Nimepigiwa simu na rafiki yangu ambaye yupo Mbeya Wilaya ya Mbarali kuwa vikosi vya FFU vimepiga kambi kule baada ya wananchi kuzuia mwekezaji wa mashamba ya mpunga (NAFCO) kuondoa machine ya kukoboa mpunga iliyokuwepo pale shirikani muda mrefu. Wananchi wanadai ni mwekezaji ni wa muda tu na kila kitu amekikuta na hakuna kuondoka na kitu na wamefunga barabara toka jana hali iliyofanya polisi wa wilayani hapo kuomba msaada wa polisi zaidi kutoka makao makuu ya mkoa ambao wamemwagwa leo pale wakiwa full na bendera nyekungu mikononi.
Inasemekana yamepigwa baadhi ya mabomu ya machozi na kuwakamata baadhi ya viongozi wa wananchi jambo ambalo limeamsha hasira za wananchi hao na sasa wanasema wanalitaka shamba lote lililochukuliwa na mwekezaji huyo. wanadai hakuna kulala hadi hadi haki itendeke.
Mwenye habari zaidi tafadhari tumwagie.
Source: Eye witness

Reply With Quote

Follow Us Here