Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

    Report Post
    Results 1 to 16 of 16
    1. #1
      PrN-kazi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Posts : 2,248
      Rep Power : 5370
      Likes Received
      307
      Likes Given
      4

      Default Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira ndo leo inasomwa: bila shaka walioko karibu na eneo la tukio wana mengi ya kutujuza hususani sisi wana-jamii wa JF.


    2. #2
      Wa kusoma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th July 2011
      Posts : 989
      Rep Power : 496
      Likes Received
      321
      Likes Given
      50

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      ameshasema ajira zimeongezeka mara dufu unasubiri nini hapo?

    3. #3
      Ngongo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th September 2008
      Location : Mlima Meru
      Posts : 4,972
      Rep Power : 6859
      Likes Received
      2415
      Likes Given
      3175

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Tunahitaji mabadiliko makubwa ya sera ya ajira Tanzania.Soko la ajira limevamiwa na raia wa kigeni sheria ya kulinda ajira ya wafanyakazi waTanzania inahitajika haraka.Leo ukitembelea sekta yoyote unayoijua utakutana na wafanyakazi wenye uraia wa mataifa mbali mbali waKenya na waHindi wanaongoza.

      Jaribu kuangalia sekta ya utalii utashangaa mpaka tour guide ni wakenya na wazungu !!!.makampuni ya uwakala wa utalii eg A & K,Sokwe Asili,Leopard Tours,Serena lodges,TGT,Grumeti Reserves,B to B,Wldersun Safaris na Ranger Safaris zinaongoza kwa kuajiri wafanyakazi raia wa kigeni kuanzia jikoni,stores,accounts,mapokez i na madereva.

      Nauliza kuna sababu zipi za kuendelea kuwa na wizara ya Kazi na Ajira wakati kazi zinazoweza kufanywa na watanzania zimeporwa na wageni ?.Ukitembelea viwanda vinavyomilikiwa na waHindi utashangaa nchi hii inavyoendeshwa wahindi wamejazwa hakuna mfano wake.Juzi nilitembelea kiwanda cha kusindika mafuta ya alizeti SUNOLA nikakutana na waHindi wanahesabu magunia ya Alizeti.Ebu fikiria mgeni analetwa kuhesabu magunia ya Alizeti ?.
      zumbemkuu and Diehard like this.

    4. #4
      genekai's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th February 2010
      Location : Loitering!
      Posts : 7,691
      Rep Power : 2122
      Likes Received
      1159
      Likes Given
      1601

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Nimemfuatilia huyu Binti Kawawa anaonekana kuwa na akili, she has really impressed me kwa alivyochangia!
      The future of this country is being jeopardized by the intellectual slavery of our top leaders

    5. FJM is offline
      FJM
      #5
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,213
      Rep Power : 2580
      Likes Received
      5344
      Likes Given
      4607

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Quote By genekai View Post
      Nimemfuatilia huyu Binti Kawawa anaonekana kuwa na akili, she has really impressed me kwa alivyochangia!
      Kasema nini huyu binti Kawawa?


    6. #6
      PrN-kazi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2011
      Posts : 2,248
      Rep Power : 5370
      Likes Received
      307
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By Wa kusoma View Post
      ameshasema ajira zimeongezeka mara dufu unasubiri nini hapo?
      <br />
      <br />
      Hata na hiyo ni habari; nashukuru kuipata.

    7. #7
      pmwasyoke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th May 2010
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 2,514
      Rep Power : 986
      Likes Received
      338
      Likes Given
      438

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Hali ya ajira kwa vijana ni tata, na ni bomu tarajiwa. Inatakiwa mikakati thabiti ya kukuza sana uchumi ili kuzalisha ajira nyingi.

