Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Kwani ni lazima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

    Report Post
    Page 1 of 3 123 LastLast
    Results 1 to 20 of 52
    1. #1
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,507
      Rep Power : 46711
      Likes Received
      16375
      Likes Given
      8453

      Default Kwani ni lazima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Wananchi wanalalimika kuwa kuna tatizo la mafuta; wafanyabiashara wanasema hawana mafuta, serikali inasema wafanyabiashara wapunguze bei n.k Nimebaki najiuliza kuna uhusiano gani kati ya upungufu wa mafuta jijini na utawala uliopo madarakani? Kwanini tatizo la upungufu wa mafuta halikutokea kwa mfano wakati mmomonyoko wa uchumi duniani umeiva? Kwanini liwe ni tatizo ambalo linaonekana kuhusiana na bei zaidi au ni kweli ugavi wa mafuta ni mdogo hivyo?

      Lakini upande mwingine inabidi ujiulize kwenye nchi inayofuata "uchumi wa soko" kwanini serikali ipange bei ya mafuta badala ya kuacha soko liamue kiasi gani kiingizwe na kwa bei gani kumeet demand?

      Je Serikali haina reserve ya mafuta kwa ajili ya hali kama hii? Kwa mfano kama tungekuwa tunaenda vitani leo hii tungeweza kuwa na mafuta ya kutosha kuhudumia vikosi vyetu?

      Lakini swali linalosumbua mimi kama wengine vile vile je is the a genuine shortage of oil or an artificial one? Kama ni genunie, kwanini serikali basi inafikiria kwa kulazimisha watu washushe bei ndio mafuta yataongezeka? Kwanini serikali isiseme wafanyabiashara wauze katika bei ya awali tuone kama mafuta yatatokea - maana kama mafuta yanatokea bei ikiwa juu na hayapo bei ikiwa chini maana yake ni kuwa kuna mtu anafanya "hoarding"? ni muhimu kujua wapi na kina nani?

      Upande mwingine, kama wenye vituo vya mafuta hawataki kuagiza mafuta katika bei ya hasara serikali inaweza vipi kuwalazimisha kuagiza mafuta bila kuonekana inaingilia "sekta binafsi"?
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      MANI's Avatar
      JF Platinum Member Array
      Join Date : 22nd February 2010
      Location : CHINI YA MBUYU
      Posts : 1,915
      Rep Power : 954
      Likes Received
      569
      Likes Given
      631

      Default Re: Je tatizo la Upungufu wa mafuta linahusiana vipi na Utawala wa CCM?

      Mkuu serekali imeshindwa kumfukuza kazi katibu mkuu iliemwajiri itakuwa kuwasimamia wafabiashara mbona hilo ni gumu sana.
      ebrah likes this.
      " TANZANIA BILA CCM INAWEZEKANA"

    4. #3
      majege's Avatar
      Member Array
      Join Date : 3rd May 2009
      Posts : 51
      Rep Power : 522
      Likes Received
      11
      Likes Given
      4

      Default Re: Je tatizo la Upungufu wa mafuta linahusiana vipi na Utawala wa CCM?

      Ndugu yangu hawa jamaa watoa pesa nyingi sana kwaajili ya kampeni ya sisiem kwa uhakika wa kuvuna baada ya uchaguzi, kilichotokea sasa ni kwamba mpaka sasa pesa zao hazijarudi na kama ilivyo kawaida selikali nayo imewageuka. ndiyo maana unashindwa kuelewa ni nani mwanye nguvu nchi hii. Ni siku nne tu zimepita Masebu alikua akijigamba kuwa Reserve ya mafuta aina zote ya siku zisizopungua 40. sasa unashangaa siku mbili baadaye hakuna mafuta. Kuna tatizo kubwa sana la viongozi wa taasisi zetu hizi za serikali kwani hawajui hata wanachokiongea.
      NguchiroTheElde likes this.

    5. #4
      kilemi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th March 2009
      Location : Dar es Salaam, Tanzania
      Posts : 496
      Rep Power : 618
      Likes Received
      51
      Likes Given
      0

      Default Re: Je tatizo la Upungufu wa mafuta linahusiana vipi na Utawala wa CCM?

