Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

    Report Post
    Page 4 of 4 FirstFirst ... 234
    Results 61 to 78 of 78
    1. #1
      nngu007's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 2nd August 2010
      Posts : 11,173
      Rep Power : 3548
      Likes Received
      3043
      Likes Given
      460

      Default Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      *Nikiangalia Picha za Mikutano ya Chadema, Naona Umati Mkubwa wa watu na sioni T-Shirt za Chadema, Khanga n.k kama picha chini zinavyoonyesha, Umati mdogo wa watu inaonyesha wamepewa asante...

      2011

      NAPE ATAMBA KUMUUMBUA DK. SLAA KESHO SINGIDA



      KATIBU wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) CCM, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye amesema leo atamwaga hadharani jinsi Katibu Mkuu wa Chadema Dk. Wilbrod Slaa anavyofanya ufisadi wa kutisha ndani ya chama hicho.

      Nape alisema ataeleza ufusadi huo, katika mkutano wa hadhara utakaofanyika kwenye Stendi Kuu ya Mabasi mjini Singida mjini, ukiwa ni mkutano wa pili, katika ziara ya viongozi wa Sektretarieti ya Halimashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM waliyoianza jana mkoani hapa.

      Akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya jengo la Ushirika Ikungi nje ya mji wa Singida, Nape alisema, anazo nyaraka zinazoonyesha Dk. Slaa na baadhi ya viongozi wa Chadema wanavyojinufaaisha na fedha za chama hicho huku wanachama wenyewe wakiendelea kumpigia makofi.

      Katika ziara hiyo ya kujitambulisha msafara wa Sekretarieti hiyo ya CCM, unaoongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM (Bara) Kapteni Mstaafu, John Chiligati Nape amefuatana pia na Katibu wa Uchumi na Fedha, Mchumi Mwigulu Nchemba na Katibu wa Oganaizesheni Asha Juma Abdallah.

      Katika mikutano iliyofanyika jana, Ikungi na Ligwa, Nape alikanusha vikali kuwepo wa waraka wa siri wa Sekretarieti mpya ya CCM ambao Dk. Slaa anadai kuwa nao.

      Amesema, kwa kujitapa kwenye majukwaa juzi mjini Sumbawanga, kwamba anazo nyaraka za siri za Sekretarieti hiyo, kwanza inadhimhirisha kwamba hajui nini maana ya siri na dhahiri.

      Nape alisema, anachokiita Dk. Slaa kuwa siri ni udhanifu wa kupuuzwa kwa sababu yote yaliyoainishwa kwa ajili ya kutekelezwa na sekretarieti ya CCM baada ya kikao cha mjini Dodoma, hakuna hata moja ambalo ni siri hadi sasa.

      Alisema, baada tu ya sekretarieti kukabidhiwa mikoba, imefanya mikutano ya hadhara zaidi ya kumi katika mikoa mbalimbali na kuelezwa kwa kinaga ubaga nini hasa kilichotokea Dodoma hadi kupatikana kwa sekretarieti mpya.

      Nape alisema, pamoja na mambo kadhaa wamekuwa wakieleza wazi kwamba kilichofanyika ni CCM kujifanyia tathmini kuona kama kweli hali ilimo sasa na inatosha kuipigisha hatua ya kuongoza sasa na baadaye.

      Alisema, baada ya tathmini hiyo, kama chama komavu kiliyakubali mapungufu kiliyobaini na kuamua kwamba ili kuondokana na mapungufu yaliyobainika, lazima uongozi wa juu uliopo uwajibike, jambo ambalo hakuna chama kingine kinachoeweza kuthubu kikabaki salama.

      "Jamani tilichofanya Dodoma ni kuwasha Mwenge kwa ajili ya kuongeza matumaini pale yalipoanza kufifia, kuongeza imani kwa chama pale ilipoanza kudorora, jambo ambalo kwa chama chenye umri mkubwa kama CCM lilikuwa la lazima", alisema Nape.

      Akifafanua zaidi kuhusu suala hilo, Chiligati alisema, anachodai kuwa nacho Dk. Slaa na kukiona kuwa ni waraka wa siri, kama kweli anacho ni gamba ililotupa CCM ambalo linamyima usingizi.

      Chiligati alisema, kwa kawaida kitu kinapokuwepo muda mrefu sana kisipojitazama upya kuendelea kuwepo kuwa kwa mashaka makubwa, na ndiyo maana CCM imeona umuhimu wa kujitathmini na kuamua bila kusita kujivua gamba.

      Alifafanua kwamba, gamba ililojivua CCM si ngozi ila ni yale matendo maovu ambayo baadhi ya viongozi walianza kuyakumbatia kama ufisadi, na kutokifanyaa chama kuwa cha wanachama badala yake kuonekana cha wenye fedha.

