Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kikwete ataka wabunge CCM waikosoe Serikali

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 22
    1. #1
      Mwanagenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2006
      Location : Mtandaoni
      Posts : 762
      Rep Power : 806
      Likes Received
      10
      Likes Given
      10

      Default Kikwete ataka wabunge CCM waikosoe Serikali

      Kama wabunge watafanya kweli labda tunaweza kupiga hatua kweli...Lakini sijui kama ni kweli!


      Mwandishi Wetu
      HabariLeo; Tuesday,February 13, 2007


      RAIS Jakaya Kikwete amewaeleza wabunge wa CCM wawe huru kuikosoa serikali mradi wawe na ushahidi na hoja zao. Katika semina ya siku moja iliyofanyika Dar es Salaam juzi, rais aliwaambia wabunge hao kuwa hayuko tayari kulinda watu wachafu ndani ya serikali yake, hivyo akatoa mwito kwa wabunge kufichua mambo yanayoenda kinyume na maadili ya uongozi.

      “Rais alichotueleza anataka tuwe wasafi kuanzia kwenye chama na serikalini,” kilisema chanzo kimoja cha habari kilichohudhuria semina hiyo. Katika kile kinachoonekana ni kuelekezwa juu ya majukumu yao wakiwa kama wabunge wa chama tawala, Rais Kikwete katika kikao hicho aliwataka wabunge hao kuisaidia serikali katika kutekeleza majukumu yake kwa kuikosoa wanapoona mambo hayaendi.

      Chanzo hicho kilidokeza kuwa rais amewapa meno wabunge hao kuhakikisha wanatimiza jukumu lao la kuisaidia serikali lakini pia na kuwa huru kuikosoa. “Siyo kwamba hataki tuikosoe serikali, lakini anataka tuwe na ushahidi wa kile tunachokosoa,” kilisema chanzo hicho cha habari.

      Habari hizo zilieleza kuwa Rais Kikwete aliwapa meno wabunge hao lakini pia akawatahadharisha kuwa siyo vizuri kupinga kila kitu wakati hawana ushahidi. Rais pia aliwaeleza kuwa hayuko tayari kulinda watu wachafu ndani ya serikali yake hivyo akatoa mwito kwa wabunge kufichua mambo yanayoenda kinyume na maadili ya uongozi.

      Mtoa taarifa mwingine alilidokeza gazeti hili kuwa Rais Kikwete baada ya mada ya Spika wa zamani wa Bunge, Pius Msekwa, aliwashauri wabunge hao wawe wazi lakini pia wasitoe hoja za kubuni na kutunga ambazo haziwezi kuisaidia serikali. “Alitushauri tusikurupuke lakini akataka tuwe wawazi na wakweli tunapoona kuna upungufu…lakini pia amesisitiza mwenye ushahidi asiogope kusema,” alisema mtoa habari.

      Awali taarifa iliyotolewa na Ikulu ilisema semina hiyo ilikuwa na mada moja tu kuhusu Kanuni na Majukumu ya Msingi ya Wabunge na Wawakilishi wa Chama Tawala (CCM) katika mfumo wa vyama vingi vya siasa.

      Katika mada yake hiyo, Msekwa kutokana na uzoefu wake wa utumishi ndani ya chama na katika Bunge alielezea na kufafanua kwa kina maudhui ya kanuni za kamati za wabunge na wawakilishi wa CCM.

      Semina hiyo iliwahusisha Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Walishiriki semina hiyo kama wajumbe wa kamati ya wabunge na wawakilishi wa CCM kwa ajili ya kupigwa msasa. Ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa jengo la Ubungo Plaza.

      Ilielezwa kuwa washiriki hao waliijadili kwa kina mada hiyo na kutoa michango ya mawazo yao kwa uwazi na ukweli, na kueleza kuwa semina hiyo ilikuja wakati mwafaka na imekuwa ni elimu tosha kwao kuhusu jinsi ya kutekeleza majukumu yao.

