Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

    Report Post
    Page 2 of 4 FirstFirst 1234 LastLast
    Results 21 to 40 of 77
    1. #1
      MwanaHaki's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th October 2006
      Posts : 1,415
      Rep Power : 1008
      Likes Received
      156
      Likes Given
      91

      Default TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi



      TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

      Isambazwe Mara Moja

      Alhamis, Julai 21, 2011


      KUITISHWA KWA MAANDAMANO YA AMANI NA MKUTANO WA WAZI
      Mahali: Uwanja wa Mwembeyanga, Temeke, Dar es Salaam
      Tarehe: 1 Agosti 2011


      Nikiwa kama Mtanzania, mpenda amani, raia wa KUZALIWA, Mzalendo Halisi mwenye kuipenda nchi yake, na kiongozi wa asasi-huru ya X Foundation yenye makazi yake Jijini Dar es Salaam, napenda kutoa taarifa kwamba, X Foundation inawaalika Watanzania wote waishio Dar es Salaam na kwingineko, kwamba, kutakuwa na Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi, siku ya Jumatatu, Agosti Mosi, 2011, kuanzia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Temeke hadi Uwanja wa Mwembeyanga, Temeke, Dar es Salaam. Watanzania mnaombwa kukusanyika KWA AMANI, kwenye eneo la wazi, nje ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Dar es Salaam, kuanzia saa 2 asubuhi. Maandamano yataanza rasmi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Temeke, takriban saa 4 kamili hadi Uwanja wa Mwembeyanga, Temeke, na yanatarajiwa kupokelewa na Mhe. Beatrice Matumbo Shellukindo (MB, Kilindi, CCM), akishirikiana na viongozi wa vyama mbali mbali vya kisiasa na kijamii, ambao watakuwa wamealikwa kuhudhuria.

      Dhumuni la Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi, tukio ambalo litafanyika kwa amani, linachagizwa na Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, toleo la mwaka 1977, kama ifuatavyo:


      1. Msingi na Mustakabali: Serikali na Watu, Sheria ya 1984, Na. 15, ib. 6, kama ifuatavyo:

      8.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
      (a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
      (b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
      (c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
      (d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.



      1. Uhuru wa Mawazo: Uhuru wa Maoni, Sheria ya 1984, Na. 15, ib. 6, kama ifuatavyo:

      18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati.


      1. Uhuru wa Kushirikiana na Wengine: Sheria ya 1984, Na. 15, ib. 6, kama ifuatavyo:

      20.-(1) Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.

      1. Kila raia anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomhusu yeye, maisha yake au yanayolihusu Taifa.



      1. Ulinzi wa Mali ya Umma: Sheria ya 1984, Na. 15, ib. 6, kama ifuatavyo:

      27.-(1) Kila mtu ana wajibu wa kulinda mali asilia ya Jamhuri ya Muungano, mali ya Mamlaka ya Nchi na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na pia kuiheshimu mali ya mtu mwingine.

      1. Watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali ya mamlaka ya nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za uharibifu na ubadhilifu, na kuendesha uchumi wa taifa kwa makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye ya taifa lao.


      Kutokana na mustakabali huu, mimi, nikiwa Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ninao uhuru, haki na wajibu wa kuzingatia masharti haya yaliyotajwa hapa juu, kama ifuatavyo:


      1. Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania imekuwa katika hali ya jumla ya kuyumba kwa uchumi wake, kuanzia mnamo mwaka 1994, wakati janga la nakisi ya nishati ya umeme lilipoikumba Jamhuri kwa mara ya kwanza, na kusababisha athari mbaya za kiuchumi
      2. Wizara ya Nishati na Madini ndiyo taasisi kuu ya Serikali ya Tanzania, ambayo, kwa mujibu wa Ibara ya 8-(1) ya Katiba, ibara ndogo ya (b), inatamkwa kwamba “wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa wananchi kwa mujibu wa Katiba hii”, kwa hiyo, Wananchi ndio wenye mamlaka ya mwisho ya kuamua mustakabali wa utendaji wa viongozi wa Wizara hiyo, ambayo ni taasisi yao, wao wakiwa wenye kutoa “madaraka na mamlaka” kwa Serikali.

