Support JamiiForums and Become a 'JF Premium Member' | Click HERE for Details
    Show/Hide This

    Topic: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

    Report Post
    Page 2 of 10 FirstFirst 1234 ... LastLast
    Results 21 to 40 of 200
    1. #1
      Bikra's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 13th May 2009
      Location : Dar es salaam
      Posts : 101
      Rep Power : 535
      Likes Received
      55
      Likes Given
      0

      Post Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
        • Mwulize jina lake
        • Mwulize namba yake ya uaskari

      • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
      • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
      • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
        • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.

      • Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.
      • Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.
      • Raia ana haki ya kuyasoma kabla ya kutia sahihi yake.
      • Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
      • Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
      • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.

      Quote By MwanaHaki View Post
      Umesahau hizi:

      • Iwapo askari polisi ataamua kumpekua mtuhumiwa, mtuhumiwa ana haki ya kumpekua askari polisi KABLA ya kupekuliwa yeye mwenyewe
      • Pia, askari polisi hawana haki ya kuingia kwenye gari, nyumba au ofisi ya mtu wanayemtuhumu, kwa madhumuni ya kufanya upekuzi, pasi na kuwapo kwa (a) hati ya upekuzi ambayo hutolewa mahakamani, (b) mashahidi wanaotambulika rasmi kisheria, kama vile, mwenyekiti/mjumbe wa serikali ya mtaa au mwenyekiti wa nyumba kumi kumi (iwapo mfumo huo unatumika), au (c) jirani wa myu anayetuhumiwa
      • Aidha, mtuhumiwa hatakamatwa au kupekuliwa na askari polisi baada ya saa 12.30 jioni au kabla ya saa 12.30 alfajiri, kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act), isipokuwa tu, kama kutakuwa na ushahidi wa kutosha kwamba, kumpekua mtuhumiwa kabla ya saa 12.30 alfajiri au baada ya saa 12.30 jioni kunaweza kuleta madhara kwa askari polisi, mashahidi au watu wengine wowote wale

      Nikikumbuka mengine nitawapa mkanda.

      Mwana wa Haki
      Last edited by PainKiller; 13th July 2009 at 00:58. Reason: Font size increased to 3
      “Tanzania, I will die for You”


    2. #21
      Mkeshahoi's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th January 2009
      Posts : 2,251
      Rep Power : 987
      Likes Received
      201
      Likes Given
      786

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      [COLOR="rgb(255, 0, 255)"]
      Quote By Bikra View Post
      • Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
        • Mwulize jina lake
        • Mwulize namba yake ya uaskari
      • Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
        [/COLOR]
      Quote By Bikra View Post
      • Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
      • Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
        • Hutakiwi kutoa fedha kama dhamana uwapo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa, isipokuwa maelezo utakayoandika.
      • Raia ana haki ya kuwaeleza polisi ama Maafisa wa Kuzuia Rushwa kwamba lolote atakalosema linaweza kutumiwa kama ushahidi mahakamani, na asiburuzwe kuandika tu.
      • Raia ana haki ya kuomba Wakili wake awepo kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa wakati anatoa maelezo yake.
      • Raia ana haki ya kuyasoma kabla ya kutia sahihi yake.
      • Raia ana haki ya kudai risiti ya orodha ya vitu vyake/fedha zake alizozitoa ama kukabidhi kituo cha polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
      • Raia kama ni mwanamke ana haki ya kupekuliwa na polisi wa kike, na iwapo hakuna polisi mwanamke, basi mwanamke yeyote na vile vile kwa mwanamume.
      • Raia ana haki ya kufikishwa mahakamani katika muda usiozidi saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha polisi.

      ya ukweli ka Bikra ilivo.... thanks..umenielimisha!!1
      Hela silaha... Kisu Mzigo

    3. #22
      Johnsecond's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 4th May 2010
      Posts : 949
      Rep Power : 657
      Likes Received
      156
      Likes Given
      68

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Jamani hizi sheria zipo tu kila siku lakini msiziamini sana wakati mwingine hata kama unazijua tulia. Sheria kubwa kuliko zote "be obedient" maana kuna vifungu ambavyo pia vinawaruhusu hawa jamaa kufanya kazi zao bila kuangalia haki hizo. hivyo msizitegemee sana mimi yaliwahi kunipata. Lakini namshukuru aliye post at least mtu unaweza kujua mahali ambapo umechezewa rough.

