JK: Vumilieni shida - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 21st July 2008, 03:21 PM   #1
JK: Vumilieni shida
Mambo Jambo Mambo Jambo is offline 21st July 2008, 03:21 PM

Chanzo: TANZANIA DAIMA, 21ST JULY, 2008

na Anna Makange, Tanga

Quote:
RAIS Jakaya Kikwete, amewataka Watanzania kuwa wavumilivu kutokana na hali ngumu ya maisha inayowakabili kwa sasa, inayosababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta duniani.

Rais Kikwete ametoa kauli hiyo katika kipindi ambacho Watanzania wengi, hasa wa kipato cha chini wamekuwa wakilia kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

Rais Kikwete alitoa kauli hiyo jana, wilayani Muheza, wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo, ikiwa ni siku ya tisa ya ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo, mkoani Tanga.

Rais Kikwete alisema kupanda kwa bei ya mafuta, kumechangia kwa kiasi kikubwa kulipuka kwa mfumuko wa bei za bidhaa mbalimbali duniani kote.

Alisema hali hiyo pia imechangia kuzorotesha kasi ya ukuaji wa uchumi hasa kwenye nchi zinazoendelea na hivyo watu wenye kipato duni kukabiliwa na hali ngumu ya maisha, hususan katika upatikanaji wa mahitaji muhimu, jambo ambalo aliongeza kuwa hata yeye limekuwa likimuumiza kichwa.

“Ndugu zangu Watanzania wenzangu…naelewa sana jinsi maisha yanavyozidi kuwa magumu siku hadi siku…na hali hii inasababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta hapa nchini, hivyo kila bidhaa kwa sasa gharama zake ni za juu sana, kuanzia vyakula hadi vitu vingine ambavyo ni muhimu kwa maisha ya kila siku. Linatuumiza sana hasa wale wananchi ambao ni maskini wa kipato,” alisema Rais Kikwete.

Hata hivyo alisema Watanzania wasikate tamaa kwa kuona kwamba maisha yataendelea kuwa hivyo, na kusisitiza kwamba yeye kama Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU) kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali duniani wanalishughulikia suala hilo.

Wakati Rais Kikwete akiwataka Watanzania kutokatishwa tamaa na hali hiyo, Chama cha NCCR- Mageuzi, jana kilisema wananchi hawana sababu ya kuilaumu Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra) kwa kupandisha bei ya nauli na badala yake lawama hizo zielekezwe kwa serikali ya Rais Kikwete.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Mkuu wa Idara ya Oganaizesheni, Kampeni na Uchaguzi, Faustine Sungura, alisema kutokana na matatizo hayo, kuna haja ya kuwepo kwa serikali mbadala, kwa madai kuwa serikali imeshindwa kutatua matatizo yanayowakabili wananchi, hasa ya upandaji wa gharama za bidhaa mbalimbali.

“Watanzania wanapaswa kujifunza kutokana na makosa, kwani muda waliowapa viongozi wa CCM kutawala unatosha na haujaonyesha mafanikio yoyote katika maisha zaidi ya kuzidisha ugumu wa maisha,” alisema.

“Watu wanakosea sana wanapoilaumu Sumatra badala ya kuilaumu serikali ambayo imeshindwa kudhibiti upandaji wa bei kwenye bidhaa mbalimbali yakiwemo mafuta,” alisema Sungura.

Alisema hata ziara anazofanya Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake, Ali Mohamed Shein ni dhihaka kwa Watanzania, kwani ahadi zao hazitekelezeki na wameshindwa kuwasaidia wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambao wanashinda Ikulu.

“Hivi hawa ni viongozi wa aina gani kama wameshindwa kuwasaidia wazee wa Jumuiya ya Afrika Mashariki wanaoshinda pale Ikulu, wataweza vipi kuwasaidia watu wa huko mikoani?” alihoji Sungura.

