Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011 - Bajeti Mbadala

    Report Post
    Page 1 of 6 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 104
    1. #1
      Maxence Melo's Avatar
      JF Founder Array
      Join Date : 20th March 2006
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 3,043
      Rep Power : 100000
      Likes Received
      1343
      Likes Given
      1432

      Default Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011 - Bajeti Mbadala

      HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI WIZARA YA FEDHA MHE.KABWE ZUBERI ZITTO (MB) KUHUSU MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2011/2012

      UTANGULIZI

      Mheshimiwa Spika, Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuweza kusimama hapa mbele ya Bunge hili, kuwasilisha Maoni na Mapendekezo ya Kambi ya Upinzani kuhusu hali ya uchumi ya nchi yetu na bajeti kwa mwaka 2011/2012 kwa mujibu wa kanuni za Bunge, kanuni ya 96(6).

      Mheshimiwa Spika, Naomba kwa niaba ya waheshimwa wabunge wote wa Kambi ya Upinzani ambao hawakupata nafasi ya kushiriki au kutoa rambirambi zao kwako kwa msiba mkubwa uliokupata wa kuondokewa na Mama yako mpenzi, nifanye hivyo kwa niaba yao.

      Mheshimiwa Spika, Kabla ya kuanza kutoa mtazamo wetu naomba nikishukuru chama changu cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA, viongozi wangu wakuu wote, kwa juhudi kubwa tunazozifanya ili kuhakikisha Watanzania wanaelewa maana halisi ya “wananchi kuwa na mamlaka kwa Serikali waliyoiweka madarakani kwa njia ya kura”. Vile vile na kwa umuhimu wa kipekee namshukuru Kiongozi wa Upinzani Bungeni Mhe. Freeman Aikael Mbowe (Mb) kwa kuniteua kuwa Waziri Kivuli wa Wizara hii nyeti katika uchumi na maendeleo ya nchi. Kama ilivyo ada yangu, nitaifanya kazi hii kwa uaminifu, uadilifu na umakini mkubwa sana.


      Endelea kusoma katika attachment hii chini
      Attached Files
      Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' |Click HERE for Details

    2. FemaTV & Radio

    3. #2
      mwanaharakat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 406
      Rep Power : 496
      Likes Received
      70
      Likes Given
      0

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      weka yote mkuu wengine tunatumia cm haziwezi kusoma pdf.

    4. #3
      Luteni's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th January 2010
      Posts : 2,269
      Rep Power : 942
      Likes Received
      239
      Likes Given
      73

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Quote By mwanaharakat
      weka yote mkuu wengine tunatumia cm haziwezi kusoma pdf.
      Mzee ina page kama 53 sidhani kama itakuwa rahisi kuiweka yote hapa.
      Luteni is a True Revolutionist.

    5. #4
      Kifulambute's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th May 2011
      Posts : 1,729
      Rep Power : 752
      Likes Received
      453
      Likes Given
      176

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Safi sana mkuu kwa updates zako nimeikubali hii

    6. #5
      mwanaharakat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 406
      Rep Power : 496
      Likes Received
      70
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Luteni
      Mzee ina page kama 53 sidhani kama itakuwa rahisi kuiweka yote hapa.
      Tupe dondoo za maeneo muhimu alizosema.

    7. Miaka 50

    8. #6
      Revolutionary's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 457
      Rep Power : 515
      Likes Received
      79
      Likes Given
      70

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Asante sana Max, the big boss!
      When you have no fear anymore, you are completely free.