    4. #23
      WAMURUBHERE's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 21st April 2010
      Posts : 335
      Rep Power : 533
      Likes Received
      17
      Likes Given
      5

      Default Re: Je, unajua haki yako unapokamatwa na polisi?

      Quote By Dilunga View Post
      Kwa hiyo jizi likivamia usiku wa manane inabidi kisheria tusubiri kuche ndio tiulikimbize kulikamata na kulisachi?
      jizi likivamia usiku wa ma8 huwa haisubiriwi kuche linakamatwa na kupekuliwa chini ya K/F 42 cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jina (criminal procedure act ) yaaani search on emergence
      mjasiria likes this.

    5. #24
      Fisherscom's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 13th March 2008
      Location : Nyanda Za Juu
      Posts : 475
      Rep Power : 670
      Likes Received
      27
      Likes Given
      62

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Ahsante sana ndugu kutuelimisha na kutukumbusha haki zetu kama raia.

    6. #25
      jeff kulola's Avatar
      Junior Member Array
      Join Date : 19th June 2010
      Posts : 2
      Rep Power : 0
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      jamani asanteni kwa hiyo elimu kweli kwa maisha ya sasa bila kujua haki zako utanyanyaswa sana na polisi


    7. #26
      Kunta Kinte's Avatar
      JF Gold Member Array
      Join Date : 18th May 2009
      Posts : 2,608
      Rep Power : 2547
      Likes Received
      614
      Likes Given
      769

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Ni Educative Bikra, tuletee nyingine tafadhali

    8. #27
      Buswelu's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 16th August 2007
      Location : Lake Victora Gold Field.
      Posts : 1,939
      Rep Power : 996
      Likes Received
      182
      Likes Given
      144

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Quote By blackpepper View Post
      Raia ana haki ya kujua elimu ya anayemkamata
      Elimu ya sheria?au una maanisha kama alimaliza hata f4,f6 au chuo kikuu hata kama ni elimu yoyote....?
      Live Life so Well That even Death Loves to see you Alive.

    9. #28
      FirstLady1's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2009
      Location : Mama Mwenye Nyumba
      Posts : 15,052
      Rep Power : 3723
      Likes Received
      3621
      Likes Given
      5885

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Asante sana bikra
      No one is in charge of your happiness except you...
      God time is the best..
      Hadi tufike 2015 tutakuwa tumekoma

    10. #29
      Munghiki's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 10th October 2010
      Posts : 153
      Rep Power : 471
      Likes Received
      6
      Likes Given
      0

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      bila kusahau police mwenye cheo koplo kwenda juu ndio anaweza kuchukua maelezo yko na co vinginevyo.

    11. #30
      Sumu Baridi's Avatar
      Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 14
      Rep Power : 440
      Likes Received
      0
      Likes Given
      0

      Default

      "kwa mujibu wa Mwendendo wa Makosa ya Jinai (Penal Code Act)"
      Mkuu MwanaHaki,naomba nikurekebishe kidogo,
      (1)Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai ni Criminal Procedure Act na
      (2)Kanuni ya Adhabu ndio Penal Code Act-Cap 16 of the Laws of Tanzania

      Ahsante

    12. #31
      Elli's Avatar
      JF Bronze Member Array
      Join Date : 17th March 2008
      Location : Kijito-Upele
      Posts : 9,022
      Rep Power : 2645
      Likes Received
      2321
      Likes Given
      2103

      Default

      Mgambo wa jiji walinipeleka kituoni kwa issue nyingine nikafika wakanigeuzia kibao eti nimewazuia kufanya kazi zao kihalali, niliwaomba wajitambulishe wakagoma wakasema watajitambulisha kituoni kufika wakageuza kibao, bado natafuta msaada lazima nije kulipa kisasi at any cost, walinisweka rumande pale urafiki hadi nikatoa 50 elfu, bado inaniuma sana, nitalipa kisasi bado natafuta msaada

    13. #32
      silver25's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 29th July 2010
      Location : DSM
      Posts : 703
      Rep Power : 591
      Likes Received
      23
      Likes Given
      19

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Mtuhumiwa hanaruhusa ya kupigwa na polisi au mgambo panapotokea tatizo

