TiGo Says
    Show/Hide This

    Topic: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

    Report Post
    Page 1 of 7 123 ... LastLast
    Results 1 to 30 of 186
    1. #1
      mashadoplantan's Avatar
      Member Array
      Join Date : 28th April 2011
      Posts : 41
      Rep Power : 364
      Likes Received
      18
      Likes Given
      15

      Default Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake





      Mshairi Muyaka Al Ghassany (1776-1840 ) toka Mombasa aliwahi kusema hivi:

      Vita vyako Fahamu
      Havimdhuru Karimu
      Ila wewe Bahaimu
      Jujue Utaumia


      Katika hali isiyo ya kawaida Jumuiya ya wa Swahili Tanzania imemjia juu Spika Anne Makinda juu ya kauli yake ya kuwakebehi watu wa Kariakoo ambako wengi wao wana asili ya Kiswahili.

      Tamko rasmi la Jumuiya ya waswahili limekuja baada ya kauli ya makinda iliyojaa dharau na kebehi kwa wabunge kuwa wasiwe kama watu wa Kariakoo. Klabu ya Saigon nayo imesema itatoa tamko lao rasmi kesho juu ya haya matamshi machafu na ya dharau ya spika Anna Makinda.

      Anne Makinda labda alitakiwa kurudi darasani na akapigwe brash kuhusu umuhimu wa Kariakoo na watu waliowahi kuishi kariakoo na Makinda should know better than most kuwa hicho chama kilichomweka kwenye hicho kiti alichokalia kilizaliwa Kariakoo na na kusema ukweli ni kuwa dharau aliyoitoa Anna Makinda kwa kariakoo itakuwa si kwa wafanya bishara ndogo ndogo walipo pale bali ni pamoja na waswahili wengine kama akina Mwinjuma Mwinyikambi, Kiyate Mshume, Jumbe Tambaza, Sheikh Hassan bin Amir and Sheikh Suleiman Takadir ambao walikuwa ni wakaazi wa Kariakoo.

      Labda Makinda angeongea na wenzie wakampeleka maeneo ya makuu 4 yaliyoifanya kariakoo :

      1.Kariakoo

      2.Gerezani

      3.Kisutu

      4.Mission Quarter.

      Spika Anna angejua watu wa Katiakoo wameshiri vipi kwenye kwenye uhuru wa nchi hii asingeweza kuwatukana wabunge kwa dharau kama alivyofanya leo.

      Najua Makinda hawezi kumwomba ZUNGU au wabunge wengine wa Dar lakini sitoshangaa kuwa huyu mama akawa hajui hata hiyo TAA ilikuwa na makao makuu wapi na sacrifice zipi mzee Bin Sudi aliziingia kutoa lile jengo mwaka 1930!

      Anna kama ulijuwa hujui basi ujue kuwa jengo hili ndio TANU ilizaliwa na mpaka leo lipo pale mtaa wa kariakoo na Mtaa Mpya ulipoungana


      Kama ulikuwa hujui basi upande wa Magharibi wa Kariakoondiko ilikokuwa Mission Quarter (NYUMA YA TBL) na eneo hili lilitengwa maalim kwa ajili ya kuwalinda wahamiaji na waswahili waliokuwa wengi kariakoo na ambao waliishhi kwa amani na utulivu kwa miaka zaidi ya 70 mpaka leo hii ambako Pspika wa Bunge unatoa kauli zenye nia ya kuvunja amani na utulivu baina ya watu wa kariakoo

      Kwa kuonyesha kuwa Waswahili wa Kariakoo walikuwa hawana kinyongo ndio maana majina ya mitaa imebaki vile vile kama vile mtaa wa Masasi, Likoma, Ndanda, Muhonda, Muheza , Magila na sasa hivi mmetuletea jina la mpuuzi wenu yule (MAKAMBA) na mkampa mtaa jina ili hali hana lolote la maana linalomsabahisha na Kariakoo (when time will come TUTALIONDOA)

      Lakini wana JAMII FORUM msimlaumu sana huyu Anna Makinda kwani naye anafuata nyayo za baba yake Mwalimu Nyerere ambaye alianza kupandikiza mbegu mbaya za kudharau not only waswahili lakini wana kariakoo kwa ujumla.

