Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

    Report Post
    Page 1 of 2 12 LastLast
    Results 1 to 20 of 22
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,235
      Rep Power : 3562
      Likes Received
      3062
      Likes Given
      462

      Default Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      *CHADEMA kutumia helikopta Igunga
      *Yaanika mikakati ya kushinda jimbo
      *CCM yavuta pumzi, yasubiri CC


      Na Benjamin Masese

      VUGUVUGU la uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga, mkoani Tabora linazidi kupanda
      huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikitangaza safu ya viongozi wa kitaifa watakaozindua kampeni za chama hicho Septemba 9, mwaka huu.

      Mbali na kuanika majina ya viongozi wake watakaozindua kampeni, chama hicho kina mkakati wa kutumia helikopta ili kufikia maeneo yote ya Jimbo la Igunga.

      "Kama kawaida yetu tayari helikopta imeandaliwa kwa mashambulizi ya kampeni jimbo la Igunga, lakini hatutaanza nayo, tutaanza na vyombo vya ardhini kwanza tukiona kuna ulazima, ndipo tutakaponyanyuka juu kwa juu na kumwaga sumu 'chini'."

      Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Habari Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Bw. Erasto Tumbo, wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu akiwa Igunga. Alisema viongozi wa kitaifa watakaohudhuria uzinduzi wa kampeni za chama hicho ni Katibu Mkuu, Dkt. Willbroad Slaa na Naibu Katibu Mkuu Bw.Zitto Kabwe.

      Bw. Tumbo alisema kuwa tayari Kamati Kuu ya CHADEMA ilikutana juzi na kupitia majina ya wagombea 16 waliochukua fomu, ambapo kwa kuzingatia sifa na mtu mwenyewe anavyokubalika kwa wananchi wa Igunga, ilimpitisha Bw.Joseph Kashindye, kuwania kiti hicho.

      "Hapa tulipo hatujaanza kampeni, lakini wananchi wameonesha shauku kubwa ya kukiunga mkono chama chetu ili kuwaongoza, kwani wamedai kwamba kwa miaka mingi walikuwa hawajapata kiongozi wa kukaa nao na kujadiliana wanachohitaji," alisema Bw. Tumbo.

      Alisema baada ya uzinduzi huo viongozi wa kitaifa watasambaa maeneo yote ya jimbo hilo kumnadi mgombea Bw. Kashindye, ili kuhakikisha jimbo hilo linaondoke mikononi wa CCM).

      Alisema utafiti wa awali umeonesha kuwa CHADEMA itaibuka na ushindi kwa zaidi ya asilimia 80, huku vyama vingine vikigawana asilimia zilizobaki.

      Alisema CCM ina hali mbaya kuliko vyama vingine vinavyoshiriki uchaguzi huo. Alisema dalili zinaonesha kuwa wananchi wamechoka na sera za chama hicho.

      "Hadi sasa tunajua tunashinda na harakati za kumwaandaa mgombea wetu kwenda bungeni zimeanza na tutampeleka kwa maandamano hadi Dodoma na kufanya hafla fupi ya kumkaribisha,"alisema.

      Naye Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi, CCM Bw. Nape Nnauye, alisema muda wowote kuanzia sasa Kamati Kuu itakutana kumteua mgombea wa chama hicho na kutangaza siku ya kuanza kampeni.

      Akizungumza na gazeti hili jana,Bw. Nnauye alisema kauli za CHADEMA kujihakikishia ushindi ni mbinu za kuwatisha watu na wagombea wengine, lakini CCM inazichukulia kama kelele ambazo zimezoeleka kwao.

      "Hakuna chama ambacho kinatangaza mikakati yake barabarani,tunatarajia Kamati Kuu itakaa muda wowote kumpitisha mgombea mmoja na kutangaza siku rasmi ya uzinduzi wa kampeni, wao ndio wanasuasua sisi tuko imara na ushindi ni wetu kama kawaida,"alisema.

