SERIKALI YA KIDEMOKRASIA vs UHURU WA HABARI - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 22nd December 2006, 02:11 AM   #1
SERIKALI YA KIDEMOKRASIA vs UHURU WA HABARI
BongoTz BongoTz is offline 22nd December 2006, 02:11 AM

Ibara ya kumi na nane (18) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inaeleza waziwazi kwamba: [1] Kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati. [2] Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbali mbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.

Ingawa kumekuwepo na ongezeko la Vyombo vya habari nchini (Redio, Televisheni, Magazeti, Majarida, Internet [Tovuti], Mishito) tangu sera ya habari na utangazaji ilipotolewa kwa mara ya kwanza mwaka 1993; ukweli ni kwamba ongezeko hilo halina maana yoyote ikiwa Idara kuu za serikali kama vile Utendaji (executive), Bunge (legislative) na Mahakama (Judicial) hazioni umuhimu wowote ule wa kufuata sheria-mama (hususani sheria ya uhuru wa habari) ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Binafsi nakubaliana na Mkurugenzi wa mradi wa Excellence in Journalism, Bw. Tom Rosenstiel kuwa vyombo vya habari ni sawa na Idara ya nne ya Serikali ambayo kando na kutoa habari, kuelimisha na kuburudisha jamii; dhima nyingine kubwa ni kuziangalia hizo Idara nyingine tatu za serikali na kuhakikisha kuwa hazifanyi mambo ambayo hazitakiwi kufanya. Hii ni kwa waandishi-wachunguzi kuwaanika wazi wale wanaotumia madaraka yao vibaya kwa kuvunja sheria zilizopo kwa maslahi yao wenyewe, ama kujichukulia njia za mkato kwa lengo la kujineemesha kupitia migongo ya raia wanyonge.

Kwa muda mrefu, vyombo vya habari Duniani kote vimekuwa ndio chanzo kikubwa cha kufichua watenda makosa wa Idara nyingine za serikali. Hili tumelishudia sana katika nchi zilizoendelea. Kadhia ya miaka ya sabini (70s) ya Watergate iliyomlazimisha Rais Richard Nixon kujiuzuru ni mfano mzuri kabisa wa kutizamwa.

Japo Serikali ya Tanzania imeridhia matamko rasmi ya Umoja wa Mataifa, na Umoja wa Afrika kuhusu uhuru wa kutoa na kupokea habari; na pia kutambua kuwa utoaji na upokeaji wa habari ni moja ya haki za msingi za binadamu, inasikitisha kusema kuwa serikali ya Tanzania, inayojitangaza duniani kama "Serikali ya Kidemokrasia" imeshindwa kabisa kuheshimu maridhio hayo na badala yake inatumia sera za vitisho kuwagadamiza wale wote wanaoripoti na kuandika habari zinazopingana na mtizamo wa serikali.

February 12, 2002: Serikali iliamua kuushangaza umma wa watanzania pale ilipotangaza kuwa Jenerali Ulimwengu sio raia wa Tanzania tena! Ati sio raia wa Tanzania? Kwanini?--Kwasababu, akiwa kama Mkurugenzi wa Habari Corporation, Ulimwengu hakusita kuwasha taa iliyomulika na kuanika hadharani maovu yaliyokuwa yanaendeshwa ndani ya serikali na kuwapasha habari wananchi ili wao wenyewe waamue kama kuna kosa limetendeka.

Ni katika kuibua kadhia mbalimbali zikiwemo zile za rushwa ndani ya serikali, ndipo alipoonekana kuwa si Mtanzania halisi. Lakini wakati akipewa vyeo mbalimbali ndani ya chama na serikali kama vile; ukuu wa wilaya (1989-1993), mjumbe wa NEC (1992-1997) na ubuge (1990-1995) suala la uraia halikuwa na tatizo!?

Kadhalika mwandishi-muchunguzi Bw. Richard Mgamba ambaye alikamatwa na sasa anakabiliwa na hatari ya kuvuliwa uraia wake wa Tanzania eti kwasababu tu alihojiwa katika mshito wa Jinamizi la Darwin! Hivi kumbe ni kosa kubwa kiasi hicho kwa waandishi wa habari kueleza mawazo binafsi ikitokea mawazo yao yakatofautiana na mawazo ya viongozi fulani wa serikali?