      Rais Kikwete aliahidi kuwa semina kama hiyo zitakuwa zinafanyika mara kwa mara ili kupata fursa ya kubadilishana mawazo na kukumbushana mambo mbalimbali.
      ____________
      Ili Tuendelee Tunahitaji Dikteta mwenye Uzalendo na Visheni
      _____________
      "UTU BUSARA UJINGA HASARA,
      "TUPINGANE BILA KUPIGANA"


    2. #2
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,048
      Rep Power : 2571
      Likes Received
      794
      Likes Given
      29

      Default

      Usaanii mkubwa huu. Maana haiwezekani akakosa kutaa kusifiwa . Yeye anasema haya jioni mshikaji wake EL anawaita kama Kamati ya Chama na uzuia hoja nk . Ujinga mtupu . Yeye mwenyewe rais si msafi anawezaje kuwakoromea wenzake ?

    3. #3
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,768
      Rep Power : 7665
      Likes Received
      4931
      Likes Given
      4509

      Default

      Lunyungu,

      Binafsi sioni kama huu ni usanii hata kidogo!
      CCM ndugu yangu sasa hivi imefikia mahala ambapo kila mtu na mzigo wake. Kuna mengi yanatokea bungenia ambayo wewe na mimi hatuyafahamu. Watu wanazimwa ovyo kwa vitisho na JK anaposema maneno haya kidogo inawapa nafasi ya kuhoji.
      Na kulingana na habari nilizozipata kuna watu wamemdokeza JK kuwa hawana nguvu wanaogopa nafasi zao bungeni kuwa katika klitabu cheusi pindi wakisema ukweli. Na kila dokezo lilikuwa likimaanisha kikwazo ni EL.

      Amina Chifupa mfano mdogo sana na wapo wengi kama yeye lakini hawana ubavu, ulimi mzito wakifikiria familia zao. Siku hizi Bongo napo kuna media za kuzusha visa kwa viongozi kutaka kuharibu majina yao na media hizi wanalipwa kufanya ufisadi huo.
      Kwa hiyo sasa hivi tutaweza kuyasikia madongo vizuri kwani JK hayupo bungeni na hawezi kuzuia midomo ambayo kaipa uwezo wa kubaini.
      Exploration of reality

    4. #4
      Kazi Ndiyo Kipimo Cha Utu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th March 2006
      Posts : 1,726
      Rep Power : 1026
      Likes Received
      55
      Likes Given
      6

      Default

      Mkandara,
      Hawa ndiyo tabia yao ,wanasema hili halafu wanatenda lile.Wabunge wa CCM ndani ya bunge hawana ubavu wa kusema lolote labda kama hawataki kupitishwa tena.Hili bunge la sasa ni afadhali bunge letu la chama kimoja lilikuwa hai kulikoni hili la leo.Mwalimu watu wanasema haambiliki lakini bunge la enzi yake lilikuwa huru zaidi kueleza na kujadili mambo mbali mbali ya taifa,kimataifa na yanayowahusu wapiga kura katika majimbo mbali mbali nchini.Lilikuwa lenye heshima na madhubuti!

    5. Ole is offline
      Ole
      #5
      Ole's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th December 2006
      Posts : 1,125
      Rep Power : 869
      Likes Received
      10
      Likes Given
      8

      Default

      JK ndio zake. kama unakumbuka alisema tena juzi juzi tu kwamba hataki kusifiwa kinafiki matokeo yake yako wapi? Tangu lini uliona mla rushwa akawakamata wala rushwa wenzie. Kama walifikiri Watanzania wote tumelala wamejidanganya.


    6. #6
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,623
      Rep Power : 46738
      Likes Received
      16722
      Likes Given
      8562

      Default

      Hivi walipoapa na Katiba Mkononi walifikiri wanatania? Sifikiri semina ya siku moja inatosha... inahitaji wiki nzima...
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    7. #7
      Kichuguu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th October 2006
      Location : Popote Porini
      Posts : 6,857
      Rep Power : 3280
      Likes Received
      1342
      Likes Given
      930

      Default

      Wabunge kukoosoa serikali siyo utamaduni wa Tanzania. baadhi wa wabeunge wanamezea mate uwaziri au ukuu wa mkoa kwa hiyo hawawezi kumkemea bosia anayetoa vyeo hivyo
      Kichuguuu: Nyumba inayohifadhi mchwa na nguchiro kwa pamoja bila mkwaruzo