      Watu wengine maarudu ambao walikuwa ni wana Kariakoo walikuwa wakazi wa MISSION QUATER ni babu yangu bwana THOMAS PLANTAN ambaye alikuwa ni rais wa African Association na al Marhum mzee JOHN RUPIA ambaye alikuwa ni tajiri mkubwa sana enzi zile.

      Anna Makinda kama hujui basi kwa taarifa yako tuu ni kuwa nyumba ya Al Marhum John Rupia ilikuwa mtaa wa Likoma na Magila, nyumba hii mpaka leo ipo na ndiko African Association ilianzishwa mwaka 1929. Nyumba hii mpaka leo ipo japi si katika hali yake ya zamani.

      Lakini pia nataka nikujulishe kuwa Mission Quarter ndiko kulikokuwepo kiwanda cha kuchapisha cha mwafrica wa kwanza ambacho kilikuwa cha mzee wangu MASHADO PLANTAN ambaye alikuwa ni mtu wa kusini na alikuwa anachapisha JAMII FORUM ya enzi hizo ilikuwa ikiitwa ZUHURA ambayo Nyerere alikuwa analitumia sana kupiga debe dhidi ya wakoloni!

      Lakini yote hayo Makinda kwako unaona ni upuuzi tuu kwani kariakoo pia ina eneo linaitwa GEREZANI ambako ilikuwa ni nyumbani kwa Omari Londo, Ally Sykes, Zuberi Mtemvu, Mashado Plantan, Muhsin Mende and Dossa Aziz. Hawa walikuwa ni majabali na wazalendo waliokutana na Nyerere baadae. Kwa kuonyesha tuu kuwa sisi si wafuata bendera, ZUBERI MTEMVU, MUHSIN MENDE na MASHADO PLANTAN waliamua kujiondoa TANU na kuanzisha chama kingine cha upinzani kwa jina la TANGNYIKA AFRICAN CONGRESS na hapo ndiko zilianza tofauti kubwa na baba yako Nyerere.

      Anna makinda unaposema waBunge wasiwe kama watu wa kariakoo unamaana hutaki wawe INDEPENDENT THINKERS kama akina Mzee Mshume Kiyate, Sheikh Hassan bin Ameir, Sheikh Suleiman Takadir, Idd Faizi, Idd Tosiri, Bantu Kasella Bantu, Abdulwahid Sykes and Dossa Aziz?

      Kwa kuendelea kukuambia tuu umuhimu wa kariakoo ni kuwa ile open space inayotazamana na viwanja vya Mnazi Mmoja ilikuwa ni plot ya JOHN RUPIA ambayo aliitoa kama zawadi kwa TANU ili wajenge ile centre. Of course kwa sababu ya serikali yako ilivyokuwa haithamini historia na heritage ili nyumba ilivynjwa wamejenga gorofa pale bila kuzingatia au kuweka kumbukumbu yoyote ile, na huyo baba yenu Nyeree mnaye sema kuwa mnahifadhi ujumbe wake historia kaye nyingi iliyokuwa mle ndani iliishia kutupwa bila mazingatio yoyote yale ya kuhifadhi yaliyokuwa mle.

      Sehemu nyingine ambayo leo hii umeitukana ni Soko la kariakoo ambalo Nyerere alikuwa haishi kwenda pale....bila kusahau kuwa hata shirika la masoko kariakoo lilikuwa linatoa SCHOLARSHIP kuwasomesha watu mpaka University of Dar.

      Leo Hii spika wa Bunge umeamua kuwatukana :

      WASHOMVI ambao walikuwa wanafanya baishara ya samaki

      WAZARAMO ambao walikuwa wanafanya baishara ya nazi

      WANYAMWEZI (wanawake) ambao walikuwa wanafanya baishara ya tumbaku kavu huku wanaume wakifanya biashara ya viazi ziliskukuwa zinalimwa Kigamboni

      WALUGURU walikuwa wanafanya biashara za machungwa na mboga za majani

      WAARABU walikukuwa wanafanya biashara ya ngano, mabucha ya nyama, na viungo mbali mbali

      WAHINDI walikuwa wanashindana sana na WAARABU kwenye biashara mbali mbali


      Je Anna Makinda unajua kama Nyerere aliwahi kufanya kazi soko la kariakoo kama Market Master? Je unajua kama ofisi yake ilikuwa kwenye junction ya mtaa wa Tandamti ( siku hizi mnauita mtaa wa Mshume Kiyate) na mtaa wa Swahili?