Katika hatua nyingine, Rais Kikwete amesema serikali itahakikisha inafanya kila jitihada za kutafuta wawekezaji wa ndani na nje ya nchi ili kuwekeza kwenye kiwanda cha usindikaji wa matunda wilayani Muheza, kwa lengo la kuwatafutia wakulima wa machungwa soko la uhakika.

Alisema lengo la kujenga kiwanda hicho licha ya kumtafutia soko mkulima, lakini pia itakuza kipato cha wakulima sambamba na kupunguza kiwango kikubwa cha machungwa yanayoharibika mashambani kwa kukosa wanunuzi hasa nyakati za msimu.

“Serikali inaamini kwa kufanya hivi tutakuwa tumemsaidia mkulima kwa kiasi kikubwa kuwa na soko la uhakika sambamba na kukuza kipato chake ambacho hivi sasa kinapotea kutokana na kiasi kikubwa cha matunda kuharibika…nawaahidi kwamba hili tutalitekeleza haraka iwezekanavyo,” alisisitiza Rais Kikwete.

Miongoni mwa ahadi alizotoa rais wilayani Muheza ni pamoja na kupeleka darubini katika zahanati ya Kijiji cha Kicheba, kuchangia sh milioni mbili katika ujenzi wa madarasa ya Shule ya Sekondari ya Mtindiro, sambamba na kutafuta magari ya wagonjwa katika wilaya zilizokosa huduma hiyo mkoani hapa.
HII SASA KALI, KAZI KWENU WADAU

 
Mambo Jambo's Avatar
Mambo Jambo
JF Senior Expert Member
Points: 274,369, Level: 100 Points: 274,369, Level: 100 Points: 274,369, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
Join Date: Fri Jul 2008
Posts: 846
Thanks: 32
Thanked 106 Times in 54 Posts
Views: 2765
Reply With Quote
  #2  
Old 21st July 2008, 03:33 PM
Rev. Kishoka's Avatar
Rev. Kishoka Rev. Kishoka is offline
Rev. Kishoka has no status.
JF Premium Member
Points: 1,760,733, Level: 100 Points: 1,760,733, Level: 100 Points: 1,760,733, Level: 100
Activity: 6% Activity: 6% Activity: 6%
 
Join Date: Mon Mar 2006
Location: USA
Posts: 3,481
Thanks: 1,019
Thanked 722 Times in 264 Posts
Rep Power: 132
Rev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to allRev. Kishoka is a name known to all
Default Re: JK: Vumilieni shida

Sawa Muungwana tumekusikia, umeshatuletea kisingizio cha Bei za mafuta. Kama sikosei ulitumia kisingizio hiki miezi kadhaa pamoja na kuyumba uchumi wa Marekani kutokana na uanguka kwa soko la nyumba na mikopo yake.

Sasa sijui Tanzania kushindwa kuzalisha mali kujitosheleza ambako ulisema ungekufanyia kazi kunaendelea kuchangiwa na sababu za nje au ukosefu wa mipango na miundombinu kutoka Serikali yako ili tusiumie sana.

Naona umehalalisha U-VDG kwa kusema kuwa kwa nafasi yako kama Mwenyekigoda wa AU, unalishughulikia hili suala!

Nitavumulia na kusubiri ahadi zako mpya Juni ya 2010!
__________________
Amani Iwe Nanyi,

Camerlengo

Plu Camerlenghi- Revolutionary Right Reverend Kishoka

"Any existence deprived of freedom is a kind of death." Gen. Michel Aoun

'Who comes to give greeting to the Inkosi-kaas? Who would taste her kiss, whereof the fruit is death? I, the Woodpecker, I, the Slaughterer, I the Swiftfooted! I, Umslopogaas!"
Reply With Quote
  #3  
Old 21st July 2008, 03:44 PM
Bubu Ataka Kusema's Avatar
Bubu Ataka Kusema Bubu Ataka Kusema is offline
Bubu Ataka Kusema says life is GOOD!
JF Premium Member
Points: 12,707,061, Level: 100 Points: 12,707,061, Level: 100 Points: 12,707,061, Level: 100
Activity: 50% Activity: 50% Activity: 50%
 