      Nafikiri serekali imejichanganya, kwenye soko huria huwezi kuagiza kwa kupayuka barabarani na "kuagiza". Ynanahitajika mazungumzo kati ya wafanyabiashara na serekali. Serekali itoe ruzuku kwa wafanyabiashara, kama kupunguza kodi, ili nao washushe bei. Tofauti na hapo serikali inaweza kuingia kwenye competition, kwa kufungua viwanda vyake vya mafuta.
      Ila kuna swali gumu wenye hisa kwenye hayo makampuni si ndo haohao wanaotuongoza? Au ni akina nani waliisaidia ccm kwenye kampeni za uchaguzi?

    6. #5
      Nyota Ndogo's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 7th August 2011
      Posts : 152
      Rep Power : 424
      Likes Received
      33
      Likes Given
      13

      Default Re: Kwani lni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Wananchi wanalalimika kuwa kuna tatizo la mafuta; wafanyabiashara wanasema hawana mafuta, serikali inasema wafanyabiashara wapunguze bei n.k Nimebaki najiuliza kuna uhusiano gani kati ya upungufu wa mafuta jijini na utawala uliopo madarakani? Kwanini tatizo la upungufu wa mafuta halikutokea kwa mfano wakati mmomonyoko wa uchumi duniani umeiva? Kwanini liwe ni tatizo ambalo linaonekana kuhusiana na bei zaidi au ni kweli ugavi wa mafuta ni mdogo hivyo?

      Lakini upande mwingine inabidi ujiulize kwenye nchi inayofuata "uchumi wa soko" kwanini serikali ipange bei ya mafuta badala ya kuacha soko liamue kiasi gani kiingizwe na kwa bei gani kumeet demand?

      Je Serikali haina reserve ya mafuta kwa ajili ya hali kama hii? Kwa mfano kama tungekuwa tunaenda vitani leo hii tungeweza kuwa na mafuta ya kutosha kuhudumia vikosi vyetu?

      Lakini swali linalosumbua mimi kama wengine vile vile je is the a genuine shortage of oil or an artificial one? Kama ni genunie, kwanini serikali basi inafikiria kwa kulazimisha watu washushe bei ndio mafuta yataongezeka? Kwanini serikali isiseme wafanyabiashara wauze katika bei ya awali tuone kama mafuta yatatokea - maana kama mafuta yanatokea bei ikiwa juu na hayapo bei ikiwa chini maana yake ni kuwa kuna mtu anafanya "hoarding"? ni muhimu kujua wapi na kina nani?

      Upande mwingine, kama wenye vituo vya mafuta hawataki kuagiza mafuta katika bei ya hasara serikali inaweza vipi kuwalazimisha kuagiza mafuta bila kuonekana inaingilia "sekta binafsi"?
      Tanzania ina genge la wasanii wanaojiita serikali.
      Siitambui herufi 'z' kwenye neno Tanzania. 'y' na 'k' ziko wapi?

    7. Miaka 50

    8. #6
      Dark City's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2008
      Location : Roaming
      Posts : 11,562
      Rep Power : 23553
      Likes Received
      6982
      Likes Given
      11331

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Mkuu unaongelea serikali ipi?

      Mimi naona hii drama ina 2 visible players (wafanyabiashara na wananchi) na 1 invisible player (hiyo inayoitwa serikali)!!

      Katika mazingira kama hayo, invisible na wale visible wanaweza kufanya kazi pamoja???
      samora10 likes this.
      "WE ALWAYS DON'T CHANGE UNTIL THE COST OF STAYING THE SAME EXCEEDS THE COST OF CHANGE....LOOKING BEYOND THE 31 OKTOBA 2010 LANDMARK"

      Retired Maj Gen DC (1947)...[email protected]

    9. #7
      Godwine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th January 2010
      Location : dar
      Posts : 1,317
      Rep Power : 742
      Likes Received
      217
      Likes Given
      124

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      kanuni ya demand na supply inafanya kazi kwenye free market lakini kilichotokea katika soko la mafuta ni wafanyabiashara wameunda catel yani ushirika wa kudhibiti bei na sheria za tume ya ushindani inaipa nguvu serikali kuingilia inapoamini kuna nanma yeyote ya umoja wa wafanyabiashara kudhibiti bei

      katika suala la upungufu wa mafuta linatokana na sababu mbili kubwa sasa.

