Kila kukicha, unajitokeza ushahidi kwamba kiwango cha kufikiri miongoni mwa wa-Tanzania wengi ni duni. Siku hizi, kwa mfano, imeibuka hii dhana ya mfumo Kristo.
Walioibuni dhana hii na ambao wanaieneza wana ajenda ya kujenga hoja kuwa mfumo wa utawala na uchumi Tanzania unaendeshwa kwa misingi ya kiKristu, na kwa lengo la kuwanufaisha wa-Kristu na kuwakandamiza na kuwanyima wa-Islam fursa na haki wanazostahili, katika nyanja mbali mbali, kama vile elimu na uongozi.
Hii ndio dhana ya msingi ya hiki kinachoitwa mfumo Kristo. Wanaojenga hoja hii wanadai kuwa serikali ya Tanzania yenyewe inaendeshwa na maaskofu kama sehemu ya uendelezaji wa huu wanaouita mfumo Kristo.
Kwanza napenda kusema, kama ninavyosema daima, kuwa kila mtu ana uhuru wa kutoa mawazo yake. Uhuru huu ni pamoja na uhuru wa kuyahoji au kuyapinga mawazo ya wengine, kufuatana na mchakato wa kujielimisha na kutafakari masuala. Ni pamoja na uhuru wa kuyapinga mawazo yako mwenyewe.
Nashangaa kwa nini mfumo mbovu uhusishwe na jina la Yesu Kristu. Dini zote mbili, u-Islam na u-Kristu, zinamtambua na kumheshimu Yesu. Yesu anatambuliwa kama Mungu katika u-Kristu. Na katika u-Islam, anatambuliwa kama mtume maarufu. Dini zote zinamheshimu sana Yesu.
Kama mfumo wa Tanzania umeoza kama inavyosemwa, hauwezi kuwa mfumo Kristo. Kuuita mfumo Kristo ni dhihaka isiyo kifani. Huwezi kuuhusisha uchafu wowote na Mungu au mtume. Kama kweli maaskofu wanaendekeza na kuulinda mfumo wa dhuluma, wanakiuka mafundisho na maadili ya Kristo. Huu si mfumo Kristo. Mfumo Kristo ni mfumo wa haki na maadili aliyotufundisha Kristo.
Sidhani kama inahitaji akili ya pekee sana kuitambua hoja hii. Lakini ni wazi kuwa watu wengi Tanzania wana kiwango duni cha kufikiri au kuelewa mambo. Kwa dhana yao ya mfumo Kristo, wanaudhihaki u-Kristo, na pia wanaudhihaki u-Islam. Ila, kutokana na akili zao duni, hawatambui hilo. Kilichopo ni kuwaombea dua njema, waweze kujitambua na kujirekebisha.
Acha uongo wewe, hiyo redio unasikiliza peke yako sasa hivi?
Kinachozungumziwa ingeneral ni ile double standard inayofanywa na serikali, mfano wakatolea mauaji ya mwembechai iliombwa tume iundwe serikali ikakataa mwaka huohuo akauliwa mbwa wa police sumbawanga tume ikaundwa haraka, wanahoji mifano kama hiyo, lingine Dr. Slaa sms aliyomuandikia IGP ya kitisho je ingekuwa wengine ingekuwaje?
Kingine kinazungumzua media zilvyokuwa na bad perception na waislamu hada kny suala la sensa. Huwa mnakaa humu na kusema ooh waislamu wanapendelewa sababu wenzao ndio viongozi kama Rais,Igp etc etc lakin haohao ndo sasa hivi wanashutumiwa pia. Huwa najiuliza humu JF watu kama wewe huwa mnawaza before kuleta humu au ili mradi nawe upost hata kama uongo?
Kajipange tena na propaganda zako za kichekechea.
Kuna kitu sielewi hapa. Waislam hawa hawa wanaolalamika ndo wanaoipigia kura CCM
Chadema ni taasisi wewe unatumia mawazo ya mtu binafsi kuihukumu.
Haiwezekani 90% ya mawazo ya wana CDM yakawa against uislam halaf ukampinga Ritz anachosema. Fatilia thread zote humu unless uwe mgeni JF. Ntajifikiria upya hata ushabiki wangu na family yangu kwa CDM bora nkawa bila ya chama kama huu upuuzi utaendelea.
