Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: (Docs): Siri ya Kesi ya Mahalu: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi Italia

    Report Post
    Page 8 of 9 FirstFirst ... 6789 LastLast
    Results 141 to 160 of 163
    1. #1
      WhoToldU's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 1st April 2011
      Posts : 6
      Rep Power : 418
      Likes Received
      36
      Likes Given
      0

      Default (Docs): Siri ya Kesi ya Mahalu: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi Italia

      I am hitting the ground while running.
      Ndugu zangu salamu zangu hizi hapa. Hebu someni attachments hizi muone nani mwongo.
      Regards

      na hii pia:
      Re: Yanayozungumzwa Ministry of Foreign and International Affairs (MFAIC) na mitaani kuhusu FITNA zilizofanywa dhidi ya Professor Mahalu na kesi anayokabiliwa nayo mahakamani Tanzania.
      1: Kwamba Balozi Mahalu alikataa begi lile la “diplomatic bag” lisitumike katika ubebaji wa PESA toka nchi za Ulaya Mashariki zilizopelekwa Ubalozini Roma ili zisafirishwe kwenda Dar es Salaam kwa ajili ya kampeni ya URAIS ya mwaka 2005.
      Inasemekana kwamba Balozi Mahalu alikataa utumiaji huo wa diplomatic bag kwani haukuwa sahihi. Kwa kuzingatia utaratibu na kanuni yeye alikomolewa kwa kufukuzwa kazi

      2: Kwamba Balozi Mahalu alikataa kushiriki katika njama za kuiba pesa ya Watanzania Euro billioni 2.4 kwani katika tathmini iliyofanywa na Wizara ya Ujenzi kuhusu Jengo la Ubalozi, bei ya Jengo hilo lingegharimu Euro billioni 5.5 na siyo Euro billioni 3.1 bei ambayo ndio bei ya Jengo iliyokubaliwa chini ya usimamizi wa Balozi katika mchakato wa ununuzi.

      Wapo maofisa wa Wizara ya Nje walioshinikiza serikali inunue jingo lile kwa Euro billioni 5.5 kwa kushirikiana na aliyekuwa Honorary Consul, Tanzania Consulate ya Milano, marehemu Avvocato Georgio. Uadui na chuki dhidi ya Balozi Mahalu ulitokana na hilo pia.

      3: Kitendo chake cha kuwakirimu Ubalozini Maaskofu wa Kanisa la Katoliki waliotembelea Italia kilionekana kama kurasimisha UKRISTO wa Ubalozi pale Roma. Tuhuma hizi zipo sambamba na kile alichozusha Shehe na Mnajimu mmoja kwamba Balozi Mahalu ni adui wa Uislamu kwani Balozi Mahalu ndiye aliyetayarisha Memorandum of Understanding (MOU) kati ya Serikali na Kanisa ili Taasisi za Kikristo zilizokuwa chini ya Serikali zirudishwe na kuwa chini ya Kanisa kama ilivyokuwa awali.

      4: Umiliki wa Balozi Mahalu wa shamba la hekta 500 kandokando ya barabara iendayo Bagamoyo haukumfurahisha aliyekuwa Bosi wake enzi zile kama Waziri wa MFAIC. Sasa hivi shamba lote limemegwa na kuwa sehemu ya EPZ ya Bagamoyo.

      5: Kama michezo michafu iliyochezwa kwenye majengo ya Ubalozi wetu Burundi, Khartoum na nchi nyingine, Balozi Mahalu alishitulia NJAMA za kuuzwa kwa jengo la makazi ya Balozi pale Roma. Njama hizi zilibuniwa na maofisa wa MFAIC.

      Balozi Mahalu alihakikisha kwamba suala la uuzwaji huo kiholela limefikishwa kwenye vyombo vya sheria kule Italia na kufanikiwa kurudisha umiliki wa hilo jengo kwa serikali ya Tanzania.

      Na hapo pia balozi Mahalu alijiongezea MAADUI ambao wamedumu hadi leo.
      Invisible, Recta, Halisi and 31 others like this.

