Ni aibu kubwa kuwa ombaomba huku tukigawa mali kama njugu!! - JamiiForums |The Home of Great Thinkers

Go Back   JamiiForums |The Home of Great Thinkers > Public Forums > Jukwaa la Siasa


Jukwaa la Siasa Tanzania & World Politics General Discussion Forum. You need to be registered in order to post your comment(s)


Reply
 
LinkBack Thread Tools Rate Thread Display Modes
Old 2nd July 2006, 10:16 AM   #1
Ni aibu kubwa kuwa ombaomba huku tukigawa mali kama njugu!!
awamu3imetulimaza awamu3imetulimaza is offline 2nd July 2006, 10:16 AM

Mkono awashushua wenyeviti halmashauri

na Charles Mullinda

MBUNGE wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono, amewashushia tuhuma nzito wenyeviti wa halmashauri za wilaya ilimo migodi ya dhahabu inayoendeshwa na Kampuni ya Barrick Gold Tanzania kwa kukubali kupokea kodi ya sh milioni 240 kwa mwaka.

Amesema kitendo walichokifanya kimewadhalilisha na kuonyesha jinsi walivyo waroho na wasivyofikiria juu ya athari zinazosababishwa na wawekezaji hao wanapochimba madini.

“Ni ujinga mtupu uliofanyika; yaani walipoona pesa, bila kufikiri wakakubali kuzichukua,” alisema.

Mkono aliyasema hayo jana alipozungumza na Tanzania Daima kwa simu kuhusu hatua ya Kampuni ya Barrick Gold Tanzania kuanza kulipa kodi ya dola za Kimarekani 200,000 sawa na sh milioni 240 kila mwaka kwa halmashauri hizo za wilaya.

Alisema kabla ya kuamua kuzichukua fedha hizo, kulikuwa na ulazima wa kukaa chini na kuangalia uharibifu wa mazingira unaosababishwa na kampuni hiyo, sambamba na kuangalia faida wanayoipata wawekezaji hao kama inalingana na kodi wanayotoa.

“Kulikuwa na ulazima wa kukaa chini na kuangalia jinsi mazingira yanavyoharibiwa, mashimo yanayoachwa baada ya kuchimba, pale kwangu katika mgodi wa Buhemba kuna vifusi vinalingana na mlima. Je, hiyo pesa wanayotoa kwa halmashauri itatosha kufukia kifusi hicho?

“Katika kazi zao, wanatumia vijana wetu ambao wamesoma, hakuna mtu ambaye hana elimu pale. Je, wanachangia nini katika elimu? Hizo fedha wanazotoa zitasaidia katika elimu? Na si elimu tu, barabara, maji na mambo mengi ya maendeleo,” alisema Mkono.

Mbunge huyo alisema kampuni hiyo inatumia vijana wa Kitanzania ambao wamesomeshwa na Watanzania bila kuchangia chochote katika elimu; wanatumia barabara na huduma nyingine za muhimu zilizotokana na jasho la wananchi wa kawaida, huku wakivuna faida kubwa.

Alisisitiza kwamba sh milioni 240 kwa mwaka zilizoanza kutolewa na Kampuni ya Barrick hazitoshi kwa sababu kazi ya kufukia mashimo yaliyotokana na uchimbaji wa dhahabu itahitaji mabilioni ya fedha.

“Nasisitiza ni lazima tuelewe ni kiasi gani cha madini wanachimba na kuchukua kuondoka nayo ili tupime na sisi kiasi kinachostahili watupatie.

“Kuweka wastani wa sh milioni 240 kwa migodi yote, ni upuuzi kwa sababu kuna sehemu ipo dhahabu nyingi kuliko kwingine, sasa kwanini iwe kiasi hicho hicho?” alihoji Mkono.

Alisema kama hoja hizo zingezingatiwa, hata Rais Jakaya Kikwete asingekuwa na sababu ya kwenda kuomba ufadhili kwa ajili ya kujenga chuo kikuu hapa nchini.

“Dhahabu ilikuwepo siku nyingi, lakini ilitunzwa na kuwekewa ulinzi kwa makusudi ili ije isaidie ujenzi wa nchi yetu na maendeleo kwa ujumla, hivi hata wewe unaona ni jambo zuri kwa rais wetu kwenda kuomba ufadhili wa kujengewa chuo kikuu wakati kuna dhahabu lukuki hapa nchini?” alihoji Mkono.

Alitahadharisha viongozi kuwa makini katika kutetea maslahi ya wananchi ili kujiepusha na migogoro ambayo inazikumba nchi nyingine zenye utajiri wa asili kama uliopo Tanzania.