Ikiwa ndivyo basi, hakuna umuhimu kabisa wa kuwa na katiba kama sheria zilizopo ndani ya katiba hazifuatwi!

Kinachokera zaidi ni sheria mbaya za magazeti na utangazaji [zilizopo] ambazo zinampa Waziri mwenye dhamana ya habari na utangazaji mamlaka ya kuadhibu vyombo vya habari ambavyo vinachapisha au kutangaza taarifa ambazo, kwa tafsiri yake Waziri, zinatishia maslahi ya umma.

Huwezi kwakweli kudai kuwa "serikali yetu ni serikali ya kidemokrasia" wakati sheria za uhuru wa habari zilizopo, zipo kwenye maadishi tu na kwamba, kwa tafsiri yake, Idara ya utendaji ina haki ya kugandamiza na kuadhibu yeyote yule anayetangaza ama kuripoti habari ambazo zinahitilafiana na serikali hata kama habari hizo ni za kweli.

Kuna msemo maarufu usemao kuwa, vyombo vya habari ni kama nuru imulikayo sehemu zenye kiza. Na madhali serikali yetu bado haijaruhusu waziwazi waandishi-wachunguzi kuwasha taa zao na kumulika maovu, kadhia na vitendo vya rushwa vilivyojificha ndani ya Idara mbalimbali za serikali, madai kwamba "serikali yetu ni serikali ya kidemokrasia" ni kejeli tu za kisiasa.

kwa wale waandishi wenzangu wanaotumia Internet [tovuti] ambayo haitawaliwi na sheria yoyote nchini, iweni hodari wala msikubali kamwe kupandisha bendera ya kushidwa! Andikeni habari zote bila kusikiliza vitisho vya Idara ya utendaji. Daima kumbukeni maneno ya aliyekuwa Rais wa Tatu wa Marekani, Thomas Jefferson, aliyewahi kusema, nami namnukuu: "kama inanilazimu niamue kati ya serikali ya kidemokrasia bila ya uhuru wa habari, au uhuru wa habari peke yake, nitachagua habari."

BongoTz
Senior Member
Points: 104,328, Level: 100 Points: 104,328, Level: 100 Points: 104,328, Level: 100
Activity: 1% Activity: 1% Activity: 1%
Join Date: Fri Nov 2006
Posts: 99
Thanks: 1
Thanked 6 Times in 5 Posts
Views: 1198
Reply With Quote
  #2  
Old 22nd December 2006, 02:16 AM
dondola dondola is offline
dondola has no status.
Senior Member
Points: 83,771, Level: 100 Points: 83,771, Level: 100 Points: 83,771, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Tue Nov 2006
Posts: 50
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 24
dondola will become famous soon enoughdondola will become famous soon enoughdondola will become famous soon enoughdondola will become famous soon enoughdondola will become famous soon enoughdondola will become famous soon enoughdondola will become famous soon enoughdondola will become famous soon enough
Default

Naam! Karibu ndugu, endelea kwanza kutapika yoote uliyonayo...
__________________
Thin line between creativity and madness
Reply With Quote
  #3  
Old 22nd December 2006, 05:01 AM
Field Marshall ES Field Marshall ES is online now
Field Marshall ES has no status.
JF Premium Member
Points: 2,215,586, Level: 100 Points: 2,215,586, Level: 100 Points: 2,215,586, Level: 100
Activity: 46% Activity: 46% Activity: 46%
 
Join Date: Thu Apr 2006
Posts: 12,617
Thanks: 1,011
Thanked 1,690 Times in 779 Posts
Rep Power: 91
Field Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the rough
Default