Join Date: Sun Feb 2007
Location: Mfaranyaki
Posts: 12,694
Thanks: 1,055
Thanked 1,211 Times in 704 Posts
Rep Power: 2049
Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!Bubu Ataka Kusema is one of most respected JF members!
Default Re: JK: Vumilieni shida

Wakati akiwataka Watanzania waendelee kuvumilia shida, Mafisadi wanaendelea na matanuzi yao na pesa za haramu. Yeye mwenyewe anaendelea na matanuzi ya safari zisizokwisha nchi za nje kila kukicha na msururu wa watu ambao wanaigharimu serikali gharama kubwa. Halafu tukisema nchi imemshinda wengine wanakasirika. Aaanze kujibana yeye kwa kufuta safari yake ya US mwezi ujao maana haina maslahi yoyote kwa nchi
__________________
~*~Life is Good~*~
Reply With Quote
  #4  
Old 21st July 2008, 03:51 PM
GM's Avatar
GM GM is offline
GM has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 149,791, Level: 100 Points: 149,791, Level: 100 Points: 149,791, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Mon Mar 2008
Posts: 548
Thanks: 7
Thanked 2 Times in 2 Posts
Rep Power: 24
GM will become famous soon enoughGM will become famous soon enoughGM will become famous soon enoughGM will become famous soon enoughGM will become famous soon enoughGM will become famous soon enoughGM will become famous soon enoughGM will become famous soon enough
Default Re: JK: Vumilieni shida

Huyu jamaa kwali kichekesho kwanza anakimbilia vijijini kwenda kuongea mbona akiwa Dar anajificha tu, kisha vitu vya muhimu kafumba macho na masikio hawezi kosa kitu cha kusingizia huyu.
__________________
"We are what we repeatedly do. Excellence, therefore is not an act but a habit" - Aristotle
Reply With Quote
  #5  
Old 21st July 2008, 03:52 PM
Mr. Zero Mr. Zero is offline
Mr. Zero has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 278,552, Level: 100 Points: 278,552, Level: 100 Points: 278,552, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Tue Jun 2007
Posts: 1,271
Thanks: 28
Thanked 70 Times in 51 Posts
Rep Power: 25
Mr. Zero will become famous soon enoughMr. Zero will become famous soon enoughMr. Zero will become famous soon enoughMr. Zero will become famous soon enoughMr. Zero will become famous soon enoughMr. Zero will become famous soon enoughMr. Zero will become famous soon enoughMr. Zero will become famous soon enough
Default Re: JK: Vumilieni shida

Hiki kisingizio wana JF tulishakijadili. Nilifikiri ataona aibu kukitumia kwa vile yeye mwenyewe hakai ofisini kila saa mguu na njia. Kama kweli anaona gharama za usafiri zimepanda kwa nini kila akitoka safari anaaza nyingine. I wonder kama anapitia document zote anazozi-sign. Actually JK anatakiwa awe muangalifu kuliko Mkapa kwa kuwa yeye hatakuwa na watu wa kumlinda. Kizazi cha enzi za uhuru cha CCM kulindana wengi wao hawatakuwepo 2015 hivyo kizazi kipya cha kina yakhe kilichozaliwa baada ya uhuru kitakuwa kinashika hatamu na kitamuhukumu peke yake.
__________________
"Money never made a man happy yet, nor will it. There is nothing in its nature to produce happiness. The more a man has, the more he wants. Instead of filling a vacuum, it makes one" by --Benjamin Franklin-- scientist, inventor, statesman, printer, philosopher, musician and economist
Reply With Quote
  #6  
Old 21st July 2008, 04:00 PM
Field Marshall ES Field Marshall ES is offline
Field Marshall ES has no status.
JF Premium Member
Points: 2,217,184, Level: 100 Points: 2,217,184, Level: 100 Points: 2,217,184, Level: 100
Activity: 43% Activity: 43% Activity: 43%
 
