Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

    Report Post
    Page 4 of 4 FirstFirst ... 234
    Results 61 to 72 of 72
    1. #1
      mchakachuaji192's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 19th October 2010
      Posts : 291
      Rep Power : 494
      Likes Received
      24
      Likes Given
      14

      Default JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, ameshtushwa kupanda kwa bei ya vyakula na gharama za maisha mijini.Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete ameagiza chakula cha akiba cha taifa kuingizwa katika masoko ya mijini hasa jiji la Dar es Salaam mara moja ili kupunguza bei ya chakula katika masoko ya miji na kupunguza makali na gharama ya maisha kwa wananchi.

      Rais Kikwete ameagiza kuwa kazi hiyo ya kuingilia soko na kupunguza bei ya chakula kwa wananchi iwe kazi ya nyongeza na ya kudumu ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na Wakala wa Akiba ya Chakula ya Taifa (NFRA).

      Amesema kuwa miji ya Tanzania ina masikini wengi na malalamiko makubwa ya masikini hao ni bei kubwa ya chakula na kuwa ni wajibu wa Serikali kuchukua hatua za makusudi kuwapunguzia wananchi gharama hizo za maisha kwa kuingiza chakula cha bei nafuu katika masoko ya mijini.

      Rais alitoa maagizo hayo wakati alipotembelea maghala ya NFRA mjini Dar es Salaam kama mwendelezo wa ziara zake na Wizara mbalimbali na taasisi za wizara hizo.

      Rais Kikwete amesema kuwa kama hatua za kuingilia soko zingechukuliwa tangu Oktoba mwaka jana wakati bei ya mahindi ilipokuwa sh. 300 kwa kilo mjini Dar es Salaam, bei hiyo isingepanda na kufikia sh. 430 kwa bei ya sasa.

      “Hii ndiyo kazi yetu kuanzia sasa yaani kuhakikisha kuwa tunaingilia soko, kuingiza chakula cha kutosha na hasa mahindi kwa sababu hiki ndicho chakula kikuu cha Watanzania na kuhakikisha kuwa tunaishusha bei hiyo ya mahindi hadi sh. 300 katika kipindi kifupi iwezekanavyo,” Rais amewaambia maofisa wa Wizara na Wakala huo.

      Amesema kuwa lazima viongozi waelewe kuwa hata mijini kuna upungufu wa chakula.

      “Tafsiri ya njaa ni kama mji haupati chakula cha kutosha basi kuna njaa, Hivyo tujipe mamlaka ya kuingiza haraka soko ili kuwalinda wananchi kwa sababu hatuwezi kuwaacha wananchi mikononi mwa wafanyabiashara binafsi wa chakula ambacho kichocheo chao kikubwa ni faida,” amesema Rais Kikwete.

      Amesema hiyo sasa ni kazi yao ya kila siku yaani kufuatilia masoko na kuhakikisha kuwa kinakuwepo chakula cha kutosha kupunguza bei.
      Amewaagiza viongozi kucheza na soko la Dar es Salaam ili kuhakikisha kuwa bei zinakwenda chini haraka iwezekanavyo.

      Amesema kuwa siyo busara kwa mahindi kubakia maghalani kusubiri njaa wakati bei za vyakula zinapanda sana. Nyie mna wajibu wa kulilisha taifa hili.

      Source: Dar leo
      My take ina maana yeye anakaa tu magogoni bila kujua changamoto zinazowakabili wananchi wake? huyu baba Rizione One day yes

    2. FemaTV & Radio

    3. #61
      Candid Scope's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 8th November 2010
      Posts : 7,606
      Rep Power : 15261
      Likes Received
      3731
      Likes Given
      2865

      Default Re: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      Angejaribu kupambanua namna gani serikali itaingilia kati kupunguza bei, isije ikawa kuwakandamiza wafanyabiashara wadogo na kuwaacha mafisadi papa wakipeta tu.

