Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

    Report Post
    Results 1 to 13 of 13
    1. #1
      Gurudumu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2008
      Posts : 2,343
      Rep Power : 1061
      Likes Received
      226
      Likes Given
      104

      Default Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      HALI si shwari ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Maswa, Mkoa wa Simiyu, baada ya viongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho wilayani humo kutakiwa kuachia ngazi kutokana na kuendeleza migogoro ya mara kwa mara na kukidhoofisha.

      Hayo yamejitokeza juzi katika kikao cha Kamati ya Siasa ya wilaya hiyo kilichohudhuriwa pia na viongozi wa ngazi za juu wa Mkoa wa Shinyanga chini ya Katibu Mwenezi wa CCM Taifa, Kapteni John Chiligati, kilichofanyika katika ukumbi ofisi za chama hicho, mjini Maswa.

      Habari za kuaminika kutoka ndani ya kikao, zilisema kuwa Chiligati ambaye pia ni mlezi wa CCM Mkoa wa Shinyanga, alitaka kufahamu kilichosababisha wakakosa viti vya ubunge katika majimbo ya Maswa Mashariki na Maswa Magharibi katika uchaguzi mkuu uliopita.

      Ndipo aliposimama Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Maswa, Jeremiah Shigalla na kueleza kwamba kulikuwa na usaliti uliofanywa na baadhi ya watendaji wa chama hicho na wanachama kwa kukiunga mkono Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hususan Katibu wa UWT wilayani humo, Nuru Mselemo na hivyo kupendekeza atimuliwe.

      Pia waliendelea kumtupia lawama Mselemo kuwa ndiye anaendeleza migogoro ndani ya chama hicho ambaye anatuhumiwa kuchakachua jina la Pili Lameck, katika nafasi ya udiwani wa viti maalum ambaye alishindwa kupata nafasi hiyo licha ya kuongoza kwa kupata kura nyingi katika mkutano mkuu wa UWT wilayani humo.

      Wakati tuhuma hizo zikielekezwa kwa Katibu huyo wa UWT baadhi ya wajumbe walipinga maelezo hayo akiwemo Katibu wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Bakari Mbonde, ambaye alieleza wazi kuwa migogoro ndani ya chama hicho wilayani humo, inasababishwa na Mwenyekiti wa CCM, Peter Bunyongoli, pamoja na Katibu Mwenezi, Jeremiah Shigala, hivyo kupendekeza waondolewe.

      “Baada ya kumtuhumu kwa muda mrefu Mselemu, wajumbe wengine tulikataa kwani tunajua chanzo cha wananchi na wanachama kukichukia chama chetu ni hawa viongozi wawili wa wilaya ambao ni Mwenyekiti, Bunyongoli na Katibu Mwenezi, Shigala,” alisema mzee Bonde.

      Walisema viongozi hao wamekigeuza chama kama kikundi cha watu binafsi, jambo ambalo limezua mgawanyiko mkubwa ndani ya chama hata kushindwa kufanya kazi na makatibu wa CCM wanaoletwa wilayani humo.

      Hata hivyo Chiligati alipata wakati mgumu kujibu sababu hizo, lakini aliahidi kwamba angeyachukua mapendekezo hayo na kuyafikisha katika ngazi ya taifa.

      Katika hatua nyingine, Chiligati alishindwa kuhutubia mkutano wa hadhara uliondaliwa na chama hicho katika viwanja wa MADECO kutokana na wananchi kutohudhuria mkutano huo.

      Chiligati ambaye alipaswa kuhutubia mkutano huo majira ya saa 10:00 jioni kulingana na matangazo yaliyokuwa yakitolewa kupitia vipaza sauti kwenye gari lililozunguka mitaa yote ya mji wa Maswa, hakuna watu waliojitokeza kuhudhuria.

      Ilipofika majira ya saa 11.56 jioni ambapo mwandishi wa habari hizi alikuwepo katika viwanja hivyo, kulikuwa na watu wanne tu wakiwa eneo la mkutano, huku wakilalamika kutokuwa na taarifa ya mkutano huo..

      Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja alipotafutwa kuzungumzia kitendo cha Chiligati kutofika eneo la mkutano alisema kuwa walipata taarifa ya misiba mitatu, hivyo watu hawakuweza kuhudhuria, ndiyo maana waliahirisha.

      Source: Tanzania Daima ya leo ukurasa wa tano


    2. #2
      engmtolera's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st October 2010
      Posts : 3,677
      Rep Power : 5197
      Likes Received
      800
      Likes Given
      672

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Chiligati hauwezi moto wa wasaliti waliomo ndani ya chama,na akumbuke kuwa chama huanguka kutokana na viongozi na wanachama ndani ya chama kuchaguliwa viongozi na ccm taifa
      kwa hiyo ni vizuri chama cha mapinduzi kuanza kubadilika ktk mitazamo yao na ikiwezekana waanze na kumwenguwa makamba na akifuatiwa na chiligati mwenyewe na hizo nafasi zishikwe na wasomi walioiva kisiasa na sio kipropaganda

      msema ukweliiii hapendwiiii daimaaaa

    3. #3
      Ruhazwe JR's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 31st January 2011
      Posts : 3,177
      Rep Power : 2893
      Likes Received
      777
      Likes Given
      723

      Default

      Quote By Gurudumu View Post
      HALI si shwari ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Wilaya ya Maswa, Mkoa wa Simiyu, baada ya viongozi wa ngazi ya juu wa chama hicho wilayani humo kutakiwa kuachia ngazi kutokana na kuendeleza migogoro ya mara kwa mara na kukidhoofisha.

      Hayo yamejitokeza juzi katika kikao cha Kamati ya Siasa ya wilaya hiyo kilichohudhuriwa pia na viongozi wa ngazi za juu wa Mkoa wa Shinyanga chini ya Katibu Mwenezi wa CCM Taifa, Kapteni John Chiligati, kilichofanyika katika ukumbi ofisi za chama hicho, mjini Maswa.

      Habari za kuaminika kutoka ndani ya kikao, zilisema kuwa Chiligati ambaye pia ni mlezi wa CCM Mkoa wa Shinyanga, alitaka kufahamu kilichosababisha wakakosa viti vya ubunge katika majimbo ya Maswa Mashariki na Maswa Magharibi katika uchaguzi mkuu uliopita.

      Ndipo aliposimama Katibu Mwenezi wa CCM Wilaya ya Maswa, Jeremiah Shigalla na kueleza kwamba kulikuwa na usaliti uliofanywa na baadhi ya watendaji wa chama hicho na wanachama kwa kukiunga mkono Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hususan Katibu wa UWT wilayani humo, Nuru Mselemo na hivyo kupendekeza atimuliwe.

      Pia waliendelea kumtupia lawama Mselemo kuwa ndiye anaendeleza migogoro ndani ya chama hicho ambaye anatuhumiwa kuchakachua jina la Pili Lameck, katika nafasi ya udiwani wa viti maalum ambaye alishindwa kupata nafasi hiyo licha ya kuongoza kwa kupata kura nyingi katika mkutano mkuu wa UWT wilayani humo.

      Wakati tuhuma hizo zikielekezwa kwa Katibu huyo wa UWT baadhi ya wajumbe walipinga maelezo hayo akiwemo Katibu wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Bakari Mbonde, ambaye alieleza wazi kuwa migogoro ndani ya chama hicho wilayani humo, inasababishwa na Mwenyekiti wa CCM, Peter Bunyongoli, pamoja na Katibu Mwenezi, Jeremiah Shigala, hivyo kupendekeza waondolewe.

      “Baada ya kumtuhumu kwa muda mrefu Mselemu, wajumbe wengine tulikataa kwani tunajua chanzo cha wananchi na wanachama kukichukia chama chetu ni hawa viongozi wawili wa wilaya ambao ni Mwenyekiti, Bunyongoli na Katibu Mwenezi, Shigala,” alisema mzee Bonde.

      Walisema viongozi hao wamekigeuza chama kama kikundi cha watu binafsi, jambo ambalo limezua mgawanyiko mkubwa ndani ya chama hata kushindwa kufanya kazi na makatibu wa CCM wanaoletwa wilayani humo.

