Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Serikali kuu moja, mbili, au tatu?

    Report Post
    Results 1 to 5 of 5
    1. #1
      George Kahangwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2007
      Location : Dar es Salaam, Tanzania
      Posts : 483
      Rep Power : 688
      Likes Received
      103
      Likes Given
      38

      Default Serikali kuu moja, mbili, au tatu?

      Mara nyingi nimekuwa nikiwaza kuhusu ni nini watanzania watachokiamua watakapopitisha katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hususan suala la muundo wa serikali.

      Nimetamani sana uwepo mdahalo uhusuo jambo hili, ili hoja zijengwe na kusikika kuhusu tuwe na serikali kuu ya namna gani. Tuendelee na mfumo wa sasa (serikali mbili)?, Tanganyika ifufuke (serikali tatu), au Serikali kuu moja? Natumia maneo serikali kuu maana natambua zipo serikali za mitaa (halmashauri za wilaya na vijiji/mitaa/sheia)

      Kama ningeulizwa iwapo muundo wa serikali kuu moja wawezafaa, nisingekurupukia kusema ndio bila kutaja yafuatayo;
      • Tanzania ni dola moja, linahitaji serikali kuu moja, na bunge moja la JMT.
      • Watanzania (mf. kwa mujibu wa wimbo wa taifa, na nembo ya Taifa) tunaamini katika uhuru na umoja.
      • Serikali kuu moja ni umbo jembamba la vyombo vya utendaji, licha ya kuleta unafuu wa gharama za uendeshaji, itaruhusu zaidi nguvu za kiutawala zipelekwe ngazi za chini kwa wananchi kuliko kuwa na kuwa na vyombo vikubwa ngazi za juu.
      • Ipo hatari ya mparaganyiko endapo kutaendelea kuwepo muundo wa serikali zaidi ya moja, harafu itokee serikali hizo tofauti zikaundwa na vyama vya siasa tofauti.
      • Yamkini serikali moja yaweza kuwa sehemu ya suluhu ya kero za muungano.
      • Kimahesabu serikali mbili ni yaleyale, serikali tatu ni hatua moja kurudi nyuma, serikali moja (yaweza kuwa) ni hatua moja kwenda mbele.
      WanaJF mnasemaje?

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      Avatar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2011
      Posts : 555
      Rep Power : 538
      Likes Received
      53
      Likes Given
      12

      Default Re: Serikali kuu moja, mbili, au tatu?

      Naamini Tanzania itakua na umoja zaidi endapo kama tutakua na serikali moja (serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania), na sio kuwa na serikali mbili kama ilivyosasa au kuwa na serikali tatu kama wanavyopendelea baadhi ya wazalendo wa nchi hii.
      - Haiingii akilini kwa nchi moja kuwa na serikali zaidi ya moja.
      - Tutapunguza chokonozi zinazoichokonoa serikali kupitia sababu zinazoitwa kero za muungano.
      - Itatusaidia kusahau kama kulikua na nchi inaitwa zanzibar, kama tanganyika inavyosahaulika na hili litaongeza mshikamano Tanzania.
      - Tutapunguza gharama nyingi zinazotumika kuwalipa wawakilishi katika bunge la zanzibar, raisi wa zanzibar pamoja na serikali yake yote, Zanzibar kubakie na wakuu wa mikoa, wilaya, madiwani na wabunge watakao wawakilisha wananchi wao katika bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania - Dodoma.

    4. #3
      GHIBUU's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th January 2011
      Location : UK
      Posts : 738
      Rep Power : 574
      Likes Received
      85
      Likes Given
      585

      Default Re: Serikali kuu moja, mbili, au tatu?

      Quote By Kahangwa
      Mara nyingi nimekuwa nikiwaza kuhusu ni nini watanzania watachokiamua watakapopitisha katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hususan suala la muundo wa serikali.