      Awali alisema CCM ina asilimia 90 za ushindi katika jimbo hilo na kuongeza kwamba kampeni za chini chini za baadhi ya vyama vya siasa zilizoanza Igunga ni mchezo wa watoto wadogo.

      "Pale Igunga, CHADEMA haina kitu hata kama wameanza kampeni za chini chini...ule ni mchezo wa watoto na kawaida ikifika saa sita usiku lazima watoto walale na ndipo tutakaposhinda. Pia tathmini tulishafanya na tumebaini zaidi ya asilimia 90 tunashinda ndio maana hatuna wasiwasi,"alisema.

      Naye Rachel Balama anaripoti kuwa Chama cha Wananchi (CUF) kinatarajia kutangaza ratiba na mikakati mingine leo.

      Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu akiwa Igunga, Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Bw. Julius Mtatiro, alisema;

      "Nipo Igunga kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi, lakini kesho nitatoa taarifa zote kuhusu kampeni za CUF."

      Naye Mwenyekiti wa Chama cha National Reconstruction Alliance(NRA) Bw. Rashid Mtuta, alisema kuwa chama chake kina nia ya kusimamisha mgombea na kinasubiri timu iliyotumwa Igunga kuangalia mazingira ya kukubalika kwake jimboni humo.

      Alisema tayari timu hiyo ya watu watano ipo kwa wiki moja sasa na inatarajia kurudi wakati wowote kuanzia leo.

      "Tunapozungumza tayari timu ya watu watano ipo Igunga kuangalia mazingira na tutatoa tamko," alisema Bw. Mtuta.

      Alisema kuwa timu hiyo inaonngozwa na Kaimu Katibu Mkuu Taifa Bw. Hassan Kisabya.

    2. Miaka 50

    3. #2
      mfereji maringo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th November 2010
      Posts : 843
      Rep Power : 599
      Likes Received
      138
      Likes Given
      47

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Quote By nngu007
      *CHADEMA kutumia helikopta Igunga
      *Yaanika mikakati ya kushinda jimbo
      *CCM yavuta pumzi, yasubiri CC


      Na Benjamin Masese

      VUGUVUGU la uchaguzi mdogo wa Jimbo la Igunga, mkoani Tabora linazidi kupanda
      huku Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kikitangaza safu ya viongozi wa kitaifa watakaozindua kampeni za chama hicho Septemba 9, mwaka huu.

      Mbali na kuanika majina ya viongozi wake watakaozindua kampeni, chama hicho kina mkakati wa kutumia helikopta ili kufikia maeneo yote ya Jimbo la Igunga.

      "Kama kawaida yetu tayari helikopta imeandaliwa kwa mashambulizi ya kampeni jimbo la Igunga, lakini hatutaanza nayo, tutaanza na vyombo vya ardhini kwanza tukiona kuna ulazima, ndipo tutakaponyanyuka juu kwa juu na kumwaga sumu 'chini'."

      Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Habari Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Bw. Erasto Tumbo, wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu akiwa Igunga. Alisema viongozi wa kitaifa watakaohudhuria uzinduzi wa kampeni za chama hicho ni Katibu Mkuu, Dkt. Willbroad Slaa na Naibu Katibu Mkuu Bw.Zitto Kabwe.

      Bw. Tumbo alisema kuwa tayari Kamati Kuu ya CHADEMA ilikutana juzi na kupitia majina ya wagombea 16 waliochukua fomu, ambapo kwa kuzingatia sifa na mtu mwenyewe anavyokubalika kwa wananchi wa Igunga, ilimpitisha Bw.Joseph Kashindye, kuwania kiti hicho.

      "Hapa tulipo hatujaanza kampeni, lakini wananchi wameonesha shauku kubwa ya kukiunga mkono chama chetu ili kuwaongoza, kwani wamedai kwamba kwa miaka mingi walikuwa hawajapata kiongozi wa kukaa nao na kujadiliana wanachohitaji," alisema Bw. Tumbo.