      Kwa msingi huo mkuu, pamoja na misingi mingine iliyotajwa hapo juu, ninao uhuru, haki na wajibu wa kuitisha Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi, kwa lengo la kuwashinikiza viongozi watendaji wakuu wa Wizara ya Nishati na Madini, yaani, Waziri, Naibu Waziri na Katibu Mkuu, kujiuzulu mara moja, ili kuwezesha utendaji wa Wizara hiyo kutendeka kwa ufanisi zaidi, kwani imeonekana dhahiri kwamba, katika kipindi cha uongozi wao wa Wizara hiyo, kipindi cha kwanza kikiwa cha 2005-2010, na cha pili kikiwa 2010-2015, hali ya ugavi wa nishati ya umeme imezidi kuwa mbaya kiasi cha sio tu kuathiri uchumi wa nchi, lakini pia, kuathiri vibaya zaidi maisha na mustakabali wa Watanzania kwa ujumla.

      Kutokana na usimamiaji mbovu wa utendaji wa Wizara, pamoja na mipango mizuri iliyowekwa hapo awali, na pia, kutosikiliza maoni ya Wabunge, hususan maoni ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya inayohusika na sekta ya nishati, viongozi hawa walioteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Jakaya Mrisho Kikwete, wamepuuza kabisa ushauri wa wataalam na wabunge, na katika utendaji wao mbovu, wameitia hasara kubwa Jamhuri hii, hivyo kusababisha upotevu wa mabilioni ya Shilingi, sio tu kutokana na Serikali kukosa kukusanya mapato kutokana na shughuli mbali mbali za uzalishaji kutoka kwenye viwanda, vingi ambavyo sasa vimefungwa, lakini pia, Serikali kukosa kukusanya mapato kutoka kwa wajasiriamali wadogo na wakati, hivyo kushindwa kujiendesha kwa ufanisi mzuri zaidi.

      Kwa kuzingatia Masharti yaliyowekwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ibara ya 27-(1) na (2), ninao uhuru, haki na wajibu wa kulinda mali ya umma, ikiwa ni pamoja na uchumi wa Jamhuri, lakini pia, kwa kuzingatia Ibara ya 18-(1) na 20-(1) na (2), ninao uhuru, haki na wajibu wa kutoa maoni yangu, na pia kushirikiana na watu wengine katika kutoa maoni hayo, ikiwa ni pamoja na kwenye hadhara, kupitia, kwa mfano, maandamano ya amani na mikusanyiko ya wazi, nikiwa na uhuru wa kutoingiliwa kati kwenye mawasiliano hayo ya amani.

      Leo, Alhamis, Julai 21, 2011, ninatamka, kwa faida ya Watanzania wote, kwamba, ifikapo tarehe 1 Agosti 2011, sisi Watanzania, tutakusanyika kwa amani na tutaandamana kwa amani, kama ilivyotajwa hapo juu, na tutafanya mkutano wa wazi na wa amani, ili kuweka bayana maoni na hisia zetu kuhusu janga hili kuu lililoifika nchi yetu.

      Tuhuma zinazowakabili watendaji hawa, wa kutaka kutoa hongo ya takriban Shilingi Bilioni Moja za Kitanzania, zitazungumziwa kwa undani na watu wenye taarifa kamili zaidi kwenye mkutano huo utakaofanyika Mwembeyanga, Temeke. Tunatoa maombi ya ushirikiano mwema kwa Watanzania wote katika maandalizi ya maandamano hayo na mkutano huo, ili kuleta ufanisi mzuri zaidi, kwani, penye umoja kuna nguvu, na penye wengi hapakosi mazuri.