    2. Miaka 50

    3. #141
      Ndallo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st October 2010
      Location : LaRusa
      Posts : 4,146
      Rep Power : 6368
      Likes Received
      1490
      Likes Given
      423

      Default Re: Yafuatayo ni mahojiano kati ya mh. Mkapa na hakimu mkazi kisutu jana mahakamani

      Mkapa: Namfahamu Mahalu kama msomi mzuri,mchapa kazi, muadilifu na kiongozi anayetenda haki! Hapa kwenye RED mkapa umeteleza!
      '' Mtu ni Utu sio Kitu''

    4. #142
      Kigogo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,202
      Rep Power : 2096
      Likes Received
      1234
      Likes Given
      313

      Default Re: Yafuatayo ni mahojiano kati ya mh. Mkapa na hakimu mkazi kisutu jana mahakamani

      Quote By Ribosome
      Hii haimtoi Mahalu kwenye wizi.

      Kifupi Mahalu ni Mwizi wa mali ya umma, kaiba na sasa anajitetea. kama si mwizi aweke hapa fedha za akaunti za nje baada ya hayo malipo, tuone kiasi gani kiliingia.

      Hachomoki huyo. Akichomoka mahakamani watu wataleta hesabu za akaunti zake, ajieleze Euro zaidi ya million 1.5 alipata wapi?
      hakuna kesi hapo ni mpunguwani mtupu na visasi vya JK..maana najua kuwa mahalu alikuwa anamdharau sana JK wakati waziri wa mambo ya nje na alikuwa anafanya maamuzi mengi bila kumuhusisha....of course alikuwa na reason ..Prof na JK wapi na wapi...
      ______________________________ _
      Niko tayari kufa huku nimesimama kuliko kuishi huku nimepiga magoti....

    5. #143
      Kigogo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th December 2007
      Location : Calabash
      Posts : 8,202
      Rep Power : 2096
      Likes Received
      1234
      Likes Given
      313

      Default Re: Yafuatayo ni mahojiano kati ya mh. Mkapa na hakimu mkazi kisutu jana mahakamani

      Quote By MULANGILA
      Mkapa amesema anashangaa kwa nini Mahalu ameshitakiwa. Na kwa kumbukumbu za haraka ni kwamba Mahalu alivuliwa ubalozi February 2006 yaani siku kama 40 hivi tangu JK alipopata madaraka. Hii imekaaje? inaelekea JK alikuwa na usongo naye. Au hakupewa mgawo wake?
      JK mtu wa visasi sana ndo maana...Yaani mambo ya kugombea mademu yeye anayaleta ofisini..Mahalu hana kesi ya kujibu...
      ______________________________ _
      Niko tayari kufa huku nimesimama kuliko kuishi huku nimepiga magoti....

    6. #144
      Capt Tamar's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 15th December 2011
      Posts : 1,715
      Rep Power : 1038
      Likes Received
      417
      Likes Given
      1

      Default Re: Yafuatayo ni mahojiano kati ya mh. Mkapa na hakimu mkazi kisutu jana mahakamani

      Kwa kweli sijawahi kuona thread iliyojaa UZALENDO hapa jf kama hii!! Hii inaonyesha wazi kuwa tukiweka ushabiki wa vyama mbali,hakika tutafika tunakotaka kufika.
      rodrick alexander likes this.

    7. #145
      bushman's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 1,443
      Rep Power : 722
      Likes Received
      309
      Likes Given
      84

      Default Re: Yafuatayo ni mahojiano kati ya mh. Mkapa na hakimu mkazi kisutu jana mahakamani

      Hawa watu wamedhulumiana kwenye mgao wa huo mlungula na aliyedhulumiwa hapo ni mkuu wa kaya ndio maana mkapa anashangaa nani kashtaki!!!!!!!!!!!!!twende tutajua mengi tu!!!!!!


    8. #146
      amba.nkya's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 7th January 2010
      Location : Downtown
      Posts : 292
      Rep Power : 535
      Likes Received
      43
      Likes Given
      47

      Angry Kati ya Rais JK na Mkapa yupi ni mkweli ktk hili?