      Alisema baada ya uzinduzi huo viongozi wa kitaifa watasambaa maeneo yote ya jimbo hilo kumnadi mgombea Bw. Kashindye, ili kuhakikisha jimbo hilo linaondoke mikononi wa CCM).

      Alisema utafiti wa awali umeonesha kuwa CHADEMA itaibuka na ushindi kwa zaidi ya asilimia 80, huku vyama vingine vikigawana asilimia zilizobaki.

      Alisema CCM ina hali mbaya kuliko vyama vingine vinavyoshiriki uchaguzi huo. Alisema dalili zinaonesha kuwa wananchi wamechoka na sera za chama hicho.

      "Hadi sasa tunajua tunashinda na harakati za kumwaandaa mgombea wetu kwenda bungeni zimeanza na tutampeleka kwa maandamano hadi Dodoma na kufanya hafla fupi ya kumkaribisha,"alisema.

      Naye Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa Itikadi na Uenezi, CCM Bw. Nape Nnauye, alisema muda wowote kuanzia sasa Kamati Kuu itakutana kumteua mgombea wa chama hicho na kutangaza siku ya kuanza kampeni.

      Akizungumza na gazeti hili jana,Bw. Nnauye alisema kauli za CHADEMA kujihakikishia ushindi ni mbinu za kuwatisha watu na wagombea wengine, lakini CCM inazichukulia kama kelele ambazo zimezoeleka kwao.

      "Hakuna chama ambacho kinatangaza mikakati yake barabarani,tunatarajia Kamati Kuu itakaa muda wowote kumpitisha mgombea mmoja na kutangaza siku rasmi ya uzinduzi wa kampeni, wao ndio wanasuasua sisi tuko imara na ushindi ni wetu kama kawaida,"alisema.

      Awali alisema CCM ina asilimia 90 za ushindi katika jimbo hilo na kuongeza kwamba kampeni za chini chini za baadhi ya vyama vya siasa zilizoanza Igunga ni mchezo wa watoto wadogo.

      "Pale Igunga, CHADEMA haina kitu hata kama wameanza kampeni za chini chini...ule ni mchezo wa watoto na kawaida ikifika saa sita usiku lazima watoto walale na ndipo tutakaposhinda. Pia tathmini tulishafanya na tumebaini zaidi ya asilimia 90 tunashinda ndio maana hatuna wasiwasi,"alisema.

      Naye Rachel Balama anaripoti kuwa Chama cha Wananchi (CUF) kinatarajia kutangaza ratiba na mikakati mingine leo.

      Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu akiwa Igunga, Naibu Katibu Mkuu wa CUF (Bara), Bw. Julius Mtatiro, alisema;

      "Nipo Igunga kwa ajili ya maandalizi ya uchaguzi, lakini kesho nitatoa taarifa zote kuhusu kampeni za CUF."

      Naye Mwenyekiti wa Chama cha National Reconstruction Alliance(NRA) Bw. Rashid Mtuta, alisema kuwa chama chake kina nia ya kusimamisha mgombea na kinasubiri timu iliyotumwa Igunga kuangalia mazingira ya kukubalika kwake jimboni humo.

      Alisema tayari timu hiyo ya watu watano ipo kwa wiki moja sasa na inatarajia kurudi wakati wowote kuanzia leo.

      "Tunapozungumza tayari timu ya watu watano ipo Igunga kuangalia mazingira na tutatoa tamko," alisema Bw. Mtuta.

      Alisema kuwa timu hiyo inaonngozwa na Kaimu Katibu Mkuu Taifa Bw. Hassan Kisabya.
      hivi nape atakanyaga igunga? naskia amepigwa marufuku asitie pua. viva chademaaaaaaaaaaaaaaaaa!
      "WE CAN NOT SOLVE TODAY'S PROBLEMS USING THE MINDSET THAT CREATED THEM"
      - ALBERT EINSTEIN

    4. #3
      oldonyo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th August 2011
      Posts : 536
      Rep Power : 500
      Likes Received
      71
      Likes Given
      0

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Kawaida ya CCM huwa ni wagumu kuelewa kwani ni watu wa kuchukulia mambo kimzaa mzaa na badae ujikuta wakiumbuka lakini nawahasa wananchi wa igunga wasichague chama wachague sera.

