Nimevumilia vya kutosha nikidhani kama kuna mtu anayekerwa na fumbuzi wa matatizo ya muungano yaliyotolea kwenye kikao cha pamoja kati ya Mh. Lowassa na Mh. Nahodha.
Kitu kinachonitisha ni kwamba yale mambo waliowaamulia wananchi yatapelekwa bungeni october kwa ajili ya "constitutional reforms".
Kwa upande wangu sikubaliana na ufumbuzi waliofikia kwa 100%
Check this out:
1) mineral and oil exploration be co-opted into the national debate on the future of the political federation.
-debate is good but mineral and oil exploration should not be political.
2)Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) should have an equal number of representatives from either side.
-Equal number kwa vigezo gani? Idadi ya watu? Tuelezene mlivyokuja na hiyo soultion equal number of people.
3)consultant on the distribution of wealth generated through mining and oil extraction be hired to advise the Union government on how it can be shared equitably.
-Please kama ni hivyo na huo muungano hatuutaki. For what?
4)It was decided that 50 per cent of the income would be used to finance the operations of the authority and the other 50 per cent be distributed on the basis of 60 per cent for the Mainland and 40 per cent for Zanzibar.
-Hivi hizo hesabu mnafanyaje? How did you come up with 60%, ardhi, watu,?????
Najua watanzania hawataki kuongelea muungano wakiogopa mizimu ya Mwalimu. Kwa upande wangu kuna mambo mawili tu hapa ambayo yanaweza kuleta ufumbuzi wa kudumu kwanza kuuvunja muungana na Zanzibar ikawa nchi kama ilivyo Kenya na tutaendelea kushirikian nao kama tunavyoshirikiana na Kenya, au Zanzibar uwe mkoa. zanzibar kuna watu wasiozidi 3 mil wakati mkoa wa Dar tu una watu 4 mil. Hapo utajiuliza ni kivitu tugawane nusu kwa nusu?
Kama watu hamtaki kuongela hili sual basi mwezi October linaingia kwenye katiba.
Mkataba wa makubaliano ya kuanzisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar ukisainiwa mwaka 1964.
Mkataba wenyewe (uliosainiwa) umeambatanishwa kama attachment.
Raza kama anataka kugombea 2010 agombee tu, nafasi anayo na sio kuwachanganya wananchi majuukwaani na kufanya kampeni kabla ya wakati. Wakati ukifika basi auze sera zake za Serikali tatu. Kwani kwenye chama si kuna vikao halali? Kwanini wasizungumze kama chama halafu wakawaambia wananchi msimamo wa chama, km. serikali moja, mbili au tatu? Sasa kila mtu kwenye chama hicho hicho anasema la kwake majukwaani...Oh, please, we are fed up with these sentiments.
Kwani kuna muungano au ukoloni uliogubikwa buibui la muungano?, huu muungano unavyoendeshwa si sawa na wakati muingereza alipokuwa na gavana wake tu, kila kitu kinaamuliwa Uingereza kama sasa ilivyokuwa kila kitu kinaamuliwa Tanganyika, hata raisi wetu anateuliwa Dodoma na uchaguzi ni kuziba macho watu tu.
Kuna ubaya gani maalim! ndo muungano huo atii
mbona huzungumzii kero ya wapemba kuzagaa ovyo bara?
zanzibar hawana hela za kujiendesha wenyewe wanaishi kutokana na (kodi na mapato mengine) yatokayo bara.
miaka yote wa bara walikua wanalipia umeme ghali, ili zanzibar watumie bure mbona hawakuwa wanalalamika
kwani hata bara siwanataka hiyo rasilimani mbona ujasema na wao wanaangalia, kutaka iwe yako ni swala jingine na kuangalia ni swala jingingine usichanganye habari.
swala la zanzibar kuangalia rasimali yake sidhani kama ni liatatokea kama wameweza kutoa msamaha wa kodi $19m na wao mapato yao ni $20m.
Mkuu Semilong salam,
Ikiwa maoni yako ni sahihi basi Zanzibar ni mzigo kwa Tanganyika, wakati wenyewe Wazanzibari wanazoza kila kukicha juu ya maswala kadhaa yahusuyo so called MUUNGANO kwanini Wanasiasa wa Tanganyika wanasisitiza KUULINDA muungano huo ambao ni mzigo kwao?????
Vipi Raza, bado hajapata wawekezaji pale Changu Soap? Hizi kelele zake mbona zinazidi kadiri inavyokaribia 2010?