    8. #8
      calmdowndear's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th July 2011
      Posts : 120
      Rep Power : 430
      Likes Received
      29
      Likes Given
      26

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      tatizo la ajira ni dunia nzima..kuanzia america mpaka eurozone na jana wenyewe mmeona stocks zilivyo plument

      tatizo letu ni umeme ...huwezi kuwa na ajira kama umeme huna....unless JK alete major infrastructure projects kama Nairobi -Thika road

    9. #9
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,475
      Rep Power : 19245
      Likes Received
      4193
      Likes Given
      3374

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Quote By Ngongo View Post
      Tunahitaji mabadiliko makubwa ya sera ya ajira Tanzania.Soko la ajira limevamiwa na raia wa kigeni sheria ya kulinda ajira ya wafanyakazi waTanzania inahitajika haraka.Leo ukitembelea sekta yoyote unayoijua utakutana na wafanyakazi wenye uraia wa mataifa mbali mbali waKenya na waHindi wanaongoza.

      Jaribu kuangalia sekta ya utalii utashangaa mpaka tour guide ni wakenya na wazungu !!!.makampuni ya uwakala wa utalii eg A & K,Sokwe Asili,Leopard Tours,Serena lodges,TGT,Grumeti Reserves,B to B,Wldersun Safaris na Ranger Safaris zinaongoza kwa kuajiri wafanyakazi raia wa kigeni kuanzia jikoni,stores,accounts,mapokez i na madereva.

      Nauliza kuna sababu zipi za kuendelea kuwa na wizara ya Kazi na Ajira wakati kazi zinazoweza kufanywa na watanzania zimeporwa na wageni ?.Ukitembelea viwanda vinavyomilikiwa na waHindi utashangaa nchi hii inavyoendeshwa wahindi wamejazwa hakuna mfano wake.Juzi nilitembelea kiwanda cha kusindika mafuta ya alizeti SUNOLA nikakutana na waHindi wanahesabu magunia ya Alizeti.Ebu fikiria mgeni analetwa kuhesabu magunia ya Alizeti ?.

      A
      . Kuna matatizo ambayo watanzania tuna paswa kubadiliaka…
      1.Uvivu 2. Kutokujari 3. kutokuwajibika 4. Lugha…kama kuna mtu anashughulika na makampuni ya utalii atakuwa anayafahamu haya vizuri jinsi watanzania tunavyofanya madudu kwa hayo niliyoyataja…

      B. kwenye kiwanda cha SUNOLA wale wahidi wana uraia wa Tanzania hivyo ni watanzania yaani utanzania wa makaratasi...
      Nobody can give you freedom. Nobody can give you equality or justice or anything. If you're a man, you take it.... Malcolm X





    10. #10
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,475
      Rep Power : 19245
      Likes Received
      4193
      Likes Given
      3374

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Quote By calmdowndear View Post
      tatizo la ajira ni dunia nzima..kuanzia america mpaka eurozone na jana wenyewe mmeona stocks zilivyo plument

      tatizo letu ni umeme ...huwezi kuwa na ajira kama umeme huna....unless JK alete major infrastructure projects kama Nairobi -Thika road
      Kama Tanzania ingejipanga tatizo la ajira lingekuwa dogo mno kama si kulimaliza kabisa ni kupe mfano kufungwa kwa kiwanda cha kutegeneza matairi(General Tyre) kumekosesha watanzania wangapi? ikumbukwe kilimo cha mpira kingepanuka na Tanzania ndiyo iliyokuwa inategemewa Afrika mashariki...kiwanda cha kutegeneza magunia nacho hivyo hivyo...Pamba kama tungekuwa na viwanda vya kutosha kilimo cha pamba kingeongezeka, watu wangeajiriwa kwenye viwanda husika na kutegeneza ngo kutoka hapa badala ya kusafirisha pamba kwenda nje...Kwenye blue tuko pamoja
      pmwasyoke likes this.
      Nobody can give you freedom. Nobody can give you equality or justice or anything. If you're a man, you take it.... Malcolm X





    11. #11
      Saracen's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th April 2011
      Posts : 127
      Rep Power : 439
      Likes Received
      55
      Likes Given
      63

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      hivi mmeona presentation ya daraja la Kigamboni?