    5. #4
      sweke34's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th September 2010
      Posts : 2,493
      Rep Power : 1255
      Likes Received
      734
      Likes Given
      1240

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      "Kama kawaida yetu tayari helikopta imeandaliwa kwa mashambulizi ya kampeni jimbo la Igunga, lakini hatutaanza nayo, tutaanza na vyombo vya ardhini kwanza tukiona kuna ulazima, ndipo tutakaponyanyuka juu kwa juu na kumwaga sumu 'chini'."
      "
      Alisema utafiti wa awali umeonesha kuwa CHADEMA itaibuka na ushindi kwa zaidi ya asilimia 80, huku vyama vingine vikigawana asilimia zilizobaki.
      "

      Wajameni , CHADEMA nao wana mbwembwe!

    6. #5
      Power G's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 20th April 2011
      Location : Msoga Kijijini
      Posts : 2,411
      Rep Power : 993
      Likes Received
      775
      Likes Given
      261

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Quote By sweke34
      [FONT=courier new][SIZE=4][COLOR=#0000ff]""

      Wajameni , CHADEMA nao wana mbwembwe!
      Hizo ni mbinu za kivita.
      SILENT ACtOR likes this.

    7. RukaaJuu Final

    8. #6
      Uwezo Tunao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th November 2010
      Posts : 6,882
      Rep Power : 2291
      Likes Received
      1151
      Likes Given
      1488

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      VITA VYA DR SLAA NA CHADEMA KUFUNGIA NDANI GWIJI LA UFISADI NCHI PALE IGUNGA NI SAWA TU NA JINSI PEOPLE'S POWER ILIVYOMFUNGIA NDANI DIKTETA GADDAFI KULE TRIPOLI NCHINI LIBYA

      Dokta wa Ukweli, kazi ya Igunga tunaomba iwe ni FULL-TIME kusudi tukifanikiwa KUNG'OA KIZIKI CHA UFISADI nchini kilichojichimbia kwenye ardhi yenye rutuba nyingi pale Igunga na basi baada ya hapo vita vikasambaa kote nchini hapo ndipo Mtanzania wa hali ya chini atakapoweza kupata ahueni.

      Makamanda wooote CHADEMA vita mbeeele kwambele Igunga mpaka kielewke lakini kwa kushirikiana kambi zima ya upinzani nchini. Kifo Cha CCM kitatangaziwa rasmi pale Igunga hata kabla ya mawaziri kibao na makada wa CCM wasioridhika na utawala wa sasa kuamua kujiengua mmoja baada ya mwingine!!!!!!!!!!!!

      Na endapo kukifanyika kosa lolote la NEC-Jaji Makame kufanya yale madudu ya mwaka jana kule Igunga basi hapo ndipo nako watakua wamerahishisha PEOPLE'S POWER kuingia mitaaani na kukatisha uhai wa hii serikali fisadi na dhalimu tuliyo nayo hivi sasa.

      Chaguo ni lao NEC pamoja CCM chenyewe hapa; ama kunyoa au kusuka!!!!!!!!!!!!!!
      only83 likes this.

    9. #7
      UNMAFISADI's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 22nd August 2011
      Posts : 1
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By oldonyo
      Kawaida ya CCM huwa ni wagumu kuelewa kwani ni watu wa kuchukulia mambo kimzaa mzaa na badae ujikuta wakiumbuka lakini nawahasa wananchi wa igunga wasichague chama wachague sera.
      <br />
      <br />
      ni kweli mkubwa, hawa watu huwa hawaelewi. itakuwa ni kama mkwala wa gaddafi na hatma itafikaaaa, PEEEEPOOZ POWEEEERRRR!..

