Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Maneno yanayonikera siasa za CCM: uchochezi, uchonganishi, kutishia amani na uvunjifu wa amani

    Report Post
    Page 3 of 5 FirstFirst 12345 LastLast
    Results 41 to 60 of 92
    1. DSN
      #1
      DSN's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st April 2011
      Location : Home Tanzania
      Posts : 1,443
      Rep Power : 4452
      Likes Received
      690
      Likes Given
      576

      Default Maneno yanayonikera siasa za CCM: uchochezi, uchonganishi, kutishia amani na uvunjifu wa amani

      Wanasayansi wamefanya utafiti na kugundua kila binadamu anayezaliwa chini ya uso wa dunia yetu hiii ni Mwanasiasa kwa kuzaliwa kwa kuwa asilimia kubwa ya maisha yake yanaimarika na kustawika au kuathirika kwa sababu ya siasa.

      Ndio maana kuna chaguzi ambazo ni haki yake ya msingi ya kuchaguliwa yeye au kumchagua mtu yoyote ambae yeye kwa imani yake anaona anastahiki kumuongoza ili kumuonyesha njia apate ustawi binafis wa maisha yake, familia yake na Taifa lake kwa ujumla.Hivyo Viongozi Serikali na Wanasiasa wa CCM siasa ni sehemu ya maisha ya Watanzania wote Millioni 40.7.

      Kupitia utafiti huo wa Wanasayansi hao hata mimi nae ni Mwanasiasa kwa kiwango changu. Kinachonikera katika siasa za chama cha Mapinduzi ni maneno ambayo viongozi wake wa kisiasa na wale walioko Serikali wanavyopenda kuyatumia sana kiasi kuwa kwa mwelevu yoyote yule maneno hayo yamesemwa sana kiasi kuwa Wananchi wameshagundua nyuma ya pazia ya matumizi ya maneno hayo kwa Viongozi na Wanasiasa hao. Japo kwa upofu wa Viongozi wetu wa Kisiasa na Serikali wanajisau na kuona Wananchi hawalijui hilo na wala hawaoni matendo yao.

      Maneno kama Uchochezi, Uchonganishi, Kutishia Amani, Uvunjifu wa Amani,hizo ni hisia ,Uthibitisho,upotoshaji wa Wananchi,Wivu,Wapinga Maendeleo,fikra potofu, Intelegensia nk.

      Yamekuwa ni maneno ambayo yameifikisha CCM hapo ilipo sasa ya kupoteza imani kwa Wananchi,kwa kuwa yamefikia kuwa yanasemwa na Viongozi wa Kichama na Serikali ambao Watu [Wananchi] huku site [Makongoro] wanawajua kuwa si wenye hadhi ya kuyatamka hayo.

      Wananchi sio kuwa hawajui adui yao ni nani, wasichonacho ni nyenzo na mbinu za kupambana na adui wao huyo.Kwa kuwa wengi wa maadui zao wako ndani ya mfumo hivyo kuwakabili inakuwa kazi ngumu njia iliyopo kwa Wananchi ni kukwangua gamba la juu la Kobe taratibuuu!! Mpaka kufikia kichwa cha Kobe.Kwa wanaojua jinsi ya kutibu virus wa TB ,dawa yake ndio itakayotumiwa na Wananchi kama TIBA ya tatizo lao hivyo nguvu ya umma ndio siraha waliyonayo mkononi.

      Chama cha Mapinduzi kitambue kuwa maneno hayo yanakera [Irritate] sana yanapotumika kwa sasa, yanaongeza ufa dhidi ya chama hicho dhidi ya Umma.Yangesemwa hivyo wakati Nchi na Wananchi wake wako kwenye ustawi yaani maisha BORA hakika kila Mwananchi angesimama kuyaunga mkono kama ambavyo Wananchi walivyounga mkono azimio la Arusha huko nyuma.

      Viongozi wa CCM na Serikali Kwa faida yao waepuke nakuacha kabisa matumizi ya maneno hayo,kwa kuwa ndio yanayoongeza moto, kama ni wimbo basi ni mwimbo wa Mwaka 47. Kama mnabisha endeleeni kuyatumia muuone moto wake.

      Sooooooooooon and very soooonnnnn!!!

