Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania? (Huyu SI LOWASSA)

    Report Post
    Page 1 of 4 123 ... LastLast
    Results 1 to 20 of 64
    1. #1
      Fake Lowassa's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 5th June 2011
      Posts : 3
      Rep Power : 0
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania? (Huyu SI LOWASSA)

      Ndugu zangu,
      Sikutaka kabisa kushiriki katika hii mitandao ya kijamii ambayo mimi niliiona kama ni ya kihuni, lakini nimegundua kwamba kuna vitu vya msingi sana ambavyo huwa vinajadiliwa humu na hii imenifanya niamue kushirikii.

      Nimesoma michango yenu mingi sana humu, kimsingi michango mingi imejaa chuki dhidi yangu na wenzangu, huwa nashindwa kuelewa sababu hasa ya kunichukia kiasi hiki. Sitaki Malumbano na yeyote, lakini sipendi pia muendelee kuendesha propaganda za kunichafua.

      Kuna watu ambao watahakikisha napotea kisiasa, sijui ni kwa maslahi ya nani, najua sababu ni kwamba na wala sijisifu, mimi ni kati ya watu ambao pamoja na matatizo ya kibinadamu niliyonayo, nina uwezo mkubwa wa kuliongoza taifa hili na hii inanifanya nionekane tishio kwa wale wote ambao wanataka kuliongoza hili taifa. Mimi sina nia ya kuwa rais wa Tanzania kwa vyovyote vile lakini ningependa kuwaongoza watanzania iwapo wananchi wangependa iwe hivyo.

      Kuhusu hizi shutuma ninazopewa, nadhani ni uonevu tu kwa kuwa hakuna hata mmoja wa wale wanaonishutumu ambaye ana ushahidi wa moja kwa moja kwamba mimi nilishiriki katika kuihujumu nchi, na kwa uzalendo wangu niliamua kuuacha uwaziri mkuu, sijui watanzania wanataka nifanye nini. Najua kama binadamu nina mapungufu yangu na kila mtu anayo lakini hiki kisiwe kigezo cha kuyaacha mazuri yote niliyoifanyia nchi hii na kunisakama, kunitushi na kunidhalilisha kwa kila njia.

      Naomba watanzania mnielewe kuhusu Richmond nilifanya kwa nia njema lakini bahati mbaya na kwa makosa ya kibinadamu kampuni ile ikawa feki, ni nilikubali kubeba lawama kwa kujiuzulu. Watanzania kosa langu ni nini hasa? Nihukumuni kwa haki tafadhali sio kwa propaganda.

      Ya CCM na dhana ya kuendelea kuchafuana ya magamba nitaileza siku nyingine. Naomba leo niishie hapa, nitaendelea kueleza ukweli wangu popote nitakapopata fursa ikiwa ni pamoja na kupitia mitandao hii ya kijamii.


    2. #2
      Speaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th August 2010
      Posts : 6,178
      Rep Power : 4565
      Likes Received
      2003
      Likes Given
      5096

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Mheshimiwa EL,...
      kwanza nakupongeza kwa kujitokeza Jamii Forums,hilo peke yake
      kwangu ni ujasiri wa ajabu,nimefurahi sana na ghafla kukuona JF,...!
      Karibu sana!

      Kwa upande wa kusema hutaki malumbano JF mheshimiwa kwa hilo pole sana
      naomba uwe tayari kuyapokea na kuya-punch malumbano yote!

      Jamii Forums ni kipimo cha uvumilivu wako!
      Uta kebehiwa,uta fanyiwa kila kitu,ila mwisho wa siku watu watataka kujua
      wewe ni nani (the inside of you)!!
      Mjinga mpe cheo...

    3. #3
      Balantanda's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th July 2008
      Location : Kusadikika
      Posts : 9,040
      Rep Power : 7163
      Likes Received
      1765
      Likes Given
      1412

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Mmmmmhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh.. .....

      Tutafika tu....
      "Tukosoane, turekebishane, tuwajibishane ndipo tusameheane" Regia Mtema.