    4. #62
      kasimba123's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 18th April 2010
      Posts : 1,056
      Rep Power : 673
      Likes Received
      152
      Likes Given
      56

      Default Re: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      waliua Tipper wakaua TPDC enewei ni maumivu kwa kwenda mbele
      "you don't need to know the right answer to know that the given answer is wrong"- Kiranga

    5. #63
      Kobello's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 20th February 2011
      Posts : 2,946
      Rep Power : 1659
      Likes Received
      1107
      Likes Given
      191

      Default Re: JK apata mshituko

      Quote By CAMARADERIE
      Hapana...unaposhusha kodi bei hupungua na watu hufanya manunuzi zaidi....kutokana na unafuu wa bei...watu watanunua zaidi(in terms of volumes) na wigo wa kodi kupanda....simple economics...kwa vile VAT sio production cost
      hapana babu.....you need to check how elastic that demand is,we're talking about food here!!!

    6. #64
      Gosbertgoodluck's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd March 2008
      Posts : 2,863
      Rep Power : 1149
      Likes Received
      334
      Likes Given
      4

      Default

      Quote By ba martha
      Hivi wachumi wanaomzunguka ****** pale magogoni wana kazi gan? Dah bora BEN kuliko huyu mtu...hata kiberiti kushusha bei hawawezi kweli?????????????
      Ni mkurupukaji asiye na maana. Mimi namjua huyu rais hakuna gazeti asilosoma mpaka ya udaku. Kinachoendelea mitaani anafahamu vizuri. Leo eti anakurupuka kujifanya anashangaa bei za vyakula ni unafiki mkubwa. Marais wa namna hii ndiyo hawatufai. Hiyo ndiyo tabia ya rais msanii na mpenda sifa zisizo na msingi. Nachojua mimi ataishia kusema hivyo na hakuna hatua itakayochukuliwa.

    7. #65
      taffu69's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th February 2007
      Posts : 1,175
      Rep Power : 861
      Likes Received
      216
      Likes Given
      133

      Default Re: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      Bei ya petroli iko sh. 2,050/lita...., KASI ZAIDI kwa kwenda mbele!!!!!!

    8. Miaka 50

    9. #66
      Mzee Mwanakijiji's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 10th March 2006
      Location : Kijijini
      Posts : 29,499
      Rep Power : 46709
      Likes Received
      16347
      Likes Given
      8417

      Default Re: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      Ni wazo ambalo naweza kusema ni linatokana na emotional response and not from a rational one. Ni uamuzi uliotokana na kushtushwa.

      a. Wakulima wa Tanzania wanazalisha vipi chakula? Nakumbuka nilikuwa miongoni mwa wakosoaji wa kampeni ya kuzalisha Jatropha ambapo vijiji vilibadilisha kutoka kulima mazao ya chakula na kuanza kulima Jatropha wakiadiwa hela ya haraka haraka;

      b. Serikali yake ilitoa Stimulus Package katika sekta ya Uchumi wa zaidi ya Shilingi Trilioni 1.6 ni kwa kiasi gani fedha hizo zilienda kusaidia kilimo cha mazao ya chakula?

      c. Kama mtu mwingine alivyoeleza hapo juu; unapotoa chakula cha ziada wakati prospect ya mazao mwaka huu bado inatisha kwa ajili ya lengo la kupunguza bei ya vyakula unajiandaa kwa janga kubwa zaidi. Itakuwaje akifanikiwa kweli kupunguza bei za vyakula (temporarily) kwa kuongeza bidhaa sokoni halafu baadaye mavuno yakawa mabaya na taifa likaanza kuwa na tatizo la njaa; NGR itakuwa haina chakula na kubidi kuagiza kutoka nje. Wale wanaoshangaa Tanzania kula Yanga wakati wa Nyerere, watapigwa na butwaa wakilazimika kula Yanga 2011!

      d. Tatizo la chakula Tanzania ni la kujitakia; na linatokana na sera mbovu za Chama cha Mapinduzi.
      [email protected]
      Tunapotaka kubadilisha watawala si kwa sababu tunataka kubadilisha sura; bali kubadilisha utawala! Yaani, tunataka kubadilisha jinsi tunavyotawaliwa siyo tu sura za wanao tutawala M. M. Mwanakijiji