Alitoa mfano wa nchi za Nigeria na Afrika Kusini, ambako kuna machafuko ya kila mara katika maeneo yenye migodi, kwamba yanasababishwa na uonevu wa wawekezaji kwa wananchi ambao ndio wenye mali.

Aidha, Mkono alisema Kampuni ya Barrick inapaswa kushitakiwa kwa kukiuka mkabata wake wa uchimbaji madini ilioingia na serikali.

Alisema Barrick haipaswi kusamehewa kwa kuwadhulumu Watanzania iliotakiwa kuwalipa mrahaba kupitia halmashauri zao za wilaya kwa mujibu wa mkataba, na pia inapaswa ieleze waziwazi imekuwa ikikiuka mkataba wake kwa miaka mingapi.

Mkono alisema mtu yeyote anayevunja sheria ni budi afikishwe mbele ya sheria, jambo ambalo linapaswa kufanyika kwa Kampuni ya Barrick ambayo imedhihirisha kuwa ilikuwa ikivunja mkataba wake kwa kutolipa kodi ambayo iko kwenye mkataba wake tangu ilipoanza shughuli za kuchimba madini hapa nchini.

Kulingana na mikataba ya wawekezaji hao, kodi ya dola 200,000 ilitakiwa kulipwa kwa halmashauri za wilaya husika baada ya kutunga sheria ndogo kuhusu suala hilo, lakini kutokana na usiri uliokuwapo katika mikataba hiyo, hazikuweza kutambua suala hilo.

Hivi karibuni, Kampuni ya Barrick Gold Tanzania ilitoa sh milioni 240 kwa kila halmashauri, ambako imewekeza migodi yake. Fedha hizo zilikabidhiwa kwa wenyeviti wa halmashuri husika katika hafla iliyofanyika mjini Dodoma Juni 14.

Mkono alionyesha kutokubaliana waziwazi na hatua hiyo baada ya kususia hafla ya kukabidhiwa fedha hizo na kuwaeleza waandishi wa habari kuwa hili lilikuwa tukio chafu ambalo hakuwa tayari kulishuhudia likifanyika mbele ya macho yake.

Mkono alikaririwa na waandishi wa habari akieleza kwamba kiwango hicho ni kidogo na kukubali kukipokea, ni kujitia kitanzi kwa sababu kisheria ukipokea hicho kidogo unakuwa umekikubali moja kwa moja.



Swali ni kwanini tumeamua kukaa kimya huku mali yetu ikiedelea kuibwa bila huruma na sisi kugeuzwa kuwa omba omba> Je hizo halmashauri ni nani aliezipa huo uwezo wa kufanya maamuzi ya utumbo kama haya???

kwa madiwani wengi ni darasa la saba huko mara! huo ni ukweli mtupu!
__________________
Hongera Rubabambe na kiranja wenu namba moja, na wengine mliotajirika kwa kutuuza!

awamu3imetulimaza
Junior Member
Points: 106,348, Level: 100 Points: 106,348, Level: 100 Points: 106,348, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
Join Date: Sun Jul 2006
Posts: 1
Thanks: 0
Thanked 0 Times in 0 Posts
Views: 4540
Reply With Quote
  #2  
Old 2nd July 2006, 04:05 PM
Ogah Ogah is offline
Ogah is Omnipotent
JF Premium Member
Points: 5,280,770, Level: 100 Points: 5,280,770, Level: 100 Points: 5,280,770, Level: 100
Activity: 13% Activity: 13% Activity: 13%
 
Join Date: Fri Mar 2006
Posts: 3,412
Thanks: 1,392
Thanked 383 Times in 211 Posts
Rep Power: 2031
Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!Ogah is one of most respected JF members!
Default

Ndg Mkono,

Pongezi, umeongea vema sana, however, ulikuwa wapi siku Bi Maua Daftari aliposema mikataba ni SIRI?, tulitegemea watu Wanasheria kama ninyi (Mliobobea + Mbunge) kupiga sana kelele kuhusu kauli ya Daftari,............. wanasheria mna usemi wenu "silence means YES" sasa naona UNAPIGIA KELELE END RESULT baada ya kukubali kilichosemwa bungeni!!!. mimi nikiwa mmoja wa wanachi wako tuliokupa kura nachelea kuona unachosema ni honest!

