamefikishwa kituoni na wengine tuliowakamata maeneo mengine, sielewi hizi siasa zinafanywaje?" alihoji Bw. Mungulu.

      Mkutano wa Bw. Wassira haukuwa na ulinzi wa Jeshi la
      Polisi kwa kuwa haukuwa katika ratiba ya mikutano
      ya kampeni. Polisi walifika katika eneo hilo baada ya
      kupata taarifa za kutekwa kwa wafuasi wa Chadema.

      Baada ya kumalizika mkutano huo viongozi wa CCM wakiwemo
      Mjumbe wa Baraza Kuu la Vijana UVCCM, Bw. Hussein Bashe
      pamoja na wabunge wa wawili, Bw. Januari Makamba wa Jimbo la
      Bumbuli na Bw. Aeshi Hilaly wa Jimbo la Sumbawanga Mjini
      walikwenda katika Ofisi za Chadema kufanya mazungumzo juu
      ya tukio hilo.

      Viongozi hao walikutana na Katibu Mkuu wa Chadema, Dkt.
      Willibrod Slaa na kumweleza suala hilo ambapo aliwataka
      waseme vijana hao walipopelekwa.

      Wakati mazungumzo yakiendelea vijana walizidi kufika katika ofisi hiyo na kutaka kuwashambulia viongozi hao wa CCM kwa lengo la kulipiza kisasi, huku wakiwataka kuwaonesha vijana wenzao walikofichwa.

      Dkt. Slaa alilazimika kuwatuliza na kuwaeleza kwamba wamefika hapo kwa nia ya kuomba radhi kwa kitendo walichokifanya, hivyo hakuna sababu ya kuendelea kuwazonga.

      “Vijana wangu hao hawakuja hapa kwa nia ya mbaya, hata hivyo hawana ubavu wa kuja hapa kupamba na Chadema, acheni tuwasikilize. Wameanza kwa kuniomba radhi kwa kitendo walichokifanya kwa wanachama wetu," alisema Dkt.
      Slaa.

      Mbali ya Dkt. Slaa kuwatuliza, bado walizidi kupandisha
      mukhari na jazba wakimtaka Bw. Hilaly aondoke kwenye eneo
      hilo na kubaki Bw. Makamba na Bw. Bashe kwani hao wanaoneka
      kuwa na uungwana.

      Bw. Bashe alilazimika kusimama na kusema: "Kwa hekima ya hali ya juu vijana tunapaswa kuwa watulivu kwani wote ni Watanzania, hatupaswi kugombana kwa jambo ambalo tunalishughulikia, tungekuwa wabaya tusingekuja hapa," alisema na kuongeza:

      “Kwanza mimi ni jirani yenu wa hapo Nzega tunataka kampeni
      ziishe vizuri ili Igunga tuiache salama, tatizo la vijana
      wenzenu waliokamatwa tumeshalimaliza kwa lugha safi, tunakwenda kuwatoa,” alisema na vijana hao kushangilia.

      Akizungumza na Majira Dkt. Slaa alisema kuwa siku zote
      Chadema haianzishi fujo bali zinaanzishwa na CCM na kuongeza
      kwamba ndio maana walifika hapo kuomba radhi na katika
      kazungumzo yetu nimewaeleza wawaachie vijana hao na tayari
      wako nje.

      "Vijana waliokamatwa sijawaona kwa macho yangu na sina
      majina yao lakini nasikia wamekamatwa, binafsi nachotaka
      wawe huru na sitaki kusikia tena CCM inawanyima uhuru
      vijana wangu, nimewaonya," alisema.

      Rage apigwa faini

      Mbunge wa Tabora Mjini, Bw. Ismail Rage ametozwa
      faini la sh. 100,000 kwa kosa la kuhutubia mikutano ya
      kampeni za uchaguzi mdogo wa Igunga akiwa na silaha aina
      bastola.

      Hatua hiyo ilifikiwa baada ya Kamati ya Maadili kuketi na
      kujadili suala hilo na kufikia hatua hiyo.

      Akitangaza faini hiyo jana baada ya kikao kumalizika,
      Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Igunga, Bw. Magayane Protace alisema
      kuwa kutokana na kosa hilo kamati imeamuru kutozwa faini
      hiyo na kuonywa kutorudiwa kitendo hicho.

      Alisema kuwa faini hiyo imetolewa wakati huo huo ambapo
      aliwaonya viongozi na wanasiasa wengine wenye tabia hiyo
      kuacha mara moja.

      HELIKOPTA YA CCM:



      Mratibu wa Kampeni za CCM, Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Bw. Mwigulu Nchemba akimlaki Januari Makamba baada ya helkopta aliyokuja nayo kutua kwenye Uwanja wa Sabasaba mjini Igunga jana. Kushoto ni Katibu Msaidizi Mkuu Itikadi na Uenezi, Bw. Sixtus Mapunda. Helkopta hiyo itatumika katika kipindi cha lala salama cha kampeni za chama hicho jimboni humo.

      CHADEMA HELIKOPTA - inaonekana kubwa zaidi ya CCM...



      CHADEMA started using a helicopter in the campaign on Tuesday
      Thousands of Igunga residents are now left to choose between listening to speeches by politicians and candidates running for the parliamentary seat for their constituency or admire helicopters hopping around and pulling big crowds.
      Last edited by nngu007; 29th September 2011 at 20:19.

    2. Miaka 50

    3. #2
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,149
      Rep Power : 3543
      Likes Received
      3036
      Likes Given
      460

      Default Re: CCM, CUF vyajibu mapigo ya Chadema; Dr. Kafumu Mkichagua Chadema hawawezi kuitoa CCM madarakani

      Yaani kila mtu IGUNGA isipokuwa Nape Nnauye???

    4. #3
      Feedback's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2011
      Posts : 4,086
      Rep Power : 1244
      Likes Received
      2061
      Likes Given
      1123

      Default Re: CCM, CUF vyajibu mapigo ya Chadema; Dr. Kafumu Mkichagua Chadema hawawezi kuitoa CCM madarakani

      Nyingi ya thread zako ingawa ni za copy and paste lakini huwa zinakuja zimechelewa sana asante lakini.
      Only in Tanzania

    5. #4
      UmkhontoweSizwe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th December 2008
      Posts : 1,991
      Rep Power : 929
      Likes Received
      547
      Likes Given
      319

      Default

      Quote By nngu007
      Yaani kila mtu IGUNGA isipokuwa Nape Nnauye???
      JK kwani yuko Igunga?

    6. #5
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,149
      Rep Power : 3543
      Likes Received
      3036
      Likes Given
      460

      Default Re: CCM, CUF vyajibu mapigo ya Chadema; Dr. Kafumu Mkichagua Chadema hawawezi kuitoa CCM madarakani

      Quote By Feedback
      Nyingi ya thread zako ingawa ni za copy and paste lakini huwa zinakuja zimechelewa sana asante lakini.
      wow i did not know that... thanks 4 your Heartfelt consideration...

    7. Study Abroad

      FemaTV & Radio

    Similar Topics

    1. Tetesi: Ruge naye anazimikia mapigo ya CHADEMA?
      By Dullo in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 26
      Last Post: 30th September 2011, 21:25
    2. Replies: 20
      Last Post: 6th September 2011, 21:53

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...