Mzee Bongo,

Lovely utafiti safiii!
Reply With Quote
  #4  
Old 22nd December 2006, 07:45 AM
Mgumu Mgumu is offline
Mgumu has no status.
Senior Member
Points: 128,427, Level: 100 Points: 128,427, Level: 100 Points: 128,427, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Fri Nov 2006
Posts: 233
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 24
Mgumu will become famous soon enoughMgumu will become famous soon enoughMgumu will become famous soon enoughMgumu will become famous soon enoughMgumu will become famous soon enoughMgumu will become famous soon enoughMgumu will become famous soon enoughMgumu will become famous soon enough
Default

Karibu sana Bongo Tz

Siasa za bongo imekuwa kama utani wa simba na yanga, hakuna anayekubali kushindwa, na pindi timu moja ikishindwa basi itapikwa fitna na kutafutwa mchawi.

Upande wa siasa za bongo fitna mbele, ukisema ukweli basi unaonekana mchochezi, fitna itapikwa kuakikisha unafungwa mdomo, na kuwatisha wengine wasithubutu kusema ukweli.

Maisha bora yatapatikana pale viongozi wetu watakapo kubali 'critic as a challenge' and not to take all who critisize the government as enemies.
Reply With Quote
  #5  
Old 22nd December 2006, 08:13 AM
Yebo Yebo Yebo Yebo is offline
Yebo Yebo has no status.
JF Premium Member
Points: 254,800, Level: 100 Points: 254,800, Level: 100 Points: 254,800, Level: 100
Activity: 9% Activity: 9% Activity: 9%
 
Join Date: Mon Nov 2006
Posts: 2,771
Thanks: 853
Thanked 240 Times in 116 Posts
Rep Power: 29
Yebo Yebo will become famous soon enoughYebo Yebo will become famous soon enoughYebo Yebo will become famous soon enoughYebo Yebo will become famous soon enoughYebo Yebo will become famous soon enoughYebo Yebo will become famous soon enoughYebo Yebo will become famous soon enoughYebo Yebo will become famous soon enough
Default

Quote:
View Post
Karibu sana Bongo Tz

Maisha bora yatapatikana pale viongozi wetu watakapo kubali 'critic as a challenge' and not to take all who critisize the government as enemies.

Hilo kufanikiwa tunahitaji viongozi wenye nia na lengo la kuleta maendeleo ya kweli kwa watanzania. Kwa hali ilivyo sasa, hakuna kiongozi hata mmoja wa sirikali ambaye ana nia na malengo hayo. Nia na Malengo yao ni kulinda na kujiongezea maslahi binafsi, na ndio maana wanakuwa hawawezi kuvumilia Free Media.

Hivi, baada ya wananchi kuambiwa kuwa Jen Ulimwengu sio raia; tulikuwa na haki ya kujua sasa hivi ameruhusiwa kuendelea kubaki nchini kwa misingi gani? Hii vacuum ya info haisaidii serikali in the long run.

Last edited by Yebo Yebo; 22nd December 2006 at 08:30 AM..
Reply With Quote
  #6  
Old 22nd December 2006, 08:29 AM
Jafar's Avatar
Jafar Jafar is offline
Jafar a believer in creativity
JF Senior Expert Member
Points: 250,471, Level: 100 Points: 250,471, Level: 100 Points: 250,471, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Fri Nov 2006
Posts: 512
Thanks: 1
Thanked 15 Times in 9 Posts
Rep Power: 25
Jafar will become famous soon enoughJafar will become famous soon enoughJafar will become famous soon enoughJafar will become famous soon enoughJafar will become famous soon enoughJafar will become famous soon enoughJafar will become famous soon enoughJafar will become famous soon enough
Default

Bongo TZ

Makala yako inanikumbusha kile kikatuni cha waandishi wa habari wa bongo kuinama na kulamba viatu vya JK.
Reply With Quote
  #7  
Old 22nd December 2006, 12:59 PM
Game Theory's Avatar
Game Theory Game Theory is offline
Game Theory has no status.
JF Premium Member
Points: 6,834,698, Level: 100 Points: 6,834,698, Level: 100 Points: 6,834,698, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Tue Sep 2006
Posts: 7,285
Thanks: 60
Thanked 425 Times in 178 Posts
Rep Power: 19
Game Theory is an unknown quantity at this point
Default