      Chiligati alisema, kimsingi ufisadi na hali hiyo ya kutokifanya chama kuwa cha wanachama ndilo gamba lililovuliwa toka CCM amabalo sasa Dk. Slaa anataka kutamaba nalo wakati CCM walishaachana nalo tangu mkutano ule mzito wa Dodoma.

      Kwa upande wake, Nchemba alisema, kwa kujivua gamba sasa CCM ni mpya, wale waliokuwa wamekimbia kutokana na kero za baadhi ya viongozi, sasa warejee kwa sababu yale hayawezi kujirudia tena.

      Alisema, sasa CCM ni itaendesha mambo yake kisasa na kisayansi zaidi kuliko ubabaishaji, amkbapo mali na miradi ya chama popote ilipo haitaweza kutafunwa na mbadhirifu yeyote bali rasilimali hizo zitakuwa kwa manufaa ya wanachama wote.

      Miongoni mwa viongozi wa Sekretarieti hiyo mpya ambao hawapo kwenye ziara hiyo mkoani Singida ni Katibu Mkuu wa CCM, Wilson Mukama ambaye ana majukumu mengine.

      Posted by: Bashir Nkoromo at Tuesday, May 10, 2011 0 Comments





      ZIARA YA NAPE, CHILIGATI NA NCHEMBA SINGIDA YAANZA




      Nape akihutubia mkutano wa hadhara viwanja vya Ushirika Ikungi nje ya mji wa Singida LEO

      Nape akikumbatiwa na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Singida Joram Alute katika mapokezi ya , Ikunga.

      Chiligati alipungia mkono wananchi baada ya kuwasili na viongozi wa sekretarieti Ikunga, Singida. Kuhsoto ni Asha Juma abdallah, Mwenyekiti wa CCm mkoa wa Singida Joram Alute, Mwiguku Nchemba na Nape.

      kina Mama wa Ikungi wakisgangilia viongozi wa sekretarieti.

      Wana-CCM wakimsikiliza Nape, Ligwa Singida.

    2. Study Abroad

    3. #61
      kinepi_nepi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th August 2007
      Posts : 878
      Rep Power : 1209
      Likes Received
      223
      Likes Given
      118

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Haya Nape tunakusubiri nasikia unataka kumpima oil Dr wa ukweli Dr wa shule. Ila kabla hujaanza wasiliana na riz1 yeye alipima wiki mbili zilizopita sasa akiulizwa anapiga mayowe.

      Nape siku tisini umezusha sasa unataka kuja na single ya Dr slaa utaiweza????? Kesho ndio leo. pop corn please
      "Power never takes a back step only in the face of more power. Nobody can give you freedom, equality or justice or anything. If you're a man, you take it."

    4. #62
      THINKINGBEING's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 9th August 2010
      Posts : 988
      Rep Power : 655
      Likes Received
      232
      Likes Given
      101

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Ajenda ya siku tisini imekwisha ngoja tuweke ingine.
      Watu wanapenda fleva tofauti;au sio jamani?

    5. #63
      Bukanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th December 2010
      Location : Mmahare!
      Posts : 1,272
      Rep Power : 681
      Likes Received
      356
      Likes Given
      718

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Huyo dogo hana lolote CCM ya leo ya kuweka mitoto ya english media kwenye secretariet ni bomb litalokuja lipuka punde, hivi baba yako akiwa kiongozi na wewe ni kiongozi? Au ndo yale ya ukikaa karibu na waridi... Halafu Chiligati achunguzwe nahisi anakula miraa(joke)

    6. #64
      Crashwise's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 23rd October 2007
      Location : Safarini
      Posts : 13,087
      Rep Power : 14280
      Likes Received
      3980
      Likes Given
      3246

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Kwasasa kama ni timu basi CHADEMA ni Barcelona - CCM ni AFC (ya ARUSHA)....yaani mashambulizi ya CDm yana wachanganya sana CCM mpka hawajui wamjibu yupi wache yupi...pole sana CCM naona vitambi vitapungua mwaka huu.....
      Nobody can give you freedom. Nobody can give you equality or justice or anything. If you're a man, you take it.... Malcolm X Nasubiri 'breaking news... '





    7. #65
      Indume Yene's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Chumbani
      Posts : 2,127
      Rep Power : 999
      Likes Received
      323
      Likes Given
      305

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Namhurumia sana huyu kijana, kama alivyosema memba mwingine kuwa huyu kijana anajaribu kudandia gari kwa mbele. Nafikiri ingekuwa vyema amalize kazi iliyondani ya sekretarieti yake na kuwaondoa wachafu kwenye chama chake kabla hajaanza kujipiga kifuani. CCM hakieleweki kinaenda wapi, ingekuwa vyema kutumia muda mwingi kujenga chama kabla ya yeye naye kulipuliwa.