    14. #33
      kapuni's Avatar
      Member Array
      Join Date : 15th November 2010
      Posts : 15
      Rep Power : 439
      Likes Received
      2
      Likes Given
      0

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Quote By Elli View Post
      Mgambo wa jiji walinipeleka kituoni kwa issue nyingine nikafika wakanigeuzia kibao eti nimewazuia kufanya kazi zao kihalali, niliwaomba wajitambulishe wakagoma wakasema watajitambulisha kituoni kufika wakageuza kibao, bado natafuta msaada lazima nije kulipa kisasi at any cost, walinisweka rumande pale urafiki hadi nikatoa 50 elfu, bado inaniuma sana, nitalipa kisasi bado natafuta msaada
      Mapolisi wanapata kiburi wakiwa kituoni,kama ishu inaweza ikaisha pasipokwenda kituoni ni vizuri zaidi.

    15. #34
      Mokoyo's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 2nd March 2010
      Location : KILIMO KWANZA
      Posts : 3,655
      Rep Power : 1208
      Likes Received
      458
      Likes Given
      324

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      excellent Bikra. elimu muhimu sana kwetu wananchi

    16. #35
      Bongemzito's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 5th November 2010
      Posts : 161
      Rep Power : 469
      Likes Received
      9
      Likes Given
      1

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Unajua Polisi wanajua raia hawafahamu haki zao za msingi wanapokamatwa na hata ukiwa unazifahamu wanakupa vitisho mwenyewe utatulia,ila ukijiamini nao wenyewe wanaona hapa pagumu..

      Vipi pale polisi wanapokuja kukukamata nyumbani au ofisini ukiwauliza nije kituoni kwa kosa gani wao wanasema hutakiwi kujua hapa utaenda kufahamu hukohuko kituoni,na ukienda huko unaingizwa moja kwa moja ndani....

      Na vipi unaweza kujidhamini mwenyewe?

    17. #36
      Quinty's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 25th March 2010
      Location : Ouagadougou
      Posts : 464
      Rep Power : 561
      Likes Received
      66
      Likes Given
      105

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Thanks this has been so useful. Please kama inawezekana mwingine atoe haki ya madereva pindi wakamatwapo na polisi usalama barabarani

    18. #37
      Kiherehere's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 1st November 2010
      Posts : 1,076
      Rep Power : 653
      Likes Received
      72
      Likes Given
      132

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      No comment... naona hamuwajui polisi wa kituo cha Buguruni. Peleka hizo sheria zako ndo utaona.
      mjasiria likes this.

    19. #38
      Mallaba's Avatar
      JF Senior Expert Member Array
      Join Date : 30th January 2008
      Location : Jerusalem
      Posts : 2,562
      Rep Power : 1094
      Likes Received
      24
      Likes Given
      28

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      hii post imenifurahisaha sana, kwanini nilikuwa najiandaa kuandaa thread yenye madhumuni kama hayo..
      kwa kifupi ni kwamba nyumbani kuna gari inayofanya biashara za usafiri, sasa jana askari akawa ameikamata na kuomba mmliki aende eti kosa ni kuwa hakuwa na insurance ya kufanyia biashara( sasa kwa kutokujua akajua kuwa labda kuna insurance nyingine tofauti na zile tunazonunua za kawaida) wakapewa faini ya tz elfu 20 , katika kujitetea yule traffic akamwambia alipe elfu kumi ili wamalizane( wakati huo mama akiwa kesha nitumia sms kunieleze kuhusu hilo swala), alipomaliza kumlipa Mama ikabidi afatilie kwenye vyombo husika ili kujua kama anatakiwa kulipa insurance nyingine, bahati nzuri kafika kule na kuelezwa kuwa hakuna bima nyingine zaidi ya hiyo uliyonayo, baada ya kama dk 45 mama akanitumia tena sms akisema "swala lile lilikuwa ni uonevu tu, wamechukua elfu kumi" . sio siri nilighadhabika sana na kumpigia simu na kumuuliza "kulikoni mtu umeshatambua kuwa ni uonevu bado unampa elfu kumi? kwa nini usirudi na kumwomba hiyo pesa yako? hivi ni kwa nini mnaruhusu kunyonywa wazi wazi kiasi hicho? akanijibu kuwa yaani huku Tanzania kila kitu ni rushwa tu iwe unataka au hutaki haki yako bila rushwa hakuna chochote..huku akiongezea kuwa sasa mimi nitafanyaje wakati sijui hata sheria zinasemaje? mmh hapo nikachoka kabisa
      je ni wangapi wanaofanyiwa madudu kama haya? unajua matatizo mengine tunayasabisha sisi wenyewe wananchi kwa kupenda kufanya haraka haraka bila kufuata procedure..
      Nimetafakari sana na kutambua kuwa wananchi wengi hawajui sheria na wanaendelea kunyonywa tena wakinyenyekea kutoa chochote ili wapate haki yao, hivi hawa matraffic wataacha huu ubabaishaji hadi lini? sio siri kama ningekuwa Tanzania ningehakikisha namfatilia huyu traffic hadi mwisho ili iwe funzo kwa wengine kama hao.
      Ee Bwana uyasikilize maneno yangu, ukaangalie kutafakari kwangu.