Sidhani kama anaweza kupata muekezaji kiwandani pale. Kwani si unajua wewe kuwa Biashara za Raza ni za kimkukumkuku tu na zinategemea kubebwa sasa zikikosa ni balaa, Changu hapana kitu cha kuvutia muwekezaji.
mimi ndo posti yangu ya kwanza hapa JF.. ila sio mgeni kwasababu ninaweza nikasema I have been much of an observer au sideman.. nimekuwa natembelea sana hii JF lakini nimekuwa na prefer sana kuwa nasoma articles (posts) na comeents za watu, mabishano na najifunza mengi sana.. ckuwawahi kushawishika kucomment hapa au kupost hoja yangu… cjui sababu kuu ni nini lakini maybe tu kujiona bado mbichi katika mambo haya yanayo ongelewa humu.. na kuwacha wazee wazima kwenye uwanja.. wakina Blue ray, yo yo, mwanakijiji, nzi, nkruhma na wengine wengi…..
lakini leo nimeamua na mimi nichangie kidogo baada ya kuguswa na mjadala na maoni ya hapa..
nimesoma comment karibia zote za mpaka sasa…
kitu kimoja nimegundua ni kuna kutupiana sana lawama hapa kati ya pande mbili… pande ya watanzania bara na Tanzania visiwani… kuanzia wanaochangia humu JF hadi viongozi wa siasa.. hii Blame game imechukua sura kubwa… serikali,bunge la pande zote wote wanatupiana lawama.. ILA bado cjajua nikitu gani haswa wanachotupiana lawama… sijajua tatizo haswa nini??? Nahili ndo swali ambalo watu wa humu JF nadhanni ingekuwa vizuri wangejiuliza kabla ya kuanza kushutumiana na kutupiana lawama… tatizo ni nini haswa??? Tukianza na hili swala nadhani tunaweza hata kufikia kijua nani mwenye tatizo.. kwasababu kama kunatatizo lazima kutakuwa na aliyesababishia kama si kilichosababisha..
Nimejaribu kujiuliza sana na mimi hilo swali?? Tatizo nini?? Well cjapata jibu hadi sasa hivi kwasababu kuna sababu nyingi sana ambazo sito zi horodhesha sasa hivi kwasababu nahitaji kuzifanyia uchunguzi.. ila ohja ya haraka haraka tu ninaweza kusema.. nimegundua moja ya tatizo ni VIONGOZI waliopo serikalini na Waliopokea madraka kutoka kwa wale walioanzisha huu muungano..
Na hao hao viongozi wamelifanya tatizo liwe lakisiasa zaidi na kuwapeleka wananchi wa nchi hizi mbili katika matatizo..
Sidhani kama mwanachi wakaida ukimuuliza kwanini unataka muungano atakupa sababu kama ‘muhimu ki uchumi, ulinzi’ …
Mimi ukiniuliza kwanini nataka muungano nitakumbia kwasababu Zanzibar is Tanganyika na Tanganyika is Zanzibar…hiyo haina ubishi.. hizi nchi mbili zina hadhina kubwa ya Mila na tamaduni.. they have so much in common and shared a lot in culture.. Ukizungumzia historia ya Tanganyika, Zanzibar imo na imecheza pati kubwa sana.. ukizungumzia Zanzibar, Tanganyika imo na imecheza pati kubwa sana..
Kwa miaka zaidi ya 100 sasa watu wamekuwa waki move na kuzaliana kati ya hizi inchi mbili kama ni miji miwili… watu wamezaliana na kuanzisha makazi from Tanganyika to ZNZ na from ZNZ to Tanganyika…
Sasa unafikiri hawa watu (wananchi) wanataka kuvunja muungano kweli….?????
Mimi ukiniuliza kwanini nataka muungano nitakumbia kwasababu Zanzibar is Tanganyika na Tanganyika is Zanzibar…hiyo haina ubishi.. hizi nchi mbili zina hadhina kubwa ya Mila na tamaduni.. they have so much in common and shared a lot in culture.. Ukizungumzia historia ya Tanganyika, Zanzibar imo na imecheza pati kubwa sana.. ukizungumzia Zanzibar, Tanganyika imo na imecheza pati kubwa sana..