Join Date: Thu Apr 2006
Posts: 12,623
Thanks: 1,016
Thanked 1,700 Times in 784 Posts
Rep Power: 91
Field Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the rough
Default Re: JK: Vumilieni shida

Sio siri hii sababu ya mafuta na dunia tulimpa last week hapa JF, lakini isiwe sababu ya kujaribu kuficha uozo wa serikali yake kwa kisingizio cha bei ya mafuta na dunia,

kwa sababu it has nothing to do na ubovu wa uongozi wa serikali yake, ambacho ndicho hasa chanzo cha matatizo mengi ya maisha ya wananchi wa Tanzania kwa sasa.
Reply With Quote
  #7  
Old 21st July 2008, 04:18 PM
Kevo's Avatar
Kevo Kevo is offline
Kevo is stuff is tough
JF Senior Expert Member
Points: 238,924, Level: 100 Points: 238,924, Level: 100 Points: 238,924, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Thu Jun 2008
Location: Around the World
Posts: 1,301
Thanks: 0
Thanked 24 Times in 12 Posts
Rep Power: 24
Kevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enoughKevo will become famous soon enough
Default Re: JK: Vumilieni shida

Only God knows that we have a fool for a president.Tuvumilie shida while the few and selected are growing rich while majority die of hunger and poverty.My heart is bleeding with anger and hatred.
__________________
'I could have annihilated all the Jews in the World,but I left some of them so you will know why I was killing them'-Adolf Hitler;Mien Kampf
Reply With Quote
  #8  
Old 21st July 2008, 04:33 PM
Field Marshall ES Field Marshall ES is offline
Field Marshall ES has no status.
JF Premium Member
Points: 2,217,184, Level: 100 Points: 2,217,184, Level: 100 Points: 2,217,184, Level: 100
Activity: 43% Activity: 43% Activity: 43%
 
Join Date: Thu Apr 2006
Posts: 12,623
Thanks: 1,016
Thanked 1,700 Times in 784 Posts
Rep Power: 91
Field Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the rough
Default Re: JK: Vumilieni shida

HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, AKIFUNGUA RASMI BUNGE JIPYA LA JAMHURI YA
MUUNGANO WA TANZANIA, DODOMA, 30 DESEMBA 2005

Mheshimiwa Spika:

Serikali ya Awamu ya Nne ambayo nimepewa heshima ya kuiongoza, inaanza kazi wakati nchi ikiwa na hali nzuri kiuchumi, kisiasa na kijamii. Mafanikio hayo yametokana na uongozi imara na thabiti wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa. Napenda kutumia fursa hii kumpongeza kwa dhati kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanyia nchi yetu. Kwangu binafsi, amekuwa mwalimu na mwelekezi ambaye amenijengea uwezo na dhamira ya kuendeleza kazi aliyoianza. Namtakia afya njema na maisha marefu, yeye, Mama Mkapa, na familia yao.
Reply With Quote
  #9  
Old 21st July 2008, 04:35 PM
Masaki's Avatar
Masaki Masaki is online now
Masaki has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 199,266, Level: 100 Points: 199,266, Level: 100 Points: 199,266, Level: 100
Activity: 55% Activity: 55% Activity: 55%
 
Join Date: Tue Mar 2006
Location: Dar es Salaam
Posts: 1,634
Thanks: 961
Thanked 639 Times in 424 Posts
Rep Power: 28
Masaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enough
Default Re: JK: Vumilieni shida

Na kweli wananchi tuvumilie tu shida labda mpaka 2010 kama atatokea mkombozi mwingine, maana JK wakati anaingia tuliambiwa yeye ni mesiah yaani mkombozi wa dhiki na matatizo yote ya Watanzania. Lakini kwa kauli yake hii anamaanisha kukiri kushindwa kutupa nchi imimikayo maziwa na asali, yenye neema kwa kila mtanzania na maisha bora kwa kila mtanzania. Nakumbuka wakati JK amepitishwa na CCM kuwa mgombea wa kiti cha urais nilipita mtaa wa Mosque nikamsikia mlemavu mmoja omba omba akisema kwamba hatimaye shida zao zitakwisha sasa na wao walemavu wataishi maisha bora. Ukweli ni kwamba nilimsikitia na kumuonea huruma kwa kuwa nilijua kwamba hiyo ni ndoto ya mchana.