Kama unasoma hii forum, tafadhali panga mikakati ya kupeleka hoja Bungeni ili wabunge kama ninyi muwa na nafasi ya kui-review mikataba kw amanufaa ya sisi wananchi
Reply With Quote
  #3  
Old 2nd July 2006, 09:41 PM
Field Marshall ES Field Marshall ES is offline
Field Marshall ES has no status.
JF Premium Member
Points: 2,216,928, Level: 100 Points: 2,216,928, Level: 100 Points: 2,216,928, Level: 100
Activity: 46% Activity: 46% Activity: 46%
 
Join Date: Thu Apr 2006
Posts: 12,622
Thanks: 1,015
Thanked 1,698 Times in 782 Posts
Rep Power: 91
Field Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the rough
Default

Huyo Mbunge ambaye ni mwizi mkubwa wa mali ya serikali anapaswa kuwa mtu wa mwisho duniani kuongelea mambo ya wizi, huyu ambaye kila siku anafanya mipango ya ujanja kupewa tenda za serikali za sheria na kui-over charge serikali kwa kugawana na mawaziri leo anaweza kuthubutu kuwatukana viongozi wa manispaa? Ama kweli nyani haoni his behind?

Hela za kuilipia ile ndege aliyomkodishia mgombea mmoja wa urais wa CCM kuzunguka bongo nzima kutafuta signatures, alizipata wapi? Kama kawaida wananchi wa bongo wataendelea kudanganywa tu na waizi kama huyu!
Reply With Quote
  #4  
Old 3rd July 2006, 01:13 AM
Mkandara Mkandara is offline
Mkandara Aviator
JF Premium Member
Points: 580,633, Level: 100 Points: 580,633, Level: 100 Points: 580,633, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Thu Mar 2006
Location: T dot
Posts: 7,289
Thanks: 463
Thanked 747 Times in 325 Posts
Rep Power: 80
Mkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the rough
Default

Mzee Es,
Samahani mkuu lakini, kuna kuna wakati nashindwa kuelewa kama kweli wewe ndiye Mzee Es aama kuna mtu anatumia jina lako. Nakuona umepooza sana kwa hoja mzee vipi umeishiwa?

Swala hapa ni hili la Barricks Gold na uhalali wa viongozi wetu kukubali kupokea hizo dola laki 2 kama ruzuku kwa halmashauri hali fedha hizi hazikupigiwa hesabu ya kimapato kama inavyotakiwa.
Huyu mbunge hata kama anayo mabaya yake hii ni kesi nyingine kabisa na unaweza kuiweka hapa tukaijadili kwa mapana lakini kuchukua hoja kwa kutazama nani kasema sidhani kama ni mwendo mzuri.
Labda mwenzetu unakubaliana na mikataba ya madini na vizuri utuambie hayo mazuri yake nasi tupate kuona ukichaa wa huyu mbunge.
__________________
Exploration of reality
Reply With Quote
  #5  
Old 3rd July 2006, 10:36 AM
Mkwawa Mkwawa is offline
Mkwawa has no status.
Member
Points: 87,422, Level: 100 Points: 87,422, Level: 100 Points: 87,422, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Sun Jul 2006
Posts: 37
Thanks: 0
Thanked 1 Time in 1 Post
Rep Power: 0
Mkwawa will become famous soon enoughMkwawa will become famous soon enoughMkwawa will become famous soon enoughMkwawa will become famous soon enoughMkwawa will become famous soon enoughMkwawa will become famous soon enoughMkwawa will become famous soon enoughMkwawa will become famous soon enough
Send a message via ICQ to Mkwawa
Default

Mzee ES, Mkono ni tajiri toka siku nyingi ana kesi ntinyi za kimataifa ana hela siyo kwa kuibia nchi. Ni kweli kama alivyosema Mkandara wakati mwingine unamchesha siyo kwa kutojua ila tu kwa chuki zako binfasi na kundi la mwalimu!

sijui mwl na kundi lake walikukosena nini??


Hivi kweli mambo anayaofanya mkono jaribu kwenda uone katika jimbo lake ! ni mkono huhyu huyu alieyatamka wazi bungeni waktai wa awamu ya Mkapa na kukemea kuhusu uuzwaji wa nyumba za serkali lakini wabunge wengine wote wlaikaa kimya! ninamnukuu" alisema mimi siyo mjamaa lakinini kwa hili la uuzinaji wa nyumba za serkali kana kwamba baadaya ya hii serkali hakutakuwa na serkali nyingine au tunaenda mbinguni ni ajabu kubwa na inatia shaka kama kweli nyie ni wajamaa!!