Kwa miaka zaidi ya 100 sasa watu wamekuwa waki move na kuzaliana kati ya hizi inchi mbili kama ni miji miwili… watu wamezaliana na kuanzisha makazi from Tanganyika to ZNZ na from ZNZ to Tanganyika…
Sasa unafikiri hawa watu(wananchi) wanataka kuvunja muungano kweli….?????
Unayozungumza hasa katika sehemu hii mimi kwa mawazo yangu nafikiri ni sahihi. Na nafikiri umefika wakati Katika Katiba na sheria zetu tukasema bayana kuwa Nchi yetu ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na inabakikia kuwa hivyo daima na milele. sasa hapo hakuna tena nafasi ya kulumbuna kama Muungano upo au la.
Kuna mfano wa Marekani wamesema hivyo kikatiba na iko hivyo. Na kule hakuna aliye hodari tena wa kuleta hoja ya kuhoji kwa nini kumekuwepo na United States of America. Kuhusu ni namna gani Muungano wetu uwe nafikiri tusingekuwa tunatawaliwa na hamasa za kutaka uwe kama vile tunavyotamani uwe.
Lakini tungeuwacha ukaendelea kuchukuliwa na mkondo asilia- ukanyumburuka kwa minajil ya hali ya maisha na mazingira yanavyokwenda.
Mathalan hivi sasa ni vigumu kusema kuwa unataka Serikali moja na uongozi wa himaya moja. Hili ni jambo linaloweza kuja wenyewe kwa kufuata mnyumburuko asilia, huko mbele, si la kulichukulia nguvu kama tunavyotamani iwe.
Unapolitaka kwa nguvu ndipo pale inapotokea nguvu ya pili (counter forces) ya kuvutia kwa nyuma na kutoa kauli ya kutaka kujitenga.
*Wadai Pinda, Nohodha hawana mamlaka kujadili kero
*Wataka mkataba wake sasa ujadiliwe bungeni
*Wahoji kufutwa Serikali ya Tanganyika
*Serikali yasema wenye Tanganyika walishakufa
*Spika Sitta amtimua John Cheyo bungeni
Na John Daniel, Dodoma
KATIKA hali isiyotarajiwa wabunge wote wa Zanzibar (wa Chama Cha Mapinduzi -CCM na Chama cha Wananchi-CUF),jana waliungana kuushambulia Muungano huku wakidai kuwa Waziri Mkuu Bw.Mizengo Pinda na Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar(SMZ) Bw. Shamsi Vuia Nahodha hawana mamlaka kujadili kero za Muungano huo.
Akichangia hotuba ya bajeti ya Ofisi ya Makamu wa Rais iliyowasilishwa bungeni jana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Dkt. Batilda Burian, Mbunge wa Chwaka Bw. Yahya Kassim Issa (CCM), alisema Tanzania Bara inawanyonya na kuwarudisha nyuma Wazanzibar katika nyanja mbalimbai ikiwemo elimu na biashara.
“Wenzetu (Watanzania Bara) mnatuwekea vikwazo, bandari ya Zanzibar imekufa, watu walikuwa wanachukua vitu kwenda na kurudi lakini sasa hakuna, vikwazo wanavyowekewa ni matatizo, leteni vitu vya kiuchumi vitakavyosaidia Zanzibar ,hatutaki kusikia hadithi.
“Mafuta ni haki ya Zanzibar, sisi hatujaomba, sisi tulikuwa nchi kamili kama ilivyokuwa Tanzania Bara, mtu akikukanyaga ukanyamaza hatajua amekukanyaga, sisi Wazanzibari tunashindwa kujizuia kuhusu mambo ya Muungano,” alisema Bw. Issa na kusisitiza kuwa mwaka 2011 watakaporudi bungeni, hawataelewa mambo yakienda mrama.
Kwa upande wake msemaji wa Kambi ya Upinzani katika masuala ya Muungano Mbunge wa Viti Maalum Bi. Riziki Omar Juma, (CUF), alilitaka Bunge kuiagiza Serikali kuvunja haraka mazungunzo kati ya Waziri Mkuu, Bw. Pinda na Waziri Kiongozi Bw. Nahodha na kuwasilisha Mkataba wa Muungano bungeni ili ujadiliwe kwa lengo la kumaliza matatizo yaliyopo.