    9. #7
      Edson's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2009
      Posts : 7,308
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      433

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      wacha niipitie nione

    10. #8
      Dickson Ng'hily's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 22nd October 2010
      Location : Dar Es Salaam
      Posts : 322
      Rep Power : 499
      Likes Received
      186
      Likes Given
      173

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Quote By mwanaharakat
      Tupe dondoo za maeneo muhimu alizosema.
      UDHAIFU KATIKA MATUMIZI YA FEDHA ZA UMMA.
      Ripoti ta CAG katika Mwaka wa Fedha 2009/10
      Mheshimiwa Spika,
      Matumizi mabaya ya fedha za umma yameendelea kuwa kikwazo
      kikubwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi.
      Uchambuzi wetu juu ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
      Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2009/2010 pekee, umebaini
      takribani jumla ya Tsh trilioni 2.4 za fedha za umma zilitumika vibaya,
      ambazo ni sawa na asilimia 25% ya bajeti yote ya mwaka huo
      ambayo ilikuwa na jumla ya Sh 9.5 trilioni. Hii inaonyesha kuwa
      katika kila Shilingi 100 tunayopitisha hapa Bungeni katika Bajeti
      Shilingi 25 zinaingia kwenye mifuko ya wezi na wabadhirifu wa fedha
      za Umma. Hali hii lazima ikomeshwe mara moja.
      Mheshimiwa Spika,
      Mifano ya fedha zilizopotea au kutumiwa vibaya katika mwaka wa
      fedha wa 2009/10 ni manunuzi yaliyofanywa nje ya mpango wa
      mwaka ya jumla ya Tsh bilioni 50.6, malipo yenye shaka ya jumla ya
      14
      Tsh bilioni 15.5, upotevu wa fedha na mali za serikali wa jumla ya Tsh
      bilioni 11.1 na malipo ya mishahara kwa watumishi waliostaafu,
      waliokufa na watoro kazini ya jumla ya Tsh bilioni 1.8.
      Aidha, Mkaguzi hakukabidhiwa nyaraka na orodha ya walionufaika
      na kiasi cha jumla ya Sh. bilioni 48 (Stimulus package) kilichotolewa
      kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa uchumi toka Benki Kuu ya Tanzania
      katika juhudi za kukabiliana na msukosuko wa uchumi ulioikumba
      dunia.
      Katika mkutano wa Tatu wa Bunge la Kumi nilimwuliza Mheshimiwa
      Waziri Mkuu kuhusu suala la Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
      Serikali kunyimwa nyaraka ili kukagua jumla ya Tshs 48 bilioni
      zilizotajwa hapo juu. Natumai sasa Serikali itakuwa na majibu juu ya
      suala hili. Kambi inaendelea kusisitiza ombi lililotolewa na aliyekuwa
      Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, Mheshimiwa Hamad Rashid
      Mohammed kwamba Fedha zote zilizotolewa kwa ajili ya Stimulus
      Package zikaguliwe na CAG na kuwasilisha Taarifa hiyo maalumu
      Bungeni. Serikali ilikubaliana na ombi hili hivyo tunaomba taarifa hiyo
      mara moja.
      Mheshimiwa Spika,
      Tunalisema hili la Stimulus Package kwa kuwa kuna ushahidi wa
      barua kutoka kwa Katibu Mkuu Hazina akiwaandikia Mameneja wa
      vyama vya ushirika vya mikoa ya Kilimanjaro na Kagera akiwaeleza
      kuwa Serikali pamoja na kuidhinisha kulipwa kwa vyama hivyo, kwa
      sasa hakuna fedha kwa ajili ya kufanya malipo hayo.
      Barua iliyoandikwa kwa Meneja Kagera Cooperative Union (1990)
      ltd ya tarehe 16 Septemba 2010 yenye kumb. Na TYC/B/40/143
      ilikuwa ikimweleza Meneja kuhusiana na serikali kulipa kiasi cha
      shilingi 734,369,379.49 . Ila ilipofika tarehe 27 Aprili 2011 Katibu Mkuu
      wa Hazina aliandika barua nyingine kwa Meneja husika yenye
      kumb.Na.TYC/B/40/143/45 kwa ajili ya kusitisha Malipo ya fidia
      15
      kutokana na mdororo wa uchumi kwa kuwa Serikali haina fedha na
      pia muda wa kulipa fidia hizo ulikwisha tangu mwaka 2010.
      Kuhusiana na chama cha ushirika cha Mkoa wa Kilimanjaro
      (Kilimanjaro Native Cooperation Union (1984), Katibu Mkuu Hazina,
      Ndugu Ramadhan Kijjah mnamo tarehe 16 Septemba aliandika
      barua yenye kumb.Na TYC/B/40/143 iliyowajulisha kuwa Serikali
      imeridhika kuwa wanastahili kupewa fidia ya shilingi 255,107,570.17
      waliyopata kutokana na mdororo wa uchumi duniani. Ila ilipofika
      tarehe 27 Aprili 2011 Katibu Mkuu huyo huyo aliandika barua
      nyingine yenye kumb.Na.TYC/B/40/143/43 akiwajulisha kuwa Serikali
      haina fedha kwa ajili ya kulipa fidia hiyo na kuwa muda wa kulipa
      fidia ulikuwa umekwisha tangu mwaka 2010.
      Mheshimiwa Spika,
      Kupatikana kwa barua hizi ni uthibitisho wa wazi kuwa kuna tatizo
      kubwa kuhusiana na fedha zilizotolewa na Serikali kwani wakati
      Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Omar Yusuph Mzee akiwa anajibu swali
      la msingi la Mhe. Mhonga Saidi Ruhanywa wakati wa Bunge la Bajeti
      la mwaka 2010/11 alisema kuwa mpango ulikuwa unaenda vizuri.
      Pia wakati Waziri wa Fedha Mhe. Mkullo akiwa anahitimisha hotuba
      ya bajeti ya mwaka 2010/11 alilieleza bunge hili kuwa mpango
      ulikuwa unaenda vizuri.
      Bushloiaz likes this.
      'Ppooooz.......Pawaaaaa
      Hakuna Kulala.......Mpaka Kieleweke'
      0716/0765/0788-030030