Ukiacha huyo ambaye "obviously ni illiterate" nilishangazwa sana siku moja nimekwenda kuwatembelea ndugu zangu fulani huko Kiwalana ambao walibahatika kuliona darasa. Wakati tunakunywa bia wakapigiwa simu kutoka US, wakawa wanamwambia yule ndugu yao kwamba wao hapa Bongo mambo yatakuwa tamabarare muda si mrefu kwa kuwa JK anaingia madarakani.

Si ajabu kuona kwamba muungwana alishinda kwa 80% ya kura zote zilizopigwa. Mimi binafsi kwa mara ya kwanza alipa matumaini makubwa sana ya Tanzania yenye neema na yenye maisha bora kwa kila Mtanzania pale alipotoa hotuba yake ya kwanza bungeni. Laiti kama leo hii tungepata nakala ya hotuba ile tuanza ku "tick" kitu kimoja kimoja tutagundua kwamba hata 20% ya aliyoyaongea hajayafanya bado. May be he was he too ambitious?

Ninachojiuliza kwa sasa ni je nafsi yake inamsuta huko aliko kwa kushindwa kuwatimizia ndoto Watanzania hawa masikini? Au ilikuwa lengo ni kufika Ikulu tu kisha mliobaki mtajijua?
Reply With Quote
  #10  
Old 21st July 2008, 04:38 PM
Masaki's Avatar
Masaki Masaki is online now
Masaki has no status.
JF Senior Expert Member
Points: 199,266, Level: 100 Points: 199,266, Level: 100 Points: 199,266, Level: 100
Activity: 55% Activity: 55% Activity: 55%
 
Join Date: Tue Mar 2006
Location: Dar es Salaam
Posts: 1,634
Thanks: 961
Thanked 639 Times in 424 Posts
Rep Power: 28
Masaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enoughMasaki will become famous soon enough
Default Re: JK: Vumilieni shida

Quote:
View Post
HOTUBA YA RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, MHESHIMIWA JAKAYA MRISHO KIKWETE, AKIFUNGUA RASMI BUNGE JIPYA LA JAMHURI YA
MUUNGANO WA TANZANIA, DODOMA, 30 DESEMBA 2005

Mheshimiwa Spika:

Serikali ya Awamu ya Nne ambayo nimepewa heshima ya kuiongoza, inaanza kazi wakati nchi ikiwa na hali nzuri kiuchumi, kisiasa na kijamii. Mafanikio hayo yametokana na uongozi imara na thabiti wa Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya Tatu, Mheshimiwa Benjamin William Mkapa. Napenda kutumia fursa hii kumpongeza kwa dhati kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanyia nchi yetu. Kwangu binafsi, amekuwa mwalimu na mwelekezi ambaye amenijengea uwezo na dhamira ya kuendeleza kazi aliyoianza. Namtakia afya njema na maisha marefu, yeye, Mama Mkapa, na familia yao.
Mzee hebu irushe link ya hii hotuba tafadhali.
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
jk, shida, vumilieni


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Walimu wanapata shida sana!! MpigaKura Jokes/Utani + Udaku/Gossips 4 6th January 2010 05:04 PM
Tanzania kuwa na shida ya umeme ni mitihani ya Mungu-JK tibwilitibwili Jukwaa la Siasa 66 19th October 2009 09:03 AM
Harakati Sasa Basi - Narudi Kubeba Maboksi! Companero Jukwaa la Siasa 96 13th October 2009 05:57 PM
Umeme na Maji ni shida Dar: Kulikoni? Lunyungu Habari na Hoja mchanganyiko 13 17th February 2007 08:52 PM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 02:01 PM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com