      Nimetamani sana uwepo mdahalo uhusuo jambo hili, ili hoja zijengwe na kusikika kuhusu tuwe na serikali kuu ya namna gani. Tuendelee na mfumo wa sasa (serikali mbili)?, Tanganyika ifufuke (serikali tatu), au Serikali kuu moja? Natumia maneo serikali kuu maana natambua zipo serikali za mitaa (halmashauri za wilaya na vijiji/mitaa/sheia)

      Kama ningeulizwa iwapo muundo wa serikali kuu moja wawezafaa, nisingekurupukia kusema ndio bila kutaja yafuatayo;
      • Tanzania ni dola moja, linahitaji serikali kuu moja, na bunge moja la JMT.
      • Watanzania (mf. kwa mujibu wa wimbo wa taifa, na nembo ya Taifa) tunaamini katika uhuru na umoja.
      • Serikali kuu moja ni umbo jembamba la vyombo vya utendaji, licha ya kuleta unafuu wa gharama za uendeshaji, itaruhusu zaidi nguvu za kiutawala zipelekwe ngazi za chini kwa wananchi kuliko kuwa na kuwa na vyombo vikubwa ngazi za juu.
      • Ipo hatari ya mparaganyiko endapo kutaendelea kuwepo muundo wa serikali zaidi ya moja, harafu itokee serikali hizo tofauti zikaundwa na vyama vya siasa tofauti.
      • Yamkini serikali moja yaweza kuwa sehemu ya suluhu ya kero za muungano.
      • Kimahesabu serikali mbili ni yaleyale, serikali tatu ni hatua moja kurudi nyuma, serikali moja (yaweza kuwa) ni hatua moja kwenda mbele.

      WanaJF mnasemaje?
      Hebu soma tena,,,serikali ya jamuhuri ya muungano wa tanzania,,,it means ni serikali ya shirikisho wa nchi,zaidi ya moja,iwe mbili au tatu ndio ikaitwa muungano,sasa sisi tuna serikali mbili ambazo zilijipatia uhuru mwaka 1961 ambayo tanganyika na zanzbar 1964,na ndipo zikaungana,baada ya muungano ilikuwa tunaita hivi Jamuhuri ya muungano wa tanganyika na zanzibar.

      Baada ya hapo ilitumika technic ya kuimeza zanzbar ndani ya muungano na kuiyuwa tanganyika na kuita tanzania tukapakiwa na serikali ya muungano ambayo ni tanganyika kuita tanzania na ikabakia zanzbar, Ni sawa zaire kiuta congo, tanganyika/tanzania.

      sasa watanganyika ikiwa nyinyi munataka kuwa serikali moja hilo haliwezikani kwa upande wa zanzibar,kwani sisi ni taifa kamili tuna serikali yetu,na kila kitu chetu,haya ni maamuzi yetu,na hatuko tayari kuuza utaifa wetu kwa kujimbambika jina la ubatizo la tanganyika ambalo ni tanzania,sisi ni wazanzbari sasa inafika miaka 500 zanzibar ipo.

      Sasa ikiwa wewe umependezewa na jina la tanzania jite mtanzania,lakini sisi wazanzbari tunafahamu kuwa tanzania ni ile tanganyika kilichobadilika ni jina tu,kwanza muungano hatuna,kwani mshiki wa muungano amekufa,ni sawa na ndoa mke kufa kubakia mume,hakuna ndoa tena.

      Pia katika makubaliano ya muungano,rais wa zanzbar ndio anatakiwa awe makamo wa rais wa muungano kwa sababu yeye amechaguliwa na wanachi wa zanzibar kwa hiyo naweza kuwakilisha wazanzbari katika muungano,sasa jiulize Doctor Bilal amechaguliwa kichama ndio kawa makamo wa rais wa muungano vipi anaiwakilisha zanzibar ? Wakati hakuchaguliwa na wanachi ?

      Kwa kweli vile vizingiti vya muungano ambavyo vilivyofanya muungano uwepo havipo na muungano umekufa,sasa muungano hakuna,uliokuwepo ni muungano wa chama tu,ASP na TANU ambayo ni ccm.

      hii symbol ukiangalia ni ile ile ambayo ikitumika kwa serikali ya tanganyika leo tunaambiwa tanzania,sasa jiulize tanganyika sio hii tanzania ? Nembo hii ndio ilikuwa ikitumika kwa tanganyika sasa inatumika kama ni ya tanzania,ni sawa zaire kuita congo,utapeli tu,nani alosema tanganyika haipo ? Ipo tanganyika,rasilimali kama migodi,almasi,mafuta na gasi,sio ya muungano sasa jiulizeni yanasimamiwa na serikali ipi ? Na pesa hizo za umma zinakwenda wapi au wanagawana viongozi ? Amkeni nyinyi.

      hii nembo sasa imekuwa ya tanzania,jiulize huu sio usanii ?
      na hii ndio ilivyokuwa baada tu ya muungano tukitambulika kimataifa angalia hiyo ramani ...Balozi zetu zilikuwa zikiandikwa jamhuri ya muungano wa tanganyika na zanzibar.