      Hata hivyo Chiligati alipata wakati mgumu kujibu sababu hizo, lakini aliahidi kwamba angeyachukua mapendekezo hayo na kuyafikisha katika ngazi ya taifa.

      Katika hatua nyingine, Chiligati alishindwa kuhutubia mkutano wa hadhara uliondaliwa na chama hicho katika viwanja wa MADECO kutokana na wananchi kutohudhuria mkutano huo.

      Chiligati ambaye alipaswa kuhutubia mkutano huo majira ya saa 10:00 jioni kulingana na matangazo yaliyokuwa yakitolewa kupitia vipaza sauti kwenye gari lililozunguka mitaa yote ya mji wa Maswa, hakuna watu waliojitokeza kuhudhuria.

      Ilipofika majira ya saa 11.56 jioni ambapo mwandishi wa habari hizi alikuwepo katika viwanja hivyo, kulikuwa na watu wanne tu wakiwa eneo la mkutano, huku wakilalamika kutokuwa na taarifa ya mkutano huo..

      Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Shinyanga, Hamis Mgeja alipotafutwa kuzungumzia kitendo cha Chiligati kutofika eneo la mkutano alisema kuwa walipata taarifa ya misiba mitatu, hivyo watu hawakuweza kuhudhuria, ndiyo maana waliahirisha.

      Source: Tanzania Daima ya leo ukurasa wa tano
      mzimu wa damu walioimwaga arusha,kuiba mali za wanyonge+wiz wa kula ndivyo vinawasumbua na wataendelea kutaabika,nawashauli wana ccm wahame mapema kabla aza haijawakuta

    4. #4
      PakaJimmy's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th April 2009
      Posts : 14,916
      Rep Power : 22571
      Likes Received
      6528
      Likes Given
      2936

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Katika hatua nyingine, Chiligati alishindwa kuhutubia mkutano wa hadhara uliondaliwa na chama hicho katika viwanja wa MADECO kutokana na wananchi kutohudhuria mkutano huo.

      Chiligati ambaye alipaswa kuhutubia mkutano huo majira ya saa 10:00 jioni kulingana na matangazo yaliyokuwa yakitolewa kupitia vipaza sauti kwenye gari lililozunguka mitaa yote ya mji wa Maswa, hakuna watu waliojitokeza kuhudhuria.


      Ilipofika majira ya saa 11.56 jioni ambapo mwandishi wa habari hizi alikuwepo katika viwanja hivyo, kulikuwa na watu wanne tu wakiwa eneo la mkutano, huku wakilalamika kutokuwa na taarifa ya mkutano huo.
      .
      Asomaye na afahamu!
      Hawa jamaa hawajaelewa bado kuwa hawatakiwi na mtu eeh?...sijui wanasubiri waone dalili gani!
      How come unategemea uwaone watu mkutanoni, wakati gia yako ya kawaida ni kwenda wakati wa kampeni na Tisheti na kofia?...
      Ukitaka kuwahutubia kikawaida ni lazima pia ulete tisheti na kapelo!...mwosha huoshwa!
      "The only thing that walks back from the tomb with the mourners and refuses to be buried is the character of a man.
      What a man is, survives him... it can never be buried"
      (GENEKAI-Jamiiforums, 4th November 2010 07:32PM).
      [email protected]

    5. #5
      Nicky82's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 14th March 2009
      Posts : 938
      Rep Power : 714
      Likes Received
      57
      Likes Given
      1

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Wakimaliza kutimuana huko wakatimuane na Mwanza na Musoma......wao wakishindwa kwny kura wanashikana uchawi eti wanahujumiwa au eti tumewakopesha wapinzani jimbo!....wanafikiri wananchi wa leo ni wale wale wa enzi za uhuru!


    6. #6
      Babu Lao's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Location : Korokocho
      Posts : 2,021
      Rep Power : 842
      Likes Received
      135
      Likes Given
      71

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Mshaanza kugawanyika wenyewe, safi sana !!!