Haiwezekani 90% ya mawazo ya wana CDM yakawa against uislam halaf ukampinga Ritz anachosema. Fatilia thread zote humu unless uwe mgeni JF. Ntajifikiria upya hata ushabiki wangu na family yangu kwa CDM bora nkawa bila ya chama kama huu upuuzi utaendelea.
umetoa wapi hiyo takwimu? Kwenye sensa au?
* LOVE COMES NATURALLY; HATE IS TAUGHT.....by nngu007 wa JF
Kweli serikali inasikiliza mawazo ya wakristu na kuyaamini, si uliona Loliondo mfano mzuri, Mchungaji alipooteshwa serikali iliamini pia. Kwahiyo wewe baki ukiamini redio imani inadharaulika huku yetu yakinyooka. Ebwana kikombe unaenda lini kupata loliondo kiby???
By Kiby
.
Mbona hayo tumeyasikia toka enzi za kina marehem sheikh Ngaliba na kina marehem Mazige? Ni watu wenye kuongea mambo ya kukaririshwa bila kuwa na ufahamu wa wanachokiongelea.
Sasa labda tujaribu kuuliza waislamu wanapolalamikia kitu wanachoita mfumo kristo ni chama gani kimeasisi huo mfumo? Na je watawala waliopo(top five) nchini kwa sasa kutokea hicho chama wanatokea dini gani? Bado hao hao wenzao wanaendelea kutowapa haki? Na je kuna harakati zozote za makusudi kwa waisilamu kukiondoa hicho chama madarakani? Si ni hao hao waislamu waliohimizana misikitini kumnyima kura Muisilamu mwenzao Lipumba na kwa nia ya kumuokoa mkristo? Mwenzao Jk? Tukisema kuwa waislamu ni mazu-zu wanaoamini wasichokitenda na kutenda wasichoamini tuna makosa? Mpaka hapo hawa watu watakaposhinda vita ya iliyo ndani ya nafsi zao wenyewe(njaa kali) hawataweza kujitambua na kuanza kupigana vita yenye maslahi mapana kwa umma mpana zaidi.
Hako karedio imani kameachwa kabwabwaje maana serikali inawajuwa kuwa ni watu wasi madhara. Hawamaanishi kile wanachohubiri. Lakini nakuhakikishia kama ingelikuwa ni radio ya kikristo ingeshafungiwa siku nyingi. Maana ni lazima serikali ihofu kwa hizo kauli maana watakuwa wakijua kuwa zinatolewa na mtu mwenye akili timamu na anaemaanisha kila anachosema.
.
Mjadala ungekuwa mzuri kama Waislamu wanaosema wanaoona wanaonewa wakaorodhesha jambo moja baada ya lingine na wanayoona Wakristo wanapendelewa nayo yawekwe halafu hoja zichambuliwe na kujadiliwa bila kejeli wala matusi ili tuweze kuwa na mshikamano na sio utengano...mijadala ni kwa ajili ya kuleta suluhisho
Mjadala ungekuwa mzuri kama Waislamu wanaosema wanaoona wanaonewa wakaorodhesha jambo moja baada ya lingine na wanayoona Wakristo wanapendelewa nayo yawekwe halafu hoja zichambuliwe na kujadiliwa bila kejeli wala matusi ili tuweze kuwa na mshikamano na sio utengano...mijadala ni kwa ajili ya kuleta suluhisho
Mfano mzuri MoU kati ya serikali na kanisa.. Tuanzie hapo
Mwalimu unayemuita kashata ndiye aliyeongoza ukombozi hata wa juzi,aliyeweza kufanya hivyo before ni MalcomX tu then Ponda. Mwambie kiongozi wenu ajaribu. vp kuna lingine??
By Remote
Leo maalim kashata po,nda anatakiwa akulipe zaidi shughuli uliyoifanya ya kuwaelimisha watu wa mfumo si mchezo hahaaaaa!
[
QUOTE=mnyanyaswaji;4593771]Website ya rc iliyotoa takwimu pia ya idadi ya waislamu na wakristu, na hata tbc zipo, una lingine??
Unaniletea porojo wewe humu JF tunajuana kwa michango yetu ndio maana niliyomjibu kakaa kimya wewe umekurupuka kujibu tu, taasisi ya wapi Kaskazini.