    20. #39
      Dar_Millionaire's Avatar
      Senior Member Array
      Join Date : 6th August 2008
      Posts : 173
      Rep Power : 589
      Likes Received
      25
      Likes Given
      175

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      Bikra na wengineo mliochangia shukrani sana kwa elimu hii. Naomba utuwekee na nukuu za vifungu vya sheria (citation) ambavyo vinatoa hizi haki.

    21. #40
      matshs's Avatar
      Member Array
      Join Date : 27th June 2007
      Posts : 26
      Rep Power : 618
      Likes Received
      1
      Likes Given
      1

      Default re: Jua haki yako unapokamatwa na Polisi

      [QUOTE=Bikra;474836][LIST][*] Raia ana haki ya kumwomba askari ajitambulishe kwako.
      • Mwulize jina lake
      • Mwulize namba yake ya uaskari
      [*] Raia ana haki ya kujulishwa kwanini anatiliwa mashaka ama kukamatwa.
      [*] Raia ana haki ya kuwajulisha ndugu, jamaa ama sehemu anakofanyia kazi kwamba ama amekamatwa na polisi ama Taasisi ya Kuzuia Rushwa.
      [*] Raia ana haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa kituo cha polisi ama Taasisi ya kuzuia rushwa.
      [LIST]



      hii kitu hapa vituo vya polisi ni ngumu sheria yetu inapindishwa sana na hawa wanaoitwa polisi!!

    Page 2 of 10 FirstFirst 1234 ... LastLast

    LinkBacks (?)

    1. 19th July 2010, 12:21

    Similar Topics

    1. Jua haki yako ukiwa barabarani ukishikwa na trafiki.
      By kauk in forum Jukwaa la Sheria (The Law Forum)
      Replies: 18
      Last Post: 3rd January 2012, 17:09
    2. Piga kura kutimiza haki yako!
      By Simcaesor in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 0
      Last Post: 13th October 2011, 06:23
    3. Kwanini ukudai haki yako unaambiwa wewe ni Chadema!?
      By Sinai in forum Jukwaa la Siasa
      Replies: 6
      Last Post: 2nd May 2011, 14:10
    4. Muajiri ana haki kujua hali yako ya hiv?
      By TWANJUGUNA in forum Jukwaa la Sheria (The Law Forum)
      Replies: 5
      Last Post: 29th June 2010, 11:17
    5. Orodha ya Haki za Wapendanao - Tumia haki yako!
      By Mzee Mwanakijiji in forum Mahusiano, mapenzi, urafiki
      Replies: 18
      Last Post: 20th June 2010, 17:52

    User Tag List

    Posting Permissions

    • You may not post new threads
    • You may not post replies
    • You may not post attachments
    • You may not edit your posts
    •  

    Who are WE?

    JamiiForums is a 'User Generated Content' site; anyone can register (MUST) and comment or start a new topic.

    You are always welcome! Read more...

    Where are we?

    We have our offices in Dar es Salaam but we still work virtually.

    For anything related to this site please Contact us.

    Contact us now...

    DISCLAIMER

    JamiiForums, its partners, affiliates and advertisers are not responsible for the content of threads/topics that are submitted by users..

    Read more...

    Forum Rules

    JamiiForums is moderated under the rules set by users and moderators to safeguard you.

    You MUST read them and comply accordingly. Read more...

    Privacy Policy

    We are committed to respecting your privacy rights when visiting any JamiiForums.com page, such as this one.

    Read our Privacy Policy. Proceed here...