    11. #9
      Barubaru's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th April 2009
      Location : Doha, Qatar
      Posts : 5,740
      Rep Power : 1919
      Likes Received
      1178
      Likes Given
      962

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Kwa kweli ni nzuri na rahisi sana kutekelezeka na imejali maslahi ya kila mtu kuanzia wale wa chini mpaka juu.

      Suala linabaki pale pale kwa waTanzania je mtaweza kuisimamia na kuitekeleza kwa 100% au ndio inabaki kwenye makaratasi tu.

      Hongera sana Zitto
      Ukiwa mchoyo, usiwe mroho.

      Man Sharaf naf'sahu, fahuwa rasul

    12. #10
      Revolutionary's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th January 2011
      Posts : 457
      Rep Power : 515
      Likes Received
      79
      Likes Given
      70

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Tanesco wamekata umeme, bila shaka ni kwa maslahi duni ya CCM, na watashindwa na kulegea!

    13. #11
      Nyambala's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th October 2007
      Location : Tahiti
      Posts : 4,402
      Rep Power : 1517
      Likes Received
      1019
      Likes Given
      938

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Nimesoma ila naona itabidi nirudie tena, hivyo vyanzo mbadala vya mapato naona kama havijaainishwa zaidi, yaani kuweka specifics.

    14. #12
      sulphadoxine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 2,115
      Rep Power : 923
      Likes Received
      550
      Likes Given
      2008

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Mheshimiwa Spika
      , Asilimia 33.4 ya Watanzania wanaishi chini yamstari wa umasikini na kwa waishio vijijini ni asilimia 37.4 wakatiasilimia 16.2 tu ya Watanzania waishio Dar es Salaam wanaishi chiniya mstari wa Umasikini. Wakati tofauti ya kipato kwa Watanzania niasilimia 35, matajiri wa juu asilimia 20 wanamiliki asilimia 42 ya Patola Taifa (consumption expenditure) na masikini wa chini kabisa
      asilimia 20 wanamiliki asilimi 7 tu ya Pato la Taifa.
      CHUKI NA UADUI NI MATOKEO YA UPUMBAVU:

    15. #13
      sulphadoxine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 2,115
      Rep Power : 923
      Likes Received
      550
      Likes Given
      2008