      WanaJF,

      Inasikitisha mno kwa jinsi mambo yanavyoendeshwa kwenye serikali ya CCM, hususan masuala nyeti ambayo yanawagusa wakuu ya nchi na maslahi ya taifa kwa ujumla. Napenda kujikita kwenye kesi ya Prof. Maharu kwa tuhuma za kununua nyumba ya ubalozi wa TZ kule Italia, kwamba Maharu alinunua nyumba hiyo kwa bei kubwa wakati bei halisi ilikuwa ndogo. Kwa wafuatiliaji wa kesi hii, bila kuingilia uhuru na mamlaka ya Mahakama, inaonyesha dhahiri kwamba Rais JK anamuona Maharu alitumia vibaya madaraka wakati alipokuwa Balozi wa Italia, hivyo anastahili kuwajibishwa kwa ubadhilifu wa fedha za walipa kodi.
      Lakini kwa upande wake Mkapa katika utetezi wake anasema Maharu alikuwa sahihi katika ununuzi wa nyumba kwa kuwa alifuata taratibu zote za manunuzi na kupata Baraka kutoka kwake kama Rais kwa wakati huo (Source: Mwanahalisi ya Leo).


      Kutokana na hali hiyo, ina maana marais hao hawakujua jinsi manunuzi hayo yalivyofanyika ambapo wangeweza kuyaweka sawa mambo hayo kabla ya kufikishana mahakamani, ikizingatiwa JK alikuwa ni Waziri husika kwa wakati huo au ndio mambo ya visasi?


      Sasa nani yuko sahihi kati ya JK na Mkapa kwa sakata hili la Maharu?


      Nawasilisha
      The Figther never gives up!

    9. #147
      fikirikwanza's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th January 2012
      Posts : 642
      Rep Power : 498
      Likes Received
      149
      Likes Given
      17

      Default Re: Kati ya Rais JK na Mkapa yupi ni mkweli ktk hili?

      Kati ya askari magereza na wafungwa nani amekaa muda mrefu gerezani? kijana JK na BM, upande mwingine na CCM wote ni wezi
      amba.nkya likes this.

    10. #148
      ocampo four's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 11th March 2012
      Posts : 249
      Rep Power : 376
      Likes Received
      31
      Likes Given
      6

      Default Re: Kati ya Rais JK na Mkapa yupi ni mkweli ktk hili?

      Mkapa mkwel,jk ni mzee wa visasi sana.
      amba.nkya likes this.

    11. #149
      Ronal Reagan's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th November 2010
      Posts : 2,636
      Rep Power : 961
      Likes Received
      615
      Likes Given
      256

      Default Re: Kati ya Rais JK na Mkapa yupi ni mkweli ktk hili?

      Quote By fikirikwanza
      Kati ya askari magereza na wafungwa nani amekaa muda mrefu gerezani? kijana JK na BM, upande mwingine na CCM wote ni wezi
      Nakubali 100%.

      CCM ndio mhimili na mwanzilishi wa huu ufisadi ambao unaitafuna nchi kama nini. Removing CCM from power is the only remedy. Strategically thereafter disband the mob!
      amba.nkya likes this.

    12. #150
      Wilawela's Avatar
      Member Array
      Join Date : 16th November 2011
      Posts : 80
      Rep Power : 396
      Likes Received
      28
      Likes Given
      454

      Default Re: (Docs): Siri ya Kesi ya Mahalu: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi Italia

      Wakuu poleni na Majikumu!
      Nashukuru sana kwa vielelezo vilivyotolewa na muasisi wa uzi huu! Sina mashaka na viambatanisho ila nina mashaka ya maelezo binafsi ya mtoa maada! Yanaonekana yako biased hayana Objectivity i.e. yako so Subjective kiasi cha Kung'amua mara moja upande wake bila kuuliza japo kasema anatuachia tuamue!

      Wapendwa ni wazi Serikali yetu iko Corrupt na watu wake wana Ubinafsi wa Kutosha kuanzia watendaji,wapambe wanasiasa na jamii kwa ujumla! Kuiba sasa imekuwa Fahari. Natoa Mfano. Ni Kawaida kusikia Nilikwenda kwa Jamaa ,alikuwa Naibu waziri,Katibu Mkuu,Mchumi wa... lakini hana lolote huwezi amini yule Lofa Kabisa ! Mimi kwa nafasi hiyo Mwezi tu Hutanikamata! Fulani Bwana ana Mwaka tu kazini lakini ana Nyumba yake,anaviwanja vitatu na Usafiri wake na mkewe yule Mwanaume Bwana! Hiyo ndiyo Jamii yetu! Hatuwezi ikana!