    4. #4
      Brutus's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th July 2007
      Location : Rome
      Posts : 212
      Rep Power : 653
      Likes Received
      18
      Likes Given
      91

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Si mchezo.. Karibu sana Ukumbini!!!!!
      Et tu, Brute?

    5. #5
      Limbani's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th April 2008
      Location : Kisiwani
      Posts : 1,233
      Rep Power : 824
      Likes Received
      261
      Likes Given
      63

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Mhe Lowassa,
      Nimefarijika kukuona kwenye huu mtandao na hayo maelezo yako. Kweli unashutumiwa na mambo mengi na kama unavyokiri mwenyewe wewe ndio gamba ambalo CCM wanataka kulivua pamoja na wenzako Chenge na Rostam. Binafsi, nilikuwa napenda sana staili yako ya utendaji kazi kama kiongozi (Ukiwa Waziri Mkuu) ingawa mimi si mwananchama wala mpenzi wa CCM.
      Pole sana kwa shutuma nyingi lakini nadhani umefika muda sasa wa kusikia the other side of the story kutoka kwako pengine pamoja na wenzako.

      Ahsante.
      Speaker and Simbaa like this.
      amidst the mists and coldest frost, he thrust his fists against the posts, and still insists he sees the ghosts...


    6. #6
      ngwini's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th April 2011
      Posts : 445
      Rep Power : 505
      Likes Received
      67
      Likes Given
      0

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Mr.Lowassa karibu sana JF...na mimi swali langu kwangu ni kwann mnatajwa nyie watatu 2 kuhusu ufisadi? Je ni kweli wewe ni fisadi?

    7. #7
      mwanaharakat's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2011
      Posts : 406
      Rep Power : 500
      Likes Received
      70
      Likes Given
      0

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Huna nia ya kuwa rais wa tz kwa vyovyote vile lkn ungependa kuwaongoza watz kama wangependa iwe hivyo! what do u mean can u elaborate? yaan watz wamchague mtu asiyekuwa na nia ya urais, si utatuburuza unavyotaka wewe mkuu coz tumekutaka wenyewe pasipokuwa na ridhaa yako.
      Kuna mazuri umefanya tz hii, yapi hebu yaweke hapa jamvin ili tucompare na mabaya yako.
      Speaker likes this.

    8. #8
      kapotolo's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 19th September 2010
      Location : Tanzania
      Posts : 2,439
      Rep Power : 1205
      Likes Received
      1289
      Likes Given
      397

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Muheshimiwa Karibu sana, hata mimi naamini una uwezo kuliko JK, jitahidi kujisafisha unaweza ukafanikiwa.
      Speaker and Simbaa like this.
      Kiongozi shupavu hawezi kutumia mabavu kuongoza, ni kiongozi dhaifu tu ndio atatumia mabavu kuficha udhaifu wake - Jenerali Ulimwengu

    9. #9
      rosemarie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 4,742
      Rep Power : 1372
      Likes Received
      285
      Likes Given
      143

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      mweshimiwa edward lowassa nafikiri ni jambo jema sana kujitokeza hapa,nakuhakikishia watanzania wote wanakuheshimu sana!!kuna baadhi ya watu ndani ya chama chako wanajitahidi sana kukumaliza!!!neno moja nataka ujue sisi watanzania tunaangalia kwa makini hatma ya hii vita!!lakini najua utatoka mshindi!!mwisho tunakutaka uwe rais wetu 2015!!thats all!
      ccm inakufa,asante mungu umesikia kilio chetu!!!!!!!

    10. #10
      Moseley's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th July 2010
      Posts : 163
      Rep Power : 490
      Likes Received
      37
      Likes Given
      54

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Quote By Edward Lowassa View Post
      Ndugu zangu,
      Sikutaka kabisa kushiriki katika hii mitandao ya kijamii ambayo mimi niliiona kama ni ya kihuni, lakini nimegundua kwamba kuna vitu vya msingi sana ambavyo huwa vinajadiliwa humu na hii imenifanya niamue kushirikii.