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Mheshimiwa Spika,
      taarifa ya Hali ya uchumi inaonyesha kuwapamoja na sekta kadhaa kukua lakini bado hazijaongeza mchangowake katika ukuaji wa pato la taifa ukilinganisha na ukuaji wa sektahusika. Kwa mfano, sekta ya mawasiliano imekuwa kwa asilimia 22.1ila mchango wake katika pato la Taifa ni asilimia 2.1 tu, shughulindogo za hoteli na migahawa ukuaji wake ulikuwa 6.1 lakinimchango wake katika ukuaji wa pato la taifa ni 2.3% tu. Hii inamaana kuwa sekta hizi hazina uhusiano wa moja kwa moja (stronglinkages) katika ukuaji wa uchumi na katika kukuza pato la taifa na
      hivyo kushindwa kupunguza hali ngumu ya maisha kwa wananchi
      CHUKI NA UADUI NI MATOKEO YA UPUMBAVU:

    16. #14
      sulphadoxine's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 2,115
      Rep Power : 923
      Likes Received
      550
      Likes Given
      2008

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Kambi ya Upinzani
      inaunga mkono ushauriuliotolewa na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Ummakwamba sasa Benki Kuu ya Tanzania ianze kutunza sehemu yaHifadhi ya nchi katika Dhahabu. Benki Kuu inunue dhahabu kutokakwa wachimbaji wadogo na pia tuangalie uwezekano wa kutozasehemu ya mrahaba katika madini kama ‘dhahabu safi’ (‘pure
      gold’).
      CHUKI NA UADUI NI MATOKEO YA UPUMBAVU:

    17. #15
      Maishamapya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Location : Dar, Tanzania
      Posts : 899
      Rep Power : 612
      Likes Received
      214
      Likes Given
      262

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Quote By Maxence Melo
      HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI YA UPINZANI BUNGENI WIZARA YA FEDHA MHE.KABWE ZUBERI ZITTO (MB) KUHUSU MPANGO NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2011/2012

      UTANGULIZI

      Mheshimiwa Spika, Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuweza kusimama hapa mbele ya Bunge hili, kuwasilisha Maoni na Mapendekezo ya Kambi ya Upinzani kuhusu hali ya uchumi ya nchi yetu na bajeti kwa mwaka 2011/2012 kwa mujibu wa kanuni za Bunge, kanuni ya 96(6).

      Mheshimiwa Spika, Naomba kwa niaba ya waheshimwa wabunge wote wa Kambi ya Upinzani ambao hawakupata nafasi ya kushiriki au kutoa rambirambi zao kwako kwa msiba mkubwa uliokupata wa kuondokewa na Mama yako mpenzi, nifanye hivyo kwa niaba yao.

      Mheshimiwa Spika, Kabla ya kuanza kutoa mtazamo wetu naomba nikishukuru chama changu cha Demokrasia na Maendeleo – CHADEMA, viongozi wangu wakuu wote, kwa juhudi kubwa tunazozifanya ili kuhakikisha Watanzania wanaelewa maana halisi ya “wananchi kuwa na mamlaka kwa Serikali waliyoiweka madarakani kwa njia ya kura”. Vile vile na kwa umuhimu wa kipekee namshukuru Kiongozi wa Upinzani Bungeni Mhe. Freeman Aikael Mbowe (Mb) kwa kuniteua kuwa Waziri Kivuli wa Wizara hii nyeti katika uchumi na maendeleo ya nchi. Kama ilivyo ada yangu, nitaifanya kazi hii kwa uaminifu, uadilifu na umakini mkubwa sana.


      Endelea kusoma katika attachment hii chini
      Asante Mkuu. Lakini mbona ina watermark ya "draft"? Ndiyo hii hii aliyosoma leo?
      "Even a fool is thought wise if he keeps silent, and discerning if he holds his tongue" (Prov 17:28 NIV)

    18. #16
      mwanaharakat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 406
      Rep Power : 496
      Likes Received
      70
      Likes Given
      0

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Ahsante wakuu kwa taarifa zenu. Bado sijasikia suala la posho hajatamka lolote?