    10. #8
      Mapujds's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2011
      Location : Dar es salaam
      Posts : 1,282
      Rep Power : 666
      Likes Received
      118
      Likes Given
      6

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Tambo ni nyingi sana,ngoja tuone.

    11. #9
      Daffi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th June 2011
      Location : Arachuga
      Posts : 2,935
      Rep Power : 987
      Likes Received
      516
      Likes Given
      239

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Kilalakheri CHADEMA, tupo pamoja nanyi katika mabadiliko ya kweli
      Walk your talk

    12. #10
      ntagunga's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 13th August 2011
      Location : Mwanza
      Posts : 223
      Rep Power : 437
      Likes Received
      35
      Likes Given
      49

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Nawatakieni kila la heri katika kufanikisha juhudi za kulikomboa jimbo la IGUNGA. Tuko pamoja waungwana

    13. #11
      Mzee's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd February 2011
      Location : DUNIANI
      Posts : 6,589
      Rep Power : 1746
      Likes Received
      698
      Likes Given
      386

      Default

      Quote By mfereji maringo
      hivi nape atakanyaga igunga? naskia amepigwa marufuku asitie pua. viva chademaaaaaaaaaaaaaaaaa!
      <br />
      <br />
      matokeo atayasubiria dar. Chadema...... vema

    14. #12
      dazu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2011
      Location : A Town
      Posts : 355
      Rep Power : 542
      Likes Received
      66
      Likes Given
      67

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Nape Acha longolongo, njoo igunga tuchuane
      A drop of Water is worth more than a kg of Gold to a Thirsty man.

    15. #13
      Mthuya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th June 2011
      Posts : 1,012
      Rep Power : 605
      Likes Received
      110
      Likes Given
      4

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Safi makamanda tupo nyumayenu

    16. #14
      Tuko's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2010
      Posts : 4,643
      Rep Power : 13839
      Likes Received
      2282
      Likes Given
      2209

      Default Do CDM expect to win in Igunga?! Are they done with their homework?

      Mimi ng mwanachama wa CDM na naomba chama changu kishinde Igunga. Hata ivo nachelea kujiuliza maswali ambayo viongozi wangu wana majibu. Is J. Kashindye the best contesant and shall make the best MP for Igunga? Je, tunakumbuka kwamba majority ya majimbo tuliyopoteza mwaka jana ni kwa sababu hatukuwa na wagombea wenye uwezo? To what extent have we ensured kwamba uchaguzi wowote ujao tunakuwa na best wagombea? Ni ukwel ulio waz kuwa CDM imeweza kuwavutia wapiga kura wengi, lakini sio wapigiwa kura wengi. Kwa tulio huku mtaani tunajua kwamba wagombea wengi wa Cdm mwaka jana walipewa hiyo chance kwa sababu ndio waliojitokeza, na katika majimbo kadhaa hakutokea mtu ndo maana hatukuwa na wagombea. wapiga kura wanashawishiwa lakin wagombea bora wanakuwa groomed, mbowe, slaa, zito mnajua hilo. Tujiulize kama Mwl Kashindye na Dr Kafumu wangekuwa wote CDM, je bado mgombea wetu angekuwa Kashindye? Kam

    17. #15
      Fasta fasta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th February 2011
      Posts : 421
      Rep Power : 503
      Likes Received
      75
      Likes Given
      158

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Hapa watapasuka vichwa tu. Peaplesss....... powerrrrrrr........