      1. kiburi cha wafanyabiashara dhidi ya serikali kwani wanaamini kuwa serikali lazima isalimu amri na haina nguvu na uwezo wa kuwadhibiti

      2.kutokana na kushuka kwa bei watumiaji wengi hawaamini kuwa bei itaendelea kubaki chini na wanadhani kuwa ni wakati mfupi tu itabaki kwenye bei hii na ndio maana wamenunua na kuweka stock yao kwa siku za karibuni kwa niliweza kuzungumza na mkandarasi wa barabara anayetarajia kufanya kazi zake muda wa karibuni yeye ameweza kununua zaidi ya lita 700,000 za diesel na kuziweka akiba kwa ajili ya mitambo yake ili pia linaongeza upungufu wa mafuta

      imefika wakati ambao serikali haiwezi kukwepa kuunda mfumo wa upatikanaji wa mafuta wa uhakika kwani katika nchi ambayo umeme ni shida na mafuta nayo yakiwa shida basi lazima ife

      serikali lazima ifikirie kufufua kiwanda cha kusafisha mafuta cha tipper ili kupunguza bei za mafuta na kuongeza ajira kwa vijana wetu la sivyo haitaweza kusalimika kutoka katika janga la mfumuko wa bei na usalama wake yenyewe








      Masaki and RealMan like this.

    10. #8
      The Stig's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 493
      Rep Power : 509
      Likes Received
      210
      Likes Given
      56

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      Wananchi wanalalimika kuwa kuna tatizo la mafuta; wafanyabiashara wanasema hawana mafuta, serikali inasema wafanyabiashara wapunguze bei n.k Nimebaki najiuliza kuna uhusiano gani kati ya upungufu wa mafuta jijini na utawala uliopo madarakani? Kwanini tatizo la upungufu wa mafuta halikutokea kwa mfano wakati mmomonyoko wa uchumi duniani umeiva? Kwanini liwe ni tatizo ambalo linaonekana kuhusiana na bei zaidi au ni kweli ugavi wa mafuta ni mdogo hivyo?

      Lakini upande mwingine inabidi ujiulize kwenye nchi inayofuata "uchumi wa soko" kwanini serikali ipange bei ya mafuta badala ya kuacha soko liamue kiasi gani kiingizwe na kwa bei gani kumeet demand?

      Je Serikali haina reserve ya mafuta kwa ajili ya hali kama hii? Kwa mfano kama tungekuwa tunaenda vitani leo hii tungeweza kuwa na mafuta ya kutosha kuhudumia vikosi vyetu?

      Lakini swali linalosumbua mimi kama wengine vile vile je is the a genuine shortage of oil or an artificial one? Kama ni genunie, kwanini serikali basi inafikiria kwa kulazimisha watu washushe bei ndio mafuta yataongezeka? Kwanini serikali isiseme wafanyabiashara wauze katika bei ya awali tuone kama mafuta yatatokea - maana kama mafuta yanatokea bei ikiwa juu na hayapo bei ikiwa chini maana yake ni kuwa kuna mtu anafanya "hoarding"? ni muhimu kujua wapi na kina nani?

      Upande mwingine, kama wenye vituo vya mafuta hawataki kuagiza mafuta katika bei ya hasara serikali inaweza vipi kuwalazimisha kuagiza mafuta bila kuonekana inaingilia "sekta binafsi"?



      EWURA imefanya kosa kubwa sana kuingilia bei ya mafuta kama ilivyofanya. Katika soko huria, hauwezi ukapanga bei. Ukipanga bei unazalisha ARTIFICIAL SHORTAGE (kuhadimika bidhaa) kutokana na wauzaji kutokuwa tayari kuuza kwa bei ya hasara. Hii nayo inatengeza BLACK MARKET (ulanguzi) na mwisho kabisa INASAMBARATISHA UCHUMI.