    7. #7
      Gurudumu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2008
      Posts : 2,343
      Rep Power : 1061
      Likes Received
      226
      Likes Given
      104

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Quote By PakaJimmy View Post
      Asomaye na afahamu!
      Hawa jamaa hawajaelewa bado kuwa hawatakiwi na mtu eeh?...sijui wanasubiri waone dalili gani!
      How come unategemea uwaone watu mkutanoni, wakati gia yako ya kawaida ni kwenda wakati wa kampeni na Tisheti na kofia?...
      Ukitaka kuwahutubia kikawaida ni lazima pia ulete tisheti na kapelo!...mwosha huoshwa!
      Mkuu?

    8. #8
      Mlangaja's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd November 2010
      Posts : 497
      Rep Power : 537
      Likes Received
      94
      Likes Given
      73

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Hili ni fundisho. Safi sana watu wa maswa.

    9. #9
      The Hunter's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th December 2010
      Location : Lubumbashi
      Posts : 910
      Rep Power : 612
      Likes Received
      233
      Likes Given
      128

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Nani yuko tayari kusimama juani kuskiliza porojo, huku hana uhakika wa kunywa hata chai, maana bei ya sukari sasa inamnyima mtu wa chini kunywa chai.
      watatafuta sababu nyingi sana lakini ule mwisho waja.
      Hakuna ca misiba wala nini.
      Kuwa na msimamo katika kile unachoamini ndio utu wako na kwa hivyo utakumbukwa

    10. #10
      mshikachuma's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd December 2010
      Posts : 2,358
      Rep Power : 904
      Likes Received
      435
      Likes Given
      2288

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Quote By PakaJimmy View Post
      Asomaye na afahamu!
      Hawa jamaa hawajaelewa bado kuwa hawatakiwi na mtu eeh?...sijui wanasubiri waone dalili gani!
      How come unategemea uwaone watu mkutanoni, wakati gia yako ya kawaida ni kwenda wakati wa kampeni na Tisheti na kofia?...
      Ukitaka kuwahutubia kikawaida ni lazima pia ulete tisheti na kapelo!...mwosha huoshwa!
      Mkuu hapa umenimaliza

    11. #11
      Msolopagazi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 26th November 2010
      Posts : 492
      Rep Power : 532
      Likes Received
      49
      Likes Given
      19

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Siku hizi wasukuma wameelimika wasifikirie ni wale mamami wa wazamani kwamba unampeleka lupango ukimsalimia anakwambia ndoho tabu wakati anaenda kunyea debe bado ndugu zetu wa kusini kama lindi na mtwara nao wanatakiwa wapewe elimu ya people power ili wawatose wapiga porojo kama kina chiligati na Makamba

    12. #12
      Gurudumu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 5th February 2008
      Posts : 2,343
      Rep Power : 1061
      Likes Received
      226
      Likes Given
      104

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Lakini mimi nina wasiwasi na hii story kidogo. yaani gari lizunguke siku nzima kuhamasisha watu waje kwenye mkutano halafu kwenye uwanja kuwe na muziki wasipatikane hata wale ambao wamezoea kushangaa?

    13. #13
      Mazee's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th December 2007
      Posts : 128
      Rep Power : 618
      Likes Received
      24
      Likes Given
      77

      Default Re: Chiligati Apata Wakati Mgumu Maswa

      Wadau wa Shinyanga Hizi Khabari zina ukweli ndani yake,,,,
      verification please..............

    Similar Topics

    1. Chiligati apata wakati mgumu Maswa
      By Rutashubanyuma in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 3
      Last Post: 4th February 2011, 19:53
    2. Replies: 46
      Last Post: 9th November 2010, 03:54
    3. Mgombea wa CCM apata wakati mgumu Musoma
      By Zak Malang in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 9
      Last Post: 27th October 2010, 22:21
    4. Dk Slaa apata wakati mgumu Kigoma
      By Ngongo in forum Tanzania 2010-2015
      Replies: 21
      Last Post: 11th October 2010, 13:21
    5. Dk.Slaa apata wakati mgumu
      By Mtu wa Pwani in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 2
      Last Post: 10th October 2010, 14:15

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...