    8. Miaka 50

    9. #66
      Mutwale's Avatar
      Member Array
      Join Date : 20th October 2010
      Posts : 66
      Rep Power : 448
      Likes Received
      18
      Likes Given
      10

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Sasa Ndugu Nape anacheza muziki wa CDM, yeye anaongelea ufisadi wa mapacha watatu tu? mbona watuhumiwa niwengi? Je anamuweka wapi Mkuu wao?

      Hiyo picha inaonyesha Nape alikuwa anahutubia watu wasiozidi 50! je sasa aoni kwamba hotuba zao hazina tena mvuto?
      Tumewachoka!

    10. #67
      Speaker's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 12th August 2010
      Posts : 6,163
      Rep Power : 4558
      Likes Received
      1997
      Likes Given
      5018

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua dk. Slaa kesho singida

      Quote By Utamaduni
      Watu wenyewe wachacheeeeeeeee hivi kweli hao ndio wapenzi wa chama huko singida?
      hahahaha,afu akaandika facebook eti mkutano ulikua na mafanikio sana,...how?
      hao hapo kama hakuwapa hela ya chumvi hawapati tena maskini
      Mjinga mpe cheo...

    11. #68
      gmosha48's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Posts : 805
      Rep Power : 596
      Likes Received
      245
      Likes Given
      474

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua dk. Slaa kesho singida

      Quote By Matola
      Jamani hapa duniani kila kiumbe mungu kampa kipaji chake, kipaji cha Nape hiki hapa chini.

      Attachment 29768

      Alamba...... alamba...... aam,.... aam. Alamba... alamba.... tena!

    12. #69
      CAMARADERIE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2011
      Location : 1 Luthuli Street
      Posts : 4,163
      Rep Power : 2719
      Likes Received
      1586
      Likes Given
      1145

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Quote By TAITUZA
      duh? amazing 90% ya wachangiaji wanaikandya ccm, lkn mbona kwenye kupiga kura hamjitokezi?
      Tunajitokeza halafu KIRAVU na shemejiye MAKAME wanaziiba....usijali 2005 walijipa 80.6%........2010 walijipa 61%.......2015
      A compliment is something like a kiss through a veil




    13. #70
      Fredrick Sanga's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 27th January 2011
      Location : Kijitonyama
      Posts : 2,982
      Rep Power : 2589
      Likes Received
      637
      Likes Given
      776

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Nape haelewi hata rythim ya muziki anaoucheza, Mukama karudishia gamba na superglue, sasa akingangania kutoa gamba lake atajichuna ngozi. ameshaambiwa hakuna alipewa siku tisini. Sijui ana lipi jipya.
      Last edited by Fredrick Sanga; 11th May 2011 at 16:27.

    14. #71
      Shenkalwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2011
      Posts : 398
      Rep Power : 486
      Likes Received
      82
      Likes Given
      0

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Hebu kwanza nielimisheni maana pengine mimi nilipitwa na taarifa fulani fulani. Nawasikia jamaa wakihutubia kuwa ccm imejivua magamba na sasa ni clean. Tena waliotoka kwa kukata tamaa sasa warudi "maana yale hayatajirudia tena" nakadhalika, nakadhalika. Sasa ambalo mimi sielewi ni kwamba sijasikia badiliko lolote lililofanyika ccm tangu mkutano wa Dodoma ambapo mabadiliko yaliyofanyika pale ilikuwa ni kumuondoa Makamba mkubwa na kumsimika Makamba mdogo, kumsimika Nnauye mdogo kwenye nafasi yake ya sasa na ile hali ya kutakiwa kujitathmini na kuchukua hatua. Hata hivyo sijasikia kama kuna waliojitathmini na kuchukua hatua hadi sasa lakini jamaa wanahubiri kuwa mabadiliko yamefanyika ndani ya ccm sijui ni yapi hayo??? Labda pengine nilipitiwa na usingizi kidogo, hebu mnijuze

    15. #72
      Shenkalwa's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd May 2011
      Posts : 398
      Rep Power : 486
      Likes Received
      82
      Likes Given
      0

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Quote By CAMARADERIE
      Tunajitokeza halafu KIRAVU na shemejiye MAKAME wanaziiba....usijali 2005 walijipa 80.6%........2010 walijipa 61%.......2015

      Hapo mkuu hesabu ni rahisi: 80.6 - 61 unapata 19.6. Sasa kwa 2015 chukua 61 toa 19.6 = 41.4 na hiyo pamoja na kuchakachua, kiinteligensia na usalama wa taifa.