      Matusi uliyowatukana wana Kariakoo leo ni matusi ambayo umewatukana wa Swahili wa Mwembe Togwa (siku hizi mnapaita Fire), Umewatukana wakari wa Ronald Cameroon Road ( sikuhizi United Nations Road) na wengineo wengi...lakini wansiasa wenye calibre za wewe Anna Makinda ndio hao hao mlioamua kuquestion maamuzi ya mzee Kitwana Kondo alipokuwa meya mwaka 1995 alipoa mua kubadili jina la mtaa wa Tandamti na kuita mtaa wa Mshume Kiyate ...tena mlipiga makelele mkisaidiwa na waandishi wa habari ambao hawaijui historia ya kariakoo kwa kuuliza huyu Mshume Kiyate ni nani? Nyie nyie ndio mlilalamika mitaa mingine ya kariakoo ilipobadilishwa na kupewa majina ya Tatu Binti Mzee, Max Mbwana, Omari Londo halafu leo hii unathubutu kututukana sisi wana Kariakoo!

      Onyo kwa Anna Makinda na wanasiasa wenye tabia za kudharau watu wa kariakoo kama Cyrill Chami na wengineo, Wana Kariakoo na Waswahili wa zama hizi hatutonyamaza kwani vyombo vya kulalama tunavyo na haki zetu tunazijua na mkiendelea na dharau zenu basi mjue kuwa pamoja kuwa waswahili hatutonyamaza na kama ikiwezekana tujibu mapigo basi tutaangalia namna bora zaidi za kuwajibu lakini hatutokaa kimya...maana leo mmeanza na waswahili na watu wa kariakoo kesho tunajua mtahamia kwa wa chagga na watu wa Moshi kesho kutwa mtahamia kwa nyakyusa na watu wa Mbeya na Iringa

      Tofauti ni kuwa sasa tumelimika na tunaouwezo wa kuona mnapoanza kutuletea dharau bila kujali wakazi na watu wa kariakoo nao ni wapiga kura kama watu wa kwenu


      Muyaka al Ghassany pia alisema hivi:
      Yu wapi Firauni
      Yuwapi wapi Karuni
      Na Shadadi Maluuni
      Wote wameangamia


      Anna Makinda leo umeamua kuwatukana wana Kariakoo, historia ya Kariakoo na wanaotafuta rizki zao Kariakoo na Waswahili wanaoishi pale lakini ukae ukijua kuwa kuna leo na kesho na sisi hili hatutosahau. Mshazowea kututukana lakini at some point someone has to stand up and say no hatukubali. Labda umesahau kuwa kwa waswahili wa Kariakoo kuna 2 extremes ambazo naona ushazowea ile moja tuu
      Last edited by mashadoplantan; 15th June 2011 at 11:18.


    2. #2
      Bajabiri's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st December 2010
      Posts : 6,465
      Rep Power : 1782
      Likes Received
      537
      Likes Given
      0

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Dah.......asante mdau nimejifunza history hapa.........akutukanae akuchagulii TUSI

    3. #3
      regam's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th January 2011
      Posts : 188
      Rep Power : 414
      Likes Received
      21
      Likes Given
      2

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Mh!kaaaaz kwelikweli!

    4. #4
      SHERRIF ARPAIO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th August 2010
      Location : The Bronx
      Posts : 1,714
      Rep Power : 756
      Likes Received
      484
      Likes Given
      170

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Kelele zooooteeeeee hizo za wanakariakoo lakini uchaguzi ukija magamba ya kijani yanapata 100% of the vote. kazi ipo
      Dingswayo, Arafat and Chilipamwao like this.
      He who knows, and knows that he knows, is a wise man, emulate him.
      He who knows not, and knows not that he knows not, is a fool, shun him.