      EWURA wa swallow their pride na kuondoa agizo lao la bei ya 2004/=.

      Inabidi Tanzania ifike mahali ambako watu wanafikiria kwa kutumia akili zao zaidi ya mioyo yao.

    11. #9
      Mwanaweja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th February 2011
      Posts : 3,475
      Rep Power : 1115
      Likes Received
      466
      Likes Given
      952

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      nchi yetu haina mwelekeo hatujui tunaelekea lakini pia tusisahau hawa wafanyabiashara ndio walipelekewa vimemo kwa ajili ya kutoa chcchote kwenye uchanguzi kwa njia nyingine ndio waliopatia hela ya kampeni Jk kwa hiyo ni vingumu kukemea hata kuwaajibisha hao wafanyabiashara.

    12. #10
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,507
      Rep Power : 46711
      Likes Received
      16375
      Likes Given
      8453

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      serikali ikiamua kukaa pembeni kutakuwa na athari gani? Maana bei ikipanda sana watu hawatanunua! Hapa ndio suala la UDA linapokuja!!
      Maganga Mkweli likes this.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    13. #11
      Ngonini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2010
      Posts : 1,307
      Rep Power : 1281
      Likes Received
      279
      Likes Given
      41

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      MKuu mimi nadhani Mungu anataka kutufundisha kitu na pengine kama kuna watu wake Tanzania waliokuwa wanaomba basi huenda ndo ukawa ukombozi wa nchi hii. Haiwezekani kwa hali yakawaida balaa juu ya balaa lingine. Balaa la mafuta juu ya balaa la umeme! Mapigo juu ya mapigo kama wana kipindi cha wanawaiziraieli walipokuwa wa kiokolewa toka Utumwani misiri?

      Kitendo cha serikali kutunishiana misuri na wafanyabiashara wa mafuta na serikali kushindwa hii inadhihirisha ulegelege wa serikali. Naamini serikali hawana ujasiri wa kutekeleza maamuzi wanayoyasema kwa sababu vituo vya mafuta ni vya mafisadi walewale na pengine familiya za wakubwa!

      Kuna thread moja humu ilikuwa inaongelea ingridients za kodi ya mafuta na kulikuwepowapo na tetesi juu ya kuwepo kwa ingridient za sirisiri ndani ya kodi hiyo. Watu wanasema pengine wafanyabiashara hawa kuna wakati wanatoa michango mingine zaidi ya hizi kodi za mafuta na kuahidiwa mavuno baadaye. Sasa mambo yamebadilika na wao walishatoa michango hiyo. Serikali imejitutumua kusema kujiosha mbele ya wananchi huku wakijua ukweli wa mambo nyuma ya pazia.


      Tusubiri tuone ila inaonekana mambo ni bandika bandua na mengi tu yatakuja na nadhani litakalofuatia ni njaa kubwa tena!
      Mkirua likes this.

    14. #12
      Nguruvi3's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2010
      Location : Kidabashi-Dongobeshi
      Posts : 3,432
      Rep Power : 2886
      Likes Received
      4786
      Likes Given
      2852

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Tatizo la mafuta ni 'artificial' na ni la wafanyabiashara. Kumbuka wakati mafuta yanapanda bei katika soko la dunia hatukuwahi kuona upungufu hata sku moja. Kitu cha kushangaza mafuta yalikuwa yanapanda bei kila siku utadhani ni maji yanayonunuliwa ruvu na kuuzwa siku hiyo hiyo. Nina maana kuwa kama kuna shehena imenunuliwa mwezi wa 3 na bado ipo kwanini bei ikibadilika usiku mmoja iathiri shehena hiyo?

      Wapo watakaosema ni soko huria, lakini soko huria na bei za mafuta linaathiri sana nchi zinazoagiza mafuta kila siku na matumizi yake ni makubwa. Huko nyuma ilishawahi kutokea TPDC walipandisha bei miezi 3 baada ya bei kupanda soko la dunia kwasababu walishagiza kwa bei ya wakati huo.