tatizo la waandishi wa habari wengi bongo wanaandika kwa ushabiki ndio maana watu wanaona bora waje jamboforums kupata latest kuliko huo udaku waanao andika waandishi wetu


kwa hili niko na BEN MKAPA alipowapa ukweli waandishi wa habari wa bongo
Reply With Quote
  #8  
Old 22nd December 2006, 01:52 PM
Ole's Avatar
Ole Ole is offline
Ole Just watching...
JF Senior Expert Member
Points: 280,360, Level: 100 Points: 280,360, Level: 100 Points: 280,360, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Sat Dec 2006
Posts: 950
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power: 25
Ole will become famous soon enoughOle will become famous soon enoughOle will become famous soon enoughOle will become famous soon enoughOle will become famous soon enoughOle will become famous soon enoughOle will become famous soon enoughOle will become famous soon enough
Default

Tatizo sio waandishi wa Habari!

Kama mtakumbuka vizuri editor wa Kulikono na This day alilalamika waandishi kadhaa walifuatwa na kutishiwa maisha yao, Je uliona nani amekamatwa? Vile vile ni culture ya waandishi wa Tanzania kuandika yale ambayo yanawapa chakula. Maana hakuna anayejali - Wabunge wako ziiiiiii, sasa unataka nini?

Wapi umeona waandishi hawaandiki vile mkono wa kula unapotaka, hili ni suala la wananchi wenyewe kuamua na kusema enough is enough. Rais anaibuka na kusema hakuna mkataba feki wa richmond n.k. Payroll yake iko nje tayari, but I'll bet you he won't last mwenyezi mungu atasikiliza kilio cha wengi kama yeye mwenyewe anavyoiombea mvua.
Reply With Quote
  #9  
Old 22nd December 2006, 02:08 PM
Kitila Mkumbo's Avatar
Kitila Mkumbo Kitila Mkumbo is online now
Kitila Mkumbo Thinking independently, deciding collectively!
JF Premium Member
Points: 544,694, Level: 100 Points: 544,694, Level: 100 Points: 544,694, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Sat Feb 2006
Posts: 3,492
Thanks: 25
Thanked 224 Times in 72 Posts
Rep Power: 31
Kitila Mkumbo will become famous soon enoughKitila Mkumbo will become famous soon enoughKitila Mkumbo will become famous soon enoughKitila Mkumbo will become famous soon enoughKitila Mkumbo will become famous soon enoughKitila Mkumbo will become famous soon enoughKitila Mkumbo will become famous soon enoughKitila Mkumbo will become famous soon enough
Default

Kilio cha wengi au cha elites? Hao wengi (80%) si ndio waliomchagua JK na ndo hao wanaoendelea kumpigia makofi kila akipita?
Reply With Quote
  #10  
Old 22nd December 2006, 02:59 PM
Game Theory's Avatar
Game Theory Game Theory is offline
Game Theory has no status.
JF Premium Member
Points: 6,834,698, Level: 100 Points: 6,834,698, Level: 100 Points: 6,834,698, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Tue Sep 2006
Posts: 7,285
Thanks: 60
Thanked 425 Times in 178 Posts
Rep Power: 19
Game Theory is an unknown quantity at this point
Default

Mwanasiasa
I second that
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
habari, kidemokrasia, serikali, uhuru


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Bunge mchezo wa kuigiza - Mbowe Zitto Jukwaa la Siasa 46 2nd August 2009 04:05 AM
Serikali kutisha Vyombo vya habari: Udikteta wenye Ukarimu? Mzee Mwanakijiji Jamii Intelligence 105 12th May 2009 04:44 PM
LOWASSA: Viongozi wapo, au ni mauzauza? Kulikoni Jukwaa la Siasa 111 13th September 2007 10:42 PM
Mapinduzi Bila Damu Wala Wafadhili Shy Habari na Hoja mchanganyiko 0 11th January 2007 09:21 AM
Wingu latanda nyumba za serikali zitakazorudishwa quarz Jukwaa la Siasa 26 4th December 2006 10:13 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 12:01 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com