      Nimesoma michango yenu mingi sana humu, kimsingi michango mingi imejaa chuki dhidi yangu na wenzangu, huwa nashindwa kuelewa sababu hasa ya kunichukia kiasi hiki. Sitaki Malumbano na yeyote, lakini sipendi pia muendelee kuendesha propaganda za kunichafua.

      Kuna watu ambao watahakikisha napotea kisiasa, sijui ni kwa maslahi ya nani, najua sababu ni kwamba na wala sijisifu, mimi ni kati ya watu ambao pamoja na matatizo ya kibinadamu niliyonayo, nina uwezo mkubwa wa kuliongoza taifa hili na hii inanifanya nionekane tishio kwa wale wote ambao wanataka kuliongoza hili taifa. Mimi sina nia ya kuwa rais wa Tanzania kwa vyovyote vile lakini ningependa kuwaongoza watanzania iwapo wananchi wangependa iwe hivyo.

      Kuhusu hizi shutuma ninazopewa, nadhani ni uonevu tu kwa kuwa hakuna hata mmoja wa wale wanaonishutumu ambaye ana ushahidi wa moja kwa moja kwamba mimi nilishiriki katika kuihujumu nchi, na kwa uzalendo wangu niliamua kuuacha uwaziri mkuu, sijui watanzania wanataka nifanye nini. Najua kama binadamu nina mapungufu yangu na kila mtu anayo lakini hiki kisiwe kigezo cha kuyaacha mazuri yote niliyoifanyia nchi hii na kunisakama, kunitushi na kunidhalilisha kwa kila njia.

      Naomba watanzania mnielewe kuhusu Richmond nilifanya kwa nia njema lakini bahati mbaya na kwa makosa ya kibinadamu kampuni ile ikawa feki, ni nilikubali kubeba lawama kwa kujiuzulu. Watanzania kosa langu ni nini hasa? Nihukumuni kwa haki tafadhali sio kwa propaganda.

      Ya CCM na dhana ya kuendelea kuchafuana ya magamba nitaileza siku nyingine. Naomba leo niishie hapa, nitaendelea kueleza ukweli wangu popote nitakapopata fursa ikiwa ni pamoja na kupitia mitandao hii ya kijamii.
      Provided wewe ni Lowasa kweli::

      Kwanza karibu jukwaani mheshimiwa!!

      Kuna mambo mengi yameelekezwa kwako kama mmoja wa watu waliohujumu taifa hili.. Yamesemwa mengi, kwa hiyo sisi kama wananchi tunataka kujua tatizo liko wapi hasa.. Kwa ujumla chama chako, kimekumbwa na kashfa za matumizi mabaya ya raslimali za umma..


      Na kikao kilichokaa cha NEC kikawa-point ninyi kama ndo chanzo cha matatizo hayo..


      Wewe kama Mbunge, uliewahi kuwa waziri mkuu, na mwenye uelewa wa mambo mengi ya CCM na serikali, tunaomba basi ututhibitishie, tatizo hasa liko wapi, na ni nani wanaolihujumu taifa.. Vinginevyo sisi kama wananchi tutaendelea kuamini kuwa wewe ni mmoja wa walioliltea matatizo taifa hili..


      Ndugu Mheshimiwa, haingii akilini nchi yetu yenye raslimali nyingi kiasi hiki watu bado ni maskini.. Wakati huo huo viongozi wengi wa CCM wanaishi maisha ya anasa kwa kutumia hovyo mali za umma..


      Kwa nafasi yako, tunaomba basi utujulishe, tatizo hasa ni nini mpaka nchi inaendelea kuwa maskini.. Vinginevyo tutaendelea kuamini kua wewe ni mmoja wa viongozi walioliletea matatizo taifa hili..


      Jaribu kujibu hoja zinazoelekezwa kwako moja baada ya nyingine..
      Speaker and engmtolera like this.