    18. #16
      only83's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th October 2010
      Location : Dodoma-Mjengoni
      Posts : 4,157
      Rep Power : 1846
      Likes Received
      1431
      Likes Given
      1539

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      ..................Wafuatao wameambiwa hawatakiwi Igunga kamwe............na wakitia pua zao ni halali kwa wakazi wa Igunga.........nao ni:

      1. Nape Nnauye
      2. Kapteni chiligati

      Hawa wakionekana kule watakiona chamoto......................h aaaa maskini katibu mwenezi Napeeeeeeeee
      "Problems can not be solved by the same level of thinking that created them"
      "Matatizo hayawezi kutatuliwa na uwezo ule ule mdogo wa watawala wa CCM walioyasababisha"




    19. #17
      politiki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Posts : 1,378
      Rep Power : 1341
      Likes Received
      728
      Likes Given
      130

      Default Re: Do CDM expect to win in Igunga?! Are they done with their homework?

      pointi yako ni ngumu kuielewa kwa maana unasema wagombea hawakuwa wazuri, je kama hao ndio waliojitokeza kugombea ni lazima wapewe nafasi na hao wazuri unaowajua hawakujitokeza kwahiyo uzuri wao hauwezi kutusaidia kitu. kuhusu kafumu na kashindye obvious the answer ni kashindye kwa record yake kabambe ya kupigania maslahi ya waalimu na uzuri wa mwakilishi siyo elimu tu bali ni ukaribu wake na wananchi, uadilifu na record yake ya utumishi. DR.Kafumu anajua uchafu, uovu na wizi wa CCM ameamua kukaa kimya hatujawahi kumsikia hata siku moja akikemea kwa sababu ya kuweka maslahi yake mbele na si ya nchi na wala sijawahi kusikia record yake yeyote ya kuwatetea wananchi kokote kule pamoja na wananchi wa igunga kuwa matatizo chungu mzima. sasa hivi ndio anajiahandaa kupita vijijini kuanza kuwaaidi watu kuwa atawatetea na kutatua matatizo ingawa matatizo hayo yapo miaka yote na yeye anayajua lakini alichagua kula raha dsm. kashindye yuko karibu na wananchi kwani yeye ni mkazi wa igunga watoto wake na familia wake wamekulia igunga mpaka leo hii. jiulizeni watoto wa Dr. Kafumu wanasoma au walisoma wapi ?? yeye mwenyewe akiumwa huwa anatibiwa wapi ?? kama majibu siyo Igunga basi siyo mwenzenu huyo anataka ubunge tu. ukaribu wake na wananchi, record yake ya kutetea maslahi ya waalimu na elimu yake ya chuo kikuu ni sifa tosha chadema walifanya homework yao.
      Last edited by politiki; 30th August 2011 at 20:27.

    20. #18
      mashikolomageni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th January 2010
      Location : Dar es Salaam, Tanzania
      Posts : 1,445
      Rep Power : 766
      Likes Received
      144
      Likes Given
      130

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Huko tunaoitakia mema nchi hii tunatamani na tuna hamu watu wa Igunga waifundishe adabu CCM kwa kuipiga chini kwa kishindo warudi kama walivyorudi Tarime usiku kwa helcopta yao.
      Peoplllllllllllllllleeeeeeeeee eeeeeeeeezzzzzzzzz Poweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeerz

    21. #19
      Malipesa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd August 2011
      Posts : 300
      Rep Power : 452
      Likes Received
      30
      Likes Given
      209

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      Kama hakuna uchakachuaji, hapana shaka ushindi mnono ni kwa CDM.

    22. #20
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,123
      Rep Power : 14288
      Likes Received
      4013
      Likes Given
      3271

      Default Re: Mbio za ubunge Igunga Dkt. Slaa, Zitto kuzindua kampeni; CHADEMA kutumia helikopta Igunga

      natamani kuwa igunga kushiliki ukombozi wajimbo hilo..

    Page 1 of 2 12 LastLast

    Similar Topics

    1. CUF kutumia Helikopta (chopa) ktk kampeni Igunga
      By mzee wa mawe in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 36
      Last Post: 30th August 2011, 19:28
    2. Maalim seif kuzindua kampeni za CUF igunga.
      By mzee wa mawe in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 23
      Last Post: 29th August 2011, 20:46
    3. Uchaguzi Igunga: Chadema kutumia Helikopta
      By kessy kyomo in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 5
      Last Post: 22nd August 2011, 15:17

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...