      Watu wote wenye nia nzuri na nchi yetu wanaombwa kuwasiliana nami kwa njia ya simu na/au barua pepe kama inavyoainishwa hapa chini. Mimi ni mhamasishaji, ninao uhuru, haki na wajibu huo, lakini mustakabali wa nchi yetu ni wetu wote, bila kujali itikadi zetu za kisiasa, au imani zetu za kidini, au rangi za ngozi zetu au makabila yetu, kwani, Tanzania ni moja, ni yetu wote, kila mtu anayeitwa Mtazania ana haki ya kuitetea na kuilinda nchi yake, akishirikiana na wenzake.

      Asanteni kwa Ushirikiano wenu.


      MwanaHaki

      Simu selula: +255-786-019019 na +255-786-019019

      Barua pepe: misterx@qi.co.tz
      Speaking Openly, without fear!


    2. #21
      Livanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th April 2010
      Location : Around the World
      Posts : 287
      Rep Power : 523
      Likes Received
      38
      Likes Given
      33

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Napitatu sitasema chochote kwa sasa
      Quote By EasyFit View Post
      We faza fox mbona madhumuni na malengo yamewekwa wazi
      GOD BLESS TANZANIA

    3. #22
      FUSO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th November 2010
      Posts : 3,047
      Rep Power : 1057
      Likes Received
      803
      Likes Given
      341

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      imeshapata kibali toka inteligensia ya nchi? maana hii ndiyo section ambayo jamaa wana peform excellent. Ili kama sivyo basi tujiandae kuja na chupa za maji ya uhai.

    4. #23
      Maishamapya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Location : Dar, Tanzania
      Posts : 915
      Rep Power : 620
      Likes Received
      218
      Likes Given
      267

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Nionavyo mimi ni kwamba hakuna maandamano hapo.
      • 1 Agosti 2011 ni siku ya kazi - Jumatatu: Ngunguri hawataruhusu
      • X Foundation - Simply means No foundation and actually NO Tanzania since it crosses the national flaf - Sina hakika kama serikali inaweza kutoa usajili kwa shirika kama hili linaloifuta Tanzania.
      • Malengo - Nukuu za katiba tupu: Je haya ni maandamano ya kuhamasisha watu kuijua katiba yao
      • Mgeni Rasmi - Beatrice Shellukindo: Atakuwa Bungeni. Hapa amewekwa ili kuongezewa ujiko tu.
      Hoja Pekee ya kufanyaMaandamano yawepo (haipo wazi kwenye malengo)
      • Urais 2015: Mama huyu (Bi Shellukindo) si ndo anayempigia kampeni EL kwa ajili ya urais 2015? Si mbio za urais zimeanza? Inawezekana maana wale mapacha wa CCJ nao wanazunguka - Hii ndo hoja pekee inayoweza kufanya maandamano yakafanyika. URAIS wa EL 2015
      Last edited by Maishamapya; 21st July 2011 at 15:34. Reason: clarity on X as No Foundation
      "Even a fool is thought wise if he keeps silent, and discerning if he holds his tongue" (Prov 17:28 NIV)

    5. #24
      kisoti's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th August 2009
      Posts : 74
      Rep Power : 514
      Likes Received
      3
      Likes Given
      3

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Nimependa jinsi ambavyo watu wanavyojaribu kutafakari mambo kwa kina badala ya kukubali kirahisi rahisi. Hata hivyo nionanyo mimi ni kwamba issue ya tatizo la umeme ni la kitaifa na lina cut accross all political boundaries. Tuweke kwanza utaifa wetu mbele na si siasa na itikadi za vyama. Tusipoweka utaifa mbele kamwe nchi hii haitaweza kuendelea. Binafsi sioni sababu ya mtu kukataa kwenda kwenye maandamano eti kwa sababu hayo maandamano yanasadikika kuandaliwa na chama fulani hata kama yana maslahi ya nchi. Hii haina tofauti na wabunge kupinga hoja hata kama ni ya msingi na yenye maslahi kwa nchi eti kwa sababu inatoka kwa mbunge wa chama kingine. Kwa mwenendo huu tutafika kweli?Tunatumikia vyama zaidi kuliko nchi na watanzania kwa ujumla. Ni vyema zaidi tukaungana kwenye mambo ya msingi na yenye maslahi kwa nchi na kutofautiana kwenye mambo yasiyo na maslahi kwa nchi. Tatizo kubwa linaloingamiza nchi yetu ni KUKOSA UTAIFA.