    5. #5
      rosemarie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 1,476
      Rep Power : 659
      Likes Received
      213
      Likes Given
      129

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Quote By SHERRIF ARPAIO View Post
      Kelele zooooteeeeee hizo za wanakariakoo lakini uchaguzi ukija magamba ya kijani yanapata 100% of the vote. kazi ipo
      wanakuwa kama hawaoni mbali,lakini wamsamehe yule mama kwani naona kama amelemewa na ile kazi

    6. #6
      Oxlade-Chamberlain's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 26th May 2009
      Location : dodoma
      Posts : 6,995
      Rep Power : 4245
      Likes Received
      618
      Likes Given
      640

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Huyo mama anahitaji aombe msamaha na afute kauli yake.
      "Nobody has enough talent to live on talent alone. Even when you have talent, a life without work goes nowhere". A. Wenger

    7. #7
      Lole Gwakisa's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 5th November 2008
      Posts : 2,590
      Rep Power : 1007
      Likes Received
      325
      Likes Given
      273

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake




      Kama kwa picha iliyopostiwa ndio reflection ya jamii ya waswahili, basi ni heri Mama Makinda wala asithubutu kuomba radhi.
      Yaani mnataka Bunge liwe na marap rap ya kiswahili kama hayo?
      Yours faithfully!

    8. #8
      Nduka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2011
      Posts : 1,237
      Rep Power : 616
      Likes Received
      213
      Likes Given
      487

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Mwaka huu mmeshikwa pabaya mtatafuta mchawi msimpate, naona mnaokoteza hoja za kulazimisha. Kila mtu hata anayekaa kariakoo anajua kuwa neno kariakoo limenasibishwa na soko na hata mitaani linavyotumika ni sawa na soko. Sasa hao wahuni wanaotaka kufananisha bunge na soko/ kariakoo wasitafute upenyo kuficha uozo wao kwa kupitia hoja hii isiyo na mashiko. Kwa kuwa ninyi ndio think tank yao waambieni dawa ni ku behave kama wawakilishi wa wananchi na wala sio wauza kahawa wa Saigoni ambao hawabanwi na sheria wala kananuni kuongea utumbo.

    9. #9
      mwanaharakat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 405
      Rep Power : 444
      Likes Received
      64
      Likes Given
      0

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Kariakoo wacha watukanwe ni wao ndo walijifanya ccm damu wakat wa uchaguzi sasa hii ndo shukran ya punda...

    10. #10
      Kimilidzo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd January 2011
      Posts : 584
      Rep Power : 489
      Likes Received
      107
      Likes Given
      1

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Bonge la historia ya kariakoo iliyoandaaliwa kwa weledi wa hali ya juu. Toa nakala kwenye gazeti kama inawezekana ili wengine kama Makinda ambao ni waoga wa kushindana kwa hoja na hawana ujanja wa kuja JF waone hiyo historia na kuipa Kariakoo heshima inayostahili.
      mashadoplantan likes this.

    11. #11
      Safety last's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th March 2011
      Posts : 2,447
      Rep Power : 850
      Likes Received
      452
      Likes Given
      0

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Asante mkuu unichambulia hiyo kariakoo mpaka nimejiskia poa hongera mkubwa unaweza ukaendlea na nyingine muheshimiwa


    12. #12
      Bigirita's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 15th June 2009
      Location : Under a mango tree
      Posts : 8,640
      Rep Power : 2345
      Likes Received
      1583
      Likes Given
      2017

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Watu wengine bana!!

      1) nini maana ya colours ulizotumia?
      2) nini essence ya kuuliza kama watu wanajua nyumba ya sijui nani na nanizilipokuwa?
      3) Mitaa ya kariakoo na ubadilishwaji wake una maana gani hapa?

      Unajua lugha ya picha wewe!!!! oooh!! sykes, sijui Shamte sijui Rupia..............ili iweje?

      Utamaduni wa kulalamika kuonewa hata kwenye mambo yasiyo na maana ni jambo baya sana!!

      Nakubali kuwa matumizi ya maneno kama haya sio mazuri, na natambua kwamba yanaweza kutafsiriwa vibaya, na the fact kwamba Makinda labda anahitaji kufundishwa Communication Skills.

      Pia usisahau Makamba alishawahi kusema same thing!!
      I'm not being rude. You're just insignificant.

    13. #13
      Chitemo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2011
      Posts : 468
      Rep Power : 458
      Likes Received
      42
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By SHERRIF ARPAIO View Post
      Kelele zooooteeeeee hizo za wanakariakoo lakini uchaguzi ukija magamba ya kijani yanapata 100% of the vote. kazi ipo
      Kwa sababu wengi wao ni waislamu wao ni cuf na ccm tu. Waache watukanwe mpaka kwenye misuli.
      aiai654 likes this.