Mzee ES tunaheshimu michango yako lakini jaribu tu kidogo kupunguza upenze na chuki zisiso za maana utakuwa kiongozi mzuri hapa kazi yetu ni kufundishana na kukosoana! Mimi Mkwa sasa nimeongia kwa nguvu mpya katika hii Formu ninaipenda kwa sasabu nimeona kuna watu wenye tofauti katika mitizamo na michango yao wote ni mizuri.
Reply With Quote
  #6  
Old 3rd July 2006, 10:50 AM
Mkira Mkira is offline
Mkira has no status.
Senior Member
Points: 207,197, Level: 100 Points: 207,197, Level: 100 Points: 207,197, Level: 100
Activity: 0% Activity: 0% Activity: 0%
 
Join Date: Wed May 2006
Posts: 231
Thanks: 0
Thanked 1 Time in 1 Post
Rep Power: 24
Mkira will become famous soon enoughMkira will become famous soon enoughMkira will become famous soon enoughMkira will become famous soon enoughMkira will become famous soon enoughMkira will become famous soon enoughMkira will become famous soon enoughMkira will become famous soon enough
Send a message via ICQ to Mkira
Default

Mwakapungi unasema kweli? au na wewe ni mmoja wao!

http://www.ippmedia.com/ipp/guardian.../03/69547.html



Huyo Mkono tumeskia kazi zake, sasa hilo la deal za kupata kesi mimi silijui ila tu kama alivyosema Mkwawa insemekana jamaa anapta international case.

Hilo la kutoa la kutoa hela wakati wa Kampeni tukianza kuulizana hapa itakuwa kazi wenye katika CC ya CCM liliwashinda! Kikwete alitumia Kiasi gani alipta wapi? Malecela alikodi ndge alipoulizwa alisema rafikia yake alimlipia! hilo ninadhani tuliache kampeni zimeisha na makundi yaishe taratibu japo walioshindwa itawachukua miaka 20 kukubali!
__________________
"True peace is not merely the absence of tension, it is the presence of justice'' Dr.Martin Luther King Jr
Reply With Quote
  #7  
Old 3rd July 2006, 11:39 AM
Field Marshall ES Field Marshall ES is offline
Field Marshall ES has no status.
JF Premium Member
Points: 2,216,928, Level: 100 Points: 2,216,928, Level: 100 Points: 2,216,928, Level: 100
Activity: 46% Activity: 46% Activity: 46%
 
Join Date: Thu Apr 2006
Posts: 12,622
Thanks: 1,015
Thanked 1,698 Times in 782 Posts
Rep Power: 91
Field Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the roughField Marshall ES is a jewel in the rough
Default

Hebu nijaribu kuwaelewa wazee,

Mwizi mmoja kwa sababu akiiba anawasaidia wananchi, na kwamba anapewa njia za kuiba mpaka nje ya nchi kwa kuwatumia viongozi wetu wa nchi na kugawana nao, na kwamba ameanza kuiba siku nyingi, basi it is ok kwake kuwatukana wezi wengine wa serikali wadogo wadogo!

Mkandara ni kweli bro kuwa sasa wewe ndiye bingwa wa issues na maneno yako humu kwenye hii forum ndio ukweli wenyewe,

lakini samahani, ninamjua Mkono tena na deal zake zote, Mkono ni another bongo Mafiya kama Mtandao nilishamzungumza toka BCS, na sikukusikia ukisema kitu, two wrongs haziwezi ku-make right, Mkono ni mwizi kama hao anaowapigia kelele na anapaswa kuwa mtu wa mwisho kuwauliza wezi wenziwe nuless kama hakupata mgawo kwenye hayto madini! Hayo maneno mengine nimeyazoea that is why I am ES!
Reply With Quote
  #8  
Old 3rd July 2006, 03:03 PM
Jasusi Jasusi is online now
Jasusi is a truth seeker
JF Premium Member
Points: 279,252, Level: 100 Points: 279,252, Level: 100 Points: 279,252, Level: 100
Activity: 18% Activity: 18% Activity: 18%
 
Join Date: Fri May 2006
Posts: 4,188
Thanks: 1,149
Thanked 633 Times in 318 Posts
Rep Power: 32
Jasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enoughJasusi will become famous soon enough
Default

Mzee ES,
Be that it may that Mkono is a thief. Does that take away anything in his message? Should he just keep quiet and watch these foreigners continue to plunder our wealth. Like Mkandara says we can debate Mkono's thievery in another forum. Let us focus on his message for now.
Reply With Quote
  #9  
Old 3rd July 2006, 04:41 PM
Mkandara Mkandara is offline
Mkandara Aviator
JF Premium Member
Points: 580,633, Level: 100 Points: 580,633, Level: 100 Points: 580,633, Level: 100
Activity: 3% Activity: 3% Activity: 3%
 