    11. #11
      Tina's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th July 2007
      Posts : 349
      Rep Power : 680
      Likes Received
      269
      Likes Given
      12

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Ama kweli UVCCM Arusha mumeamua kumbeba baba yenu. Kwa kifupi tokea Mwalimu Nyerere akukatae umekua kama una laana. Kabla sijaanza kumwaga data ambazo hazijawahi kusikika popote ikiwa ile ya kumtuma UAE Naibu Gavana,ushirikiano wako na Wasomali na safari zote za Geneva, fafanua uliposema umeshiriki Richmond.

    12. #12
      TIMING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th April 2008
      Location : Roaming...
      Posts : 20,208
      Rep Power : 12280
      Likes Received
      6065
      Likes Given
      6929

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Quote By Edward Lowassa View Post
      Ndugu zangu,
      Sikutaka kabisa kushiriki katika hii mitandao ya kijamii ambayo mimi niliiona kama ni ya kihuni, lakini nimegundua kwamba kuna vitu vya msingi sana ambavyo huwa vinajadiliwa humu na hii imenifanya niamue kushirikii.
      karibu sana mkuu, ni huu huu uhuni ndio ulioleta mabadiliko nchi za uarabuni na vuguvugu lake linazidi kuendelea hasa kutokana na simu za kisasa kutupa access zaidi.

      Quote By Edward Lowassa View Post
      Nimesoma michango yenu mingi sana humu, kimsingi michango mingi imejaa chuki dhidi yangu na wenzangu, huwa nashindwa kuelewa sababu hasa ya kunichukia kiasi hiki. Sitaki Malumbano na yeyote, lakini sipendi pia muendelee kuendesha propaganda za kunichafua.
      hapo kwenye red mkuu ndipo ulipoanza vibaya, kwanza umesema hutaki malumbano na mtu yoyote, in JF hilo haliepukiki, kwani huku hakuna bosi wala mkuu, lakini la pili ni generalization yako... you have just fallen to the same problem.... at least ungesema baadhi ya members, kwani nafahamu kuna threads humu ziliwahi kukupamba sana tu!
      Quote By Edward Lowassa View Post
      Kuna watu ambao watahakikisha napotea kisiasa, sijui ni kwa maslahi ya nani, najua sababu ni kwamba na wala sijisifu, mimi ni kati ya watu ambao pamoja na matatizo ya kibinadamu niliyonayo, nina uwezo mkubwa wa kuliongoza taifa hili na hii inanifanya nionekane tishio kwa wale wote ambao wanataka kuliongoza hili taifa. Mimi sina nia ya kuwa rais wa Tanzania kwa vyovyote vile lakini ningependa kuwaongoza watanzania iwapo wananchi wangependa iwe hivyo.
      hapa sasa mkuu umechemka... Hivi wewe tangu uzaliwe hujawahi kutamani kumpoteza mtu kisiasa kweli?? i doubt, hivi wewe sio tishio kweli? i doubt, unasema huna nia ya kuwa rais lakini at the same time unasema ungependa kuwaongoza watanzania... HOW?

      Quote By Edward Lowassa View Post
      Kuhusu hizi shutuma ninazopewa, nadhani ni uonevu tu kwa kuwa hakuna hata mmoja wa wale wanaonishutumu ambaye ana ushahidi wa moja kwa moja kwamba mimi nilishiriki katika kuihujumu nchi, na kwa uzalendo wangu niliamua kuuacha uwaziri mkuu, sijui watanzania wanataka nifanye nini. Najua kama binadamu nina mapungufu yangu na kila mtu anayo lakini hiki kisiwe kigezo cha kuyaacha mazuri yote niliyoifanyia nchi hii na kunisakama, kunitushi na kunidhalilisha kwa kila njia.


      Quote By Edward Lowassa View Post
      Naomba watanzania mnielewe kuhusu Richmond nilifanya kwa nia njema lakini bahati mbaya na kwa makosa ya kibinadamu kampuni ile ikawa feki, ni nilikubali kubeba lawama kwa kujiuzulu. Watanzania kosa langu ni nini hasa? Nihukumuni kwa haki tafadhali sio kwa propaganda.
      ulifanya nini tena mkuu?