    8. #8
      Halisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th January 2007
      Posts : 3,037
      Rep Power : 2182
      Likes Received
      455
      Likes Given
      243

      Default

      Naona hilo gazeti halikupata habari kamili. Kwa kweli katika kikao hicho, JK aliweka wazi, "Muko huru kujadili kila kitu kama vile Richmond na mengine yote, mradi tu muwe na ushahidi wa kutosha," hiyo ni baada ya EL kusema kwamba Richmond ni majungu na maneno yasiyo na ushahidi wowote. Akibuka Mwenyekiti wa Kamati ya Biashara na Uwekezaji, Williami Shelukindo, yeye akasema, "Hakuna tatizo lolote katika Richmond", akaibuka mjumbe wa kamati ya uwekezaji, Ole Sendeka (wa Simanjiro), akasema, "Kwa kweli Mwenyekiti wangu hakusema yote, tulitembelea Richmond, na wajumbe wenzetu wakamati ya uwekezaji na biashara, wengine wakiwa ni wa upinzani, tuliona mambo mengi yasiyofaa na tumekuta wamo wakubwa," akaibuka Hamisi KAgasheki (wa Bukoba Mjini), akasema ndani ya Richmond kuna wakubwa na humu ndani wabunge wanajua, ila wanaogopa kusema, ni lazima tuseme", akaibuka Wilson Masilingi (wa Muleba), akasema, "kuna tatizo ndani ya serikali, kwanini Dk, Ibrahim Msabaha aanze kujibu hoja za Wizara ya Nishati na MAidini wakari ameshahamia Afrika MAshariki?", ikiwa moto juu ya motyo, ndipo JK akafanya ziara ya ghafla kutembelea Richmond.

    9. #9
      Mwanagenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th September 2006
      Location : Mtandaoni
      Posts : 762
      Rep Power : 806
      Likes Received
      10
      Likes Given
      10

      Default

      Kwa hiyo JK kamtuma EL nje (Ufaransa) ili amshughulikie wakati hayupo?
      ____________
      Ili Tuendelee Tunahitaji Dikteta mwenye Uzalendo na Visheni
      _____________
      "UTU BUSARA UJINGA HASARA,
      "TUPINGANE BILA KUPIGANA"

    10. #10
      FairPlayer's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th February 2006
      Location : UK
      Posts : 4,382
      Rep Power : 1555
      Likes Received
      456
      Likes Given
      205

      Default

      Mwanagenzi,

      wrong observation!!! EL bado ana watu ndani ya bunge wanaoweza kumpa data!

      FD
      A positive thinker!

    11. #11
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,623
      Rep Power : 46738
      Likes Received
      16722
      Likes Given
      8562

      Default

      Ndugu zangu, CCM imekaa njia panda, haijui wapi iende na kama mtu ambaye amekalia mtumbwi ulio katika hati hati ya kuzama ni bora waangalie wanakalia upande gani, ama sivyo, watauzamisha mtumbwi huo kiurahisi kweli!
      [email protected]
      The Best of Tanzanian Socio-Political Blogging - http://www.mwanakijiji.com

    12. #12
      Halisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th January 2007
      Posts : 3,037
      Rep Power : 2182
      Likes Received
      455
      Likes Given
      243

      Default

      kama alivyosema Fikiraduni, ni kweli its wrong kumfikiria EL kwa urahisi hivyo, yy ni mtu mwenye nguvu kubwa. Mtu wa kuangaliwa sasa ni SS (Samwel Sita) ambaye ana wakati mgumu kupambana na EL. Hoja ya msingi ni JK kuacha maji yafuate mkondo na hatimaye kwa tabia ya WATZ mambo yataishia hewani na kusahaulika, na ikawa kama kawaida shughuli zinaendelea. Mumepiga kelele, NSSF weeeeee, PSPF weeeeee, Manji weeeeee, leo wanaibuka kina Malima ndio wanacheza ngoma waliokula fweza (Manji and others) zao wanakula kuku wakichekea pembeni nyie wazawa (Malima vs Mengi) munashikana mashati. Hapo ni watu kuachwa waseme wafumue vifua vyao then whant next. Hakuna kitakachoendelea. Sana sana watakaoumizana ni sisi kwa sisi tunaohangaika kupata mlo wa siku moja