Join Date: Thu Mar 2006
Location: T dot
Posts: 7,289
Thanks: 463
Thanked 747 Times in 325 Posts
Rep Power: 80
Mkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the roughMkandara is a jewel in the rough
Default

Mzee Es,
Siku zote wewe bingwa ktk kuendesha hoja ndani ya mada. Na mara kadhaa nimeona watu wakitaka kutafsiri hoja zako nje ya mada kwa sababu umehusisha mtu wasiomtegemea ndani ya mada husika. Kwa mtazamo huo nimekuwa nikikubaliana nawe kwa sababu walitaka kukutoa nje ya mada. Kwa hiyo binafsi huangalia mada yenyewe, hoja inayohusika kisha huitazama shilingi yangu kwa malengo ya kutafuta reality ama correct way ya ku-deal na swala hilo. Mara nyingi nimejikuta nakubaliana na wewe kwa sababu hizo hizo na sio swala la Right or Wrong! kwani hatupo kanisani wala msikitini hapa.

Lakini hapa Mzee Es kidogo umetoka nje. Wana mtandao umewasema sana kwa mabaya na mazuri yanayotokea ndani ya hoja ama mada yenyewe. Wengine tumeshindwa kuamini hadi yalipotokea kweli.
Kwa mfano hapo zamani ungesema mambo kibao ya MKONO yanayohusu yeye na madini na jinsi alivyotaka kuwafanyizia watu wa Mara. Ama uhusiano wa Mkono na Jambazi fulani la madini.
__________________
Exploration of reality
Reply With Quote
  #10  
Old 3rd July 2006, 05:50 PM
FairPlayer's Avatar
FairPlayer FairPlayer is offline
FairPlayer is rolling ball fairly
JF Premium Member
Points: 726,671, Level: 100 Points: 726,671, Level: 100 Points: 726,671, Level: 100
Activity: 2% Activity: 2% Activity: 2%
 
Join Date: Mon Feb 2006
Location: UK
Posts: 3,363
Thanks: 52
Thanked 185 Times in 122 Posts
Rep Power: 30
FairPlayer will become famous soon enoughFairPlayer will become famous soon enoughFairPlayer will become famous soon enoughFairPlayer will become famous soon enoughFairPlayer will become famous soon enoughFairPlayer will become famous soon enoughFairPlayer will become famous soon enoughFairPlayer will become famous soon enough
Default

WanaTEF,

Nionavyo afadhali ya huyu Mkono anayeiba kisha kurudisha baadhi kwa wananchi kuliko hao manyang'au mengine kama Mahalu. Alichokemea ni sahihi na hili alilianzia toka siku ya kukabidhiwa hizo hela.

ES kutofautiana ni jambo la kawaida miongoni mwa watu, Unaweza kuwa upo sahihi lakini sio kwenye hii mada. Nami naungana na wengine kusema umeteleza kidogo na kutoka nje ya mada.

FD
__________________
A positive thinker!
Reply With Quote
Reply

Bookmarks

Tags
aibu, huku, kama, kubwa, kuwa, mali, njugu, ombaomba, tukigawa


Currently Active Users Viewing This Thread: 1 (0 members and 1 guests)
 
Thread Tools
Display Modes Rate This Thread
Rate This Thread:

Posting Rules
You may not post new threads
You may not post replies
You may not post attachments
You may not edit your posts

BB code is On
Smilies are On
[IMG] code is On
HTML code is Off
Trackbacks are Off
Pingbacks are Off
Refbacks are On


Similar Threads
Thread Thread Starter Forum Replies Last Post
Katiba ya Tanzania: Ilivyo na mapendekezo ya mabadiliko mzeewabusara Jukwaa la Siasa 489 6th November 2009 07:09 AM
Bunge mchezo wa kuigiza - Mbowe Zitto Jukwaa la Siasa 46 2nd August 2009 04:05 AM
Hoja Nzito: Makala mbalimbali maggid Jukwaa la Siasa 17 13th June 2007 08:55 AM
Mapinduzi Bila Damu Wala Wafadhili Shy Habari na Hoja mchanganyiko 0 11th January 2007 09:21 AM

Tuma Ukurasa huu kwa rafiki yako!


All times are GMT +3. The time now is 01:29 AM.

Powered by JamiiForums.com
Copyrights reserved to JamiiForums.com