      Nimepata fursa angalau ya kuziona Sera,Sheria ,Taratibu ,kanuni,Miongozo,Nyaraka(Circu lars) mbalimbali za nchi hii generally ziko njema ,lakini Utekelezajia wake uko People Centered i.e. They are Subjective not Objective yaani zinategemea ni nani kasema nani anashika nafasi ipi na anataka kuzitumia kudeal na Nani? "Tuna jadili nani Kasema na Si Kasema nini". Sheria ya Uvuvi iliyotumika kumfunga Captain na Kutaishisha Samaki na Meli ya Magufuli ipo siku zote lakini ilitumiwa na John Pombe tu,Shera ya Hifadhi ya Barabara tunaambiwa ni ya Ukoloni(Road Ordinance) lakini aliyeitumia ni Magufuli tu.

      Shida iliyopo ni kuwa tools hizi zinatumika kisiasa zaidi,kukidhi matakwa Binafsi kama kupiga dili ,kumkomoa aduai na kadhalika. Unaweza ambiwa hiki kitu hakiwezekani ukakikosa japo jana ulishudia XXXX kafanyiwa na kesho YYY atapewa tena na mtu yule yule! yaani kuna Double standard na hili ndiyo Tatizo la Msingi!

      Sipingi hata Kidogo kuwa Prof.Mahalu Hakupata cha juu na siamini kuwa ni yeye tu na huo ubalozi wa Italy pekee ndiyo walikula deal,lakini je Kwa nini yeye tu! Nadhani hii ndiyo hoja ya Msingi tunayopashwa kuijibu kwa kina na bila kuacha maswali. majibu Mepesi kama Mkatoliki,Muadilifu,n.k hayatusaidii na hayakati kiu kwani wakatoliki waadilifu au wabovu wapo wangapi? Why Him?

      UDINI!

      Jinamizi hili litaimaliza nchi yetu ,naomba tujitazame kwanza kama watanzania haya ya uislama,Ukristo, Seekism, Budhism, Hindu,African Tradition Religions ,Usukuma,uhaya,U-Tanganyika,Upemba yafuate.
      Inasikitisha sana leo hii mtu yeyote akikutendea Jemaa au baya unawaza dini,eneo,kabila nk. Hili ni Tatizo! Wakati mwingine matendo yenyewe ni yakawaida sana hata baba yako mzazi mwenye maadili na Objective angekufanyia! E.g. Uteuzi,kufukuzwa kazi,kusimamishwa n.k.

