Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
Stori: Makongoro Oging'
SERIKALI imethibitisha kuwa kitendo alichokuwa akifanya babu wa Loliondo, Mchungaji Ambilikile Masapile, cha kutoa dawa ya kutibu magonjwa, ukiwemo Ukimwi aliyokuwa amedai kuwa ameoteshwa na Mungu ni cha kitapeli.
Utafiti umebaini kwamba dawa hiyo ya babu wa Loliondo ni feki na kwamba haina uwezo wa kutibu Ukimwi wala kisukari.
Kwa mujibu wa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Hussein Mwinyi (pichani), utafiti wa kulinganisha wagonjwa wa Ukimwi na kisukari waliokunywa dawa hiyo na wale ambao hawakunywa, umebaini kwamba hakuna utofauti wa afya ya mgonjwa.
Alisema utafiti huo unafanywa na Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMRI), ulianza Machi mwaka huu na kwamba unahusisha wagonjwa 200 wanaofuatiliwa kwa kupimwa damu, kinga ya mwili (CD4) na uzito wa mgonjwa, ambao ulifanyika tangu mgonjwa alipokunywa kikombe cha babu.
“Matokeo ya awali ya utafiti yameonyesha kuwa hakuna utofauti katika vipimo vya kimaabara pamoja na damu, CD4, uzito na ubora wa afya ya wagonjwa kati ya waliokunywa na wale ambao hawakunywa dawa ya mchungaji,” alisema Dk. Mwinyi.
Alisema lengo la utafiti huo ni kubaini uwezo wa dawa hiyo katika kutibu magonjwa aliyosema dawa yake inayatibu ili kuona kama kuna utofauti wowote baada ya mgonjwa kutumia dawa.
Kufuatia hali hiyo, jeshi la polisi nchini limesema kwamba linafuatilia kwa makini sakata la Mchungaji Masapile anayeishi katika kijiji cha Samunge mkoani Arusha kufuatia malalamiko ya wananchi kuwa licha ya dawa yake kuonekana haitibu, bado watu wanakwenda na kunywa.
Akizungumza na gazeti hili hivi karibuni ofisini kwake makao makuu ya jeshi hilo jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Advera Senso, amesema kwamba kutokana na malalamiko hayo polisi watawasiliana na wizara ya afya ili kuchukua hatua stahiki.
Msemaji huyo amesema kwamba wanataka kujua kama wizara ya afya imepiga marufuku dawa hiyo au inasema nini baada ya kubainika kuwa haitibu na amewataka wananchi kutoenda huko.
Wananchi wengi waliozungumza na gazeti hili wamedai kwamba Babu amewatapeli wananchi na kinachowauma ni kuona kuwa kuna watu wanaendelea kwenda kunywa kikombe japokuwa hawatangazwi.
“Wananchi wengi waliuza mali zao na kukimbilia kwa babu kupata tiba, kumbe ulikuwa ni utapeli, ukweli ni kwamba serikali imechelewa mno kutoa tangazo hili,” alisema mwananchi mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja tu la John.
Naye Mwenyekiti wa Mtandao wa Vyama vya Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi nchini (TAMOPHA), Julius Kaaya, ameitupia serikali lawama kwa kuipigia debe dawa ya Babu na kuwafanya wagonjwa kutoroka hospitali huku wengi wao wakiacha kuendelea na dawa wakiamini wangepona baada ya kunywa kikombe kimoja .
“Huyu Babu inatakiwa ashitakiwe apelekwe mahakamani afilisiwe mali zake zote alizochuma toka kwa wagonjwa na ikiwezekana afungwe ili iwe fundisho kwa watu wengine,” alisema Kaaya na kuongeza kuwa wao wanajiandaa kumfungulia kesi.
Mchungaji wa Kanisa la Pentekoste (TAG) Mkoani Arusha, Steve Wambura, amemtaka babu huyo amrudie Mungu kwa kutubu kuwa aliwatapeli wananchi.
Naye Mwenyekiti wa Waganga wa Tiba Asili Mkoa wa Dar es Saalam, Maneno Tamba, amesema babu huyo siyo mwanachama wao na walishangazwa na serikali kumpigia debe, hali iliyosababisha vifo vya watu wengi waliomkimbilia na kuacha tiba sahihi.
Baadhi ya mawakili, akiwemo Mabere Marando wamesema kwamba wapo tayari kumfikisha mahakamani babu huyo wakijitokeza waliotapeliwa na watamfungulia kesi ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu.
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
Vyombo vya habari navyo havikuwa nyuma kupigia debe 'dawa' hiyo ya kitapeli ...
