Amefariki muda si mrefu kwa ajali ya gari akitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam eneo la Pandambili (kama sijakosea).
PICHA:
Marehemu Chacha Wangwe...
Mzee Mwiguni George aliyefika katika eneo na kumsaidia Chacha na wenzake!
Deus Francis Mallya aliyetoa maelezo yenye utata na sasa watu wanamgeuzia kuwa kuna jambo analificha! (Huyu pia aliwahi kujitambulisha kuwa yeye ndiye (mimi) Invisible wa JF.
Gari lililohitimisha maisha ya Chacha likiwa limeharibika vibaya
Mudhihir alipata ajali baada ya kulumbana na Zitto Kabwe. na chacha Wangwe amelumbana na chadema sana hivi karibuni kama mawazo amesababishiwa na mambo kadhaa wa kadhaa.
1. Hivi Mudhihir na Zitto "walilumbania" wapi? Mie nadhani aliyelumbana na Zitto ni Karamagi.
2. Kabla ya Chacha wangwe kufariki amelumbana na watu wengi, hata kwenye gesti alikolaa Dodoma, na wala hayakuwa masuala ya Chadema, bali ugomvi wa kawaida tu kama mnavyojua. lakini sidhani kama malumbano hayo ndiyo chanzo cha ajali na kifo chake.
3. Mtu yeyote aliyefuatilia michango ya Mgagagigikoko hapa, atajua anakotaka kutupeleka, anachekelea kifo hiki kwa sababu anataka kukitumia kwa maslahi anayojua....watu wanaomboleza yeye anakenua...
Re: Chacha Wange Afariki dunia - Katika Ajali ya Gari
Jamani ama kweli uhai wetu wanadamu unaweza kuzimika kama mshumaa tu!!! Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi na kuwapa faraja na subira wafiwa katika kipindi hiki kigumu kwao.
Mgagagigikoko, nadhani una matatizo yako unatafuta wa kumuambukiza, bahati mbaya hapa wote ni watu wazima, watoto mko wachache sana. Unayoandika na unayemwandikia (siju unamwaddress nani?) ni vitu viwili ambavyo vinaonyesha hicho ninachokisema. Pole, kama unataka kutumia msiba kuonyesha udhaifu wako. pole. Hapa si mahali pake, na sina dawa kwa ugonjwa wako. Utajadiliana na watoto wenzio...
sijamjua Wangwe leo kwenye msiba niko nae toka mlipoanza kumuwekea zengwe,soma mada zangu kwenye Chacha Wangwe na Chadema.kiasi cha kijana wako Mushi akanibatiza jina la Wangwe na kusema bora apigwe Risasi.
LAKINI AIRBAG SYSTEM YA MASHANGINGI NI BORA KULIKO YA MARK 11...,NDIO MAANA WATAALAMU WA USALAMA WANAPENDEKEZA MASHANGINGI KWENYE OFFROAD AU SAFARI NDEFU.......HATA UKICHUNGUZA MISAFARA YA RAIS..OR THE LIKE KAMA ANAENDA SAFARI NDEFU ZAIDI YA KM 100 AU KWENYE BARABARA MBAYA ..HUPANDA MASHANGINGI..YAPO SECURED ZAIDI...
...AIRBAG INASAIDIA SANA..UKIONA ILIVYOMSAIDIA MTU KAMA KAPUYA ..UTAAMINI ...NA UKIONA NAMNA MAMA MBATIA AMBAYE KWA BAHATI MBAYA ILE NISSAN PATROL YAKE ILIKUWA OLD MODEL KIDOGO NA HAIKUWA NA AIRBAG...INGEKUWEPO ANGEWEZA KUTOKA MZIMA.....hata mtu kama MUDHIHIR alipopata ajali na cruizer yake kama sio AIRBAG zaidi ya kuumia angeweza hata kupoteza maisha...
SIKU ZA KARIBUNI WABUNGE WAMEKUWA HAWAPEWI CHAGUO LA MAGARI AMBAYO WANATAKIWA KUYANUNUA YAKIWA MAPYA..BUT I REMEMBER KABLA ..KILA BUNGE JIPYA LINAPOANZA DEALERS WA MAGARI MAPYA...LANDROVER,TOYOTA,NISSAM,MITSUBISHI ..ets walikuwa wanakaribishwa bungeni na wabunge walitakiwa wachague magari miongoni mwa make zinazoaminiwa na serikali.....baadaye naona huu utaratibu umeachwa na hii imesababisha wabunge wengi kuingizwa mkenge na wauzaji wa USED.....najua wabunge wengi tu ambao sasa hivi magari yao yanawasumbua sana...na hayakidhi mahitaji ya wanakotokea ..kutokana na kuchakaa haraka....