      Observation yangu:
      Tatizo kubwa lipo kwa Wakristu na Waislamu watu hawa siku hizi wanashindana!
      -Uteuzi watu wanaangalia Majina ,wanahesabu hili ni Tatizo!
      -Waislamu wanalalamika waliachwa nyuma hivyo ni wakati wao wa kwenda mbele ,bila kujali kwa nini waliachwa,offcourse wanadai ni mpango kabambe wa makusudi. Wanadai hata Nyerere aliwabangua ,sina uhakika ila kwa taarifa nilizo nazo waleta dini wetu yaani waaarabu(Uislamu) na Wazungu( Ukristu) walikuja na Packages mbalimbali kama Elimu Dunia na Ahera ,Huduma za Afya na Utamaduni. Waislam wali base zaidi kwenye elimu ahera na Wakristu kwenye elimu Dunia na ili kusoma ulihitaji kwenda shule za misheni na wazee wetu walikataa utasilimishwa i.e. Dini Kwanza Elimu Dunia baadaye! Mwl. Nyerere aliliona hili ni Tatizo ndipo alipo taifisha shule za Dini na Kuzifanya za Serikali na watu wote wakasoma ikumbukwe hapa advantage kuu ilikuwa kwa waislam kwani wanaweza kusoma bila Kuslim! Lakini wanasisa wachache wakiwemo Prof.Kighoma Ali Malima(RIP) wakawasadikisha waislam Nyerere aliwapendelea wakristu na kuwadumaza nyie kwanza waliwakata majina na kuwapendelea wakati mzee wa watu ilifikia mahali selection isifuate marks tu bali pia Proportinality i.e. Singida Nafasi 100.Mtwara 70,Kigoma 50, Pwani 65 ili kila makoa upate fursa ya kusoma kupitia utaratibu huu mwenye maksi 80 Singina anaweza achwa na mwenye 50 Mtwara akachukuliwa ili kuwapa fursa maeneo yote!
      -Wakristu naona wakati mwingine wanajihisi(inferiority Complex) mfano Rais akiteua James Mbatia, Janeth Mbene, Sospita Mhongo no Udini, but akiteua kesho yake Saada na jana(08/05/2012) MwanaHamis Udini! au Tume ya Katiba Udini kwa kuwa ni Mwislam! Kwa wakristo watasema ameangalia sifa na kwa waislam hawataangalia sifa zao wataangalia dini yao. Hili ni tatizo! Si mtetei JK yako mengi yanasemwa juu yake kuwa ana agenda ya udini(sina uhakika) lakini tusimhukumu kwa hisia! Je hana fursa ya kuwateua waislam kwa kuwa ni Muislam. Yawezekana kwa kuwa waislam wengi walikuwa hawajasoma elimu dunia huko nyuma na ndiyo kigezo cha ajira na uteuzi mlizoea kuteuliwa sana leo wamesoma wanastahili tubadilini mazoea tu face reality. JK na wanasiasa na wengine wa namna na kama una agenda hiyo iache haitujengi kama taifa! Utaifa ulijengwa kwa gharama kubwa mno tunaubomoa kwa cheap politics! Mwanza Kilikuwa na Kina Lawi Mnangwanda wabunge toka kusini,kina Mwapachu leo tunaulizana dini , kabila.
      -CCM mki perform mkaacha kulindana na mkawajibika na kuweka clear priorities za taifa hakika hakuna atakaye washinda lakini you do not leave your talk mtaishia sema CUF cha waislam,CDM ni cha wachaga na wakatoliki haifanyi maneno hayo yawe maendeleo for sure you will loose na historia itatuhukum!

      -JK ni kweli mfumko wa bei upo juu,mishahara midogo ,corrupt scandals zipo hamzijali na visasi mnavyo why MRAMBA and YONA ONLY wakati wengi tu tunashihudia! Mtaani hadi ikulu! Ukiandamwa usiseme kwa sababu ni mwislam ni mfumko,
      hukuwajibika , huwa taiti wateule wako full stop!
      -Kwa akili yangu mimi Nyerere,Mwinyi,Mkapa na JK .Kila mmoja kafanya vyema kuliko aliyemtangulia. Mkapa alifanya vyeama lakini kwa kubinafsisha, Kuuza madini kwa 97:3, Kuuza uongozi wa CCM na Taifa imekuporomosha! Ukawa wa Tatu! Tena JK akikomaa kwangu BEN utakuwa the worst President! JK bado una 3 years to recover please use it!

      Kauli za Nasari,Lusinde,Mkapa,Mwigulu Wasira zote mbovu why only Nasari. Nawaomba sana wa TZ wenzangu tuwe OBJECTIVE na Si SUBJECTIVE . JK kama ulivyo dare kwa Prof. Mahalu do it to EL, RA, Maige,Ngereja, JAIRO,Mponda, Mishahara Hewa(Ghasia) etc. Na watendaji wote tutaamini hulipi kisasi but you are Objective!

      Tukianza na KESI ya Prof.Mahalu Tusimhukumu JK wala mahalu kwa dini zao issues hapa je as per Case Proceedings,Presendeces, Authorities, Laws na Docs on Table Mahalu anstahili mashitaka? Je JK anastahili kutetea Raslimali zetu? Je anafanya hivyo Objectively au Subjectively?

      Nawasilisha.
      Halisi, mtalae72 and Setuba Noel like this.