    13. #13
      Lunyungu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th August 2006
      Location : Malampaka
      Posts : 8,048
      Rep Power : 2571
      Likes Received
      794
      Likes Given
      29

      Default

      Mkandara mko watu wachache sana nina heshimu michango yenu humu ndani lakini kwa hili I wil beg to differ . Nasema JK ni mnafiki mkubwa tena mzandiki mpenzi sifa na mpika majungu makubwa . What is he trying to tell the Wabunge wa CCM ? He is not sincere is a man with no honest and intergrity .He never wish or intend well at all for Tanzania and Tanzanians.

      Uchafuzi wa majina kupitia Media the archtecture ni JK nani hajui hili ? Huyu anapata kutuzina macho na kumuona ni Mr.Clean lakini hata Richmond yeye JK alikuwa msemaji .Leo itakuwaje tunakomaa na EL pekee ? JK na EL ni wahuni wanatuchezea tu hapa .

    14. #14
      Nyangumi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2007
      Posts : 593
      Rep Power : 755
      Likes Received
      5
      Likes Given
      1

      Default

      Watanzania!!Kakauli kadogo kakutafuta misifa kanatufanya tujiliwaze,jamani!!!!.Inamaana wabunge walikuwa hawafahamu wajibu wao au mpaka wapate ruhusa ya kusema kutoka kwa JK.Jk ni mR Misifa.Yeye kama rais ambaye watanzania wajinga wamemwamini anashindwa nini kuunda kamati ikafuatilia hizi harufu chafu(Kashfa) zinatokea wapi na kusababishwa na nani?Eti mpaka aletewe ushahidi!!

    15. #15
      Kitila Mkumbo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2006
      Posts : 3,940
      Rep Power : 6971
      Likes Received
      1102
      Likes Given
      36

      Default

      Ngoja tumsubiri hiyo Jumamosi kama kweli JK anapenda kukosolewa na kuwa engaged kwenye debate.
      A Struggle Without Casualties is No Struggle-Steve Biko

    16. #16
      Mkandara's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 13,768
      Rep Power : 7665
      Likes Received
      4931
      Likes Given
      4509

      Default

      Lunyungu,
      Sina maana kuwa JK ni perfect ama napenda jinsi anavyo deal na mambo lakini pia tukumbuke tulikotoka. Wakati wa Mkapa wabunge walikuwa hawana kabisa nafasi na huu ni urithi ambao umekuwepo. Ukisema kitu hakipendwi utaambiwa kaa chini wewe hujui unalosema na vitisho kibao!... Kuna watu wamekufa ama kuuawa, wengine leo hii hawana kabisa nafasi ndani ya serikali hata wakienda tambika.
      Ebu nambie kama wewe ungekuwa JK ungesema kipi ambacho wananchi wangeridhika nacho mahala ambapo wabunge wamesimama kutoa hoja zao na wasiwasi wao jinsi wanavyotendewa bungeni.
      Na wanabodi wengine...
      Jamani toka JK achukue madaraka nchi kidogo tumeweza kusimama huru tukiyachambua yote haya. Wakati wa Mkapa hii forum ingeisha fungwa siku nyingi sana. Kisha hakuna wakati siasa imeweza kusimama nchini tanzania kama wakati huu wa JK kwa sababu kaacha uwanja wazi kwa sisi sote kurusha madongo. Unafikiri kweli wakati wa Mkapa hao jamaa wa vyama vya Upinzani wangepata nafasi ya kuandamana?.