    12. #12
      Ernesto Che's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2011
      Posts : 616
      Rep Power : 551
      Likes Received
      100
      Likes Given
      24

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Tatizo la ajira haliwezi kuisha kirahisi kwani wanaoitwa wawekezaji wanakuja mikono mitupu na briefcase kisha wanahamisha fedha zote kwao, mafasi zote za juu wanakamata wao tena mishahara yao mikubwa mara hata 10 ya wazawa, pia hawawekezi chchote mitaji wanaiba hapa hapa. Mifano mizuri ni kampuni ya Airtel, Zantel, GGM, Kiwira, NASACO, TAZARA, TRC kila sehemu zimehujumiwa na viongozi na ajira za watu kwa maelfu zimeotea.
      JK anaota ndoto za kuongza ajira wakati kwa vitendo anazidi kupunguza ajira... hii ni n ini? (nahifadhi maneno)....Hakuna kiongozi yeyote wa CCm aliye serious kabisa
      "If there is no struggle, there is no progress.”

    13. FJM is offline
      FJM
      #13
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,213
      Rep Power : 2580
      Likes Received
      5344
      Likes Given
      4607

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Nimebahatika kuona Waziri Gaudensia Kabaka na Naibu wake Makongoro wakijibu hoja/maswali ya wabunge jioni wakati wa hitimisho wa bajeti ya wizara ya kazi ajira na vijana. Tatizo kubwa nililoona na la msingi sana ni kwamba both Waziri na Naibu wake hawaonekani kujua mambo mengi kuhusu Wizara yao! Na hasa Makangoro, anaonekana hata haelewi maswali yaliyouliuzwa na matokeo yake anaishia kusoma vifungu vya sheria. Kwa mfano, mwenyekiti wa Kamati inayosimamia wizara hii Jennista Mhagama aliuliza nafasi ya Wizara katika kusimamia upatikanaji wa haki kwa wafanyakazi "wanyonge" pale mahakama inapoamuru. Makongoro anasema tatizo ni watu kutojua sheria!

      Jambo kubwa alilouliza Mhagama hapa ni "Haki za wanyonge". Hawa watu hawana uelewa mpana wa sheria yes, lakini wanaelewa pale wanapodhulumiwa. Hata hivyo ukweli ni kwamba baadhi ya wamiliki wa hivi viwanda i.e Jambo Plastic wana ukaribu na 'wakubwa' na hivyo wanakuwa na jeuri ya hata kutotii amri ya mahakama. Na hapa ndipo serikali kupitia wizara anayokalia Makongoro wangetakiwa wasimame na hawa wanyonge. Matokeo yake amejibu - hawajui sheria! Sasa Wizara inafanya nini ili hawa wanyonge wajue sheria?

      Lakini kubwa zaidi ni nafasi ya KITI CHA SPIKA kutosimamia hoja za wananchi kama zinavyowakilishwa na wawakilishi wao yaani wabunge. Nilitegemea Naibu Spika aliyekuwa anaongoza kikao atamke waziwazi kuwa waziri na naibu wake wamekuwa wanatoa majibu yasiyoridhisha na wanaonekana hata kutofahamu vizuri mambo mengi yanayot0kea katika wizara hii. Hivyo angewapa muda i.e 24hrs waje na majibu! Hii ndio tafsiri halisi ya nini maana ya kuwa na kiti cha spika.

      Kama kuna mtu yuko karibu na Makongoro na bosi wake Mama Kabaka basi wawape somo maana majibu yao leo bungeni yameanika utupu wao 'upstairs'. They just dont seem to know what is happening around their Ministry. What a shame!

    14. #14
      Freedom Of Flag's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Location : Home
      Posts : 376
      Rep Power : 482
      Likes Received
      143
      Likes Given
      156

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Nilidhani wangezungumzi ku ammend the Employment & Labour Relation Act no 6, imejaa wizi mtupu, Kapuya na Kipenka waliiforce ipite in favour of the Employers/Owners.

    15. #15
      Mapujds's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th May 2011
      Location : Dar es salaam
      Posts : 1,282
      Rep Power : 670
      Likes Received
      118
      Likes Given
      6

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      Hakuna mikakati maalumu ya serikali katika kuwapatia ajira wananchi wake.