      Nawasilisha.

    2. FemaTV & Radio

    3. #41
      Kima Mchanga's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 3rd October 2011
      Location : Dynamic
      Posts : 4,471
      Rep Power : 11219
      Likes Received
      598
      Likes Given
      446

      Default Re: Amani ya Tanzania haina maisha marefu...

      Amani gani unayo izungumzia ndugu?
      Amani ilishatoweka muda mrefu;umebaki utulivu tu,tena wa bandia!!!
      Do what you feel in your heart to be right-for yot will be criticized anyway.You will be damned if you do,and damned if you don't

    4. RMA
      #42
      RMA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2010
      Posts : 410
      Rep Power : 518
      Likes Received
      87
      Likes Given
      0

      Default Re: Amani ya Tanzania haina maisha marefu...

      Kikwete ndio chaguo la Mungu ili watanzania mjifunze!! Ni vema maisha yaendelee kuwa magumu zaidi ili mpate akili. Safari nyingine msifanye ushabiki wa Yanga na Simba katika siasa bila kutazama uhalisia wa mambo! Mnapiga kura kama vipofu halafu mnalalama kama vichaa! Maisha duni kwa kila mtanzania ni haki yenu! Mnastahili kwa kuwa huyo rais mnayemlalamikia ni ninyi mliomchagua!
      Mungi likes this.

    5. #43
      NusuMutu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th September 2011
      Location : Mpulungu
      Posts : 421
      Rep Power : 470
      Likes Received
      74
      Likes Given
      20

      Default

      Tazama jinsi Wanasi-hasa,viongozi wa dini na wafanyabiashara walivyo tumika kuhakikisha tunaishi maisha haya tunayoishi. Waliwadanganya wananchi kuwa bw.mkubwa ni chaguo la Mungu,hivi Mungu anapenda watu wake waongozwe na kiongozi asiye na maamuzi? Na bado wanawasafisha wachafu kunuka na wavivu wa kufikiri kwa maslahi yao,nchi inaangamia.watu wengi wamenya lakini kwa sababu sikio la kufa haliskii dawa,haya ngoja tuwepo tuwepo kwanza

    6. #44
      Mungi's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 23rd September 2010
      Location : Hapa!!!
      Posts : 10,142
      Rep Power : 24265
      Likes Received
      4659
      Likes Given
      2294

      Default Re: Amani ya Tanzania haina maisha marefu...

      Tanzania hakuna Amani inayotokana na Mioyo iliyoridhika, kuna Amani inayotokana na nguvu ya jeshi la polisi, ambayo sasa inafikia ukingoni. RIP amani ya Tanganyika.

    7. #45
      dotto's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th September 2010
      Posts : 1,395
      Rep Power : 717
      Likes Received
      156
      Likes Given
      16

      Default Re: Amani ya Tanzania haina maisha marefu...

      amani ya kuambiwa tupige mbizi au turudi vijijini. Manake kukaa vijijini ni adhabu!!?

    8. Miaka 50

    9. #46
      NGUVUMOJA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2011
      Posts : 863
      Rep Power : 571
      Likes Received
      138
      Likes Given
      26

      Default

      Quote By Kinto
      Du!!! leo nimeamka na jumbe za ajabu kuhusu amani ya Tz kuwekwa rehani na viongozi wasio waadilifu, maana nimetoka kusoma jumbe huu hapa chini. Mie sijui kama ni kweli au la...lakini nikiunganisha na thread yako...naanza kupata mashaka.