      JK kama binadamu nadhani kuna mengine anajaribu kuyapokea toka kwa wananchi na ni jukumu letu kutumia nafasi hizi kuzungumza hoja zinazohusika kuliko kila wakati kumzungumza mtu. hakuna asiyekubali kuwa JK ni Msanii, Misifa na Mtalii mzuri lakini bado kuna madogo ambayo yametuweka hapa kwa muda mrtefu inabidi tuyaangalie pia. trust me guys ni wakati huu wa JK, kijiwe hiki kimekuwa kikigopwa na baadhi ya watu kwa sababu JF inasomwa na watu wengi walioko karibu na JK. Wengi wanapenda kifungwe na walitegemea JK angekifunga badala yake kijiwe kipo hai na msisitizo unaendelea kuwa viongozi lazima wajifunze kutoka kwa wananchi!.
      Jamani haya yote sii haba pamoja na kwamba kikombe bado kimejaa nusu lakini sii kweli kuwa kimepungua nusu!
      Exploration of reality

    17. Dua is offline
      Dua
      #17
      Dua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2006
      Posts : 3,534
      Rep Power : 1369
      Likes Received
      9
      Likes Given
      0

      Default

      Hivi hilo rungu kuna mtu amelipiga picha? kama picha ipo jamani tuwekeeni hapa, nakumbuka Mzee ruksa walimpa FAGIO LA CHUMA hata lilikoishia wanajua wale waliokuwa magogoni.

      Kwa kweli hawa CCM mambo yanawaendea mrama imekuwa kama hadithi za Chakubanga au ile ya Pwagu na Pwaguzi. Kila siku utasikia mpya na kila siku kuna bonge la skendo.....................tut afika tu.
      Dua la kuku halimpati mwewe

    18. #18
      Kazi Ndiyo Kipimo Cha Utu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th March 2006
      Posts : 1,726
      Rep Power : 1026
      Likes Received
      55
      Likes Given
      6

      Default

      Quote By mwanasiasa View Post
      Ngoja tumsubiri hiyo Jumamosi kama kweli JK anapenda kukosolewa na kuwa engaged kwenye debate.
      Amini usiamini nimehudhuria vikao viwili vya huyo Mh.Rais,Baada ya kumaliza wote mtakata tamaa kwa kurudia yale yale na kuyatetea yale yale ambayo hayajetekelezwa hadi hii leo na haoni umuhimu wa mabadiliko ya haraka kurekebisha hayo.Tusubiri Labada kuna mabadiliko katika kipindi cha miezi mitano Tangu nihudhurie mkutano wake wa mwisho.Tunasubiri Taarifa zenu wa LOndon.

    19. #19
      Invisible's Avatar
      Robot Array
      Join Date : 11th February 2006
      Location : Here...!
      Posts : 9,336
      Rep Power : 100000
      Likes Received
      5036
      Likes Given
      5931

      Default


      Mwandishi Wetu
      HabariLeo; Tuesday,February 13, 2007


      RAIS Jakaya Kikwete amewaeleza wabunge wa CCM wawe huru kuikosoa serikali mradi wawe na ushahidi na hoja zao. Katika semina ya siku moja iliyofanyika Dar es Salaam juzi, rais aliwaambia wabunge hao kuwa hayuko tayari kulinda watu wachafu ndani ya serikali yake, hivyo akatoa mwito kwa wabunge kufichua mambo yanayoenda kinyume na maadili ya uongozi.

      “Rais alichotueleza anataka tuwe wasafi kuanzia kwenye chama na serikalini,” kilisema chanzo kimoja cha habari kilichohudhuria semina hiyo. Katika kile kinachoonekana ni kuelekezwa juu ya majukumu yao wakiwa kama wabunge wa chama tawala, Rais Kikwete katika kikao hicho aliwataka wabunge hao kuisaidia serikali katika kutekeleza majukumu yake kwa kuikosoa wanapoona mambo hayaendi.

      Chanzo hicho kilidokeza kuwa rais amewapa meno wabunge hao kuhakikisha wanatimiza jukumu lao la kuisaidia serikali lakini pia na kuwa huru kuikosoa. “Siyo kwamba hataki tuikosoe serikali, lakini anataka tuwe na ushahidi wa kile tunachokosoa,” kilisema chanzo hicho cha habari.