    13. #151
      geophysics's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Location : Kigali
      Posts : 770
      Rep Power : 588
      Likes Received
      115
      Likes Given
      54

      Default Re: (Docs): Siri ya Kesi ya Mahalu: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi Italia

      Sasa nimefumbuka macho, nilienda Rome-Italy baadhi ya watanzania wanashangazwa na unyama alioanza kufanyiwa Professor Mahalu. Wanamsifu na kumpenda maskini... Kwa nyaraka hizi naendelea kuelewa kuwa ni chuki binafsi.... Natamani angemaliza kesi akagombea ubunge....kwa tiketi ya CHADEMA au hata kuteuliwa mahali...It seem he is a hard worker and was OPEN

    14. #152
      Mzalendo80's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th October 2010
      Location : Magogoni, Tanganyika
      Posts : 2,270
      Rep Power : 959
      Likes Received
      815
      Likes Given
      1589

      Default Re: (Docs): Siri ya Kesi ya Mahalu: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi Italia



      Hapo kwenye uduara wa njano sijapaelewa bei mbili To Chief Secretary ? official and real price?
      Halisi and mtalae72 like this.
      The CCM is a crime syndicate, Most members and MPs of CCM are corrupt. No conceince, No brains no nothing, just bunches of criminal and theft. Corruption cost mlalahoi in de street.

    15. #153
      queen matara's Avatar
      Member Array
      Join Date : 29th April 2011
      Posts : 24
      Rep Power : 413
      Likes Received
      20
      Likes Given
      210

      Default Re: Yafuatayo ni mahojiano kati ya mh. Mkapa na hakimu mkazi kisutu jana mahakamani

      Quote By bushman
      Hawa watu wamedhulumiana kwenye mgao wa huo mlungula na aliyedhulumiwa hapo ni mkuu wa kaya ndio maana mkapa anashangaa nani kashtaki!!!!!!!!!!!!!twende tutajua mengi tu!!!!!!
      Profesa Mahalu anamfahamu Kikwete vyema sana tangia Kikwete akiwa mwanafunzi University of Dar es Salaam. Alipopewa ubalozi, Kikwete alikuwa ndiye waziri wa nchi za nje. Nasikia Prof, alikuwa haukubali utendaji kazi wa waziri wake, akiuona kuwa ulikuwa na mapungufu, na hata kudiriki kuu-challenge mara kwa mara.

      Sakata lilikuja aliposikia kuwa Kikwete alikuwa mmoja wa wagombea urais ndipo Mahalu alisema mbovu juu yake na Kikwete akayapata yote. Habari nilizozipata kiundani kabla hata Kikwete hajawa rais ni kwamba Prof. anadaiwa kusema,"huyu bwana mdogo ninaeujua uzuzu wake tangia chuo, na utendaji wake mbovu wa kazi,leo anataka urais?Akiupata si nchi itakwenda mrama kabisa?". Basi baada ya Kikwete kutonywa hayo na afisa mmoja aliyekuwa kwenye ubalozi wetu huko Roma, nasikia akaapa kumshughulikia Prof, akijaliwa kuingia magogoni. Nasikia na Mkapa anayajua hayo.
      mtalae72 likes this.

    16. #154
      MAMA POROJO's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd November 2007
      Posts : 4,858
      Rep Power : 1844
      Likes Received
      593
      Likes Given
      413

      Default

      Quote By mwalimu
      ndio maana kesi inasuasua...kwa mtaji huu profesa atapeta kiulaiiini!!
      tuiachie mahakama

    17. #155
      Gamba la Nyoka's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st May 2007
      Posts : 1,642
      Rep Power : 959
      Likes Received
      267
      Likes Given
      97

      Default Re: (Docs): Siri ya Kesi ya Mahalu: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi Italia

      Hii issue ya "real price" na "official price" imekaaje wadau?- je jengo laweza kuwa na bei mbili tofauti?- hapa kengele ya tahadhari imelia!
      Halisi likes this.
      Chadema kama mnapokea misaada kutoka nje bila kufanya tathmini, angalieni mkishika dola msije mkaiuza Tanzania na watu wake kwa vijimisaada vichache- Hao wanaowapa misaada hawana permanent Friends/Enemies, bali wana permanent Interests.