    16. #16
      Tango73's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2008
      Posts : 1,060
      Rep Power : 748
      Likes Received
      294
      Likes Given
      2

      Default Re: Bajeti ya Wizara ya Kazi na Ajira

      ni hatari kubwa sana kuwa na mawaziri wasio jua nini maana ya unaemployment au watu wasio na uhai. wakulima wa kitanzania ni wale watu wanaowakilisha jamii ya watu wasio na uhai, pamoja na wavuvi na wauza sokoni. Wizara ya kazi na Ustawi wa jamii maana yake , ni wizara inayohusika katika kujenga working class na kuwapeleka watu katika dalaja la pili kimaisha katika jamii. Yaani watu wenye uwezo wa kujihudumia wenyewe kiafya,kielimu,kupata mikopo benki ya kutatua matatizo yao na kuborsha maisha ya familia zao. Yaani watanzania wote waishi ki-oysterbay type.

      Unapokuwa na waziri asiyejua nini maana ya wizara ya kazi na ana -thubutu kusema watu wasio na kazi hawajui sheria. Huyu waziri ni hatari ni hatari katika jamii kupita hata majambazi sabini wenye mastola. nani sasa ategemewe kuwasafilisha wanyonge kuelekea katika maisha ya daraja la pili, kama siyo yeye? Kasumba ya maisha ya kitanzania ni kuwa mtu kuishi maisha ya daraja la pili lazima uwe msomi, viongozi wote wenye kasumba hii, hawajengi nchi ila wnatesa wanyonge.

      Baba akizaliwia katika nyumba ya nyasi, lazima mtoto wake azalie katika nyumba ya bati na mjukuu wake naye aolee na kushi katka nyumba ya vigae. haya ndio masiha ya kusafilisha mnyonge toka mashambani mpaka maisha ya mjini . Ndio maana tuna waziri na wizara ya kazi.

      Kuwapatia watu kazi ni muhimu kupita kabisa kuwapatia watu kadi za chama. Viwanda vya wawekelezaji lazima viwe na masharti mazuri ya kuwekeleza ili mzalendo apewe kipaumbele. Lakini wakiwa na amsharti ya kutaka raia zao waletwe kufanya kazi na kutaka watanzania wafaidike kidogo katika ajira. Huo tena ni utumwa na safari ya mnyonge kuelekea maisha ya dalaja la pili katika jamii yatagonga mwamba. Tutajikuta tuna viwanda vingi lakini ajira kwa mzawa ni kero.

      NI vizuri kabisaa kuwatafuta wawekelzaji wa Ulaya, marekani na Israel wawekeze katika viwanda na kilimo, maana wao hawaleti watu wao kufanya kazi za wazalendo kama ilivyo kwa waasia au waarabu, bali wao wa ulaya , hufundisha wazalendo jinsi ya kufanya kazi zao.

      Mataifa ya ulaya marekani na Israel hayana shida ya kuwatafutia soko la Ajira watu wao nje ya nchi zao kama ilivyo kwa asia na uarabuni. Hivyo hata marekani akikodisha ardhi ya kulima mahekali mia, atafaidika mtanzania kwa kupata kazi. Naomba raisi amfukuze kazi waziri wa kazi na naibu wake pamoja na watendaji wakuu wote wa wizara ya kazi. La sivyo mnyonge wa nyumba ya nyasi atapata mjuukuu katika nyasi nae atazalia nyumba ya nyasi..

    Similar Topics

    1. Replies: 24
      Last Post: 11th April 2012, 04:41
    2. Kwa serikali, uhamiaji na wizara ya kazi ajira na vijana,
      By Chasha in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 6
      Last Post: 12th November 2011, 20:17
    3. Replies: 8
      Last Post: 25th August 2011, 15:57
    4. Wizara ya Kazi, Ajira na maendeleo ya vijana- Tovuti yenu inatia aibu
      By Sisimizi in forum Tech, Gadgets & Science Forum
      Replies: 1
      Last Post: 5th July 2010, 23:17
    5. Wizara ya kazi: Tatizo la ajira nchini lapungua toka 16% mpaka 13%
      By Hofstede in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 13th December 2008, 07:48

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...