    19. #17
      samora10's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st July 2010
      Location : Kwa-Gude
      Posts : 3,252
      Rep Power : 1102
      Likes Received
      729
      Likes Given
      1163

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      Quote By ng'hily
      UDHAIFU KATIKA MATUMIZI YA FEDHA ZA UMMA.
      Ripoti ta CAG katika Mwaka wa Fedha 2009/10
      Mheshimiwa Spika,
      Matumizi mabaya ya fedha za umma yameendelea kuwa kikwazo
      kikubwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi.
      Uchambuzi wetu juu ya ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa
      Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2009/2010 pekee, umebaini
      takribani jumla ya Tsh trilioni 2.4 za fedha za umma zilitumika vibaya,
      ambazo ni sawa na asilimia 25% ya bajeti yote ya mwaka huo
      ambayo ilikuwa na jumla ya Sh 9.5 trilioni. Hii inaonyesha kuwa
      katika kila Shilingi 100 tunayopitisha hapa Bungeni katika Bajeti
      Shilingi 25 zinaingia kwenye mifuko ya wezi na wabadhirifu wa fedha
      za Umma. Hali hii lazima ikomeshwe mara moja.
      Mheshimiwa Spika,
      Mifano ya fedha zilizopotea au kutumiwa vibaya katika mwaka wa
      fedha wa 2009/10 ni manunuzi yaliyofanywa nje ya mpango wa
      mwaka ya jumla ya Tsh bilioni 50.6, malipo yenye shaka ya jumla ya
      14
      Tsh bilioni 15.5, upotevu wa fedha na mali za serikali wa jumla ya Tsh
      bilioni 11.1 na malipo ya mishahara kwa watumishi waliostaafu,
      waliokufa na watoro kazini ya jumla ya Tsh bilioni 1.8.
      Aidha, Mkaguzi hakukabidhiwa nyaraka na orodha ya walionufaika
      na kiasi cha jumla ya Sh. bilioni 48 (Stimulus package) kilichotolewa
      kwa ajili ya kuchochea ukuaji wa uchumi toka Benki Kuu ya Tanzania
      katika juhudi za kukabiliana na msukosuko wa uchumi ulioikumba
      dunia.
      Katika mkutano wa Tatu wa Bunge la Kumi nilimwuliza Mheshimiwa
      Waziri Mkuu kuhusu suala la Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
      Serikali kunyimwa nyaraka ili kukagua jumla ya Tshs 48 bilioni
      zilizotajwa hapo juu. Natumai sasa Serikali itakuwa na majibu juu ya
      suala hili. Kambi inaendelea kusisitiza ombi lililotolewa na aliyekuwa
      Waziri Kivuli wa Fedha na Uchumi, Mheshimiwa Hamad Rashid
      Mohammed kwamba Fedha zote zilizotolewa kwa ajili ya Stimulus
      Package zikaguliwe na CAG na kuwasilisha Taarifa hiyo maalumu
      Bungeni. Serikali ilikubaliana na ombi hili hivyo tunaomba taarifa hiyo
      mara moja.
      Mheshimiwa Spika,
      Tunalisema hili la Stimulus Package kwa kuwa kuna ushahidi wa
      barua kutoka kwa Katibu Mkuu Hazina akiwaandikia Mameneja wa
      vyama vya ushirika vya mikoa ya Kilimanjaro na Kagera akiwaeleza
      kuwa Serikali pamoja na kuidhinisha kulipwa kwa vyama hivyo, kwa
      sasa hakuna fedha kwa ajili ya kufanya malipo hayo.
      Barua iliyoandikwa kwa Meneja Kagera Cooperative Union (1990)
      ltd ya tarehe 16 Septemba 2010 yenye kumb. Na TYC/B/40/143
      ilikuwa ikimweleza Meneja kuhusiana na serikali kulipa kiasi cha
      shilingi 734,369,379.49 . Ila ilipofika tarehe 27 Aprili 2011 Katibu Mkuu
      wa Hazina aliandika barua nyingine kwa Meneja husika yenye
      kumb.Na.TYC/B/40/143/45 kwa ajili ya kusitisha Malipo ya fidia
      15
      kutokana na mdororo wa uchumi kwa kuwa Serikali haina fedha na
      pia muda wa kulipa fidia hizo ulikwisha tangu mwaka 2010.
      Kuhusiana na chama cha ushirika cha Mkoa wa Kilimanjaro
      (Kilimanjaro Native Cooperation Union (1984), Katibu Mkuu Hazina,
      Ndugu Ramadhan Kijjah mnamo tarehe 16 Septemba aliandika
      barua yenye kumb.Na TYC/B/40/143 iliyowajulisha kuwa Serikali
      imeridhika kuwa wanastahili kupewa fidia ya shilingi 255,107,570.17
      waliyopata kutokana na mdororo wa uchumi duniani. Ila ilipofika
      tarehe 27 Aprili 2011 Katibu Mkuu huyo huyo aliandika barua
      nyingine yenye kumb.Na.TYC/B/40/143/43 akiwajulisha kuwa Serikali
      haina fedha kwa ajili ya kulipa fidia hiyo na kuwa muda wa kulipa
      fidia ulikuwa umekwisha tangu mwaka 2010.
      Mheshimiwa Spika,
      Kupatikana kwa barua hizi ni uthibitisho wa wazi kuwa kuna tatizo
      kubwa kuhusiana na fedha zilizotolewa na Serikali kwani wakati
      Naibu Waziri wa Fedha Mhe. Omar Yusuph Mzee akiwa anajibu swali
      la msingi la Mhe. Mhonga Saidi Ruhanywa wakati wa Bunge la Bajeti
      la mwaka 2010/11 alisema kuwa mpango ulikuwa unaenda vizuri.
      Pia wakati Waziri wa Fedha Mhe. Mkullo akiwa anahitimisha hotuba
      ya bajeti ya mwaka 2010/11 alilieleza bunge hili kuwa mpango
      ulikuwa unaenda vizuri.