    6. #25
      hans79's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2011
      Posts : 1,667
      Rep Power : 804
      Likes Received
      163
      Likes Given
      0

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Mhe. Beatrice Matumbo Shellukindo (MB, Kilindi, CCM), kishirikiana na viongozi wa vyama mbali mbali vya kisiasa na kijamii, ambao watakuwa wamealikwa kuhudhuria.


    7. #26
      hans79's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2011
      Posts : 1,667
      Rep Power : 804
      Likes Received
      163
      Likes Given
      0

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi


    8. #27
      hans79's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2011
      Posts : 1,667
      Rep Power : 804
      Likes Received
      163
      Likes Given
      0

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      ffoxy muulize huyu

    9. #28
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 16,045
      Rep Power : 14670
      Likes Received
      2954
      Likes Given
      2093

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Mpasuko ndani ya CCM ni kitu kinachojulina siku nyingi. Yanayoendelea sasa hivi ni "ukimwaga kitoweo, namwaga ugali".

      Hii ndio nguvu ya RA na EL na wenzao.

      Ngoja nitafute bisi nikae mkao wa kutazama bonge la senema.

    10. #29
      The Emils's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th April 2011
      Location : Unga LTD
      Posts : 562
      Rep Power : 530
      Likes Received
      122
      Likes Given
      71

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Quote By FaizaFoxy View Post
      Mantiki na uwepo wa hayo maandamano ni nini? nimelisoma tamko lakini sijaona ni maandamano hayo ni ya nini? kupinga hayo kwenye katiba? kutaka yabadilishwe? au? nisaidieni
      Kitu gani ueleweshwe? Au kisa ngeleja anatakiwa kujiuzulu?
      "A man who won't die for something is not fit to live"

    11. #30
      zomba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th November 2007
      Posts : 16,045
      Rep Power : 14670
      Likes Received
      2954
      Likes Given
      2093

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Mpasuko ndani ya CCM ni kitu kinachojulina siku nyingi. Yanayoendelea sasa hivi ni "ukimwaga kitoweo, namwaga ugali".

      Hii ndio nguvu ya RA na EL na wenzao.

      Ngoja nitafute bisi nikae mkao wa kutazama bonge la senema.

    12. #31
      SEAL Team 6's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th June 2011
      Posts : 656
      Rep Power : 537
      Likes Received
      115
      Likes Given
      155

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Quote By FaizaFoxy View Post
      Mantiki na uwepo wa hayo maandamano ni nini? nimelisoma tamko lakini sijaona ni maandamano hayo ni ya nini? kupinga hayo kwenye katiba? kutaka yabadilishwe? au? nisaidieni kuelewa.
      Maandamano ya kueleza ujinga wa CCM unakaribishwa usikose, njoo na chai na vitafunwa vyako, hapatakuwa na Bahasha za JAIRO.

    13. #32
      Junior. Cux's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd February 2011
      Posts : 832
      Rep Power : 590
      Likes Received
      153
      Likes Given
      24

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      nadhani hakuna tatizo na shelukindo kupokea hayo maandamano, tunachokitaka ni hao viongozi watatu wa wizara kuachia ngazi ata kama jk ndo apokee maandamano bora tu watuachie wizara yetu..

    14. #33
      Mpui Lyazumbi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st September 2010
      Location : Matemanga to Tunduru
      Posts : 1,373
      Rep Power : 724
      Likes Received
      162
      Likes Given
      67

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Nimesoma tu
      "A Country which lacks its own culture is no more than a collection of people without the spirit which makes them a nation".(Freedom & Unit-JKN)

    15. #34
      Arafat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th November 2009
      Posts : 2,372
      Rep Power : 966
      Likes Received
      583
      Likes Given
      576

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Lowasa?
      Siku tutakapoacha kuwa mashabiki wa wanasiasa ndio siku hatua ya kwanza ya kujikomboa itakapo anza