    14. #14
      MAURIN's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 14th June 2011
      Posts : 129
      Rep Power : 375
      Likes Received
      5
      Likes Given
      4

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Huyu mama hafai kuwa spika wa bunge la TANZANIA,yeye na serikali yake ya CCM wanadharau kwa wananchi wa TANZANIA,ILA MWISHO UMEFIKA

    15. #15
      figganigga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th October 2010
      Location : dar es salaam
      Posts : 4,166
      Rep Power : 1562
      Likes Received
      923
      Likes Given
      652

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      duh...!!mkweli aombe msamaha.

    16. #16
      Nduka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th February 2011
      Posts : 1,237
      Rep Power : 616
      Likes Received
      213
      Likes Given
      487

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Nenda kawaambie waliokutuma wajipange upya, tamko halifanani na makala za Lula mwana nzela, andika hapo jina na tarehe kisha utueleze hiyo jumuiya ya waswahili unawaowaita wa kariakoo ilisajiliwa na mamlaka gani hapa nchini.

    17. #17
      JF-BAN1's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 13th April 2011
      Posts : 10,447
      Rep Power : 0
      Likes Received
      3752
      Likes Given
      2889

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Tena huyu mama katukosea vibaya sana. Anashangaza! Khaa, haoni haya wala hajui vibaya!

      Mengi kayasema Mashado, mimi sina zaidi ila namuandikia barua rasmi huko huko bungeni atuombe radhi.

    18. #18
      Bigirita's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 15th June 2009
      Location : Under a mango tree
      Posts : 8,640
      Rep Power : 2345
      Likes Received
      1583
      Likes Given
      2017

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Quote By MAURIN View Post
      Huyu mama hafai kuwa spika wa bunge la TANZANIA,yeye na serikali yake ya CCM wanadharau kwa wananchi wa TANZANIA,ILA MWISHO UMEFIKA
      Jamani eeh! sasa hivi ni zmu ya akina mama!!!
      Mwenyekiti wa chama alisema!
      I'm not being rude. You're just insignificant.

    19. #19
      Kiranga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th January 2009
      Posts : 8,122
      Rep Power : 17490
      Likes Received
      2209
      Likes Given
      243

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Anna Makinda is a disgrace to all clear thinking Tanzanians.
      It is hard not to argue about right and wrong- The 20 Difficulties.

    20. #20
      Jombi Jombii's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 4th June 2011
      Posts : 173
      Rep Power : 385
      Likes Received
      9
      Likes Given
      27

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Huyu Bibi Makinda anachemka kila eneo lakini yote ni jazba yake kwa mambo ambayo angeweza kutoa maagizo bila kuropoka.Nadhani alimaanisha zile patashika za wafanyabiashara wa sokoni kariakoo wakati wa kuuza na kununua ambapo kila mtu anaongea bila mpangilio.MSAMEENI BURE WALIOMPONZA NI WALIOMSHAWISHI ACHUKUE NAFASI YA BOSI WAKE

    21. #21
      Mkandara's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 12,007
      Rep Power : 3877
      Likes Received
      3142
      Likes Given
      2816

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Lakini wana JAMII FORUM isije msimlaumu sana huyu Anna Makinda kwani naye anafuata nyayo za baba yake Mwalimu Nyerere ambaye alianza kupandikiza mbegu mbaya za kudharau not only waswahili lakini wana kariakoo kwa ujumla.

      Unaposema huyu mama anafuata nyayo za Baba yakeMwalimu Nyerere una maana gani? haya ni matusi makubwa na nadhani kuna haja ya wewe kuwaomba wana JF msamaha..


      Exploration of reality

    22. #22
      Matola's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 5,872
      Rep Power : 10399
      Likes Received
      2479
      Likes Given
      1794

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Mimi sioni kosa la Anna Makinda, kwa sababu ushaidi upo, vibaka wote wapo kariakoo, watu wa porojo wasio na kazi za kufanya wapo kariakoo, nyumba mbovu na duni zipo kariakoo, mashoga wapo kariakoo.
      Sasa aombe radhi ya nini? au kwa sababu ni mkristo? mbona ikulu kule kuna wavuta bange wa kumwaga tu kwenye eneo la feri ambapo ni opposite na makao ya Rais?
      Nasisitiza Spika ni mtu mkubwa hawezi kushinikizwa na kikundi cha wanywa kahawa kama huyu alieleta mada hii.
      Kanigini and MAKAH like this.
      WAFU: Hawa ni maiti wako Hai ila ni mazoba, hata wakiambiwa na CCM walipie PUMZI na USINGIZI watalipia ingawa hawana kitu. Wanakubaliana na kila hali hawajui kupinga wala kukataa, hawana tofauti na mabehewa ya treni kinakokwenda kichwa ndiko wanakokwenda wao.

