Kwa mtazamo wangu, mtoa mada ana hoja mbili, ya kwanza ni kutokuwepo uhakika wa UBORA wa ARVs, na pili ukosefu wa wafamasia wa kutosha, naomba nichangie kama ifuatavyo.
1.Tatizo la UBORA wa ARV.
Kwa maoni yangu, ni vigumu sana kutoa kauli ya kuthibitisha kwamba ARVs hazina ubora unaotakiwa kwa maneno tu. Tunahitaji ushahidi wa kisayansi wa aina mbili, ya kwanza ni Ushahidi wa maabara, huu utatuonyesha kwamba ARVs zinazotumika hazikidhi viwango vya ubora, na njia ya kupata ushahidi huu ni kupata data (kama zipo) toka mamlaka husika ambayo ndio hushughulika na mambo ya ubora wa dawa kwa kupitia kitengo chake cha Quality Assurance. Kwa kawaida Dawa yoyote inapoingizwa nchini lazima iwe registered, na ili iwe registered lazima itimize vigezo vyote vya ubora (siwezi kuvitaja hapa kwani ni shule nyingine). Na kama ikitimiza inaingia sokoni, na ikishaingia sokoni kuna ufuatiliaji mwingine unaitwa Post-market surveillance, kwa maana ya kufuatilia ubora wake ikiwa sokoni, huu ni muhimu sana kwani utaonyesha kama dawa iliyoikuwa registered ina'maintain' ubora wake. Tunahitaji kupata hizi data za hii post-market surveillance hasa kwa ARVs zinazotuhumiwa kukosa ubora ili kuthibitisha au kukanusha UBORA wa hizo ARVs. Mwenye uwezo wa kupata hizo data atupe au afuatilie kwani zitatusaidia kupata picha halisi.
2.Njia nyingine ambayo si nzuri au sio ya uhakika sana ya kupima ubora wa dawa ni pale ambapo mgojwa au wagojwa wanaotumia dawa hiyo hawapati nafuu inayotarajiwa katika muda fulani, yaani kama ni mgojwa anayetumia ARVs kwa kufuata maelekezo sahihi, tunategemea kuwa atakuwa na improvement clinically, yaani kuongezeka uzito, kupungua kwa magonjwa nyemelezi n.k. Kingine ni kuongezeka kwa chembechembe za kinga (CD4) na kupungua kwa virus mwilini. Kama haya hayatokei KWA WAGONJWA WENGI, sababu mojawapo inaweza kuwa ni ukosefu wa ubora wa dawa.Tunahitaji data kwa hili pia, ila hii inaweza kuwa research ya Phd.
CHA MSINGI ni kuwaomba TFDA na mamlaka husika wahakikishe ubora wa dawa unakuwepo kwa kufanya chunguzi za kisayansi na KUUELIMISHA umma dalili mbalimbali za dawa zisizokuwa na Ubora
UKOSEFU WA WAFAMASIA
Kweli ni wachache na wengi wako mijini, na kwa uchunguzi wangu naona hata hao wa diploma hawatoshi, kuna vyuo sidhani kama vinazidi viwili nchini kote. Pamoja na uchache wao sijaona kama wana ORGANISATION yao na kama ipo sijaisikia. Ninaamini wanaweza kutumia elimu yao kuufahamisha umma na kushauri kuhusu mambo haya muhimu.
Wafamasia wafikirie jinsi ya kuungana na fungua shule zaidi, na serikali isaidie katika hili.Kuna vyuo vingi vya AMO, nurses, lakini vya wafamasia ni vichahce mno, AU HAWAHITAJIKI? Inawezekana kazi zao huweza kufanywa na Nurses, na inawezekana umuhimu wao hauonekani Sijui kama hilo ni la kweli!!!!Mimi siamini!!!
Ninaamini kwa elimu walioipata hawa (Four Years) wanaweza kufanya zaidi ya wanavyofanya sasa kwani wengi wapo kwenye madirisha ya kutolea dawa tu,kazi ambayo pia hufanywa na technicians na wenye certificate. Naiomba Wizara ikae na hawa jamaa ili waone ni jinsi gani wanaweza kutumiwa kikamilifu kwenye shughuli za afya kwani kwenye nchi nyingine Pharmacists hufanya zaidi ya haya yanayofanywa hapa Bongoland.
Peace be with You.
Follow Us Here