    16. #35
      Laurence's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th June 2011
      Location : ULIMWENGUNI
      Posts : 2,116
      Rep Power : 1413
      Likes Received
      197
      Likes Given
      46

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Nimerudi tena, baada ya kupita asubuhi,mimi nasema hivi siji huko ng'o then ati mpokea maandamano wana Magamba tena Shellukindo alojitoa kwenye lililokua kundi la wapigania ufisadi na kujiunga na mtandao wa Lowassa? Umepotea mama janja yako tumeijua hyo X kama jina mlotumia ni geresha tuuu wapo wana Magamba wengi nyuma yenu.

    17. #36
      Laurence's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th June 2011
      Location : ULIMWENGUNI
      Posts : 2,116
      Rep Power : 1413
      Likes Received
      197
      Likes Given
      46

      Default

      Quote By Maishamapya View Post
      Nionavyo mimi ni kwamba hakuna maandamano hapo.
      • 1 Agosti 2011 ni siku ya kazi - Jumatatu: Ngunguri hawataruhusu
      • X Foundation - Simply means No foundation - Sina hakika kama serikali inaweza kutoa usajili kwa shirika kama hili.
      • Malengo - Nukuu za katiba tupu: Je haya ni maandamano ya kuhamasisha watu kuijua katiba yao
      • Mgeni Rasmi - Beatrice Shellukindo: Atakuwa Bungeni. Hapa amewekwa ili kuongezewa ujiko tu.
      Hoja Pekee ya kufanyaMaandamano yawepo (haipo wazi kwenye malengo)
      • Urais 2015: Mama huyu (Bi Shellukindo) si ndo anayempigia kampeni EL kwa ajili ya urais 2015? Si mbio za urais zimeanza? Inawezekana maana wale mapacha wa CCJ nao wanazunguka - Hii ndo hoja pekee inayoweza kufanya maandamano yakafanyika. URAIS wa EL 2015
      Mkuu hili nimeliona mapema kabisa wanataka kupima upepo wa watu hapo huyu mama Shellukindo haaminiki kabisa na mpango wake mzima ni kutaka kumcaimpenia Manywele

    18. #37
      JACADUOGO2.'s Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th December 2010
      Posts : 782
      Rep Power : 588
      Likes Received
      184
      Likes Given
      0

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Hayo maandamano ya chama cha magamba nani aje? Utaandamana mwenyewe!

    19. #38
      Magarinza's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 9th May 2008
      Posts : 114
      Rep Power : 589
      Likes Received
      12
      Likes Given
      12

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Huu ni ----- na upumbavu mwingine tena wa kupotezea watu muda na siasa uchwara.

    20. #39
      Triple DDD's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 151
      Rep Power : 4176
      Likes Received
      16
      Likes Given
      3

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Kazi ipoe kweli kweli

    21. #40
      Triple DDD's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 19th January 2011
      Posts : 151
      Rep Power : 4176
      Likes Received
      16
      Likes Given
      3

      Default Re: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI - Maandamano ya Amani na Mkutano wa Wazi

      Haya bwana yetu macho.

    Page 2 of 4 FirstFirst 1234 LastLast

    Similar Topics

    1. SIKIKA: Taarifa kwa vyombo vya habari
      By n00b in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 7
      Last Post: 29th November 2011, 15:12
    2. TAARIFA (attached) KWA VYOMBO VYA HABARI
      By USTAADHI in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 17
      Last Post: 17th November 2011, 08:47
    3. TANESCO: Taarifa kwa Vyombo vya Habari
      By EMT in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 43
      Last Post: 17th August 2011, 21:15
    4. Kutoka TANESCO: Taarifa kwa vyombo vya habari
      By Maxence Melo in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 23
      Last Post: 3rd June 2010, 09:34
    5. Taarifa kwa Vyombo vya Habari - 09/01/2007
      By Mzee Mwanakijiji in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 0
      Last Post: 9th January 2007, 08:56

    User Tag List

    Tags for this Topic

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...