Angalia article hii kwenye Guardian la 29th march 2011.
'Babu' cupful gets initial nod
By Patrick Kisembo
29th March 2011
The concoction has no harm on human beings - researchers PM: Govt to create conducive environment for pastor`s services
Retired pastor Ambilikile Masapile
Ministry of Health and Social Welfare has endorsed the “miracle cure” administered by retired pastor Ambilikile Masapila (his proper names) as fit for human consumption, adding however that efficacy tests were going on.
“It is a long process which cannot be completed in a short period of time,” said Tanzania Food and Drugs Authority Acting Director General Charys Ugullum when unveiling results of the laboratory analysis on the sample of the “miracle cure” to journalists in Dar es Salaam yesterday. “The investigation which has been conducted so far has yielded satisfactory results that the measurement used by “Babu” in dispensing the concoction is not harmful to human beings,” she said, adding: “So far we are satisfied by its safety.”
She however said that the researchers were continuing with investigation into whether the herbal medicine can cure the five diseases as claimed by pastor Masapila.
“This task, implemented according to world scientific rules and regulations, takes a long time to achieve acceptable national and international standards,” Ugullum said.
She said the researchers were also following up on the health of some 200 patients who have taken the herbal medicine.
“These patients have volunteered to be involved in the investigation to know their health status after taking the medication,” Ugullum said.
She said the government was planning to make a follow up on the use of the “treatment tree” in other parts of the country because there were reports that it has been used by other tribes like Wagogo, Maasai, Wabarbaig and Wasonjo. The investigation team included people from TFDA, Muhimbili University for Health and Allied Sciences, Government Chemist and National Institute for Medical Research (NIMR).
"Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi. " - Yakobo 04:17
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
By Tram Almasi
Hapo kwenye red hapoo, ina maana hata watafiti wa NIMRI na wengine wamepata false results kwa kuwa wameipeleka dawa nje ya eneo husika. Na je, walipoichukua kwa ajili ya utafiti walipata ruhusa ya babu?
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
Nchi ya Wajinga huongozwa na wajinga na hutapeliwa viile vile.. Tuliyasema haya toka mzee huyu alipojitokeza watu wakatuona wajinga.
Sasa ebu jiulizeni ni viongozi wangapi walienda Loliondo wakapa kikombe, halafu mnataka kuongozwa na kundi la watu wanaoamini sana uchawi na Utapeli wa watu wanaodai kwamba wao wako karibu sana na Mungu na mkawaamini..
Umaskini wetu sio bure, sisi kichwani hamna kitu..
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
By Mu-Israeli
Hilo sharti la 'kutotoka na dawa nje ya Loliondo' ndio lilikuwa sharti kuu la kuwezesha wagonjwa 'kupona'.
Hapo ndio uongo wake ulipokuwa wazi kabisa.
Watu ilibidi washtuke hapo, maana, haiingii akilini kusema kuwa 'dawa' haifanyi kazi nje ya Loliondo, halafu dawa hiyo-hiyo ichukuliwe ikachunguzwe nje ya Loliondo !!
Hatimaye, NIMR wakatoa tamko kuwa 'dawa' haina madhara !!
NIMRI na hata TFDA were right kusema dawa haina madhara kwa sababu haidhuru. lakini uwezo wa kutibu (pharmacological efficacy) ndio ''zero'' Mkuu.
"YouR MoST UNhaPPy CuSToMers ArE YoUr GREateST SOurCE Of LEarNInG"- BiLL GaTEs
Huyo mchungaji aliwatahadharisha wananchi kuwa wasiache kutumia madawa yao ya hospitali. Kwa uzembe wa Serikali na wakapuuza ushauri wake wa katazo wakaenda kwa kasi kubwa. Leo wasimulaumu kwa kuwa alitoa tahadhali sisi watu makini hatukwenda, lakini pia bei ya dawa yenyewe ilitia mashaka. Wamuache babu wasimuletee shida, maana hata Prof. Maji Marefu baada ya kutapeli watu sasa hivi ni Mbunge mbona hamjapiga kelele. Serikali DHAIFU.
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
Bado upumbavu anaendelea.
Hivi Babu alikuwa anatoa risiti kwa waliokunywa 'Kikombe' chake? Unawezaje kuthibitisha kuwa ulikuwa mteja wake?
Pili, kuna aliyelazimishwa kwenda Loliondo? Babu wala hakutoa matangazo mahali popote. Watu walimfuata nyumbani kwake kwa hiari zao. Na aliwaonya kuwa dawa yake inaendana na imani. Sasa kama hamkupona kwa kukosa imani yeye angefanyeje?