      MAONYO JUU YA VIONGOZI WA NCHI YA TANZANIA.
      Bwana wa Majeshi, Muumba mbingu na dunia; Asema, nimesikia kilio chao wanaoonekana ni wanyonge. Nami nitaondoa amani na kuleta vita, itakayodumu kwa muda wa mwaka mmoja. Ili nikikomeshe kiburi cha mwanadamu, mpate kujua kuwa mimi Mungu ndiye niletaye Amani ya nchi. Kwa sababu hamtendi haki!!. Vilivyopaswa kula wajane na yatima mmekula viongozi. Mimi Mungu nitamfutilia mbali kila aliye na utukufu wake mwenyewe na aliye jiinua juu ya nchi atakufa yeye pamoja na nyumba yake.Sikieni ninyi nyote mnaoijua siri hii kuwa nchi hii siyo masikini! Nanyi mnajua kuwa nchi hii siyo masikini; Kwa nini mnasema uongo kuwa nchi hii ni masikini? Basi mimi Mungu nimesikia msemayo. Maneno yenu, na vinywa vyenu vinanuka mbele zangu kwa sababu yote mliyoyasema ni kwa ajili ya faida zenu wenyewe. Ili kuwaficha watu wachini na wanyonge. Kuwafumba wasijue ukweli wa uzuri wa nchi yao pamoja na utajiri wake. Ili ninyi mpate kufaidi na kuwadhulumu haki yao.Tanganyika (Tanzania) ni nchi yenye utajiri mwingi sana, fikirini kwa makini ninyi mnaosema kuwa nchi hii ni masikini!! Je mimi Mungu ni muongo? Mimi niliyeweka utajiri mwingi kwenye nchi hii; utajiri wa aina mbalimbali pamoja na madini ya aina nyingi mengine hamjayajua?Kwa nini mnathubutu kusema kuwa nchi hii ni masikini?. Mmeufungua utajiri wa nchi hii na kuwapa wageni kwa faida zenu viongozi. Hakika Mimi Mungu nimeyaona mateso ya wanyonge wa Tanganyika (Tanzania)!!.Geukeni basi mkatende haki! Lakini msipogeuka hakika maombolezo yanakuja. Asema Bwana wa Majeshi ambae ni chanzo cha Tanganyika !Basi tazama nimenyoosha mkona wangu juu yako, nami nitakutoa uwe mateka ya mataifa. Nami nitakukatilia mbali na kabila za watu, nami nitakuangamiza usiwe katika nchi hizi; nitakukomesha nawe utajua yakuwa mimi ndimi Bwana! Ezekiel 25:7Walikuwa kama farasi walioshiba wakati wa asubuhi, kila mmoja akalia kwa kutamani mke wa mwenzake. Je nisiwapatilize kisasi juu ya taifa la namna hii? Pandeni juu ya kuta zake mkaharibu, lakini msiharibu kabisa, ondoeni matawi yake kwa maana si yake Bwana - Yeremia 5:8-10Ujumbe huu Bwana alisema nami alfajiri ya tarehe 8/01/2012 saa 10-11 alfajiri. Ujumbe kwa ajili ya viongozi wa Taifa la Tangayika (Tanzania)
      Mimi..MJOLI WA BWANAREBEKA SHIJA MASANJASIMU: 0718- 600 557
      Bangi+gongo=ukichaa. Tangu lini mlevi wa gongo akawa Mungu?. Wehu mtupu!

    10. #47
      NGUVUMOJA's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st July 2011
      Posts : 863
      Rep Power : 571
      Likes Received
      138
      Likes Given
      26

      Default

      Quote By NG'OMBE
      Ubinafisi wa viongozi wetu, kutokusoma alama za nyakati na uzembe wa kufikiria ndiyo umelifikisha hapa Taifa hili, migomo vyuo vikuu, mfumuko wa bei, wizi wa fedha za umma, viongozi makatili wasio na huruma na watoto wa masikini ndiyo watakaoamusha hasira za watanzania wote. Nawaomba waendelee tu na tabia hizo za ukatili lakini mwisho wao umekaribia.Iko siku tutawafanyia ukatili mkubwa sana wao na familia zao na hawataamini kitakachotokea muda si murefu. Vijana kwa wazee tuendeleze harakati za kudai haki ndani ya nchi yetu ambayo imeporwa na viongozi wenye ROHO YA SHETANI. vijana mnaoonewa vyuoni msikate tamaa jipeni moyo MUNGU wetu ni mwaminifu mwisho tutashinda tu dhidi ya uongozi dhalimu wa nchi yetu.
      Nyie tuchocheeni tu eeenh? Siku vikija kuwaka kiukweli mtaimba 'maweeee!'. Vurugu hazina macho, hayo sio mambo ya kuyachochea na kuyashabikia hata kidogo.

