RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, ameshtushwa kupanda kwa bei ya vyakula na gharama za maisha mijini.Kutokana na hali hiyo, Rais Kikwete ameagiza chakula cha akiba cha taifa kuingizwa katika masoko ya mijini hasa jiji la Dar es Salaam mara moja ili kupunguza bei ya chakula katika masoko ya miji na kupunguza makali na gharama ya maisha kwa wananchi.
Rais Kikwete ameagiza kuwa kazi hiyo ya kuingilia soko na kupunguza bei ya chakula kwa wananchi iwe kazi ya nyongeza na ya kudumu ya Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika pamoja na Wakala wa Akiba ya Chakula ya Taifa (NFRA).
Amesema kuwa miji ya Tanzania ina masikini wengi na malalamiko makubwa ya masikini hao ni bei kubwa ya chakula na kuwa ni wajibu wa Serikali kuchukua hatua za makusudi kuwapunguzia wananchi gharama hizo za maisha kwa kuingiza chakula cha bei nafuu katika masoko ya mijini.
Rais alitoa maagizo hayo wakati alipotembelea maghala ya NFRA mjini Dar es Salaam kama mwendelezo wa ziara zake na Wizara mbalimbali na taasisi za wizara hizo.
Rais Kikwete amesema kuwa kama hatua za kuingilia soko zingechukuliwa tangu Oktoba mwaka jana wakati bei ya mahindi ilipokuwa sh. 300 kwa kilo mjini Dar es Salaam, bei hiyo isingepanda na kufikia sh. 430 kwa bei ya sasa.
“Hii ndiyo kazi yetu kuanzia sasa yaani kuhakikisha kuwa tunaingilia soko, kuingiza chakula cha kutosha na hasa mahindi kwa sababu hiki ndicho chakula kikuu cha Watanzania na kuhakikisha kuwa tunaishusha bei hiyo ya mahindi hadi sh. 300 katika kipindi kifupi iwezekanavyo,” Rais amewaambia maofisa wa Wizara na Wakala huo.
Amesema kuwa lazima viongozi waelewe kuwa hata mijini kuna upungufu wa chakula.
“Tafsiri ya njaa ni kama mji haupati chakula cha kutosha basi kuna njaa, Hivyo tujipe mamlaka ya kuingiza haraka soko ili kuwalinda wananchi kwa sababu hatuwezi kuwaacha wananchi mikononi mwa wafanyabiashara binafsi wa chakula ambacho kichocheo chao kikubwa ni faida,” amesema Rais Kikwete.
Amesema hiyo sasa ni kazi yao ya kila siku yaani kufuatilia masoko na kuhakikisha kuwa kinakuwepo chakula cha kutosha kupunguza bei.
Amewaagiza viongozi kucheza na soko la Dar es Salaam ili kuhakikisha kuwa bei zinakwenda chini haraka iwezekanavyo.
Amesema kuwa siyo busara kwa mahindi kubakia maghalani kusubiri njaa wakati bei za vyakula zinapanda sana. Nyie mna wajibu wa kulilisha taifa hili.
Source: Dar leo
My take ina maana yeye anakaa tu magogoni bila kujua changamoto zinazowakabili wananchi wake? huyu baba Rizione One day yes

Reply With Quote


Follow Us Here