    10. #67
      Kalila's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th September 2010
      Location : tanzania
      Posts : 248
      Rep Power : 490
      Likes Received
      57
      Likes Given
      28

      Default Re: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      cdm walisema nini kanda ya ziwa na yeye anatimiza tu kiaina na bado atafanya mengine tu pipoz power kumbe noma eh

    11. #68
      POMPO's Avatar
      Banned Array
      Join Date : 12th March 2011
      Posts : 2,955
      Rep Power : 0
      Likes Received
      1090
      Likes Given
      625

      Default Re: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      Hana maana vipi kuhusu mfumuko wa mafuta? Coz fuel is everything on inflation rate. Mpaka cdm waandamane ndio atekeleze? Sh*t

    12. #69
      MartinDavid's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 22nd May 2009
      Posts : 690
      Rep Power : 647
      Likes Received
      37
      Likes Given
      16

      Default Re: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      Kweli jk ni hamnazo kweli!!

      Yeye alikuwa wapi wakati chadema wanaandamana kupinga kupanda kwa bei za bidhaa na maisha!!!

      Si yeye alisema chadema wanataka afanye mambo ambayo hata maraisi waliopita walishindwa??

      Sasa haya maamuzi ya sasa alikuwa anasubiri lini ndiyo atoe!!!
      "Nothing in all the world is more dangerous than sincere ignorance and conscientious stupidity."

    13. #70
      Chesty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th August 2009
      Posts : 1,046
      Rep Power : 704
      Likes Received
      155
      Likes Given
      22

      Default Re: JK apata mshituko

      Quote By mchakachuaji192
      Huyu jamaa waliopendekeza awe kiongozi wa nchi sijui waliona nini maana hata wizara alizokuwepo kabla ya hapo ameacha maneno mengi sana
      Mkuu usifikiri kuwa Rais wa Tanzania ni sawa na rais kama wa Botswana, Namibia, South Afrika, Ghana, n.k. Rais wa Tanzania can be ANYTHING!!

    14. #71
      apakati's Avatar
      Member Array
      Join Date : 19th March 2009
      Posts : 19
      Rep Power : 521
      Likes Received
      0
      Likes Given
      6

      Default Re: JK apata mshituko

      Quote By MTM
      hIZI MOVES ZITALIPUNGUZIA TAIFA MAPATO
      Mapato ya nini wakati wa janga? Unataka kusaidia huku unataka kukamua? The two wont work!!
      "Heri Bubu Kuliko Chiriku"

    15. #72
      Duduwasha's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 3rd November 2010
      Posts : 2,620
      Rep Power : 6248
      Likes Received
      523
      Likes Given
      418

      Default Re: JK apata mshituko juu ya ongezeko la bei ya vyakula; aagiza serikali kuingilia kati

      Hivi kuna analoagiza likatekelezwa kweli? zaidi ya polisi tu ndio huwa wanatekeleza....

      Bomu la Tumbo

    Page 4 of 4 FirstFirst ... 234

    Similar Topics

    1. Kikwete aagiza Nyumba za Serikali zilizouzwa zirejeshwe
      By tibwilitibwili in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 211
      Last Post: 27th October 2012, 18:11
    2. Chadema:ni sahihi serikali kuingilia uhuru wa mahakama??
      By kulwa12 in forum Habari na Hoja mchanganyiko
      Replies: 4
      Last Post: 7th November 2011, 21:58
    3. Replies: 9
      Last Post: 7th November 2011, 11:58
    4. Tetesi: Rais aagiza Lema aachiwe kwa dhamana ya serikali
      By Kanigini in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 68
      Last Post: 2nd November 2011, 14:24
    5. Serikali yaombwa kuingilia mgogoro Bulyanhulu
      By BAK in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 1
      Last Post: 2nd November 2007, 15:05

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...