“Hatuoni kwamba vikao hivi vya pamoja (Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano na waziri Kiongozi wa SMZ ) vinakuja na suluhisho la tatizo la Muungano, vyenyewe ni sehemu ya tatizo, ili kutimiza wajibu wetu kama Bunge la watu lenye jukumu la kusimamia matumizi ya fedha za walipa kodi, liitake Serikali ya Muungano isitishe mara moja vikao hivi, badala yake Mkataba wa Muungano uletwe hapa bungeni kama nukta kuu ya mjadala, hapo ndipo tuanzie na tumalizie kero za Muungano.
“Ofisi ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi hazina uwezo wa kujadili Muungano, hapa ni kizungumkuti kinachofanyika. Katika Mkataba wa Muungano, hakuna sehemu inayosema kufutwa kwa Serikali ya Tanganyika,”alisema Bi. Juma.
Alisema Kambi ya Upinzania inaona kazi inayofanywa sasa na Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi kujadili Muungano, ni kama sehemu ya kuongeza kero kwa kuwa ajenda kuu wanayoina ni ukiukwaji wa Mkataba wa Muungano hivyo kero zinazojadiliwa ni matokeo ya tatizo na si tatizo lenyewe.
“Watanznzania waniwie radhi kusema kwamba wakubwa wetu wameufanya Muungano huu ushabihiane sana na kile kisa cha Mfalme Jeta aliyemo kwenye riwaya ya Kusadikika akiwa amekaa katika eneo ambapo mto uliokuwa unakokozoa kila kitu, mawe, magogo, majengo, unatiririka kinywani na kuishia tumboni, lakini mara alisikika akilia 'njaa !njaa!' kiu!kiu!”alisema Bi. Juma.
Alisema katika suala la Muungano hakuna mkubwa wala mdogo na kusisitiza kuwa nchi zilizoungana zilikuwa nchi kamili na suala la udongo halipaswi kuwepo na kuongeza kwamba Serikali ya Muungano ndio inayopaswa kubeba lawama kuhusu Muungano.
Alidai kuwa mazungumzo yanayofanywa kati ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi ni sawa na watu wanaokutana kunywa kahawa au chai na si kufanya jambo la maana.
Naye Mbunge wa Mkanyageni, Bw. Mohamed Habib Mnyaa (CUF),alisema timu ya Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi hazitoshi kujadili suala la Muungano kwani linawagusa Watanzania wengi hivyo lilipaswa kushirikisha nyanja mbalimbali.
Bw. Mnyaa alikwenda mbali zaidi na kutoa mfano wa swali la mwanawe kuhoji uhalali wa kiongozi mmoja (marehemu Mwalimu Julius Nyerere) kuonekana akichanganya udongo peke yake,jambo linalotia dosari kwenye misingi ya Muungano humo.
Bw.Mnyaa alisema tangu mwaka 1990 hadi 2000 zimeundwa tume 12 kushughulikia matatizo ya Muungano lakini hadi sasa hakuna muafaka uliopatikana.
Hivi karibuni Serikali iliweka wazi mambo matatu yaliyopatikana kupitia mazungumo kati Waziri Mkuu na Waziri Kiongozi kuwa ni pamoja na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Uvuvi katika bahari kuu na shughuli za biashara ya meli.
Katika Hotuba yake, Dkt. Burian alisema Serikali imepiga hatua katika mazungumzo kati ya viongozi hao wawili na kueleza kwamba vikao hivyo vitaendelea kwa kasi zaidi ili kuboresha Muungano.
Akijibu hoja hizo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Bw.Muhammed Seif Khatib alisema suala la Serikali ya Tanganyika kwa sasa halina nafasi kwani wenye Tanganyika walishakufa.
Alisema wakati wa Muungano Tanzania ilikuwa na watu milioni 10 tu na sasa wapo zaidi ya milioni 40.
Alisisitiza kuwa Waziri Mkuu na Waziri kiongozi wana uhalali kujadili kero za Muungano kwani mwenyekiti suala hilo ni Makamu wa Rais.
Source: Majira
__________________ "Ask not what your country can do for you, ask what you can do for your country"-JFK.
ukweli mficha maradhi kifo kitamuumbua huu ni wakati muafaka kuweka kila kitu wazi
au mnasubiri mpaka waasisi wote wafariki halafu wajukuu zetu watumbuane macho?
nnaamini upeo na uelewa watanzania uko juu wajuulishwe na wafahamishwe nn kilitokea na washirikishwe ktk maamuzi hapana cha kuogopwa juu ya hilo
__________________ Our job is not to make up anybody's mind, but to open minds and to make the agony of the decision-making so intense you can escape only by thinking. ~Author Unknown