      Quote By Edward Lowassa View Post
      Ya CCM na dhana ya kuendelea kuchafuana ya magamba nitaileza siku nyingine. Naomba leo niishie hapa, nitaendelea kueleza ukweli wangu popote nitakapopata fursa ikiwa ni pamoja na kupitia mitandao hii ya kijamii.
      hayo ya kuchafuana si mlianza wenyewe tangu enzi zile za hizbo au ??
      ....Time is the wisest counselor !!!

    13. #13
      Kitty Galore's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th May 2011
      Posts : 336
      Rep Power : 476
      Likes Received
      84
      Likes Given
      39

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      mkuu una kazi kubwa na ngumu sana mbele yako, kutufanya watanzania tukuone msafi na usie na mawaa ni kazi kubwa sana, hii inatokana na chama chako cha magamba kutujengea dhana watanzania tuwaone kuwa nyie ndio mnaorudisha nyuma na kutufanya tuishi katika umaskini mkubwa katika nchi yetu yenye utajiri uliotukuka. Leo umeweza kutueleza yaliyoko moyoni mwako sisi tulio na uwezo wa kupata internet na kuingia JF Je yule mtanzania aliyeko kijijini ambaye hajui hata mchana wa leo atakula nini utamuambiaje? Kiufupi hapo mlipofikia panatosha na kwa sasa watanzania tunahitaji mabadiliko, tunataka tupate viongozi wengine wenye uchungu na nchi yao na sio nyie mliojilimbikizia mali na kufikiria matumbo yenu tu.
      Samahani kama nitakuwa nimekukwaza ila na mimi ni mmoja wa wananchi wenye uchungu na nchi yao tusiopenda mafisadi kama nyie
      Speaker and afrodenzi like this.

    14. #14
      graceirene's Avatar
      Member Array
      Join Date : 26th May 2011
      Posts : 24
      Rep Power : 412
      Likes Received
      4
      Likes Given
      0

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      hongera kwa kuamua kujitokeza na walau itatupa fafanuzi za kina kuhusu hizo unazodai kuwa shutuma na propanda zinazoelekezwa kwako kwa lengo la kukuchafua.
      Karibu mbunge wa monduli

    15. #15
      mwacheni77's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 519
      Rep Power : 522
      Likes Received
      63
      Likes Given
      0

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Pole sana muheshimiwa omba sana mungu lakini ukumbuke mungu wako ww ndio wetu ss watanzania,ukweli wa kila kitu kama unaonewa au kucngiziwa unaujua ww na upo moyoni mwako,hata watanzania wameona utendaji wako uliotukuka ulikuwa na lengo zuri tu la kujenga shule za kata,na hii ilikuwa na maana ya quality education for the people of quality ss watanzania wa hali duni tuendelee kuwa na elimu duni tunashukuru kwa hili

    16. #16
      Mawenzi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st September 2010
      Posts : 714
      Rep Power : 586
      Likes Received
      144
      Likes Given
      820

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      EL, can you tell us how wealthy you are? Can you account for all your wealth?? Mradi umejitokeza humu, tafadhali jaribu kujibu maswali yetu

    17. #17
      Fake Lowassa's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 5th June 2011
      Posts : 3
      Rep Power : 0
      Likes Received
      13
      Likes Given
      0

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Quote By ngwini View Post
      Mr.Lowassa karibu sana JF...na mimi swali langu kwangu ni kwann mnatajwa nyie watatu 2 kuhusu ufisadi? Je ni kweli wewe ni fisadi?
      Kama umesoma vizuri hapo juu, nimeeleza mengi, lakini kubwa nchi yetu imeingia katika siasa mbaya sana ya kuchafuana. Nakiri nina ukaribu na Mhe Chenge na Rostam na labda hii ndio sababu mmoja wetu akiwa na kashfa wote tunaingizwa humo. Lakini kama nilivyoeleza mwanzo, mimi ni kati ya watu tishio wa urais na hivyo lazima nitafanyiwa mizengwe. Ufisadi sijui nimeufanya wapi mimi, naamini mimi ni mtu safi, nina mali lakini zote naweza kuaccount nimezipata vipi, si kwa hila, za halali na Mungu wangu ndie anajua.
      Speaker, Pena and 'TF' like this.