    23. #23
      maandamano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th March 2011
      Location : Dar es Salaam
      Posts : 916
      Rep Power : 547
      Likes Received
      290
      Likes Given
      856

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      nampongeza mh.spika kwa kuwadiss hawa wanacarrier corps,waliipigia kura nyingi sana ccm wakati wa uchaguzi..na bado
      Women are not allowed to attend school. You can be jailed for owning a television. A man can be jailed in Afghanistan if his beard is not long enough.George W.Bush,2001

    24. #24
      Mafie PM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th March 2011
      Posts : 1,099
      Rep Power : 585
      Likes Received
      157
      Likes Given
      550

      Default

      Quote By Puuuuu View Post
      Kwa sababu wengi wao ni waislamu wao ni cuf na ccm tu. Waache watukanwe mpaka kwenye misuli.
      Hilo nalo neno! Ingekuwe imetoka kwa CDM hiyo kauli wallah kesho wangejilipua.

    25. #25
      Kichwa Ngumu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 6th November 2010
      Location : In the Computer
      Posts : 1,083
      Rep Power : 597
      Likes Received
      132
      Likes Given
      130

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Ni kiashiria kuwa hafai kuwa kiongozi.heshima na nidhamu haipimwi kwa kuomba msamaha ila mwenye heshima na nidhamu anajizuia kufanya makosa ambayo yatamtaka aombe samahamani.maneno kama haya hatukuyaona wakati wa uongozi wa Mr. 6
      Mi Bosi ofisini kwangu lakini sio mtaani

    26. #26
      Mkandara's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 2nd March 2006
      Location : T dot
      Posts : 12,007
      Rep Power : 3877
      Likes Received
      3142
      Likes Given
      2816

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Quote By Matola View Post
      Mimi sioni kosa la Anna Makinda, kwa sababu ushaidi upo, vibaka wote wapo kariakoo, watu wa porojo wasio na kazi za kufanya wapo kariakoo, nyumba mbovu na duni zipo kariakoo, mashoga wapo kariakoo.
      Sasa aombe radhi ya nini? au kwa sababu ni mkristo? mbona ikulu kule kuna wavuta bange wa kumwaga tu kwenye eneo la feri ambapo ni opposite na makao ya Rais?
      Nasisitiza Spika ni mtu mkubwa hawezi kushinikizwa na kikundi cha wanywa kahawa kama huyu alieleta mada hii.
      Mkuu samahani ningerudisha matusi mazito lakini hapa sii mahala pake. Nyie wepesi sana kutukana watu lakini dhahiri matendo yenu ndio yale Yesu alisema anajiona msafi awe wa kwanza kurusha jiwe..
      Kwa uhakika hukuyajua yote haya uloyasema pasipo wewe mwenyewe kuwa mshiriki..
      Exploration of reality

    27. #27
      Matola's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 18th October 2010
      Posts : 5,872
      Rep Power : 10399
      Likes Received
      2479
      Likes Given
      1794

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Quote By Kichwa Ngumu View Post
      Ni kiashiria kuwa hafai kuwa kiongozi.heshima na nidhamu haipimwi kwa kuomba msamaha ila mwenye heshima na nidhamu anajizuia kufanya makosa ambayo yatamtaka aombe samahamani.maneno kama haya hatukuyaona wakati wa uongozi wa Mr. 6
      Nasisitiza sioni kosa la spika alichozungumza ndio ukweli wenyewe. anaetaka kuthibisha ukweli huu basi aende sokoni kariakoo, alafu atapata jibu.
      WAFU: Hawa ni maiti wako Hai ila ni mazoba, hata wakiambiwa na CCM walipie PUMZI na USINGIZI watalipia ingawa hawana kitu. Wanakubaliana na kila hali hawajui kupinga wala kukataa, hawana tofauti na mabehewa ya treni kinakokwenda kichwa ndiko wanakokwenda wao.