      Sisi wazanzibar tunasema tena hatutaki hatutaki muungano,kwa sababu hauna jema kwetu,hauna fadhila,unatudhulumu sisi,na nyinyi watanganyika kama munaona ni mzigo kwenu basi bora iwe end.

    5. #4
      Ngekewa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th July 2008
      Posts : 4,488
      Rep Power : 1452
      Likes Received
      388
      Likes Given
      181

      Default Re: Serikali kuu moja, mbili, au tatu?

      Quote By Kahangwa
      Mara nyingi nimekuwa nikiwaza kuhusu ni nini watanzania watachokiamua watakapopitisha katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hususan suala la muundo wa serikali.

      Nimetamani sana uwepo mdahalo uhusuo jambo hili, ili hoja zijengwe na kusikika kuhusu tuwe na serikali kuu ya namna gani. Tuendelee na mfumo wa sasa (serikali mbili)?, Tanganyika ifufuke (serikali tatu), au Serikali kuu moja? Natumia maneo serikali kuu maana natambua zipo serikali za mitaa (halmashauri za wilaya na vijiji/mitaa/sheia)

      Kama ningeulizwa iwapo muundo wa serikali kuu moja wawezafaa, nisingekurupukia kusema ndio bila kutaja yafuatayo;
      • Tanzania ni dola moja, linahitaji serikali kuu moja, na bunge moja la JMT.
      • Watanzania (mf. kwa mujibu wa wimbo wa taifa, na nembo ya Taifa) tunaamini katika uhuru na umoja.
      • Serikali kuu moja ni umbo jembamba la vyombo vya utendaji, licha ya kuleta unafuu wa gharama za uendeshaji, itaruhusu zaidi nguvu za kiutawala zipelekwe ngazi za chini kwa wananchi kuliko kuwa na kuwa na vyombo vikubwa ngazi za juu.
      • Ipo hatari ya mparaganyiko endapo kutaendelea kuwepo muundo wa serikali zaidi ya moja, harafu itokee serikali hizo tofauti zikaundwa na vyama vya siasa tofauti.
      • Yamkini serikali moja yaweza kuwa sehemu ya suluhu ya kero za muungano.
      • Kimahesabu serikali mbili ni yaleyale, serikali tatu ni hatua moja kurudi nyuma, serikali moja (yaweza kuwa) ni hatua moja kwenda mbele.
      WanaJF mnasemaje?
      Ndugu yangu sijui hii mada yako inaeleza nini? Kwani Tanzania ina Serikali mbili zaidi ya ile ya Kikwete? Au unafikiri Zanzibar ni Tanzania ya pili? Kuna Tanzania na kuna Zanzibar na kila sehemu ina Serikali moja tu.

    6. #5
      George Kahangwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th October 2007
      Location : Dar es Salaam, Tanzania
      Posts : 483
      Rep Power : 688
      Likes Received
      103
      Likes Given
      38

      Default Re: Serikali kuu moja, mbili, au tatu?

      Quote By Ngekewa
      Ndugu yangu sijui hii mada yako inaeleza nini? Kwani Tanzania ina Serikali mbili zaidi ya ile ya Kikwete? Au unafikiri Zanzibar ni Tanzania ya pili? Kuna Tanzania na kuna Zanzibar na kila sehemu ina Serikali moja tu.
      Nataraji kuona misimamo ya hivi ikiibuka wazi wakati wa kutafuta maoni ya kuandikwa kwa katiba mpya

    7. Miaka 50

    Similar Topics

    1. Replies: 0
      Last Post: 4th December 2011, 10:28
    2. Moja, Mbili, Tatu, Nne.....
      By Digna37 in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 21
      Last Post: 10th March 2011, 16:51
    3. Replies: 14
      Last Post: 8th February 2011, 11:10

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...