      Soko huria ni zuri likiachiwa kufanya kazi kwa maana hiyo, lakini wafanyabiashara wameamua kufanya ushirika kinyume na taratibu za soko hilo popote duniani. Kwa hivyo, kuachia huria ni kuhalalisha maumivu zaidi kwasababu watakaa vikao na kusema tuuze lita 7,000. Ni kwa msingi huu ndipo EWURA iliundwa si kuthibiti bei bali kumlinda mtumiaji 'consumer'.

      Hata nchi zilizoendelea zina consumers organizations, sio kudhibiti bei bali kuhakikisha kuwa soko linakuwa huru kwa maana hiyo na kuwa mtumiaji hakamuliwi mpaka tone la mwaisho la damu kwa ushirika wa wafanyabiashara, bali bei zinapangwa na soko lenyewe.

      Kama TPDC ingekuwa katika ushindani wafanyabiashara wasingefika hapa walipo kwasababu soko lingekuwa huru na si la ushirika. Hatujajifunza kuwa kuweka sekta muhimu kama hii mikononi mwa watu wawili au watatu ni hatari, na kwamba ikitokea dharura sijui tutafanya nini.

      Wafanyabiashara hawa wana nguvu sana na wanatumia umoja to creat demand, na wanajua serikali haina pa kutokea. Ndio manaa hadi leo suala nyeti na la hatari kama hili linashughulikiwa na EWURA inayoonekana kutokuwa na uwezo kukabiliana nao. Serikali ipo kimya na sijui ni kwanini inawaogopa.

      Marekani ina stategic reserve na ndio wenye soko huria, sasa tujiulize kwanini wana reserve. Kuna wakati waliachia mapipa milion 30 na yaka stabilize bei kiasi, na ile psychology tu kuwa uwezekano wa kutumia strategic reserve upo ulishusha bei sana. Sisi ya kwetu ipo wapi?

      Hili ni tatizo la kutokuwa na mkakati, nguvu kubwa ya waagizaji inayoizidi serikali na madudu mengine ambayo tutayafahamu tu huko mbeleni. Sitashangaa nikisikia wanahisa ni viongozi, nani alijua Kapuya ana hisa Simon au mwenyekiti wa bodi ni consultant pia !!

    15. #13
      samora10's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st July 2010
      Location : Kwa-Gude
      Posts : 3,252
      Rep Power : 1103
      Likes Received
      729
      Likes Given
      1163

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      nchi hii haijawahi kua na serikali tangu 2005!!!
      Mamndenyi likes this.
      ''Mipango na Mikakati imekamilika na sasa tuko kwenye mchakato wa mazungumzo na wafadhili"- M Pinda

    16. #14
      Lord's Avatar
      Member Array
      Join Date : 13th February 2009
      Posts : 87
      Rep Power : 540
      Likes Received
      16
      Likes Given
      4

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      MM, Hivi nchi hii ina serikali au genge la wezi?? Si umesikia juzi wanaambiana wanafikiri kwa makalio. Sasa mtu anayefikiri kwa vifaa vya kukalia unategemea anafikiria nini hasa zaidi ya kushibisha tumbo ili makalio yakue.
      samora10 likes this.

    17. #15
      Godwine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th January 2010
      Location : dar
      Posts : 1,317
      Rep Power : 742
      Likes Received
      217
      Likes Given
      124

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      tetesi: rais kikwete amewapa maagizo wanajeshi kuingilia shell binafsi kuzikagua na kuwalazimisha na ikibidi MPs wa jeshi wauze kwa nguvu

      note:bado sijaweza kuzithibitisha habari hizi




    18. #16
      Dark City's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2008
      Location : Roaming
      Posts : 11,562
      Rep Power : 23553
      Likes Received
      6982
      Likes Given
      11331