    18. #156
      hans79's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2011
      Posts : 1,533
      Rep Power : 774
      Likes Received
      144
      Likes Given
      0

      Default

      Quote By Ribosome
      Unamsikia tu Kikwete lakini nakuhakikishia humjui. Kikwete hajakisia wala hakuwekwa kwenye Urais kwa kupachikwa, alikuwa so ambitious kwa miaka mingi sana na alilenga siku moja awe Rais. Mtatafuta madudu ya Kikwete mpaka mchoke hamtayakuta, huyo jamaa ni super clean.

      Hana mnampachika na mnashindwa, Jee, angekuwa nayo si ndio ingekuwa mwao?

      Na bado atazidi kuyaibuwa! Kama alivyoibuwa ya wachungaji kuleta unga na wachungaji kukutwa na mabaki ya Albino, tutayaona mengi tu, ambayo wakati wa Mkapa yalikuwa yakifichwa kwa kila njia.

      Nna uhakika Mkapa kashinikizwa na Mahalu aje ku "save" la sivyo ataumbuliwa, lakini wapi? tutayaona tu, kama si leo kesho.
      Mbona pana barua alisaini ya kuthibitisha ya kuwa nyumba hiyo haina tatizo lolote na ununuzi wake ni sawa. Hiyo barua niliiona mahakamani wakati nasubiri kesi za epa, siku hiyo shahidi upande wa serikali alishindwa kueleza wasifu wa elimu yake na pia alisema jk mwongo.
      Mahojiano kati ya wakili utetezi na shahidi serikali :-
      WU wewe ulikuwa nani wakati wa unumuzi?
      SS mkuu wa protocol na mwenyekiti wa nyumba za serikali nje.
      WU majukumu ni yapi ?
      SS ni kusimamia ununusi na pia kuangalia nyumba hizo.
      WU taratibu zipoje kama mkiti?
      SS kuongoza watalaam toka taasisi mbalimbali za serikali na kuangalia ubora wa hizo nyumba.
      WU je kwa nini unasema nyumba thamani yake si sawa?
      SS kutokana na uzoefu wake wa kujenga.
      WU tupe wasifu wa elimu yako?
      SS nimesoma la la mbaka juu.
      Kwangu nilipata funzo moja ya kuwa pana tatizo upande wa serikali, ndo maana kesi nyingi inashindwa kutokana na mashahidi dhaifu na pia chanzo cha mikataba mibovu.

    19. #157
      JahGun's Avatar
      Member Array
      Join Date : 24th May 2011
      Posts : 72
      Rep Power : 419
      Likes Received
      15
      Likes Given
      20

      Default Re: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi ITALIA

      Educated Fools !

    20. #158
      Halisi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th January 2007
      Posts : 3,037
      Rep Power : 2178
      Likes Received
      455
      Likes Given
      243

      Default Re: (Docs): Siri ya Kesi ya Mahalu: Ununuzi wa Jengo la Ubalozi Italia

      Quote By WhoToldU
      I am hitting the ground while running.
      Ndugu zangu salamu zangu hizi hapa. Hebu someni attachments hizi muone nani mwongo.
      Regards

      na hii pia:
      Re: Yanayozungumzwa Ministry of Foreign and International Affairs (MFAIC) na mitaani kuhusu FITNA zilizofanywa dhidi ya Professor Mahalu na kesi anayokabiliwa nayo mahakamani Tanzania.
      1: Kwamba Balozi Mahalu alikataa begi lile la “diplomatic bag” lisitumike katika ubebaji wa PESA toka nchi za Ulaya Mashariki zilizopelekwa Ubalozini Roma ili zisafirishwe kwenda Dar es Salaam kwa ajili ya kampeni ya URAIS ya mwaka 2005.
      Inasemekana kwamba Balozi Mahalu alikataa utumiaji huo wa diplomatic bag kwani haukuwa sahihi. Kwa kuzingatia utaratibu na kanuni yeye alikomolewa kwa kufukuzwa kazi

      2: Kwamba Balozi Mahalu alikataa kushiriki katika njama za kuiba pesa ya Watanzania Euro billioni 2.4 kwani katika tathmini iliyofanywa na Wizara ya Ujenzi kuhusu Jengo la Ubalozi, bei ya Jengo hilo lingegharimu Euro billioni 5.5 na siyo Euro billioni 3.1 bei ambayo ndio bei ya Jengo iliyokubaliwa chini ya usimamizi wa Balozi katika mchakato wa ununuzi.