    11. #48
      timbilimu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd September 2010
      Location : DSM
      Posts : 2,658
      Rep Power : 973
      Likes Received
      576
      Likes Given
      10

      Default Re: Amani ya Tanzania haina maisha marefu...

      Amani haipatikani bila kumwaga damu,hii unaona sasa ni utulivu tu hakuna amani.
      Mungi likes this.

    12. #49
      ndevu mzazi's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th November 2011
      Posts : 245
      Rep Power : 429
      Likes Received
      35
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By RMA
      Kikwete ndio chaguo la Mungu ili watanzania mjifunze!! Ni vema maisha yaendelee kuwa magumu zaidi ili mpate akili. Safari nyingine msifanye ushabiki wa Yanga na Simba katika siasa bila kutazama uhalisia wa mambo! Mnapiga kura kama vipofu halafu mnalalama kama vichaa! Maisha duni kwa kila mtanzania ni haki yenu! Mnastahili kwa kuwa huyo rais mnayemlalamikia ni ninyi mliomchagua!
      Ni NEC waliomchagua sio sisi.
      Mungi likes this.

    13. #50
      Adharusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd January 2012
      Location : Mtwara
      Posts : 466
      Rep Power : 462
      Likes Received
      62
      Likes Given
      295

      Default Amani yetu watanzania imetusaidia katika jambo gani???

      Uchumi
      siasa
      kijamii
      katika miaka 50.!!!.5

    14. #51
      Adharusi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd January 2012
      Location : Mtwara
      Posts : 466
      Rep Power : 462
      Likes Received
      62
      Likes Given
      295

      Default Amani yetu imetusaidia nini watanzania??

      Kiuchumi
      kisiasa
      kijamii
      Nataka mnipe tofauti na nchi zenye vita,mfano sudan,na zilizowahi ingia katika vita,mfano Nigeria,Libya(mapinduz1967)alg eria n.k
      kwanini sisi ni watatu kwa kuomba duniani,wakwanza afrika.5

    15. #52
      Angel Msoffe's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st June 2011
      Posts : 6,266
      Rep Power : 1825
      Likes Received
      1397
      Likes Given
      0

      Default Re: Amani yetu imetusaidia nini watanzania??

      amani na uoga wetu vimetuletea umaskini

    16. #53
      Third Eye's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 8th January 2012
      Posts : 165
      Rep Power : 460
      Likes Received
      26
      Likes Given
      13

      Default Re: Amani yetu imetusaidia nini watanzania??

      hata hyo amani yenyewe ipo?mi naona utulivu tu ndo tunao

    17. #54
      Snitch's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 22nd October 2011
      Posts : 163
      Rep Power : 414
      Likes Received
      36
      Likes Given
      6

      Default Re: Amani yetu imetusaidia nini watanzania??

      Kichaa sio lazima atembee uchi

    18. #55
      Laura Mkaju's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 31st January 2011
      Posts : 194
      Rep Power : 458
      Likes Received
      35
      Likes Given
      0

      Default Re: Amani yetu imetusaidia nini watanzania??

      Vimetuletea umaskini wa kufikiri

    19. #56
      bombu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th June 2011
      Posts : 1,035
      Rep Power : 878
      Likes Received
      497
      Likes Given
      592

      Default Re: Amani yetu imetusaidia nini watanzania??

      Kweli Laura, yaani hata kujifikiria wenyewe tumeshindwa. Eti, tuilinde amani tuliyoachiwa na waasisi, total ----, twafa na njaa zetu. Ingawa mie naamini, kimya kingi kina mshindo mkuu

    20. BAK
      #57
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,523
      Rep Power : 44948
      Likes Received
      8272
      Likes Given
      8280

      Default Re: Amani yetu imetusaidia nini watanzania??

      ...Nchi kuendelea kuangamia katika kiwango cha kutisha.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    21. #58
      mikatabafeki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th December 2010
      Posts : 4,835
      Rep Power : 1396
      Likes Received
      765
      Likes Given
      1463

      Default Re: Amani yetu imetusaidia nini watanzania??

      mbona na bado kazi tunayo.
      when love goes wrong,nothing goes right.