Chadema inakunyima raha sana ndugu yangu,vumilia tu,huwezi pingana na mabadiliko. kama vipi ungana nasi kwasababu huwezi kutusimamisha ktk harakati za ukombozi wa taifa letu.
wanafanya kazi kwa misingi ya katiba na chama chao.
Wangekuwa wanafanya kwa misingi ya uislam tungekuwa na mahakama ya kadhi, tungesha jiunga na oic, kungekuwa na kipengele cha dini kwenye sensa na matakwa mengine ya waislamu yangetekelezwa.
Pili hao wote wapo ktk hizo nafasi kwasababu walipitishwa na vyama vyao baada ya kupigiwa kura na hawakupendekezwa kwa sababu ya dini zao.
Umenielewa mkuu?
Hujaeleweka mkuu.. Ina maana ccm ndio mfumo kristo? Nieleweshe
Hizi dini zote tumeletewa tu. je tunajua asili yake nini. Sometime naona mtawala wa hii dunia hapendi kabisa watu wawe na amani na hutumia uvivu wetu wa kufikiri na kukosa maarifa kutumaliza. Mimi siamini mungu kama ameshawahi kupigana kwa ajili ya kutetea neno lake, ila aliwaadhibu wale ambao walikataa mitume. waTanzania tujue na kutambua kuwa ni nyakati za mwisho na za shida huyo mtawala wa dunia ataleta shida ambazo kwayo tutapewa mashari ambayo si ya kiutu kuyatimiza ili tuweze pata kupona njaa. Kwa macho ya kibinadamu hatuwezi ona ila kwa wale wa roho. Maana tumerithi maagano ya ajabu na ibada za ajabu zilizotuletea mateso mpaka leo. Nadhani ukisema mkristo ni yule haswaa atendaye ya kristo, mwislimu simjui tabia yake. Kwa hivyo Tanzania ya leo ni ya wapagani waabudio vitu na watu maarufu wategemeao lamli je kwa maana hiyo bado ni waumini wa hicho muaminicho. Tunatumika na mtawala wa hii dunia bila kujielewa.
Kwani kutokulalamika maana yake ni kuridhika???
I think, we should stop this. Waislamu na wakristo na wasio na dini, WOTE NI WA TZ. Period.
Utanzania utazingatiwa endapo hakuna kukashifiana dini na kufanyia dhuluma yeyote. Waambie hao walengwa wa kushoto sisi waislam hatuna shida, remember Islam=peace=Amani. Je hapo utakuwa na doubt na sisi?? Naamin akina Ritz wote watakubaliana nami
Hizi dini zote tumeletewa tu. je tunajua asili yake nini. Sometime naona mtawala wa hii dunia hapendi kabisa watu wawe na amani na hutumia uvivu wetu wa kufikiri na kukosa maarifa kutumaliza. Mimi siamini mungu kama ameshawahi kupigana kwa ajili ya kutetea neno lake, ila aliwaadhibu wale ambao walikataa mitume. waTanzania tujue na kutambua kuwa ni nyakati za mwisho na za shida huyo mtawala wa dunia ataleta shida ambazo kwayo tutapewa mashari ambayo si ya kiutu kuyatimiza ili tuweze pata kupona njaa. Kwa macho ya kibinadamu hatuwezi ona ila kwa wale wa roho. Maana tumerithi maagano ya ajabu na ibada za ajabu zilizotuletea mateso mpaka leo. Nadhani ukisema mkristo ni yule haswaa atendaye ya kristo, mwislimu simjui tabia yake. Kwa hivyo Tanzania ya leo ni ya wapagani waabudio vitu na watu maarufu wategemeao lamli je kwa maana hiyo bado ni waumini wa hicho muaminicho. Tunatumika na mtawala wa hii dunia bila kujielewa.
Habari nzima ya uwapo wa mungu imeletwa na watawala ili kuhalalisha utawala wao.
Mungu hathibitishiki kwamba yupo, na ingawa kuamini mungu kunaruhusiwa -kama vile kuamini kuwepo kwa vinyamkera kunavyoruhusiwa, kama kutabaki kuamini- kuwapo kwa mungu si kitu kinachojulikana.
Hivyo, hutakuwa umekamilisha vita dhidi ya udhalili wa hawa wanaotaka kutawala dunia kwa kutumia hii dhana ya mungu kama bado utakuwa unaamini katika uwepo wa mungu.
Allow others to say their say, but always say your piece, it's only right.
Follow Us Here