    18. #18
      Mzalendo80's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th October 2010
      Location : Magogoni, Tanganyika
      Posts : 2,280
      Rep Power : 964
      Likes Received
      822
      Likes Given
      1589

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Karibu Mheshimiwa katika JF, Mengi tumeyasikia kuhusu wewe lakini tunashindwa kujua kulikoni, ingekuwa vizuri sana kama tungepata your side story kuhusu mambo ya Richimond, EPA na habari nyingine ili Watanzania tuwezekujua ukweli na kuchagua pumba na mchele.
      The CCM is a crime syndicate, Most members and MPs of CCM are corrupt. No conceince, No brains no nothing, just bunches of criminal and theft. Corruption cost mlalahoi in de street.

    19. #19
      rosemarie's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 4,742
      Rep Power : 1372
      Likes Received
      285
      Likes Given
      143

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      Quote By edward lowassa View Post
      kama umesoma vizuri hapo juu, nimeeleza mengi, lakini kubwa nchi yetu imeingia katika siasa mbaya sana ya kuchafuana. Nakiri nina ukaribu na mhe chenge na rostam na labda hii ndio sababu mmoja wetu akiwa na kashfa wote tunaingizwa humo. Lakini kama nilivyoeleza mwanzo, mimi ni kati ya watu tishio wa urais na hivyo lazima nitafanyiwa mizengwe. Ufisadi sijui nimeufanya wapi mimi, naamini mimi ni mtu safi, nina mali lakini zote naweza kuaccount nimezipata vipi, si kwa hila, za halali na mungu wangu ndie anajua.
      mweshimiwa naomba tuhakikishie kama kweli ni real edward lowassa
      LAT likes this.
      ccm inakufa,asante mungu umesikia kilio chetu!!!!!!!

    20. #20
      Magogwajr's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 16th November 2010
      Location : Behind u
      Posts : 221
      Rep Power : 484
      Likes Received
      20
      Likes Given
      15

      Default Re: Edward Lowassa Nimewakosea nini Watanzania?

      napata tabu sana kuamini kama ni wewe au kuna mtu ameingia kwa jina lako but kama ni wewe tutafahamu tu hasa kupitia majibu yako...

      karibu sana jamii forums mheshimiwa..... wewe ni miongoni mwa watu ambao jamii ina sintofahamu nyingi kuhusu kashfa, maisha na mustakabali mzima wa matumizi ya rasilimali za nchii hii. kujiunga kwako jamii forums kutatoa fursa ya kupata majibu ya maswali yote na naomba uwe mvumilivu tu kwa michango yote na maswali utakayo ulizwa kwa sababu watu humu jamvini hatupo kusifiana kama facebook na mitandao mingine.

      pili naomba majibu yawe yanatoka direct kwako na si kwa msemaji wako au secretary or anybody else. me kwa sasa hv ni hayo tu ntaruci badae kuanza kutoa duku duku langu...

    Page 1 of 4 123 ... LastLast

    Similar Topics

    1. Mazuri ya Edward Lowassa
      By quarz in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 201
      Last Post: 1st October 2012, 10:10
    2. Mh. Edward Ngoyayi Lowassa: Acha kucheza na akili za Watanzania
      By apolycaripto in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 85
      Last Post: 9th December 2011, 08:02
    3. Mhe: Edward ngoyai lowassa
      By Meitinyiku L. Robinson in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 16
      Last Post: 26th November 2011, 16:19
    4. In Edward Lowassa, I trust...
      By Rev. Kishoka in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 416
      Last Post: 12th February 2010, 19:46

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...