    22. #59
      sammosses's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2011
      Location : Shinyanga
      Posts : 905
      Rep Power : 602
      Likes Received
      167
      Likes Given
      238

      Cool Tuache unafiki ,tuimbe tunachokiamini kujenga amani na upendo ndani ya taifa letu

      Mungu ibariki Tanzania,dumisha uhuru na umoja,wake kwa waume na watoto ,hekima umoja na amani,hizi ni ngao zetu Tanzania na watu wake.Maneno yalitomkwa katika wimbo wetu wa taifa ni mazito,yamekuwa yanatumiwa sana hususani pale panapotokea wageni wa kiserikali wakiingia nchini kwetu,ama viongozi wa kitaifa wakihutubia Taifa au kuna tukio kubwa ambao wananchi wanapaswa kulisikiliza kwa makini.Mashairi ya wimbo huu yamesheheni ujumbe mzito juu ya mstakabali wa taifa letu na uzalendo miongoni mwa wananchi wake.

      Maneno yaliyobebwa kwenye beti zote mbili za wimbo huu yana ujumbe mzito bila kuwabagua watu wake.Ukisikiliza kwa makini utagundua yanazungumzwa kwenye mashairi haya hayafanyiwi kazi bali unafiki na uzandiki umetawala ndani ya mioyo yetu.Umojaunaozungumziwa humo haupo kwa vitendo japokuwa walioubuni wimbo huu walilenga kudumisha amani na upendo ndani ya taifa letu.Kinachofanyika leo mazingaombwe matupu,hakuna anaye muamini mwenzake si kwenye taasisi za umma wala sekta binafsi,kila mmoja ni adui wa mwenzake.Huwezi ona mtu anaacha maji yake wazi,kwa kuogopa kunyunyuziwa sumu toka ughaibuni,hii ni hatari sana.Kuna haja gani ya kuimba tusichokiamini ilihali kila mmoja nia adui wa mwenzake.

      Uzalendo ninao zungumzia humu ni ile hali ya mapenzi na nchi yetu,mapenzi haya yametoweka ndani ya mioyo ya Watanzania ama kwa kusababisha na kuvunjika kwa imani iliyojengwa na wananchi kwa viongozi wake
      au taifa limepoteza maadili ya kitaifa.Si ajabu leo ukasikia kiongozi aliyepewa dhamana ya uongozi akitumia jukwaa hilo la uongozi kwa kuwakejeli wananchi waliompa dhamana hiyo.Viongozi wanayoyasema hayaendani na matendo yao,nchi imepoteza amani na upendo na kuzalisha matabaka ya kijamii kati ya watwana na mabwana kwa kutumia rasilimali ya taifa katika kujineemesha wao binafsi bila aibu.

      Uzalendo huu uliopotea miongoni mwetu ni lin utapatiwa tiba maridhawa kama Watanzania hatuacha uoga na kuwa waadilifu ili kuhifadhi amani na upendo tuliouimba kuwa tutaudumisha.Tumekuwa kama utawala wa kambale kila mmoja ana ndevu,mama ndevu,baba na watoto halikadhalika.Tuwe wepesi kutenda tunachokiamini kuliko kuwa
      wanafiki kwa kuimba nyimbo za kudumisha amani upendo wakati sisi wenyewe ndiyo tunaibomoa amani kwa mikono na matendo yetu.

      Mwisho,mustakabli wa amani na upendo miongoni mwetu upo mikononi mwa kila mmoja wetu,tukimuogopa Mungu na kuacha unafiki tutajenga taifa lenye kuheshimika na maadili.Tufanye siasa zetu na kuonyesha ukomavu wa demokrasia bila kujali maslahi yetu binafsi,tuache imani ya kujiaminisha kuwa kuna baadhi ya wenzetu walizaliwa kuwatawala wenzao ikibidi kwa mabavu ili kutimiza malengo yao ya siku.Imani na upendo tunaoimba si tu ujumbe wake ubaki kwenye mashairi ya nyimbo hiyo bali huonyeshwe kwa vitendo nchi inatawalika kwa amani bila unafiki unaofanywa na wapenda madaraka ambao uwezo wao wa kiuognozi umefika kikomo lakini hawataki kuonyesha wamechoka kifkira na kiuwezo wa kiutendaji,kwani hata Karumekenge alipogoma kwenda shule alikubali kadhibiwa na kwenda shule pale alipogundua hakufanya kinachostahili kwa mgomo wake wa kutokwenda shule.Kila mmoja si tu atimize wajibu wake bali ahakikiishe ni mlinda amani na upendo ndani ya taifa letu.