      Habari hizo zilieleza kuwa Rais Kikwete aliwapa meno wabunge hao lakini pia akawatahadharisha kuwa siyo vizuri kupinga kila kitu wakati hawana ushahidi. Rais pia aliwaeleza kuwa hayuko tayari kulinda watu wachafu ndani ya serikali yake hivyo akatoa mwito kwa wabunge kufichua mambo yanayoenda kinyume na maadili ya uongozi.

      Mtoa taarifa mwingine alilidokeza gazeti hili kuwa Rais Kikwete baada ya mada ya Spika wa zamani wa Bunge, Pius Msekwa, aliwashauri wabunge hao wawe wazi lakini pia wasitoe hoja za kubuni na kutunga ambazo haziwezi kuisaidia serikali. “Alitushauri tusikurupuke lakini akataka tuwe wawazi na wakweli tunapoona kuna upungufu…lakini pia amesisitiza mwenye ushahidi asiogope kusema,” alisema mtoa habari.

      Awali taarifa iliyotolewa na Ikulu ilisema semina hiyo ilikuwa na mada moja tu kuhusu Kanuni na Majukumu ya Msingi ya Wabunge na Wawakilishi wa Chama Tawala (CCM) katika mfumo wa vyama vingi vya siasa.

      Katika mada yake hiyo, Msekwa kutokana na uzoefu wake wa utumishi ndani ya chama na katika Bunge alielezea na kufafanua kwa kina maudhui ya kanuni za kamati za wabunge na wawakilishi wa CCM.

      Semina hiyo iliwahusisha Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Walishiriki semina hiyo kama wajumbe wa kamati ya wabunge na wawakilishi wa CCM kwa ajili ya kupigwa msasa. Ilifanyika katika ukumbi wa mikutano wa jengo la Ubungo Plaza.

      Ilielezwa kuwa washiriki hao waliijadili kwa kina mada hiyo na kutoa michango ya mawazo yao kwa uwazi na ukweli, na kueleza kuwa semina hiyo ilikuja wakati mwafaka na imekuwa ni elimu tosha kwao kuhusu jinsi ya kutekeleza majukumu yao.

      Rais Kikwete aliahidi kuwa semina kama hiyo zitakuwa zinafanyika mara kwa mara ili kupata fursa ya kubadilishana mawazo na kukumbushana mambo mbalimbali.
      Ni miaka miwili tu imepita, sasa wanatafuta mchawi ndani ya chama... Kamati ya Mwinyi imeundwa, mamilioni yanatafunwa kutafuta mchawi!

      Lingeandika gazeti jingine watu tungeongea kivinginevingine, ni HabariLeo... La Serikali yetu.

      Nadhani tumerogwa!
      Ficha Upumbavu wako; Usiifiche Hekima yako!
      24/7 Email SUPPORT: [email protected]


    20. #20
      Juma Contena's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st May 2009
      Posts : 1,137
      Rep Power : 744
      Likes Received
      49
      Likes Given
      7

      Default Re: Kikwete ataka wabunge CCM waikosoe Serikali

      Quote By Mzee Mwanakijiji View Post
      Ndugu zangu, CCM imekaa njia panda, haijui wapi iende na kama mtu ambaye amekalia mtumbwi ulio katika hati hati ya kuzama ni bora waangalie wanakalia upande gani, ama sivyo, watauzamisha mtumbwi huo kiurahisi kweli!
      Kaka,Mkuu, Generali, Mh, Mwkjj

      Lakini si ndio tunachokitaka hiki au tena tume-change priority zetu?
      the difference between fantasy and realism is that, one is based on wishful thinking and the other purely on facts.

      jambo usilolijua ni kama usiku wa kiza......

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 5
      Last Post: 27th July 2011, 10:10
    2. Ataka serikali imkabidhi viwanda vyote Kilimanjaro
      By nngu007 in forum Business & Economic Forum
      Replies: 9
      Last Post: 17th May 2011, 02:23
    3. Replies: 26
      Last Post: 19th March 2009, 15:16
    4. Zitto ataka wabunge wa zamani waombe radhi
      By BAK in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 25
      Last Post: 11th December 2008, 14:42
    5. Mbunge ataka Serikali ya Uingereza ishtakiwe
      By Jembajemba in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 19th July 2007, 07:21

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...