      aiseee hii ishu ya stimulus package lazima tuzae nao hawa.. watueleze kinagaubaga hizi fedha zimekwenda wapi na zimefanya nini kumsaidia mtanzania wa kawaida
      ''Mipango na Mikakati imekamilika na sasa tuko kwenye mchakato wa mazungumzo na wafadhili"- M Pinda

    20. #18
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 9,741
      Rep Power : 2884
      Likes Received
      1115
      Likes Given
      52

      Default

      Quote By mwanaharakat
      weka yote mkuu wengine tunatumia cm haziwezi kusoma pdf.
      sure mdau

    21. #19
      Edson's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th March 2009
      Posts : 7,308
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1799
      Likes Given
      433

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      kitu kimesimama.....page 53 zilizoshiba..........

    22. #20
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,605
      Rep Power : 1330
      Likes Received
      780
      Likes Given
      655

      Default Re: Hotuba ya Zitto Kabwe Bungeni Juni 15, 2011

      stimulus package nadhani itakuwa inatumika ktk mambo tofauti na ilivyokusudia,na hakutakuwa na majibu sahihi juu ya hilo,unaweza kuta ndio inayotumika kujinunulia ktk kusomesha watoto wa vigogo hapa tz

    Page 1 of 6 123 ... LastLast

    LinkBacks (?)

    1. 4th October 2011, 14:14

    Similar Topics

    1. Replies: 1
      Last Post: 25th August 2011, 18:07
    2. Mchango wa mheshimiwa Zitto Kabwe Bajeti 2010/2011
      By Ntemi Kazwile in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 10
      Last Post: 14th June 2010, 17:55
    3. Hotuba ya Dr. Slaa Bungeni Juni 2009
      By BAK in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 63
      Last Post: 24th June 2009, 07:35
    4. Hotuba Ya Mheshimiwa Zitto Zuberi Kabwe Kuhusu Miundombinu Bungeni
      By Mpaka Kieleweke in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 39
      Last Post: 18th December 2008, 00:15

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...