    23. #60
      Mwangaza's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 12th August 2010
      Posts : 112
      Rep Power : 467
      Likes Received
      15
      Likes Given
      15

      Default Amani hakuna tena,ni vitisho,vipigo,mateso,sumu,mau aji.. Bora kinuke tu!

      Wadau,

      Amani ya Tz aliyoienzi baba wa Taifa haipo tena.

      Polisi walioapa kulianda raia na mali zao, wakiishi kwa mishara ya kodi zetu ..dio wanaongoza mashambuliz na mauaji ya raia wasio na hatia.

      Viongoz walipewa dhamana ya kutuongoza, wamegeka kuwa za viongoz wa kupola rasimali zetu, kutunyanyasa,kutupiga na kutuua sababu tu tuna tofautiana nao kisiasa.

      Tumeshuhudia wakala wa CHADEMA igunga (Bwana Masoudi) akipoteza maisha kwasababu za kisiasa, na wengine hawajulikani walipo..mpaka leo hakuna aliyekamatwa.

      Tumeshuhida ndugu zetu wakiuwawa na pilisi kwenye migodi ya Norh Mara,Nyamongo n.k..mpaka leo hakuna aliyekamatwa.

      Tumeshuhudia kiongoz wa CHADEMA Arusha akitekwa,kunyanyaswa na kumwagiwa tindikali...mpaka leo hakuna aliyekamatwa.

      Tumeshuhudi watu mbali mbali walio mstari wa mbele kuttea haki na kutufumbua macho wakitaka kuwawa,kumwagiwa tindikali,kuwekewa sumu,kubambikizwa kesi nk..mfano Mh Mwakyembe, Sued kubenea, Mwibala,Gobless Lema,Mama Anenelia Ankya, n.k n.k

      Na hii ya sasa inazidi kuvuka mipaka...viongoz wetu, wabunge wetu (Mh. Kiwia na Mh Machali)..wamekatwa mapanga, kiasi cha kutaka kuliwa mbele ya macho ya polisi. bila polisi kuchukua hatua zozote.

      Pamoja na kuwekwa wazi kwamba kada wa UVCCM, Ahmed Mkilindi aliongoza uvamiz huo na anamjeruhi mkononi, na gari zilikuwepo eneo la tukiao ni namba T 377 ARF la mh. Kiwia, T 729 DAD la Mohamed Juma pamoja na T 397 ANU aina ya Land Cruiser ambalo mmiliki wake hakupatikana, (kwanini hakupatikana, Polisi inashindwaje kumpata/kumjua mmiliki siku zote hizo?)...lkn mpaka sasa hakuna hata mtuhumiwa mmoja alikemmatwa, japo kwa mahojiano tu.

      Pamoja na matukio mengi tu kama haya yanaondelea mitaani kwetu, ambayo yanafichwa..JE NANI ATAFUATA? JE NANI YUPO SALAMA TZ, KAMA HATA VIONGOZ WANATAKA KUWAWA NA POLISI WANAANGALIA?

      JE TUTAENDELEA KUISH HIVI, KTK NCHI YETU MPAKA LINI?

      HAKIKA, HAUTAWEZA..NI VIGUMU KUVUMILA.KARIBU UVUMILIVU UTATUSHANDA... BORA KINUKE TUJUE TU!
      KAMA UNAYO HAKI UNASTAHILI KUPEWA, KAMA HUJAPEWA DAI KWA NGUVU ZOTE.

    24. Study Abroad
    Page 3 of 5 FirstFirst 12345 LastLast

    Similar Topics

    1. Replies: 4
      Last Post: 19th December 2011, 07:42
    2. Replies: 4
      Last Post: 23rd November 2011, 13:32
    3. Replies: 1
      Last Post: 13th November 2011, 09:26
    4. Mchango wa vyombo vya habari na wanasiasa katika uvunjifu wa amani
      By luckman in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 3rd October 2011, 08:56
    5. Replies: 4
      Last Post: 2nd October 2011, 13:20

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...