PM,
Aliyekuambia hivyo kakudanganya. Faida ya hizo 4WD ni kwamba ni comfortable, kwahiyo kama unaenda safari ndefu basi zinakufanya usichoke sana. Pia zinaweza kupita kwenye matope na mashimo lakini sio kwenye suala la safety.
Soma mail niliyomjibu invisible, wameongelea mambo hayo hayo. Kwenye barabara nzuri kama Dar mpaka Dodoma, una nafasi kubwa ya kupona kwenye gari dogo kuliko shangingi, kama yote yana ubora sawa.
Mudhihir alipata ajali baada ya kulumbana na Zitto Kabwe. na chacha Wangwe amelumbana na chadema sana hivi karibuni kama mawazo amesababishiwa na mambo kadhaa wa kadhaa.
Acha fikra potofu!! Basi wangekuwa wameshakufa watu wengi sana katika kipindi ambacho Zitto amekuwa hapa duniani. Maana kuanzia utoto wake hadi utu uzima atakuwa amelumbana na wengi tu na hatujasikia lolote kuhusiana na hizo dhana zako potofu. Mbona wale walioamua kumfungia Bungeni pamoja na kuwa alikuwa hana kosa lolote hawajafa hata mmoja!!!? Au wale waiodai alikuwa anatembea na marehemu Amina Chifupa!!!? Mwe! Kuna watu wana fikra potofu!!!!
Re: Chacha Wange Afariki dunia - Katika Ajali ya Gari
Poleni sana Wazalendo wenzangu, Watu wa Tarime na Watanzania kwa ujumla.
Wangwe alikuwa ni mpenda maendeleo.
Asubuhi hii nilikuwa Dodoma ambapo pamoja na mambo mengine nilihudhuria bunge la asubuhi na baadaye kuonana na baadhi ya wadau kuhusu TPN akiwemo Mzalendo Slaa na wengineo kabla ya jioni hii kuondoka na kurudi DSM.
Sina uhakika chanzo cha Ajali ya Mh. Wangwe ni nini, lakini traffic ya magari wakati mwingine ni kubwa. Malori mengi husafiri usiku na barabara ya Dodoma ni nyembamba japo ni nzuri. Baadhi ya madereva si waangalifu. Sina uhakika kama vitu hivi vilichangia, lakini ni vyema kwa miaka ya mbeleni kuangalia ni namna gani ya kuboresha mapungufu haya.
1. Hivi Mudhihir na Zitto "walilumbania" wapi? Mie nadhani aliyelumbana na Zitto ni Karamagi.
2. Kabla ya Chacha wangwe kufariki amelumbana na watu wengi, hata kwenye gesti alikolaa Dodoma, na wala hayakuwa masuala ya Chadema, bali ugomvi wa kawaida tu kama mnavyojua. lakini sidhani kama malumbano hayo ndiyo chanzo cha ajali na kifo chake.
3. Mtu yeyote aliyefuatilia michango ya Mgagagigikoko hapa, atajua anakotaka kutupeleka, anachekelea kifo hiki kwa sababu anataka kukitumia kwa maslahi anayojua....watu wanaomboleza yeye anakenua...
wewe mnafiki Wangwe hajagombana na watu wengi,huo ni uzushi na ulikuwa unafuatilia nyendo zake hadi guest ya Dodoma? huo nao uzushi, amekwisha kufa bado unamzulia? nadhani furaha unayo wewe kuona kuwa mambo yako sasa yako tambarare, nakutakia uchaguzi mwema kwani unagombea na kivuli.
Re: Chacha Wange Afariki dunia - Katika Ajali ya Gari
This world is not my home I'm just a passing through
My treasures are laid up somewhere beyond the blue
The angels beckon me from heaven's open door
And I can't feel at home in this world anymore
Oh Lord you know I have no friend like you
If heaven's not my home then Lord what will I do
The angels beckon me from heaven's open door
And I can't feel at home in this world anymore
I have a loving mother just up in Gloryland
And I don't expect to stop until I shake her hand
She's waiting now for me in heaven's open door
And I can't feel at home in this world anymore
Oh Lord you know I have no friend like you
If heaven's not my home then Lord what will I do
The angels beckon me from heaven's open door
And I can't feel at home in this world anymore
Just over in Gloryland we'll live eternaly the saints on every hand are shouting victory
Their songs of sweetest praise drift back from heaven's shore
And I can't feel at home in this world anymore
Oh Lord you know I have no friend like you
If heaven's not my home then Lord what will I do
The angels beckon me from heaven's open door
And I can't feel at home in this world anymore
__________________
kuchagua CCM 2010 ni sawa na kufukia mashimo bila kuweka mbegu...utavuna nini?