Amefariki muda si mrefu kwa ajali ya gari akitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam eneo la Pandambili (kama sijakosea).
PICHA:
Marehemu Chacha Wangwe...
Mzee Mwiguni George aliyefika katika eneo na kumsaidia Chacha na wenzake!
Deus Francis Mallya aliyetoa maelezo yenye utata na sasa watu wanamgeuzia kuwa kuna jambo analificha! (Huyu pia aliwahi kujitambulisha kuwa yeye ndiye (mimi) Invisible wa JF.
Gari lililohitimisha maisha ya Chacha likiwa limeharibika vibaya
wewe naye!!!
Nipe jina mbunge wa mwaka 1990 ,mkuu wa wilaya wa mwaka 1996 na mkuu wa polisi wa mwaka 1998 na Mbunge kabla ya Chacha anatoka kijiji gani? maana nawasi wasi na wewe kidogo.
CHADEMA ndipo sehemu ya kuanzia kuchunguzwa.
1.CHACHA alikua ktk mchakato wa mwisho kukipeleka CHADEMA mahakamani ili waeleze na kuthibitisha waliyomzushia.
2. Wangwe alivuliwa umakamu na CHADEMA kwa kua ni mzigo na anayemega siri zao
3. MBOWE alisema hawezi fanya kazi na mtu kama CHACHA
4.CHACHA alikituhumu chdema kwa kufisadi fedha
5. Ktk uhai wake watu wa chadema walidai apigwe risasi na kweli dalili za mwanzo zinaonyesha CHACHA kapigwa RISASI mbili za kichwa.
Hata ktk hali ya kawaida mtu akikwambia aisii wewe subiri nitakuchoma kisu cha **** ,na baada ya siku kadhaa kweli ukachomwa kisu ,polisi wanakuja moja kwa moja kwa yule jamaa aliyetamka hakuna cha kujadiliana hapo.
Sehemu ya kuanzia ni CHADEMA ndio waende kwingine unless labda ajali hiyo ni ya kawaida kama ajali zingine.
Sehemu ya kuanzia ni humu JF ,kwani aliyesema kuwa apigwe risasi ni Jmushi ambaye tayari kaomba radhi, sasa naona mnatafuta kumhusisha Jmushi hivi huyu ndio Mallya? Huyu JMUSHI NDIO MALLYA?
Acha unafiki wako, kumuunga mkono Wangwe sio lazima uandike pumba zako mtandaoni. Kuna watu wanafanya vitendo zaidi ya maneno. Maneno yako ya chuki na dhihaka kwenye msiba huu yanaonesha jinsi gani usivyojali feelings za watu wa Tarime.
Heshima ni kitu cha bure, ungepungukiwa na nini kama ungesubiria siku chache tu wenzako tukaomboleza na kuzika ndio ulete unafiki na upuuzi wako hapa?
pumba unazo wewe, umesikia marehemu kafa unajifanya mtu wa karibu wa marehemu au unataka kuwadhulumu mirathi watoto wa Marehemu Wangwe?
ulikuwa wapi wakati anazomewa hapa hapa JF? au unataka ushike daftari la mchango wa marehemu?
Wewe ni laghai na mzushi sana, na uzushi wako unatisha mno! Ni mtu gani wa chadema alisema Chacha apigwe risasi? Hivi huu uzushi unamtumikia nani na kwa manufaa gani, au una-abuse anonymity yako hapa?
Unafikiri kwa kuwa unatumia jina bandia basi una uhuru wa kuropoka na kupayuka unavyotaka?
Amekasirika sana baada ya kuona aliyotaka yatokee Tarime hayakutokea. Yeye alitaka watu wa Tarime waanzishe ugomvi dhidi ya wachaga na wanachadema lakini mambo yamekuwa tofauti kwani viongozi wa upinzani wote wamepokelewa vizuri sana.
yeye alitaka watu wa-Tarime waonekane kuwa ni wapenda fujo kwa mgawanyiko wa kikoo - wanyabasi dhidi ya watimbaru au koo zingine lakini watu wa Tarime wote wameungana na kuwa kitu kimoja wakati huu wa majonzi makubwa.
Aibu sana kuwa Tanzania ina watu kama Mkamap wanaotaka kupata pointi za kisiasa kwenye misiba ya wenzao.
5. Ktk uhai wake watu wa chadema walidai apigwe risasi na kweli dalili za mwanzo zinaonyesha CHACHA kapigwa RISASI mbili za kichwa.
.
smart attempt... "watu wa chadema" waliodai "apigwe risasi" ni kina nani na wapi walifanya hivyo? Hii ni new information, kwa sababu ukiweza kuwaonesha hao "watu wa chadema" na mimi nitakuunga mkono.
__________________ Nchi hii imewahi kung' oa masultani wa kila aina. Tukianza kuvumilia masultani wakuchaguliwa tutapanda mbegu ya masultani wa kuzaliwa. - Nyerere katika "Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania"
Sehemu ya kuanzia ni humu JF ,kwani aliyesema kuwa apigwe risasi ni Jmushi ambaye tayari kaomba radhi, sasa naona mnatafuta kumhusisha Jmushi hivi huyu ndio Mallya? Huyu JMUSHI NDIO MALLYA?