    28. #28
      Zing's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th June 2009
      Posts : 1,780
      Rep Power : 3128
      Likes Received
      423
      Likes Given
      552

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Quote By Mkandara View Post
      Lakini wana JAMII FORUM isije msimlaumu sana huyu Anna Makinda kwani naye anafuata nyayo za baba yake Mwalimu Nyerere ambaye alianza kupandikiza mbegu mbaya za kudharau not only waswahili lakini wana kariakoo kwa ujumla.

      Unaposema huyu mama anafuata nyayo za Baba yakeMwalimu Nyerere una maana gani? haya ni matusi makubwa na nadhani kuna haja ya wewe kuwaomba wana JF msamaha..



      Nyerere aliwadharau alafu akaruhusu Soko la kariako lijengwe hapo. Ebu jaribu kuonyesha busara zako katika kuandika. Mi nadhani kauli yake sio nzur lakini mnaikuza na kufanya exagaration out of proportion. Mbona tunawaita watu "wamachinga"

      Jamani mbona watu wengine kama wanakuwa sawa a huyo A na makinda. Hili neno sio sahihi lakini siyo la ajabu sana kiasi hicho.
      Last edited by Zing; 14th June 2011 at 22:32.

    29. #29
      Bigirita's Avatar
      JF Premium Member Array
      Join Date : 15th June 2009
      Location : Under a mango tree
      Posts : 8,640
      Rep Power : 2345
      Likes Received
      1583
      Likes Given
      2017

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Quote By Mkandara View Post
      Lakini wana JAMII FORUM isije msimlaumu sana huyu Anna Makinda kwani naye anafuata nyayo za baba yake Mwalimu Nyerere ambaye alianza kupandikiza mbegu mbaya za kudharau not only waswahili lakini wana kariakoo kwa ujumla.

      Unaposema huyu mama anafuata nyayo za Baba yakeMwalimu Nyerere una maana gani? haya ni matusi makubwa na nadhani kuna haja ya wewe kuwaomba wana JF msamaha..


      Mkuu, watu utawajua kwa maneno yatokayo midomoni mwao.

      Swala lilikuwa dogo tu la kumwambia aombe radhi!!
      Sasa matokeo yake hadi mitaa ya kariakoo na nyumba za akina Sykes zimeingizwa kwenye ugomvi.

      Kuna mambo ya kitaifa yanapitishwa bungeni kwa hoja za mdioooo!! lakini hakuna anayekuja kusema kama Sykes and Co wangekuwepo leo na kuona hili!!!
      Yani watu wanaona hoja ni majina ya mitaa tu!!! na historia ambayo hainipunguzii bei ya gas wala petrol!!
      Wakati mwingine unaweza ukatukana mtu!
      aiai654 likes this.
      I'm not being rude. You're just insignificant.

    30. #30
      Masuke's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 28th February 2008
      Posts : 1,031
      Rep Power : 727
      Likes Received
      148
      Likes Given
      47

      Default Re: Jumuiya ya Waswahili Kariakoo wampa onyo Makinda na wenzake

      Mimi nadhan mama spika alimanisha kariakoo kwa maana ya soko, harakati zinazofanyika sokoni, kelele zile, labda angetumia neno msiwe kama watu wa sokoni pengine kusingekuwa na malumbano yote haya, lakini yote kwa yote sioni kosa kubwa kihivyo mpaka watu wanatuletea stori ndefu na kejeli nyingi kwa spika pamoja na baba wa taifa.

    Page 1 of 7 123 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Makinda: Wabunge msiwe kama watu wa Kariakoo!
      By GHOST RYDER in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 45
      Last Post: 20th June 2011, 10:34
    2. Ndiyo Waswahili na Yanayotufanya Tuwe Waswahili??
      By Mkwaruzo in forum Jokes/Utani + Udaku/Gossips
      Replies: 6
      Last Post: 20th May 2011, 15:37
    3. Tetesi: Chadema wampa sumu Zitto ?
      By Mwiba in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 0
      Last Post: 20th December 2010, 19:12
    4. Waswahili wa Uarabuni
      By Boflo in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 24
      Last Post: 5th August 2010, 15:11

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...