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Quote By samora10
      nchi hii haijawahi kua na serikali tangu 2005!!!
      Unamaanisha 2005 au 1985???
      "WE ALWAYS DON'T CHANGE UNTIL THE COST OF STAYING THE SAME EXCEEDS THE COST OF CHANGE....LOOKING BEYOND THE 31 OKTOBA 2010 LANDMARK"

      Retired Maj Gen DC (1947)...[email protected]

    19. #17
      Mkirua's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th September 2010
      Posts : 3,421
      Rep Power : 1036
      Likes Received
      1173
      Likes Given
      599

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Quote By Mzee Mwanakijiji
      serikali ikiamua kukaa pembeni kutakuwa na athari gani? Maana bei ikipanda sana watu hawatanunua! Hapa ndio
      suala la UDA linapokuja!!
      Mkuu I beg to differ. Hakuna serekali makini duniani isiyomlinda mwnanchi wa kawaida (mlaji) kwa kisingizio chochote kikiwemo cha Free Market. Kilichofanyika hapa kwetu ni muendelezo wa chama lege lege kilichozaa serekali legelege ndio maana hata TIPPER ikapelekwa kuzimu na hao wafanyabiashara wa mafuta. Ilikuwa ni kosa kubwa kwa serekali kujiondoa kwenye hiyo biashara kwa asilimia 100 na ndio maana wafanyabiashara wamehamua kuichezea kama wanavyotaka na kwakuwa wanajua serekali haijui A wala B ya biashara hiyo at the end watasalimu amri na kuwaacha wauze kama wanavyotaka wao na kuendelea kuneemeka huku walalahoi wakikamuliwa zaidi. Najiuliza kama ni kweli walikuwqa na akiba ya mafuta iliyooagizwa kabla ya bajeti mbona mafuta ya taa yalipopandishwa bei hawakusema wana akiba wakaendelea kuuza kwa bei ya zamani hadi walipoagiza shehena mpya? Huu ni uhuni wa wafanya biashara na ni nafasi ya serekali kuachana na ulege lege na kuonesha makucha. Kama wanapata hasara hawa wachache wanaouza wanafanya kazi msikitini/kanisani? hawataki hasara? Big Born kila siku anauza yanaisha anainweka na kuuza tena yeye ndo hataki faida? Narudia huu ni uhuni lazima serekali makini ichukue hatua na ilinde watu wake.

    20. #18
      Mamndenyi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 12,109
      Rep Power : 31819
      Likes Received
      5992
      Likes Given
      19547

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Serikali gani??????????? naungana na aliyesema nchi haijawahi kuwa na serikali since 2005.

    21. #19
      CAMARADERIE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2011
      Location : 1 Luthuli Street
      Posts : 4,163
      Rep Power : 2720
      Likes Received
      1587
      Likes Given
      1145

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Wauza mafuta ndio walioiweka serikali madarakani kw michango mikubwa aliyoifanyisha MAKAMBA SR......jeuri yao ipo hapo
      A compliment is something like a kiss through a veil




    22. #20
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,507
      Rep Power : 46711
      Likes Received
      16375
      Likes Given
      8453

      Default Re: Kwani ni azima serikali iingilie sekta binafsi ya Mafuta?

      Kwanini hawakuboresha UDA? kwani watu wote DAR wanahitaji kuwa na magari na pikipiki?
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    Page 1 of 3 123 LastLast

    Similar Topics

    1. Je kwani watanzania ni lazima tukihitimu elimu zetu tuajiriwe na serikali
      By BUMIJA in forum Jukwaa la Elimu (Education Forum)
      Replies: 2
      Last Post: 25th November 2011, 18:01
    2. Serikali yaridhia sekta binafsi kuzalisha na kusambaza umeme!
      By nngu007 in forum Business & Economic Forum
      Replies: 3
      Last Post: 10th September 2011, 21:46
    3. Kuna umuhimu wa serikali kuwabana waajiri kwenye sekta binafsi
      By Fredy John in forum Nafasi za Kazi na Tenda
      Replies: 0
      Last Post: 9th August 2011, 09:31
    4. Replies: 4
      Last Post: 16th June 2011, 12:03
    5. Replies: 17
      Last Post: 22nd April 2010, 12:53

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...