Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Hivi ni kweli kazi yetu ni kunung'unika tu?

    Report Post
    Results 1 to 2 of 2
    1. #1
      mapambano's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2008
      Posts : 538
      Rep Power : 682
      Likes Received
      8
      Likes Given
      15

      Post Hivi ni kweli kazi yetu ni kunung'unika tu?

      Habari za Kitaifa
      Mzindakaya ataka wabunge kuacha kunung’unika
      Mwandishi Wetu, Dodoma
      Daily News; Sunday,April 20, 2008 @00:03

      MBUNGE wa Kwela, Chrisant Mzindakaya (CCM), amewataka viongozi na wabunge nchini kuacha kunung’unika kama wafanyavyo wananchi, badala ya kuchukua hatua ya kuondoa matatizo husika.

      Akichangia maazimio manne yaliyowasilishwa juzi jioni bungeni ya Wizara ya Miundombinu, Mzindakaya alisema inaonekana wanachosomea viongozi ni shutuma tu na kunung’unika, bila ya kuwa na nini cha kufanya kuondokana na hali hiyo.

      “Inaonekana kila mtu ananung’unika. Waziri Mkuu alikwenda pale bandarini akasema kweli hali ni mbaya. Wananchi wanalia; TICTS wanalia; wabunge wanalia; nani atafanya kazi wakati tunalia,” alisema Mzindakaya na kuongeza:

      “Viongozi wananung’unika; tulichosomea ni critics, hakuna way forward; wabunge wanalalamika; viongozi wanalalamika. Nani ataiondoa nchi katika matatizo kama kila mtu analalamika. “Kule kwetu kuna mdudu anaitwa tengaruzi; yeye kazi yake ni kuzunguka hapohapo alipo ndani ya maji.

      Nasi tumekuwa kama tengaruzi; tunazunguka hapohapo, hatuendi,” alisema mwanasiasa huyo mkongwe. Alisema viongozi wanapaswa kuchunguza kwa nini bandari ya Dar es Salaam imekuwa na msongamano na kupendekeza wabunge na wataalamu kukaa chini na kuchunguza msongamano huo.

      Lakini pia alisema tatizo kubwa la Tanzania ni kutokuwa na miundombinu mizuri hasa ya usafirishaji kwa kutumia reli, na kwamba uchumi wa kutegemea barabara, utaiumiza nchi.

      Maazimio yaliyofikishwa bungeni na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Dk. Maua Daftari kwa niaba ya Wizara ya Miundombinu ni Itifaki ya Marekebisho ya Mkataba ulioanzisha Kamati ya Kudumu ya Kiserikali ya Usafiri wa Baharini mwaka 2006 na Mkataba wa Kuanzisha Wakala wa Uwezeshaji wa Uchukuzi wa Mizigo Ukanda wa Kati wa mwaka 2006.

      Mengine ni kuridhia Mkataba wa Shirika la Kimataifa linalosimamia Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) na kuridhia Itifaki ya Mkataba kuhusu Masuala Maalumu yahusuyo vifaa vya ndege vinavyohamishika.

      Wabunge wengine pia waliochangia maazimio hayo yaliyoridhiwa na Bunge jana asubuhi, walipendekeza kuimarishwa kwa bandari nyingine za Tanga, Lindi na Mtwara pamoja na miundombinu.

      Mbunge wa Muheza, Herbert Mntangi (CCM), alisema wakati umefika wa Watanzania kuamka sasa na kutumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo kwa kutumia reli na bandari zilizopo.

      Mbunge wa Tabora Mjini, Siraju Kaboyonga (CCM), alisema Tanzania imejaliwa bandari nzuri, lakini imelala usingizi. “Hatuna injini, hatuna mabehewa, barabara mbovu. Bila ya kuwa na biashara katika usafirishaji, hatutafika,” alisema.

      Kwa upande wake, Mbunge wa Tandahimba, Juma Njwayo (CCM), aliitaka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuacha kuweka vikwazo kwamba kutakuwa na upotevu wa mapato kama mizigo itashushwa katika bandari ya Mtwara.

      Wazo hilo la Njwayo liliungwa mkono na Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi, aliyehoji wafanyakazi wa TRA wanachagua wapi pa kufanya kazi. “Eti mizigo itaporwa, itaibwa. Kwa nini tuliamua kujenga bandari,” alihoji Zambi.


    2. BAK is offline
      BAK
      #2
      BAK's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 11th February 2007
      Location : Mfaranyaki
      Posts : 26,842
      Rep Power : 45017
      Likes Received
      8689
      Likes Given
      8754

      Default Re: Hivi ni kweli kazi yetu ni kunung'unika tu?

      Naona serikali na CCM ndio tengaruzi, tena hata tengaruzi ana afadhali maana anazunguka hapo hapo, wao wanarudi nyuma kwa kasi kubwa badala ya kwenda mbele.
      Let your graceful words fly out into the World, carried on winds of courage, imagination and joy. Let them inspire others to step into action

    Similar Topics

    1. Hivi kuna wategea kazi maofisini kama members wa JF kweli?
      By mojoki in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 40
      Last Post: 20th September 2011, 23:10
    2. Hivi kweli Serikali yetu ipo serious na suala la nishati??
      By sekulu in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 1
      Last Post: 7th June 2011, 19:34
    3. Hivi kweli TRA wana nia njema na nchi yetu?
      By Kaduguda in forum Business & Economic Forum
      Replies: 6
      Last Post: 23rd February 2009, 11:25
    4. Replies: 34
      Last Post: 27th October 2008, 14:22
    5. Hivi ni kweli serikali yetu haipo makini hivi ??
      By KadaMpinzani in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 13th August 2007, 21:08

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...