Waliokwenda kwa Babu nyote mgeona aibu, kufunga midomo yenu na kuficha nyuso zenu kwa sababu ni wapumbavu. Sina nia ya kutukana mtu ila ni kuelezea hali.
Wa kushitakiwa ni watu wakubwa kama mawaziri, wakuu wa mikoa hata maaskofu, ambao walishabikia na kwenda huko bila kuwa na ushahidi wowote kuhusu hiyo dawa. Wao ndiyo walitoa mfano mbaya na kuzidi kuhamasisha watu.
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
wa kulaumu ni pamoja na viongozi wa serikali na wa ccm (jk, salma, el, lusinde, makamba, kandoro, mwigulu, etc. ) ambao pamoja na wake zao walishiriki ktk kufanikisha huu utapeli kwa kunywa `uchafu ` huo. inasemekana lengo lilikuwa ni kuondoa habari za cdm kwa muda kwenye media outlets zetu
'... Knowledge is good, but wisdom is even better ...'
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
Babu kateseka sana maisha haya, katuliza kichwa kaja na mchongo wake makini wa uzeeni mnaanza kumletea gozigozi acheni zenu kwani Hosea yeye sie polisi mbona kalambishwa kikombe, nasikia mpaka mkuu wa kaya kalamba na hajadondoka tena jukwaani........ yaoneni kwanza!
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
maarifa ya Mungu huanzia kwenye upumbavu wa mwanadamu. Swala la imani lilithibitishwaje maabara?siku za kuishi za watu waliokunywa dawa je, zilirekodiwa kabla ya kunywa dawa ili zilinganishwe kama ziliongezeka ama kupungua?
Ingekuwa kwa wenzetu serikali nzima ingeachia ngazi. Huwezi kuachia watu watumia dawa then baadae ndio unasema ni utapeli!
Ni kweli ndugu.Viongozi wangapi wa serikali walienda kunywa dawa hiyo na wakaipigia debe,leo babu ndio mwenye makosa.SERIKALI HII YAANI NI DHAIFU SANA.Hawataki kuboresha huduma za afya ili kuhalalisha watu wakaliwe na waganga wa kienyeji.
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
By egbert44
Babu kateseka sana maisha haya, katuliza kichwa kaja na mchongo wake makini wa uzeeni mnaanza kumletea gozigozi acheni zenu kwani Hosea yeye sie polisi mbona kalambishwa kikombe, nasikia mpaka mkuu wa kaya kalamba na hajadondoka tena jukwaani........ yaoneni kwanza!
Mkuu hapo nakubaliana nawewe, sioni kosa la Babu, hakulazimisha mtu yeyote kumfuata na bado waliomfuata aliwataadhalisha. katusaidia kutuelewesha aina ya watu tulionao katika nchi yetu.
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
serikali ndio ilifanya makosa na ndio imesababisha watu wengi wafe kutokana na dawa ya babu maana mpaka mawaziri walienda kupata kikombe na pengine hata jk aliletewa ikulu kwa siri siri
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
Mambo yanayokwenda kiimani ni vigumu kuchukuliwa hatua za kisheria wengi wanadanganya au kwa kuwa hawatoi dawa mfano Kakobe, Lusekelo na wengineo kwa nini nao wasichukuliwe hatua kwa kutapeli juu ya kutibu watu UKIMWI kwa maombezi wakati sio? Mzee wa Gombe, Nkono na viongozi wengi sana wa Taifa hili walikunywa dawa hiyo tunasikia na mkuu wa kaya pia sasa isiwe wanataka kumuadhibu babu wa watu kwa sababu ya uzembe wao wenyewe wa kujipeleka na kunywa hiyo dawa.
re: Imethibitishwa na Serikali... Babu wa Loliondo ni Tapeli
By Amiliki
Kweli hapa Serikali Hatuna. Yaani kama ingekuwa ni sumu mpaka leo ndio serikali inastuka, je wangekuwa watu wangapi wamepoteza maisha?
Mkuu malizia tu kwamba viongozi wetu walikunywa sumu,maana karibia serikali yote ilikwenda huko na kupata kikombe kwa uthibitisho huo wa serikali inamaanisha viongozi wetu wa nchi walitapeliwa.Kweli serikali DHAIFU haina maono,waziri wa afya hata kama utafiti wake ni kweli angekaa kimya kumtunzia heshima mkubwa wake wa kazi.
Follow Us Here