    16. #73
      MAN OF CHANGES's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 9th January 2011
      Posts : 175
      Rep Power : 459
      Likes Received
      33
      Likes Given
      19

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Chama cha magamba kwa kweli kina kufa,labda waanze kujivua na ngozi kbs,ikishindikana wabadilishwe damu labda itasaidia kuondoa damu chafu ya ufisadi,uropokaji na roho ya unafki kwa wananchi.

    17. #74
      Uliza_Bei's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 17th February 2011
      Posts : 794
      Rep Power : 576
      Likes Received
      112
      Likes Given
      45

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Si wameapa kufa na zigo la mafisadi, CCM watakosa kura!
      ukipenda asali usiogope ukali wa nyuki

    18. FJM
      #75
      FJM's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th April 2011
      Posts : 7,168
      Rep Power : 2566
      Likes Received
      5318
      Likes Given
      4585

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Let me think... kuna uwezekano huyu dogo kupata msaada toka vyombo vya usalama waka-foji document kulingana na matakwa yao ili watumie kuhuburi kuwa ni ufisadi wa Dr. Slaa! mmm... tusubiri tuone.

    19. #76
      Sikonge's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th January 2008
      Location : Sikonge, Tabora
      Posts : 7,847
      Rep Power : 2330
      Likes Received
      2855
      Likes Given
      5504

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      HAwa ni WAJINGA sana maana hapo ni kijiji anchotoka mshikaji wangu.......

      Ni barabarani kabisa na hapo inapita RELI na barabara kwenda Mwanza-Dar es salaam. Ni kijiji alichotoka TUNDU LISSU.

      Sasa walitegemea waende hapo na wavunje rekodi ya shujaa wao?

      Ni sawa na uende MSOGA na utegemee utapata umati wa watu wakati wee ni mtu wa Iringa.
      Nguruwe pita leo sina Mkuki(By Malila wa JF).

    20. #77
      kanta's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 24th January 2011
      Posts : 277
      Rep Power : 476
      Likes Received
      42
      Likes Given
      20

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Hana jipya, anatapatapa tu lakini tunaofahamu hatushangazi.CCM walikuwa wanatafuta pa kummalizia na sasa wamepapata.Hako kacheo ni njia ya kumpleka kwenye kaburi lake kisiasa.Aendelee tu na propaganda,Nape mwisho wake upo karibu sana kisiasa.RIP NAPE.

    21. #78
      Kiby's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th November 2009
      Posts : 3,499
      Rep Power : 1187
      Likes Received
      599
      Likes Given
      33

      Default Re: Picha sio umati: Nape atamba kumuumbua Dk. Slaa kesho Singida

      Sisiem wametegwa kwenye mtego na Chedema na bila kujitambua wametumbukia kwenye 18. Sasa chama tawala kimetangaza rasmi kurudi kwenye kampeni, na ukizingatia kwamba wao hawaungwi mkono wa watu bila kuwapa chochote basi tutarajie Epa nyingine kuzalishwa ili kuendesha hizi kampeni.
      Ccm ndio walioshikilia serikali tunataka tupate jibu ni kwa nini mfumoko wa bei umeshamiri na gharama za maisha kupanda kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa toka uhuru.
      Nape atueleze ni gamba gani wamelivua ccm na kama ni kweli ajibu je EL, EC na RA wamekwisha kujiondoa kwenye nyadhifa zao ndani ya chama?
      Atueleze pia mkuu wao yaani Jk nae anasubiri nini kujivua gamba? Maana kama wametumia tuhuma, yeye jk ni miongoni mwa wanaotuhumiwa(rej: Epa) hao watakaojivua gamba ni lini watafikishwa mahakamani? Vinginevyo namshauri dogo Nape aache kupiga bla bla maana sisi raia tunasumbuliwa na njaa ya kusababishiwa na viongozi mafisadi w chama chake.
      AISE NAPE BABAANGU NYAMAZA KIMYA TUTAKUTOA ROHO ATI! TUNA NJAA ILIYOCHANGANYOKANA NA HASIRA KALI!!
      .

    22. FemaTV & Radio
    Page 4 of 4 FirstFirst ... 234

    Similar Topics

    1. Replies: 15
      Last Post: 24th May 2011, 18:03
    2. Songea: Dr Slaa umati haujawahi tokea!
      By BONGOLALA in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 23
      Last Post: 30th October 2010, 10:44
    3. PICHA: Dr. Slaa in Singida today
      By n00b in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 28
      Last Post: 20th October 2010, 16:09
    4. Umati wa Songea ni tishio kwa Slaa
      By Zawadi Ngoda in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 60
      Last Post: 14th October 2010, 00:43
    5. Dk Slaa avuta umati wa watu mkoani kwa Pinda
      By MziziMkavu in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 12
      Last Post: 7th October 2010, 19:33

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...