      Wapo maofisa wa Wizara ya Nje walioshinikiza serikali inunue jingo lile kwa Euro billioni 5.5 kwa kushirikiana na aliyekuwa Honorary Consul, Tanzania Consulate ya Milano, marehemu Avvocato Georgio. Uadui na chuki dhidi ya Balozi Mahalu ulitokana na hilo pia.

      3: Kitendo chake cha kuwakirimu Ubalozini Maaskofu wa Kanisa la Katoliki waliotembelea Italia kilionekana kama kurasimisha UKRISTO wa Ubalozi pale Roma. Tuhuma hizi zipo sambamba na kile alichozusha Shehe na Mnajimu mmoja kwamba Balozi Mahalu ni adui wa Uislamu kwani Balozi Mahalu ndiye aliyetayarisha Memorandum of Understanding (MOU) kati ya Serikali na Kanisa ili Taasisi za Kikristo zilizokuwa chini ya Serikali zirudishwe na kuwa chini ya Kanisa kama ilivyokuwa awali.

      4: Umiliki wa Balozi Mahalu wa shamba la hekta 500 kandokando ya barabara iendayo Bagamoyo haukumfurahisha aliyekuwa Bosi wake enzi zile kama Waziri wa MFAIC. Sasa hivi shamba lote limemegwa na kuwa sehemu ya EPZ ya Bagamoyo.

      5: Kama michezo michafu iliyochezwa kwenye majengo ya Ubalozi wetu Burundi, Khartoum na nchi nyingine, Balozi Mahalu alishitulia NJAMA za kuuzwa kwa jengo la makazi ya Balozi pale Roma. Njama hizi zilibuniwa na maofisa wa MFAIC.

      Balozi Mahalu alihakikisha kwamba suala la uuzwaji huo kiholela limefikishwa kwenye vyombo vya sheria kule Italia na kufanikiwa kurudisha umiliki wa hilo jengo kwa serikali ya Tanzania.

      Na hapo pia balozi Mahalu alijiongezea MAADUI ambao wamedumu hadi leo.
      Kwa kweli Mkuu umefanya kazi nzuri sana na inayozidi kuipa hadhi JF. Ingekuwa vyema kwanza ukajua msingi wa kesi ya Mahalu ni wapi hasa. Kwa haraka haraka na kwa jicho lisilohitaji kuwa mwanasheria tatizo si ununuzi wa jengo, tatizo si bei, tatizo si kibali cha kununua, tatizo si mawasiliano, tatizo si nani alijua na nani hakujua: TATIZO AMBALO Ndio msingi wa kesi iliyopo KISUTU ni kuwapo kwa mikataba miwili, mmoja ukiwa halali na mwingine ukiwa wa kienyeji. Na hili Benjamin Mkapa alilizungumzia mahakamani akasema alilijua na kuliidhinisha KWA MDOMO na akasema ipo mifano ya mchezo kama wa Italy ambao serikali ya Tanzania imefanya kwa nchi nyingine lakini akakataa kuzitaja kwa madai kwamba italeta mgogoro wa Kidiplomasia, bila kusema mbona Italy haogopi huo mgogoro. Hapa tuangalie uhalali wa ama kukwepa kodi kunakofanywa na serikali ama uhalali wa kula njama na mwenye nyumba ili kugawana fedha zilizozidi kwenye bei. Yote mawili ni makosa kwa Tanzania kisheria na ni makosa hata kwa Italy. Bahati mbaya sana Mkuu hujaweka hiyo mikataba zaid ya mawasiliano yakionyesha kuwapo kwa hiyo mikataba miwili mmoja wa bei ya Euro 1.03m kuwa ni mkataba rasmi kisheria (Official price) na mwingine wa bei ya Euro 3.0m kuwa ni mkataba wa "real price" (sina Kiswahili chake).