Heheh!! Mkuu angalia usijefanya watu wakose usingizi!!
[QUOTE=Mzee Mwanakijiji;258829]smart attempt... "watu wa chadema" waliodai "apigwe risasi" ni kina nani na wapi walifanya hivyo? Hii ni new information, kwa sababu ukiweza kuwaonesha hao "watu wa chadema" na mimi nitakuunga mkono.[/QUOTE
Ana ugomvi na jmushi, kwani ndio aliandika na kashaomba radhi tangia awali,wametumwa hawa.
Sehemu ya kuanzia ni humu JF ,kwani aliyesema kuwa apigwe risasi ni Jmushi ambaye tayari kaomba radhi, sasa naona mnatafuta kumhusisha Jmushi hivi huyu ndio Mallya? Huyu JMUSHI NDIO MALLYA?
Inawezekana sio JMUSHI ila mhusika mkuu aliposoma ushauri wa JMUSHI akaamua kuufanyia kazi. JMUSHI anaweza kuwa shahidi kwenye kesi hii na akajikuta anafungwa kwa kuuua bila kukusudia(Manslaughter).
na kauli zote kama vile SIWEZI KUFANYA KAZI NA WANGWE ukitizama sana zinaweza kuwaweka watu pabaya,kama Mwanakijiji alivyoishauri Polisi hivyo hivyo na MKAMAP anajaribu kuweka mawazo yake kama Mwanakijiji na baya zaidi pale Mwenyekiti aliposema kuwa Wangwe anashiriki kukihujumu chama kwa kutoa siri za chama nje. walimwita kwenye vikao vingi kumuonya asitoe siri,hakusikia na wakampa muda ajirekebishe, wanasema hakujirekebisha,hatuleti siasa ila kama sheria inafuatwa Chadema wana kubwa la kujibu.
pumba unazo wewe, umesikia marehemu kafa unajifanya mtu wa karibu wa marehemu au unataka kuwadhulumu mirathi watoto wa Marehemu Wangwe?
ulikuwa wapi wakati anazomewa hapa hapa JF? au unataka ushike daftari la mchango wa marehemu?
Sio lazima uongee hapa JF ili uonekane mtu wa karibu na Wangwe. Mimi na Wangwe ni marafiki wakubwa sana na tunajuana kwa muda mrefu. Kuongea mambo ya uchochezi kama yako ni sababu moja au zaidi inayofanya watu wengine kutoongea hapa JF.
Ninajaribu kuelezea ukweli kuhusu Tarime ambao watu wengi kama wewe na kwenye media mnataka kuigawa na kupanda chuki kwa wakazi wake. Michango ya marehemu itanisaidia nini maishani? Mimi ni mtu ninayetumia jina langu hapa na hiyo inafanya nia yangu kujulikana wazi.
Labda watu wakuulize wewe unayeonyesha dharau kubwa kwa watu wa Tarime hapa mtandaoni kwa kutumia jina la bandia kuwa utafaidika na nini?
Kufuatia kifo cha aliyekuwa mbunge wa Tarime Bw. Chacha Wangwe, Chama cha Mapinduzi (CCM) kimelazimika kuteta na hatimaye kutoa salamu zake kuhusiana na kifo hicho.
Kwa Mujibu wa taarifa iliyosambazwa kwa vyombo vya habari, ikitolewa na Katibu Mkuu wake, Bw. Yusuf Makamba, chama hicho kimeelezea kusikitishwa kwake na msiba wa Mhe. Wangwe na kueleza kuwa mbunge huyo ameacha pengo kubwa kwa wapenzi wa demokrasia nchini.
Inawezekana sio JMUSHI ila mhusika mkuu aliposoma ushauri wa JMUSHI akaamua kuufanyia kazi. JMUSHI anaweza kuwa shahidi kwenye kesi hii na akajikuta anafungwa kwa kuuua bila kukusudia(Manslaughter).
na kauli zote kama vile SIWEZI KUFANYA KAZI NA WANGWE ukitizama sana zinaweza kuwaweka watu pabaya,kama Mwanakijiji alivyoishauri Polisi hivyo hivyo na MKAMAP anajaribu kuweka mawazo yake kama Mwanakijiji na baya zaidi pale Mwenyekiti aliposema kuwa Wangwe anashiriki kukihujumu chama kwa kutoa siri za chama nje. walimwita kwenye vikao vingi kumuonya asitoe siri,hakusikia na wakampa muda ajirekebishe, wanasema hakujirekebisha,hatuleti siasa ila kama sheria inafuatwa Chadema wana kubwa la kujibu.
Nakushauri ndugu yangu kwa mara nyingine uachane na unafiki na upuuzi wako hapa wakati wengine tuko kwenye msiba. Mbowe na viongozi walikuwa kwenye msiba Tarime na watu wa Tarime hawakuwa na tatizo lolote na uwepo wao huko.
Kama mnajaribu kubadilisha ukweli kwenye hili huku mkitaka kuanzisha fujo na vurugu Tarime mmenoa. Wakazi wa Tarime ni smart kuliko watu wenye bias kama wewe mnayofikiria.